Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

JESTINA GEORGE ON AFRICAN FASHION & DESIGNS

>> Thursday, May 31, 2012








Jestina George is a fashionista, blogger, Presenter and a model based in London, from Tanzania the land of Kilimanjaro.


 AILTV caught up with her at the the launch of READY TO WARE by Anna Luks. Jestina is speaking.... is expressing her concerns about African fashion and designs.

Read more...

CHAGAS disease !




NDIO,..
.. MIE mpare LAKINI KATIKA hii ,...

... SITANII wachaga!:-(

Read more...

GHAFLA!- Na kwa ghafla unaweza kubanwa hata na haja ISIYO kubwa kwa WENGINE!

Ila GHAFLA,....
.... labda wala sio GHAFLA,....
...... kwa kuwa yasemekana kila kitu hapa DUNIANI huchukuwa MUDA,...
.... na inategemea tu na uharaka wa KIPIMO cha MTU kuhusiana na KITU uwezeshao  kugeuza SEKUNDE igeuke MWAKA.

Swali:
  • Si ghafla tu KIJANA anaweza kujikuta MZEE na anahangaika UZEENI kisa hakustukia UGHAFLA wa UZEE ukaribiavyo- kitu kilicho chelewesha KUJIANDAA?

Ndio,...
....labda inategemea tu na jinsi ulipavyo SWALA umakini,...
.... na kama humakini,...
.... kila kitu chaweza kuwa MITOKO YAKE  ni ya kighafla tu,...
.... na hapa wala siongelei  MTOKO kishahawa , kibaruti orgazimu ,ughafla wa KUHARIBU URAFIKI, Ughafla wa KUJIMIMINIA dhambi,ughafla wa kuingia ofisini na  KUJIFUNZA UFISADI , ufuska kiduchu wa GHAFLA mtu akihisi haonwi......
... au tu HATA  jinsi gani ghafla  UTAKAVYOSAHAU hii topiki,...
..... baada ya KUNISOMA!:-(

Swali:
  • Kwani si umeshawahi kubanwa hata na HAJA ghafla halafu baada ya kujisitiri ghafla UKASAHAU  ulivyobanwa kabla ya FARAGHA?

Ndio,...
.....labda kitu ``GHAFLA´´,...
...... hutegemea tu na spidi yako katika SWALA.:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Nakutakia SIKU NJEMA!

Hebu Billy Ocean aingilie kati,...
... na kuongelea jinsi PENZI lilivyo leta maana GHAFLA katika kitu-SUDDENLY

Read more...

Hebu Joshua Ledet aanzishe kwa -ITS a MAN's WORLD!

>> Wednesday, May 30, 2012

Yeah!




Au tu D'Angelo ajaribu kulainisha kwa -Brown SUGAR

Read more...

Tahadhari: MTU MAKINI MBELE!

>> Tuesday, May 29, 2012

Katika UMAKINI,...

..... lakini inategemea aliyemakini ,...
.... katika UMAKINI wake YUKO MAKINI na NINI!:-(


Swali:
  • AU?

Na katika UMAKINI,....
.... yasemekana,...
.....kuna walio makini katika kukosoa ya WENGINE  TU ,....
.....huku wakiruka YAO!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!





Hebu Mighty Shadow aingilie kwa-Lookin' for HORN




Mighty SHADOW aulize tena-Whats wrong with me




Adai -Swing de TING




Halafu ajaribu kuzima kwa -Columbus Lie






Ila hebu tu tena Burning Spears ndio azime kwa shule - Christopher Columbus

 

Read more...

Leo katika UCHOKOZI: Gen. Colin Powell na WAPENZI wa JINSIA MOJA wakitaka KUOANA!

Read more...

LABDA jaribu UNACHOOGOPA, fanya uogopacho kama nia ni KUKUZA Ujasiri WAKO!

Ndio LABDA,...
.... siri kubwa ya kutofanikiwa KITU ni kutojaribu,....
......kisa UNAOGOPA.

Swali:
  • Si unajua hapa siongelei NANILII?


Ndio,...
..... kama unataka UWE shujaa wa YAKO kiwewewewe,...
.... labda ACHA KUOGOPA,...
.... hasa kwa kuwa vingi viogopwavyo wala haviui,...
.... sana sana vinakupa tu NGUVU na UJASIRI wa KUISHI kama wewe -kiwewewewe bila KUOGOPA MTU wala KITU,....
.... ambacho labda ndicho kisa kuna MAMBO muhimu kwako HUFANYI bado!

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Nakutakia SIKU NJEMA!



Hebu ORCHESTRA MAKASSY warudie-MAMBO BADO

Read more...

Kwa KUWA kuna matatizo yaletwayo hata na KUSHIBA!

>> Saturday, May 26, 2012

Ndio,...
....wenye NJAA yasemekana  wanamatatizo yao,...
.... ila  kuna matatizo kibao yaletwayo na WALIOSHIBA kisa wameshiba ,...
.... kwa hiyo njaa KWAO  sio tatizo na inabidi watunge tatizo jingine hasa kwa kuwa,...
.... CHAKULA wanacho, NYUMBA wanazo, MTOMBO garantiidi, WAWASUJUDIAO wanao,....
... basi inabidi tu watunge TATIZO!:-(

Swali:
  • AU?
  • Kwani ulifikiri tatizo la kushiba ni MTU kujisikia tu KULALA?
Ndio,...
... na yasemekana BINADAMU akishatibu KITU,....
... huwa anamchezo wa kutafuta CHAKUTIBU hata ili tu angalau ajisikie yuko HAI!:-(

Swali:
  • Kwani unauhakika KUWA  hua huhitaji tatizo jipya kisa umemaliza KUTATUA lililopita?
Ndio,...
... tatua tatizo,...
... ila kumbuka labda TATIZO hilo ndilo likupalo sababu za kuamka  ASUBUHI,...
... ukilisawazisha ,....
.... waweza kujikuta unahamu na TATIZO jingine kitu kisemekanao kufanya WATU wengi KILUKUKI tu YANI ,....
...mpaka kujitungia MATATIZO mapya YANI!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu tubadili ,...
.....kwa msaada wa Cocoa Tea na Cutty Ranks katika :
- Waiting In Vain

 


Au tu COCOA TEA ajaribu kuzima kwa-HURRY UP and COME!





Halafu huyuhuyu COCOA TEA ,.....
......akiwa na BUJU Banton wazime kwa-TOO YOUNG

Read more...

``KIDOGO´´ na ``SANA´´ ya NANILII!

Kuna kuzidisha ,....
.... lakini labda KUZIDISHA ni lakshari za WENYENAVYO tu!


Swali:
  • AU?
  • Kwani UNAWEZA kuzidisha kama hakuna vya KUZIDISHA?

Ila labda PIA ,...
.... ``KIDOGO´´ na ``SANA´´´ni vipimo tu binafsi MTU ajifunzavyo KIBINAFSI,...
.... kitu kifanyacho kwangu  kilicho KAWAIDA kwako kinaweza kikawa tayari ni kupitiliza na kwahiyo tayari ni UMALAYA ki -SANA TU kiulafi!

Swali:
  • Lakini si unakumbuka kuwa LABDA wingi wa kitu kama tu UCHACHE WAKE kitu  hutegemea SANA kipimo cha kitu kingine ambacho MPIMAJI analinganisha nacho hata bila KUJUA- kitu kifanyacho KILO moja ya SUKARI  ni ``SANA´´ kama inalinganishwa  na KIKOMBE wakati labda ni ``KIDOGO´´ kama kipimo ni PIPA`?

Ndio,...
.... na kidogo tu KIUJAZO  wa NANILII,....
.... inaweza kuwa inatosha kama lengo ni kufanya mtu apate HATA mimba KIIMANI!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Nakutakia SIKU NJEMA MKUU !


Hebu Burning Spear aingilie kati kwa-AFRICAN TEACHER






Burning Spear aongezee-Man in the HILLS


Aongezee-CRY BLOOD AFRICA




Halafu azime tu tena kwa -This Experience

Read more...

Mimi na Profesa Bhekizizwe Joseph Siphatimandla Mxoveni Mshengu Bigboy Shabalala

>> Thursday, May 24, 2012

Kama unaladha fulani ya nanihii KIMIZIKI ,...
... utajua hii ilikuwa BOMBA sana kwangu na wajanja fulani,...
.... kukutana na HATA nikiacha KILE cha zaidi KILICHOONGEZEA kutengeza uhusiano na NGULI haswa ikiwa ni NGULI HUYU!!





Hebu nimuachie NGULI HUYU  akiwa na kundi lake ....na zaidi...


...katika ndude-Knocking on Heavens Door

 

Read more...

Kuhusu kipaji cha KUNYANYAPAA asiye na UKIMWI kisa ETI sio MALAYA vizuri!

>> Wednesday, May 23, 2012

Ndio,...
..... labda ukichunguza ,...
.... sio tu wenye UKIMWI ndio wanaodili na MNYANYAPAO!:-(

Swali:
  • Si si lazima aliyekaa vibaya KWA BAHATI MBAYA ikastukiwa UREMBO wa chupi yake ni UZEE au UCHAFU -ndio  tu maswala ya chupi yake- ndio TU  yaanzishe mjadala wa kumfanya ajisikie KATENGWA?
  • Lakini UMESTUKIA jamii ya WASTAARABU ile ya WATANZANIA ambayo hudai hata matusi haitaki kustukia - bado inaongoza kwa kutenga WAATHIRIKA - na hapa wala sigusii MAALIBINO?

Ndio,...
... labda kuna MTU una MNYANYAPAA bila hata kujua,...
... kisa tu ,...
... UNAMTENGA kwa sababu zako tu hata zile ZA kuwa hata KIPOMBE  yeye sio MLOKOLE INAFU- na kiukarimu hata wa UJI yeye  kwa kugawagawa kisa ni mkarimu ,...
... basi huo ni UMALAYA!:-(

Swali:
AU?



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Ndio naenda leo kuwadeku Ladysmith Black Mambazo ....
....hebu waanzishe - Hello My Baby




Au wajaribu kuzima kwa -Homeless




Au tu na Paul Simon wazime kwa -Diamonds On The Soles Of Her Shoes

 


Au tu hebu tubadili KIDOGO katika majaribio ya  KULAINISHA kwa kumsikiliza Asathecomic katika -Will Smith SLAPS Reporter for Kiss!

:



Hebu tupate picha za Ladysmith Black Mambazo
wakati nikiwa nao SEHEMU SEHEMU














Read more...

Haya tena! MAZISHI ya STAILI nyingine hayo!

Haya ,...
.... kama unataka kumgeuza MAREHEMU kuwa ALMASI,....
.... inawezekana!

Read more...

Kwa ajuaye SEHEMU yasemekana barabara yake KUU ni UCHOCHORO!

>> Monday, May 21, 2012

Ndio,...
.... Labda katika YA MAISHA kuna njia nyingi,....
... ingawa  zote ni NJIA,...
... ila njia nyingine hufikisha hata bundi waendako MAPEMA!:-(


Swali:
  • AU?

LAKINI yasemekana hata kama UCHOCHORO hufikisha mtu MAPEMA,...
..... bado UCHOCHORO sio BARABARA kuu,....
...... hasa kama kitafsiri kwako bado huo ni UCHOCHORO,...
.... ingawa UCHOCHORO unaweza kuugeuza akilini uwe ni BARABARA KUU!:-(

Swali:
  • Lakini kwani unafikiri kama unaenda MAHALI ujanja ni kufika mahali MAPEMA hata KIUTAMU?
  • Na si kuna sehemu barabara ifikishayo NI MOJA na   ingawa ni BARABARA kwa wengine , hiyo bado si niuchochoro tu kwa MWINGINE?
  • Na UCHOCHORO kwa MENDE- si kwa SISIMIZI ni bonge la haiwei?


Ndio,...
.... labda MAISHANI kuna njia NYINGI,...
.... ingawa   kwa WAJANJA bado ni UJANJA kutofika MAPEMA hata KIUTAMU ,...
.... na KWAO njia NZURI wala sio UCHOCHORO!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Jumatatu NJEMA Njemba au tu ewe KIGOLI!


Hebu tubadili na kulalamikia tena JUMATATU kwa msaada wa SNOW katika LONELY MONDAY MORNING



Halafu tu hebu Lagbaja  aingilie kati kwa -Konko Bellow





Lagbaja aongezee-Skentele Skontolo




Au tu Lagbaja azime kwa- Feyin' E



Read more...

KUHUSU sura NZURI hata CHOONI!

Ndio,...
.... labda kila mtu ana SURA nzuri,....
.... na kisa kuna MPAKA wafikiriao SURA ikikunjwa MSALANI basi hiyo siyo nzuri,....
.... ni LABDA kweli kabisa ni MITAZAMO tu ya WATU ,...
... kama tu isemekanavyo,....
....UZURI wa KIDUDE u-JICHONI tu mwa ATAZAMAYE kidude.:-(

Swali:
  • AU?

Ndio,...
... labda ukipenda ,....
... weye ushapenda na PENGO hugeuka MWANYA kama tu MATEGE yageukavyo BOMBA tu kivilevile isamehewavyo wanukao maeneo kisa MTU kapenda!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu ghafla tugewe YA UREMBO kwa VIGOLI- samahani- UREMBO kwa WADADA kutoka kwa  MDADA KOKOFEMME akiongelea  SHUGHULI ambazo kwetu wengine zimekaa kichina...

... katika ya-BEAUTIFUL FACE!




Au tu Remmy Ongala arudishe zote zisizo na SURA MBAYA...

Read more...

R.I.P Robin HUGH GIBB!


Robin Hugh Gibb,(22 December 1949 – 20 May 2012)

R.I.P Robin!


Na miziki yako hasa ya enzi za The BEE GEES ,...
.... bado naisikiliza na yanikuna aisee!

Hebu nikusikilize tena ukiwa na KAKA zako tena katika-

STAYING alive


Read more...

Kwa kuwa labda ``MAADILI ndiyo KICHAA´´- wacha WAJANJA wajitafutie tu MKE au BWANA zaidi ya MMOJA kiMAADILI!!!

>> Sunday, May 20, 2012

Kabla sijaanzisha kubenjua TARALILA:

  • Unauhakika katika MAADILI kuna mwenye  MKE au MME mmoja .... bila kusahau KIPENZI hata kama ni KIKITU tu?:-( 




Yasemekana siri ya USAHIHI  wa kitu ni MAADILI,....
.... tena ambayo MTU mpaka JAMII hujifunza tu KIMAPOKEO.


Swali:
  • Lakini si ikumbukwe pia USAHIHI wa MAADILI nayo ni kitu-na sio tu USAHIHI wa KITU ndio MAADILI?
  • Si ndio maana kwa MAADILI kwa Rais OBAMA katika kitu  kama USENGE kwake ni SAHIHI hata kama  kwa MWINGINE amzimiaye RAIS OBAMA kwa MAADILI MENGINE - hayo ya OBAMA kutopinga UTOAJI MIMBA sio MAADILI?

Na kikubwa katika MENGI yaonekanayo ni SAHIHI au sio SAHIHI,...
...... labda tukumbuke NI za watu  TU za kitu TAFSIRI.:-(


Swali:
  • Si inawezekana LAKINNI ni KWELI usahihi wa MAADILI ya WATU ni TAFSIRI tu za MTU?


Na ndio,....
.... labda kitu SAHIHI bado ni SAHIHI tu hata kama kimaadili yako,....
......weye hicho kwako ni DHAMBI na UTOVU wa NIDHAMU hata kwa MUME kumfanyia mnyonyo wa kisicho adili kivyako  MKE WAKE  wa ndoa CHUMBANI kimaadiliyo binafsi ambayo kwao ni SWAFI KABISA.:-(

Swali:
  • AU?

Ndio,....
.... na usishangae,....
.... katika JAMII hii yetu ya sikuhizi ya KINAFIKI,....
.... labda yaliyo SAHIHI ndiyo yaonewayo AIBU kisa kimaadili  ya JAMII hayo yamekaa UCHI na kwa hiyo ndiyo YAAIBU na kwa waungwana inabidi yafungiwe macho na MASIKIO,...
... au ikibidi MSTAARABU ajifanye hatambui kuwa YAPO katika JAMII yake kama sio mpaka kwenye FAMILIA YAKE!:-(



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!



 

Halafu  hebu GAHAFLA  turudi Africa KUSINI ili Abdullah Ibrahim aka Dollar Brand...
....  aingilie kati na kubadili mchezo kwa - Soweto - Sathima (part)


 

Dollar Brand aongezee-Mannenberg

 



Abdullah Ibrahim na Ekaya waongezee dozi kwa - The Mountain / Nisa / Mississippi

 




Huyu huyu Abdullah Ibrahim aongezee - Cape Town Flower


 


Ila tu tena hapa hapa KUSINI ya AFRIKA hebu Ringo Madlingozi azime kwa -Into Yami


Read more...

KATIKA urafiki wa MWANAUME na MWANAMKE-labda UMPENDAYE mkwepe ili abakie kuwa ``JUST a FRIEND!!




Kuna wadaio,....
.....URAFIKI usiowakinafiki kati ya MWANAUME na MWANAMKE,...
.... huwezekana tu kama RAFIKIYO hakuvutiii.:-(

Swali:
  • Si umestukia nimerahisisha hoja?
  • Na kwani si ni UNAFIKI kama kuna ajenda za siri katika udaiwao kuwa ni URAFIKI wakati kwako LENGO  ni zaidi ya u ``JUST a friend´´?

Ndio,...
..... labda udhaniaye ni RAFIKI TU,...
.... . uhusiano wenu umejengwa KINAFIKI kwa kuwa hakuambii tu kuwa atakacho ni zaidi ya URAFIKI tu wakuchekeana na kusikilizishana UDAKU!:-(

Wadeku hawa....





Ni uchokozi tu huu MKUU!
Nakutakia siku NJEMA!

Read more...

KATIKA yahusuyo UCHI mzuri!

>> Friday, May 18, 2012

Na kuna YAVALISHWAYO nguo MAISHANI,...
.... ingawa bado yasemekana MAISHANI yale ya KIKWELI ni yale  yaliyoko UCHI,...
.... hata kwa ALIYEVAAA!:-(

Swali:
  • AU?
  • Na  si YALE mazuri hata yakikaa UCHI huwa yana mchezo wa KUPENDEZA?


Ndio,...
... labda ni kweli UCHI mbaya hufichwa na mwenye UCHI,...
.... hata FARAGHANI!:-(


Na ni  wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu J. Martins aingilie kati tena kwa -OYOYO





Halafu Fally IPUPA aingilie ya J. Martins halafu kwa pamoja wazime kwa -JUPKA

Read more...

R.I.P DONNA SUMMER!

Dadaaa DONNA SUMMER (December 31, 1948 – May 17, 2012)

PUMZIKA DADA!


Au hebu tu turudie kitu yako ile  -I FEEL LOVE




Au tu turudie kukusikiliza katika tamutamu -HOT STUFF

Read more...

Maisha yana SAFARI zake!

>> Thursday, May 17, 2012

Enzi fulani ,...
...eti hawa walikuwa ni MAMA, BABA na MIMI!:-(




Hebu ghafla THEM MUSHROOMS waingilie kati kwa-MTOTO SI NGUO

 


SNOW aingilie kati kwa -Lonely Monday Morning





Halafu SNOW ajaribu kuzima kwa -Informer




Ila tu Naughty by NATURE ndio wazime kwa -FEEL me FLOW

Read more...

R.I.P the LEGENDARY Chuck BROWN!

Tukiachia kuwa ndio ulianzisha ya ``GO go´´...
.....Mkuu umenisaidia sana TU  kupitisha siku na MAMBO  kistaili zako yani ,....


R.I.P CHUCK BROWN!











CHUCK BROWN tafadhali   come again angalau ki....

.

Read more...

Katika kutafuta MICHUBUKO ya MAJERUHI ya BAHASHA iliyolambwa - BAADA ya BAHASHA kulambwa!

Ndio,....
... KUJERUHIWA kwa majeruhi PANZI -kwa  mdomo wa KUKU,...
.... LABDA  sio mpaka  KUKU achubue  mpaka chini ya manyoyanyoya ya PANZI  ili nako kuwe na MADOADOA yaringiayo wenye macho na wafikiriao ni wajanja KISA NI KWA kuona kwao,...
..... ili tu IWE KUNA ushahidi PANZI asiye na MANYOYA,.....
... chini ya MANYOYA kachubuka ,...
.... ili tu KIUSHAHIDI iwe wazi kwa kuwa INAONEKANA  kwa macho kuwa PANZI ni MJERUHIWA basi KAJERUHIWA!:-(



Swali:
  • Unafikiri sio kweli kuwa kwa ABAKWAYE kikweli -sio mpaka KIKWELI kuwe na waitwao wataalamu huhitajika  hata katika hilo ili tutofautishe aliyebakwa na aliyekubali mwenyewe mtalimbo hivyo hajachubuka hata kama kuna KUKU wenye nyuchi PANA ambao kubakwa kwao na mwenye  mtalimbo  sindano  huwa hakuna USHAHIDI hata KIBATA ambaye kimtalimbo yuko kistaili ya MNYOO?
  • SI ACHUBUKAYE hata kwa KUDHALILISHA KWANGU MTU - si ni SI  lazima KIKUCHUBUKA kuwe na alama IONEKANAYO kwa mimacho au tu ki tutegemeavyo?



Na kwa kuwa ,...
.... YASEMEKANA majeruhi wengi MAJERUHI YAO huwa YANATAFUTWA KWA DARUBINI ya MACHO kisa watakao uthibitisho wana MACHO,...
.......labda ikumbukwe tu MICHUBUKO yao  WENGI WENGINE huwa  haihitaji DARUBINI ili aliyejeruhiwa AWE AMEJERUHIWA NA HATA KAULI YAKO YENYE HARUFU MBAYA  ili TUTHIBITISHE kiuhaueni wa KUJERUHIWA kachubuliwa TU kimjeruho ,...
.... kwa hiyo KAJERUHIWA!:-(


Swali:

  • Si unakumbuka kuwa labda kwa kulamba STEMPU huwa umeijeruhi STEMPU kama kidarubini kabla hujagandisha stempu kwenye BAHASHA yenye BARUA YAKO nzuri kwa MPENZI -bado STEPU imekwaruzwa na liulimmi lako na kwa hiyo ni stempu nlabda tayari ni  MAJERUHI?


Ndio,...
....na KUJERUHIWA kwako hata kwa KUNG'Ong'wa,...
... na kugeuke kuwa BARAKA kwako MKUU!





Ni hilo tu MHESHIMIWA!
Na ni wazo tu hili MUKULU!


Hebu Eddy Grant arudishe ya -VILLAGE LIFE





Au tu Mkuu Eddy Grant azime tu tena kwa ya - Frontline


Read more...

ELIMU YETU - TANZANIA

>> Wednesday, May 16, 2012

WANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA  SHULE YA MSINGI MAKUMBUSHO KAMA
WANAVYOONEKANA DARASANI LEO HII



HAWA NI BAADHI YA WANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA  KATIKA SHULE YA
MSINGI MAKUMBUSHO YA JIJINI  DAR ES SALAAM WAKIWA DARASANI, SIJUI WAPO
WANGAPI, WATOTO HAWA HULAZIMIKA KILA MWEZI KULIPA Tsh1000 YA MTIHANI
WA MWEZI,Tsh 1500 YA MTIHANI WA TERM,Tsh500 YA KILA SIKU YA UJI HAPO
BADO TIUSHENI,USAFI, MLINZI,LEBO,VIDUMU,FAGIO, NA MADAFTARI PIA
HULAZIMISHWA KUNUNUA HAPOHAPO.





Nimetumiwa hii Banangenge na:
BIG RIGHT

Read more...

WAKATI labda UKWELI uko palepale kuwa- HARUFU sio tatizo kwa HARUFU!

Ndio,...
.....labda HARUFU ya ANUKAYE ni dalili za tatizo la ANUKAYE,...
......au tu na ni TATIZO sumbufu kwa wanukiwao na hiyo MIHARUFU,....
.... lakini ngoma iko palepale kuwa HARUFU sio tatizo kwa HARUFU.


Swali:
  • AU?
  • SI unakumbuka HARUFU yenyewe KIYENYEWE huwa haina PUA ya kunusia harufu -na ni MIJIVIUMBE  tu mingine tu yenye mchezo wakunusanusa hata UVUNDO kisa inaMIPUA ndio imegeuza HARUFU kuwa DILI?

Na  WEWE labda sio tatizo kwa WEWE,...
.... ingawa bado  LAKO  labda ni chanzo cha tatizo LAKO,....
...... na lako  ni TATIZO sumbufu kwa wanukiwao wengine na hilo LITATIZO  lako,...
....... ingawa ngoma bado iko palepale  kuwa WEWE ni WEWE na WEWE  sio TATIZO.


Swali:
  • AU?
  • Una uhakika WEWE na yako WEWE huwa UNAYATOFAUTISHA hasa ukizingatia labda WEWE na YAKO WEWE ni vitu viwili TOFAUTI?
  • Na si HARUFU inaweza kuwa ni ile ya KUNUKIA na sio tu ile ya KUNUKA?


Na kama unafikiri MIMI  au MTU mwingine ndiye  tatizo LAKO,...
....labda ngoma iko palepale kuwa UMEJIONGEZEA tu MWENYEWE  yasiyo TATIZO LAKO,...
... na sasa WEYE MWENYEWE  unaelekea kuwa TATIZO la wengine!:-(


Swali:
AU?
Kwani ni kweli HARUFU ni tatizo la HARUFU?

Ndio,...
..... labda siri igeuzayo HARUFU kuwa tatizo ni pua za WENGINE tu,...
.... kwa kuwa kama JALALA ni LAKO,....
..... harufu ya jalala lako lazoeleka,...
.... na hilo sio tatizo LAKO bali la WENGINE.

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA,..
...kutolinyaka KIMAANA RUKSA!
Nakutakia SIKU KABAMBE MKUU!




Hebu tena Tony! Toni! Tone! waingilie kwa kuriwaindi - Whatever You Want

 


Au hebu tubaki na Raphael Saadiq katika -Good Man




Halafu Raphael Saadiq ajaribu kuzima kwa - It's a shame

 


Halafu D'angelo ndio azime kwa - She's always in my hair

 

Read more...

Kweli YAKO , SIKU IKIANZA kukudanganya!

Katika MTU kuna ya LEO ,...
....na ya KESHO!

Na ya KWELI katika MTU leo ,...
..... labda mipaka yake ni tofauti na ya MTU huyohuyo  KESHO.


Swali:
  • SI KIBINADAMU kuna mpaka hata KUZEEKA?

Ndio,...
... labda UNOGEWAVYO na kitu leo ,...
..... ni tofauti na utakavyo nogewa na kitu KESHO.

Swali:
  • SI unakumbuka hata GLASI ya PILI ya PEPSI inautamu tofauti na GLASI ya kwanza ya PEPSI kama tu utamu wa BIA ya kwanza utofautianavyo na wa BIA ya TATU?


Ndio,...
.... kweli yako hata ya MKE wa KWANZA mwaka huu,...
.... inaweza kuwa ni UONGO kama itakuaminisha kuwa TAMU ni tamu tu kivilevile,...
... kitu kifanyacho ufikirie utamu wa MKE wa nne utakuwa ni uleule kama wa LEO wa mke wa kwanza.

Swali:
  • AU?
  • Kwani kwa mama watoto , mme anogavyo leo ndivyo atanoga kesho?


Ndio,...
.... hata tukiacha mengine,....
...... labda kumbuka MAISHA na LADHA zake sio MGANDO,....
........ na uking'ang'ania kuamini hata wali uleule ni MTAMU vilevile kisa unafikiri kwa kuwa ni uleule basi uko VILEVILE,...
......KWELI yako labda imeanza KUKUDANGANYA.


Swali:
  • Si yasemekana hakuna hata kitu kimoja hapa DUNIANI kibakiacho vilevile (tukiruka MUNGU) na kila sekunde  chochote kile ukikiweka kwenye bonge la darubini waweza kustukia MABADILIKO hata kama ni yale ya jicho lako au tu angalau jinsi UONAVYO?


Ndio,...
..... labda KWELI yako jana,....
.....LEO imeshaanza kuwa ``ONGO´´ ,...
.... na ukiibinua waweza stukia imeshaanza kukudanganya.


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!






Hebu tuachane na hili na moja kwamoja tujiburudishe kwa ushambenga wa walionasiana....



Au tulainishe tu zaidi kwa Zouk Love A l'ancienne

 

Read more...

Bado NIPO/niko BAFUNI......

>> Saturday, May 12, 2012

.... na kabla sijarudi hapa KIJIWENI rasmi!:-(


YEAH!
NIPO aisee!
















Baada ya kujiswafi ,...
....natarajia KURUDI hapa kijiweni RASMI  kihivi KESHO
.... au ki- KESHOKUTWA!
NI HILO TU !


Hebu N.W.A. waanzishe tena kwa - Express Yourself 

 


AY na Maurice Kirya wajaribu kulainisha kwa ndude -BINADAMU




Au tu Maurice KIRYA abakie tu peke yake hapa UGANDA halafu azime tena kwa -If I EVER 


 

Read more...

Nipo bado na naahidi ntarudi na nguvu MPYA kikipengele GHAFLA!

>> Tuesday, May 01, 2012

Samahani wadau ambao niliwazoesha UJINGAbusara  marakedekede KILA MARA hapa KIJIWENI !




Nipo na NTARUDI na NGUVU  zaidi ki KUBWA KULIKO!






PAMOJA SANA MDAU!



Hebu tena TRACY CHAPMAN ajaribu kurekebisha kwa-Baby can I hold U?





Au tu Gregory Isaacs ajaribu kuharibu kwa -If I Don't Have You





Au GREGORY ajaribu kuzima kwa-My ONLY Lover






Halafu ajaribu tena kuzima  kwa-HUSH Darling



Halafu azime kwa-Cool down the PACE


Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP