Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tatizo la kudai MWALIMU ni MZURI kwakuwa ANARAHISISHA kuelewa!

>> Friday, July 24, 2009

Binadamu ni mvivu ndio maana asilimia kubwa ya yamzungukayo HAYAELEWI

Na ukimpa nafasi atakuelezea kwanini HAELEWI.

Utasikia eti kitabu ni kibaya kwa kuwa HATUKIELEWI.

AU tu Mwalimu ni MBAYA kwa kuwa HATUMUELEWI.


Labda tukumbuke tu LABDA ni MWANAFUNZI ndio MBOVU kama HAELEWI.


Na tukumbuke tu kuwa WENGI wajuao sana ndio ambao kirahisi HATUWAELEWI.


Na kama unampenda Mwalimu kwa kurahisisha SOMO usishangae kujikuta mengi magumu HUYAELEWI.

NI wazo tu KINGUNGE na wala HUU sio MSAAFU!


Hebu tuulizwe- NAni ni Mwalimu wa MAPENZI....


Au tupate wimbo wa Omar Kopa -UNYAGO

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Fadhy Mtanga 9:07 am  

Sasa kama mwalimu harahisishi uelewa wangu nimpende wa kazi gani? Kila mutu ya bantu napenda mambo rahisi rahisi.

Yasinta Ngonyani 7:39 pm  

Kazi kwelikweli Duh!!

Simon Kitururu 1:15 pm  

@Papaa Fadhy: :-)
@Dada Yasinta: :-(

Christian Bwaya 3:52 pm  

Nakubaliana na wewe kihivi: Mwalimu mzuri harahisishi, anakufanya utumie akili vizuri.

Kama una mwalimu anayekurahisishia, hiyo ni hasara kwa sababu utaendelea kuwa mjinga wa yaliyo magumu.

Tafakari nzuri Mkodao.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP