Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kuhusu UGONJWA wa MAHITAJI hata kama MAHITAJI yenyewe ni PIPI kwa mwenye hitaji hasaaa la WALI!

>> Tuesday, January 31, 2012

PIPI huweza kugeuzwa kuwa HITAJI,...
.... hata kwa ambaye hitaji lake la  kweli kwa kihitajikacho ni NGUNA na MLENDA.
Swali:
  • Unauhakika UNAHITAJI ufikiriacho kwako ni HITAJI?
  • Si unakumbuka kuna mahitaji watu hujifunza tu kuyachukulia kuwa HITAJI yasemekana?
  • Na UKIHITAJI UGALI na ukapata UGALI - si uleule UGALI yasemekana unakuwa MTAMU zaidi kitofauti?

Na katika GONJWA la HITAJI,....
....kuna WAHESHIMIWA hubaka kuku,...
... kisa wamegeuza kitu HITAJI,...
.... na kihitaji fulani MTU akiamini ndilo HITAJI,....
....labda ndio maana WATU huwa na mahitaji tofauti hata kama wako kwenye CHAMOTO KILEKILE,...
..... na labda ndio maana katika ``CHAMOTO UNAKIONA KILEKILE kwenye MAISHA´´  yasemekana  kuna wamkimbiliao YESU, MOHAMEDI, au hata MGANGA WA KIENYEJI hata kwenye hoja ambazo wangeweza kujitetea wenyewe bila NUKUU za MWALIMU NYERERE alisemanini kuhusu HILO kama tu jinsi ambavyo kuna wachaguao KUFA MOYO na kusubiria tu litokealo na LIWE!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na USIKONDE!







Hebu KANDA BONGOMAN arudi tena na kuanzisha upya kwa-JT




Halafu sijui kwanini ngojea KANDA BONGOMAN arudie-Wallow



Burning Spear aingilie ghafla nakukumbushia - Identity



Ili tu eti BURNING SPEAR apunguze spidi ya muwasho tena kwa-SHE IS MINE



Au tu Burning Spear alainishe mzimo wakati anazima kwa-Reggae Physician

Read more...

HISIA ni HALIHALISI ingawa sio lazima HISIA ni UKWELI kiuhalihalisi wa KITU!

Na LABDA ukihisi ,...
.... wewe labda UMEHISI TU na  hiyo kwako ni HALIHALISI,....
.... ingawa labda pia kuna umuhimu wa KUKUMBUKA,....
.... HISIA sio lazima ni UKWELI.

Ni wazo tu hili BINGWA!

Hebu tena SAM MANGWANA aingilie kati na kurudia mdinyo-AFRICA




Halafu Kanda BONGOMAN azime la njugu live kwakuanza na -Isambe

Read more...

Eti kuna watakao BABA kwenye MUME kama wageuzao MKE kuwa kama MAMA YAO!

>> Sunday, January 29, 2012

Ndio,...
.... inawezekana kuna wake za watu ambao MME kageuka BABA na wala sio MPENZI wala rafiki,....
..... kama tu isemekanavyo kuna MIDUME kwa MKE  inadeka kama MKE ni MAMA na sio limpenzi!:-(

Swali:
  • Unabisha?

Ndio,....
.....UNACHOTAFUTA,.....
...... saaa nyingine unaweza kuwa unacho ila umekigeuza na wakummtongoza umemgeuza DADA au KAKA  ambayo ni hatua ya mbali zaidi ya ile BINAMU nyama ya HAMU!:-(

Swali:
  • Unabisha?



Ndio,...
......UNACHOTAFUTA,....
.... saaa nyingine unaweza kuwa unakitafutia kwenye FIRIGISI wakati kiko kwenye MCHICHA  ambao UNAO.:-(

Swali:
  • Unabisha?
  • Unauhakika kwako BABA ni BABA, Mama ni MAMA na RAFIKI sio PADRE kama HAUSIGELI /Hausiboi alivyo kisiri ni MPENZI?

Ndio,...
.... kuna wageuzao ,....
..... ambacho KIPO hata kifudifudi MBELE ZAO!:-(

Ni hilo tu na ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(


Hebu Bassekou Kouyate arudishe mdinyo - Segu Blue




Halafu ghafla The Commodores warudishe tena kile kitu fanki kile - Brick House

Halafu The Temptations watubakize kwenye fanki na kuzima tena kwa -Shakey Ground


Read more...

Huwa NAJARIBU!:-(

Hebu Kaka Joseph Hill anisaidie katika-I  TRIED





Au ngoja tu Jean-Claude Naimro alainishe kwa - En Balaté

Read more...

Kuhusu yule KISURA ambaye kwako LABDA ni KISURA tu mpaka ukiunganisha umfikiriavyo akiwa UCHI!

Ndio,...
.... labda NGUO ukatizia denge katika kuficha kitu,...
... na umtamaniye labda ni nguo tu ambazo zaongezea matamanio kwa kuwa ukimfumania chooni wakati anakunya labda hapendezi kama akuvutiavyo UKIMTAZAMA wakati ANALIA kisa unamemfumania USO UKO UCHI ingawa hata umjuavyo huwa hafuniki USO hadharani!:-(

Swali:
  • Si unajua ni RUKSA kunibishia?
  • Na si wajua kuwa UCHI si lazima uvue NGUO?


Ndio,...
... labda kuna ambao unapenda mpaka mawazo yao,......
.... LABDA kwasababu tu hata KIMAWAZO ,...
.....mawazo yao yanakufikia wakati yameshavalishwa CHUPI,...
... na yangekufikia  HAYO MAWAZO wakati yako UCHI kama walivyo UCHI,....
..... labda ungetafuta MWAVULI kujikinga ili usinyeshewe MAVI hata KIMAWAZO!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
JUMAPILI NJEMA MKUU!



Hebu Chaka Demus na Pliers waanzishe zaidi kwa-Gal wine




Chaka Demus , Pliers na Jack Radics waingizie pia kamanyola bila jasho ile -Twist and SHout




Halafu ghafla BUJU BANTON aingilie kati kwa-HUSH baby HUSH




SHABBA RANKS ajaribu kuzima kwa tusi-Wicked in a bed




Ila INNER CIRCLE ndio wazime tena kwa- SWEAT

Read more...

Kabla HUJAONDOKA,....

>> Saturday, January 28, 2012

..... LABDA kuna MAHALI unaelekea TAYARI,....
..... hata kama unafikiria umekaa tu KITAKO kwenye eneo ulokalia HATA KAMA ni lile  uliitalo KIGODA.

Swali:
  • Unabisha?

Ndio,....
..... na KIMAWAZO,....
.....labda hata sasa hivi HAUKO ulipo hapohapo udhaniapo ndipo ULIPO!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu tupate TUKUNYEMA kutoka kwa EDDY GRANT katika -WAR PARTY




EDDY GRANT arudishe ile tukunyema-Walking On Sunshine





EDDY GRANT arudie na tukunyema-HELLO AFRICA



Adinye kiduchu tena -Gimme HOPE Joanna

EDDY GRANT atungunyue kiduchu pana zaidi ile tukunyema-Killer on the RAMPAGE


Halafu azime kwa-Living on the FRONTLINE


Read more...

....labda MTU hawezi kusema kaona aibu ya kuchungulia kabla ya KUCHUNGULIA!

Ndio,....
..... na labda AIBU za MTU ,....
.... ni MATUNDA na FUNUNU za VIJULIKANAVYO vidude kwa MTU,...
.... na aoneacho aibu mtu ,...
.... kwenye hicho LABDA kuna kitu ANAJUA kimfanyacho aone aibu.


Swali:
  • AU?

Ndio,...
..... labda UKIONEACHO aibu,...
.... umekiona hicho hata kwa kukichungulia!

Swali la kizushi:
  • Unafikiri VIPOFU hawana aibu?
  • Na unafikiri VIPOFU hawaoni hata kwa jicho la ndani?
Ndio,...
...na KIPOFU huchungulia pia ,....
.....kama ukiangalia kiundani!

Ni wazo tu hili MKUU!
Jumamosi Njema MKUU!

 Hebu Nit Doff aingilie kati kwa - Sunugal



Halafu Kool & The Gang waingilie kati na kurudisha -Fresh



Halafu Kool & The Gang wazime kwa -Hi De Hi Hi De Ho

Read more...

Kwa kuwa ETI kunawadhaniao hakuna JINSI ya kuutafutia UTAMU jina JIPYA!

>> Friday, January 27, 2012

LAKINI,...
..... tokea enzi za kale LABDA,....
..... utamu ni uleule ila ni MAJINA tu unapewa MAPYA!

Swali

  • Si wajua CHACHU , chungu, tofauti ya utamu wa uke na kachumbari, tamu kama WAZO LA  ngono .... au tu tamutamu kama sukari -ilikuwepo tu tokea enzi na LABDA ni majina TU inapachikwa tu ili JUMA na ROZA waelewane wanaongelea PILIPILI au BAMIA kiutamu katika hoja za KITUMBUA?

Ndio,...
.....ni wazo tu hili NGULI!
Ijumaa na WIKIENDI NJEMA Bingwa!


Hebu La Chepuya waingilie kati kwa - Checo Acosta


UB40 wajaribu kupunguza spidi kwa kulalamikia ya PANYA FULANI katika -Rat in mi Kitchen




Halafu BUSTA a busti kwa kuzima katika -HATARI

Read more...

Wakati bado TUNAPENDA yale MAJIBU tuyapendayo!

>> Thursday, January 26, 2012

Ndio unaweza kubisha,...
.... LAKINI,...
... labda ni kweli WATU WENGI hata UWAJUAYO hawapendi MAJIBU TU,...
... ila KIPENZI  ``KIJIBU ´´ kwao ni MAJIBU wasiyoyajua,...
... na  ila MAJIBU ni  yale AMBAYO  yanaegemea kwa wayaaminiyo ndiyo MAJIBU  HAAAASAAAA kistaili ya WAAMINIVYO,...
.... kitu kifanyacho  katika ukweli wa ni nani kiudaku ni CHANGUDOA  waaminio hata KIHISIA TU  kabla  ,....
.....kuwa ni CHANGUDOA,...
.....watafurahia au hata kukubaliana nawe KIRAHISI ni CHANGUDOA hata kama hakuna USHAHIDI yule umsemaye ni kweli ni  CHANGUDOA  ambaye tayari wanahisi ni CHANGUDOA.

Swali:
  • SI ni kweli hata kama majibu ni ya kihisia tu na hatuna uhakika kiushahidi au KISAYANSI- majibu yakaayo KIKRISTO yanaweza furahisha kama sio kukubalika na WAKRISTO kama tu yale MAJIBU ya KIISLAMU yawezavyo kukubalika na WAISLAMU kama sio kuwafurahisha  hata kama hayana UTHIBITISHO?

Ndio,...
...labda TUNAPENDA majibu tuyapendayo,...
.. na kwa MLEVI majibu yafagiliayo ULEVI hunoga zaidi kuliko yale yaonao WALEVI kuwa mambo zao DUKINAA tu!:-(

Swali kiaina:
  • Hivi enyi wachawi WA  TANZANIA mbona Hamsifiwi wakati fani yenu  ya KICHAWI ni imara tu tokea enzi za mababu  TANZANIA na wengi wenu HAMJITOKEZI kunenepea fani yenu ilivyo nene TANZANIA mpaka muwe mnaumiza tu?
  • Halo MCHAWI hivi kweni MAZERUZERU mnawafanyia nini kikweli?
Ndio,...
... jibu la nililouliza hapo juu naweza KUOGOPA JIBU,...
... ila NIMEULIZA!:-(

Ndio,...
... ni wazo tu hili MHESHIMIWA Kibanangenge!
PAMOJA SANA BANDUGU BAPENDWA!

Hebu tubadili kidude kwa msaada wa Bi KIDUDE kwa kuanzisha upya kwa -KIJITI



Bi KIDUDE azime tena kwa-AHMADA

Read more...

Stori za MTOTO Mzuri avutiaye KWA MBALI kwenye BAA kabla HUJAONGEANAYE!

Kuna MTOTO MZURI kwenye baa ambaye anavutia kabla hujaongea naye hata KITAFSIDA!
Ila kuna MAMBO labda ongea na mtu NA utasahau mwanzo mapaja, KIFUA CHAKE KAMA SIMBA au sura yake ilikuwa ndiyo SUMAKU kimvuto ili uongee naye hata kuomba ambayo kimajina ni mazuri hasa bila kuya ita- KITAFSIDA!

Swali:
  • Kwani hujastukia kwa mbali MVUTO unaweza kuuawa  na kusikiliza AVUTIAYE anaongea NINI baada ya kumsogelea?
  • Na si ushastukia saa nyingine  ni MIAKILI au TABIA zijitokezazo kwenye UONGEAYENAYE na wala SIO kwenye ndoto za utakaye kuongea naye - ndizo huua MVUTO wa MTOTO MZURI yule kwa nje anakalio kama malaika au MHESHIMIWA ambaye akifunga mdomo unakuwa unauhakika anamiakili na masuluhisho kuliko BULICHEKA na suluhisho la kujenga NYUMBA juu ya MTI?


Ndio,...
... fantansi zako hata za Rais KIKWETE  wa jamuhuri wa muungano wa TANZANIA labda zinamvuto zaidi kabla HUJAMSIKILIZA ,....
.....na ukimsikiliza ASKOFU TUTU kama tu BABU wa LOLIONDO na SHEKHE YAHYA waweza kuhitimisha labda SURA ni NZURI kuliko waongeleayo!

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Siku NJEMA!


Hebu OffSide Trick na Baby J warudishe tena kidude- Kidudu Mtu




OFFSIDE TRICK waongezee kipele-FATAKI




OFFSIDE TRICK waongezee SHUGHULI kwa-Samaki






Halafu hebu OFFSIDE TRICK na Mzee Yusuph wazime tena kwa jipu lawalawa-BATA




Read more...

Katika TASNIA ya KIFICHO ile ya MHESHIMIWA kuonea aibu anachowaza HADHARANI!

Kuna tasnia ya AIBU,...
....NA LABDA ILE AIBU ya kuonea aibu hata UNACHOWAZA,....
.....kisijulikane  unakiwaza HADHARANI bila sababu MAALUMU!:-(

Swali:
  • AU?

Ndio,...
....na LABDA KUNA KITU katika  yasemekanayo HATA katika  kila KITU,....
... kama katika ya kila KITU,....
.... inahitajika kukisema katika HADHARA  fulani hata kama HADHARA yako ni BAFUNI wakati unaoga na UKO PEKE YAKO kisa unakionea aibu ingawa wakati huo hicho ndicho KILA KITU!:-(

Swali:
  • AU?
  • Kwani haujui kikusumbuacho rohoni moja ya dawa ni kukitamka?
Na kama unajiheshimu na utakacho ni kutosikika katika ambacho wakati huo kiumuhimu ndicho kila kitu kwako,...
....labda BAFUNI  ukiwa peke yako ni MUHADHARA,...
.... na peke yako kwenye kelele za maji SEMA KWA SAUTI utoe DUNGUDUNGUDUNGUNYIKO ROHONI  kwa kuwa hapo bafuni ni HADHARA yako ya kuongelea ambacho bado huna nguvu yakuongelea hadharani katika hata swala la kwanini chupi yako na sio MAWAZO YAKO ,...
....ghafla NDIO  inachafuka zaidi NANIHII kuliko zamani INGAWA bado wataka hiyo iwe siri yako kwa watu walio HADHARANI kwenye wambea, WAZAZI uwaheshimuo mpaka kwa mpenzi wako kibogoyo bado wadhani ni busara iwe SIRI kwa siri ili utunze woga wako uliouzoea wakutotaka kuchafua NANIHII!:-(

Swali:
  • Unabisha?
  • Na si unajua kuchafua hata hali ya hewa kimawazo au kiushuzi  maranyingi ni tatizo kubwa kisaikolojia kwa alipaye uzito chafuo hasa kwa kuwa kwa wengine labda wala sio CHAFUO?

Ndio,...
.... LABDA kuna tasnia za watu zilengazo ya KUONEA AIBU WATU ambayo usipoona aibu utatia AIBU kisa maswala tu ambayo JAMII imejijengea mpaka YAFANYA WANAJAMII BAADHI WALIO WENGI wanawazo MPAKA  la kuficha ndani ya CHUPI YA MAWAZO yale MAWAZO yahitajikayo kuwa UCHI HADHARANI katika jamii,....

.... kwa kuwa ETI labda TU labda visivyosemwa HADHARANI ili MHUSIKA ATUNZE ADHANIAVYO NI HESHIMA hadharani,....
.....na labda ndio MAANA kuna watu wanaendelea KUFA BILA SABABU SASA HIVI PIA kisa WAVIJUAVYO WANAAIBU navyo  HADHARANI na wanajiheshimu navyo ambavyo visingewaua ila wanavionea AIBU ,...
....ila VYAWAUA  kwa kuwa WAHESHIMIWA  wale WAATHIRIKA wawaheshimuo ,...
.....kwa matendo yao yametabiri YASIYOHESHIMIKA ni NINI- na yawafanya WAATHIRIKA wajisikie AIBU mpaka KUFA kwa yatibikayo kisa WANATAKA waheshimike KATIKA JAMII YA wawaheshimuo!:-(

Ni wazo tu hili NGULI!
Siku Njema Mkuu!

Hebu Al Green abadili tena kwa KURUDISHA old schooL soul ile-Tired Of Being Alone




Al Green aongezee ndude-Love and Happiness





Halafu Aretha Franklin aongezee dozi kwa -Chains of FOOLS



Aretha Franklin alainishe kwa makali-Respect



Ila tu hebu SHAGGY , RIHANNA na Mr BEAN wajaribukuzima kwa -Bombastic



Au tu SHAGGY mwenyewe ndiye azime kwa-Boombastic




Read more...

Etta James!

>> Tuesday, January 24, 2012

Nimechelewa kidogo kukuaga rasmi!
R.I.P Miss James! !

Jamesetta Hawkins a.ka Etta James (January 25 1938-January 20 2012)



Bado nasikiliza kazi zako MISS kama hii-AT LAST

Read more...

Eti kisa ni kwamba KACHUMBARI huwa haisifiwi kuwa ni CHAKULA!

KACHUMBARI ni CHAKULA,...
.... ingawa bado kuna wadaio  kama KILIWACHO  sio UGALI kwa kuwa ni WALI basi kiliwacho sio CHAKULA na alaye anapasha tu moto kabla hakijaletwa cha kikweli CHAKULA..


LAKINI  ukikaa mkao wa kuchukulia KACHUMBARI kama CHAKULA,...
.... kachumbari hushibisha  tu pekee hata bila chipsi dume au chipsi mayayi ambayo  kwa wengine ni kifungua kinywa tu  au  kionjo tu cha barabarani kabla hujaenda nyumbani  kwenye FULU KUBUGIA NANIHII kwa watazamavyo baadhi CHAKULA.

Swali:
  • Si umestukia SHUKA ni nguo yakutosha  hata bila chupi kama ukiliangalia kimtazamo wa KILUBEGA Kimasai?
  • Kwani kwako chenye sifa fulanifulani hakiathiri ukipavyo sifa FULANIFULANI? 
  • Unafikiri KACHUMBARI PEKEE haishibishi?

 Ndio LABDA,...
....ukigeuza mtazamo  ,....
.....KACHUMBARI ni chakula tosha TU hata kama hiyo sio SIFA YAKE ,....
.... na hata kama kachumbari yenyewe tuongeleayo hapa NI baiskeli  katika ya wafikiriao usafiri lazima iwe ni wa GARI na yabaiskeli hayaitwi SAFARI!


Ni wazo tu hili kinanihii MHESHIMIWA!
Jumanne NJEMA sana MKUU!


Hebu UB 40 waingilie kati kwa - Please Don't Make Me Cry



UB40 waongezee dozi kwa -The Way You Do The Things You Do



Halafu hawahawa UB 40 wazime kwa -Here I am Baby





Juzijuzi niliwadaka UB40 wakiwa live kama katika baadhi ya picha za juzijuzi zifuatazo...








Read more...

Jinsi ya kuanza KUKALISHA Mawazo sio KIBIBLIA!

>> Monday, January 23, 2012


Kuna MKAO fulani MAWAZO yako yamekaa,...
... hata kama hayajakaa KIPAGANI au KIKURUANI!


Swali:
  • AU?
  • Si yasemekana kunawasahauo kuwa mawazo yao labda yameegemea MRENGO fulani?

Ndio,...
.... labda kukalisha MAWAZO ni jambo MTU ajifunzalo tu,.....
.... na kuna uwezekano MAWAZO ya mtu hata yale yasiyokaa KIKURUANI au KISABATO bado yamekaa tu MKAO fulani ambao LABDA   ni wa KIVYAKOVYAKO!


Ndio,...
... ni WAZO tu hili MHESHIMIWA!
Jumatatu NJEMA Mwayego!


Hebu Mighty SHADOW arudishe makalipso katika -Universal Language




Mighty Shadow aongezee-I wish







The Mighty Shadow atekenye pia - Doh Mix Meh Up



Halafu ghafla Mrisho Mpoto na Maunda waturudishe Tanzania kwa pini - Samahani Wanangu



Read more...

NI rahisi KUJENGEA MIPAKA uyajuayo kama tu UWAJUAO ingawa labda uhitajiyo ni yale USIYOJUA na wale USIOWAJUA!

>> Sunday, January 22, 2012





Na siye TUSIOFITI kwenye UYAJUAYO na UWAJUAO,...
.... labda  usipoangalia  waweza kufikiri kwenye MAISHA yako UNATURUKA.

Ila tusiofiti na YASIYOFITI kwenye ULIMWENGUWAKO,...
... yapo tu AISEE na labda tuna na YANAKUGUSA hata kiusivyotegemea,.....

....ingawa hutustukiii hata katika tukojoayo pembeni ya BARABARA hadharani.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka YAKO na YA DUNIA YAKO labda bado nni nukta tu hata katika INSHA ya ULIMWENGU wako?


Ndio,...
... YAKO  hata tukiyajumlisha na YANGU YOTE,...
.... labda kihesabu bado sio YOTE!

Na ni wazo tu hili MKUU!

Hebu turudi ANGOLA ili David Zé aanzishe upya kipengele kwa - Mwangolé(O guerrilheiro)







David Zé aongezee dozi kwa -Undenge Uami


'
Tuhame kidogo kwa msaada wa Stephen Marley katika kitekenyeo - Made In Africa





Halafu hebu Damian Marley na Nas wazime kwa kuchezea wimbo wa DAVID Zé katika -Friends


Read more...

UPOLE!

UPOLE  labda ni ni SANAA tu ya kuficha HASIRA au tu HAMAKI!

Swali:
  • AU?
Ndio,...
...LABDA upole wa MTU ni tafsiri yako tu!


Ni wazo tu hili BINGWA!
Jumapili njema MHESHIMIWA!
Hebu KASSAV waingilie kati tena kwa -Ave'w Doudou



Halafu Ambelique azime kwa - New Sheriff In Town


Read more...

SIRI ya MAPISHI ikiwa ni ile aliyenayo ni yule AMCHUNGULIAYE MPISHI!

>> Friday, January 20, 2012

Ndio,...
... siri ya utamu wa MAPISHI sio kama utamu wa MATAPISHI kwa atapikaye ,...
.... kwa kuwa kuna uwezekano saa nyingine SIRI YA MAPISHI aliyonayo si yule MPISHI ajuaye KUPIKA apikacho kiladha ,...
.... kwa kuwa MARA KIBAO ajuaye pia ya MPISHI ni amuangaliaye MPISHI akipika hata kama MUANGALIAJI hajui KUPIKA yapikwayo magimbi yenye chachandu:-(

Swali:
  • AU?
  • Si unajua LABDA siri ya ladha tamu ya chakula upendacho ni kuwa MPISHI labda  anajambia chakula chakula chako ? :-(
Ndio,...
... labda ukinogewa ,...
.... usitake kujua sana kwanini nanihii inanoga ,...
... kwa kuwa hata katika LADHA YA  matundu BAADHI ,...
.....nasikia MATUNDU mengine kinogeshacho  TUNDU kimshawasha ni MAVI kwa baadhi ya wanogewao na TUNDU!:-(

Ni hilo tu MHESHIMIWA na ni WAZO tu AISEE!
Ijumaa na WIKIENDI NJEMA Kingunge!




Hebu KASSAV waingilie kati ....





Kassav waendelee...


Sijui kwanini Fela Kuti aanzishe tena upya kwa-Lets Start



Sijui kwanini ila ngojea FELA aweke pia chuchu-FOGO FOGO




FELA apunguze kwa kuweka chuchu iliyotayari kunyonywa ile-Just Like THAT




Halafu FELA KUTI hebu azime tena  kibatari kwa-Waka Waka

Read more...

Kuhusu NYEGE YA MTU ile ya KUPIGA MTU!

Ndio,...
... hata UKIBISHA,...
..... LABDA moja ya silika ya BINADAMU ni kupigana na labda ndio maana hakuna BINADAMU atakaye ISHI bila kusikia VITA za WATU fulani au NCHI fulanin mahali ,...

... ingawa kwa hilo kama anashangaa labda anaruka VITA azianzishazo YEYE MWENYEWE.:-(


Swali:
  • AU?
  • Unataka kusema hakuna siku kikutekenyacho mpaka unachekelea kanyau hakikufanyi utake kukwida MTU kwa kuwa ndicho kikuuzicho siku hiyo mpaka unataka kumpiga mtu MBATA?


Na LABDA usidhani ni WAKOSAO HOJA TU za KUTETEA HOJA ZAO NZURI hata za kuwa MHESHIMIWA kajamba halafu HAWAAMINIKI,...
....kuwa NDIO  ni kweli wasemalo ndio hufikia kupandisha  MWENYE HOJA ASHINDWAYO KUTETEA  mzuka wa kupiga MTU abishaye hata bila SABABU halafu ndiye asikilizwaye ingawa hana HOJA.:-(

Swali:
  • AU?
  • Unabisha?


Ndio,..
... kujikontroli NI  muhimu na ni poa sana,...
... ila NYEGE nyingine za KUPIGA mtu labda zipo tu ndani ya MTU hata kama zinaangaliwa vibaya kama zile ZISIKIWAZO kwenye REDIO za MBAO kuwa ni  za michezo ya MHESHIMIWA kutamani kulawiti MTU,...
... na HIZO labda hata kama ZINASABABU ,...
... bado katika jedwali zawewa kuwa ziko kwenye LILE fungu la zile HAMU zifikiriwazo kuwa ni za BILA sababu kwa kuwa huyo mtu ni BINADAMU,...
..... kama tu zile zikufanyazo labda hata wewe kujisikia kufinya MTOTO asiye na kosa kisa analialia tu na hata ukimpa peremende hanyamazi.:-(

Swali:
  • Si unakumbuka kutonielewa RUKSA?

Na ndio,...
... labda tukiondoa neno KUPIGA mtu,...
... labda hata wewe ushawahi kukasirikia MTU bila sababu maalumu na hilo hukulioanisha na NYEGE ya kukasirika tu!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu tena JAZZ ipande kiaina kwa msaada wa DUKE ELLINGTON katika mnuso-Sophisticated LADY


DUKE ELLINGTON na JOHN COLTRANE warudishe kitumbua-In a SENTIMENTAL MOOD



Halafu ASHERU na TALIB KWELI wazime tundu kwa- MOOD SWING

Read more...

Vituko vya Slaa kwenye mazishi ya Mtema….”Mchumba” wake amzuia asisalimiane na JK, kisa? Italeta maneno…!

Mazishi ya Mbunge wa Chadema, Mheshimiwa Regia Mtema yamethibitisha kuwa vituko na vioja vya Katibu Mkuu wa Chadema, Mheshimiwa Wilbroad Slaa na “mchumba wake,” Josephine Mushumbusi havijaisha hata kama sasa wanaishi pamoja.

Kwa namna ambayo sasa imethibisha nani hasa mwenye madaraka, mamlaka na kauli ndani ya nyumba yao, Josephine Mushumbusi amemzuia “mchumba/mume” kwenda kumpa mkono Kiongozi wa nchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

Mara baada ya Rais Kikwete kuingia katika makaburi ya familia ya Mtema mjini Ifakara kiasi cha saa tisa unusu mchana, Mheshimiwa Slaa ambaye alikuwa amekaa peke yake na Josephine pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini, Mheshimiwa Godbless Lema, alionyesha ishara ya kwenda kumsalimia Mheshimiwa Rais Kikwete ambaye alikuwa jukwaa kuu.
Lakini Josephine Mushumbusi alimzuia mchumba wake asiende kumsalimia Rais Kikwete akimwambia, “usiende…italeta maneno ya bure.”
Kwa namna inayothibitisha nani bosi ndani ya nyumba, Mheshimiwa Slaa alijikunja na kusalimu amri akisema, “haya bwana”.

Kila dalili za tukio hilo zimethibisha kuwa ubabe na ushujaa ambao Mheshimiwa Slaa huonyesha hadharani kwa kutukana, kukejeli na kuwashambulia wenzake katika siasa akiwamo Rais Kikwete ni nguvu za soda tu zisizotamba mbele ya Josephine ambaye alionyesha udhitibi na umwamba wake hadharani leo.

Lakini tukio la leo pia limethibitisha kwa mara nyingine kiwango cha kinyogo ambacho familia ya Slaa na mchumba wake wanayo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kikwete tokea Rais alipowabwaga na kumsambaratisha kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka juzi, 2010.

Tokea wakati huo, Mheshimiwa Slaa hajapata kumsema vizuri Rais Kikwete, hajapata hata kumtambua hadharani pamoja na kujua kuwa alishindwa kihalali, hajapata kumsalimia wala kumpa Kiongozi huyo wa nchi mkono hadharani hata fursa inapojitokeza kama leo.
Kwa ufupi, tukio la leo na mengine mengi yalimtangulia limethibitisha kuwa Mheshimiwa Slaa ni kiongozi mwenye kinyongo na asiyekuwa na heshima kabisa.

Kama ambavyo wamepata kusema wengine hana sifa za kuwa na kiongozi mkuu wa nchi yetu hii inayoongozwa kwa misingi ya maelewano na siyo kwa misingi ya chuki ambazo anazionyesha Mheshimiwa Slaa. Kwa hili Dr. Slaa Kachemsha, kadhihirisha wazi kuwa hana siyo tu ukomavu wa uongozi bali pia ukomavu wa kisiasa. Sasa naelewa pia kwa nini Slaa upadre ulimshinda.

Ni jambo la ajabu kuwa mfiwa kama alivyokuwa Slaa leo kwa sababu yeye amempoteza Mbunge anakataa vipi kwenda kumsalimia mwombolezaji ambaye amekwenda kumpa pole na kumjulia hali. Huu ni ubinadamu na uungwana kweli?

Mzee Slaa anashindwa na wadogo zake kama vile Mheshimiwa Freeman Mbowe na Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe ambao walipeana mikono na kukaa pamoja na Mheshimiwa Rais, kubadilishana mawazo na kuomboleza kwa pamoja.


---------------------------------------__________________________________-------------------
Nyongeza kinanihino:

HII ni habari Kikrosi kiaina  na si mie Muandishi.


Inakuja kutoka kwa MZALENDO  ajiitaye:
MTANZANIA MKWELI mwenye email:mtanzaniamkweli@gmail.com
Mie nimepiga krosi tu:-( 

Read more...

AJIRA MPYA ZA WALIMU ZATANGAZWA MAJINA YATOLEWA

>> Thursday, January 19, 2012



Kwanza Tunapenda wasalimu wakubwa wetu Shikamoo na vijana wenzetu Mambo vipi..  Tunatambua kuwa Wanavyuo wenzetu walimu walikuwa hawana kazi kwa muda mrefu Jambo ambalo liliwafanya wengi kuwa na wasi wasi na mwajiri wao. Tunapenda kuwapa tarifa kupitia mtandao wenu wa Matukio na wanavyuo (www.tzwanavyuo.blogspot.com)  kuwa, Walimu wahitimu wote  Jana usiku majira ya sa saba Nafasi hizo zilitangazwa Rasmi, Pia sisi Tunapenda kuwasilisha majina ya wanafunzi ambao wamechaguliwa Tunaomba mchukue Muda wenu kutazama kwa umakini majina yenu yote yapo hapa. Hongereni sana.


Imeandaliwa na,
Matukio na Wanavyuo Crew 

Read more...

HELMETI ya MOYO uliopenda HATA ingekuwa ni ya CHUMA,....

....LABDA bado  moyo wa APENDAYE ungeuma ,...
..... hasa kwa kuwa MOYO wa APENDAO chuma sio ngao ya kuzuia mishale ichomayo MOYO!



HELMETI ilindayo  MOYO uliopenda HATA ingekuwa ni ya DHAHABU kama sio ALMASI,...
.....bado  YA moyo THAMANI yake kipimo kizuri hakipatikani kitu kifanyacho ya MOYO kuwa na thamani kubwa kuliko chochote cha BINADAMU hapa DUNIANI halafu kwa maajabu ya MUSA  YA MOYONI MWA MTU ndio yenye  ULINZI MDOGO zaidi kuliko yote kwa kuwa ASKARI alindaye moyo ULIOPENDA ,...
... kupenda humfanya KIPOFU!.:-(

Swali nanihino kiaina:
  • Unafikiri ULINZI wa moyo wako ili  USIUMIZWE NA PENZI unauimara gani wakati labda hata kupenda kwako KWENYEWE  sio CHAGUO lako KIMAAMUZI kitu ambacho naweza kuamini UKISEMA chanzo chake PENZI LAKO chaweza kuwa ni kitu kidogo tu KILICHOWASHA BARUTI kama vile kile cha  KUCHEKEWA TU kidogo na KIJEBA MUUZA MITUMBA au tu hata kutingishiwa tako na KIGOLI- na wala sio TABIA ya MPENZI wala NINI?

Ndio,...
.....HELMET ni KOFIA,...
... na labda hata HELMET ya mwendesha PIKIPIKI hailindi kichwa kizima!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!





Hebu MAD ICE aanzishe upya kwa- Te Amo



Jamhuri Jazz Band waingilie tena kati kwa-Shingo la Upanga



Halafu Ndedi Dibango azime tena kwa -Eyo Mè





Tuko Pamoja WADAU!

... nipo na baadhi ya picha kutoka kaskazini ya dunia  ambako nako nilipita mitaa ya hivi karibu ni hizi:
























Read more...

Prawns in Coconut Sauce - Kamba wa Nazi & Cookbook from A Taste of Tanzania -Coming Soon!


Dear Friends,

Prawns in coconut sauce/ Kamba wa nazi is now uploaded on Taste of Tanzania website.

To see, just click the "Visit My Site" button in this email. Or copy and paste on your address bar http://tasteoftanzania.com/blog/2012/01/15/prawn-in-coconut-sauce-kamba-wa-nazi



Halafu :

Coming soon! Cookbook from Taste of Tanzania

Dear friends and family,

I'm excited to update you about the cookbook from Taste of Tanzania website.





I am starting self marketing early in advance. I pray this will be a year for Taste of Tanzania and Tanzania in General. I am determined to make sure this book reaches many countries, but first I need my fellow Tanzanians and Africans.

To see, just click the "Visit My Site" button in this email. Or copy and paste on your address bar http://tasteoftanzania.com/blog/2012/01/06/coming-soon-cookbook-from-taste-of-tanzania/

Mingi Love,

Miriam Rose
With TasteofTanzania.com

Read more...

Kama WANAUME ndio wangekuwa wanapata MIMBA,...

...LABDA  hiyo kitu ingegeuka kuwa KAWAIDA!:-(



Samahani nariwaindi na kuanza upya hii TARALILA.


Imetokea mara kadhaa katika michakariko hoja ikajitokeza kuwa kutokana na mfumo dume DUNIANI  wanaume  hujisahau kustukia kazi na majukumu makubwa yabebwayo na WAMAMA ikiwa ni pamoja na MIMBA kwa miezi kadhaa wa kadhaa.


Pamoja na upana wa MADA kama hii ningependa kuchokonoa kipele kidogo tu ambacho labda huchangia ni kwanini hata MWENYE NYUMBA huweza kusahau hata ya HAUSIGELI mwenye umri wa kwenda shule asipoenda shule kwa kuwa anamfanyiakazi mwenyenyumba ,...
.. na hicho ni kipele kiitwacho ``KAWAIDA´´

Na tatizo la KAWAIDA,...
.... ni kugeuza CHOCHOTE KILE kuwa ``KAWAIDA´´,....
.... kitu kifanyacho hata kunyanyasa MKE au hata kutothamini ya MKE huweza kugeuka ``KAWAIDA´´.

Swali:
  • Si unajua kuwa ukizoea kuishi pembeni ya JALALA linukalo hicho kitu hugeuka KAWAIDA kitu kifanyacho hata harufu mbaya USISIKIE kwa kuwa ishakuwa ``KAWAIDA´´?


Ndio,....
.....hata kwa baadhi ya BUIBUI  ,...
...kidume kuliwa na BUIBUI JIKE kama bonge la msosi baada  ya tendo la NDOA nalo KIBUIBUI hao  ni KAWAIDA.:-(


Tatizo/ANGALIZO ni:
  • Hufikiri moja ya TATIZO kubwa lifanyalo HATUTATUI MATATIZO YETU yawe ya NCHI zetu au hata yetu BINAFSI ni kwa kuwa yameshageuka KAWAIDA?

Ndio,...
... ``KAWAIDA´´ ikizidi,...
.... yaweza geuza usistukie kuwa USICHOSTUKIA ni kwa kuwa tu kimeshageuka ``KAWAIDA´´!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu tubadili kwa kumuangalia MIKE KALOMBO akitengeneza muziki katika- Party Everyday




Au tu hebu tubadili na kurudi miaka ya nyuma zaidi katika maswala ya Les Mangelepa katika kibao - Mimba



Halafu Don Campbell abadili mchezo na kuzima kwa - Storm Is Over Now


Read more...

ZAWADI ni TAFSIRI- na tafsiri nzuri inamchezo wa kugeuza mavi kuitwa MBOLEA!

>> Wednesday, January 18, 2012

Na kwa TAFSIRI,...
... waweza kuchukia MTU,...
.... kwa kuwa tu UMETAFSIRI kifanyacho asipendeke MTU.

Na kwa tafsiri,....
...... MTU aweza kuua MTU,....
.......kwa kuwa KITAFSIRI kifanywacho ni kupiga MWIZI au tu kuua MWIZI ,...
... kitu ambacho kwa tafsiri za wengi wapiga MWIZI swala hilo  sio LA  kuua MTU.

Na kwa TAFSIRI,....
...... Watanzania waweza MPAKA kukuapia NYERERE hakuwa DIKTETA kwa kuwa WAMETAFSIRI,...
.... na kitafsiri jamaa alikuwa MTAKATIFU ki wake UTU.

Swali:
  • Na siunakumbuka ZAWADI ni uitafsirivyo kitu kifanyacho kuna asiye na CHUPI ambaye akipewachupi atatafsiri kadharauliwa  kwa kuhisiwa hana chupi hata kama aliyenunua chupi kama Zawadi hakujua Mdada kutokana na uhaba wa chupi kavaa kaptula ya KAKA?
  • Na si unakumbuka UKITAFSIRI waweza kustukia MAFISADI nni jina tu lenye maana ileile ya MWIZI kitu kifanyacho kuwa labda NCHI na DUNIA inaongozwa na WEZI hata kama kimajina wapeanayo hutambulika kama WAHESHIMIWA?



TAFSIRIIIIIIII!

Na kwa kutafsiri ndio maana LABDA hakuna DINI moja DUNIANI,...
....kama tu ilivyokuwa hakuna ZAWADI ya aina MOJA kitu kifanyacho MAUA ni ZAWADI kwa MWINGINE jinsi ileile ilivyo ZAWADI kwa KIJEBA mwingine achukuliavyo ZAWADI ni ile kitu KIFUKO cha DHAMBARAU  TU ambacho kwa kutojiamini kimegeuka ZAWADI kisa mtoaji ni MDADA ambaye haamini ni LEVO zake aka Katika KIJIJI cha UJAMAA huyo ni Katibu KATA na kwa mkulima wa kawaida kugawiwa vyake ni ZAWADI tu kwa kuwa mgawiwa HASTAHILI kikawaida !:-(



Ndio,....
..... tafsiri ndio MSINGI na NGUZO mpaka  ya yote yadhaniwayo kuwa ni MATUSI,...
...... na ukitafsiri vizuri ,...
...LABDA chochote ni ZAWADI hata kama kinamdudu,...
...kama tu ilivyokuwa labda kuna maneno tu ambayo UKITAFSIRI yanaweza kuitwa SALA!:-(


Ni wazo tu hili MKUU!

Hebu ghafla Eduardo Paim aturudishe tena Angola kwa - Xinguila



Halafu tupitie Japan kidogo ili Marehemu NUJABE apoze kwa kurudia ndude  -Counting Stars




Halafu Jaziel Brothers wazime kwa sindimba ile - Woza


Read more...

Ya KESHO kama si MASWALA ya KESHO!

>> Tuesday, January 17, 2012

Ya kesho ,...
.....LABDA karibu kwa asilimia mia huanza kabla ya KESHO,...
.... hata kwa wafikiriao YA KESHO yako KESHO ,....
.... kama ya LEO yakumbwavyo na WATU leo.

Swali:
  • Unafikiri yako yatakayokukumba KESHO mwanzo wake hauko kabla ya KESHO?

Ndio,...
.... hata MIMBA za kesho hata za KIMAWAZO ,...
......labda  mbegu  za KIBABA WATOTO na mayai yake MAMAWATOTO wa SWALA yalishaumbwa kabla ya KESHO katika utekelezaji utakao ipasifa KESHO kwa watakao kuamini LILILOTEKELEZWA kesho lilianzia KESHO!

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na wala USIKONDE!


Hebu tena tuanzie Sierra Leone ili King Masco 
aanzishe kubadili kidogo kwa zilipendwa -Mao Mao




Tuhamie Nigeria ili King Sunny Ade aendeleze kwa zilipendwa - Ja Funmi




Halafu hapahapa Nigeria yule Fatai Rolling Dollar arudie na kuzima kwa zilipendwa-Easy Motion Tourist


Read more...

Nimerudi KIBANANGENGE kijiweni WAKUU!

>> Sunday, January 15, 2012

Na nimatumaini yangu wote WADAU wa kijiwe HII mnapata bado CHOO swafi MWKA HUU!


Madhumuni ya BARUA hii KWENU ni kuwatakia HERI YA MWAKA MPYA wote ile KIBONGE yani!

PAMOJA SANA Mwaka HUU!
-Simon




Hebu Manu Dibango & Ladysmith Black Mambazo watekenye- Wimoweh



Halafu MDADA wa KIETHIOPIA yule MEKLIT HADERO adinye pia kilainisho -Leaving Soon


Au tu  halafu Sister PHUMI asigine na kujaribu kuweka nukta kwa sindimba-AFRICA








Halafu tu The Temptations ndio waweke nukta kwa FANKY ile ya kwenye   kidude-Shakey Ground


Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP