Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LABDA kunahaja ya kuongelea UDINI Tanzania hasa kama ni kweli UDINI unaogopwa TANZANIA!:-(

>> Tuesday, November 30, 2010

Kwa kukwepa MADA za UDINI Tanzania,....

..... kunaweza kukawa kunachelewesha tu TATIZO ingawa hakuliondoi au KULITATUA tatizo la UDINI Tanzania.:-(


Swali:

  • Si kuna uwezekano kwa KUTOONGELEA tatizo haimaanishi ndio unatatua TATIZO kwa kuwa tu umefunga bakuli lako na UCHEMI kitu?


Ndio,....
.... kuna tabia ya KUOGOPA kuongelea mambo TANZANIA kwa kuhofia  ukiongelea vibaya  TUKIACHILIA DINI ,....
....labda hata CCM kuna kibano utapata au tu kulipandisha JAZBA tatizo ambalo INADHANIWA  usingelichokonoa lisingejitokeza.:-(



Ila kwa bahati MBAYA,....
.... inawezekana kwa kukwepa TOPIKI ndio kwanza unachangia UKUBWA wa tatizo ,.....
....na wala wakati huo HUTATUI tatizo.:-(


NI WAZO TU HILI!

Hebu Fally Ipupa na Krys wabadili tu wazo kwa-Droit chemin



Au tu P Square warudie tu- Ifunanya




Au tu Bracket na P Square wamalizie tu na -NO TIME

Read more...

Kuna mambo kama DINI na MAPENZI labda MSHINDI ni yule asiyetumia AKILI!:-(

Na labda ni KWELI,....
....kama mtu anatumia sana AKILI kupenda MTU,.....
.....afanyacho ni MAHESABU na wala sio KUPENDA.



Na ukifuatilia dini ,.....
....utastukia kuwa misingi yake ni IMANI ZAIDI kuliko uhalisia na ukweli wa dini,.....
.....kitu kifanyacho kila mtu aamini DINI yake ndio ya KWELI na za wengine KUNAKITU ZIMEPUNGUKIWA  kwa kuwa ,......

....labda ukweli wenyewe UKITUMIA AKILI ZA MKICHWA KIBINADAMU kinachoongelewa na DINI hakieleweki.:-(



Swali:

  • SI umestukia kila mtu hufagilia DINI YAKE zaidi kuwa ndio ipelekayo watu JEHANAMU ukikosea jinsi ya kuifuata?

  • Na si ushawahi kustukia KAMA UMEPENDA VIZURI MTU kwa kawaida wewe utakuwa hunajibu zuri lielewekalo kuwa ni KWANINI katika watu wote LIMPENZI lako KIBOGOYO kwake ndio umejifia?


Ndio,....
.....kuna mambo KUTUMIA AKILI ndio chanzo cha MATATIZO,......
....kwa kuwa usingetumia AKILI labda wala usingejua HAPA duniani umepungukiwa nini .:-(

Na kwa kutumia AKILI SANA katika kuingia undani sana wa DINI YAKO,......
....waweza kujikuta ndio wazidi KUJICHANGANYA uelewa wako wa HIYOHIYO dini,.....
....kitu kiwezacho kufanya AAMINIYE TU bila uchunguzi mwingi wa kitabu cha DINI ndiye ajisikiaye kuwa na uhakika sana kuna MBINGUNI na yeye huko atakwenda angalau kunywa mataputapu kisa hapa duniani apendacho sana zaidi ya GONGO wakati anasikiliza nyimbo za dini ni MATAPUTAPU.:-(


NI wazo tu hili MTAALAMU!
SIKU NJEMA MHESHIMIWA!



Hebu Coco Mbassi adinye - O Bi





Douleur aingie tu na- Nyouma Nyouma



Au tu na Ndedi Dibango amalizie tu na -Eyo Mè

Read more...

STAHA ya aliye na STAHA uchi!:-(

>> Monday, November 29, 2010

Kistaha ,...
....labda sio lazima ni STAHA!:-(

Swali:

  • Si unajua kuna WAHESHIMIANAO WENGI ambao kiheshima bado  kuna wakati wanakaliana UCHI kiheshima hata kama ni ki BABA na MAMA?


Ndio,...
...kiheshima KULIA inaweza kuwa kikweli ni KULIA ya KUSHOTO:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
JUMATATU NJEMA!




Hebu Lionel RICHIE afikirie bado ni JUMAPILI katika kinu-EASY



Lionel RICHIE asalimie tu kwa-HELLO




Au tu The Commodores wabadili tu mchezo kwa-BRICK HOUSE



Au tu Lionel Richie ajaribu kurudia ndude hiihii -Brick house




Bado nipo...:-(



Read more...

Ukichezea MITA BENDI labda zaweza kukusikilizisha mpaka REDIO ZA MATUSI badala ya redio ya SAUTI YA INJILI!:-(

>> Sunday, November 28, 2010

Na yote ya INJILI,...
...kama tu MATUSI yanawezekana.:-(




Na katika kutembelea KIBANDA cha kuku,...
.... kumbuka tu kuwa kuna uwezekano mkubwa wakati huo  kukanyaga MAVI YA KUKU.:-(






Swali:
  • Hivi MHESHIMIWA ushawahi kuchezea MITA BENDI katika kutafuta MATOKEO?
Ndio,...
...na wakati unawasiwasi na REDIO TUMAINI,...
...unaweza KIMITABENDI kupata mpaka  BBC halafu ghafla UKASTUKIA  utakachosikia  bado KWENYE bbc, cnn,TBC ..... mpaka FOX  labda ni aina  TU tofautitofauti  ZILEZILE za harufu za UCHI wakati unachojaribu NI kujisahaulisha uwezekano kuwa UNACHOAMINI ni kuwa harufu halisi ya UCHI ni kama samaki aliyeoza a.k.a harufu mbaya katika kujiaminisha kwakuwa TAMU labda ni lazima ikinuna ITABIDI NDUDE inukie vizuri.:-(



NI HILO TU Mheshimiwa mwenye KIPENGELE!:-(


Hebu ghafla Eric B. na Rakim waingie ghafla na - Don't Sweat The Technique



Au tu hebu SEAN PAUL abadili mfereji kwa -Temperature



Au tu SEAN PAUL aunguze kidude kwa-We Be Burning




Ndio,...
...kwenye pati hii SEAN PAUL alikuwepo live pia .....






























































Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP