Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUNA UWEZEKANO hakuna nchi TANZANIA ingawa kuna eneo wajanja walilitungia jina muda si mrefu sana kuwa linaitwa TANZANIA!

>> Tuesday, November 17, 2009

[Tahadhari: Wazo limepinda!]

Ngojea nijaribu kukokotoa swala KIHISABATI banangenge:


Inasemekana :
TANZANIA= TANGANYIKA+ZANZIBAR


Kwa hiyo labda mjanja ambaye nahisi alikuwa ni mtu mmoja katika kukokotoa HILI ili kufikia jina TANZANIA aliona :

Katika TANGANYIKA + ZANZIBAR kitu TANganyika +ZANzibar.

Au ngojea nilainishe kachori ;
na maana katika: TANGANYIKA +ZANZIBAR mjanja akaona TAN + ZAN nakupata kitu TANZAN.



SASA ndio tunaingia katika siri yenyewe ya kwanini MUUNGANO wa TANGANYIKA na ZANZIBAR bado kama ni gari basi NI bonge la MKWECHE, nalo lilianzia katika swala la katika TANganyika + ZANzibar, tufanyie nini GANYIKA na ZIBAR zilizo baki.

UBISHI ulionzia hapo ambao ni ubishi wa KUKAA KIMYA kwa kuwa ni HESHIMA kumsikiliza MHESHIMIWA ,ndio unaendelea kuota matawi mpaka sasa hivi KUFIKIA MATAWI YA KOROKOCHO ZA MPAKA BAADHI KUJIULIZA hivi ni kweli TANGANYIKA na ZANZIBAR wanautamaduni UNAOFANANA wakati hata kimlo na HAPA SIGUSII kimtazamo wa dini- ukideku LABDA mchanganyiko hata wa MAGIMBI YA FUTARI unatofauti kinamna hata kwa staili ya kuonja?


Narudia:
Lakini kwakuwa waliokuwepo kwenye kikao cha kuchagua jina KABLA YA KUCHUNGUZA VIZURI WANAUNGANISHA NINI KIHITAJICHO JINA walikuwa wanamuheshimu zaidi mtu mmoja wakashindwa kutoa dukuduku lao na kumkubalia MHESHIMIWA.

Na kwa bahati mbaya DUKUDUKU linaendelea mpaka leo, ndio maana TANZANIA ambako inadaiwa ni NCHI MOJA ukipima joto utastukia wengi tu wanajisikiao TANZANIA ni kama NCHI MBILI kwa kuwa hata MUUNGANO wake labda hauna cha zaidi ya kuwa lugha ni moja tu,.....
..... UKIONDOA mchango mkubwa wa TISHA TOTO ya kuwa kuna bonge la kuhitajiana na TUSIPOKUWA NCHI MOJA basi tutabwengana kinamna na kamwe hatutastukia kuishi kwa amani kama tuishivyo na KENYA.

Nalikatizia hili wazo hapa!

Siku nyingine tutajaribu kuangalia kama ni kweli kihisabati banangenge,...
...Hivi ni kweli Zanzibar= Unguja+ Pemba?
Swali zaidi kiduchu:
  • Kwani unaswali wakati Nyerere na Karume hawapo?
  • Kwani unaweza kushindwa kumuelea asiye endekeza UZALENDO Tanzannia kama TANZANIA yenye kama ilivyoitwa baada ya MUUNGANO , muungano wenye bado kama ni mkokoteni basi ni ule mkweche na uhitajio matairi mapya ambayo labda ni ghali kuliko kununua mkokoteni mpya?
  • Hushangai kustukia Binadamu wengi watambuliwao kwa mipaka ya nchi kwa kawaida huwa hawajawahi kufika mipakani mwa nchi?
  • Kwani usingesoma ramani ungejua Tanzania inaishia wapi KIBAHA,- AU unafikiri Tanzania imeendelea mpaka MOROGORO na kufika KIGOMA wakati viongozi wenyewe kuwaamishia DODOMA tu ni kasheshe?
  • Haki ya nani tena kwani weye usingesoma ramani ungejua Tanzania inaishia wapi ?
  • Na baada ya kusoma ramani una uhakika Tanzania imeishia wapi?
  • Si unakumbuka tekinikale MALAWI na TANZANIA wako vitani wanagombea mpaka usiojulikana wa ziwa NYASA?
NI WAZO TU HILI na NAKIRI lina asilimia kadhaa za UJINGA!:-(

USIKONDE mwanakwetu hasa kama MKEREKETWA !

Ngojea CHARLIE CHAPLIN abadili kwa kipengele kutoka katika movie CITY LIGHTS


Ngojea PHATS and Small wabadili zaidi kwa-Turn Around

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP