Na kwa UGUMU,.... .... ingekuwa bomba au kupendeza kama UGUMU ungekuwa unatukumbusha URAHISI.:-(
Na labda kwa UGUMU,.... .... tunakumbushwa UBINADAMU sio RAHISI.
Na wakati jambo ni GUMU,... .... kumbuka kuwa kama wewe si malaika hakuna cha zaidi ... ..... zaidi ya jambo lifuatalo gumu , HATA KAMA nalo ni GUMU ,kuleta hata danganyatoto itakayolifanya ukilifananisha na lililotangulia lioneakanalo gumu, hili ni RAHISI.
Leo kwanguNAHISI ilikuwa NGUMU,.... .... na labda kuongelea jambo GUMU ndio wenyewe URAHISI!:-(
Swali:
AU?
NI hilo tu MKUU wa MEZA !
Ngojea Black Star- Shakila adai-Moyo unalia macho yanacheka
Au tu Raphael SaadiqftQ TIP abadili kwa kitu-Get involved
[Tahadhari: Kumbuka lijamaa LIFIKIRIALO hivi hili swala, kamwe halitamki kwa sauti MPENZI ASIKIE!:-(]
Katika haya MAISHA ambayo hakuna BREKI ya UMRI kwenda,... .... siwezi kuendelea kusubiri KWA KUWA UMRI UNAKWENDA wakati NIAMINIYE ninampenda kikweli kubwa kuliko SIJAWAHI KUKUTANA NAYE na bado namuona tu kwenye MAGAZETI hata yale ya kiuchiuchi au tu kwenye mpaka KWENYE taarifa za HABARI hata za hali ya hewa kwenye TV a.k.a LUNINGA.:-(
Inabidi tu HISIA zangu za kukuzoea hata kwa ILE michezo yetu iwezayo mpa mimba mtu ZIGEUKE tu kuwa ni za kwa dhati nakupenda,... .... kwa kuwa yule mwingine nimpendaye kuliko wewe niliyewahi mpaka kukutana naye , MIYE kanishinda na KWELI hata nikijaribu kumsabahi ANARINGA.:-(
Na wakati hata nikitakakujiaminisha sijazidiwa bahati mbaya, ETI wakati MAISHA YANGU yanaelekea CHINA kama tu yako POOZEO TOTOZ yanapokwenda,....
.... yule watatu nimpendaye zaidi kuliko wewe ,ingawa HUYU nimpendeacho tu ZAIDI hakina zaidi ya kwamba anatako TU zuri kuliko wewe, ETI naye wakati huu wakati KIMAISHA naelekea China, MAISHA YAKE nayo ndio kwanza yako Tanzania na ndio kabisaaa yanatoka mpaka DAR-es SALAAM nilikokuzoea na kuzidi kuelekea IRINGA.:-(
Lakini kama tu WENGINE WAFANYAVYO kihalihalisi ya MAHUSIANO ya WATU WAWILI ,sina ujanja zaidi tu ya wewe kukupenda,...
.....kwa kuwa kwa jinsi nionavyo WALIOKO KATIKA MAHUSIANO waliooa na KUOLEWA au tu wenye wapenzi tayari UCHOCHORONI watokwavyo na denda wakati wanatamani vya wengine hata kama DOGO DOGO ni saizi ya watoto wao, NAANZA KUAMINI LABDA ni FANTASI a.k.a NDOTO ZA ALINACHA ndio MPENZI wa kweli WA MTU duniani,....
.... na naahidi NTAJIFUNZA KUKUPENDA kwa dhati KIHIVYO,.....
.....kama tu HAO WENGINE wapendavyo kwa kuliambia wanalipenda JITU HILI wakati katika FANTASI hata za wakati wanashughulika na shughuli zijazazo UJAUZITO MTU walikuwa wanaendeleza penzi na JITU JINGINE KIFANTASI ndani ya tendo , kwa kuwa KIFANTASI HIZO a.k.a ALINACHA ZA aina ya TAMU ZAIDI IKO NYUMBA YA JIRANI NA SI KWAKO hunogewa zaidi ILE TAMU na KWA HILO wanajisikia vizuri hata kwa habari za kutoka REDIO ZA MBAO kuwa walipendalo KIFANTASI limeonekana sehemusehemu linaafya hiloo na limependezaa ingawa lilipoonekana , BONGE LA kamasi lilikuwa kwenye kadamnasi LINAPENGA.:-(
Swali:
Unauhakika HASA kama sasa hivi una-LIMTU, ungeweza kimapenzi au hata kimahusiano usingelibadili hilo LIMTU?
Namaanisha:
Kama uko kwenye UHUSIANO, unauhakika kama MATUMAINI YAKO tokea uanze KUWASHWA KIKUBWA yangetimia, ni huyo uliyenaye ungekuwa naye AU TU ume-SETTLE a.k.a IMEBIDI TU UWE NA HILO LIMTU kwa kuwa katika mazingira yaliyopo ndio -The best U can DO a.k.a ndilo LIMTU lidakikalo na kinamna unaweza KULIVUMILIA?
Una uhakika wewe ni chaguo la kwanza la wako mpenzi na kama sio kuna madhara?
Si inasemekana kwa kawaida wazuri wote wamfaao mtu ATAFUTAYE MPENZI huwa washaoa au kuolewa?
NIMEACHA! Kumbuka hili ni WAZO TU MKUU wala USITISHIKE ! IJUMAA na WIKIENDI NJEMA MHESHIMIWA!
Hebu tupate sindimba kidogo..
Au hebu ENOMIZIZI wadai tena -Kiviringishe Tena
Basi bwana tuendeleze tu na SWAHILI NATIONwakiwa naChameleon wakileta-Chakacha
Nikikuonea donge,.... .... LABDA ni DALILI kuwa siridhishwi na yangu na NA SIKUJUI vizuri wewe ndio maana natamani kuwa wewe au tu kuwa na VYAKO!:-(
Ila mwenye DONGE,... ..... ukweli wenyewe si kwamba hana au ataridhishwa na YAKO.:-(
Na kama HATA vile kwenye UGALI ushuhudiavyo wafinyangao TONGE,... .... kuna wapendezao na tonge utafikiri walizaliwa ili wasilie uma na kisu, au tu UKIWADEKU utafikiri wanaundugu vile na tonge KWA WAPENDEZAVYO NALO ingawa wanalifinyanga kwa staili tu kama YAKO.:-(
Lakini wakati unaona DONGE,... ... KIPINDI HICHO haki ya nani WEYE kunauwezekano MKUBWA unawaza ya WENGINE kuliko uliyonayo kibao ambayo ni baaab kubwa, YAKO.:-(
Swali:
Unakumbuka sababu kubwa ya kumuonea wivu mtu ni kutomjua vizuri huyo mtu?
Unakumbuka wivu WA MTU hutokana na kutoridhika tu na chake KITU huyo mtu, na cha ajabu ni kwamba KURIDHIKA kwa kawaida mtu WALA hahitaji kitu?
Umeridhika na yako,?
Hivi kuridhika ni siri ya WAPUMZIKAO au ni ile ya UZEMBE?
NI WAZO tu MHESHIMIWA Othrong'ong'o!
Hebu MOMBASA ROOTS watuletee-DISCO CHAKACHA
Aut u MOMBASA ROOTS washauri ukatike katika kibao-KATA
Au turudi BONGO NYOSOThe KILIMANJARO BAND waongelee ya -KACHIRI
Labda ni kweli kuna watu ni mpaka WAFE a.k.a ZE KUKATA ROHO,.... ..... ndio kuna watu hustukia UZURI au UMUHIMU wao katika yao wayaonayo ni ya muhimu.:-(
Lakini bado kwa marehemu aliyekata ROHO,... .... KUNAUWEZEKANO MKUBWA hazina faida tena SIFA , na KWA aliye hai ASIFIAYE MFU kunauwezekano kwa hilo kuna utaahira AU NI SWALA LA UBINAFSI TU WA WALIO HAI kwa kusifia mfu ILI WAJISIKIE VIZURI kwa kuwa sifa nyingi asifiwazo marehemu UKICHUNGUZA, labda angekua hai labda ndio kwake zingekuwa MUHIMU.:-(
Swali kiduchu:
NI watu wangapi HAI SASA HIVI unaoweza kuwasifia NA huwasifii ingawa unauhakika wakifa utadai ''MAREHEMU ALIKUWA MTU MZURI KWELI!''!?
Unauhakika wasifiao wafu hawafanyi hivyo kujiridhisha na kujifariji wao WENYEWE au walio hai WENGINE wasikiao hizo sifa ambao MSIFIAJI MFU anajua ni wenye kumzimia MAREHEMU?
NI HILO TU Kingunge na ni WAZO TU!
Hebu tubadili hali ya hewa kwa kwenda Brazil kukutana na Kaoma waturudishie tena -Dançando Lambada
Au tu COCOA TEA atulize KIBARUTI kwa kuzungumzia tu ya jelajela katika -Riker's Island
Ukitaka kujua BINADAMU ni kiumbe cha ajabu sana,... ....hebu kiangalie kiumbe hiki wakati kiko BIZE kinashabikia kitu!
Swali:
Unauhakika ushaliangalia BINADAMU vizuri wakati lishangiliacho eti NI watu wanafukuza KIDUDE CHA MVIRINGO kinachodundadunda ?
Ushaangalia wakati binadamu washangiliacho ni mtu anampiga mwenzie kwa kuwa eti inaitwa NDONDI?
[Wakati unafikiria swali langu JARIBU PIA kufumba macho na utafakari jinsi hata Kunguru na Bata wanafikiria nini KUHUSU akili za binadamu wakiona binadamu wanashangilia mtu anafukuza mpira]
Tukiachana nahilo naweza sema.
USHABIKI ni aina ya UBAGUZI ,... ....ambacho ukipendacho ndicho wataka kishinde.:-(
USHABIKI ni UBINAFSI,.... ..... kwa kuwa unazalisha upendeleo na ikibidi KIUSHABIKI utajipendelea.:-(
USHABIKI ni aina ya UKICHAA,.... ..... angalia tu na wala huhitaji HATA kuchunguza na utakuta mpaka WATU WAZIMA wanashangilia kabisa au WAMENUNA TU kisa eti labda kuna mtu kapiga teke mpira.:-(
USHABIKI ni PENZI,.... ..... wawezajikuta unashangilia udhaifu au umjuaye anakosea na UKWELI USIUKUBALI kama tu ung'ang'aniavyo kuwa WATU TU WANAMUONEA WIVU MKE WAKO na si malaya, kisa umependa.:-(
USHABIKI ni DINI,....
..... nadhani unajua kuwa DINI kama tu USHABIKI ni vitu visivyoeleweka na HUPATA UMUHIMU kwa BINADAMU kwa kuwa binadamu katika mapungufu yake anajaribu kujazia UTUPU WA MOYO katika KUFARIJIKA ,.....
......ndio kisa cha kwanini unadundwa moyo KWA KUSIKILIZA YA MUNGU ambayo hujazia ya roho......
....NA ......
....UNADUNDWA MOYO PIA hata kwa kushabikia eti Miss Matombo ndio mzuri zaidi WAKATI HATA KAMA unajua katika uzuri wa kitu LADHA HUTOFAUTIANA jichoni mwa mtu na MTU , kwa kuwa tu kitendo hicho CHA KUSHABIKIA UJINGA nacho hata kama ni chakijinga , bado kinajazia kama DINI kwa kukuna ILE KITU ROHO INAPENDA.
DUH NAKATIZA HILI WAZO naona linaanza KUNISHINDA n'sije pitiliza bure halafu ukajikuta UMEKUWA MSHABIKI WANGU!:-(
Swali:
Unauhakika USHABIKI wa kitu au tu PENZI sio aina ya UKICHAA?
Si unajua BINADAMU ukimpa nafasi anaweza kushabikia hata mende kama hata kuku wakushabikia hawapo?
Umestukia labda ushabiki ni moja tu ya kitu kionyeshacho BINADAMU KUNA KITU KAPUNGUKIWA ndio maana ananogewa KUSHABIKIA KITU yote ikiwa ni katika KUJAZIA kitu tu vile maishani ambayo mara BWELELE maana zake zimejaa UTUPU?
BASI NIMEACHA na kumbuka MHESHIMIWA hili ni WAZO TU!
Tupumzike kwa kwenda U.S.A kuwaangalia Binadamu wakishangilia Mende HAPA
Hebu tu twende na NAMIBIA tena TATE BUTI arudie kitu -EFENGE
Au tu turudi BONGO NYOSO kukutana na PROFESSOR Jay adai tena-Hapo VIPI
Labda si kuku na bata tu BALI ni mpaka kila MTU ni MSTAARABU kama ukiuelewa wake ustaarabu!
Swali:
AU?
Kumbuka ingawa KWA WENGINE ustaarabu ni kula kwa MKONO mkekani,... .....kuna waaminio ustaarabu ni kulia MEZANI kwa VIJITI a.k.a chopu stiki na kudharau ustaarabu wa UMA na KISU.
Kwa hiyo wakati unadharau watu kwa kuwa una TISHU chooni,.... ..... kumbuka kuna ambao ustaarabbu ni kuchambia mchanga na mawe au tu wale waaminio kwa dhati katika chambio la maji na huo ustaarabu wa TOILET PAPER kuupiga VISU.
Swali:
Si unajua USTAARABU kunauwezekano asilimia kubwa ni JAMBO LAKUFIKIRIKA TU?
NI WAZO TU MHESHIMIWA ingawa nakushauri usiache kuchamba lakini baada ya KUJISAIDIA!
Hebu ARROW warudishe ustaarabu kwa kitu -HOT HOT HOT
....zaidi ya kutaka atambuliwe kwa vyake atakavyo viwe maarufu.
Na kwa sababu binadamu hana wa MALAIKA umaarufu,.... .... kumbuka kama ni mtu HATA KAMA anajulikana sana VIPI , huyo bado ukimnusa eneo ana harufu. Swali:
Umeshawahi kuhesabu angalau vitu vijazavyo idadi ya mkono mmoja vimfanyavyo hata yule maarufu sana ajulikane kwa huo umaarufu?
Ndio , LABDA ni baadhi ya vitu tu vichache, kama sio KIMOJA ambavyo vimfanyavyo mtu ajulikane kuwa ni maarufu,.....
.....na kumbuka tu hakuna fomwula katika hili ndio maana hata kwa kutembea uchi, KUJIPIKILISHA, wizi , UMALAYA na sio tu UANASIASA na kabumbu viwezavyo kukufanya maarufu.
Na inatisha kwa kuwa inamaana hata wewe kama sio bado maarufu,.....
.... labda uko hatua moja tu pembeni ya kitakacho kufanya uwe maarufu ingawa cha kusikitisha labda wala WEYE hutaki UMAARUFU!:-(
NIMEACHA na hili ni WAZO TU MHESHIMIWA ! Kumbuka wazo la Mtakatifu SIMON KITURURU wala sio KORANI wala BIBLIA imlengavyo mwenye dini, kwa hiyo kulibishia RUKSA na hutaenda kwa hilo JEHANAMU ukachomwe na MUNGU apendaye watu!
Ngojea Dr Dre anipe-Lil' GHETTO boy
Au tu Dr DrenaICE CUBE wanipe-Natural BORN Killaz{Tahadhari: lugha na stori vyote vichafu kiaina!:-(}
NI kweli MALENGO ya mchagua chupi sio yale yale,...
.....ndio maana kuna wenye chupi kama BICHIKOMA.
Ngojea nifafanue:
Tabia ya mtu unaweza kujifunza hata kwa kumuangalia chupi,...
.... na kwa bahati mbaya MHESHIMIWA na CHANGUDOA wote wanaendeshwa na WANACHO kilenga kufanikisha na kwa hilo WANAFANANA.
Na nikifafanua ZAIDI kipengele kwa kutumia chupi naweza kusema:
Uchaguzi wa chupi una sayansi zake kama tu uchaguzi wa Gari au Matunda.
Ndio maana ni vigumu kujua nia na MADHUMUNI ya mchagua chupi ,.... ... na kama ingekuwa ni rahisi namna HIYO, tungekuwa na CHUPI za aina moja tu zenye mshono MMOJA na labda saizi tu ndio zingekuwa tofauti kutokana na UKWELI kuna watu wengine sehemu zao ZA kuvalishwa chupi ujazo ni SAIZI pipa wakati kamwili kenyewe debe.
UCHAGUZIII! Ndio , binadamu ukimpa nafasi ya kuchagua atachagua kwa sababu binafsi, na UBINAFSI WA BINADAMU ndio vifanyavyo MHESHIMIWA na CHANGUDOA kufanana hata katika uchaguzi wa CHUPI!:-(
NIMEACHA!
Swali:
Kwani unauhakika ilikuwa lazima wanaume na wanawake wawe na chupi tofauti?
Si unakumbuka CHANGUDOA ni MHESHIMIWA kwenye eneo lake?
Si unajua tukidai dhumuni la kuwa na gari ni USAFIRI TU na kuna COROLLA, ina maana tunamaanisha wote wauzao COROLLA na kununua gari saizi ileile uthamani BENZI ni wajinga?
Hebu tu tubadili hali ya hewa kijiweni kwa kwenda tena South Africa kukutana na Soul Brothers
Au Yvonne Chaka Chaka audhi watu TENA kwa kusifia pombe katika - Umqombothi
[Tahadhari: Nia na madhumuni ya taralira hii ni kugusia kidogo vijambozi kwa staili ya kukuna TAMADUNI kinamna katika MFANANISHO wa BONGO na FINLAND!]
Ukitoka TANZANIA ukajikuta uko FINLAND ambako govi ni TUKUFU, unaweza kushangaa ukichekwa kisa mtu kastukia dume zima UMETAHIRIWA hasa ikiwa wewe ndiye ulikuwa bingwa wakucheka wenye MAGOVI !
Samahani NAANZA UPYA hii TARALIRA na safari hii kiheshima......
Utamaduni ni kitu cha ajabu sana!
Na moja ya njia NZURI ya mtu kujifunza kuhusu utamaduni wako ni kuishi katika utamaduni wa watu WENGINE.
Kuna mambo ambayo katika utamaduni wako AMBAYO yanakuumiza kichwa, yanaweza kukusumbua mpaka ustukie watu wengine waishivyo bila kuhitaji uaminicho NI MUHIMU kwenye utamaduni wako ndipo utakapo gundua kuna mengi ni muhimu kwako kutokana tu na staili yako ya KUFIKIRIA na wala LABDA si kweli hata MAMA MKWE akikuvulia lichupi kwa hasira UTALAANIKA kwa kuwa unashuhudia JAMII ambayo watoto hawapofuki kwa kuona vipengele vya wakubwa na HAWANA KIITWACHO KULAANI katika tamaduni na staili ya kufikiria.
Na haki ya nani ni mtazamo tu NA JINSI YA KUFIKIRIA usababishao GUINEA PAPUA kibuyu kwenye kikojoleo cha mwanaume IWE ni chupi tosha, na kwa akinadada BICHI BRAZIL iwe ni vikamba tu vimefunika kidude huku tako liko nje ionekane KIMWANA KATOKA, wakati wewe chupi lako BONGE na linafanyakazi kwa ufanisi utafikiri lina iga NEPI, halafu wajanja wanakucheka na mpenzi anakuona wakuja.:-(
Tupumzike kwa kuangalia jinsi ufikiriavyo kwa utamaduni wako wa asili na mpaka wa kuiga uwezavyo mpaka kukuchagulia aina ya chupi kama ifuatavyo:
Chupi yetu ya asili/Kitamaduni.
Mimi niko hapo kwa nyuma ukiangalia vizuri pichani.
Hii chupi inamanufaa sana na naamini kama wewe unahusudu mambo ya chapuchapu unanielewa.
Chupi ya dada afikiriaye au ajijuaye ni bingwa wa kuchamba vizuri na atakudaka ukimchungulia au tu kufarijika kwa- ua zuri lapendeza - kabla hujaendeleza dhambi.
[Tubu Mkuu LAKINI kama umeingia majaribu ya dhambi ya kiuasherati !]
HILI ni Bonge la chupi lifanyalo tu kazi VIZURI SANA kama itegemewayo kufanyika na chupi.
Swali:
Bado hujastukia jinsi utamaduni na afikiriavyo mtu kunavyo mchagulia aina ya utamaduni wa CHUPI?
NGOJEA TURUDI kwenye hoja ya taralila ambayo ni FINLAND vs TANZANIA kiutamaduni...
Kama Mtanzania unaweza kushangaa sana baadhi ya mambo ukikatiza mitaa ya Ulaya Kaskazini kama vile :
Maswala ya fikira za UCHI
Mahusiano ya Mtu na Mtu
Dini
Msosi
Ufanyaji KAZI
Nk.
UCHI
Ndio , kama umetokea katika jamii kama ya Tanzania unaweza ukatishika siku ukikaribishwa SAUNA na familia nzima ya watu - Kuanzia BIBI mpaka wajukuu zake ambao wote wako UCHI.
Au tu unaweza kushtushwa ukistukia umekwenda kwa mtu halafu ukakuta ni Baba na Binti yake wanatoka uchi kwenye SAUNA ili kwenda kujidumbukiza ZIWANI kupoza joto la sauna huku wakiwa FULU kuchekelea. Hapa kama MTIZED unaweza kujikuta unaanza kufikiria labda JOGOO ninaonja kifaranga chake ,wakati wahusika waongeayo na kufikiria wala hayagusi sehemu za KUJIGIDANIA kimwili. Yani wako fulu Baba na Mwana na swala ni sauna na si kingine.
Kwa kifupi WAFINI na WATANZANIA katika swala la kukaa uchi na tuwafikiriavyo waliouchi kunatofauti kubwa. Na kwa kawaida UFINI ni TITI KUBWA ndio kidaka BUZI na sio tako kubwa kama liwapalo MACHUNA BUZI wa BONGO ndoano.
Na govi ni TUKUFU mitaa ya FINLAND, na kama dume zima limetahiriwa basi ujue ni YAHUDI au ISLAMU kitu ambacho kwa nchi kama FINLAND asilimiani zero nukta ziro zero sifuri tano au kitu kama hicho, ndio ujazo wa Mtu hizi zenye mila ziaminizo katika kukatajando zilivyo kiidadi.
Kwa hiyo usishangae ukijichanganya DUME ZIMA kwenye MASAUNA , watu wakawa wanaacha kushangalia nyonyo ya mdada aliyekaa pembeni yako waliyoizoea kuiona na kuikodolea pembejeo yako iliyonolewa, na labda ILINOLEWA kwa sababu usizozijua.Ndio, wanaweza kukuchungulia pia kuhakikisha kama kweli watu weusi wanabaraka za punda kwa ukubwa wa pembejeo za uasherati.:-(
Swali:
SI unakumbuka katika ngoma zetu kibao Bongo ilikuwa kawaida akinadada kucheza nyonyo nje na kwa watazamaji kucheki nyonyo ya mkatika kiuno mambo yalikuwa si fulu kuyatamani kimfadhaiko?
Mtu na MTU
Kama umezoea kusalimia kila mtu unaweza kujisikia vibaya!
Mtu anaweza kustuka kama vile umemtukana kwa kusikia salamu yako , na kama YEYE bado ni mstaarabu badala ya kukujibu anaweza akakuulia'' DO I know U?''.
Kwa kifupi FINLAND kila mtu kivyake na ingawa watu hudai kuwa karibu nchi zote za magharibi ziko hivyo, kwa uzoefu wangu binafsi wa nchi kadhaa wa kadhaa ,NCHI nyingine za MAGHARIBI hazijafikia FINLAND hasa kwa sababu WAFINI ni wakimya na hawana porojo a.k.a small talk katika tamaduni yao.Wao ni watu wakuchuna zaidi a.k.a no non sense kwa wasiyemjua.
Na kingine ni kwamba FINLAND ni moja ya nchi ambayo mfumo wake WA SERIKALI unafanyakazi haswa na karibu kila kitu serikali inafanya ikibidi. Na maanisha, ikibidi serikali INAINGILIA MPAKA FAMILIA YAKO - itamsomesha mtoto wako mpaka Chuo Kikuu tokea ikunyang'anye kwa kuwa TU ulimfinya akapigia simu wahusika umemfinya. Na kutokana na Serikali ilivyokuwa inafanyakazi ipaswavyo imefikia mpaka hata mtoto wako hakuhitaji sana kama Bongo na huwezi kumtisha mtu kwa lolote kwa kuwa kama yeye ni Mfini basi Nyumba hawezi kukosa na anauhakika kuwa hafi na njaa. Kirahisi kuanzia asiye na kazi na Mkurugezi wa Kampuni kila jioni unaweza kuwakuta baa moja na kila mmoja anakunywa kwa starehe yake bila kuomba ofa wala kutishwa na mwenye hela katika maswala ya kipooza koo kabla ya kwenda nyumbani.
Kwa kifupi uhusiano wa mtu na mtu ni tofauti FINLAND ukilinganisha na TANZANIA au tu NCHI kama UINGEREZA na akuitaye rafiki kama ni Mfini mara karibu zote huyo ni rafiki kweli na sio porojo kwa kuwa mpaka kuzoeana naye kwenyewe mkizoeana basi kazi ilikuwapo hasa kwa kuwa MTU HIZI hazina sana porojo.
Dini
Finland inasemekana ni nchi ya KIKRISTO na kanisa kuu ni la KILUTHERI ingawa waendao kanisani wanahesabika.
Kutatua hilo swala la mahudhurio , FINLAND inawatoza sadaka Wafini kutoka kwenye mishahara yao. Yani inamaana ukipata mshahara wanakata sadaka huko huko , kwa hiyo uende au usiende kanisani weye sadaka umetoa.
Unaruhusiwa lakini kujitoa katika KANISA , na kama ujuavyo kuna wale wasio wakristo pia kama Wayahudi, Waislamu, ...nk. Ila kasheshe inayojitokeza ni kwamba karibu maeneo yote ya makaburi humilikiwa na makanisa, kwa hiyo kama unampango wa kufia FINLAND si jambo la busara kujitoa kanisani iliwasiilambe sadaka yako kwa kuwa watakudaka ukifa kwa kuwa kama sio memba wa kanisa kaburi sio bure kwako.
Na kama kawaida WAZEE ndio fulu kujichanganya MAKANISANI na sababu nadhani unajua! Na FINLAND unaweza kutukania MUNGU kirahisi bila watu kupandisha jazba wala kukuona waajabu. Naamini DINI na aidia nzima ya MBINGUNI na JEHANAMU havina sana nguvu kama BONGO Tandale au kule Matombo.
CHAKULA Kwa kawaida kama umezoea bonge la UGALI utashinda na njaa.
Na mapishi ya Kifini kibao si yakutumia viungo sana kwa hiyo kirahisi unaweza usilisikie supu kama umezoea angalau pilipili na binzari kwa mbali , bila kusahau kitunguu swaumu. Kwa kifupi kiungo kikubwa ni mate yako a.k.a ladha ya kutokuungwa.
Kirahisi menu ya kifini ina:
Viazi ulaya, Mikate, Sausage/Makkara, Majani majani kwa mbali,Mtakatifu Nguruwe kwa sana, Samaki- unajua tena wana maziwa elfu kibao, Kwa kifupi mchanganyiko wa vyakula hivyo nilivyovitaja huliwa tu kutegemea na ni nini kinaendelea....Soseji huenda sana na Ketchup na Mustard hasa iitwayo Turun SinappiChakula cha wanafunzi kilichozoeleka ni -SandwichIngawa chakula cha wanafunzi kutoka bongo kilicho zoeleka zaidi ni -Kuku kutokana na beiPombe Wafini wanapandisha sana . Kinywaji wanywacho sana ni Koskenkorva kwa sana, Bia, kila kilevi, Wine lakini hainywewi kama wanywavyo Wafaransa.Wafini kwa asilimia kubwa kinywaji wakinywavyo ni fulu kubugia na si mambo ya adoado.
KUFANYA KAZI!
Hawa jamaa ni wafanya kazi sana! Yani wakienda kulewa ni fulu kunywa pombe lakini wakirudi kazini ni KAZI na kahawa sana.Na ukizoea ufanyaji kazi wao ukirudi bongo lazima udhani BONGO watu wanafanyakazi katika SLOW MOTION.
Halafu ni ma- perfectionist. Kwa hiyo hata siku moja usiamini Mfini akikuambia hajui Kingereza, Kifaransa, Kijerumani kwa kuwa hata aongeaye hizo lugha kukuzidi ukimuuliza anaweza kudai hajui kisa labda kama ni Kingereza anaamini asiposaundi kama Queen Elizabeth basi yeye bado Kiingereza hajui. Na kama unaingia kwa gia za kisanii, kumbuka karibu asilimia themanini ya Wafini kuna chombo cha mziki wanakipiga na kujua kukisoma kimziki ingawa hawajiiti wanamziki kwa kuwa wanafanya shughuli nyingine na wanaona aibu kwa kutojiamini kuwa wanabwenga chombo. Kwa kifupi ukiingia kichwa kichwa unaweza kutoka nishai kwa kukutana na mtu ambaye anaweza akakufundisha mambo ya Bongo ambayo wewe mwenyewe huyajui.
NAACHIA HAPA MKUBWA na natumaini unakumbuka GOOGLE ipo ukitaka kuelewa mpaka Wafini wanapendelea Chupi za aina gani!
BAADAYE MHESHIMIWA!
Ngojea nimuachie mwanadadaKOFI ajivunie weusi kitu ambacho nahisi Wazungu wakijivunia Uzungu inaweza kuitwa ni ubaguzi katika-BLACK PRIDE
Au tu ni muachie naye mvulanaVivian Jones alete kitu-Good Morning
Duniani hakuna ambaye hajawahi KUKUBALI,.... .... na inasemekana mtu aliyekubali kinamna huyo KABADILIKA tokea tu akubali!
Mimi naamini kilichopo ndani ya aliyekubali,.... ......kilikuwepo tokea hajapewa ombi na akakubali.
Swali:
Unafikiria ni maisha yako au wewe mwenyewe unayebadilika baada ya kukubali mtongozo?
Labda,... ...UKITONGOZWA UKAKUBALI kilichobadilika sana ni hicho tu kuwa UNAJIJUA ulitongozwa UKAKUBALI,....
.....hata kama siye wengine HATUJUI NANI MAISHANI UMEWAKUBALIA kwa kuwa ukweli wenyewe wewe mwenyewe uko vilevile MGUMUUUU kukubali.
Kukubali kunaweza kukuua uhuru,.... ..... ingawa pia kwaweza kwenye mwanga kukutoa NURU.
Lakini kumbuka hata kwa idaiwaye kabadilika kwa kuwa baada ya kutongozwa akakubali sikuhizi anakukuru,.... ..... kumbuka aliyeshwari anakukuru PIA ukimpa kiwanja na sababu ya kuonyesha zake kukuru.
Na INAWEZEKANA kila mtu ana mpaka umalaya ndani yake akijipa uhuru,.... .... na si kweli limtu malaya hujifunza tu umalaya kutokea zero wakati linataka kuwa malaya NA HALIKUWA NA CHEMBECHEMBE ZA WAZO LA KUGAWA KIRAHISI LIKICHEKEWA TU tokea bado LINAFIKIRIA KILOKOLE , kama ukichunguza ubongo wa binadamu ufanyavyo kazi na kwa hilo ukapata NURU.:-(
TEKENYO LA HOJA Kwa kifupi :
Naamini tunavyokutananavyo katika MAISHA ikiwa ni mpaka hili la KUTONGOZWA na mpaka MWANADADA, ....
....... vifanyacho ni kuamsha TU sehemu ambayo tunayo tayari ndani yetu, ......
......kwa hiyo yule asiyeosha sehemu za siri kabla ya kutongozwa bado ni yule yule wakati ni MUME WA MTU na ana MAKENDE SAFI sikuhizi AU TU anaonekana msafi - katika USWAFI nikiwa na maana sehemu yake ilipalo swala lakujiswafi UTUKUFU imeamka/IMEAMSHWA TU siku hizi lakini alikuwa nayo tokea enzi za wakati habadili chupi wakati hajapata mke CATALYST wa mpaka MAKENDE usafi.
Nakatizia wazo hili HAPA!
Swali:
Kwani wewe kama MTANZANIA tokea ukubali mtongozo wa Rais KIKWETE unafikiri URAIS wake umekubadili kitu?
Unauhakika ukitongozwa ukakataa tatizo sio tu mtongozaji kakosea kukutongoza LABDA kwa kukupa kauli kibao wakati labda udhaifu wako ni vitendo kama vile vya kuliliwa ndio angalau ujisikie kumpa mtu cheo?
NIMEACHA MKUU na kumbuka HILI NI WAZO TUna lisikutishe hasa kama wewe unaamini kuwa baada ya kutongozwa ukakubali basi ULIBADILISHWA na mahusiano yako na LIMTU lilitokukubalisha.
Au tu nimuachie Ali Gna Shaggy katika -Me Julie[Tahadhari:kuna ujinga tani katika video hii kwa hiyo kama uko bize au ni zee la kukwazika unajuachakufanya!]
....WATU kibao wakiogopacho KULIKO VYOTE wala hakiko katika mfumo wa Mungu, Nyoka, N'ge, BABA, Ukimwi, Sehemu za siri kubwa za lijamaa au..........
Naamini kiogopwacho sana DUNIANI kinaweza kuvumbuliwa na swali:...
''HIVI WATU WENGINE WANANIFIKIRIAJE?'' a.k.a
''MAONI YA WATU WENGINE''.
Kwa ung'eng'e huu uoga ukondani ya hii PHOBIA iitwayo Allodoxaphobia au Fear of opinions.
Ingawa woga huu watu wengi hawautambui na hata UKIWAULIZA utastukia wajuacho AU WASTUKIACHO TU ukidadisi kuwa wanaogopa nini, watadai LABDA ni MENDE,....
....lakini UKWELI WENYEWE mimi naamini huu uoga wa MAONI YA WENGINE ni MKUBWA kiasi kikubwa na moja ya matatizo/ATHARI zake ni kulazimisha watu wasiishi AU KUFANYA kama wao kivyao ,na kusababisha MPAKA mwenye roho mbaya kujikuta ili kutimiza afikiriayo ni MAONI YA JAMII, anasomea UDAKTARI wakati wagonjwa wenyewe hawapendi.Au tu unawezakukuta mwenye kipaji cha UFAGIZI wa JIJI anajikuta ndio NESI wako wakati anaogopa damu na harufu za dawa kisa anaogopa tu kutumia kipaji chake kwa kuwa KIMAONI YA WATU kuwa mfagizi sio poa.:-(
Usipoangalia dume zima mpaka UNAWEZAKUOLEWA na dume lenzako kisa unaogopa MAONI YA JAMII UISHIYO au tu kusemwa vibaya,...
.... kama tu....
.......yawakutavyo AKINADADA WATUKUFU katika jamii ya BONGO waogopavyo kuachika katika ndoa ZIWASULUBUZO kisa woga wa MAONI ya NDUGU, Mchungaji, SHEKHE na bila kusahau MAONI YAWATISHAYO ZAIDI yaliyoko kwenye vicheko vya kipashkuna vya MASHOGA wa nyumba ya pili waendako kusukwa nywele.:-(
Kwa kifupi MAONI ni BALAA! Unaweza kujikuta maisha yako yote KAMA UNAVYOYANG'ANG'ANIA SASA HIVI mpaka ufikiriavyo yatakayo tokea MBINGUNI au JEHANAMU ukidedi/KUFA ,....
..... yote ni MAONI YA WENGINE ,......
......au kwa asilimia uzito bonge la tani YAMEATHIRIWA NA MAONI YA WENGINE!:-(
Swali:
Hujastukia binadamu hawaogopi Mungu KULIKO WAOGOPAVYO WATU WANAWAFIKIRIAJE ,ndio maana kila kona uiangaliayo watu ni FULU KUFANYA DHAMBI wajuazo ni dhambi chini ya mwavuli wa kudhani wafanyacho machoni mwa WENYE MAAONI NI BAAAB KUBWA, na mpaka hata wale waendao makanisani au misikitini wengi ni kwa ajili ya FULU KUJIONYESHA dini zinapanda hasa kama wako katika jamii zenye ustaarabu wa kinafiki wakujifanya KAMA NI MSTAARABU basi jifanye dini inapanda?
Unauhakika hata nguo uliyoivaa sasa hivi hukufikia kuivaa hiyo kwa kufikiria MAONI ya wengine watu yatakaa mkao gani katika kukufikiria?
NI HILO TU nilitakakugusia na unaruhusiwa KUNIBISHIA! JUMAPILI NJEMA!
Mie namsikiliza 2PAC katika-I wonder if Heaven's got a Ghetto.
Moja ya kitu kilichonisikitisha wiki hii kuhusu Watanzania,... .... kina uhusiano na MTANZANIA aliyeua mke DENMARK.
Kama hujui kisa hiki unaweza kukifuatilia katika website ya TANDENHAPA
Ingawa tukio zima ni la KUSIKITISHA, kitishacho ni kustukia baada ya kutembelea websites na CHAT ROOMS kadhaa kuwa kuna WATANZANIA ambao kirahisi KUKITOKEA MATATIZO huwageuka Watanzania wenzao kwa misingi ya kikabila.
Nimekutana na kuchat na watu ambao wamegeuza tatizo la Mtanzania huyu kuua MKE kuwa ni tatizo la Wasukuma. Nashangaa Watanzania ambao kirahisi hupenda kujishebedua kuwa Watanzania si wakabila WATANZANIA TUKISIFIWA KWA HILO , kirahisi kutenga watu kwa kufikiri mpaka jamaa ni kabila gani.:-(
Utashangaa kisa hiki kuwa kuna watu wanakitumia kuhalalisha kuwa kuna makabila ni wauaji kiasili kwa kuwa eti kuna ripoti za maalibino na vibibi vizee kuuawa mitaaa ya kwao.Na kitishalo kwa hilo ni jinsi ionyeshavyo watu waaminivyo sana msemo samaki mmoja akioza basi wote wameoza.:-( Na kwa mtazamo huo potofu naamini ukiachiwa utambulike kuwa ndio kweli yenyewe, BASI naamini kujikwamua kwa Tanzania na Watanzania kutabakia kuwa ALINACHA TU.
JAMANI tukumbuke tu kuwa UKABILA UPO SANA Tanzania na unawezashangaa ujitokezapo ,na kama wewe ni MTANZANIA USIJISAHAU kuwa pamoja na kupenda kabila lako basindio iwe ni misingi ya kudharau MAKABILA YA WENGINE.
Mimi naamini UKABILA si kitu kiwezacho kuwa msaada kwa Tanzania na kwa WATANZANIA sasa hivi!
Na JAMANI kumbukeni kuwa hakuna kitu kizuri kama umoja hasa wakati wa matatizo ingawa imezoeleka tu kuonyesha umoja WAKATI MAMBO NI SHWARI!
Na katika tukio hili la kuua mtu, tukumbuke kuwa tatizo sio USUKUMA au UTANZANIA kama unazingatia kuwa hili jambo ni binafsi. Na mambo binafsi ya kifamilia mtu wa nje kuyaelewa ni vigumu kwa kuwa KAMA WEWE sio MHUSIKA na huyaishi maisha ya mhusika, kumbuka UELEWAJI WAKO WA KITU UNAATHIRIWA na UDHAIFU wa kuwa unajaji kitu cha mwingine kwa kutumia uzoefu wa maisha yako ambayo hayafanani na unayemjaji MHUSIKA.
NI MTAZAMO TU WANGU katika swala baada ya kukerwa na UKABILA ULIOJITOKEZA katika kumjaji huyu MBONGO aliye.........:-(
Mungu amlaze pema MAREHEMU ! Mungu ibariki Tanzania!
Mie ngojea niendeelee kumsikiliza Warren G katika -Regulate
[Tahadhari: Katika kichwa cha habari sentensi ''NIPE YOTEYOTE, yote tu JAMANI!'' imebaniwa pua na Limdada zuuuri!:-(]
KIDOGO ni chachandu,.... .... na ikizidi kwa kawaida utavimbiwa.:-(
KIDOGO ni utundu,.... ..... ikizidi maana yake huweza kutafsirika kuwa umeharibikiwa.:-(
Na kijuacho ukubwa kwa kawaida KAMA ni tundu,.... ....basi kwa hilo si lazima mpaka tundu liwe KUINGIZWA limejaribiwa.:-(
Ila kwa kuwa Binadamu ni watundu,... ....DUNIA INAHARIBIKA SASA HIVI kwa kuwa TU mpaka binadamu wakijuacho kidogo wanakitaka kwa ukubwa na MAKUBWA YOTE KILAFI , na ndio maana wanaonja mpaka VYENYE SUMU VILIVYO tayari JARIBIWA.:-(
NALIKATIZIA HILI WAZO HAPA na unaruhusiwa kuliendeleza KIVYAKO MHESHIMIWA!:-(
Lakini swali KIDUCHU:
Unafikiri si kweli kuwa WALIOONJA KIDOGO na kujua ni tamu kwa kawaida hutaka makubwa yote ingawa wanajua kuwa hata asali ingawa tamu kuinywa, KUNYWA LITA kwa kawaida ni tofauti na kuilamba asali kidogo katika ujazo na KWALITI wa uupendao utamu?
SI unajua siri ya kilele cha utamu hupatikana kwa kuonja kidogo tu?
NIMEACHA na kumbuka hili ni wazo tu! KUMBUKA PIA kuwa KIJIWE HIKI cha MTAKATIFU Simon Kitururu sio YESU wala NYERERE kikukorokochoa!:-(
JUMAMOSI NJEMA Mheshimiwa OTHRONG'ONG'O!
Hebu basi tusukutue uchafu wa wazo kwa kumsikiliza M-Ivory Coast mdada Monique Seka akilainisha kwa ndude iitwayo-Okaman
Au tubaki naye tu Monique Seka afanye matusi katika kitu -Missounwa
[Tahadhari: Kama unajiheshimu unaruhusiwa kutosoma hii taralira!:-(]
Fumba macho ,....
.....halafu tafakari kama ungetaka kumuomba KIZALISHIO mtu kwa tumizi la burudani au la kuzalisha MGAGAGIGIKOKO msiyeelewana lugha, uhisi ni sauti NA NENO gani ungelitumia kumuelewesha katika mtongozo MGAGAGIGIKOKO asiye wa KIMANDENGO utakacho kitumbua SIO binamu ya andazi KITUMBUA.
Halafu fungua macho,....
.... na jaribu kutafakari kama unanjaa halafu ni ombaomba, ni sauti au vitendo GANI utatumia kuomba chakula KUTOKA KWA mtu msiyeelewana lugha hata kama chakula chenyewe UOMBACHO ni kitumbua KITUMBUA.
Swali:
Unafikiri UNAHITAJI YENYE MANENO lugha kama unahitaji kuwasiliana na ujuaye hamuelewani lugha ZA MANENO hata kama ujumbe ukupao nyege ya kutamka ni kumtusi tu Mwalimu Nyerere '' BICHWA kama mbwa''?
OK! NIMEACHA hili WAZO Mheshimiwa!
Ngojea tu ABETI MASIKINI arudishe utulivu na ustaarabu kwa kitu-Yamba Yamba
Au tu tena ABETI MASIKINI adunge kitu-Je suis fache
Na ni kweli,... ...wengi wasifiwao kwa akili NI kwa sababu TU wanasomea ambayo kwao kirahisi wangeyajua tu bila MWALIMU!:-(
Na ni kweli,....
.... karibu kila mtu kuna kitu KWAKE ni rahisi kama KUNYA TU na wala si vigumu kama KIWASUMBUAVYO WENGI CHA kujulia jinsi ya KUTAWADHA VIZURI baada ya kuachia TIMBA , ingawa haki ya nani hata katika hilo la STAILI YA KUCHAMBA VIZURI wengi hufikia UGWIJI bila msaada wa MWALIMU!:-(
Swali:
Unabisha?
Kwani unataka kusema BADO hujastukia KUWA mpaka wenye vipaji vya asili vya kusukuma mkokoteni wapotezavyo muda kusomea kusukuma mkokoteni hata kama UDHAIFU wao uhitajio SHULE uko katika kumridhisha mama watoto na KWA HILO hata siku moja haistukiwi labda SHULE bora kwao ingekuwa ni ya kuridhisha mke na sio ile waahangaikayo nayo wakati hawaihitaji SANA ya kusukuma mkokoteni?
Kwani hujastukia kama MFUMO usingekuwa UNA VYETI vihakikishiavyo watu kuwa KIBONGE KAENDA SHULE kuna wengi wenye DIGIRII za VYUO VIKUU elimu yao katika swala ni BOMBA LA KINDEGATENI?
HILI NI wazo tu KISHTOBE na wala usitishike! Ijumaa NA wikiendi njema MHESHIMIWA!
Hebu tupate tena ambacho kwa MAFISADI labda NI burudani kutoka TANZANIA kama iletwavyo na ile kitu -DARWIN's NIGHTMARE
Au tu hebu huyu Mbenini WALLY BADAROU atupe ile NDUDE roho ilipenda iitwayo - HI LIFE
Au tu Mkameruni BEBE MANGA amwage tena ndude roho ilipenda kwa jina-AMIO
......UJIKONDESHE kama huwa unakunwa na HIZI VITU NYOKO za kitafiti AMBAZO saa nyingine ni NYOKO kuzifuatilia na kuziamini....
What is prosperity, and how is it achieved?
Following a turbulent year marked by a global economic crisis, the Legatum Prosperity Index seeks to answer these two fundamental questions. It defines prosperity as both wealth and wellbeing, and finds that the most prosperous nations in the world are not necessarily those that have only a high GDP, but are those that also have happy, healthy, and free citizens.
How we created the Index
The Prosperity Index accounts for 90% of the world’s population and is based on years of statistical analysis and research of objective data and subjective responses to surveys. The data comprises 79 different variables organised into nine sub indexes – each identified as a foundation of long-term prosperity. A country’s performance in each sub-index is given a score, and the overall Prosperity Index rankings are produced by averaging the scores of the nine sub-indexes for each country. Those countries that perform well across each sub-index do best in the overall rankings.
The nine sub-indexes are:
Economic Fundamentals – a growing, sound economy that provides opportunities for wealth creation
Entrepreneurship and Innovation – an environment friendly to new enterprises and the commercialisation of new ideas
Democratic Institutions – transparent and accountable governing institutions that promote economic growth
Education – an accessible, high-quality educational system that fosters human development
Health – the physical wellbeing of the populace
Safety and Security – a safe environment in which people can pursue opportunity
Governance – an honest and effective government that preserves order and encourages productive citizenship
Personal Freedom – the degree to which individuals can choose the course of their lives
Social Capital – trustworthiness in relationships and strong communities
Rankings
Finland tops this year’s Index, with the United States ranking ninth, ahead of large European nations such as Britain, Germany and France, which all still make the top 20. Finland is narrowly ahead of Switzerland, Sweden and Denmark. Zimbabwe ranks last, following Yemen and Sudan.
TANZANIA kwa kuwa TOP TENI ya takoni OYEEE!:-(
AU tujibaraguze hatujali kwa kuangalia akinadada wakifundishwaGOLF na kudakwa na SEXY CAM katika- The Golf Course