Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama CHAKULA hakitoshi - labda BINADAMU kugombania hata UKOKO ndio UBINADAMU wenyewe!:-(

>> Thursday, December 16, 2010

Kama MSOSI hautoshi,...
..... labda ni UBINADAMU kwa MTUZ kugombania chochote ADIMU kilikacho,...
... na sio UBINADAMU kwa BINADAMU kuwa mstaarabu wakati huo na kuachia wengine KIDUDE wale!:-(



Tukiachana na swala la BINADAMU kugombania TONGE kisa FINYANGO halitoshi,....
....yasemekana KIUMBE BINADAMU alivyojengeka kukabili swala la SURVIVAL a.k.a kupigania kuendeleza UPUMUAJI,....
.... kama kuna UADIMU wa kusaidia kitengeneza KINYESI au tu chochote kimsaidiacho BINADAMU   amani ya kuishi-  MTUZ kwa kawaida zimeumbwa ziwe na KIBEZI hata cha kupiga BONGE la konde   SIMBA ili mradi tu ikiwa ni katika  kutetea  TONGE hata bila kufikiria zifanyacho   ili ZILE  KIDUDE ndio pengine baadaye baada ya kutia ndani ZIANZE KUFIKIRIA wapendwa  wengine katika kinyang'anyiro nao waonje kidude  a.k.a  nao WALE.:-(


Ndio ,...
....yasemekana KWA WASTAARABU ni UBINADAMU,....
..... KHALIFA kumuachia JUMA ale kidude,....
..... katika mazingira ya ustaarabu wa KHALIFA ambaye kistaarabu  anaamini JUMA ndiye mwenye njaa zaidi ya kidude.:-(

Swali:

  • Lakini unauhakika BINADAMU ni wastaarabu  hivyo wakati wana njaa?

Ndio,....

... inasemekana MAMA  anaweza asigombee chakula na mtoto wake  na kukubali kushinda na njaa ilimradi MTOTO wake ale.

Swali:
  • Si inakumbukwa hakuna MAMA ya wote  na ndio maana kuna WAITWAO MAMA  WA KAMBO ambao chakula kama hakitoshi  huchagua watoto wake ndio wale KWANZA vya kutosha wakati toto la KAMBO limetumwa  kwenda kumwaga majivu kwenye choo cha shimo ili kisinuke?


Nawaza tu hapa MKUU na wala USIKONDE!
Umekula lakini leo MKUU bila kupigania ukoko?
Tunashukuru kama umepata kisaidia kwenda haja kubwa bila taabu leo MHESHIMIWA!

Basi BWANA ngojea tu pate Funky COLD MEDINA kutoka kwa TONE LOC

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP