Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nawatakieni KILA la KHERI wadau wote wa BLOGU HII!!

>> Friday, December 31, 2010

Tutakutana KALENDA ya wajanja ikibadilika  na kudai ni mwaka 2011,....
....kama MUNGU akipenda!







 
Asanteni kwa YOTE !
Tuko pamoja sana tu !

Wenu,
 -Simon Kitururu




Rafiki yangu kanitumia salamu hii niliyoipenda:


I don't want to be bothered Next Year,

Let me finalize with you once and for all.

Happy new year, Happy Birthday, Happy Valentine, Happy Easter Holiday.
Happy Father's /Mother's Day, Good Morning x 365 days, Good Afternoon x
365 days, Enjoy all the weekends, I don't have money X 365 and have Merry
Christmas, Happy Women's day, sorry there is no men's day, Happy Halloween,
Happy thanksgiving, Good evening X365, Goodnight X365.....

I am done with you for 2011 .



Have a good year 2011!

Read more...

R.I.P Billy Taylor!

Kwetu wapenda Muziki wa Jazz ,....

.....Billy Taylor hatasahaulika!


Billy Taylor (July 24, 1921 – December 28, 2010)



R.I.P   Dr Billy Taylor!

Hebu  tujikumbushe  enzi za Duke Ellington akiwa na Duke na Willie the Lion wakileta -Perdido


Billy Taylor atupe-I Wish I Knew How It Would Feel To Be Free



Hebu aongee-





Au aendelee  tu kuongea -




Unaweza kumfahamu Dr Taylor kwa kuanzia hata HAPA kama wataka kujua zaidi.

Read more...

Kama KUKOSEA ni UBINADAMU,....

..... KUSAMEHE ni zaidi ya UBINADAMU,...
..... na ndio maana  ni moja  ya SHUGHULI ihusianishwayo na kazi  mpaka afanyazo MUNGU.

Swali:

  • Si inakumbuka MUNGU huwa hahusianishwi na KUKOSEA?
  • Hivi kwanini bado kuna wadaio KUMZIMIA Mungu lakini wagumu kumuigilizia MUNGU  katika ya KIMUNGU zaidi yale ya  KUSAMEHE  na kung'ang'ania yale yasemekanayo pia ni ya KIMUNGU ya kutoa ADHABU tu  kama Mungu  ?

Ndio,....
....pamoja na yote ambayo hufanya kwa mtu KUSAMEHE kuwe kugumu,....
.....BADO yajulikana  kusamehe kwa mtu ni bonge la TIBA kwake.:-(


Swali:
  • Kwani unafikiri ni ALIYESAMEHEWA TU ndiye anufaikaye na kitendo cha KUSAMEHE?


Ndio ,....
....katika kusamehe kuna wafikiriao  ni VYEMA kusamehe aliyeomba MSAMAHA TU  kwa  kuonyesha kastukia alipokosea,....

....ingawa pia kuna WADAIO  wenye busara zaidi husamehe hata wasioomba MSAMAHA kwa kuwa labda hata hawajastukia WALIPOKUKOSEA hasa kwa kuwa KIBINADAMU hawastukii kila kitu  WAKIGUSACHO kikugusacho ambacho kwako ni MAKOSA,....

.....kwa hiyo,....



....wasamehe tu  akina SIMON KITURURU,  Babu Seya,  Limpenzi lako, NDUGU LAKO, Rais KIWETE ,jamaa tu lililokusonya bila sababu wakati unanunua nyanya na bamia  KIGENGENI huku ukimtamani muuza genge kimahaba, .....

......kama tu labda walivyosamehewa akina Mheshimiwa Rais IDI AMIN,  Winnie Mandela na Rais Mandela, Mheshimiwa CHENGE  na ......,.....,.......,.......


........hata kama  BADO hawajisikii kukuomba msamaha,....:-(

...MIYE nawaza tu hapa MHESHIMIWA jamani!:-(




Mimi Simon Kitururu naomba MSAMAHA kwa yote lakini MDAU  hasa  kama kunamaeneo nimekukwaza KIZEMBE!!:-(




Tubadili wazo  kwa kumsikiliza CHUCK BROWN...



Chuck Brown aturudishe enzi hizo kwa-Bustin' Loose



Au tu CHUCK Brown arudie-The Party Roll

Read more...

R.I.P Roberto "Bobby" Alfonso Farrell!

Kama uliwahi kuwa mpenzi i wa BONEY M nafikiri unaweza kumkumbuka huyu Jamaa!



Bobby Farrell (October 6, 1949 – December 30, 2010)



R.I.P Bobby!




Mcheki enzi hizo za DISCO akiwa kazini katika-DADDY Cool



Kwa wasiomfahamu huyu MWANAMUZIKI habari zake kiduchu unaweza kuzidokoa ,...



Au HAPA

Au tu :

Ask Arubian "Bobby" born, Alfonso Farrell what he wants his music to convey and he replies, " I want my music to make people feel good and to create sweet memories. The energy in my music has no limit; I want people to feel entertained and to hear the love that I have for creating music, translated into my songs."

Bobby's career in music reads like a manual for how to cultivate a perfect marriage of ambition, talent and a splash of Caribbean spice to produce what is a honourable 26 years of making hip shaking music. At 61 years old, his showman ship in music is a far cry away from the young boy who left his home land of Aruba to become a sailor, only to fall upon uncertain conditions on European soils before eventually moving to Germany to pursue a career as a DJ.

Despite the weathering conditions of his former life, his eminent love for music remained present and his growing passion for making people dance is what caught the attention of Katija Wolff, whom at the time, was scouting for performers to front the epic group, Boney M. Having been fully bowed over by his eclectic style and charismatic island charm, in 1974 Bobby was chosen as the single male in the Caribbean collective, Boney M along side fellow group members, Liz Mitchell, Maizie Williams and Marcia Barrette.

By 1979, Boney M had received worldwide recognition with hits such as ‘Daddy Cool', ‘By the Rivers Of Babylon/Brown Girl in the Ring' and ‘Sunny' all of which became instant number one hits across Europe. Boney M played an infinite role in Bobby's music history, moulding him into the class act that he has since then become. Even after the split of the group in 1986, Bobby Farrell's jubilant energy and unyielding love for music has enabled him to spawn a solo career of 15 years, earning himself the title "King of Disco".

Forever reinventing his sound and fuelling his creative engine, it comes as no surprise that Bobby's latest material integrates 70's Disco with multiple different genres, only working with creative like minded individuals on the way to breathe life into his artistic foresight. Always regaining his love for traditional Calypso music, Bobby's fusion of Disco music with Arubian influences also remain as dominant features in his songs, reaffirming his meritable pride in his Caribbean culture.

In 2010, Bobby continues to tour the world, gracing the global stage with his flamboyant style, infectious rhythms and glamorous backing singers, Edna Proctor, Maureen Pengel and Jacqueline Jonkers. "I like to look good on stage and to release all my energy in my shows. I still wear my glitter costumes and my girls always look glamorous along side me"

Currently housed under Swedish Production Company, Roasting house, Bobby's desire to create good music lives on as he readies his untitled new album, due for a late 2010 release.

Read more...

Tafsiri ya KITU!

>> Thursday, December 30, 2010


Tukumbuke tu,....
.... karibu kila KITU kina tafsiri nyingi,....
..... ingawa moja ya TAFSIRI ambayo  maarufu KWA KAWAIDA hugeuzwa ndio UKWELI na watu!:-(


Na tukumbuke tu,....
..... umaarufu wa MTAZAMO  au tafsiri ya mengi,.....
.... sio ushahidi wa USAHIHI wa jambo kimtazamo hasa kama wahusika WATAFSIRIO JAMBO ni binadamu ambao wanamadhaifu ya KIBINADAMU kwa kuwa ni watu!:-(

Swali:
  • SI inajulikana KUTAFSI KITU hutegemea sana atafsiriye anajua nini kabla ya kutafsiri jambo?
Tafsiri!
Labda cheki wanaotafsiri MAMBO tofauti na weye,....
....kama nia ni kuendelea kujifunza kutoka katika TAFSIRI ZAKO ZA MAMBO ambazo ni misingi ya misimamo yako.

NI wazo tu HILI Mheshimiwa!





Hebu Robert Cray aingilie kati kwa -All Your Lovin 




Robert Cray aendelee na -Nothin' but a woman




Au hebu Khaira Arby and Her Band warudie - Sourgou

Read more...

Weka KIPORO , kwa kuwa kina mchezo wa KULIKA tu hata KESHO!

>> Wednesday, December 29, 2010


KIPORO bado ni CHAKULA,....
..... na mengi yasiyolika LEO kwa kuwa UMESHIBA leo,....
.....kumbuka yanalika tu hata KESHO.:-(







Swali:
  • Au?
  • Unauhakika unanielewa?

NI HILO tu MHESHIMIWA na ni wazo tu HILI!:-(









Hebu Yellowman aingilie kati shughuli kwa -Still Be A Lady na Zungzungzungzeng



OUTKAST wabadili kabisa kwa-Love HATER



Weird Al Yankovic atulize boli kwa - Eat It



Halafu hata sijui kwanini , hebu "Weird Al" Yankovic arudie tu na - Fat

Read more...

Labda watu WAKUBALI TU YAISHE kuwa - wanahamu saa nyingine!:-(

Swali:

  • Si kwa BINADAMU kukosa hamu ni aina ya KILEMA?
  • Na hata kama unafikiri hatujui , -SI labda ni kweli UNA HAMU sasa hivi?
  • AU?





Kubali yaishe,...
....kwa kuwa LABDA kama hakuna hamu hata angalau ya ELIMU ,....
.....mahitaji yake hata ELIMU  hayatakuwepo kinanihino,...
... kwa kuwa labda yote afanikishayo BINADAMU hutokana na hamu ya NANIHII YOYOTE hata inukayo KIAINA!:-(







Swali:

  • AU?

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(












Na hebu tumtembelee MZEE YUSUPH .....


Mzee YUSUPH na Zanzibar STARS  warudie-NAJIAMINI



Mzee Yusuph aendelee na ndude hiihii -NAJIAMINI



Au tu mdada Carola Kinasha abadili zaidi kwa - Ujasiri

Read more...

Halafu BINADAMU akaingiza KIDOGO!:-(

Yaweza kuwa:

Ilikuwa  ASUBUHI isiyotegemewa BAADA YA ya  usiku  ambayo hayakutegemewa,...
....kidume PASKALI  aliamka  na KUJINYOSHA huku akitabasamu kwa sana tu bila kujizuia,...
.... kwa kuwa USIKU WA JANA kuna kitu aliingiza kidogo.





Na ilikuwa ASUBUHI nyingine yenye MAMBO MENGINE ingawa  kwa ASHURA hayo yalitegemewa,....
....Ashura aliamka kwa haraka na kutupilia BLANKETI kule mbali  huku akijamba kidogo kwa sauti kama afanyavyo kila akiwa peke yake kwa UHURU ambao hadharani anajizuia,...
....lakini AKILINI  akiirudia mistari ya UJUMBE ambao kuanzia kwa apangacho tu KUVAA hata kabla  hajasema kitu atakacho KUSEMA akitoka nje kwenye UMATI anajua nia  YA APANGACHO  ni HEKIMA na BUSARA hasa katika yale ambayo JAMII kwenye ubongo ingawa ni YA MSAADA watu hawataki kwenye UBONGO  kuyaingiza hata angalau  KIDOGO.:-(

Swali :
  • SI  labda  ni tatizo kwa kuwa BINADAMU hutosheka na KIDOGO   kitu kifanyacho waendao shule baada ya MTIHANI kutupa vitabu kwa kuwa kama wamepasi MTIHANI basi yanatosha waliyo ingiza  hata kama ni kidogo?


Na labda yote ya AJIVUNAYE kwa kujua ni yale tu ,....
.... ubongoni yaliyoingia  tu KIDOGO!:-(


Ni wazo tu MKUU na kutolielewa RUKSA!:-(

Hebu EDDY GRANT atusaidie kurudisha ustaarabu hapa KIJIWENI kwa ndude-Hello AFRICA





 EDDY GRANT arudie -War PARTY




Au tu hebu Eddy Grant amalizie tu na -LIVING on the FRONTLINE

Read more...

Ni KWELI kuna waonao TUNDU na bado HUNYA na KUKOJOA pembeni ya CHOO!:-(

Kuna mambo NI KWA MTU MWINGINE TU labda ndio yako wazi,....

...... kuliko idhaniwavyo kuwa NI WAZI  kwa kuwa tundu liwazi  NI LAZIMA liingizwe MTALIMBO wakati kuna  pia WADHANIAO wanajua kwa uhakika KIUHAKIKA  kuwa WAO kama tundu li wazi basi hilo tatuzi  ni moja tu kuwa hilo tundu LIFUNIKWE!:-(

Swali:

  • AU?


Na kama ILIVYOWAZI  KWA WENGINE ajisaidiaye kwenye CHOO CHA KUKAA na chenye MAJI akimaliza KUJISTAREHESHA kwa kwenda HAJA KUBWA inabidi a-FLUSH mharo tepwetepwe  ,...
.... bado kuna waondokao CHOONI na ni WASTAARABU TU kwa mtazamo wa JAMII ambao wakimaliza kunya hung'atuka HUKO maliwatoni bila kuvuta  maji kitu ambacho kuna MTU MWINGINE anadhani si kawaida,....


.... kama ishangawavyo na WENGINE kuwa KUNA waondokao  NYUMBANI KWA MTU WALIKO ALIKWA na mtu bila KUAGA ,...
.... na  kama ishangawapo VILE VILE mpaka kwenye SIASA ilivyo kuwa  KUNA wasiotimiziwa ahadi wawezavyo MARA kwa MARA kurudia KUMPIGIA KURA YULEYULE MBUNGE  kwa ridhaa yao wenyewe  WAMJUAO hana msaada KWAO.:-(

Swali:
  • Kwani BINADAMU hawakushangazi  kwa kupenda kikojoleo wakati hawapendi mkojo?
Ndio,...
.....labda KUNA wote WAONAO tundu,....
...ingawa tumizi la tundu HUTOFAUTIANA kutokana na TAFSIRI tu za watu,....
...ndio maana .kuna BAADHI tu  YA WATU HATA KAMA NI WENGI ,....
....ndio wakubalianao tumizi la TUNDU ni lile la goli kuingizwa TU hata kwa  TIKITAKA wakati TUNAJUA kunawadhaniao kama GOLIKIPA  TU kuwa MATUMIZI MAZURI YA TUNDU LA GOLI  ni yale ya TUNDU LA GOLI kulindwa  KITU  MTALIMBO kisiingie!:-(

Ndio,...
...hili ni WAZO TU hapa MHESHIMIWA!:-(



Hebu tugawiwe MUSTANG SALLY  na Wilson Pickett




Au tu hebu tucheki ALBUM version ya hiihii ndude........

Read more...

Binadamu HAJAUMBWA kupigana KILA VITA!:-(

>> Tuesday, December 28, 2010

Kwa hiyo,....
......CHAGUA vita yako,...
...chagua cha muhimu kwako,...
...kwakuwa MWANADAMU hategemewi kukabili yote!


Swali:
  • Si inasemekana  MAISHA YA BINADAMU ni mafupi na hakuna aliyewahi KUISHI aliyemaliza kila kitu ?



Na inasemekana,.....
.... kama MTU anajitahidi sana na bado haelewi SWALA,....
....labda  HILO SWALA sio lake na ni la  WENGINE hilo KUELEWA!:-(

Swali tena:
  • Si inasemekana kila mtu kuna ambayo kwake ni MARAHISI kwa hiyo isifikiriwe ni kwa kila mtu  UMALAYA ni mgumu?
Na labda fanya UWEZAYO ,...
...na usiyoweza waachie wawezao,....
....huku kikubwa KIKIWA ni kujifunza kuridhika na yale katika JITIHADA ndiyo yaliwezekana kama nia ni FURAHA maishani.:-(

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu Billy Ocean arudie-SUDDENLY


Na IMAGINATION wakumbushie tu-Just an Illusion

Read more...

Kama uko MAENEO ya HELSINKI , Vantaa au ESPOO, FINLAND tarehe 31 December 2010 na unataka kuwa na WABONGO!

Unakaribishwa KERHOHUONE  

Kyyhkysmäki 2
Leppävaara.
Espoo



Kwenye New Year Eve Party
Start time: 7PM
HOST:Ronaldo


Bring ur drinks with U!


Au 



 Mcheki HELSINKI  DJ  Ray One 4 One

Bar EXODUS
Kaarlenkatu 10
Helsinki
Tel: +358 737 085



Read more...

R.I.P Teena Marie!:-(

>> Monday, December 27, 2010

Kwa wapenzi HASA  wa R&B wakutoka zamani kidogo  ,...

.....watakuwa wanamjua HUYU mama na kazi zake!


March 5, 1956 – December 26, 2010





Kwangu mara ya kwanza nilimstukia kupitia kazi za Rick James,...
....na nilikuwa nafikiri ni Mdada Mweusi,...
....mpaka baadaye kidogo kupata kanda yake ya  KASETTI yenye picha yake.

Unajua tena mambo ya enzi za MIKANDA ya  KASETTI ndio ujanja.


R.I.P Teena Marie!



Ngojea aongee....




Au ngojea tujikumbushe moja ya nyimbo zake Teena Marie  na Rick James wa enzi hizo uitwao-Fire and Desire



Duh Rick alitutoka ,...
.......na sasa Teena Marie! 
:-(

Hebu tujikumbushe pia na Rick James maana ghafla nimeanza kummisi tena naye katika -Super Freak


Au tu na Marehemu Rick James arudie tena wimbo unikumbushao pia mbali wa  -Cold Blooded

Read more...

Jibu kwa DA MIJA lenye kucheza karibu na DINI na IMANI za watu kwa hiyo CHEZA kwa stepu usimkanyage MWENZIO!

 [Tahadhari: Nachoandika ni kutokana na tafsiri yangu BINAFSI ya mambo kama Simon Kitururu na mie sio Mwanahistoria wala Aliyesomea DINI ingawa kila siku mambo haya mawili nayaingia kichwakichwa kivyanguvyangu kutokana na VIANZO vyovyote vya TAARIFA  nibahatikavyo kuvipata kwa hiyo KUKOSOA mtazamo wangu RUKSA- na  bila kusahau MLENGWA hasa wa hii taralila ni Da MIJA!:-( ]




Nafasi ya kiboxi cha maoni kwenye Blogu ya Da MIJA haikunitosha,....


....kuingia kichwakichwa swala  HILI lililoanzishwa na Da Mija kutuonyesha PICHA ya ZIZI au MAHALI alipozaliwa YESU kama lionekanavyo siku hizi baada ya Miaka Elfu kadhaa ....

Hebu tupadeku.....


Na chachandu ya kuongelea swala nilijuavyo mimi kama SIMON KITURURU ililetwa na  Swali la Da MIJA:
  • Swali langu ni kwamba kwa nini tunakataa hiyo siyo sehemu alipozaliwa Yesu? ni kwa vile Yesu alizaliwa zamani sana na kumbukumbu ya mahali hapo haiwezi kutunzwa au? na kama hiyo ndio sababu mbona Kaaba kule Mecca inasemekana ilijengwa kwanza na Abrahamu ambaye aliishi miaka mingi tu kabla ya Kristo?


JIBU langu kwa kifupi kwa swali hilo hapo juu kwa wale wapenda NJIA YA MKATO ni :
  •  Si wote wakataao hapo ndipo alipozaliwa Yesu ndio maana kuna watu wanapata ulaji hapo kwa kuwa kuna MTUZ kibao zinaamini ni hapo ndipo palikuwa MATENITE WODI.

  • Kwa tupingao kuwa swala hilo lina utata wengi wetu ni baada tu ya kufuatilia HISTORIA ya BIBLIA na pia ya eneo lenyewe kitu kifanyacho kama mimi niamini hapo ukweli wa swala hilo misingi yake ni IMANI na sio KWELI kama kweli ya FACTS aka data nyomi ziwezazo kuhakikiwa.:-(

  • Na kuhusu KAABA bado ni vile vile kama utafuatilia HISTORIA yake  utastukia sio watu wote wanaafiki unalo- SUGGEST kuwa  kila mtu anaamini hivyo  kuwa palijengwa na ABRAHAMU, ingawa asilimia ya wengi wakubalianao na wewe ni WAISLAMU ambapo tutarudi tena katika swala la DINI na imani ambavyo AAMINIYE huo utakuwa ni KWELI TUPU hata kama asiyeamini atakuwa na vigezo vyake. Na kunawatakao kusahihisha kidogo ambao ni WAISLAMU  kwa kusema :

Abrahamu na Ishmael kwa KIISLAMU  walirudia tu  tena KUJENGA katika misingi ya zamani  kwa kuwa  mtu wa kwanza kuijenga KAABA alikuwa ADAM ,na  kuna wengi  waaminio HAPA DUNIANI kuwa  hapo ndipo kulikuwa na jengo la kwanza DUNIANI.

Hebu tudeku KAABA  katika mchoro kabla sijaendeleza kulima N'GWE kitaralila:

KAABA



1 - Black Stone on the south-west corner.

2 - Entry door, on the East wall 2.13 metres above ground level. It is accessed using a set of portable steps.

3 - Rainwater spout made of gold. This was added in the rebuilding of 1627 after rain the previous year caused three of the four walls to collapse.

4 - Gutter, also added in 1627 to protect the foundation from groundwater.

5 - Hatim, a low wall originally part of the Kaaba. Pilgrims do not walk in the area between this wall and the Kaaba. Some believe this area contains the graves of Hagar and Ishmael.

6 - Al-Multazam, the part of the wall between the Black Stone and the entry door.

7 - Post of Abraham. Abraham is said to have stood on this stone during the construction of the upper parts of the Kaaba, raising Ishmael on his shoulders for the uppermost parts.

8 - Corner of the Black Stone (South-East).

9 - Corner of Yemen (South-West). Pilgrims traditionally acknowledge a large vertical stone that forms this corner.

10 - Corner of Syria (North-West).

11 - Corner of Iraq (North-East).

12 - Kiswa, the embroidered covering, replaced annually.

13 - Marble stripe marking the beginning and end of each circumperambulation.

14 - Post of Gabriel






Kabla sijaendelea cheki  zaidi  BAADHI ya Hoja kama hizi zilizotangulia HAPA kwa DAMIJA :

Anonymous said...

  • Sista huu uongo usiuvalie njuga na wewe utaonekana mwanamke wa fimbo sio shoka tena! ni uongo mtakatifu waliotudanganya miaka tele na bado wajinga wanaendelea na upuuzi huu mpaka kwa watoto wao??!! jamani hebu tutoke huko, tuwaachie wazungu na fantacy zao, waafrika tuna yetu tulioyadharau, tumebaki kupokea kila kitu... WAKE UP


Blogger nyahbingi worrior. said...

  • we nani kakwambia?au ndio vitabu vinavosema?kwa habari kama hii naamini vizazi havitokaa kamwe kujuwa ukweli kuhusu 25/dec/...



SIMON KITURURU said...

  • Binadamu kweli kiboko! Wamegundua Yesu alikuwa ana sura gani ingawa kwa mamia ya miaka inajulikana hakukua hata na mchoro wa sura ya YESU,...
.... na eti siku hizi wanajua mpaka ni zizigani alikozaliwa Yesu ingawa ukisoma BIBLIA utajua ZIZINI alipozaliwa YESU hapawezi kuwa katika hali ambayo kiujengaji ingedumu kiasi hicho ukizingatia kwa mtazamo wa sasa palikuwa ni kakijiji fulani tu!

Anyway,...

X-mas njema!




OOOOOKAY!One two one two Microphone check:

NAANZA  kuvamia stage zaidi kidogo KIKIFUPI :

Nianze kwa kusema IMANI ni kitu chaajabu sana na NDIO MAANA  ni kwa imani pekee ndio mpaka waaminio Ng'ombe huamini ni kweli Ng'ombe anamchango wake baada ya kifo hata kama wasio na imani hiyo kutoona uhusiano wowote wa Ng'ombe na nguvu za KIUNGU.

Kwa hiyo kabla sijaendelea;...
.....Ningependa kurudia busara za WAUNGWANA wapenda DINI kuwa kama unaamini na unataka kutunza imani yako``Don't  let a little KNOWLEDGE wreck your FAITH, kwa kuwa ni FAITH na SIO KNOWLEDGE iaminiwayo KUOKOA MTU hasa kwa kuwa kwa KUJUA unaweza kirahisi kuona katika yote ya imani ni UJINGA na ni FAITH aka IMANI ifanyayo uamini hata KISICHOLETA maana.

And as they say wale waponyaji KIMOSESI KULOLA : ``Imani yako ndio ITAKAYO kuponya hata gono na ukiwa vuguvugu labda mambo yatakuwa madangachee kinoma``.:-(



Niendelee kwa kukumbusha;...
.....Moja ya tatizo la KANISA na WANAHISTORIA,...
....kihistoria ilikuwa ni msuguano wa WANAKANISA kuamini BIBLIA ni kitabu chenye historia sahihi ya ulimwengu na WANAHISTORIA ambao walikuwa wanabunbulua ukweli kuwa Mengi kihistoria yaliyoandikwa kwenye BIBLIA hata ukifuatilia yajulikanayo kuhusu MISRI kutoka kwenye MAPIRAMIDI na maandishi mengine HAYA machi aka HAYAFANANI  na ukweli wa FACTS ,......
.....kitu kihakikishiacho wanahistoria kuwa BIBLIA sio kitabu cha HISTORIA kama WAAMINIO BIBLIA wapendavyo kukinukuu kihistoria. 


Na nagusia hili kabla SIJACHOKONOA zaidi swala,...
....kwa sababu hili pia HUJITOKEZA kwenye dini nyingine za hapa ULIMWENGUNI za waumini kutaka sana kitabu cha miongozo ya IMANI kiwe ndio jicho la kila kitu KIHISTORIA pia jambo ambalo huleta msuguano hasa ukizingatia KNOWLEDGE and FAITH mara lukuki havishabihiani na mambo mengi katika dini umuhimu wake uko tu KIIMANI na ukiuchokonoa KIHISTORIA matokeo yake moja ya mfano wake ni vita vya WAYAHUDI na WAARABU visivyoisha.:-(

Nanirudi kwenye hoja KWA KURUDIA  kuwa;.....

......tukiachana na ya UKRISTO na kwenda mpaka ya UISLAMU mengi misingi yake iko kwenye IMANI na ukifuatilia utastukia kukuta sentensi nyingi zisemazo``INASEMEKANA ´´ kwa kuwa ni stori ambazo ni inasemekana na wakati zinapata umaarufu hakuna aliyekuwepo kushuhudia - kwahiyo ndio maana kwenye KAABA katika ile POST of Abraham mara karibu zote sentensi itumikayo ni ``INASEMEKANA hapa ndipo ABRAHAM alisimama wakati KAABA inajengwa sehemu ya juu huku amembeba Ishmael MABEGANI.  

Note neno :``INASEMEKANA´´



Nianze kuiingia hoja kutoka ANGLE nyingine:....
.....Ukifuatilia HISTORIA ya mji wa Makkat Al Mukarramah aka MECCA na mpaka  KAABA lenyewe ,....
......utakutana na mambo kibao ambayo VYANZO tofauti vya habari vitakueleza kitu kingine.

Kwa mfano ;..


Kuna vyanzo vya habari vidaivyo jiwe BLACK STONE liliwekwa na Nabii Mohammad na kuna vidaivyo ni Abraham na Ishamael waliloliweka.
Kuna waaminio kati ya Hatim na KAABA ndiko waliko zikwa Haggar na Ishmael ingawa kuna wakataao hilo.
Na kuna wadaio Makkah a.k.a BAKKAH a.k.a  Makkat Al Mukarramah au tu MECCA ,....
....ulikuwa MJI muhimu  katika BIASHARA kama kazi za Ptolemy zidaivyo mji huo wakati unaitwa Macoraba kitu ambacho wanahistoria na ARCHAEOLOGY kwa ujumla inapinga kwa kuwa kipindi kinukuliwacho hakuna hata andishi au vinyangarakata vyovyote viashiriavyo uwepo wa MECCA ingawa FALME kibao za eneo hilo na miji mingine katika eneo iko kwenye recodi za kihistoria .


Kwa hiyo ukimsoma Wensinck katika Encyclopedia of Islam, halafu ukaja kusoma ya IMOTI adaiye kuwa kipindi hicho kulikuwa na Kaaba nyingi ila hii iliyobaki leo ndio pekee iliyokuwa ya JIWE na kusababisha iwe ya kiania yake , ukaenda kwa Patricia Crone katika Makkan Trade and the Rise of Islam,.......mpaka ukaja kwa akina Karen Armstrong katika Islam: A Short History, ukaenda kwenye majibu ya Dr. Amaal Muhammad Al-Roubi kwenye kitabu cha -A Response to Patrica Crone's book,......
....HADITH , na mpaka ukaja kumaliza na KITABU KITAKATIFU cha KORANI ,....
....unaweza kujikuta kama LAINI KIIMANI umeshaitia uvuguvugu IMANI yako kama tu WATUMIAO akili baada ya KANISA kuruhusu waumini kujisomea wenyewe BIBLIA wapaparikavyo na MADHEHEBU mbalimbali kisa kuna kitu tu KUHUSU MUNGU wanadhani wanajua.:-(







Kuna watakaodai lakini kuwa ,....
....uhakika tu ni kwamba KAABA ni ya zamani zaidi ya dini ya KIISLAMU na kabla ya UISLAMU wapagani washaabudu sana hapo na HUBAL akiwa ni moja wa miungu MAARUFU wasemekanao waliwahi kuwepo hapo ingawa pia kuna wadaio kuwa mpaka sanamu la Yesu na Maria vilishawahi kuwepo hapo kama MASANAMU tu mengine ambayo inadaiwa kunakipindi yalifikia 360 hapo yote yakiabudiwa.




NIKIRUDI kwenye SWALI lako Damija :

Naongea yote haya na LABDA HATA KUTOKA NJE YA ULICHOULIZA yote ikiwa ni kujaribu tu kusema kuwa ;...
.....sio KWELI watu wote wanakubaliana na MECCA na KAABA kama swali lako ninavyoonyesha KUEGEMEA au tu KUSAJESTI.

Na ni rahisi sana kuhakiki hilo kwa kusoma vitabu tofauti tofauti vya historia ya UISLAM au tu hata kwa ku -GOOGLE hili swala kwa kuwa kirahisi TU  hata kwa kulisoma  pasipo aminika sana kama kwenye WIKIPEDIA na utakuta pamoja na udhaifu wake kama CHANZO CHA HABARI ZA UHAKIKA lakini utastukia kitu kimoja ambacho hakipingiki KIRAHISI  kuwa,....

... hata kuhusu KAABA na MECCA kama tu PICHA uliyotuletea ya padaiwapo alizaliwa YESU,... ....ukiutafuta utata kuhusu UKWELI wake utaupata KWA KUWA UTATA UPO,...
...na kwa hiyo labda tuachie IMANI kuongoza katika hili SWALA  kwa kuwa ni WENYE imani tu ndio watakuwa na asilimia MIA ya KUAMINI vinenwavyo ni FACT.:-(




NACHOJARIBU KUSEMA pia  ni kwamba:


Na kama ilivyo wasio WAISLAMU wengi waaminivyo kuwa kwa kuwa WAISLAMU katika kuswali huelekea KAABA basi hawatofautishi kitendo hicho na cha WAKANISA la KIROMA cha kupigia magoti sanamu ya MARIA ambavyo vyote kwao ni MAKOSA hata kama kwa WAISLAMU KAABA haiko mbele yao kama sanamu ya MAMA Maria ilivyo kwa  WAKATOLIKI,....
..... kitu KIJITOKEZACHO TU TENA  tena ni jinsi WAHUSIKA WATAFSIRIVYO,...
....na tafsiri za watu KIIMANI ni HATARI kitu  ambacho ukicheza nacho kuna maeneo unaweza hata KUKOLIMBWA kwa kuongea wazi wazi mitazamo ambayo huweza kugeuza IMANI za watu kuonekana ni ZA Kibulicheka tu.:-(

Na moja ya DINI ambayo WENGI huogopa kujiingiza waziwazi kuongelea mambo yake ni ya KIISLAMU kwa kuwa  ni moja ya DINI ambayo waumini wake hawataki mchezo na TAFSIRI za ajabu ajabu ya wakiaminicho kitu kifanyacho hata kati ya WAISLAMU na WAISLAMU  ukiwa MSHIA ujihami na WASUNNI na ukiwa MU- AHAMADIYYA ufuataye mafunzo na TAFSIRI za KORANI za Mīrzā Ghulām Aḥmad,...
...wajikuta unakwepa WASUNNI na WASHIA kwa kuwa wote wanaweza kukukolimba,....
.....kitu kichangiacho pia kuzuia kusikia kwa wengi  tafsiri tofauti tofauti watu wazitoazo kwenye KORANI kwa kuwa  kuna hofu kama tu ilivyokuwa kwenye UKRISTO zamani ambapo kama unajua kitu kama vile DUNIA HAIKO kama MEZA inabidi ULE TU KOBISI kwa kuwa ukitamka PAPA na TIMU yake wange KUKOLIMBA.:-(





Na tukiachana nahilo ;...
....nukuu muhimu kuhusu SWALA ZIMA hili nashauri soma mwenyewe: Korani.


Au jaribu pia kucheki watu kama :

Hafiz Ghulam Sarwar's -Muhammad The Holy Prophet

Wensinck, A. J; Ka`ba- Encyclopaedia of Islam

Diane Morgan 's Essential Islam: A Comprehensive Guide to Belief and Practice



Na kwa kuwa siku hizi  Google IPO, basi jaribu pia kutafiti mwenyewe VITABU na SITES unazofikiria zina aminika zaidi hasa ukizingatia:

  1. 1. Chunguza mwandishi ni nani na hakuna hila za kisiri katika aandikacho.
  2. 2.Zingatia kuwa WENGI waandikao wanaweza wakawa wameathiriwa tayari MTAZAMO -nanafikiri unatambua kuwa ni kawaida KITABU alicho andika MSABATO kuhusu kanisa la KIROMA kwa kawaida huwa tofauti na ALICHOANDIKA Padre wa kanisa la Roma kuhusu Kanisa la Roman Katholiki kuhusu swala hilo hilo.
  3.  3.Na wategemeao WIKIPEDIA kunukuu wakumbuke katika WIKIPEDIA hujui ni nani kaandika na anania gani katika hili kuwa ni moja ya UDHAIFU wa kuitegemea kama kweli tupu ingwa inaweza kukupa mwanga kidogo hasa kukupa pia majina kadhaa ya VYANZO vya waliotafiti HABARI hii ukawatafuta na kuwanukuuu moja kwa moja katika mkao wa nani unapenda kuamiani asemacho ndicho kiko karibu zaidi na ukweli.


Na narudia :

SWALA HILI ni la KIIMANI zaidi na umuhimu wa UKWELI utategemea zaidiIMANI YA MTU kwa hiyo cheza nalo KIUANGALIFU la sivyo unawezajikuta umekuwa MPAGANI hivihivi!:-(


Kumbuka inasemekana katika IMANI:
.....A little knowledge is a dangerous thing ,...
...DON'T LET A LITTLE knowledge wreck YOUR FAITH kwa kuwa kunauwezekano- YOU are JUSTIFIED by FAITH alone!:-(


Na kama HITIMISHO:...
....DaMIJA kuhusu swali lako BILA kutaka kuchezea sana  zaidi IMANI za watu kwa kuongea sana mpaka nikwaze zaidi mtu NALIACHIA hapa:-(



Tubadili swala kwa kwenda BRAZIL kukutana na Carlinhos Brown arudie-Ashansu



Carlinhos Brown aendelee na -Zanza


Au tu Carlinhos Brown amalizie na - A Namorada

Read more...

Kuna madhara ya KUKOSA wa kumuigilizia ustaarabu hata wa BAADA ya kwenda haja NDOGO kujifuta utupu!:-(

Na ukikosa ROLE MODEL,...

.... kwa kujifunza mwenyewe UYAJUAYO hata kama kwako ni USTAARABU na juhudi zako za kuyajua zinahitaji KUPIGIWA MAKOFI,...
.... kwa wakuangaliao kwa pembeni wasiofuata ustaarabu wako wanaweza kukuona weye MWANAHARAMU TU!

Swali:
  • Si unajua moja ya kwanini WENYE MYWELE za RASTA kama ZANGU Simon KITURURU hawaheshimiki sana na baadhi ya watu DUNIANI  kwa kuwa kwa USTAARABU wao hawajawahi kukutana na kuona MWENYE NYWELE ZA RASTA astahilie KUHESHIMIWA hasa kutokana na misingi ya USTAARABU wao kutofautiana kitu kiwezacho kuwafanya wafikiri kuwa ni kweli yeyote MWENYE Rasta labda SIO MCHAFU, hatumii madawa ya KULEVYA au tu SIO MVIVU wa mambo mengine yoyote ya kujenga jamii KISTAARABU kama yafanywao na wenye VIPARA na BONGE la kitambi hata kisicho cha uvivu wa kwenda haja KUBWA?


Ndio,...
...wenye VIPARA na vitambi wana wawakilishi katika wadhaniwao ni WASTAARABU,....
... kama tu watembeao uchi KISTAARABU kwa kuwa jamii inakubali ustaarabu wa KUUZA SURA KI-UMISSI KARIAKOO,...
....na kwa hiyo kionekanacho kama CHUPI kikiitwa ni nguo ya KUOGELEA kwa wastaabu hawatakiona ni chupi hasa kama mayoyanyoya ya sehemu za siri ya KIMWANA yalikatwa kabla hajatembea kwa mwendo wa MARINGO mbele ya MAJAJI akitingisha vitako vidogo VIPENDWAVYO katika ustaarabu wa UMISSI NANIHII,....
...na kwa hilo na MAMBO kama HAYO JAMII ndio  hupata ustaarabu na WASTAARABU wa kuwaigilizia KATIKA JAMII.:-(

Swali:
  • AU?
  • Kwani huna MAFISADI wakupao hamu ya kuwaigilizia USTAARABU wao wa KIFISADI wakati ndio WAHESHIMIWAO kwenye jamii?

Ndio,....
..... kuna MADHARA ya kukosa wa kumuigilizia,....
... na moja la MADHARA yake yasemekana ni kuweza MPAKA  kumgeuza KIJANA ASIYE MSENGE mwenye hamu ya kujua YA UKUBWA wafanyayo WAKUBWA FARAGHANI kugeuka BASHA ili ale JICHO la KALIO LA MWANAMUME MWENZAKE wakati MADEMU wapo na mgao wa embe dodo nzuri tu iliyotuna na ISIYO HARAMU kisa wameigilizia kusikofaa KUIGILIZIWA!

Ndio,...
....PAMOJA na mapungufu yake HILI NI WAZO TU MHESHIMIWA na usikonde!:-(


Hebu UB40 katika kubadili MKAO hapa kijiweni warudie-Tell Me - Is It True ?




Au tu SHAGGY abadili zaidi kitoweo kwa PAMBIO iitwayo- Boombastic

Read more...

TIBA ya WOGA wa mende au tu ya wa WATU wengine WATASEMA nini!:-(

>> Sunday, December 26, 2010



Woga kiboko,...
....ndio maana unaweza kuogopa BILA sababu!:-(

Woga ni kiboko,...
... ndio maana ASILIMIA kubwa ya WATU huogopa bila hata kuchunguza KIOGOPWACHO kina madhara kweli YAWATISHAYO matokeo yake unaweza kukuta kuna WAOGOPAO mende , FISI au tu MBWA kuliko BINADAMU WENZIO wajulikanao kwa kuua WATU hata kuliko MBWA na fisi na kufanya hivyo hata BILA za maana sababu.:-(





Swali:
  • AU?

Na TIBA ya woga wa MENDE,....
..... labda ni kumkabili MENDE na katika kuchunguza na kuukabili woga kitu kiwezacho kuwa tiba kwakuwa kwa kumkabili MENDE unaye muogopa unaweza kustukia katika kupigana NGUMI kwa mtu na mende kirahisi sio MENDE atashinda!:-(



Na ukichunguza yote yaogopwayo kama GIZA na sio mende,...
....unaweza kugundua karibu WOGA wote hutokana na kutofikiria hasa nini kinaweza kuwa gizani huko chumbani kwako ambako mwenye funguo ni wewe tu mwenyewe na ukastukia kunauwezekano vyote viogopwavyo MTU hana sababu za kuviogopa kihivyo kwa kuwa labda kitishacho NI HIYO TU HOFU kuliko kitu chenyewe KISABABISHACHO HOFU aka WOGA hasa kwa kuwa ukweli uko pale pale UKIKABILIANA nacho kuna uwezo mkubwa tu ni weye utakayeshinda.

Swali:

  • Hivi leo unakumbuka UNACHOOGOPA ni nini na umekibingilisha kucheki kuwa kina sababu kweli ya kuogopwa au unaogopa tu?
  • SI nasikia mtu aogope asiogope HATA KUTETWA siku ya siku ikifika hata ufanye nini utajikuta umewekwa kati ukisutwa hata umbeya wa enzi za BIBI na MASHOGA zake enzi hizo wakisukana mabutu?


  • Na hata ukiogopa si siku ya siku KUFA kuko palepale tu hata kama kwa kumuogopa MENDE umefanikia kumkwepa maishani mwako yote?


Ndio,...
...KWA BAHATI MBAYA,....
.... labda MENGI yastahiliyo TUYAOGOPE ndio HATUYAOGOPI na yale ambayo tulihitaji kutotishika nayo ndio YANATUTISHA,...
... kitu kifanyacho yale yastahiliyo KUKUMBATIWA ndio tunatoka baruti kuyakwepa na YALE YASTAHILIYO kuogopa ndio twayaingia mpaka chumvini kwa kutoogopa na kulamba visivyolambwa kama ICECREAM aka AISHIKIRIMU  vile-LOH!:-(



Na nimelikatiza hili WAZO Mheshimiwa nisije KUPITILIZA bure likazidi utamu!:-(



Hebu MZEE Yusuf na  Zanzibar Stars waingilie kati kwa -Najiamini



James Brown aseme-I'm BLACK and I'm  Proud



Herbie Hancock aturudishe mwaka 1975 katika kitu-Chameleon


Au tumcheki tu Lenny Kravitz asipokuwa mbele ya kipaza sauti akiimba na badala yake awe kwenye Drums katika wimbo huuhuu wa Herbie Hancock ujulikanao kama -Chameleon

Read more...

MAISHANI kama kingeonjwa PIA kirahisi kila KIDUDE kinukacho VIBAYA,....

>> Saturday, December 25, 2010

.... labda WENGI wangegundua HARUFU na utamu labda havina uhusiano wa karibu KIHIVYO.:-(


Swali:
  • Si inawezekana mtoto wa PWANI azimiaye PILAU anaweza asihusishe harufu ya MATOKE na utamu wa MATOKE  azimiayo MHAYA?

Na  kunusa,...
.....ndio moja ya siri  KWANINI kuna virukwavyo VITAMU ,...
....ingawa PIA kuna vijulikanavyo tu ni kwa kuwa vimeoshwa ndio maana wakati vinaonjwa havinuki na wanusao,...
....  ambao wamezoea kuoanisha  HARUFU na utamu,....
...huku wakijua HARUFU sio UTAMU!:-(


Swali:
  • Si inakumbukwa EMBE halinukii kama NDIZI ingawa labda vyote ni vitamu?


Ndio,...
....kama alivyo SENENE na harufu zake mtamu,...
.....kuna waaminio kiutamu zaidi ni KUMBIKUMBI  hasa  wakati anakaangwa kifanyacho  harufu yake pia iwe moja ya UTAMU!:-(





NAACHA wazo!

Na hebu tubadili wazo na kukumbushwa UTUMWA na Burning Spear katika -Slavery days


Read more...

Labda KUNA maigizo KANISANI , maigizo katika GWARIDE la KIJESHI uwanja wa TAIFA kama tu ilivyo ni maigizo kwa WALIOVAA ULIMBWENDE watikisao tako MTAANI!:-(

Ukiangali,....
...... kuanzia majoho ya MAASKOFU na WACHUNGAJI makanisani,....
..... mpaka mwendo wao  katika kutaka kuonekana ni watakatifu zaidi  labda  NI MAIGIZO tu kwa kuwa MUONEKANO wao  hauna uhusiano na neno  waumini walilolifuata lile la MUNGU.:-(





Hebu mchungulie PAPA BENNY  kabla hajaanza kuongea KITU katika mavazi na UTEMBEAJI wake na uniambie kifanyikacho hapa hakina uhusiano na VIFANYWAVYO na akina Mzee Jangala katika kudaka watazamaji ki-THEATRICAL a.k.a kimaigizo....



Ndio,...
....naamini MENGI yafanywayo na WAHUBIRI katika sehemu za DINI karibu zote nizijuazo,....
....hayana tofauti  sana na yafanyikayo kwa WAGANGA wa kienyeji katika kufanya vituko KUCHEZA MAIGIZO ili kukuweka mkao wa KUINGIZWA mkenge  ,...
......kwa  kuwa vingi ni vituko vya MAIGIZO TU ambavyo kwa mfano MAKANISANI havina uhusiano na NENO la MUNGU na kwa mganga wa KIENYEJI huwa wala havihusiani na tiba utakayo pewa ni kwanini MGANGA anatoa sauti za ajabu na kukuvalia mafuvu ya BUNDI au kibwaya cha ajabu ajabu katika MAIGIZO ya kukufanya uamini afanyacho kina ukweli  kwa kuwa kinakufanya ukae KISAIKOLOJIA mkao wakutishika au kujisikia unashuhudia kikweli NGUVU za KILICHO na nguvu zaidi yako.:-(


Swali:
  • AU?
  • Unafikiri MAJOHO ya WAHUBIRI neno la MUNGU pamoja na sauti zao walizojifunza kutolea NENO LA MUNGU vina uhusiano na nini hasa MUNGU anataka kusema?



Tukiachana nahilo,....

...... na  tukiangalia wafanyayo WANAJESHI kwenye magwaride ya KIJESHI  mpaka ya KUPIGA KWATA mpaka VIATU VINACHAKAA SIKU MOJA kama sio mpaka kuruka juu mbele ya JUKWAA LA WAHESHIMIWA,...
.....hasa wakati wa AMANI ,....
....unafikiri sio MAIGIZO tu wafanyayo na YUNIFOMU zao ili WANANCHI waingie mkenge kuwa mpaka TANZANIA inaweza kulidindishia hata jeshi la Africa Kusini kama likileta KIBEZI  tu kama cha JESHI la MAREKANI,...
.....kitu ambacho inaweza kuwa ni ALINACHA ukizingatia hata RADAR yenyewe mtumba wajanja walio kula dili kuna uwezekano ni moja ya pambo tu  kama mapambo mengine ya uwanja wa MAIGIZO kabla MZEE JANGALA hajaingia kuigiza?




CHeki tisha toto za wanajeshi KOREA KUSINI.....



Tukiachana na hilo.....

..... bado  nadhani kuna atakaye kubaliana nami kuwa,....
...... kuna watu wana mwendo wa MITAANI kama ilivyo kuwa kuna nguo wazivaazo tu MITAANI kwa kuwa wanategemea kuangaliwa na watu kama tu walivyo wenye nguo maalumu CHUMBANI na vitendo tofauti kama ni a ni kuangaliwa na mpenzi  ,....
.....kitu kigeuzacho wafanyayo mtaani KAMA CHUMBANI katika MWENDO na vitendo kuweza  kukwalifai kama MAIGIZO tu .lwa kuwa kihalihalisi CHOONI kusiko na washuhudiao mambo huwa tofauti.:-(



Swali:
  • Unafikiri umzimiaye kwa mwendo na sauti OFISINI ana mwendo uleule na sauti ileile nyororo katika choo cha ofisi aliko pekee?


Nawaza tu kwa SAUTI Mheshimiwa na wala usikonde!:-(


Hebu Tabu LEY arudie- SARAH




Jacob Desvarieux aingilie kati na-Mwen malad aw


Au tu naye  Papa Wemba amalizie tu tena kwa kinu-Oldies are goodies

Read more...

Nawatakieni NOELI njema WADAU wote wa BLOGU HII!

>> Friday, December 24, 2010

Ndio huwa sisherehekei HII KITU,...
.....kwa sababu KADHAA wa kadhaa ,...
...au ngojea nijaribu kujielezea KUHUSU kwanini shamrashamra  hizi NIKIWAZA huwa zinanikwaza......




Kwa msherehekeao,....
.....KHERI ya X-MASS!








Asanteni sana pia  WADAU wa  blogu ya,....
....CHEKA UPASUKE ,....
......kwa kadi mwanana hii....



Tuko Pamoja sana tu  Wakuu hata katika SIKU za kubunia ANGALAU tarehe kama HIZI !






Hebu watoto wa mujini ya  BONGO kwa jina UMABE arts COMPANY warudie  tena jiwe -MERRY Xmas AND HAPPY NEW YEAR!

Read more...

Kificha NYETI ni UBONGO,...

... na KATIKA  kiona nyeti  labda macho yanasingiziwa kwa kuwa hata yakichungulia HAYAELEWI kile  UBONGO unafanya mtu akiona ATAJUA.:-(

Na mwili wa mtu ni UDONGO,...
..... na hata nyama za mwili labda zasingiziwa na kuna mpaka KABURI la MTU laweza kutoa ushahidi wa hilo kwa WASIOJUA.:-(


Na labda HATA matatizo ya LADHA yako kwenye ulimi na sio wote MDOMO,....
.... na labda  wala sio TUMBO lenye tatizo na chakula chenye ladha iliyochacha NA mwenye njaa na asiye na chaguo la CHAKULA anaweza hilo KUJUA.:-(

Na mtu akinywa hata sumu LABDA  kiuacho sio tumbo ,....
....sumu ilikonyonyewa KUINGIA KWENYE MZUNGUKO WA DAMU  kama kizimikacho KUDUNDA ni moyo na ubongo ufanyao aliye hai  AKIFA iwe kuwa  MAREHEMU aliwahi TU kitu KUJUA.:-(

Swali:

  • SI kwa wenye macho husahau ni UBONGO uonao na MACHO bila ubongo hakutakuwa na sababu ya kujitahidi kumchungulia aliyevaa sketi fupi na kakaa vibaya kwa kuwa hakuna KILICHOKUNJA SURA huko chini kitakacho tambuliwa kama kuna macho NA UBONGO utambuao konokono katikati ya vyura hakuna ?


  • Na si  kificha nyeti hugeuka tu kwa baadhi kutambulika kama CHUPI kama UBONGO ndivyo hivyo unatambua?
Ndio,...
... kificha NYETI ni UBONGO,....
....na siri nyeti ni UBONGO uwatunziao WANAOJUA.:-(

NI WAZO tu hili MHESHIMIWA!:-(
Siku njema BASI Mkuu!







Hebu Boyz II Men waingilie kati shughuli kwa - Doin' Just Fine




Brian McKnight asawazishe kwa - Back At One




Au tu turudi Kameruni RICHARD  BONA abadili tu kwa -Eyando

Read more...

Kwa KAWAIDA aoaye zaidi ya MKE MMOJA KWA MAPENZI KAMILI kutoka MOYONI huoa WANAWAKE wasiofanana!:-(

Kuna uwezekano BINADAMU hana kipimo cha uhakika  kithibitishacho kuwa,...
....haiwezekani kwa MTU kupenda vyakula viwili vya aina tofauti tofauti kwa usawa,...
.... kitu kifanyacho WATU waamini kama wewe ni MPENZI  wa UTANDU SANA hauwezi kuupenda na UKOKO hivyo hivyo sawasawa kama idaiwavyo kama mtu anapenda sana UGALI hawezi kuupenda wali hivyohivyo kwa kipimo cha UPENDO sawa,....
... kitu kifanyacho watu waamini kuwa kama unampenda sana ASHURA kwa kuwa ana bonge la sura lenye MWANYA kama mfereji wa maji machafu na DIMPOZ kama kama  mashimo ya choo cha shule ya msingi ya jirani ihitajiyo msaada wa DANIDA ili choo kimalizike,...
.........
......basi huwezi kumpenda hivyo hivyo KWA MAPENZI SAWASAWA kimwana ASHA ambaye umpendeacho ni TABIA na  kiuno chake kama NYIGU mjamzito na MAKALIO YAKE aka SANGARA WAMO  kama masufuria  makubwa ya kupikia ubwabwa MSIBANI.:-(

Swali:
  • Kwani unauhakika UPENDO unapimika mpaka uamini aina tofautitofauti za mapenzi  yako KUMI kwenye mzani wa MAPENZI sio ngoma DROO?


  • SI ni kawaida hata kwa MPENDA magari  kununua magari ya aina tofautitofauti  kwa kuwa MAPENZI hutosha kupenda  zaidi ya PICK UP truck?


Ndio,...
....LABDA mapenzi ya MTU yanauwezo wa KUKUMBATIA upendo wa AINA NYINGI kiaina nyingi,...
.... ndio maana MTU MMOJA amepewa uwezo wa kupenda watu wengi wenye TABIA za aina nyingi TOFAUTITOFAUTI ,...
.... na hapa siongelei uwezekano wa kuwa mtu anaweza kumpenda MAMA YAKE sawa tu kiujazo na  ampendavyo SHEKHE wake amfundishaye DINI  na kumfanya ajisikie kuwa AHERA hata enda ,...
.....hata kama katika hilo KUNA wadhaniao kuna tofauti KIUPENDO.:-(

Swali:
  • Si nasikia kuna wadaio wanamapenzi tofauti kwa MAMA na kwa BABA waliowazaa kitu ambacho labda kungekuwa na mzani upimao tani za upendo labda ingegundulika hilo si sahihi kwa kuwa Mapenzi kwa MAMA hata kama ni tofauti bado = kwa mapenzi ya mwana kwa BABA?

Na samahani,...
.....labda kwa kuwa UMEPENDWA,....
.....weye unakuza uwezekano tu wa atakaye kuja KUPENDWA mwingine asiwe na LIPUA kama lako aka asifanane na WEYE kwa kuwa ni kweli DUNIA IMEJAA wengi wazuri na ukiacha wale wafananafananao na WEYE KIUZURI MWANANA ,...
... wapo  pia wengi tu aka CHUNGU MZIMA wenye sura na tabia tofauti halafu kwa bahati mbaya eti na kwa hilo nao WANAVUTIA na kupendeka tu.:-(

Swali:
  • Ukifuatilia uliowapenda tokea SHULE ya vidudu hustukiii labda umpendaye siku hizi ndiyo yule mwenye BONGE la pua?




Ndio,...
... UPENDO ni  KIBOKO,....
...na ndio maana kuna walitumiao PENZI kama kiboko kuwachapia wenzio na chamoto wanakiona!:-(

Naendelea KUWAZA!:-(

Hebu tumuachie Myahudi Barbra Streisand aimbe kuhusu wasichoamini WAYAHUDI katika-Silent night

Read more...

Nguvu!

Kama NI NGUVU kweli,...
....labda haihitaji msaada wakiitwacho KUTUMIA NGUVU!:-(





Na siri ya UDHAIFU ya kweli,.....
.... labda aijuaye ni  aonekanaye katika suluhisho akitumia NGUVU.:-(




Na ni kweli,...
...kama MTU anatumia NGUVU  kuna  kitu katika yeye hata kama ni HOJA TU hakina nguvu.:-(



NGUVU!

Kama kijambo tu mwilini ,...
...nguvu kila MTU anayo:-(

Na UBONGO ukipewa nafasi ya kukokotoa na kutambua mambo AKILINI;...
.... labda mengi ya watu YENYE NGUVU YATASTUKIWA  na ya watumiao MISULI kwa kutatua kwa kiitwacho ndio matumizi ya nguvu UKIZINGATIA  labda wameamrishwa na KIONGOZI wao ASIYE NA MIJISULI ndo utafahamu kama ni kweli KIITWACHO NGUVU ni wao wanacho KAMA VILE  moja ya miongoni mwa WAJIVUNIAYO katika waliyonayo.:-(

NGUVU!

Siri ya nguvu ya MTU yaweza kuwa ni jinsi tu atikisavyo tako,....
.... kama mwendo wa maringo huo UTIKISAO kalio ndio siri ya UDHAIFU wa achunwaye buzi  kwa kuwa ndicho kifanyacho awe mnyonge kwa mtikisa tako na YOTE bila ubishi  akubali!

Swali:
  • Si inajulikana ASILIMIA KUBWA ya wenye nguvu sana duniani  kwa WENGI hata mpaka  JUU YAKO ni WALE ambao hawajawahi kutumia kitafsiriwacho kwa lugha ya kawaida kama ni nguvu zihitajizo angalau msuli  JUU YAKO?





Naendelea KUWAZA.....:-(


Hebu tujifunze matumizi ya BIBLIA kwa kumsikiliza Joshua Evans katika -How the Bible Led Me to Islam





Hebu tutishane kidogo  kwa-OBAMA Worships SATAN




Au tu ngojea Snoop DOGG na Dr Dre wabadili tu mkao hapa kijiweni na kutuliza mshawasha KIBUSARA ZAIDI kwa ujumbe mzito kwa walengwa kuwa -Let me ride/Still Dre

Read more...

Uzuri wa CHUKI hata kama kichukiwacho sasa hivi ni CHUPI na sio MTU.:-(

>> Thursday, December 23, 2010

CHUKI huweza kuwa ndicho KIMPANDISHACHO mtu,....
....nguvu ya kutatua swala ALICHUKIALO.:-(


Swali:
  • Hivi unafikiri hakuna uwezekano WATANZANIA kuna kitu hawajakichukia vizuri kama CHUKI zao bado hazifanyi kivitendo yadaiwayo kwa maneno yanachukiwa  KUTATULIWA badala ya kuwa ndio kwanza yananeemeka?

  • Kwani unauhakika ASILIMIA MIA hakuna uzuri wa kuchukia hata MTU kama mapendo yako ndio yangemtia matatizoni ?

Ndio,...
.... labda kila KITU kina UZURI WAKE PIA ikiwemo mpaka CHUKI.:-(


Ndio,...
.....labda hata SHETANI ana UZURI WAKE  kama ndiye akufanyaye ujipendekeze kwa MUNGU ili usiingie mkenge na kuvaa ihubiriwayo ya wenye DHAMBI  uaminio ni ichukiwayo na  MUNGU WAKO hata kama huamini MUNGU WAKO ana  CHUKI!:-(


SAMAHANI naendelea KUWAZA......:-(






Hebu SHA SHA JONES arudie-Blow my MIND



Au tu BAHA MEN waingilie kati shughuli kwa -WHO let the dogs out?

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP