Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kumbuka kila AKOJOAYE kuna kitu ANAKIKOJOLEA!:-(

>> Saturday, November 28, 2009

Kwa BAHATI MBAYA ,...
...BINADAMU hawaelei HEWANI ingawa labda vieleavyo hewani bado navyo VIKIKOJOA kuna akumbwaye na MIKOJO.:(





Swali:
  • Unakumbuka wakati UNAJIHARIBIA YA BINAFSI kuna AMBAO ambayo unawaharibia yao BINAFSI?

NI WAZO TU MKUU HILI!

NA nakutakia UBARIKIWE kubanwa haja kubwa ili ujisikie mjanja kuliko walioshinda na NJAA!





Swali:
  • Si unajua katalisti kubwa ya kubanwa haja kubwa ni kula tena?


NIMEACHA!



Au ngojea Tabou Combo na Kassav warudie- Pi Gro Pi Long

Na tu Jocelyne Béroard atulize kwa kitu -VINI SéRé



Au tu Jocelyne Béroard amalizie na kitu -SIWO

Read more...

Labda SIRI YA KWA UHAKIKA KUDOKOA ni hisia za uhakika UKIONACHO ni kitamu!

Kumbuka kuna WADOKOAJI na WAONJAJI.

Kumbuka ukitaka kuonja wakati unaweza kukata tonge SWALA ,... .... inamaana unawasiwasi na UTAMU wa swala.:-(
Kwa hiyo,...
... kati ya MDOKOZI na MUONJAJI kwa kawaida mwenye uhakika na afanyalo ni MDOKOZI!.:-(


NIWAZO TU HILI na NALIKATIZIA HAPA.:-(


Hebu KASSAV wabadili kwa kuleta kitu -WEP



Au tu Kassav walete pia kitu-DOMEYIS

Read more...

Kuhusu kimpandishacho Maimuna NYEGE ya UDAKU!

>> Friday, November 27, 2009

[Tahadhari: Wazo limepinda !:-(]

Meseji kutoka kwa MAIMUNA:

''Aku babu wee! MAKALA ZENU ZA UCHAMBUZI huko huko MCHELE NICHAMBUE halafu wataka tena mpaka FIKIRA nazo nichambue? Koma babu wee KOMA na kama unantaka si sema tu?´´mwisho wa nukuu.

...................................._________________.................................





Samahani naanza tararila hii UPYA!:-(


MAISHANI YAPO AMBAYO NI MUHIMU KWETU ili tuishi na KWA WENGINE UMUHIMU NI MPAKA kujaribu KUJUA na KUCHAMBUA kuwa labda YESU havai chupi.[Tahadhari: kama unakwazika na jina YESU kumbuka kwa Waspanish Yesu a.k.a JESUS ni jina la mtu yoyote yule na huyu ni Mpuetoriko:-(]


NDIO!

Kwa WENGINE kujua YASIYOWAHUSU ni muhimu kama TU wale wasioendekeza ya wengine wachokonoavyo YAO WENYEWE ili kujijua zaidi, - kitu ambacho kwa kawaida huhitaji MAISHA YOTE kama ukikumbuka kuwa yako MWENYEWE ya JANA, si YA LEO wala KESHO:-(


NA, kitu kidhaniwacho ni muhimu KWA MTU , kwa kawaida AIDIA NZIMA ni kitu cha ajabu sana hasa ukianza kufananisha ni kitu gani kwako ni MUHIMU na kusahau watu wengine sio WEWE.:-(


Ila kinachoudhi ni kwamba kitu cha muhimu kwako kinaweza kuwa ni kipoteza muda kwa wengine na kiwapotezeacho muda wengine kikawa ndio unauhakika ni muhimu na unaona mpaka jinsi wasiostukia umuhimu wake wanavyopotea au KUINGIA MKENGE .:-(


NA CHAKUSIKITISHA ZAIDI ni kwamba ingawa UDAKU LABDA ni muhimu KWA KILA MTU ,...
....ila UDAKU UKIZIDI inakuwa sio tena BURUDANI,....
....NA kwa hili na MAANISHA kuwa ukizidisha UDAKU,- UDAKU huachakuwa burudani NA kugeuka SHULE.

Na katika shule ya UDAKU kirahisi wakati KICHWA NI MUHIMU unaweza kujikuta unafikiria TAKO,....
....Nikiwa na maana;.....

...katika kubobea katika UDAKU matokeo yake swala la'' HIVI jirani ni kweli TAKO LIMEKUA'' linaweza chukua nafasi ya-'' hivi tufanye nini ili MTAANI kwetu pawe pasafi watoto wetu wasiugue'' katika maisha ya Binti Kadoda.


Na swala la ''Hivi Mheshimiwa ni kweli anatoa jicho a.k.a tigo'' linaweza likawa ni swala lichukualo nafasi MAWAZONI ya ''Hivi kama Rais wa Brazil LULA na James Brown walianzia kupiga kiwi viatu vya watu Mtaani NAKUFIKIA MAFANIKIO WALIYOFIKIA ,hivi kweli mimi siwezi kwenda mbali kwa kuwa kwanza HAPA NILIPO na taaluma KALI na kubwa kuliko ya kupiga kiwi viatu!'' kwa Kijeba mtaaani ambaye CHANZO CHA HEKIMA ni gazeti la UDAKU.


Samahani ngojea nirudi kwenye SWALA la nyege za UDAKU za MAIMUNA!:-(

Sababu za nyege za udaku ni nyingi NDIO MAANA kuanzia PROFESA, Meneja wa CHOO cha STENDI na shoga ambaye taaluma yake ni kulala chali Bwana akirudi kutoka KAZINI wananyegeleshwa nao.:-(
Lakini ukifuatilia utakuta :

1.Udaku NI kujitafuta wajijuavyo wapenda UDAKU katika stori za UDAKU za wengine.

Nikiwa namaaana -wajijuayo wanayo watu, ndio AMBAYO huwachekesha wakiyastukia jinsi yachezavyo kwenye maisha ya wengine.
Kielelezo :
''Ndio maana ni rahisi kuchekelea ukistukia nyege kama zako zimemponza Mheshimiwa mpaka kadakwa gesti na mke wa jirani.''


2. Maisha Magumu na yanaboa.

Kwa hiyo badala ya kuhangaika na swala gumu zaidi kama la kutatua matatizo yako , ni rahisi kujisikia UNAFUU kwa kustukia na wengine halizao sio MSWANO 100% kama wewe kitu kikupacho unafuu au pia kukusaidia mpaka kuwacheka ustukiao wana hali mbaya kuliko weye.

3. Ni kweli kwa wengi KUFIKIRI ni KUGUMU.

Kwa hiyo MTUZ hujikuta zinakwepa MAKALA ZA UCHAMBUZI kwa kuogopa kufikirishwa mambo mapya ambayo yanahofiwa ni magumu. Basi ndio maana MAGAZETI YA UDAKU yaongeleayo swala ambalo kila mmoja anahisi ni rahisi kama vile lile la KULALANA. Na ni kweli stori za NANI ANAMLALA NANI ni rahisi kuzielewa kwa hiyo naweza kuelewa kwanini MTU ANAWEZA fikia jawabu la '' KWANINI ajihangaishe na KUJIFIKIRISHA KUTATUA MAMBO MAGUMU ILI AFARIJIKE wakati stori ya Mke wa Mheshimiwa ANATOA JICHO a.k.a TIGO ni starehe tupu kwake a.k.a FULU KUFARIJI?:-(


4. UBINADAMU kwa kawaida unakuja na UVIVU !

Kama BINADAMU ukirahisishiwa hata kwa kujengewa ngazi , choo ndani, kupikiwa, - ni fulu kukenua meno kwa kuwa jinsi urahisishiwavyo jambo ndio unafikiri mambo ni MSWANO. Na haki ya nani UDAKU ni TAARIFA YA HABARI MUHIMU kwa yeyote ajisikiaye UVIVU wa kufikiria la muhimu lifikirishalo MUDA HUO aanogewao na UDAKU.:-(

NALIKATIZIA WAZO HILI HAPA KIJEBA na tutaendelea SIKU NYIINGINE na kitu MAKALA ZA UCHAMBUZI vs MAKALA ZA UDAKU nini TAMU na KWA NANI!:-(

Swali:

  • Unafikiri kwanini MAKALA ZA KICHAMBUZI kwa wabongo wengi hazinogi?





Nawatakieni wote KAMANYOLA BILA JASHO Ijumaa na WIKIENDI HII WAHESHIMIWA!







Tupumzike kwa katuni hii nilioitoa katika BLOGU ya MUMY HERY JP yenye bonge la swali baada ya KITENDO.























Hebu tupewe BONGO FLEVA na Hot galz Ft Dully Sykes waongelee ile KITU roho ya Wabongo inapenda ambayo ni-Raha ya Tunda

Ama tu Fresh JUMBE arudie- AMA ZAKE AMA ZANGU

Read more...

Kwa kawaida WANYONGE wakimshindwa MTEMI hubwengana WENYEWE kwa wenyewe!

Narudia tararila:

''Kwa kawaida JEMADARI ANDUNJE hugombana na ANDUNJE mwenziye ndio maana ni rahisi kwa WATANZANIA kugombana na WAKENYA kuliko kuzua ugomvi na UINGEREZA.
Au nikilainisha zaidi kachori naweza kusema:


''Katika TANZANIA ni rahisi kwa vyama vya upinzani kupigana vita vyenyewe kwa vyenyewe na kuiacha CCM shwari kwa kushindwa tu gia za kuivaragiza CCM au kwa kufikiri TU kuwa CCM ni maji mazito a.k.a katika maswala ya kung'ang'ania kidude ni MTEMI.'':-(


Au namaanisha:

'''Ndio maana SOUTH AFRICA ni rahisi kwa WASAUZI WEUSI kuwabwenga WAAFRIKA WENZAO KUTOKA NCHI NYINGINE kuliko kuwabwenga wasio waafrika ambao nao ni wageni South Africa kama ulivyoshuhudia walivyofanya tayari.''

Naweza pia kusema na maana:

''Ndio maana toto temi lililokuwa linakubwenga makonzi CHEKECHEA lilikuwa zaizi YAKO na hadi lile lililokuwa linakuonea HIGH SCHOOL ukifikiria utastukia lilikuwa halifuati wakubwa kuliko yeye''.:-(

Pia:

''Tukienda PAKISTANI utakuta vita imegeuka kuwa ni Wao (Wapakistani matalinbani] kwa WAO (Wapakistani -serikali]na MTEMI wanamuacha kakaa pembeni.''

Pia :
''Iraki Waislamu(SHIA] kwa Waislamu[SUNNI] wanabwengana na mtemi wamuachaye simtaji.'':-(


Swali:
  • Umenielewa MKUU kwa kusema kuwa TEMI huachwa na wanyonge hata majalalani ni rahisi kwao kubwengana wao kwa wao?



Kumbuka hili ni WAZO TU MKUU na kulibishia RUKSA !
Na nakutakia mafanikio MEMA hata kama nia yako ni kwenda kusaka DOGODOGO saizi yako !




Sasa ngojea tupate shule TISHATISHA-Genetic Link in Black Aids Epidemic?




Au tu BOB MARLEY apeleke reggea maeneo katika -Reggae on the Broadway

Read more...

SAMAHANI MSIONIELEWA!

[Tahadhari: Hii post iliandikwa nami tarehe 30.09.2007 ila tatizo nililoliongelea kipindi hicho limejirudia ndio maana nimeidesa tena leo kutokana na uvivu wa kurudia topiki.:-(]





..............................

LAKINI inajulikana ....

......ukisema KITU si lazima mtu aelewe.

Naongea hivi kutokana na watu kadhaa kunitumia ujumbe mtukufu kuwa, kwanini nafanya mazingaombwe blogini , nakufanya kauli zangu na UJUMBE , kutowafikia chobisi.

WAKUU MLIONILENGA kwa manati, nashukuru kwa kunitonya kuwa, kigagagigikoko, nachoongea hapa bloguni, inawezekana ujumbe haufiki chumbani.

Nashukuru , kwa sababu , wengine hamnistui kuwa napitiliza katika kuandika vitumbua.


DONDOO:

Ukija hapa kijiweni, kumbuka jina la blogu hii.

Kumbuka blogu hii ni ya Simon Kitururu mawazoni.

Tatizo ni kuwa, sina wakati wakukupa mambo yote yanipitiayo MAWAZONI,
Najitahidi kukumegea sehemu fulani

Swali:
  • Hivi mambo mangapi yamekupitia akilini leo hii au saa hii?
  • Mangapi yaliyoko mawazoni mwako, ambayo ,ulitaka sie watundu tuyajue, umeya ndika sehemu ?

DUH!

Nawaheshimu watu waitao blogu zao, zetu.
Hii blogu ni yangu ndio maana nahisi naruhusiwa kutoeleweka ingawa sio nia yangu kutoeleweka.

AU?

Si unajua kwako, mwingine ajapo, anapewa jina mgeni?
Mgeni ni muhimu akigundua uko kivyako na ni ukweli unapenda ugali na mlenda.


Lakini......
.....
si unajua mgeni ndio huchinjiwa kuku mwenyeji umfaidio siku fulani ambazo haziitwi Maulidi wala Krisimasi?

DUH!

Nakuacha zaidi na picha zangu!

Nazidediketi kwa walioniambia,
...
kwanini kila nikiweka picha lazima na mimi niwepo pichani.
Sijui kwanini .
Najua wengine hawaweki picha zao, lakini mimi ni mimi.

AU?




Samahani kwa washikaji, kaka na dada, mama, baba na wote ambao hii posti haiwahusu.(Mambo mengine, inabidi yatamkwe kinamna kama wanitakiao mema, wana rudia kuniuliza hata kwa kutumia majina nisiyoyajua.)


DUH!
Endelea na picha
basi ambazo hazijapoa zangu na wadau.....

Naanza na za Cirque du Soleil ambazo nilizipiga kisiri.Nyingine zote zilipigwa kihalali:-)




Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket



DUH!
Samahani picha zangu na washikaji zimezidi!

Ngojea nikuache na picha angalau moja ya JEFF aka DJ JAZZY JEFF ambaye alikuwa anatusaidia kupitisha wiki mwisho hii...

Nimekusikia.
Ndio yule yule aliyemfanya WILL SMITH KUWA maarufu.
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

DUH!
Nahisi nimezidisha picha...

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Msikilize basi na ile Klasiki....

Read more...

sababu NATAKA kweli kwenda MBINGUNI!

>> Thursday, November 26, 2009

1. Nimetishwa kuhusu ya Jehanamu!

2. Nimetishwa

3. Nimetishwa

4. Nimetishwa

5. Nimetishwa

6. Naogopa kufa, na sijui baada ya kufa bado kama nilikufa na vipele , vipele vitaendelea kuwasha au vipi!

7. Wauza ya MBINGUNI wana -AHADI kibao NONO kuhusu kwenda mbinguni na napenda VINONO.

8. Kibano kimezidi DUNIANI.:-(

9. Ulafi kwa kuwa nasikia MBINGUNI kila kitu BWELELE.

10. Vakasheni kidogo , -si unajua tena kubadili kiduchu hali ya hewa Mkuu!


Swali:
  • Wakati weye mzinzi ujuaye KUGUNA TU na kuimba na mapera hupendi, ukidai unatamani kwenda MBINGUNI unauhakika unatamani nini?
  • Unauhakika hakuna kitu kimoja tu ambacho husababisha MTUZ kibao ziamue kujitahidi KUJARIBU kwenda mbinguni zikifa?

  • Halafu nyie muaminio ya -reincarnation, au tu nyie wapagani ambao hamzimii MBINGUNI hamfikirii ni kwa sababu hamjakutana na TISHA TOTO MZURI au tu yule auzaye uzuri wa mbinguni kama chokoleti vile?YAONE VILE!
  • Unafikiri baada ya muda fulani MBINGUNI hutataka VAKASHENI kidogo duniani kwa kuchoshwa na kila siku kumsifia MUNGU?
  • Unauhakika ni kweli kimoja kikuvutiacho kuhusu MBINGUNI nikutaka kumuona MUNGU?
  • Unafikiri SISIMIZI anamuona mtu na UKUBWA WAKE WOTE, na kama unahisi hamuoni ,huhisi kuwa labda SISIMIZI hudhani WATU NI MUNGU?
HILI NI WAZO TU MKUU usikonde!


Au hebu tuwasikilize wajanja watuelezee sababu zakutaka kwenda Mbinguni katika -NATAMANI KWENDA MBINGUNI


AU tu Naughty By Nature wadai tu - Everything's Gonna Be Alright

Read more...

Kama HUSAFIRI!




SWALI:

  • Umestukia kuwa kila siku kuna wasafiri stendi?
NI HILO TU!

Na moja kwa moja hebu tupate shule katika -Guide to the Hajj pilgrimage


Au tu SANDRA Nkaké na BOOSTER warudie kitu na kubadili hali ya hewa kijiweni hapa kwa kitu-Sex Friend

Read more...

KIFIKIRIWACHO kikiandikwa!

Kilichoandikwa LABDA ,...
...kinatiaaibu KILE kilichofikiriwa ndio maana UKICHAMBUA wawezakuta KATIKA wasomaji kila mtu kakielewa kivyake!


Na LABDA,...
... ukifikiria kuandika UFIKIRIACHO, -wakati wa kukiandika sio utakachokiandika ingawa UTARIDHIKA kwa kuwa kimebeba tu baadhi ya sifa za ULICHOFIKIRIA kiaina yake.:-(


Na hakuna LABDA,....
...... katika ukweli ulichofikiria ukajaribu kukiandika wasomao wengi tu hawata kuelewa kivyako kwa kuwa MTUZ zinamchezo wa kuelewa VITU kila mtu kivyake.:-(


Swali:
  • SI unajua unaweza kuandika stori ya maringo ya bata ya kutembea anajisaidia haja tukufu ya uharisho halafu kuna mtu akafikiri unamsema YEYE wakati anajijua yeye sio bata na siri yake ya kuwa aliwahi kujiharishia kidogo wakati anakaribia choo huijui?
  • SI umestukia kwa hiyo hata ujitahidi kuziandika fikira zako za busara kiaina gani kuna watakazozielewa ni PUMBAVU?
  • Unauhakika umewahi kuandika ufikiriacho na ukakidaka katika maandishi kisawasawa kiasi ukipewa nafasi huwezigeuza sentensi?
  • Unafikiri kilichoandikwa kinadaka hali halisi ya kilichofikiriwa?
NI WAZO TU!

Hebu FALLY IPUPA abadili kwa kitu- MABELE

Read more...

R.I.P Brother Haydain Neale!

>> Wednesday, November 25, 2009


Nilihusudu na NAHUSUDU sana kazi zako Mkubwa!

Ndio!- nilihusudu kazi za bendi yako pia ya JACKSOUL .




Ingawa nimechelewa kustukia umetutoka JUMAPILI iliyopita na sina uhakika kuwa wafu husikiliza waliohai katika stori za: ''MAREHEMU ALIKUWA MTU MZURI!'',....
.........R.I.P brother!




Kwa wasiomjua Haydain Neale ambaye wengine tulizimia kazi zake na JACKSOUL bofya hapa upate fununu ya alikuwa ni nani.

Kazi zako zinaendelea kuishi na mie naendelea kukusikiliza kama hivi katika kitu -Unconditional



Kitu-Shady Day


Au tu kitu-Still Believe In Love

Read more...

Kama wewe LEO UNASIFIWA ni MZURI labda CHUKIA swala zima la kuwa kuna KESHO!:-(

Kesho ni nishai kwa kuwa inaleta katika soko la wazuri ,......
....WAZURI WAPYA.:-(



Na kama maisha ya mtu ni yale yakuuza sura nzuri,.....
....labda chukia KESHO kwa kuwa kila kesho utake usitake yaondoa katika sura yako na mpaka sehemu za siri UPYA!:-(



Swali:
  • Unabisha?

Tushukuru tu kuwa BINADAMU wanamchezo wakujisahaulisha na vitu vya MUDA tu kwa hiyo MTOTO mzuri mwenye machavu mazuri kama embe dodo anawezajisahau mpaka AKASHINDWA KUSTUKIA kuwa wamsifiao sasa hivi WAMEBADILIKA na wampendao sasa HIVI a.k.a washabiki wenye KELELE wanampenda kwa kuwa shavu LA MTOTO MZURI lishageuka na kuwa na mvutio wa embe ng'ong'o nasio tena kama embe dodo .

Na labda tushukuru pia UJANA kwa kusahaulisha vijana ya UZEE.:-(

Swali:
  • Si unajua kila aina ya tako ina mshabiki wake ndio maana kila tako lina mmendeaji hata kama limetepeta?


MTOTO mzuri kama unasikio,...
....JIANDAE KWA SIKU uzuri wako utakapoanza kuongelewa kwa LUGHA ZILIPENDWA a.k.a Lugha imekaa kisentensi -TENSI zilizopita/past tense.

Mfano1. Lile toto liliwahikuwa zuri kweli .:-(
Mfano 2. Mama yenu alikuwa Kijiji kizima kinamtambua kwa kuvutia.:-(


CHakujiuliza:
  • Je uzee sio tu aina ya uzuri?


NIMEACHA WAZO na kumbuka MHESHIMIWA HILI NI WAZO TU!:-(

Na ngojea JOJO aunganishe swala la-Beutiful Girls



Au Christina Aguillera atutie moyo wenye sura mbaya kwa kitu-Beautiful

Read more...

NISIFIE nianze KUHARIBU!

Kuna waharibuo baada ya KUSIFIWA,...
.... kwa kuwa BAADA YA KUPATA SIFA wanapandisha mdadi wakuongezea MANJONJO,....

... bila kusahau kuwa kuna WAHARIBUO baada ya KUSIFIWA kwa kuwa wanaanza kufikiria SIFA WASIFIWAZO zaidi na kuacha KUFANYA tena KILE KILICHOWAPA sifa.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka kuwa duniani kuna sifa za uongo?
  • Si labda unakumbuka jinsi wewe mwenyewe ulivyobingwa kila upatapo chansi ya kusifia watu ujuayo ni UONGO?


Tukiachana na hilo:

Inasemekana SIFA,....
....... ukimsifia hata MTOTO - mtoto anaweza akajitahidi zaidi katika USIFIALO.

CHAKUSIKITISHA kuhusu SIFA,...
...sifa kama tu yalivyo MAISHA MAGUMU, - sio CHANGAMOTO kwa kila MTU ili AJITAHIDI vizuri katika LIMKABILILO.


Nachojaribu kusema ni:

WATU tunatofautiana na katika hilo KUNA AMBAO ili WAJITUME huhitaji sio kusifiwa, - bali ni KUFINYWA!:-(


Swali:
  • Si unajua kuna watu AMBAO ni MAISHA MAGUMU ambayo ndio siri ya kujituma na mpaka ya MAFANIKIO YAO na kuna watu wengine ambao MAISHA MAGUMU HAYOHAYO ndio sababu wanampango wa KUJIUA?

  • Hujawahishuhudia MWANAFUNZI aliyesifiwa na kuanza kudharau Mwalimu kwa kuwa anafikiri bila ushahidi kuwa kakubuhu kwa kujua kuliko MWALIMU?


Ngojea AVANT ashauri-Lie about US

Read more...

Binadamu ni MCHAGUZI WA MAMBO mpaka ya NI AKINA NANI akifumba macho ATAVUMILIA kushuhudia KUWAONA wakifanya tendo la NDOA!:-(

Binadamu ni WACHAGUZI wa mpaka wavumiliayo,....
... na ndio maana hasa kama UKIJIPENDEKEZA MWENYEWE utajikuta unavumilia zaidi KULIKO KAWAIDA hata kuonwa KICHEKESHO na WALE unaojipendekeza KWAO.:-(

Binadamu ni MCHAGUZI wa avumiliayo,...
....na hata akifumba macho WAKATI NIA ni KUWAPIGIA CHABO wafanyao tendo la ndoa - ANAWEZA KUTAPISHWA na wazo tu kuwa UASHERATI UENDELEAO kwa alowastukia MIDUME MIWILI katika SHUGHULI WAFANYAYO ambayo kwa kawaida huhitaji mwanamke -DUME moja katika kufanikisha limeamua kuwa ni JIKE katika tendo LAO.:-(

Na KATIKA UCHAGUZI ni nini CHA kufikiria yote yavumiliwayo,...
....USISAHAU kuwa karibu kila MTU ni kawaida KUJARIBU kujisahaulisha kuwa ANAJUA WAZAZI WAKE wali/WANAFANYA tendo la ndoa a.k.a MCHEZO wa BABA na MAMA, ambacho ndio siri ya KUZALIWA KWA watoto WAO.:-(

Swali:

  • Si unakumbuka ukifumba macho KAMA UNATAFAKURI NZURI YA PICHA a.k.a IMAJINESHENI unaweza kumuona mtu yoyote yule uchi?
  • Kwani umesahau kuwa kuna uwezekano ni uchaguzi kuivumilia kitu chochote mpaka hata CCM Tanzania?
  • Unauhakika huwa huchagui ni MHESHIMIWA GANI ukifumba macho ndiye hutaki kushuhudia kuwa ndio siri ya kuenea kwa gono MTAANI KWENU kwa kuwa tu unamheshimu na hutaki kustukia jinsi anavyojishebedua akipekecha utafikiri afanyacho CHA UZINZI MTAANI KISIRI ni kitamu kama peremende vile?


NI WAZO TU HILI MKUU na NIMEACHA!


Ngojea Henri Dikongue alete-Ndol'a Su



Au tu STEEL PULSE wakumbushie kuwa BIBLIA yao ni -Not King James Version

Read more...

Staili ya WANAUME kuongelea MIMBA WASIZOPATA ifananavyo na jinsi WALOKOLE waongeleavyo MBINGUNI ambako bado HAWAJAFIKA!:-(

>> Tuesday, November 24, 2009

[Tahadhari : Wazo limepindia kushoto zaidi kidogo ya kulia ingawa si KWA sana!:-(]





Labda MIMBA,....
....... aijuaye vizuri ni MWANAMKE tena yule aliyewahi kupata MIMBA.:-(

Na kwa bahati mbaya kwa wanaume pia hata ile kazi ya KULIJAZA LIMTU MIMBA,...
..... tamu zake hata kwa kuwasikiliza TU WALIOJAZA na KUTOTOLESHA MTU utastukia kila mtu anashuhudia utamu KITOFAUTI ndio maana staili zipendelewazo kupekecha kila KIDUME upendeleo sio wote ni MUGONGOMUGONGO hata kama nia si kulijaza LIMTU mimba:-(


Ila kwa kuwa JAMII imefanya ni kawaida kuwa hata nikiwa maarufu KWA KUCHEZA MPIRA WA KABUMBU kuna watu wanadhani NAFAA UBUNGE au na ushauri mpaka wa KUCHEZA SINDIMBA,....
....kwa hiyo usishangae kwenye semina ya wajawazito ukakuta mkufunzi ni MWANAUME ambaye labda hajui kuwa hata watoto wake siyeye bali ni HAUSIBOI wake ndio aliyemsaidia kumjazia mke wake MIMBA.


Nakubali kuna MAGAIKOLONOJIST wanaume ambao shughuli yao kila siku ni kucheza na na maeneo yaingiziwayo MIMBA,....
.... ila kama MLOKOLE tu akuuziaye stori za MBINGUNI kuna uwezekano ajuaye mbinguni ni aliye wahi kufika MBINGUNI na kama watakakujua mimba labda suluhisho ni;'' PATA MIMBA!'':-(


NALIKATIZIA WAZO HILI HAPA!:-(

Swali:
  • Unauhakika kuna wanawake wawili wajisikiao MIMBA sawasawa?
  • Mheshimiwa hata kwa kuangalia tu pembejeo za kuzalishia ZA BINADAMU huwezi kustukia kati ya mwanaume na mwanamke utake ustake kuna mtaalamu wa kuingiza na Profesa wa yahusianayo na kuingizwa?
  • Kama wewe ni MWANAMKE uliofanikiwa kupata MIMBA unafikiri LIMTU lako lililofikiri linapata uroda ukapata mimba linaelewa nini kiliendelea katika YAKO MIMBA wakati unalea MIMBA?
  • Lakini hivi haiwezekani uchungu wa mwana akaujua BABA?

SAMAHANI kwa wazo na kumbuka NI WAZO TU HILI na KULIFYONZA ruksa!

Ngojea tushuhudie wapendao kula samaki mzima katika-Fried Fish Eaten Alive



Au tu SIZZLA abadili kwa kudai -Love U for who U are

Read more...

Kwa WATANZANIA wamkumbukao Mwl. NYERERE ingawa katika KUMBUKUMBU husahau wake UFASHENISTA!

Mzee alikuwa anatoka ulimbwende na kama ulikuwa makini ungestukia:

Mzee katika VAZI alikuwa na mpaka KIFIMBO,...
.... asichotumia kuchapia.


Mzee alikuwa anavaa mpaka SUTI za MAO,...
.... ambaye itikadi zake kwa makini hakufuatilia.

Mzee alikuwa anaweza KUKUULIZA swali juu ya lako SWALI,...
....ingawa swali lako jibu kalichunia.

Mwalimu alikuwa anahusudu na kushuka Kiingereza,...
....na Kiswahili ndio alitaka WATANZANIA wengine wabobee na kufuatilia.





Na tukiachana na jambo la FASHENI ZA Mwl NYERERE ambazo wakereketwa hawazungumzii kwa kuwa hunogewa zaidi na SIASA zake zaidi :



Swali:
  • SI unakumbuka kitu chochote kama ni FASHENI huja na kama NYERERE hupitwa mpaka na wafuasi wake wakereketwa kama wanauziwa ulimbwende hata wajinsi ya kufikiri KIJINGA upya kama tu uuziwavyo FASHENI MPYA?

  • Kwani hukumbuki Nyerere TUKIACHILIA MBALI SIASA ZAKE alikuwa ni bonge la FASHENI TRENDI SETA kimavazi na labda kwa hilo ndio alikuwa anaeleweka zaidi kuliko sera zake za kujaribu kufanya maofisi ya serikali yasiwe sehemu za kujipatia ulaji kwa wajanja??

  • Wewe kama MTANZANIA unafikiri ulimuelewa NYERERE wakati sasa hivi HISTORIA inazidi kututhibitishia kuwa hata wafuasi wake wakereketwa aliowaachia madaraka walikuwa HAWAMUELEWI?
  • Unafikiri kwa kawaida unakumbuka mambo mangapi ya Mwl NYERERE ambayo unauhakika siyo ya Kawawa au Kingunge?



NI wazo tu hili kada wa chama na wala USIKONDE!:-(

Hebu tubadi mrengo wa mawazo na kwenda KENYA kwa Stella Mwangi aongelee-Biashara/biacara


Au tu Bob Marley asawazishe tena kiutu uzima kwa kitu-Dance Do The Reggae

Read more...

Kuna uwezekano ugumu wa MAISHA huongezeka kutokana na MIPANGO YAKO TU!:-(

>> Monday, November 23, 2009

Busara za mipango ya KUKU wa kienyeji kikubwa ni kukumbuka tu jioni kurudi BANDANI.

Binadamu na busara zake za kupanga MIPANGO mingi ya kurahisisha maisha aweza kujikuta mpaka kafanya MAISHA MAGUMU yazidi UGUMU ZAIDI kwa hata kufikia kufikiria anahitaji NYUMBA wakati yote yalio muhimu yake angeweza kuishinayo TU kwa raha KIBANDANI.:-(

Swali:
  • Hujawahi kukutana na atakaye gari wakati baiskeli yake inatosha kwendea kigengeni kumvizia muuza nyanya?
  • Unafikiri kimaisha Binadamu anamzidi Kuku busara?


NI WAZO TU HILI MKUU na usikonde!

Hebu Lenny Henry adai-BEcause I am Black


Alpha Blondy ngojea abadili kwa -I wish U were here

Read more...

Kisiri labda ni hulka ya MWANADAMU kutotaka kuwa huru!:-(

UKICHUNGUZA unaweza kustukia mpaka BINADAMU wenye makende HURU,...
... LABDA wahangaikiacho sana ni kutafutia KORODANI chupi ili makende nayo yakose UHURU.:-(

Swali:
  • SI umeshawahi kustukia BINADAMU HURU akipewa uhuru anaweza kuamua kujikosesha uhuru kwa kuamua KUOA au KUOLEWA?

  • Unafikiri kuna aliyeoa au kuolewa ambaye ni HURU?

Ni wazo tu hili BINGWA na kulibishia RUKSA!

Hebu Abby Sourya atupe kitu - Bokila

Read more...

Mazoezi ya KUNYA ni CHOO chochote ATI! - [Sentensi hii wakati inakoholewa ILIBANIWA PUA na mtoto wa PWANI]

>> Sunday, November 22, 2009

Kwa kifupi:

MAISHA ni NISHAI na kila ufanyalo labda ni zoezi tu kwa kuwa LABDA wajuao hilo vizuri,....


.....WAMEKUFA!
:-(


Na labda nachojaribu kusema ni;.....

... katika mazoezi ya kula KAMA UNA NJAA huhitaji KIJIKO kizuri kwa kuwa tu kuna vijiko wakati NIA NA MADHUMUNI katika UGALI ni kukata TONGE.:-(





Ngojea nijaribu kulainisha KACHORI kimaana na KATIKA SWALA ZIMA LA kumaanisha;.....

LABDA na MAANA kuwa ukiiishi unaweza mpaka kustukia Marashi ya TANGA au ya mpaka ZANZIBAR ya KARAFUU kama wewe ni MTANZANIA ingawa labda ,...


....KWAKO yote hayo kwa umuhimu NI kama umuhimu wa miguu kuwa na FUNZA!:-(



Swali:
  • Si unakumbuka sio lazima unielewe?
  • Kwani hujawahi kufanya matusi na kustukia eti utamu wote huo wa usiloliita tusi eti PADRE UMSIKILIZAYE kama tu SHEKHE , - anapunguza TAMU YA onjo KWA kuuita uroda ETI ni UASHERATI halafu dhambi?

NI WAZO tu hili MKUU na usikonde!
JUMAPILI NJEMA MHESHIMIWA!




AU hebu Lenny Henry akumbushie kuwa kuna muda mzuri wa kujamba MAISHANI pia katika ndude -Bad Time to Fart


Au tu Sekou ''Bembeya'' Diabaté abadili kwa kitu-Bitouman











NIPO....

Photobucket


Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket


Photobucket



Photobucket





Photobucket





Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP