Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

JAMBA TU!Si uko peke YAKO?

>> Friday, December 26, 2008

Inasemekana kila kitu kina mahali pake hasa kwa WAHESHIMIWA wenye tabia nzuri.

Binadamu anajifunza tabia nzuri tokea azaliwe na ikibidi ahisicho ni tabia mbaya hawezi kukifanya kwenye umati kama hakilipi ,INGAWA ni machoni mwa jamii yenye watu wenye tabia mbaya wajulikanao kwa ustaarabu wa mazuri.

Kujamba ni muhimu!

Staili ya kujamba na mahali ajambapo mtu inaweza kukuambia TABIA ya mtu ,alivyolelewa MTU na hata UHURU wa MTU kisaikolojia kama sio hata jinsi alivyo MBUNIFU katika MAISHA.

Unaweza kuchagua mpaka MKE kwa kufuatilia anajambaje na anajamba wapi.

Staili ya mtu kuficha kajamba, inaweza kukuambia jinsi gani ni MUONGO au awezavyo kukudanganya hata kwa vitu vya kawaida.

Swali:


  • Kujamba si ni kitu cha kawaida kwa binadamu alaye kuliko hata kuvaa nguo?

  • Unakumbuka mavi na wenzie huanza kunuka kabla ya kunya na labda HUNUKA tokea tumboni?

Na pia...
...UHURU ni kitu cha ajabu!


Kama unataka kupima jinsi gani uko huru, jamba uhisipo si pa kujamba halafu sikilizia kama unaona aibu au unajisikia kuondoka maeneo kwa sababu ya MAFANIKIO ya USHUZI au LA , wakati watu wanajua ni WEWE uliyeachia ushuzi.

Kumbuka lakini...

.....kuna tamaduni , kama hujajamba au kucheua, hujashiba wewe, na ugali utaongezwa!

Na labda...
... ni busara kabla hujaoa au kuolewa ujue staili za kujamba, mahali pa kujamba au tu wajambavyo UKWENI.

Kumbuka lakini..

...labda kujamba haimaanishi KUJAMBA katika HADITHI HII, ingawa tabia fulani za binadamu ni USHUZI!:-(

JAMBA TU, hatusikii wala hatukuoni!

Jamba tu mtoto MZURI, utajisikia AHUENI!

DUH!
Naacha!

SIKU NJEMA!

AU hebu Tutembelee kidogo PARIS kuangalia jinsi WANAFUNZI wa VYUO VIKUU TANZANIA watakavyokuwa wakiandamana Mwakani....




AU ngojea Future MAN , Fleck na Victor Wooten wanisaidie KUfankifai kama sio Kujazzifai ,katika LET ME BE THE ONE.....



Au turudi tu KENYA kwa Safari Sound Band waendeleze CHAKACHA...

Read more...

Swala la UJANJA ni kusikiliza MIZIKI topu teni!

Kuna wadaio miziki mizuri iko topu teni!

Na..
...wakipenda labda penda kwa sababu WANAPENDA ingawa wapendacho kama ni BEBERU ,basi anapenda KUNUSA mpaka uvundo wa sehemu za haja kubwa za mbuzi inagawa sehemu hizo kwa mchoma nyama labda sio shilingi teni.


Inasemekana umaarufu wa kitu topu teni ni kwa sababu masikioni mwa wengi ni bomba.
Ingawa swala hili laweza kukufanya ujiulizea pia mchango wa video zisindikizao muziki hufanyanini katika kuufanya wimbo mzuri wa mazishi uwe bomba harusini.

Na nikweli..
....miziki mizuri ya dini utaisikia mpaka kwenye vilabu vya pombe Uchagani kama tu ile ikatazayo uzizi ipigwavyo kwenye gesti ya jirani.

Swali:

  • Kwani miziki mizuri ni ile tu uisikiayo redioni?
  • Hivi unafikiria ni kwanini kuna wapendao hard rock na wapendao ngwasuma?
  • Unauhakika hujashawishiwa kupenda miziki uipendayo na labda mlio wa mbuzi kwako ungekuwa mziki tosha?



Lakini.....
.. miziki topu teni ya Baba , labda kwa Babu ilikuwa makelele masikioni.

Na ...
... miziki mingi rahisi ndio hua maarufu kwa wengi ndio maana iko topu teni.

Na labda ...
... kama wewe ni mpenda miziki iliyo topu teni, inawezekana unapenda vitu rahisirahisi kama maharage ya Mbeya, na usishangae KISAIKOLOJIA kuwa, wewe si mvumilivu na labda mvivu hata kama ni mvivu wa kusukuma mkokoteni.

Lakini...
.. Chekibobu na SistaDU labda waonekana wajanja na ni maarufu KWENYE PATI kwa kujua miziki topu teni!

Ila..
.. ukifikiria sana , inawezekana miziki upendayo umechaguliwa na sio chaguo lako kwa sababu wewe mvivu na usikilizacho ni usikilizwacho na ndio maana kwenye pati yetu ya kunema usipokuja labda tutapata ahueni.

Swali:

  • Ushawahi kusikia mziki kwa kumsikiliza aliaye?


Samahani naenda kukojoa!
Baadaye!


Au pata kidogo muziki wa Eartha Kitt ambaye ametutoka jana . Pamoja na kwamba alifanya show Afrika Kusini kipindi cha ubaguzi wa rangi , R.I.P Eartha...

Asante kwa wimbo huu Santa Baby

Au tu turudi Kenya kukutana na Safari Sound Band watuletee ya MPENZI ,kwa sauti ya kubaniwa pua....

Read more...

Kwa MWALIMU tishaTOTO!

>> Thursday, December 25, 2008

Umejifunza KUTISHA asikuulize....
...kwa imani akiuliza labda hujui.

Katika jamii ya ujanja kujua...
......yasahaulika mwalimu ni mwanafunzi, na mwanafunzi hajui.

Usingetisha...
....ungehakikisha hujui kwa sababu unajua HUJUI.

Labda..
...ungejiuliza kwanini hujui!

Labda ungejiuliza kwa nini HUJUI.

Yasemekana malaika wa Mungu hawajui ,
.. ndio maana malaika shetani anamjaribu Mungu kwa kuwa hajui.

Lakini kwanini ujiulize...
...ikiwa ukijiuliza haitabadili UKWELI tunajua HUJUI nautabaki hujui?

Sijui , hujui!

Labda...
...Unajua , sijui!


Lakini....
...Kifurahishacho ni nini kama sijui?

..........................._________________------------------------

Naacha!
Nawaza tu hapa mkuu!
Nakutakia mafanikio chooni leo!

Ngojea tujifunze jambo muhimu kama kufungua SIDILIA.....katika How To Undo Her Bra With One Hand...(Usiangalie kama wewe mtoto, padre, sister au utakwazika tu!)



Au tu Tenor Saw anisaidie katika Ring the Alarm....

Read more...

Busara za:LABDA jishikize TU katika ujuacho, usije ukajinyea BURE, kwa kutokujua!

Kujitahidi inaruhusiwa!

Lakini...
...kuna wanaoshauri mtu ajitahidi kwa liwezekanalo.

Swali:

  • Ni nini hakiwezekani kama kila binadamu anaweza mpaka kufa?
  • Lakini unafikiri kuna aliyejitahidi kunya keki?

Labda..
...kama watu wasingefanya wasichojua , hakuna ambaye angezaliwa, halafu kungekuwa hakuna VIBATARI.

Tumezaliwa hatujui ingawa matumizi ya CHUCHU ya NYONYO yalivutia mtoto, LABDA kwa sababu tusizozijua kama tu ziendeleavyo kutushangaza kwa kuvutia wanaume MIDEVU ya MVI katika kulilia nyonyo hata wasizozijua.


Sikatai!

Ukijishikiza katika ujuacho kunauwezekano hauta haribu kwa kutokujua.

Tatizo ni....

...labda maana ya maisha ni kutaka kujua ndio maana tulizaliwa hatujui.

Na ni kweli....
....labda KATIKA kuhangaikia kujua , unaweza ukakosea kujua kuwa Mwanaidi sio Sikujua, ingawa wote ni watu na ndio maana ADUI YA MTU mkubwa, ni MTU, na kisingizio cha kwanini nimeharibu ni; SIKUJUA.

Swali:

  • Hivi si ulijifunza hata kunanihii kwa sababu hukujua?
  • AU?



Naacha!
Ngojea SHAGGY ft Rihanna na MR BEAN watusaidie kupata hekima katika ....


Au WAHESHIMIWA wazee a.k.a Senior Citizen Choir watuburudishe kwa HIP HOP....

Au nimuachie COMMON enzi hizo, amalizie katika...Take it Easy


Read more...

FURAHIA KRISMASI haraka haraka KAMA UNADHAMBI, Yesu asijerudi ghafla BURE kabla hujamalizia DHAMBI!

>> Wednesday, December 24, 2008

YESU akirudi SIKU YA KRISMASI kama wewe ni miongoni mwa waaminiyo ya Nabii Issa a.k.a Mwokozi, kuna watakaostukia zawadi za krismasi walizopewa na KUTAKA ,ni MATUSI.


Labda..
....krismasi ni nzuri kama inakukumbusha ya YESU na ufanyacho ilikufurahia kuzaliwa kwa YESU si dhambi.

Na..
... kama huamini ya YESU kwa kuwa ulistukia dini nyingine za wajanja wakutishao pia, kazi kwako kwa sababu inasemekana kwa waaminio; YESU ni MTOTO wa MUNGU mwenye huruma na NI MUNGU mwenye huruma asiyesita kukuchoma kama UNA DHAMBI.

ANZA KUFURAHIA!
Yesu anaweza kurudi kabla UBWABWA haujaisha!

:-(


Kama wewe unamchezo wa kuamini, TUBU ,SHAURI ZAKO!

Swali:

  • Hivi ubwabwa hautoshi katika kufurahia PASAKA mpaka utake nanihii?
  • Kwa waaminio , unachekelea zaidi kufa au kuzaliwa kwa MWOKOZI ,ndio maana una suti ya PENTEKOSTE?



NAACHA!
Niombeeni kama huwa mnakumbuka KUSHUKURU na sio KUOMBA TU , nisifanye dhambi siku ya Krismasi na ubwabwa upatikane!


Kumbukeni wasionahata chakusherehekea kutokana na maumivu ya kila siku ya kuchacha, magonjwa na hata wale wasahauo ukweli wa siku hii kuwa NI ya kubunia na labda yesu alizaliwa Julai kama Father Krismasi!

KRISTMASI NJEMA KWENU WOTE!

Tulia na STRAIGHT no CHASER waongelee KRISMASI.....katika....The 12 Days Of Christmas



Au tu tuendelee na ZOUK kutoka kwa JOCELYNE BEROARD aendeleze za - VINI SéRé

Read more...

SWALA la WAAMINIO umasikini wa RAIS NYERERE kwa KUFARIKI bila BENZI la KIFISADI!

Umaskini wa mwenye ghorofa ATOSHEKAYE na KIBANDA, ni wa afaye na GHOROFA.

Na...
...tajiri wa KIMASAI mwenye katambuga, labda KATAMBUGA ni MOKASINI.

Udhanialo linakupa umaarufu kwa wadhaniao WEWE BABU KUBWA kwa kuwa UNABONGA UNG'ENG'E, linaweza kukukosesha MWANADADA wa KIPARE kijijini kwa ukosefu wako wa KITHEMBE kwenye lugha.

Swali:

  • Utajiri wako unausikilizia kwenye gari gani wakati utajiri ni baiskeli au baiskeli bomba mbili ya hamilton kama ya swala hauna?



Ndio....
.....wajuzi wa lugha hawawezi kukubishia kuwa neno fisadi linaweza kuwakilisha kitumbua kama kitumbua kingeitwa jina FISADI.

Na...
.... neno fisadi si msaada kama litalengwa kwa waliodakwa tu wakiFISADI na wadhaniwao mafisadi wakati fisadi analipa mishahara ya wachunguzao MAFISADI .

Tatizo ni...
.....wadhaniwao ni mafisadi ni wengi na labda si kweli ni mafisadi ingawa jamii yenye uchungu iko bize kutafuta wakumlaumu a.k.a ze FISADI, kutokana na hali halisi ngumu ingawa kwa mazingaombwe fulani kunaambao wananawili na labda KIFISADI.

Hapa sisemi kuwa akina Kikwete, Mkapa au Mwalimu wao Nyerere ni mafisadi , kwa kuwa sina uhakika na haisaidii kitu ikiwa mara zote ni kibaka ATAUAWA na sio FISADI.

Na....

Mungu amlaze mahali pema peponi Rais Nyerere, na kama hataki kulala anataka kwenda disko ,na iwe hivyo kwa angalau kutupa cha kufananisha wakati hali halisi kibano inatusababisha tumtafute MCHAWI FISADI.

Swali:

  • Hivi kipindi cha Nyerere hakukuwa na kibano ingawa waliozaliwa juzi walienda shule?
  • Wakati mafisadi wanatufisadi , kibano gani kizuri kuvumilia na RTC hakuna?
  • Katika wafisadi mia uwalalamikiao , ni mafisadi wangapi unauhakika na kuthibitisha WAMEFISADI?

    NAACHA!

    Ngojea tumpate Louis Armstrong aJAZIFAI katika Wonderful WORLD yenye UFISADI...

Read more...

SIMULIZI za titi KUBWA-chuchu HAKUNA.

>> Tuesday, December 23, 2008

Akitaka kunyonya inyonyeke ,
......labda titi lahitaji MSAADA wa chuchu hata kama maziwa hakuna.


Labda.....!,,

Mtoto mpenda maziwa kunyonya,
...atanyonya mpira hata kama chupa ya maziwa hakuna.

Uzuri wa titi dogo-CHUCHU kubwa,
.....ni ahadi ZA UWEZEKANO wa kabali ya midomo kwenye titi,
............hata kama hamu ya KUNYONYA au WAKUNYONYA bado hakuna.

Umuhimu wa titi kubwa ni nini,
.....kama angalau ahadi zipigiwazo debe na chuchu
........kuwa mtoto atanyonya hakuna?

Na ..
..ni kweli TITI ni muhimu,
.....ingawa uzuri wa TITI labda ni kilema kama CHUCHU hakuna.

Na...
...ndani ya tamaduni,
...... WAHESHIMIWA tulikuwa hatufuniki chuchu wala titi
............ na SIDILIA zilikuwa hakuna!
----------------------------------________________------------------------------------------
NAACHA!

Swali:


  • Chupi KUBWA ya nini kama hata matako MADOGO hakuna?


Tupumzike kwa kurudi Tanzania kwa Mr Blue aendeleze simulizi za MAPOZI..


Au FRANKIE PAUL azungumzie ya SHUB IN...

Read more...

SIMULIZI za teremka TUKAZE!

Teremka tukaze ni kitanda ,
....ingawa chini ya godoro au mkeka hakuna SPRINGI

Tunawaelewa wajivuniao KITANDA kwa sababu ya springi,
........ingawa kitanda inajulikana si lazima kiwe na SPRINGI.

Kuna wanesao katika usafiri GIA BOKSI manyoya kwa spidi ,
........na torori lisinyemke kutokana na UKUBWA wa SPRINGI.

Kasi ya spidi si muhimu,
..hata kwa msaada wa teremka tukaze
........kama UMECHOKA-hajaCHOKA na juhudi zake za SPIDI,
..............matunda yake hayashikiki kama saa uhitajiwayoKUKIMBIA
....................hauna SPIDI.



Teremka!
Basi likikwama,
....labda MAMBO YAKO CHINI, na TARATIBU ni spidi.

Na ...
...labda ni aina tu ya utakavyo kunesa ikuamliayo ulale mkekani
........ na sio kwenye kitanda cha SPRINGI.

Swali:

  • AU?
  • Kwani unafikiri naongelea nini?

Naacha!

Ngojea mke wa John Depp a.k.a Venessa Paradis atulize kwa stori ya JOE le TAXI...


Au tu twende Holland kwa ANOUK azungumzie ya ASIYE MKE wa MTU katika NOBODY'S WIFE.....

Read more...

UMEMSAIDIA marehemu KUFA LEO?

>> Sunday, December 21, 2008

Labda....
.... ni kweli marehemu hahitaji msaada wakuendelea KUFA.

Na..
... kuna mengi tunafanya bila kufikiria mchango wake kwa YAI ni YAI kuwa YAI VIZA.

Yapo tufanyayo katika kujaribu kubomoa GESTI YA MAKUTI bila kustukia tunachangia sehemu sehemu pajengwe GUEST HOUSE ya ghorofa.

Na ni kweli...
... mfurahia paja la kuku ni amlaye MAREHEMU KUKU.

Na bado ni kweli...
...binadamu aliyemjengea banda BATA wa kufugwa, anaweza kusahau KUKU alikuwa anaishi bila KIBANDA , bila viatu, KABLA YA KUFUGWA.

NA NI UKWELI...
....mchango wa binadamu kwa kuku mwenye KIKOHOZI labda ni ugonjwa wa MDONDO.

Swali:

  • Pamoja na kutonielewa, UMEMSAIDIA MTU KUISHI LEO?

NAACHA!
_________________________________________________
Leo ni JUMAPILI hebu tukumbushwe NABII ISSA a.k.a YESU ingawa sinauhakika na staili ya wimbo....


Au GYPTIAN azungumzie MWANAMKE MZURI...katika BEAUTIFUL LADY

Au LUCKY DUBE azungumze MAPENZI katika.....I Want To Know What Love Is

AU tu GYPTIAN aendeleze mapenzi katika..I CAN FEEL UR PAIN...


JUMAPILI NJEMA!

Read more...

KAMA bado unashindana na ASIYE asili ya SHINDANO!

Unaweza kujisifia mpaka kumshinda anywaye juisi ya machungwa kwa kuwa UMEKULA MACHUNGWA.

Inawezekana tatizo utibulo kwa kula machungwa , mwenzio uliyemshinda kalitibu kwa kunywa juisi ya machungwa.

Tusipo angalia tutapigana na mesenja wakati asili ya ujumbe ni kwa kibosile tujipendekezaye kwake kwa kumuona ni mtakatifu kwa kuwa anatupa Fanta ya machungwa.

Swali:

  • Si ni kawaida kuwafukuza na kuwalalamikia ombaomba masikini barabarani bila kutatua au kuondoa umasikini barabarani?

Unaweza kushinda kula machenza katika shindano la MSHINDI kupewa Machungwa ingawa tatizo ni ukosefu wa DAGAA.


Na ..
... inasemekana ushindani ni bora kwa sababu huboresha kuwepo kwa watu wenye mbegu nzuri zifaazo kutengeneza bomba la MKE TREKTA.

Wakati unashindana jaribu kukumbuka kuwa labda UNASHINDANA na ALIYESHINDWA.

SHINDANA LAKINI!
Swali:
  • SI ukishinda tutajipendekeza?
  • AU?


NAACHA!

Endelea kidogo na BEEGEES wajaribu kutukumbusha kuwa hai katika STAYING ALIVE..

AU tuendelee tu na MANU DIBANGO.....

Read more...

AISEE dada , njoo katika dunia IELEKEAYO kwa kina KAKA kupewa MIMBA!

>> Saturday, December 20, 2008

Hapo zamani , wadai palikuwa dhahabu.
....Eti sasa na tuelekeako kuna MIBA


Lakini....

Babu mzaa babu alimpa adhabu
....babu kwa mapotofu ya babu ya KUVUnja AMIBA.

Baba akasifiwa na babu kwa kuwa na adabu,
...na kufunzwa ni nani mwenye tabia nzuri katika DUNIA ya JANA afaaye kupewa MIMBA.

Baba alifunzwa nani afaaye
... kwa kuwa kulikuwa na wasiofaa katika ULIMWENGU WA JUZI kupewa MIMBA.

Leo,
..... wa leo wadai WA TAIFA LA KESHO wachezea mikuki kama vile MIBA

-Umesahau wa DUNIA YA JUZI alionya wa DUNIA YA JANA wasichezee MIBA
......ILI dume zima JUZI lisije pata MIMBA?

----------_____________________________---------------------

Nawaza tu MKUU!
Swali:

  • Kama ya zamani ni dhahabu , tunaongelea zamani ya babu , baba au ya mjukuu wako?
  • Unakumbuka NI KIZAZI GANI kilianzisha kulaumu vijana wa siku hizi wameharibika kwa kuvaa PEKOSI?


Au ngojea tushauriwe KUFIKIRI TOFAUTI katika THINK DIFFERENT



Ingawa kuna wasio kuamini mpaka watafikiria KUKUNUSA maeneo kama....(Usisikilize kama mtoto au utakwazika)...


Au ngojea tu MANU DIBANGO arudishe USTAARABU kijiweni kwa kuzungumzaNASI kwa VIPULIZO....

Read more...

Hivi NI TATIZO kwa mwenye PENGO , kujivunia PENGO kwa kuliita pengo MWANYA?

Kama huna, cha kupoteza HUNA.
......Labda pengo ni zuri kama mwanya ikiwa jino hUNA.

Kama huna , ulichonacho ni uwezo wa kuwa na ambacho hUNA,
...ingawa labda ukiwa huna una SUNA.

Tatizo lakujazia ambacho huna,
..kuna wanunuao koroboi ingawa SI KWELI umeme hakUNA.

Mwenye pengo si kweli meno yote hUNA,
.... na waweza kula nyama ingawa kuna wadaioUNA PENGO na mwanya hUNA.

-Mwanya ni nini , kama si ukubwa wa pengo ambapo jino HUNA?

Na....

Mfurahia mwanya labda ni kweli mapengo hana

Na....

Aridhikaye na mapengo,
.... ana meno ya kutafunia kigumu na labda ambacho huna.


-Nini kikuonyeshacho nani kibogoyo ,wakati chako cha kutafuna na meno yako HUNA?


-Kama una mapengo na mwanya, nini huna kama wenye meno watafunavyo cha kujivunia hakUNA?
---------------------_______________-----------------------

Nawaza tu Mkuu!

Tupumzike na NANKO katika LUCKY U


Au tu BASCOM X aje na - Eyes On The Prize

Read more...

Kuna WAFURAHIO na kusikia raha kwa KUKUNA KIDONDA!

>> Friday, December 19, 2008

Kama ilivyo kwa wapatao faraja kwa kulamba makamasi, wapo wengi wenye kufarijika na visivyo kufariji ingawa ulivijaribu kwa siri gizani.

Pamoja na kuwa kwako busara ni kutibu kidonda, kuna wapatao maana ya maisha na kuishi kwa kuwa na kidonda.

Inawezekana siri ya nguvu zako za kutaka kumponya mwenzio kidonda ni kutibu kidonda chako moyoni cha mapungufu ambayo yanajaziwa kwa kujishughulisha na YAWENZIO ili kuleta maana katika maisha yako ambayo yamepoteza maana au umepoteza jicho la KUONA MAANA.


Lakini...
..... kama unataka kupona kidonda kama ulivyopona kipele , usikune kidonda!

Tatizo ni.....
......unakingine cha kufanya kidonda kikipona?

Kama huna kijaziacho ya kidonda kikipona ,TONESHA KIDONDA kisipone!

SIku na wiKIEndi njEMA!

Ngojea basi Waziri MKUU Silvio Berlusconi ambaye ni tajiri kuliko wote ITALI atufundishe tena jinsi ya KUNYWA CHAI kwa MAKAMASI


Au Dawn Penn akumbushe HUNIPENDI katika NO NO NO (Dj Dope's jungle mix)

Au tu Wenge Musica walete - Kalayi Boeing

Read more...

Jifunze SIASA YA UJAMAA, ikusaidie kufaidi UBEPARI!

Utamu wa chachu husaidia kujua kwanini unaridhika na UTAMU wa BWIMBWI kama tu ukinaivyo uiitayo TAMU na si chachu.

Na...
...ukiwa nje ya kiwanja , unaweza baadaye kupata mdadi wa kuingia ndani ya kiwanja kwa nguvu zote na mara zote kwa kudhani kunakitu ulikuwa unakosa ULIVYOKUWA nje ya kiwanja ambako shoo yenyewe haikuwa ya YESU.

Swali:

  • Si Michael Jackson kwa kutochezea madoli utotoni , bado ananunua madoli ya kuchezea ukubwani?

Ujamaa MTAMU kwa sababu kuna iwafanyao kudhani walikosa ubepari kwa kuwa ndani ya UJAMAA.

Kuna stori nzuri za UJAMAA za kukuhamasisha kuwa bepari kama ukisikia :
  • Kuna watu hawatasita KUkuBEPARI kwa sababu wanadhani wanajua kwanini SIASA YA UJAMAA jinsi ilivyo washinda WANA SIASA YA UJAMAA kama Rais Mkapa, Kikwete na wengineo kwa nguvu zaidi BAADA ya Nyerere kufa kama tu KAMBONA kabla ya Nyerere kufariki.
  • Waziri Mkuu Sokoine alijitahidi kabla ya kufa kutunza maadili ambayo baada ya yeye kufa YALIKUFA NAYE katika mtiririko uliohakikishia umati HATA azimio la Arusha lilishaanza kufa.

Na tunasikia:
  • Wengi hata hawamkumbuki mchapakazi aliye kuwa anahakikisha kisemwacho kinatokea aitwaye KAWAWA , ambaye alifanikiwa kusababisha utekelezaji wa uwepo wa VIJIJI vya UJAMAA mpaka baadaye kidogo wajanja walipostukia staili za CHAKO CHANGU , CHANGU CHANGU.
Lakini.....
....siasa ya ujamaa ni ugonjwa tu kama ubepari umetibu matakwa ya Kalumekenge.
Kwa asiyepona kwa ubepari ,UJAMAA bado ni dawa kwa Kalumekenge.


Labda...
.... tatizo liko pale tu watu wasahaupo kuwa dunia haigandi na mfumo wowote ukimaliza kuuandikia kitabu kama Nyerere, labda MFUMO ushaanza kupitwa na wakati na unahitaji umakini wa kukimbia nao kwa kustukia hali halisi ambayo inaweza isiwe ni mfumo wa ubepari wala wa Kijamaa andunje, ukila nao bega kwa bega.

Lakini...
.....Labda jifunze UJAMAA!
SI ubepari unakuja kirahisi kupitia hulka ya KIBINADAMU ya UCHOYO na UMIMI?


AU?


Samahani naenda kukojoa!
Baadaye!




Ngojea tu TONTO IRIE adai IT a RING


Au nimuachie Lokua Kanza na WENZAKE , Live in South Africa...

Read more...

Sukari HUZUNI, kabla ya KULIA!

>> Thursday, December 18, 2008

Kifungua kinywa ni huzuni
...kama chakula NI mwenye huzuni KULIA

Furaha kushoto ukilia ..
...ingawa huzuni si lazima KULIA.

Ingawa kwa furaha......
....unaweza KULIA.

Huzuni ni siri ya utamu wa furaha
...ukiacha KULIA

Utamu wa huzuni,
...chukua muda kabla ya KULIA.


_______________ __________________ _____________

Nawaza tu MKUU!

Swali:

  • SI unajua huwezi kuharakisha HUZUNI hata kama UNATAKA au UKO TAYARI kulia?
Tubadili topiki au tupumzike kwa kumsikiliza Malcolm Gladwell atumie mfano wa SPAGETI katika : What we can learn from spaghetti sauce



Au Lord Kitchener aje na - Old Lady Walk Ah Mile



Au tu Lord Kitchener aendeleze tu muziki wa aina ya SOCA katika "kaka roach"...

Read more...

LABDA kunahitajika MAPINDUZI ya mnyonge KUACHA kumpigia makofi MHESHIMIWA pipi.

Labda...
.....ni kweli BIN-ADAMU wengi hupenda kuongozwa ndio maana kuna KIONGOZI wa VIONGOZI hata katika ujinga.

Unaweza KUBISHA!

Lakini...
....wanyonge ni kiboko kwa kushangilia WAHESHIMIWA hata kama ni wezi wa nyeti kinuka mkojo kama tu Kawawa na Mkapa kama sio Kikwete na Mwinyi wamsifiavyo Nyerere kwa azimio la ARUSHA lililokufa WASILOLIFUATA.

Hukawii kusikia sifa KEMUKEMU za KIONGOZI wetu zimzidivyo kiongozi WENU hata kama KIONGOZI WETU anamsaada ZAIDI kwao kuliko msaada wa kutuibia KWETU .

Ganzi KIYOYOZI ipatikanayo kwa kumpigia makofi mtu hata kwa usichokielewa kwa sababu ni MHESHIMIWA kada wa chama chako , kinamna , ni kama kuwa na mapoozeo ndugu, MKIZAA mtoto ni KILEMA.


Inasemekana kuna visababu LUKUKI kama vya tamaduni, elimu, dini, NJAA au na kadhalika tano na nusu , viongezeavyo UMAARUFU wamwenyenacho KIONGOZI wetu, KWETU.

Lakini.....
...wenye nguvu ni wanyonge walio wengi kama wakiamua KUDINDA kiongozi asidinde.

Lakini....
..... shangilia tu ili uongozwe !

Swali:

  • Si ndio maana kuna GWARIDE umshangilie MREMA kama Mtikila ingawa Kikwete ndio chekibobu?
Naacha, topiki imenishinda. :-(

Tulia na BECK wanisaidie katika spirit ya KUSHINDWA katika kibao LOSER.....


Au tu mwanadada akumbushe maswala ya KIJINGA au MAANA kama KUOSHA katika WASH ya ASS...

Read more...

WASTAARABU katika kujifanya hawamuelewi MWANADAMU atoleaye macho WALIOVAA uchi!

>> Wednesday, December 17, 2008

Wastaarabu wanaeleweka!
Swali:

  • Si wana tabia nzuri?
Tatizo ni...
...pale tabia nzuri zijengapo UNAFIKI.

Unaweza ukajikuta unakufa KISABUNI kwa kuishi kwa kujitutumua hupendi ukoko wakati mzimu wako ni wa UTANDU na UKOKO katika starehe ya WALI.

Mila , desturi , dini au mpaka tu staili yako binafsi ya kukwepa harufu ya mavi hasa KAMA WEWE ni MHESHIMIWA, inaweza kukujengea au kujengea mpaka jamii yako MIIKO ya ambavyo si MWIKO.

Swali:
  • Hivi ushawahi kumshangaa padre au PAPA JOHN PAUL kwa kuvaa gauni?
Lakini...
...Unaeleweka,Una TABIA nzuri!:-(

Tusiwe wanafiki lakini!

Binadamu kibaologia ameumbika atamani kuchungulia hasa kwa sababu pachunguliwapo pana AHADI za KUZALISHANA kitu ambacho binadamu ni shujaa hata uwaweke kwenye kambi ya WAKIMBIZI kwenye njaa, vita na hakuna KICHAKA GESTI.

Lakini ...
..... jamii imenifunza tabia nzuri na labda itabidi nikushangae kwa KUDOKOA wakati jamii nzima inajua UNANJAA na chakula haikupi:-(

Tatizo sugu ni...
.....labda JAMII nzima inaishi kinafiki ndio maana asiyemnafiki JAMII inamtambua kama KIBAKA au KAHARIBIKIWA na anatabia mbaya kwa kuchungulia ANYIMWACHO!:-(

Topiki IMENISHINDA!
NAACHA na natumaini unajua NAWAZA tu hapa MKUU!
SIKU NJEMA!

Ngojea TUPUMZIKE kwa kumsikiliza mwanadada ashauri WANADADA katika Black Women Should Date Outside The Race

Au David Blane atoe TU moyo wake katika Heart Exposure(Usiangalie kama unaogopa damu au mtoto)


Au tu TONI BRAXTON aseme LET IT FLOW

Read more...

KATIKA kukwepa KUKUMBUKA Simon Kitururu ataKUFA!

Kama bado sijafa , IPO SIKU na sekunde nitaKATA roho kabla au baada YAKO.

Mtu akifa tunastuka kama vile tulikuwa tunajua ni sekunde gani ataanza kivyake kwenda kunako bila viatu au kwa lugha maarufu KUFA.

Na...
....kujichulia si tabia nzuri hasa katika MILA na DESTURI za jamii kibao, ingawa mara nyingine kuna tusionauhakika na kujichulia ikiwa kuna aaminiye si kweli mtu akifikiria tu jambo la kisenge anaweza akajikuta kawa msenge.


Swali:

  • Lakini si kuna watu walikuwa wanajua muda wa Saddam Husein kufa?

Kuna mambo usijiombee kama unasababisha kuongezea maji juisi TAMU halafu ukifa kweli kuna watu wanaweza kufikiri stori za kufa kwako NI UTANI wakati ni kweli imekufa hata ukitumia VIAGRA.

Lakini...
... labda Simon Kitururu alianza kufa tokea kabla hajaona dunia, pale chembechembe hai mwilini ziumbazo binadamu ZILIPOANZA kufa ILI zipishe mpya baada ya LIJAMAA kumpa mimba JAMAA na ndio maana LIJAMAA chembechembe zinakufa na LINA mba.

Sibishi!
Kuwa hai ni bahati tu!
Swali:
  • Unajua ni bahati tu sisimizi hawakuingia masikioni na puani ulipolala jana na usingeweza kuzuia kwa sababu ulikuwa umelala?
  • Hivi ukifa utakumbukwa kweli , ikiwa wewe mwenyewe hukumbuki asilimia 98% za ndugu zako wa damu waliokufa hapa duniani ?


Samahani kwa kuwaza ujinga!

Lakini labda....
....nipo hai ndio maana naongea ujinga.

Si ujinga kufa ingawa inasemekana kunawaaminio kuwa kuna wafao KIJINGA.

Pamoja na kwamba niongeacho ni cha kijinga, NAKUTAKIA KILA LA KHERI katika kujisahaulisha TUTAKUFA!

Jiandae kama unajua jinsi ya KUJIANDA au UTAJISIKIA VIZURI kuwa angalau unajitahidi kujiandaa kwa kusali chini ya MBUYU!


NAACHA!

SIKU NJEMA kama UKO HAI!

Tupumzike kwa kuangalia KIFO......katika just for laughs-DEATH


AU PHIL COLLINS astue katika IN THE AIR TONIGHT


Nipo sijafa bado lakini ,kama unionavyo katika picha mbili tatu za juzi ya jana....
Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

AU tu William Baldé atuchangamshe kwa kibao Un rayon de Soleil

Read more...

Hakuna MATIBABU ya kuponya HAMU YA KUTUKANA kama tu kusivyokuwa na matibabu ya KUCHEUA.

>> Tuesday, December 16, 2008

Kuna wakutukanao bafuni na sio sebuleni!

Cha kushangaza...
....wengi wakasirikao baada ya KUONJESHWA tusi, hawafikirii undani wa tusi.

Kuna wengi wanakutukana kama akutukanaye UMFAHAMUYE.
Akutukanaye UMFAHAMUYE kuna kitu tu KABAHATIKA kama kukufikishia TUSI iliujisikie ambavyo watu kibao kadhaa WANAJARIBU kukuhamasisha UJISIKIE.

Utamu wa tusi ni pale atukanwaye anakasirika hata kwa matusi yasio na maana sana kama UNA KIIOO, kama:

  • Kichwa kama pua!
  • Mbwa wee!
  • Mdomo kama kinyeo cha bata!
  • ....na nakadhalika kadhaa mbili ZA MATUSI na nusu.
(SAMAHANI kwa MATUSI, na nitajitahidi kunawa mdomo !)

Sasaa....
....Naamini kuwa tunakasirika tukitukanwa kwa sababu tumeshushiwa heshima.
Lakini...
....mara nyingi heshima inaongezewa sifa na uzito hata usio wake, na mfano mzuri ni wale usiowaheshimu walivyo kuwa WAHESHIMIWA katika jamii ingawa kwa wizi ni namba moja ndio maana wengine ni WABUNGE au mawaziri wakisubiria URAIS kama tu WALE WENGINE wajulikanavyo kwa kuhubiri dini wasizofuata maadili yake.
Swali:
  • SI unakumbuka AKUTUPIAYE KIATU Iraki , ni sawasawa au ZAIDI ya akutukaniaye tusi la nguoni TANZANIA?

Nakubali...
...kuna matusi yanauma hasa yale yalengayo vikojoleo vya wazazi wasiohusika katika ugomvi wangu au wako na lijamaa wa nani mjinga zaidi.

Lakini ....
....kuna mahiri wa fani ya kutukana.

Kama tu katika fani kuna wenye hamu mpaka wanaweza kutongozea mistari ya KORAANI au BIBLIA ili wapate angalau KASHATA kama sio kupata UAMINIFU WAKO, wako wenye hamu ya kukutukana tu kwa sababu binafsi na wanajisikia ahueni kukutolea mvuke wewe Binti Maimuna kama vile tu Rais KIKWETE.

Hakuna matibabu ya hamu ya kutukana, na labda kama dini zenu zinaruhusu kutubu , TUBU tu kwa hamu ya kutaka kumtukana mzazi wako KWA KUFUNZA ADABU ,kama tu dereva wa daladala , kisa hakuelewi na hafuati sheria za TRAFIKI za mbuzi.

Labda hupendi MATUSI ingawa mara moja moja unajisikia kutukana!
Kumbuka ufanyacho ukitukana na watu kusikia umetukana ni kitendo tu.

Tusi ulisha tukana MOYONI na nia na sababu za kutukana zipo tu moyoni ingawa hujasema wala kufanya kitu.

Swali:
  • Umtukanaye anaelewa UJUMBE nyuma ya tusi?
  • Uliyetukanwa unakasirikia tusi au UJUMBE nyuma ya tusi?

Naacha TOPIKI imenishinda!
SIKU NJEMA!

AU tupumzike kwa kushuhudia Rais GEORGE BUSH akipewa tusi LA NGUONI kwa kurushiwa viatu......


AU DIDO ashukuru katika.. THANK U.

DUH!
Turudi tu AFRIKA kwa KING SUNNY ADE ambaye ndiye MWANAMUZIKI wa JUJU MUSIC nimzimiaye katika fani , kwa mara nyingine atupe AFRICA and AMERICA......

Read more...

Mpe POLE aliyepona ! Karudi TU kujiandaa KUUGUA tena.

Kuna waliokufa kabla ya kuugua kama vipele vya mkojo chini ya nepi sio ugonjwa.

Aliyepona ataugua tu tena kama hata kufa baadaye kidogo ya kupona.
Na...
...staili ya kujiandaa kuugua tena ni kupona.

Wakati unakikohozi yakiongezeka mafua kinachoendelea kinajulikana kama ; wewe mgonjwa tu.

Na kama huumwi mguu mzima , MAUMIVU ya KUCHA yanatosha kukukosesha usingizi zaidi ya asumbuaye usingizi wako kwa KUKOROMA au kujamba.

Swali:

  • Unauhakika umepona wakati waliopona kila siku wanasogelea kifo kama SISI wenye bahati ya kuugua?
Lakini...
...labda njaa ni ugonjwa tukiamua kutafsiri chakula kuwa ni TIBA ya njaa.

Naacha!
Nawaza tu hapa MKUU!
Ngojea Bob Marley azungumzie....STIFF NECKED FOOLS


Au Biggie Smalls a HYPNOTIZE

Read more...

Tangazo: FUNGA MWAKA ARUSHA




















MWANAFA, AY NA C4 DJS UNIT KUFUNGA MWAKA ARUSHA
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya (AY) na Hamis Minyijuma (MwanaFA) wanaotesa katika anga ya muziki kwa sasa, wanatarajia kutoa burudani ya aina yake kwenye uzinduzi wa kundi la C4 DJs linaloundwa na wachezeshaji muziki ambalo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika mkesha wa sikukuu ya Krismas ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’ jijini Arusha. Kundi
hilo linaundwa na Ma-DJ wenye uzoefu wa siku nyingi wakiwemo DJ Joe, DJ Peter, DJ Gerry na DJ A-Plus. Pia kutakuwa na Madj wengine wakali kusindikiza uzinduzi huu wa aina yake.

Aidha maandalizi kwa ajili ya uzinduzi huo na sherehe za funga mwaka yanaendelea vizuri hivyo mashabiki wakae tayari kupata burudani ya aina yake. Uzinduzi huu ndiyo mwanzo wa mfululizo wa burudani ndani ya Ukumbi wa Club Triple ‘A’ hadi mwaka 2009.

MaDJ hao wa kitanzania waliobobea katika fani hiyo wameamua kuzindua umoja huo ili kuonyesha kwamba wapo pamoja na watatoa kipaumbele kwa wahusika wote katika tasnia hii. Baada ya uzinduzi kutakuwa na program ya burudani kabambe ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’.

Siku ya Krismasi kundi la C4 litaandaa onyesho litakalofahamika kama ‘White Party’ambapo wateja watakaopendeza ndani ya mavazi meupe watapewa zawadi kemkem za papo kwa papo.

Na kwa mara ya kwanza katika historia ya burudani katika Ukumbi wa Triple ‘A’ Arusha kutakuwepo na shindano la kumsaka malkia wa Desemba (Miss Desemba). Shoo hiyo itafanyika usiku wa tarehe 26 Desemba. Shoo hii ya aina yake itawahusisha warembo kumi wenye vipaji mbali mbali.

Burudani ya Funga Mwaka katika jiji la Arusha inatarajia kuleta mageuzi makubwa katika fani ya muziki na burudani nchini Tanzania.

Funga mwaka hii itatoa fursa kwa C4 DJs kupata fursa ya kuonyesha umahiri wao katika kupangilia muziki ikiwa ni moja ya lengo la kuendeleza fani hiyo ya muziki ambao ulishika chati zaidi katika miaka ya 80 na 90 kabla muziki wa dansi haujateka soko na watu kuwapa kisogo maDJ.

Katika kuhitimisha Funga Mwaka Kundi la C4 limeandaa bonge la Bethdei party kwa ajili ya kusherehekea mafanikio ya Club Triple ‘A’ zaidi ya miaka kumi.

JOSEPH NAMALOWE (DJ JOE)

MRATIBU

Read more...

ASIYELEWA katika UJUZI wa kwanini MLEVI kalewa!

>> Monday, December 15, 2008

Ingawa profesa ujuzi hewa,
......aheshimiwa na cheo kapewa.

Kashaendelea MHESHIMIWA hajalewa,
.....ndio maana haelewi waliolewa.

Ujuzi wa moja si lazima mbili waelewa,
.....ingawa sifa ni pombe waweza kulewa.

Cheo kipo ndio maana profesa hewa,
.....hisabati na dini MTAALAMU anaelewa.

Kabatizwa kwa moto na sio hewa,
...msikitini afunzwa JINIPEPO si hewa.

Katika jamii aileayo alilelewa,
...na nyumbani watoto alelea.

Walelewao SIRI ya profesa wamsifiaye wangeielewa,
....Mjinga asingechekwa KALEWA.

__________ ______________________ _______________________
NAACHA!
Swali:

  • Hivi mara zote sababu ya mlevi kulewa, si ni kwa sababu kanywa pombe ili alewe?

Nawaza tu MKUU!
Jumatatu njema!
Au ngojea tusikilize mjadala TV yaKUSAIDIWA KUJIUA katika British debate: Suicide on TV?


AU TITI kutoka SENEGAL atuburudishe kwa kibao ...- J't'aime

Nimuachie TITI tena atafsiri wimbo wa BOB MARLEY katika staili ya MBALAX...katika kibao kiitwacho Tayumako....

Read more...

LABDA wewe au MIMI ni MDHAIFU wa KUFIKIRI kama UNAFUATA DINI fulani au una amini kuna MUNGU.

>> Sunday, December 14, 2008

......................................LABDA!.......................................
Swali:

  • AU?
  • Hivi kwa aaminiye, HARAGE ni kubwa kwa KIHARAGE?
Naacha!
Tusikilize tu MAHUBIRI ya matumizi ya KINYEO....katika Is Anal Sex REALLY Dangerous?(Usiangalie kama MTOTO, mdogo KIMAWAZO au utakwazika)

Au labda Jim Reeves akatusogeze kwa MUNGU au Krismas fulani katika Senor Santa Claus


AU tu SALIF KEITA atuimbie huu wimbo mzuri uitwao KUMA

Read more...

Kama UNAMAPENGO, kula pipi UOZE meno.

>> Friday, December 12, 2008

Taaluma yako ya kuondoa bikira labda haihitajiki SASA HIVI ikiwa hakuna kibogoyo mwenye bikira.

Lakini...
....labda muda au BAADAYE italeta bikira.
Swali:

  • Hivi si kuna wenye mapengo?

Lakini.....
...Ukisomea kilimo cha umwagiliaji kwenye mvua za kutosha ,LABDA utatuelewesha mahitaji mpaka wafikiriavyo wahitajio umwagililiaji JANGWANI .

Profesa wa mambo ya malaria pasipo malaria, labda ndio aliyechangia kuwepo KLOROKWINI itibuyo wa kwenye malaria kama TU muarobaini.

Swali:
  • Ushajiuliza kwa nini nchi zilizoendelea zina maprofesa wa masomo ya nchi zinazoendelea?

  • Hivi nchi zilizoendelea au ziitwazo za dunia ya kwanza, haziendelei?

  • Hivi kuna dunia ngapi?

Kula pipi ingawa ukizidisha utaoza MAPENGO kama matumizi yenyewe ya mswaki wa mti hayakidhi mahitaji ya pembejeo.

Pembejeo inaweza KUTOONEKANA muhimu kama MAHITAJI ya pembejeo HAYAONEKANI kama tu mkojo wa bata.

Lakini....
... UMUHIMU wa pembejeo UKO PALEPALE kama itakujakumrahisishia atakayekuja tumia au kumhamasisha MTUMIZI awezaye kuponya UKOMA wa KITUKUU chako ,KAMA SIO hata pamoja na jamiii yako ,HATA KAMA ni baadaye kidogo baada ya WEWE , MIMI na YULE kuaga dunia au kwa lugha ya matusi;' KUFA ' ,na kikwapa kugeuka UDONGO.

Ya LEO yanamadhara kesho hata kama hayaonekani LEO.

Labda ...
....ni kweli mpata MIMBA leo hazai LEO.

DUH!
NAACHA!
TOPIKI IMENISHINDA na imeisha !

Lakini, pembeni kidogo ya katikati ya topiki,...
Swali:
  • Ushawahi kumsikia asimuliaye ya mbinguni bila kufika PARADISO?
  • Unafikiri ni raia wangapi wa TANZANIA ambao si mafisadi, wamewahifika IKULU na wanajua labda vyooo vinanuka ?


BWANA na BIBI ASIFIWE!
IJUMAA na wiKIENdi njEMa!

Tulia na Bembeya JAZZ NATIONAL watukumbushe ya WHISKEY SODA...


AU Chakachas watupe JUNGLE FEVER....


Lakini ngojea tu tupate chakacha ituhamasishe wikiendi kutoka kwa...ZUHURA SWALEH alonge ya SHANI.....halafu wengine tupate dhambi.

Read more...

Labda SIRI ya utajiri ni UBAHIRI wa KUNYA!

Utatajirika kama unaingiza zaidi ya kutoa.

Swali:

  • Si inajulikana?

Lakini....
...unaweza ukaota KITAMBI kwa uvivu wa kutoa HAJA NZITO.

Kujilimbikizia GUNIA ni UDHAIFU ikiwa KIBABA cha kumbikumbi kingeua nyege mshindo ya embe bolibo na pia MAHITAJI ya WAHITAJI.

Utajiri wa kujirundikia matusi hata kama tusi moja lingetosha, matusi au lugha chafu inaweza isimuumize mlengwa wala kumkwaza ustadhi na mlokole ,ikiwa tusi lenyewe halina UTAJIRI wakulenga UDHAIFU wa mlengwa katika tusi.

Swali:
  • Umuitaye tajiri KAJILIMBIKIZIA nini?

Kama unapata uhitajicho , huhitaji zaidi.
Kama hujazidisha uhitajicho, wewe si tajiri.
AU....
....zidisha TU uvimbiwe, kama kwako ni UJANJA!

NAACHA!
Hebu tuangalie ya aliyechoka kuzinguka nakuamua kujitengenezea MCHUMBA....


Au tu Diana Ross na Michael Jackson watukumbushe ya UPSIDE DOWN

Read more...

KAMA umebanwa na VINUKAVYO, mahali popote ni CHOONI.

>> Thursday, December 11, 2008

Kila mtu ni STADI wa kutafuta pakujisaidia KICHAKANI, na katika ubunifu , majani, mchanga,jiwe au chupi , VYOTE ni VICHAMBIO.

Tofauti ipo lakini....
.......kwani , katika jitihada za kujaribu kusahaulisha UMATI kuwa umetoka KUJISAIDIA kichakani, KUNA WAPIGAO MLUZI.


Lakini....
...kama kuna aringaye , mtunza heshima wakati kukosa adabu hakudhuru, au adharauye, HAJABANWA HUYO!

Ukibanwa vyakula vyote VITAMU.
Ni UTU tu uzuiao MBWA kula MTU ndani ya KIBANO cha watu.

Swali:

  • Unafikiri wote wajiuzao wanasikia starehe ya kuuza chini ya KITOVU ili wapate vyakula JUU ya KITOVU?
  • Kwani nani hapendi raha akiona wasikiao raha hata kama raha yenyewe ni maumivu ya KUFUNGA?
NAACHA!
Topiki Imenishinda!
SIKU NJEMA!

Basi ngojea mtoto AMTAHADHARI mama yake ;''KWEPA WANAUME WEUSI'' katika Son Warns White Mom: Avoid Black Men

Au tutulie MSAUZI, Abdullah Ibrahim a.k.a DOLLAR BRAND aJAZZIFAI katika - Mannenberg

Basi bwana naacha ingawa YingYang Twins wanataka kunon'gona MATUSI[ usisikilize lakini kama utakwazika au kuingia dhambi:-(]

Read more...

UTAALAMU wa kujisahaulisha kuwa UNAKUMBUKA mwendo wa KWENDEA chooni , kabla HUJABANWA.

Hatusahau,
....viko tu UBONGONI
.

Hawasahau wakihisi ni wewe wa kuwakwamua
....... na mafanikio umebeba MGONGONI.


Hata ujisahaulishe,
...jukumu unalo MGONGONI.

Utajilaumu kichwani,
....kabla lawama hazijawatoka mdomoni.

Waliyonayo kuhusu wewe kichwani,
........yanajengeka moyoni.

S
i kosa la kichaa ukichaani,
....umahiri wa kichaa PIA watoka ubongoni.

H
uwezi jisahaulisha hali halisi kichwani,
......ukweli uko moyoni.

Labda....
ubongo unajisahau uko kichwani
Lakini,

uko kichwani.

K
wa yote mazuri na mabaya yaliyo moyoni,
.......uko kimya na HUSAHAU, uwapendao wako moyoni.

------------------------------------------------------------------------------

NAWAZA tu MKUU!
Swali:

  • Kwani unasahau hata kama umeshindwa na unajitahidi kujisahaulisha kwa KUTO kukumbuka ?

Hebu basi tubadili topiki kwa kujaribu kuwasikiliza wajadilio sababu za LIMTU JEUSI kuwa na liMPENZI, liMKE au liMME la RANGI ya KIJANI.....katika Ulterior Motives behind Interracial Dating....


Au tu LUCIANO aimbe kuhusu -ULTERIOR MOTIVE

Read more...

SIUJANJA kubishana na ALIYEJIANDAA na JIBU!

>> Wednesday, December 10, 2008

Aliyejiandaa na jibu , yuko tayari KUKUBISHIA.

Aliyejiandaa na JIBU, LABDA anajua unataka KUULIZA nini.

Aliyejiandaa na jibu anaweza kukuandaa uulize SWALI wakati unajua jibu.

Lakini...
....aliyejiandaa na JIBU utajua tu jibu lake ukimpa muda bila kumuuliza swali kwa jinsi MAJIBU yanavyo MTEKENYA mukichwa akisubiri ajibu.

Swali:

  • Umeshastukia atakaye kukunyima anavyokusubiria KWA HAMU umalize kuomba?
Lakini....
.....mbishi atakubishia hata ukweli ingawa kastukia JIBU LAKE halifanani na SWALI LAKO.

Na...
.....dunia haigandi na jibu la jana laweza likawa LILIKUWA sahihi jana na leo linahitaji MBOLEA ya chumvichumvi.

Tatizo ni...
..... mbishi hazuii ukuaji wa mimba kama MIMBA imeingia DODOMA.


DUH!

NAACHA!
SIKU NJEMA!

Tulia na rebecca malope alete za MUNGU katika - uyingcwele


AU tu Nusrat Fateh Ali Khan aendelee kumsifu ALLAH katika - Allah Hoo

AU turudi tu katika ZA zisizojali mitazamo ya DINI a.k.a za PENDO LAKIBINADAMU kupitia kwa Onyeka Onwenu na MFALME wa JUJU MUSIC a.k.a King Sunny Ade waongelee maswala ya KUSUBIRI KANYAU katika: Wait for me.....

Read more...

Leo ni MIAKA 47 ya UHURU wa TANZANIA na BADO binadamu wote wanafanana na MUNGU!

>> Tuesday, December 09, 2008

LAbda..
....Tufurahie UHURU kama wewe uko HURU!

Swali:

  • Si kwa mtazamo wa baadhi ya dini chekibobu ,wote tumeumbwa kwa mfano wa Mungu?




Wengine wako ndani ukiwa nje.

(Picha kwa hisani ya Issa Michuzi)





















Wengine hoi:-(








Heri ya siku ya UHURU!

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP