Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kitu cha ajabu kama vile : - MWANADAMU kuwa na UHAKIKA!

>> Friday, November 20, 2009

Kama unajua au ushashuhudia udhaifu na MAPUNGUFU ya MWANADAMU,...
.... unaweza kunikubalia kuwa ni KITENDO CHA AJABU SANA kwa binadamu kuwa na UHAKIKA.


NA cha ajabu ,...
..... KUNA binadamu wana UHAKIKA!:-)

Na labda kuwa na UHAKIKA ,...
.... ni TABIA TU kama ile ya UMALAYA ambayo inafundishika kwa kugeuza tu zile TABIA ZA UTOTONI ZA KUGAWA PEREMENDE kwa kustukia kuna kitu KINGINE unaweza kugawa ukubwani KAMA PEREMENDE tu kwa kuwa ukubwa umekufumbua macho KUWA UNACHAKUGAWA KIPENGELE MWILINI, na kifuatacho ni kutumia tabia ya kugawa uliyokuwanayo tokea utotoni KUGAWA KITU KINGINE,...
...- na kama weye ni SASA HIVI NI MALAYA ukichunguzwa hili tunaweza KULIJUA au uhakikisha kitaalamu kwa UHAKIKA.:-(


NDIO,....
.... TABIA ya kugawa KAMA YA KUNYIMA huanzia UTOTONI ingawa kuna aina ya kugawa kama ya MALAYA ambayo hustukiwa tu ukubwani na wakubwa KWA UHAKIKA.:-(

Kwa hiyo kutokuwa na uhakika kwa MKONGWE kama tabia, kunaweza kuwa kulizaliwa UTOTONI na kukua naye MKONGWE kwa kuwa tokea utotoni alikuzwa na WALIOMKUZA au tu MAZINGIRA ALIYOKULIA yalimfanya akue hana UHAKIKA.:-(

Swali:
  • Si umeshakutana na wenye uhakika KUWA wataenda kwa Mungu ingawa ukiwadadisi hawana uhakika na ya MUNGU ingawa watakuapia mbinguni wataenda kwa uhakika?


NA kutokuwa na UHAKIKA ni bonge la NYOKO!

Kuna uwezekano ni jambo la kujifunza hili la KUTOKUWA NA UHAKIKA ndio maana katika DUNIA yenye wenye UHAKIKA kuna ambao hatuna UHAKIKA.:-(

Ingawa wenye UHAKIKA ukichunguza sana labda ni aina ya UKICHAA hasa ukizingatia hakuna mwenye uhakika wakufikisha hata dakika ijayo kwa UHAKIKA,....
.....UNAWEZA UKAJIKUTA UNAWAADIMAYA a.k.a KUWAONEA DONGE kwa hata CHEKO LAO a.k.a BATASAMU/tabasamu INGWA labda kiwapachofuraha ni UHAKIKA ambao kwako DHAMBI kwa kuwa tu labda FARAJA YAO INATOKANA NA KUJUA TU KUWA wikiendi ijayo ulempango wa kwa mara ya kwanza KUONJA NJE YA NDOA uko mswano kwa kuwa GESTI imeshalipiwa na limpenzi nalo lishaaga kwa mwanandoa wake lina safari ya kikazi wikiendi ijayo halafu MSHAHARA utatoka kabla ya wikiendi ijayo ANAUHAKIKA.:-(

DUH!
Nasitisha hili wazo hapa !

Swali:
  • Unauhakika kuwa unauhakika?
  • Unafikiri ni nini kinakufanya kuna kitu una uhakika?
  • Unauhakika utafika kesho hasa kama umeandaa chupi safi ya kesho?


SAMAHANI hili ni WAZO TU MHESHIMIWA hata kama huna UHAKIKA kwa hilo!:-(



Ngojea Notorius B.I.G abadili mshawasha kwa ku-Hypnotize


Au tu Lauryn Hill alete busara kwa kukumbushi kuna wadoezi wa kidude katika-That thing

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP