Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

MUNGU! Wakati bado simuelewi hata BINADAMU ULIYEMUUMBA avaae nguo SIKU HIZI!:-(

>> Friday, July 31, 2009

Nizidishie imani MUNGU,...
....ili nizidi kuelewa imani MUNGU.


Labda nitakuelewa MUNGU,...
.....kama utakavyo tukuelewe MUNGU.

Kwa kuwa wengi watuuziao zisemekanazo ni zako dini MUNGU,...
.....wamekuwa wengi kama zao watuuziazo dini MUNGU.

Na kwa upungufu wetu wa kibinadamu MUNGU,...
... twatoana mpaka DAMU katika kujazia mapungufu ya imani kibinadamu MUNGU.

NI hilo tu MUNGU!


NA ijumaa NA Wikiendi NJEMA kwenu wote WADAU wa BLOGU HII !


Ngojea kiumbe Phil Collins atusaidie kusubiria baadaye kwa kitu- Another day in Paradise


Au tu kijana aliyetutoka Michael Jackson atupe-Man in the Mirror

Read more...

Kwa waogopao MDUDU bila kuogopa LISILO na macho DUDU!:-(

Wapo wapendao kukwaa kwa kionjeo DUDU,...
.... na inasikitisha KWAKUWA inasemekana ndio wengi wapatao MDUDU!:-(


Eti hawaogopi DUDU,...
... kwa kuwa katika SHUGHULI walikubuhu tokea shule ya VIDUDU.:-(


Eti wengine ni MADUME WAZIMA ambao wana DUDU,...
... lakini eti ni kweli NAO wajisikia angalau kwa nyuma kupewa DUDU.:-)


Na siwajaji hawa madume WAPENDA DUDU wenye DUDU,...
.... kwa kuwa yao SIYAJUI VIZURI na jamii yenyewe imefanya wengi wao wajifiche ambao labda ni wetu tuwaheshimuo na si kwa kuogopa MDUDU.


Lakini kumbuka likimtemea mtu DUDU,...
...wapo wadaio hunyonya ENEO kama embe sindano,...
.... wakiamini huathiriki kwa KUNYWA togwa yake hata kama kokwa lina MDUDU.:-(

Wengine KIDUDE waringishia wenye DUDU,....
..... wasahau kuwa hata kama kuna vizuia MZALISHO labda bado HIVYO havizuii MDUDU.

Lakini ni chaguo lako mpenda DUDU,....
.... lakini JUA tu wakati unachekelea dudu, kuna MDUDU!:-(

TUNAKUMBUSHANA TU MHESHIMIWA na wala sileti za KULETA!:-(
Swali:
  • AU?
  • Hivi bado SI unakumbuka kuna UKIMWI a.k.a MDUDU mdau HATA wakati unacheza nayo?
NI HILO TU!:-(


Ngojea Cristofer a RANT kuhusu ambacho katika malezi sijui kama kinatokea bado Bongo katika-Purity Ball and Promise Ring..

Au tu KINGWENDU FAMILY warudie -Huyu DEMU MAPEPE..

Read more...

Tuangalie tena SWALA ZIMA la kuhalalisha KUFANYA MATUSI ili iwe ni TENDO LA NDOA.

>> Thursday, July 30, 2009

[Tahadhari: stori hii haikufai kama mtoto au hujawahi kufanya matusi!]


NI binadamu na wala si tu BINAMU ambaye kwa binadamu ni nyama ya HAMU,...
....na hamu ni zilezile ingawa hutofautiana tu pale HAMU zinaposuuzwa kwa VITENDO.:-(


NA kufanya matusi ni kitendo KILEKILE kiletwacho na HAMU,...
...na inasemekana ni haramu na uhalalisho hutofautiana jamii MPAKA jamii kwa VITENDO.


NA wakati jamii ya leo NI kama ILEILE ya jana yenye HAMU,...
....kifikira uhalalisho wa leo wa kufanya matusi umezoeleka MPAKA jamii haina uhakika watofauti ya matusi na CHA NDOA KITENDO.


Na siku hizi kukutana na bikira ni nadra hata kama una hiyo HAMU,...
...na sasa katika jamii bikira ni yule ambaye hujafanya naye matusi kabla na sasa mfanyacho ni CHA NDOA KITENDO.

NA kumbuka siku hizi NI HATARI hata kama ni kweli UNAHAMU,...
...jamii imebadilika mpaka WENGI waliofunga ndoa wafanyacho bado ni MATUSI kwa kushindwa kutofautisha utamu wa MATUSI na THAWABU za CHA NDOA KITENDO.

Na kumbuka UTAPIGIWA makofi SIKU YA NDOA hata na boyfriend wa mke wako mwenye ya mke wako HAMU,...
....na wewe MWENYEWE na labda BADO waingia chumbani kufanya YALEYALE ila leo kwa kuwa ni ruksa ufanyacho chaitwa CHA NDOA KITENDO.


NA yasemekana KITANDA HAKIZAI HARAMU hata kama wakati unakula URODA kuzaa mtoto huna HAMU,...
..... na kumbuka hata kama mimba si yako mtoto asipofanana na wewe basi kafanana na MPWA WAKE Moshi MAJENGO au tu babu mzaa babu wa upande wauliyefanyanaye KITENDO.


DUH Nalikatiza wazo hili NUKSI na Shenzi Taipu!

Kumbuka ni wazo tu !

Swali:
  • Unafikiri ni ASILIMIA NGAPI katika jamii ya leo hualalisha MATUMIZI YA KITENGO kabla ya kuhalalishwa kitendo?
  • Hivi ni baraka na pete kweli ndio hugeuza kufanya matusi liwe tendo la ndoa?
  • Hivi si labda tendo la ndoa ni matusi tu katika jamii isiyojua ndoa?
  • Unafikiri ndoa sio AINA YA UBAHIRI WANGU wakutaka yangu iwe yangu PEKE YANGU na nyie wengine msinionjee?

Basi bwana nakupa siri nyingine kuwa sababu ya kuacha topiki hiii ni kwa sababu IMENISHINDA labda ndio maana unaweza ukakuta WAJANJA swala hili kwao Mtaalamu hata wa KONDOMU au tu NDOA eti ni Padre au PAPA wa ROMA ambao wote isemekanavyo hawajawahi kuonja MATUSI wala CHA NDOA KITENDO. HALAFU eti malaya mjuzi wa swala na aliyeshindwa ndoa kadhaa hasikilizwi akiongelea SOMO!:-(

Kwa mara nyingine NAACHA!
SIKU NJEMA MHESHIMIWA!
Na BWANA na BIBI WASIFIWE!

Au tuangalie hawa jamaa wanaopenda kufanya tendo la ndoa na WANYAMA katika-Two Women Describe Losing Their Virginity To a DOG!!


Au tu nimrudie Omar Kopa aongelee-UNYAGO




...

Read more...

Nikome BABU WEE! Mie SILI KWAKO!:-(

Na labda ni vizuri huli KWANGU,...
.....labda unajitegemea.

Na labda kuwa na wasiwasi kwa kuwa sili KWAKO,...
....labda sikuhitaji!:-(


Na tuwe na wasiwasi wa afya ya jamii kama imefikia tunawaza kuwa NANI ala KWA NANI,...
....labda maana yake jamiii IMEZIDIWA MUDA WA MAJUNGU na KAZI inahitaji .

Na tuwe na wasi wasi kama sijali yako kwa kuwa si YANGU,...
...labda maana yake hujali pia YANGU kwa kuwa una YAKO na kama ni kweli kujifunza UTU tunahitaji!:-(

Swali:
  • Nani kakwambia usiwe na wasiwasi kwa kuwa sili kwako?
  • Huwa ni kawaida kwako kuoanisha WASIWASI na MLO a.k.a KUPIGA TONGE?

NIWAZO TU KIJEBA wala usiwashwe!

Hebu twende tena Cape Verde kukutana na Lura alete-Na ri NA


Au tubaki tu Afrika hapahapa Cape Verde Calu de Brava adai-Terra Love

Read more...

Pamoja na yote HALI HALISI bado ni SIRI!

>> Wednesday, July 29, 2009

Na kama HALI HALISI,.....
.....isingekuwa ni SIRI labda watu wote wangeshastukia ni nini KITU HALISI!

Ndio!Pamoja na kuwa kufa na njaa NAKO ni HALI HALISI,....
.....na pia wengi WAWASAIDIAO WAFAO NJAA hufanya hivyo kwa kujisadia wenyewe labda KIMSHAHARA wa N.G.O au tu KIKUSUUZA ZAO ROHO wajisikie ni watu wazuri ,na hiyo pia NI HALI HALISI.:-(


Na wakati UNAKUA kihalisi,...
... labda hustukii ukweli kuwa si kweli wazazi wanataka unywe chai na kiporo cha ugali kwa mlenda wa jana kwakuwa labda MSHAHARA wa WAZAZI HAUTOSHI na hiyo ndio HALI HALISI.:-(


Na labda isingekuwa siri HALI HALISI,...
.... ungekuwa unajisikia kufakufa sasa hivi UNGEJUA HALIHALISI kama hali yako halisi sasa hivi haikusikilizishi kufakufa kwa kuwa kwetu sisi ukitukenulia meno tunahisi unafuraha HATA KAMA hiyo kwako si HALI HALISI.

Nalikatiza wazo HALISI,...
... usije mpaka ukaanza kuwastukia ni WATU wangapi hata ukiwaza unaweza kuwahukumu kuwa washadakwa na SHETANI na labda UKWELI NI KWAMBA wako karibu zaidi yako na MUNGU na hiyo ndio HALI HALISI.:-(

Swali:

  • Siriasli unafikiri ni watoto wangapi kwa hali halisi hustukia labda maisha waishiyo ni kwa sababu wazazi wao wamechacha na hiyo ndio hali halisi?

  • Kwa hali halisi unayoifahamu unafikiri ni MARAFIKI zako au ndugu zako wangapi wana UKIMWI au tuseme tu MINYOO na hiyo ndio hali halisi?

  • Unauhakika kuna mtu hata mmoja hapa duniani ajuaye yote kuhusu YAKO hali HALISI?


NAKATIZA WAZO MHESHIMIWA lakini TUKO PAMOJA MKUU!
Hebu twende kidogo UK tukacheki WACHAWI wakiomba kazi na hii ni hali HALISI...



Au tupitie tu Mozambique tukutane na MARIZA adai-Africa Calling[Meu FADO Meu]



Au tubaki tu Mozambique Djaaka adai-Djogoro

Read more...

Swala zima la KUANZA UPYA!

Kwanza,...
.... ukiamka tu kuna uwezekano hakuna UJANJA zaidi ya kulazimika kuanza UPYA.:-(


Pili,...
....kama ulijaribu na kuumia KWA KUKATA TAMAA inaweza ikawa ni KUKATA TAMAA unako KUANZISHA UPYA:-(

Tatu,...
.... labda ni kweli safari iliyopita NANIHII ilikosewa kama hutaki kukiri uwezekano kuwa ULIKOSEA,.........................
....SASA kwa nini usijiunge nami Mtakatifu Simon Kitururu /Muzee wa Kukosea TUANZE UPYA?

Nne,...
..... kumbuka hata kama ulipatia jana hiyo ilikuwa JANA leo mchezo hata uleule ni MPYA.:-(

Swali:
  • AU unasemaje katika swala zima la katika maisha ,TUANZE UPYA au TUKATE TAMAA?


NIMEACHA wazo halafu SAMAHANI KIDOGO MHESHIMIWA naenda kukojoa KIDOGO!:-(


Unaweza kumsikiliza Peter Tosh akikumbusha katika - Pick Myself UP

Read more...

STAREHE za watu za kuumiza roho MTU!:-(

Labda ni ubinadamu kwa binadamu kuwa na hamu ya kuumiza MTU!

Na kiubinadamu kuna mtu anahalalisha ni nani marafiki na nani maadui hata katika kuchagua wa kumuumiza MTU!

Cha ajabu hata undugu tukiachia mbali urafiki waweza ukawa ndio uletao nafasi ya mtu kuumiza MTU.


Ni vizuri kukumbuka tu,...
.....MKUKI kwa nguruwe unaumiza hata nguruwe ingawa kuna mtu hutaka kuhalalaisha ya mkuki kuwa mchungu tu kwa MTU.

Swali:
  • AU?
  • Hivi ukijisachi kumoyo hautakuta angalau chembechembe za nyege za kutaka kuumiza MTU roho?


Ni wazo tu MUZEE WA KUPEKECHA na wala USITISHIKE!

Hebu Fatboy SLim abadili hali ya hewa kwa kitu-Praise You


Au tu FAT man Scoop amalizie kwa-Put Ur Hands UP

Read more...

Haloo mpenzi NATAKA SITAKI, sogea basi ili NISIJE anza mpaka FIKIRIA jinsi ya KUKUDANGANYA mpenzi!

>> Tuesday, July 28, 2009

[Tahadhari:sina uhakika na maudhui ya topiki hii leo mawazoni endelea kuisoma kwa uamuzi wako tu mi sikushiki KIBINDO uisome!:-(]

Kwa Mpenzi TAMUTAMU,....

Najua NIA yangu UNAIJUA,....
... ingawa NAHISI wadhani ni ustaarabu kwako nihahe kwanza kwa kuwa hutaki tupitie NJIA YA MKATO.


Sogea basi mpenzi kivulini ili tusiungue JUA,....
.... na unavyochukua muda nashindwa mwenzio kuacha KULIANDAA NENO ili angalau USINIJIBU KWA MKATO.


Kumbuka mpenzi INACHOSHA ukiringiwa sana na nahisi hilo UNAJUA,....
.... kumbuka hata samaki siwapendi na unanifanya katika kwako kujipendekeza nimeanza kumsifia mpaka SATO.

Na ukizidisha NATAKA SITAKI unajua,...
...siku hizi kuna wafanyao kisasi kwa kukupata wakati waliacha kukutaka na hapa siongelei KIDALI -PO.


Kama hunitaki Mpenzi unajua,...
.... si vizuri kunifanya nihahe wakati wangu udhaifu waujua naKIRI kama wajua hutaki kunigawia kitamutamu KIPATO.


Ushaniingiza DHAMBI unajua,...
....au wataka nianze kutubu wakati kitendo chenyewe ni penzi na ni penzi tu lifanyalo udhani nina MCHECHETO.

NTAKUDANGANYA unajua,...
.... lakini kwanini nikudanganye wakati nina uhakika ukijua ukweli UTAJUA nachokuandalia ni zaidi ya KITO?


DUH naacha WAZO halafu hapa NAKIRI simuongelei yoyote maalumu zaidi ya leo kuingiwa hili wazo baada ya KUSHUHUDIA jamaa likimwaga kauli!


Swali:
  • Hivi ukimpata mpenzi kwa njia za uongo maana yake penzi lenyewe ni la uongo?

  • Unauhakika hujadanganya katika kumlenga mtu hata kwa kujipodoa wakati chini ya kipodozi ngozi mbaaaaya?

DUH NAACHA na ni wazo tu MKUU WA MASWALA KUMBUKA!


Ngojea EDDY MURPHY naye aongelee wake mtazamo katika-CHEATING[Tahadhari : Lugha chafu na labda si stori ya watoto kuchungulia katika mila fulani!Hapa na maanisha kama mtoto au utakwazika sikushauri ucheki kideo hiki!:-(]



Au tu Simply Red wadai- If U don't know me by NOW..

Read more...

labda ni WIZI MTUPU!:-(

Sadaka,...
.... kama ukifuatilia ziendako SADAKA.

Ukweli,...
.... ukifuatilia BAADHI YA NIA za aliyeamua KUKUAMBIA UKWELI.




Kupendeza,....
.... ukifikiria USAHAULISHWAVYO labda aliyependeza bado ananuka MAENEO kwa kuwa tu eti leo KAPENDEZA.


UONGO,...
.... ukifikiria labda umeepushwa kustukia USHALIZWA lakini watembea kifua mbele kwa kutostukia udhaniayo ni kweli karibu yote ni UONGO.


YA WEWE,...
.... kama yanakusahaulisha BINADAMU WOTE tunahusiana kwa kuwa unakazania YA WEWE.


YANGU,...
.... kama yamenisahaulisha twafa twayaacha na labda ukweli ni kwamba DUNIANI hakuna chochote kwa asilimia mia nawezasema si CHAKO na ni CHANGU.


Wizi,....
.....ukikumbuka VINGI VIIBWAVYO havina msaada kwa MWIZI!:-(

DUH!
Swali:
  • Unakumbuka aliyezoea kuiba husahau afanyacho ni WIZI?
NI wazo tu MHESHIMIWA na nakutakia kila lakheri katika SIKU YAKO Mkurugenzi!


Hebu sie wengine tuendelee na THE TRIBE CALLED QUEST katika-Can I kick it



Au tupate tu LAPDANCE kutoka kwa NERD

Read more...

UTAAHIRA wa ALIYEPENDEZA!

>> Monday, July 27, 2009

Adhaniaye KAPENDEZA,...
...anaweza akakusumbua HALAFU labda jeuri yote HIYO ni kwakuwa ETI LEO kavaa KIBWAYA.:-(


Na mwenye kutaka KUONGEA kwa VAZI,....
.... kwako ANAWEZA akawa hakutishi KWA KUWA kwako alichovaa ni MIDABWADA hata kama WEWE kama MIMI hatuna uhakika chupi aliyo vaa HAIJAPWAYA.:-(


Na kama UNASIFIWA umependeza,....
.... jaribu KUKUMBUKA ufinyu wa SWALA ZIMA la KUPENDEZA katika DUNIA HII yenye ufinyu wa kujua ni NINI MUHIMU mpaka unaweza fikiri LABDA BINADAMU BICHWA KUBWA na ajazavyo dunia ni UJINGA na LABDA katika kitengo cha BICHWA KUBWA ni kweli ubongo UNAPWAYA.:-(



NI wazo tu MKUU WA KITENGO na wala USITISHIKE!


Swali:
  • Katika swala la BICHWA KUBWA ubongo unapwaya unafikiri najiongelea mimi, wewe au kama kawaida tudai ni YULE?

NARUDIA kuwa hili ni WAZO TU KISHTOBE au MUZEE wa KUPARAMIA !


Ngojea ni muachie mdau Fally IPUPA aongeleee-AssociƩ



Au tu Fally aongelee -Bakanja

Read more...

SABABU za KUMPENDA msichana MZURI halafu unajua ni MJINGA!{Samahani : NI katika KIUME point of VYUU!:-(]

Mwanamke MWEREVU labda anaweza kukukumbusha MAMA YAKO!:-(


Halafu MWANAMKE mwerevu na ana MIAKILI KEDEKEDE ukileta za kuleta anaweza KUKUNYIMA na akajazia shughuli kwa kukutukania mpaka MAMA YAKO!:-(


Swali:
  • Kwani ni kweli wakati unashughulikia YA UNYUMBA wewe mwenye akili ni kweli UNAFIKIRI huwa UNATUMIA AKILI SANA?

NIMEACHA wazo !


Hebu twende tena KAMERUNI kukutana tena na Richard Bona aninyanyase tena-



Au tu tubakie tu tena KAMERUNI Manu DIbango aendeleze kuninyanyasa katika kitu-NEW BELL

ASANTENI WADAU WOTE pamoja na hawa ambao HAWAKUNITENGA juzi ya jana!:-(



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket




Photobucket








Photobucket



Photobucket


Photobucket




Photobucket




Photobucket









Photobucket




Photobucket



Photobucket







Photobucket



Photobucket



Photobucket








Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket









Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket






Photobucket




Photobucket





Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket






Photobucket














Photobucket







Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket

Read more...

Wakati tunaendelea kuangalia UWEZEKANO wa kuwa LABDA suruali ni CHUPI ndefu tu!:-(

>> Saturday, July 25, 2009

Na kabla hatujaangalia hata UWEZEKANO wakuwa KANZU ni GAUNI,...
...labda tukumbuke tulizaliwa UCHI.

Na wakati tunajaribu kujadili wavaavyo WAHUNI,...
.... labda TUKUMBUKE tu achaguaye nguo kwa nia ya zaidi ya KUJISITIRI huyo kashatatua tatizo la KUJISITIRI na kwa staili zake za kuvaanguo usishangae akitembea UCHI.:-(


Na labda ni uhuni,....
....kama sio kujilimbikizia MAVAZI wakati tukifumba macho siye wengine kwa shahuku na IMAJINESHENI labda BADO twakuona uko UCHI.

Na katika madai ya kujitunzia heshima au tu kuonyesha UALIWATANI,...
...Padre mvaa JOHO na SHEKHE mvaa kanzu hata kama jichoni mwako yote ni aina tu ya magauni YA HESHIMA , waweza kosa kazi sehemu ukiwaiga vazi sehemu waungwana waombeazo kazi na suti au tu pale kwa WAUZA MWILI ambapo ujanja ni kutembea UCHI.


Na labda ujanja ni kila sehemu na vazi lake MUUMINI,...
.... lakini ukitimiza hilo la kujali MITINDO YA NGUO labda maana yake NGUO kwako umuhimu wake si TENA kuficha UCHI.

Swali:

  • AU?

NI wazo tu MKURUGENZI na WALA Usitishike!
SIKU NJEMA ALWATANI!


Hebu Talib Kweli anisaidie kidogo kibao-Niggas lie a lot

Au tu Notorious BIG azungumzie tena ya - Big Poppa

Read more...

Wakati tuna wasiwasi na HEKIMA za UJINGA wa MWENYE AKILI TIMAMU!:-(

Kumbuka MWENYE akili timamu,...
.... maana yake LABDA TU ni yule atumiaye akili tusiujue ujinga wake ANAOUKWEPA.

Na labda WENYE akili SANA timamu,...
.... NDIO hutumia zaidi akili TUSISTUKIE ukubwa wa asilimia ya ujinga wao WALIOTUFICHA ndio maana hatuujui INGAWA labda bado HAWAJAUKWEPA.


Na katika KUUANGALIA wasiwasi wa KUOGOPA kuonekana wajinga wa wenye akili timamu,...
... mpaka MWENYE AKILI anaweza kusahau kuwa KAMA UNAAKILI huwa unajijua tu UNAAKILI hata wakati unafanya ujinga NA HILO huwezi KULIKWEPA.:-(

Na hakuna mwenye akili timamu,...
.... ambaye hana ujinga na ndio maana VITA YA KUFUTA UJINGA kama UNA AKILI huwezi kamwe KUIKWEPA.

Swali:
  • Unabisha?
  • Unakumbuka kuwa kama mwerevu anajisomea kinamna anakiri kuwa yeye bado MJINGA?
  • Halafu unakumbuka kuwa KUNAUWEZEKANO taahira ndiye hutumia akili sana kuhakikishia UMATI yeye sio MJINGA?
  • Unafikiri mwenye akili huhitaji kukumbushwa anaakili ili atumie akili?

NIMEACHA na NI WAZO tu MHESHIMIWA!

Ngojea Nina Simone abadilishe hali ya hewa kwa kitu- My baby just cares for Me




Au tu James Brown na Lenny Kravitz wakumbushe- Papa's got Brand new BAG


Read more...

Hivi BLOGU ni NINI?

Swali:

  • Unakumbuka?



Au tu Gil Scot Heron akumbushe- The revolution will not be Televised


Au tu Grandmaster Flash & The furious Five walete-The Message

Read more...

Udhaifu wa hotuba NZURI kama tu MAHUBIRI MAZURI!

>> Friday, July 24, 2009

Hotuba nzuri LABDA haina cha zaidi,....
.... kwa kuwa HAKUNA cha zaidi kikumbukwacho ZAIDI YA KUWA hotuba ilikuwa nzuri .

UNAWEZA kunibishia zaidi,....
...lakini YALIYOMO kwenye hotuba huwa hayakumbukwi hata kama mazuri.

NDIO!
Labda Hotuba ni maneno tu na hakuna cha zaidi,....
.....na kama kungekuwa na cha zaidi mbona HATUJIFUNZI hayo mazuri kutoka kwenye HIZO zidaiwazo NI hotuba NZURI?
Swali:
  • Pamoja na hotuba au mahubiri mabaya kudaiwa kuwa huwa hayakumbukwi, unafikiri ni nani anakumbuka hotuba nzuri?
  • Unafikiri huwa unakumbuka asilimia ngapi ya yaliyomo hata kwenye kitabu udaicho ni kizuri?
Kuna hawa WATU wako mawazoni mwangu leo na labda YALIYOMO katika waongeacho hakuna chochote cha zaidi ndio maana huwa hatukumbuki waliongea nini mara tu baada ya kudai tuliwasikia wakiongea!:-(

Hebu tuanze na Iddi Amini DADA....


Halafu huyu jamaa ajulikanaye kama Mwalimu Nyerere.....


Halafu kuna huyu MADIBA...


Halafu kuna huyu OBAMA....



IJUMAA na WIKIENDI njema MHESHIMIWA!

Read more...

Tatizo la kudai MWALIMU ni MZURI kwakuwa ANARAHISISHA kuelewa!

Binadamu ni mvivu ndio maana asilimia kubwa ya yamzungukayo HAYAELEWI

Na ukimpa nafasi atakuelezea kwanini HAELEWI.

Utasikia eti kitabu ni kibaya kwa kuwa HATUKIELEWI.

AU tu Mwalimu ni MBAYA kwa kuwa HATUMUELEWI.


Labda tukumbuke tu LABDA ni MWANAFUNZI ndio MBOVU kama HAELEWI.


Na tukumbuke tu kuwa WENGI wajuao sana ndio ambao kirahisi HATUWAELEWI.


Na kama unampenda Mwalimu kwa kurahisisha SOMO usishangae kujikuta mengi magumu HUYAELEWI.

NI wazo tu KINGUNGE na wala HUU sio MSAAFU!


Hebu tuulizwe- NAni ni Mwalimu wa MAPENZI....


Au tupate wimbo wa Omar Kopa -UNYAGO

Read more...

Kama BADO hujawahi kufikiria kula PANYA!

Kuna uwezekano Bado hujawahi kuumwa njaa VIZURI!:-(


Ni hilo tu nilitaka kukukumbusha Mheshimiwa!

Read more...

CHAKUKUMBUKA!

>> Thursday, July 23, 2009

Ni muhimu KUSAHAU,...

.... hata kama ni ujanja UKIKUMBUKA.


Na kwa kuwa TUNASAHAU,....
... LABDA ndio maana tunarudia hata yaumizayo tusiyo vizuri KUMBUKA.


Na kama leo UTASAHAU,...
.... labda kuna utakayefikiri baadaye ni JINIASI kwakuwa eti ANAKUMBUKA.:-(


Na unaweza kwa kula njegere UKASAHAU,...
... lakini kumbuka mtupa maganda ATAKUMBUKA.:-(

Swali:
  • Unakumbuka LABDA kuna jambo ulikuwa unalikumbuka miaka yote na ni leo hii umelisahau?


NAACHA wazo au tu Ujinga kama kwako ni UJINGA niandikacho katika BLOGU hii Mheshimiwa!:-(

SIKU NJEMA lakini MHESHIMIWA!


DUH ngojea Ochestra Makassy waongelee- Mosese



ASANTENI SANA Wadau ambao hamnichoki kama PAPAA Martin Mtefu,TOMMY, Peter na Marwaan ambao ni hawa hapa ndani ya baadhi ya picha hizi zangu...:-(

Photobucket




Photobucket






Photobucket










Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket





Photobucket



Photobucket

Au tu Lord Kitchener amalizie kwa kuongelea MENDE katika- KAKA ROACH

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP