Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

USIONJE - ukinogewa NA DHAMBI kabla YA kuizoea JE?

>> Friday, November 13, 2009

Kuna uwezekano KUONJA ndio chanzo cha KUNOGEWA na KITU,......

..... INGAWA kumbuka,....

....ili mtu azoee KITU kwa kawaida INABIDI kuwe na WINGI WA HICHO KITU ,....

....na HAKI YA NANI TENA wala labda sio kweli MAZOEA HATA YA KUNOGEWA KIDUDE au KITU ni kwa sababu ni kitamu KIDUDE au HICHO KITU kama tutachunguza wingi wa matumizi yako ya KIDUDE au hicho KITU.

Swali:
  • Unauhakika ugali ni mtamu au ni mazoea tu YA UGALI yafanyayo ufikiri si maharage ulayo na ugali yasababishayo uzoee kunogewa na ugali ambao kwenu BONGE LA UGALI KWA WINGI ni dozi kwa siku mara tatu?
  • Unafikiri bila kuonja - hasa kama wewe ni miongoni mwa waoga kuonja- utakuwa na uhakika ungeonja ungenogewa na kuzoea kweli kitu?
  • Si inasemekana ikibidi unaweza jikuta umezoea hata kuchambia mchanga kama maji, jiwe , majanijani , randi zilizoanza kubanduka katika ukuta wa choo, na tishu mchangani uendako kuchimba dawa havipo na wala havikuwahi kukunogea?

NI WAZO tu hili MHESHIMIWA!

Kwa mara nyingine SHIKAMOO basi na IJUMAA na WIKIENDI NJEMA ,nikisisitizia KAMA UTACHEZANAYE ukumbuke kucheza kwa STEPU na USIMKANYAGE MWENZIO!


Hebu Labi Siffre arudishe-Watch ME



Au tu AWILO LONGOMBA aanzishe ijumaa na kitu -MONDONGO

10 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! 2:20 pm  

Hapo kaka itabidi uombe radhi kwa wasukuma na wakurya hasa kipengele cha 'ugali'.....lol

vinginevo tutakupa likizo kama Zito....lol

Simon Kitururu 2:32 pm  

@Kadinali CHACHA aka Ngwanambiti: Samahani kwa Wasukuma na Wakurya!

Lakini hivi ugali wa Wasukuma kwa Wakurya ni Mtamu?

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! 3:25 pm  

tena sana...lol

hapo tena usipime...lol

Tena unapikwa mkubwa kinoma ambao hamuonani mpaka mnaulizana 'ng'wana-masangu, uli-he?'.....lol

Yaani mtoto wa masangu....uko wapi?...lol

Yasinta Ngonyani 5:53 pm  

Mmmmhhh hapa kazi ipo kaka Simon imechokoza nyuki:-(

chib 6:56 pm  

Mkuu... hapo umezidi, nani alikuambia rangi zinazobanduka chooni unaweza kuzichambia?!!! :-)

Simon Kitururu 8:57 pm  

@Kadinali Chacha a.k.a Ng'wanambiti & Da Yasinta: :-)

@Mkuu CHIB:Enzi za boarding school nilistuliwa ni kwanini rangi chooni zinabanduliwa hasa magazeti ya kuchambia yakiadimika.:-(

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa 11:22 am  

Chacha tehe tehe tehe..................

@kitururu, Chamba tu

John Mwaipopo 11:36 am  

Mie mgeni hapa. umesahau magunzi! nani hajawahi kutumia gunzi ajitokeze hapa.

hivi mazoea ni kwa vitu vizuri tu. hivi mmewahi kusikia mtu aliyepelekwa kwenye raha akidai kurudishwa kwenye shida eti hajazoea raha bali amezoea shida?

chib 1:32 pm  

We Mwaipopo :-), mie nafikiri hiyo ya magunzi ni staili ya nyanda za juu kusini.
Watu wa sehemu za majabali sisemi ni wapi, lakini wao wanajua kuserereka kwenye mawe baada ya kutoa volkeno mbaya

Simon Kitururu 3:47 pm  

@ Wote: :-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP