Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Habari usizohitaji KUZIJUA,...

>> Saturday, April 30, 2011

... inawezekana ndio HABARI zijaazo MAGAZETINI , radioni na kwenye LITIVII lako MKUU!



Swali:
  • SI inajulikana MAISHANI labda ni machache sana uyahitajiyo ili UISHI ndiyo yapewayo KIPAUMBELE na vyombo vya HABARI?
  • Kwani unakumbuka mangapi uliyojifunza kwenye HABARI ni kweli yamekuwa na mchango muhimu sana ambao usingeweza KUISHI bila kuyafahamu HAYO?


Ndio,...
.....DUNIA na WANADAMu walikuwepo MIAKA mingi kabla ya VYOMBO vya habari ,...
... kuingilia shughuli ya KUBREINIWOSHI  watu kuwa kitu kikiwa kwenye TAARIFA zao za HABARI ni muhimu na labda ni ujanja kukijua!:-(


Ndio,...
.... kama cha MUHIMU kwako ni MAGIMBI kwa MBIRIMBI ambavyo TAARIFA za HABARI huziruka,...
.... si labda stori za vita za akina GADDAFI au tu zile za Prinsi William amuoa KATE katika maisha yako si hazikusaidii kitu?


Ndio,....
....labda katika SIKU nzima ,....
.... vifikiwavyo ni HABARI,...
... sio HABARI muhimu kama zidhaniwavyo!



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA lenye udhaifu fulanifulani tu  ila SASA mie NIFANYEJE!:-(


Hebu tu badili wazo kwa kusikiliza ndude kutoka kwa Sandra Nkake ile- Happy





Au tu tugewe pia

-Jazz Fusion Cantelope Island



Read more...

MTU alichojifunza UTOTONI chaweza kuwa ndio kinalemaza ya UKUBWANI hata yale ya kuhusudu NGURUKA lakini sio DAGAA!:-(

>> Friday, April 29, 2011

Nilichojifunza UTOTONI,...
... haki ya nani chaweza kuwa kinalemaza UKUBWA WANGU!:-(


Na ulichojifunza UTOTONI,...
... kinaweza kuwa ndicho kinacho CHORA RAMANI ya uzungukayo nayo UKUBWANI katika UFANYAYO, upendayo au hata UAMINIYO yale ya ni njia gani unasadiki kirahisi ndio inapeleka watu kwa MUNGU.:-(

Swali:
  • AU?

Ndio,...
... labda hata upenzi wako wa UGALI kuliko WALI,....
.... mpaka uchaguzi wako wa MALAYA/changudoa gani utalipia HUDUMA za CHAPUCHAPU kwenye GESTI bubu KAMA IKIBIDI na   kama unahisi haitastukiwa na JAMII ijajio WANUNUZI wa HUDUMA za CHAKULA CHA USIKU  kwa kuwa wewe ni MHESHIMIWA,...
... vyote ni matunda ya ulivyojifunza tokea UTOTONI!:-(



Ni wazo tu hili MKUU!
Ijumaa na WIKIENDI njema!

PS:
Niko Norrkƶping -SWEDEN kwa muda NAHANGAIKIA tu MAISHA kwa hiyo kama uko mitaa hii tuwasiliane!


Katika kubadili wazo :

Hebu Offside Trick wakiwa na AT warudie-Mduara uko Uwanjani



Au tu OffSide Trick Ft AT wanun'gunike pia  ya kuhusu aliwavyo  - Samaki


Ngojea tu Offside Trick amalizie tu kwa - Cheza


Read more...

Mipaka ya BINADAMU,....

... kwa kawaida inawekwa na BINADAMU hasa atafsirivyo VITU.


Na mpaka hata wa NCHI waishizo BINADAMU,....
.... kama mipaka ya nini UKIVUKA hata KIFIKIRA unaonekana umevuka MPAKA,....
.... kwa kuwa inawekwa na BINADAMU,....
.... labda kwa BINADAMU hivyo sio vitu vya KUDUMU!:-(

Swali:
  • SI unaweza kukuta labda asilimia zote za MIPAKA uliyojiwekea MAISHANI hata ile ya kuhofia ukivuka hapo UTAVUNJA maadili ya JAMII labda kikweli ni WEWE mwenyewe UMEJIWEKEA na KUJIPIA hizo N'gwe?


Mipaka ya BINADAMU ,....
.... inapindika BIANDAMU wakitaka,....
.... inaongezeka kama tu WAKIMBIAJI waongezavyo rekodi kila siku ambazo huvunjwa,...
... lakini labda kikubwa labda MIPAKA ni  chazo cha kujinyima UHURU,....
.... na ukishakosa UHURU na UKAZOEA kutokuwa HURU  unaweza usielewe WAVUNJAO mipaka na kuwa HURU angalau hata kwa kusema wanachowaza bila kuhofia JIRANI na JAMII kwa ujumla itasema nini.


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu tu Herbie Hancock na CĆ©u warudie - Tempo de Amor




Kama unataka kujua maneno ya wimbo kwa ung'eng'e ni:

Oh, it would be so much better to live in peace Without having to suffer Without having to cry Without having to want Without having to give yourself (2x) But you have to suffer and you have to cry and you have to want To be able to love Oh, deceiving world peace doesn't mean "love" anymore Oh, there is no sadder thing than to have peace and to regret and to submit and to protect yourself of a love, of loving

Read more...

Kumbukumbu,...

>> Thursday, April 28, 2011

....ndio tulichonacho,...
...KIFANYACHO,...
....hata WEWE,....
.... ujisikie ni kweli ni WEWE!



Swali:
  • SI unakumbuka kuwa kama HUKUMBUKI labda WEWE na YULE tofauti zake kwako zinaweza kubumbuluka  akilini?
Ndio,...
.....kumbukumbu ni MUHIMU,....
.... ingawa KUSAHAU tusisahau mchango wake ambao unasaidia mpaka waliowa kufiwa na KULIA SANA msibani,...
...kusahau kitu na siku hizi hao ni fulu kuchekacheka kwa kuwa kunakitu kilichowaumiza WAMESAHAU!



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu Eric WAINAINA atukumbushe- Dunia Ina Mambo

Read more...

WEE MTANZANIA labda SIMAMA na kusikiliza WIMBO wa TAIFA wa ZAMBIA kisaundi!

Kuna haja ya AFRIKA kukumbuka kwanini NYIMBO hizi katika nchi kadhaa ukitoa maneno ZILIFANANA!



Haya wewe pale simama na sikiliza hili BITI toka ZAMBIA halafu wakati huohuo  fananisha na wa BONGO kisaundi!



Endelea kusimama TWENDE Sauzi AFRIKA wakati umesimama na sikio lako linasikiliza BITI la wimbo,....



AU endelea KUSIMAMA tuusikilize tu na wa TANZANIA tena...





Kama hujastukia:
Madhumuni ya BARUA hii ni kuuliza:
  • SI unajua wimbo wa TANZANIA haukutungwa na MTANZANIA?
  • Au unafikiri ni MTANZANIA alitunga wimbo huu KI SAUNDI wakati nakuchokoza ujikumbushe jina lake ni nani?


  • Na si unakumbuka ni KWANINI nchi kadhaa AFRIKA zilitumia BITI moja ingawa  maneno tu ndio tofauti wakati AFRIKA tuna UMOJA enzi hizo?


Ndio,...
....inawezekana akina NYERERE Kaunda  na WENGINE  walioanza kukubaliana MPAKA nyimbo za TAIFA zianze kufananafanana KUTOKANA na UMOJA labda walikuwa ,....
.... na BIG PICTURE kuhusu AFRIKA tuelekee wapi kiasi kwamba usipokuwa MFIKIRIAJI unaweza kusahau HILO siku hizi.:-(




Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(





Hebu tubadili wazo kwa kusikiliza wimbo wa ZIMBABWE ambao nahisi ukiondoa neno ZIMBABWE na kuweka TANZANIA laweza kufiti TAITI TU  na kuendeleza MAANA ileile,....
.....na HEBU Henry Olonga mcheza KRIKETI maarufu duniani kutoka ZIMBABWE aimbe huu -OUR ZIMBABWE -na  wakati wewe unausikiliza kwenye ZIMBABWE weka TANZANIA uone kama haufiti KIAINA hata kwa wale wadaio Tanzania hatujawahi kuwa na Segregation na kuita WAHINDI magabachori sio ubaguzi wa rangi:



Read more...

Wakati MTOTO MZURI anajiandaa kutoka nje ya NYUMBA nusu uchi!

Inawezekana ni WAFIKIRIAO UCHI  kwa kuwa  MTOTO MZURI hasa WA KIKE  kavaa KIMINI  cha KIMINI ,...
....hata kama HICHO ni kirefu  kidogo kuliko KIBWAYA ambacho ndicho vazi la KIAFRIKA kiutafiti wa wengi maeneo fulani AFRIKA ,....

......ndio wamuonao  UCHI KIMWANA HUYO  hata kama  labda kwa watokeao kwenye MILA ZA KUCHEZA SINDIMBA ambapo WACHEZA SINDIMBA huvaa mavazi asili ya KUCHEZEA sindimba hayuko UCHI HUYO ,...


............................

... Au tu hata tu ki,....
...SISI ambao UCHI sio CHUPI au PAJA kutokana na mila zetu za KIAFRIKA,...


...au hata WALE watu wa TARIME wajuao mila za TARIME  kama WAMASAI  wanaume  ambao kimila CHUPI ni kitu cha kigeni kama kwa WAPARE TU ,...
....labda hayuko huyo MTOTO mzuri  UCHI Tanzania kama MTANZANIA anajua mila zake!:-(




Swali:

  • SI inasemekana ANAYEWAZA  UCHI ataona UCHI kama awazaye chakula iwezekanavyo ndiye aunganishye kila VILIKAVYO  kwa BINADAMU labda hivyo ni chakula wakati wasio na njaa wanaweza kusukia hivyohivyo  MKEKA hata kimawazo kwa kuwa kwao hivyo sio VYAKULA?
  • SI inasemekana  WATU kwa kawaida huona WANAVYOFIKIRIA na ndio MAANA katika barabara SIO KILA MTU huona shilingi  iliodondoshwa BARABARANI ingawa kuna uwajuao WAOKOTAO SHILINGI  katika BARABARA ileile uliyoipita iliyodondoshwa na walio TANGULIA walio KUPITA ?
  •  Hivi nusu UCHI na UCHI ni kitu kile kile?-  kwa kuwa si labda yoyote ALIYEVAA nguo hata kama unaona PAJA  lote na kutokea juu mpaka kitovu ila bado  UCHI NI UCHI na kama hujaona uchi LABDA  hakuna aliye uchi?

  • Kwani Uchi ni sketi fupi au sehemu za siri ziwezeshazo watu kutengeneza MTOTO wakizigusanisha kimuingiliano?
Ndio,...
... inasemekana wawazao UCHI hata kama ni WAHESHIMIWA,...
... ndio wastukiao kirahisi  UCHI kwa kuwa wakati wanastukia  UCHI  labda walikuwa wanawaza UCHI!:-(


Swali:
  • Si unajua ni RUKSA kunibishia?
Ingawa NASIKIA wahisio WENGINE  kuwa wako UCHI ,...

....ambao ukiwaulizia ramani ya uchi wa wafikiriao HAO walikuwa UCHI  wanajua kuwa hata kisilaha za KIZIBO cha kipengele hata kama hiyo SILAHA  ni CHUPI  hawakuona kitu zaidi ya HISIA ZAO  walizotumia kuhisi waliona hata kwenye KIZIBO wakati kuna  sketi  fupi,...


.....na  HUWA WANAJUA WAHESHIMIWA ambao ni walalamikaji sana HAWAKUONA EMBEDODO kwa kuwa wao NAO KATIKA MIILI YAO  ni wenye MENGI yatunzwayo kwenye  UCHI kuanzia ustaarabu mpaka starehe ndogondogo,....


... kitu ambacho hata kama WENGINE wanaachia mwanzo wa PAJA au tu karibu tu na chini ya kitovu kwenye KIBOXI manyoya,....

...inajulikana nao WAKILALAMIKA mara nyingi  bado UKWELI UKO PALE PALE  kuwa hawakuona GOLOLI kwenye BELINGI,...
... au kwa lugha ya KISANIFU KIJIWENI ,...

...hao hawakuona kitu hao hata angalau  mkenuo wa bonge la NDUDE ,...


...ila KIHESHIMA kwa kuwa WANAHISI KITU na kwa kuwa mara nyingi HADHARANI kuna kufaidika kwa KUSEMA KITU,...
.....lazima ni WAKALI  kwa kuwa hata kwenye SKETI wao tayari kwa kujihami WANAFIKIRI kiheshimiwa  CHAKUJIFUNZIA UKUBWANI ,....
.....wameona UCHI ukiwadadisi kwa juujuu ingawa kiundani WANAKEMEA kwa kuwa wanahisi wawasikilizao WANAHESHIMU mtindo wa mkemeo wao!:-(




Ni wazo tu hili  MHESHIMIWA na nimeliacha ,....
....na halikufanyiwa UTAFITI wa kitaaalamu MHESHIMIWA na samahani MHESHIMIWA ambaye paja KIDOGO au hata kuona CHUPI KWA MBALI TU  unafikiri CHUPI ni UCHI wakati labda UCHI ni ule chini ya KIFICHA NYETI/CHUPI!:-(




Na wakati tunabadili HOJA hii nyoko ,....


NDIO....
....nilikutana na Bobby McFerrin katika pitapita mpaka nikajikuta napata kazi zake live siku fulani zilizotuna hivi karibuni .....


.... baadhi za picha za siku migongano ilipotokea  ni  .....









Kwa waliomsahau Bobby McFerrin hebu adinye-DON'T WORRY be happy!:-(




Bobby McFerrin aongele wakati mie na wengine tuna kifikira - Thinkin' About Your Body



Adinye-Ave Maria




Au tu Bobby a-Drive

Read more...

Hatua ya PILI,....

... labda ilianzishiwa nguvu na HATUA ya KWANZA!

ILA kiletacho MATUMAINI ni kuwa hata kwenye HATUA ya TATU maishani,....
... inaweza kuwa bado MTU hajachelewa KUBADILI anakoelekea!

Swali:
  • AU?

Ndio,...
.... labda HATUA ya NNE ,...
.... inaweza kuwa  ni mwanzo pia wa SAFARI MPYA,....
.....ya mtu kuelekea upande tofauti na ule aliokuwa anaelekea wakati anapiga hatua ya KWANZA!

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Au tu hebu FRANCO amsifie tena Rais MAARUFU sana AFRIKA katika MARAIS tokea kabla wengine AFRIKA hawajastukia utamu wa kuwa FISADI katika ndude-Candidat Na Biso Mobutu


Read more...

Katika JITIHADA tena za MTU za KUHAKIKISHA anaheshimiwa HADHARANI,....

.....si kuna UWEZEKANO imefikia mpaka  kuna WENYE busara na HEKIMA wanakaa kimya HADHARANI,...


....na labda ni mpaka UKUTANE NAO pembeni wakati mnaongea wakati WATU wengine hawasikii ndio waweza kujikuta unastukia HEKIMA busara na majibu ya maswala ya maisha yasumbuayo ULIMWENGO jinsi walivyo nayo?

Ndio,...
....kuna jamaa ni mpaka ukutanenao PEMBENI,....
... ambao HADHARANI hukaaga KIMYA kwa kuwa wamefikia KUAMINI hadharani,...
.... ni mahali  ambapo MHESHIMIWA asipochagua cha KUONGEA atajiharibia HESHIMA!



Ni wazo tu hili baada ya kukutana na MHESHIMIWA ambaye hukaa kimya HADHARANI hata kama tunaongelea CHIPSI na MISHIKAKI ili asije julikana anahusudu  vitu hivyo na UMATI!:-(

Hebu King Yellowman aongee anavyofikiria hadharani kuwa-FOOLS GO TO CHURCH on SUNDAY



Au tu Mister Yellowman  aombe tu na kidude kitu ambacho sidhani wengi wanaweza kuomba aombavyo hadharani katika ngoma-Gimme KIDUDE/gimme vagina





Kabla ya kutuliza kitu kwa kustukia- Wrong Girl To Play With

Read more...

Leo katika UCHOKOZI: Si unajua UGALI ni chakula cha KIGENI Tanzania hasa kama ni kweli MAHINDI ni kitu kilicholetwa tu na WAGENI Tanzania?

>> Wednesday, April 27, 2011

Inadaiwa sana kuwa MAHINDI asili yake ni Mesoamerika au tu America ya KUSINI,....

.... kama tu idaiwavyo kuwa ASILI ya MCHELE ni ASIA kitu kiwezacho kuwa wapenda UBWABWA Tanzania  ambao wanajivunia vitu vya kiasili Tanzania bado NGUNA ya unga wa MAHINDI na bonge la  tonge wakatalo kwenye MISIBA la UBWABWAZ yote ni msaada wa vitu visivyo na asili yake Tanzania!:-(

Swali:
  • Ushawahi kuwa unafuatilia asili ya VYAKULA vyako BONGO angalau kujua asili yake ni wapi hata kama hapa tunaongelea MATOKE?

  • Hivi WAGENI nishai eeh kwa wenyeji kama kunauwezekano BIA kwa wapenda KILAJI hata kama ni SAFARI  ze LAGA wanywacho ni zao la wageni?


Ni uchokozi tu huu wa wazo tu HUU MHESHIMIWA na usikonde!

Hebu Franco akumbushie zao jingine la kigeni MAARUFU Tanzania lijulikanalo kama UKIMWI katika -Attention na SIDA


Read more...

MWIZI,...

...huiba aisee!


NI hilo tu MHESHIMIWA!
SIKU NJEMA!

Read more...

Umuhimu wa UFUNGUO labda upo tu kama tu kuna MLANGO!

>> Tuesday, April 26, 2011

Na ufunguo ni UFUNGUO kama kunacho UNACHOFUNGUA,...

.... hasa kwa kuwa LABDA ufunguo ni kitu tu  uonacho jalalani kisicho na mpango ,....
.... kama hauna unacho FUNGUA!:-(




Swali:
  • SI ushastukia UFUNGUO na MLANGO ufunguliwao inatakiwa VISHABIHIANE ili UFUNGUO ufanyekazi zakufungua na kufunga?



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu SANCHEZ aingilie kati wazo kwa- Baby Can I Hold You Tonight



Au tu FOXY Brown abadili mchezo mzima kwa kurudia -Hot Spot


Read more...

Kama ishawahi kukutokea MOYO na AKILI vinabishana UAMUE NINI!

Kuna MAAMUZI yatumiayo MOYO,....
.... ambayo ukitumia AKILI labda usingeamua hivyo!

Na moja ya kitu ambacho kama unatumia AKILI badala ya MOYO labda hujadakwa vizuri,...
... ni mambo yale yahusuyo,..

...NI NANI UNAMPENDA!:-(


Swali:
  • Au?
  • Si MOYO ukipenda maamuzi yako yanaweza kumchagua MPENZI ambaye ungetumia AKILI kuchagua labda ungemkwepa kwa kuwa ni AROSTO halafu ana bonge za MWANYA kama mfereji wa MAJI machafu?


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu Ambelique arudie - Penny Lover


AU tu Ambelique aongezee doz i kwa - New Sheriff In Town

Read more...

Dambisa MOYO aongee....




Read more...

Mara NYINGINE hata kama mara ya kwanza WAKATI kitumbua kikutumbuliwa haikuwa TAMU!

Mara nyingine ,...
....ikijulikana ni MARA NYINGINE,....
......labda  utamu wa mara nyingine unatokana ukweli kulikuwa na mara nyingine iliyofundisha mtu utamu wa CHUMVI ni mtamu kama CHUMVI mara ya kwanza.:-(

Swali:
  • AU?

Na mara NYINGINE kama inafikiriwa ni tamu,...
.... labda huo ni USHAHIDI kuwa MARA NYINGINE ilitanguliwa na MARA NYINGINE nyingine ambayo hata kwa mjanja ilikuwa ndio SHULE:-(



Swali:
  • AU?
Kama kuna mara ya kwanza hata katika kumpapasa MHESHIMIWA kiheshimiwa,....
.....ilikuwa MPAPASAJI PAJA  anaogopa hata kumgusa MHESHIMIWA  kwa kuwa  mpapasaji  ANAHESHIMA,...
.... kumbuka tendo hilo labda  BADO linaweza kuwa NDILO lililomrahisishia MPAPASAJI MWENYE AIBU  kujisikia huru kirahisi MARA NYINGINE!:-(

Ni wazo tu HILI  Mheshimiwa !:-(

Hebu LAGBAJA  aingilie kati na kubadili wazo kimtuno kwa -Konko Below



Au tu LAGBAJA adinye tu na -Gragra

Read more...

Kama MHESHIMIWA hadharani AMEKUNYA bila kujisikia vibaya!:-(




Maishani ambako kuna mpaka vitu vizuri kama  KULA wa wapendao chakula ,....

......kunya ambako labda nako ni muhimu katika maisha ya BINADAMU,....
... kwa sababu fulanifulani huwa HAKUHESHIMIWI eti!:-(




Swali:
  • SI umestukia yafikiriwayo ni MAZURI  kwa BINADAMU hasa wajifikiriao ndio wenye tabia nzuri yawezavyo kufanywa kama vile YALE yasiyo mazuri kwa binadamu haohao KIFIKIRA kuonekana ni MABAYA wakati yawezekana hayo mabaya ndio siri ya hao WAHESHIMIWA WATU WAZURI wastukiavyo kitu kizuri?

Ndio ,...
.....MHESHIMIWA labda hadharani usinye,...
.... ingawa labda ni kweli siri ya kwa nini kama UNAHESHIMIWA usinye hadharani inaweza kuwa ni kwa sababu kuna jamaa siku moja ALIKUNYA hadharani aisee!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu Pat Shange abadili mkao kwa -Sweet mama



Yvonne Chaka Chaka atunishe kwa - Thank You Mr DJ

Au tu Yvonne Chaka Chaka aweke tu kigunzi kwenye tobo-I'm  in Love with the Dj

Read more...

Labda usiogope wa kitu MWANZO!

>> Monday, April 25, 2011





......kwa kuwa CHENYE MWANZO,.....
....inasemekana kina mchezo wa kuwa na MWISHO.:-(

Na kama umeanza na uko MWANZO,...
.... kama kuna maumivu kumbuka tu kuwa tamutamu labda haiko MWANZO na inawezekana hata kama unachekwa sasa hivi,...
......kunauwezekano mchekaji kijemedari atakuwa ni wewe MWISHO!:-(


Ni hilo tu MHESHIMIWA na hili ni wazo tu MKUU!:-(


Hebu Brenda Fassie adinye - Vulindlela





Au tu hebu Kool & the Gang wabonyezebonyeze nao embedodo kwa - Get Down On It


Read more...

Msauzi GOODMAN MANYANYA PHIRI wa kibongobongo!

Kuna baadhi ya watu wanafanya nijifunze sana vitu kirahisi VITU!


Huyu Mkuu GOODMAN MANYANYA PHIRI ambaye anatoka AFRIKA KUSINI kwa jinsi asapotivyo WATANZANIA na au tu aandikavyo KISWAHILI kitu ambacho kama usingejua ni MSAUZIAFRIKA labda ungefikiria ni MTANZANIA,...
.... mie kuna kitu hata kwa utu wake ananifurahisha nakunifunza!





Kama hujamstukia ,....
Ni huyu hapa KIMTANDAO


Nimewaza tu kwa SAUTI WAHESHIMIWA!:-(



Hebu Msauzi mwingine anizinguaye ambaye ni Hugh MASEKELA aanzishe vita mpya kwa ndude iliyotuna-Khawuleza





Aendeleze vita kwa -Thanayi



Au tu na Msauzi mwingine nimzimiaye Abdullah Ibrahim atekenye tu - Cape Town Flower



Au tu Abdullah Ibrahim amwage tu na rojorojo  - IshmaĆ«l


Read more...

Katika JICHO LA anayebakwa!

Inawezekana wakati huo anabakwa moja ya asichokiona NI huko KUBAKWA,...

.... ingawa maumivu YAMVURUGO WA SEHEMU ZA SIRI anasikia!


Na visikilizwavyo labda KWA JICHO  hata kisaikolojia  vyote huwa havionekani hata kama wakati vinabakwa,...
.....kitu kifanyacho kuna ushahidi wa KWELI  kuwa kuna kilichotendeka KWENYE SEHEMU ZA SIRI hata kama kwa JICHO hakikuonekana kikitendeka na kimebakia KISIMULIZI kwa wengine  ni TU cha kusikia!

Swali:
  • Hivi unafikiri ni mangapi ambayo JICHO halioni  kwa nyuma kwa kuwa tu MACHO  yako kwa mbele ya mtu wakati tukio limuhusulo mtu LAWEZA KUWA liko nyuma yake tu mtu ambako hakuna macho ila kuna bonge la tako?


Ndio,...
.... labda hata kwenye jicho la ambaye habakwi,....
.... labda kunayaliyomtokea ambayo JICHONI  wakati sio kipofu hayakuonekana!:-(




Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu Saul Williams katika kubadili wazo arudie-Gypsy GIRL



Au tu hebu Mah Kouyate arudie tu mdinyo - Folo

Read more...

Katika swala la -TUJIFUNZE UPUMBAVU na Simon Kitururu!:-(






Kuna werevu DUNIANI,...
.... ambao  uwerevu WAO huwa KIUEREVU WAO kwa kawaida hautafutwi sana CHANZO CHAKE,...
......hata kama ni kweli chanzo cha uerevu wa YOYOTE ufikiriaye ni MWEREVU labda ni UJINGA!:-(




Swali:
  • Kwani unaamini  UPUMBAVU kama tu UJINGA  unafundishika ?
  • Kwani werevu wa WEREVU silabda nikitu walichozailiwa nao tu hao WEREVU kwa kuwa labda kirahisi apatiaye UEREVU labda alikuwa MWEREVU kabla ya kujifunza UEREVU?

Na wakati kuna isemekanavyo kuwa kuna mtu amejifunza kwa KUIGA,....
... labda waigao HUIGA TU VIZURI vile vitu hata kama ni vya KIPUMBAVU kama tayari akilini walielemea tayari ki MRENGO huo wa walichoiga kukujifunza kabla hata HAWAJAIGA!:-(

Swali:
  • Unabisha?



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(



HEBU  tu Mr DALE abadili zaidi kwa -Soca Junkie




Kabla  tu The soca boys hawajatuliza boli kwa -Follow the leader






Read more...

Kuna maisha ya NENO yaishiyo kwenye MANENO!




Na katika MANENO ,...
.... labda kuna neno ambalo utastukia halina maana likikaa peke yake kama NENO bila kuchanganywa kwenye mengine MANENO!

Swali:
  • AU?
Ndio,...
... kuna NENO umuhimu wake ukikugusa kumbuka ,...
... labda lilikuwa katikati ya MANENO.:-(




NI wazo tu hili ambalo nalo ni neno tu MHESHIMIWA!:-(


Hebu SAM MANGWANA abadili kwa - Maria Tebbo



Sam Mangwana atoneshe zaidi kitundu kwa kumuongelea mtoto mzuri kutoka Afrika Mashariki- KABIBI





Nipo na tupo hata kipicha kiduchu......
























































































Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP