Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

MOJA ya sababu KWA KAWAIDA MFIKIRIA SANA UKE , hadharani anaweza kujulikana na KUWA MAARUFU kwa KUONGELEA SIASA tu!:-(

>> Sunday, February 28, 2010

MAZOEA yaweza kumzoesha MTU kuongelea SIASA wakati shida yake ihitajiyo kuongelewa  ILI IPATE VITENDO MSWANO ni ILE  ya UKE.:-(

NDIO,...
... tatizo moja la BINADAMU AWAZAYE ni kufikiria pia kama AWAZACHO chafaa kuongelewa HADHARANI.:-(

Swali:
  • Si  umestukia hilo  hata kwa kufikiria ni vingapi ulivyowaza leo ambavyo huna-KIBEZI cha kuviongelea hadharani ili MAMA Mkwe asikie?
  • Umeshafikiria ukweli wa UPOTOFU wa kwamba ukiwazacho NI SIRI na   watu hawajui ndicho UWAZACHO?




Katika MAWAZO ELFU  YA MTU ndani ya siku ,...
.....inawezekana kabisa  BINADAMU huongelea kitu kimoja tu HADHARANI!


Ila BINADAMU ni MUWAZAJI wa maelfu ndani ya siku ,...
..... na waweza kirahisi kusahau hilo kwa kuwa MTUZ  ni CHAGUZI wa cha KUONGELEA hadharani.:-(




Swali:
  • Si unakumbuka hilo?



MAZOEA yanaweza yakawa yanasaidia  ni nini UNAONGELEA HADHARANI  zaidi,....
... wakati kikuwashacho KUNAKO NANIHII  zaidizaidi ufanyacho zaidi ni KUKIFIKIRIA TU.:-(


MAZOEA yanaweza yakawa ndiyo yasababishayo kirahisi MTU anaongelea SIASA zilizo maarufu  HADHARANI   zaidi,...
.....wakati tatizo lake ni UKE  na UMASIKINI usioguswa na SIASA  ZISIZOMAARUFU kuongelewa HADHARANI ambazo KIHESHIMIWA hufikiriwa TU.:-(



Swali:
  • Katika ulivyoviwaza leo si unakumbuka ni kipi UMEAMUA hautaweza kukiongelea HADHARANI ?
  • Umeshawahi kufikiria vizuri  ni nini kinachofanya baadhi ya uongeleavyo CHUMBANI hutaki wageni wajue huwa unavigunia,  SEBULENI?

Ndio,...
....kiongelewacho hadharani  labda wala si CHEPESI kuongelewa ki hivyo na MUONGEAJI ,...

......na kiwezeshacho KUKUTIA NGUVU ya KUKIONGELEA HADHARANI labda ni  ULIVYOJIFUNZA TU kuamini  HICHO  kinakubalika kuongelewa  HADHARANI ,....

....hasa kwa kuwa wote TWAFUNZWA KIHESHIMA hata bila kufikiria sana   kujua na kuamini  MAISHANI ni  VIPI vichache vifikiriwavyo ambavyo   ni sahihi KUONGELEWA HADHARANI.:-(

Na chakusikitisha zaidi  ni kwamba,...
....WATU wengi  sababu zao za kukalia KIMYA SHUGHULI ni za KUFIKIRIKA tu kwa kuwa kihalihalisi WAJARIBUCHO kuficha  kwa kutokiongelea kama kile cha kuwa wakati BADO WADOGO waliwahi kulamba KAMASI ,....

..... labda wamfichaye bado AKIWA NA KAMASI na  akihisi hakuna watu badala ya KUJIFUTIA kwenye KIJAMBA KOTI, Suruali  au KOCHI kamasi , kirahisi hulilamba KAMASI katika staili ya kulimeza tu kisa anaamini hakuna watu wampigao chabo HADHARANI :-(.




Swali:
  • Unafikiri kwa uhakika HII ni porojo tu?


Ndio,...
.... mpaka katika vitu MAMILIONI VIFIKIRIWAVYO  viwezwavyo HATA  kuanzishiwa BLOGU kuna waliochagua kuongelea FASHENI TU  hadharani.

Ndio,....
.... katika vitu MAMILIONI VIFIKIRIWAVYO viwezavyo kuanzishiwa BLOGU,  Mtakatifu Simon Kitururu huchagua kuongelea CHUPI na UJINGA  TU hadharani.:-(


Swali:

  • Unauhakika wewe unaongelea nini kirahisi HADHARANI?
  • Si unakumbuka  tukiachana na vile  BINADAMU afikiriavyo unavyoweza kumfanya kirahisi AVIONGELEE, -SI WAJUA BINADAMU MWENYE AIBU  ukimuandaa afikiriavyo waweza kumfanya kirahisi aonyeshe chupi hadharani kisa umemfunza kuita kificha nyeti `` BIKINI´´?

  • Si unajua katika vitu MILIONI alivyowahi kufikiria MTU huwa  kunasababu tu ni YESU Mtu FULANI apendacho kuongelea hadharani na sio ukweli kuwa kimsumbuacho  hata kusikiliza mahubiri vizuri ni NYEGE mshindo?



Ndio,....
.... kunasababu kuna  VITU milioni  ufikiriavyo wakati katika HIVYO ni KIMOJA ambacho uko huru kukizungumzia HADHARANI.:-(


Na kikubwa ni kwamba  UMEJIFUNZA tu ,...
.... ni NINI huwa KINAONGELEWA HADHARANI kitu ambacho ndicho KIKO NYUMA  ya  uchaguzi WAKO wa nini unakiongelea HADHARANI.


Na baada ya kujifunza ni nini katika kundi la wadaku ni RUKSA KUKIONGELEA HADHARANI kama unataka ufikiriwe UNAJIHESHIMU ,...

... kinachofuata katika uongeleayo kirahisi HADHARANI  ni MAZOEA tu ya ni nini unajisikia huru kurudia kuongelea  kitu ambacho husababisha aliyezoea kuongelea UDAKU kirahisi  ATARUDIA kuongelea  udaku  tu  HADHARANI.:-(


Na  haki ya MAMA KISEBENGO TENA !- ukishazoea kitu,....

..... si ajabu katika MATUSI yote  DUNIANI weye kirahisi UKIPANDISHA nyege ya KUTUSI  utatukania MAMA kama matusi ya MAMA ndicho ambacho  ULICHOJIZOESHA kutukana HADHARANI.:-(


Na ukishazoea kitu,....
......  katika  MAELFU YA UFIKIRIAYO  waweza kujikuta ukumbukayo kuyaongelea kwa kuwa ulichozoea kuongelea ni SIASA ,....

.....utakaCHOkumbuka kuongelea ni SIASA TU  kwa HATA wapenda FASHENI wakati kikusumbuacho wakati huo ni JINSI YA KUPATA UKE hadharani.:-(


Swali:
  • Si unakumbuka unaruhusiwa kunibishia?

Ndio,...
.... mengi  UYAFIKIRIAYO hujawahi kuyaongelea na sababu kubwa HUYAONGELEI  UYAFIKIRIAYO  MENGI ni za kufikirika tu NA  ni ALINACHA tu  ,...

.....na kwa hilo SAMAHANI kwa kukukumbusha  MHESHIMIWA!


NAACHIA HAPA WAZO Mheshimiwa!:-(

Hebu Naughty by NATURE katika kubadili warudie.- Jamboree



Ice Cube arudie - Today Was A Good Day[JIHADHARI: :LUGHA fulanikatika wimbo KAMA wewe ni msikiliza NDOMBOLO KATIKA NENO INASEMA NINI ... ndude  inatumia lugha ya namna gani kiheshima inaweza kumkwaza MLOKOLE.:-(]




Au tu Snoop Dogg abadili zaidi kwa- Pump Pump[Tahadhari: KWA mheshimiwa asikilizaye MANENO  anaweza kusikia lugha chafu!:-(






Nipo,....:-(

Photobucket




Photobucket



Photobucket





Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket

Read more...

MTOTO MZURI labda JAMBA tu usiahirishe,...

>> Saturday, February 27, 2010

.... kwa kuwa  kama umewahi KUBANWA na kijambo,....
..... wajua  JUHUDI  na  JEURI za waliobanwa kijambo WASIOJAMBA HADHARANI  sana sana ni za kusogeza MUDA tu  WAKUJAMBA iliusisikie wakijamba  ,...
.... na AFYA YA KIJAMBO  CHAO kwa bahati mbaya bado huwa iko PALEPALE.:-(


Na MTOTO MZURI  labda   NI BUSARA PIA  kijambo usilazimishe,...

....kwa kuwa ALAZIMISHAYE KUJAMBA  anaweza akafanikiwa KUHARISHA PIA juu ya kijambo hasa KWA KUWA  nukta ya kutolea uharisho NI ILEILE ambayo ukizidisha JUHUDI hewa itaongezewa CHEMBECHEMBE NA ROJO  katika MTOKO  utumiao tobo   ambalo wengi hutambua kuwa  HUWA linanunia shughuli  sehemu mbali mbali lakini katika tundu lililopo  PALEPALE.:-(



Swali:
  • Unafikiri kwa kuahirisha UJUACHO utafanya WATU WENGINE wasipokuwepo kuna badili kuwa utakachofanya ni KILEKILE?


  • Unafikiri ukidokoa MBOGA bila kuonekana  kitendo chako hugeuka kuwa NI kuonja MBOGA?


NDIO,...
... moja ya BUSARA za BINADAMU ni kuficha  vitu vijulikanavyo SIO SIRI na  kuwageuza wavifanyao HADHARANI mahawayani ingawa LABDA uhawayani WENYEWE WENYE TAKO KUBWA  ni ule   UTU na HESHIMA ZA MTU   zenye misingi  ijengwayo kwa kuwa tu NI HESHIMA eti MJUACHO ANAFANYA kafanya SIRI.:-(



NIMEACHA!

Tahadhari: MHESHIMIWA  hii taralila HAINA uhusiano na KUJAMBA!:-(


Hebu tubadili wazo HASA kwa kuwa kwenye taralila isiyona uhusiano na KUJAMBA inaneno JAMBA  lisilo la HESHIMA kwa  BAADHI YA WAUNGWANA WAJAMBAO  kwa kuwaachia En Vogue wadai- My Lovin' (Never Gonna Get It)



Salt N Pepa wazungumzie - Shoop




Au tu NAUGHTY by NATURE warudie tu.- FEEL me FLOW

Read more...

Kwa kuwa , ...KUWA na DHAMBI ni tofauti na JINSI ya kujisikia una DHAMBI!

[ Tahadhari: JIHADHARI na WAZO hasa kama ULIVYO na unavyojisikia UNAFIKIRI  ni sawasawa!:-(]



Kuna UWEZEKANO  kabisaaa...
...kuwa  MASIKINI ni tajiri kama hujamfundisha MHUSIKA  jinsi ya kuusikilizia UMASIKINI!:-(


MATATIZO ya UMASIKINI ni MATATIZO tu kawaida  ,...
... na LABDA mpaka uyaoanishe tu na UMASIKINI ndio matatizo AMBAYO NI MATATIZO kutokunya KIKAWAIDA kwenye jedwali la MATATIZO  kuna ambayo utayaambatanisha na  SEKSHENI a.k.a kipengele cha MATATIZO yaletwayo na kibano cha UMASIKINI na kuyafanya kuwa MATATIZO HAYO ni MATATIZO YA UMASIKINI.:-(


Samahani,....

..... nimekumbuka , NIA na MADHUMUNI  ya taralila hii ni kuongelea DHAMBI.:-(



DHAMBI ,...
....ni FIKIRA aliyokuwanayo MTU  hasa baada ya TENDO,...

.... kwa kuwa DHAMBI inaweza ikawa ni TENDO LA NDOA  kabla HUJAFIKIRIA na kulioanisha kifikira na UZINZI.:-(


Kwahiyo ;...
...DHAMBI usiishangae kama  ni  tamu!


Na labda unajua  hata kama naheshimu kwamba HUTAKIRI,...

....  wala DHAMBI  hainauhusiano na UCHUNGU ingawa KIFIKIRA neno dhambi linamchezo wakufanya hata utamu wa ULICHODOKOA  ufikiriacho ni KISAFI  KIFISADI katika TAMU yake  YA MSHIKAKI  ukahisi KWAKE kunyunyiziwa chembechembe za kamasi la MPIGA CHAFYA ambalo husababisha utamu wa peremende usikilizwa kwa mikwaruzo ya ujuaji labda moja ya ifanyayo PEREMENDE tamu ni kamasi.:-(!


Swali:
  • AU?



Ndio,...
....DHAMBI ingekuwa MCHICHA,...
....kuna watu tungejaza TENGA!:-(


Ila kwa jinsi DHAMBiI ilivyokuwa NYOKO,...
.... ahubiriye DHAMBI mara karibu zote ndiye aliyekuwa na TAFSIRI FULANI  ya uhakika kwake YA DHAMBI ,...
....kitu kifanyacho awe miongoni mwa WATU ambao kwa uhakika wanajua wafanyavyo ni DHAMBI.:-(




Ndio ,...
...jinsi yako YA  kufanya DHAMBI  yaweza kuathiriwa na STAILI yako ya  unavyoisikilizia DHAMBI.

Na kwa kuifikiria dhambi,...
waweza kustukia  katika  dunia ya WENYE DHAMBI, watu wengi wanakustukia WEYE ni MWENYE DHAMBI kwa kuwa tu  NI KWELI  katika wafunikao kwa GWAGURO ,...
...WEYE unaikalia uchi na kuionyesha masharubu ya chini  DHAMBI .:-(



Tukiacha MZAHA ;....
Swali:

  • Unauhakika DHAMBI ni nini?
  • Unafikiri UMASIKINI USIKILIZIWAVYO kama tu DHAMBI  , unauhakika MASIKINI ni muda gani  HUWA anajisikia MASIKINI?
  • Unauhakika TAJIRI anajisikia tajiri wakati anakunya?
  • Unafikiri wewe kama ni MKRISTO ambaye  kwako ruksa ni kuonjeshwa kidude kimoja tu NA MKE WAKO  WA NDOA huwa unaelewaje na KUIGEUZA NI DHAMBI   ya MUISLAMU ambaye kwake SIO DHAMBI ,- ile ya KUONJESHWA VIDUDE VINNE  kutoka kwa WAKE WANNE WA NDOA  awawezao kuwapa huduma WAJISIKIE NI WAKE WA MTU  wapatao matekenyo yote ya NDOA   kwa maadili  ya KIISLAMU?
  • Unafikiri dhambi yako ya UZINZI  inafanana na dhambi ufikiriayo ni  HIYO HIYO kwa mwingine YULE aliyedakwa UGONI na wewe ambaye hafikirii kama WEWE?

  • Unafikiri kuna MTU anajisikia ana DHAMBI kama alivyo na DHAMBI?


NI HILO TU!
JARIBU TU  kukumbuka  ni TAFAKURI tu hii  MHESHIMIWA  na KUNAUWEZEKANO  kama WAZO HILI  limevalishwa chupi , basi chupi INATOBO!:-(


Hebu ANDREW SAMUEL alainishe na kubadili HALI YA HEWA KIJIWENI kwa ndude-Pinacolada



Maxi Priest abadili zaidi kwa ndude-Close to U



Au tu MAXI Priest amalizie tu kwa ndude-Just a little bit longer

Read more...

WAKATI kunauwezekano UFIKIRIACHO ni FIKIRA tu!:-(


NDIO,...
... ..labda kuna WATU unafikiri,...
....wanakufikiria UNAVYOFIKIRIA unavyofikiriwa.:-(


Swali:

  • Lakini unafikiri WATU wanakufikiriaje WEYE?

Ndio,...
....kuna PADRI katika fikira haoanishwi na NYEGE  YA DHAMBI,....
.....kwa kuwa  ni kweli ndani ya siku yake HUHUSIANISHWA  na mtekenyo ulazimishao baadhi ya watu WACHUMBIE malaya ambaye NI KWELI afanyacho kwa kawaida ndani ya siku SIO DHAMBI wala UMALAYA.:-(

Swali:

  • Unafikiri MALAYA afanyacho ni UMALAYA  siku nzima?
  • Si unakumbuka wewe sio UNAVYOFIKIRIWA kwa kuwa kitu halisi sio FIKIRA?



NIMEACHA tafakuri hii!
Kumbuka hili ni WAZO TU   MKUU na labda  si AJABU  kujaribu KUPATA POINTI ya hoja YAKE  MHESHIMIWA!:-(


Hebu Macy Gray abadili kwa -I TRY




Au tu Corinne Bailey Rae abadili kidogo zaidi kwa -I'd Like To

Read more...

Jiografia NGUMU Tanzania!:-(

>> Friday, February 26, 2010

[Tahadhari: Hii taralila ina TAFAKURI ambayo inaweza isikufundishe kitu hasa kama wewe sio mtumiaji RAMANI !:-(]




Hebu tujifunze RAMANI ya kwenda kwa akina KHADIJA akaaye karibu na kwa FUNDI VIATU,...
....katika kujaribu kukukumbushana jinsi ya kusoma RAMANI ukiwa TANZANIA.





Jinsi ya kumuelekeza mtu mahali TANZANIA ni bonge la SANAA!



Jinsi ya kumuelekeza MTU kwa akina KHADIJA ,....

....kwaweza MPAKA kukujulisha KIPAJI chako MWENYEWE kile cha KUNUSA HARUFU MBALIMBALI  ambacho wazazi wako hawakufanikiwa kukistukia,....

....kwa kuwa waweza kujikuta ili kurahisisha kumuelekeza KIJEBA kwa akina KHADIJA inabidi ugusie mpaka aina za HARUFU mtu atakazo kutananazo NJIANI ,....


....harufu za TOKEA mlipo MPAKA   kwa akina KHADIJA ili tu kuhakikisha NJEMBA MWENYE RAMANI, ramani    haimpotezi MUELEKEO na kumkosesha KUFIKA kwenye  mihadi na KHADIJA MTOTO MZURI,....
....kisa tu  harufu ya mfereji wa chooo hakuinusa.:-(




NDIO,...
....jiografia na USOMAJI WA RAMANI ufunzwao MASHULENI  Bongo NYOSO  hautoshi,...

.....kwa kuwa kirahisi waweza kujikuta inabidi  ili kumuelekeza MTU kwa akina KHADIJA inabidi  bila kuangalia ramani,...



.....  umuelekeze  :


``......ukifika MBUYUNI  weye ulizia kwa Simon Kibaka wa MINAZINI na utaelekezwa,....

......na wakati unaelekea huko kabla ya hata hujafika  MINAZINI utastukia kuna sehemu inanukia mavi,....

......basi hapo kata kulia utaona kuna kauchochoro ,....

... ukishakata kona na uko kwenye UCHOCHORO  weye nenda weee , NENDAAAA WEEEEE,  mpaka mwisho wa uchochoro ambako kunanukia KOROSHO za KUCHOMA, halafu  kata kulia ambako utatokea kwenye nyumba ambayo ina kibao MBWA mkali,....

....hapo KWENYE MBWA MKALI  utatolewa baruti a.k.a  KUTOLEWA MKUKU , nikiwa na maana UTAFUKUZWA NA DOGI a.ka MBWA Mweusi ,....

Wakati unatolewa BARUTI NA MBWA  hakikisha unakimbilia kushoto mwa FENSI YA MICHONGOMA  na MBWA huyo atakufukuza kupita NYUMBA kadhaa.

Akimaliza kukutoa NDUKI MBWA  na kugeuza kurudi kwao angalia kulia utaona kuna nyumba ina BATI jeusi ,...
....basi nenda hapo kwa kufuata barabara yenye mfereji unukao MIKOJO mpaka ukute kuna genge la nyanya. MUULIZIE MUUZA nyanya kwa akina KHADIJA ni  wapi atakueleza.


SI umenielewa EEE?

.....YANI ni hapo hapo tu na haita kuchukua hata dakika kumi utakuwa umefika kwao ambako jifanye unakiu ya Maji kwa kuwa BABA yake Khadija BADO ana UNOKO WA ENZI za wakati  kuna ISIDINGO kwenye TV ZANZIBAR tu,...


....na bara ni kwa NYERERE  TU ambako kulikuwa na TV na wakati huo  MZEE MZIMA alikuwa anadeku BBC  tu kwenye TV a.ka LUNINGA ,...


....na  kwa hiyo usimuulizie KHADIJA kwao kwa jina LAKE  moja kwa moja lasivyo utatolewa BARUTI na KHADIJA kipenzi chako atakula KIBANO na matumizi yako yote ya RAMANI hayatafanikisha uzinzi.:-(´´





Ngojea nifupishe somo hili la  jiografia  ya  kwa akina KHADIJA kwa ufafanuzi zaidi hasa kwa aliyezoea kusoma RAMANI.:


Kwa kifupi,...
....kama nia ni watu wafike kwa akina KHADIJA,....

..... hatua ya kwanza ni kuhakikisha wewe ni BINGWA wakukariri,...

...kwa kuwa KUKARIRI KWAKO ndiko kutamsaidia mwenye ANUANI na RAMANI ya kwa akina KHADIJA wakati anaenda KIMUELEKEO  hafuati tu ramani ,...

....kwa kuwa RAMANI aliyonayo inaweza kuwa hainakazi kama hujatamka RANGI za MABATI , MIBUYU iliyokuwepo NJIANI na bila KUSAHAU HARUFU UZINUSAZO NJIANI  kwa kuwa TANZANIA kwa kiasi kikubwa ujenzi bado haufuati RAMANI ya MJI  na  KIBOSILE hakawii kujenga banda la MBUZI  sehemu ionyeshayo ni njia kwenye RAMANI.:-(


Swali:

  • Unabisha?
  • Ushajisikiliza wakati unamuelekeza MTU mahali Ze BONGO?


Kwa hiyo,...

...jaribu kukariri kila kitu ulichokiona wakati unaenda kwa kina KHADIJA na ikibidi HARUFU zilizo tekenya pua yako na fundi viatu  chini ya MUEMBE ndio alama umekaribi  upalengapo.


Kwa hiyo ,...
.... kumbuka kuwa bado KUULIZIA watu ni muhimu katika RAMANI zetu BONGO na kama huna heshima na HIYO ikupe MOTISHA ya kusalimia watu kwa kuwa huwezi jua ni nani ambaye utamuhitaji angalau kuwa na uhakika  vichaka viko wapi ikibidi uchimbe dawa kabisaa kabla hujagonga hodi kwa akina KHADIJA.
Unajua TENA mara nyingi ni vigumu kuomba kwenda msalani haraka haraka UGENINI na ni balaa ukienda msalani  baada ya mafanikio ya choo kikubwa ukastukia kwa mpenzi KHADIJA maji yamekatika na huja falashi malighafi yenye ukubwa wa kutosha UGENINI.:-(



Tukiachana na hilo:
Swali:

  • Miji ina RAMANI Tanzania lakini unafikiri ni kwanini RAMANI za mipango ya MIJI hazifuatwi mpaka siku hizi katika ujenzi wa nyumba MPYA mahali lukuki?

  • Si unakumbuka tunavyoongea kuna viwanja vinavyoendelea kuuzwa ambavyo haviko katika ramani ya MIJI ?

  • Unafikiri kati ya MJENGA holela na MUUZAJI VIWANJA ambaye ndiye MSIMAMIAJI wa viwanja HOLELA nni nani mwenye kosa?


Ndio,...
...... matatizo yajulikanayo tayari kama tu ya KUPANGA MJI yanaendelea kuachiwa kuwepo TANZANIA na unaweza kukuta azibaye BARABARA na MIFEREJI ya ENEO iliyoko kwenye ramani ndiye MKUU wa eneo KIOFISI na kiutawala katika  eneo.:-(



Ndio,....
....JIOGRAFIA ngumu TANZANIA ,...
...na kuna uwezekano RAMANI kama zifundishwavyo katika somo la JIOGRAFIA MASHULENI hazijitoshelezi ,...


.... na  kwa hiyo RAMANI YAKO labda haitoshi kukufikisha kwenu kama HUKUJUI  KWENU Mheshimiwa.:-(


Swali:

  • AU?


TUNAKUMBUSHANA TU MKUU na usikonde!

IJUMAA na WIKIENDI NJEMA!

Heb kwa wasikilizaji maneno Ras NAS atusaidie kubadili mshawasha kwa kibao-Dar-es Salaam



Eddy Grant arudie kwa wasikilizaji maneno kitu -Gimme HOPE Jo' anna




Eddy GRANT arudie pia kwa wasikilizaji maneno ndude- War Party




Au tu EDDY GRANT amalizie tu na  ndude -Living on the frontline

Read more...

Nakusabahi tu MKUU!

>> Wednesday, February 24, 2010





Vipi MAMBO Mkuu!
Ni matumaini yangu weye MDAU wa hii blogu  MAMBO ZAKO Dukinaa !


Vipi ;...
.... siri yako na leo  iko SALAMA ?




Nimebanwa KIDOGO leo MHESHIMIWA kitu ambacho chasababisha nishindwe kufanya   WAZO litoke STEREO.:-(








NAKUTAKIA kila la kheri upate angalau kisaidiacho  UWE na UHAKIKA wa KUPATA choo cha uhakika  MHESHIMIWA!
KESHO BASI kama sijafa na KAMA inawezekana !









Kabla ya hiyo kesho TULIZA basi mshawasha kwa kumsikiliza KALA JEREMIAH akishusha kitu- WIZI MTUPU

Read more...

JINSI ya KUJIFUNZA kukitaka kidude ULICHONACHO!

>> Tuesday, February 23, 2010

Tatizo ni:

... WATU WENGI hufikiri  ILI WAWE NA FURAHA,...
... wanahitaji WASICHONACHO,...


.. wakati WALIVYONAVYO hawana hata MUDA  WAKUVIFIKIRIA kwa kuwa WAKO BIZE wanahangaikia WASIVYONAVYO.:-(



MTU alichonacho tayari ,....
... kinaweza kirahisi kuwa NDICHO MUHIMU ZAIDI MAISHANI kuliko chochote ASICHONACHO ambacho kinamtoa raha kwa  jinsi tu ANAVYOHENYA kupigania KUKIPATA.


NA usichonacho,....
..... hicho HUNA na labda huna nafasi yakukifikiria  na kujua kitakavyokupoza ROHO ukilinganisha na AMBACHO unacho TAYARI.:-(

Swali:
  • Unafikiri umeshajifunza KUFURAHIA kikojoleo chako kabla ya KUTAKA  na kile kikojoleo  cha MWENZIO usichonacho?

  • Kwani  umeshajifunza KUHESHIMU elimu yako ya SHULE YA MSINGI ULIYONAYO TAYARI iliyokusaidia kujua kusoma na kuandika kabla ya KUJIKOSESHA FURAHA kwa kufikiria inahitajika  uende CHUO KIKUU au UWE PROFESA ili ufurahie KUELIMIKA?


KUMBUKA,...
.... kunauwezekano MKUBWA,...
.... ukijifunza KUKITAKA na KUHESHIMU ulichonacho TAYARI,...


.... unaweza kustukia WALA huhitaji cha ZAIDI kingine ili  MAMBO YAKO yawe DUKINAA,....
.... kwa kuwa kuridhika hakuna uhusiano na ni kiasi gani UMEJILUNDIKIA ndude .:-(

Swali:
  • AU?
  • Si unajua hata uelimike vipi utakufa wakati kunakitu HUJUI?
  • Unafikiri maishani mwako  UMEFANIKIWA kujifunza kuendelea   KUKITAKA ulichonacho?




...kabla sijaacha ngojea nibonge ung'eng'e kwa kudai,...
.....FIKIRIA kwa kuwa labda ;...
- ``HAPPINESS IS NOT what YOU WANT;.... its WANTING what YOU HAVE!´´.:-(


NIMEACHA!

SIKU NJEMA Mheshimiwa!


Au tu ISASHA abadili tu kabisa kwa ndude-Don't U know?



Au tu Dr Remmy arudie -NDUMILA KUWILI

Read more...

TUKIACHANA na DUNIA tuishiyo SASA ambayo WENYE NGUVU ndio walindwao na MABODIGADI !:-(

[TAHADHARI : Taralila HII  imelalia mtazamo wa KIUME ZAIDI  katika kugusia na kulishikashika SWALA!:-(]




Hadithi Hadithi!

Hapo zamani za kale kulikuwa na WENYE MABAVU na WANYONGE,...
...ingawa kwa kawaida ilikuwa WENYE MABAVU ndio wanalinda WANYONGE.

Na ilikuwa ni jambo la kujivunia kweli  kama NJEMBA bode lako a.k.a MWILI lina mamisuli ya KIKULIMA na sio KITAMBI , kwa kuwa  WEYE USIYE na KITAMBI  ulijulikana unaweza kulima PUNDA KASINGIZIWA na kwa hilo tu  MADEMU warembo wa kijijini walikuwa hawakawii kukuchekea KISIMANI  na kukuchungulia ukienda kuoga MTONI ,wakati  ndoto zote zao hata zile za  wakati TU ndio wanavunjavunja  UNGO  zilikuwa zina DONDOO mpaka za  unavyonukia vizuri KIKWAPA CHA NGUVU  kwa jinsi  tu ulivyo na juhudi SHAMBANI.

 NGUVU ilikuwa inamaanisha NGUVU kweli na kama wewe KIDUME unalegalega a.k.a UMELEGEALEGEA   , wazee wazima  walihakikisha hutoki JANDONI  kwa hata kudai uliliwa na simba huko; kitu ambacho Wapare walidai umemezwa na MSHITU. JANDO lilikufunza  sehemu ya MWANAMKE na jinsi ya kumshungulikia apate kirahisi mbele yako kujisikia MWANAMKE.

Na hapo zamani za kale  mwenye akili alikuwa ni yule ajaliye famili  na jamii yake. Mwenye akili alihakikisha familia na jamii yake INAPATA MSOSI , inalindwa, ina nyumba ambayo umejenga kwa nguvu zako MWENYEWE , na angalau kila mtu aliyepita UMRI WA KUCHEZA UCHI  WA KITOTO a.k.a kila aliyekaribia kuanza kuota  NYWELENYWELE KUNAKO umehakikisha  kavaa vazi la kisasa KIJIJINI  ; ambalo la weza kuwa ni chupi ya MKEKA au tu ile CHUPI ya  ngozi itokanayo na MNYAMA  uliye mdaka kazubaa msituni MWENYEWE , ambaye kitoweo chake  kingine bado kimekaushwa kwa moshi jikoni juu ya jiko la kuni.

Hapo zamani za kale , ukishajulikana unamiguvu ya kutosha na umetahiriwa safi au tu KUFUNDWA VIZURI  kama unatoka katika  jamii yenu ishabikiayo  magovi, BADO NI WAZAZI  ambao walihangaikia swala la kukupatia  POOZEO LAKO  la maisha  a.k.a  kukutafutia MZAZI MWENZAKO.

Na binti mzuri alikuwa SIO  yule mwenye bomba la tako au tu chuchu ya kutosha , kwa kuwa ilibidi kwanza WAZAZI wafanye utafiti kuangalia MASWALA YA FAMILIA YA KIGOLI ,  kama yale ya  UKOO wa  Kimwana MNONO mlengwa KUWA hawana KIFAFA kwao  , BIBI YAKE  hana UKOMA au tu  kama UCHAWI  KWAO  haupandi vizuri.

Kwa hiyo MTOTO mzuri aliyenona kabisa  waliweza kumstukia DNA yake  ni ya KICHAWI  KABLA HUJADAKA KIMWANA , na  kwa  hilo ukastukia VIJANA BOMBA  wanukao kikwapa cha kutosha kukuhakikishia ni wakulima safi WAMEFUNGA BREKI ZA MATAMANIO na wakawa wana Mruka KIMWANA  MZURI  mwenye macho ya gololi, mashavu ya KUMIMINA, tako mtikisiko ´´SINGIDA-Dodoma´´,  kwa kuwa tu kwao  MAMA YAKE MKUBWA anakifafa na aliwahikuzaa MAPACHA kitu ambacho kwenye MILA zenu ni NUKSI..:-(


Swali:
  • SI kunauwezekano MWENYE NGUVU siku hizi siye yule alindaye wengine, ila ni YULE alindwaye aepukane na wanyonge na  ASKARI?
  • Si mwenye nguvu siku hizi ni yule MWENYE PESA?
  • Si mwenye akili sikuhizi ni yule AJILIMBIKIZIAYE MALI wakati wengine hawana  , aliaye  katika ofisi ya UMMA mali za UMMA , na unaweza kumtambua KIRAHISI kwa kuwa kwa kawaida yuko katika KUNDI ambalo huitwa MHESHIMIWA?

  • Si Msichana  aonekanaye Mzuri siku hizi Tanzania ujazo wa TAKO  kipimo chake kimepunguzwa ingawa titi saa sita bado lakubalika?

  • Na si unajua kwa wadada  LIMJAMAA lao WALILENGALO au WALITEGEMEALO sasa hivi kwa kuwa ni jizi kwa kukusaini tu MAKARATASI   na lina MIPESA KEDEKEDE hapo zamani kuna uwezekano wangekufa -NALO kwa njaa?

  • Si unakumbuka PIA hapo zamani bonge la demu lazima linuke KIKWAPA vya kutosha ili KIJIJINI NJEMBAZ na WAZAZI WENU mjue ni bonge la mfanyakazi na likiingia shambani hilo ni BONGE la  TREKTA na  lafaa kuwa MKE?

NDIO,...
.....HAPO ZAMANI kulikuwa na MABAYA na MAZURI kama SASA HIVI.:-(

Swali:
  • Unafikiri kizazi cha SASA hivi kimejifunza ni yapi MAZURI ya zamani yafaayo kutunza na ni yapi hayafai kuyang'ang'ania kwa kuwa tu bado yana tamu zake sasa hivi  kwa baadhi ya watu?


Hapo zamani,...
...... kulikuwa na TAMU zake lakini pia  usisahau MABAYA kwa kuwa tu unajuakubonga UNG'ENG'E siku hizi na kamsemo ka ``OLD is GOLD ´´ umeshakakariri na KUKAAMINI kuwa NI KWELI TUPU.:-(

Hapo zamani labda UNGEKEKETWA usikiliziacho tamu  wewe ,OOOHO  wee  SHAURI YAKO!


Hapo zamani  kabla ya watu kuanza kuwa na NGUO na VIATU vya JUMAPILI au IDI ungekuwa unabonge la chupi la NGOZI au MKEKA wewe, Ohoo wee  SHAURI YAKO ! 

Halafu HEBU LIONE VILE,...
....eti siku hizi linaturingia na chupi lake  la GUCCI na wala sio la KITENGE.:-(





Tukiachana na mzaha,....
Swali:
  • Unafikiri siku hizi si WENYE MABAVU ndio walindwao na MGAMBO , POLISI , MAHAKAMA  na mpaka JESHI wakati wanyonge hawana Mlinzi?
  • Na siku hizi si mpaka WIZI ni shughuli ya  asifiwaye kwa MIAKILI?


Na katika HITIMISHO la hii HADITHI HADITHI,...
..... napenda kukukumbusha Mheshimiwa kuwa HIVI SASA bado kuna WENYE MABAVU na WANYONGE  ingwa labda kuna ukweli kuwa siku hizi mambo yote ni  MNYONGE  MNYONGENI na HAKI ZAKE CHUKUENI na sio MNYONGE MNYONGENI lakini HAKI zake MPENI.:-(


NI HILO TU na ni Mwisho wa HADITHI HII!
KUMBUKA TU,  NI  wazo tu HILI MKUU!




Hebu Ringo Madlingozi na Oliver Mtukudzi wabadili kwa kurudia  kitu-Into Yami




Au tu Sipho Hotstix Mabuse arudie tu -Shikisha

Read more...

UJUMBE MZURI ni kama UGALI uhitajio msaada wa MBOGA tamu ili SWALA ZIMA la kusukumiza TONGE lifanikiwe!:-(

>> Monday, February 22, 2010




UJUMBE MZURI labda hautoshi kwa kuwa tu ni UJUMBE MZURI,...
... ukizingatia walengwao  wanaweza wasiupokee USIPOSINDIKIZWA na kulainishwa na  NJIA ambazo walengwa hawafikirii ni MBAYA.:-(

Swali:
  • Si unajua kuna watu bila TAARABU  mahubiri yako YENYE UJUMBE MZURI WA BUSARA kuhusu mapenzi hawatayaelewa?


 UJUMBE MZURI ,..
....kwa kawaida hausikilizwi  kwenye WIMBO MBAYA.:-(

Na kuna wengi WASIKILIZAO matusi  vizuri,...
... ambao ni UJUMBE WASIOUPENDA  kwa kuwa tu wanapenda mrindimo wa muziki  AMBAO KWAO ni  wenye UJUMBE MBAYA .:-(


Ndio,...
....kuna wamsikilizao pia  MTU vizuri ,....
... kisa WANALAZIMIKA kuwa watulivu nakusikiliza  KWA KUWA wanatishwa na sura lake BAYA.:-(



Swali:

  • AU?
  • Si unakumbuka ugali  unaweza usiliwe kama hauletwi mezani na MBOGA tamu? 
  • Si unakumbuka UGALI mbaya unaweza kuliwa kama mboga tamu?
  • Kwani wewe hakuna wimbo uupendao ambao unajua UJUMBE WAKE NI NYOKO lakini hata hivyo unaurudiarudia NA MPAKA KUUKARIRI  WIMBO huo  wenye UJUMBE MBAYA KWAKO na kwa  MATOTO YAKO huku ukitingisha bichwa lako kisa mirindimo ya MUZIKI na SAUTI ya muimbaji  vinakukuna nanihii kunako?


Ndio,...
....TATIZO ni ,...
...ujumbe MZURI katika hata HOTUBA ,....
... labda inahitaji SURA fulani au tu SAUTI fulani  ili walengwao na UJUMBE wasikilize UJUMBE bila kushikiwa VIBOKO.:-(

Swali:

  • Si nasikia kuna wamsikilizao Barrack Obama  Marekani kisa wanapenda sauti na WANAOMSIKILIZA Rais KIKWETE Tanzania kisa wanampenda sura?
  • Si unakumbuka kuna sababu  si kila mtu  WEWE unamsikiliza ?
  • Si unajua kuna uwezekano majibu ya matatizo yako ulishapewa ila hukuyasikia kisa hukupenda wimbo au sura tu ya MTOA suluhisho?
  • Si unajua upendaye kumsikiliza unaweza kunogewa kufuatilia azungumziavyo jinsi ya kutatua matatizo ya kujisaidia kwa bata kuhitajivyo bata wavalishwe chupi kuliko USIYEPENDA kumsikiliza akizungumzia jinsi ya KUTATUA matatizo yako?




Ndio,...
.. labda  HATA MAANDISHI  usiyopenda KUYASOMA yanasomeka bado,...
... na husomi hata  BIBLIA na  KORANI   ingawa unajua vina UJUMBE  MWEMA tu,...

....kama tu kwenye kitabu cha KAMASUTRA ubobeavyo kwenye PICHA na sio MAANDISHI kisa kwa ladha yako VITABU hivyo banangenge vimekosewa kuandikwa VIZURI katika mirindimo  ikupandishayo MDADI WA KUSOMA  kama vile yaandikwavyo MAGAZETI YA UDAKU katika mirindimo iwezayo kukufanya uone HABARI ya KHADIJA hapendi kuvaa chupi ni HABARI MUHIMU SANA kuliko habari ya KUNA MAFURIKO Ludewa. .:-(

 Swali:

  • AU? 
  • Si unakumbuka pia kuwa  UJUMBE MZURI NA WA BUSARA kwa MTU MWINGINE  inawezekana ni KILE ukiitacho wewe  MATUSI?



 Staili ya MUANDISHI wa habari,...
... yaweza kusababisha usomee UANDAJI wa UDONGO walao wajawazito, HISTORI  au tu  angalau upende kujisomea stori za  UCHAWI uziogopazo,.....
..kisa STALI YA UANDISHI  kukufanya usiyependa kusoma uhusudu KUHAMIA mstari unaofuata katika HADITHI kisa kanogewa na SENTENSI ya kwanza ,...


..... kama tu kwa ASIYE PENDA UGALI WA MUHOGO kujikuta kamaliza bonge la sima kisa MBOGA tamu kusababisha tonge la kwanza kumshawishi MLENGWA kukata TONGE la pili na mpaka kumaliza MAAKULI bila kukumbuka huwa HAPENDI UGALI wa MUHOGO kwa kuwa yeye ni MUTU ile inapenda YUGALAI (Ugali kwa Kizungu) iliyopikwa kwa kutumia  UNGA WA SEMBE.:-(



Ndio,...
... UGALI bila MBOGA unalika bado .:-(



NI wazo tu HILI MHESHIMIWA!:-(


Hebu India.Arie, Dobet Gnahore, Idan Raichel na Blue Miller walete- Palea




Au tu India Irie na Dobet Gnahore waendelee na -Pearls


Bila kumsahau ALI KIBA katika kibao-Mac Muga

Read more...

HIARI IPO hata kama kwa HIARI atendwavyo MWINGINE yachokoza na kuchokonoa HURUMA YAKO kwa kuwa ANAVYONANILIWA hupendi!:-(





NDIO hata ubishe ,...
... katika KUNANILIU ,....
...kuna WANANILIWA pia ,...
.... ambao  WANANANILIWA VIZURI kwa bidii TU  kwa hiari yao wenyewe.:-(


Swali:
  • Kwani unafikiri  WATANZANIA katika kunaniliu a.k.a KUCHAGUA CCM na sio vyama vya UPINZANI unafikiri WENGI TU  hawafanyi hivyo kwa HIARI yao tu hata kama WEWE hupendi CCM Mkuu?

  • Kwani unafikiri  ni MANGAPI  utendewayo ambayo unasaidia WEWE MWENYEWE  yafanikiwe  UTENDWE VIZURI TU kwa faraja?

Kuna yalazimishwayo,...
.... lakini  HATA KAMA HUPENDI haiondoi ukweli kuwa kuna  WAUMIZWAO,...
... ambao yaumizayo  ni ya HIARI  KWAO.:-(


Kuna yalazimishwayo,...
....lakini hayohayo usipostukia hasa   KAMA WAUMIZWAO NI WAJANJA  unaweza kushabikia mchokonoo UNAOUMIZA bila kujua  kwa kuwa WAJANJA  wanaweza tu kutungia jina tofauti  MCHEZO wakati KITENDO NA  maumivu  ni YALEYALE.:-(

Swali:
  • Si unajua adhabu nyingi tu  wapewazo watu kama tu KURUKA KICHURACHURA ,  zikifanywa kwa HIARI wajanja HUZIBADILI JINA na kuziita  ni  MAZOEZI?

  • Si unajua KUBAKWA, na  MAMA WATOTO  kulazimika kuwa kiburudisho kwa baba watoto bila kuandaliwa   kwa kuwa baba watoto SAA HIYO  anataka kula mali zake alizozitolea MAHARI   ,kwa MDADA kunaweza kukawa na maumivu sawa kimwili ,  ingawa moja MDADA kabakwa MIGOMBANI na JINGINE ni  IMEBIDI KWA HIARI  mdada  avumilie MAHITAJI YA MUME WAKE kwa kutii MAFUNDISHO YA SOMI wake KWENYE UNYAGO kuhusu HIARI YA MWANAMKE ni MAAMUZI YA MUMEWE , na kwahiyo  haliitwi KUBAKA?




NIMEACHA !
HILI  ni WAZO tu MHESHIMIWA!
Jumatatu  NJEMA!


Au tu Jean-Claude Naimro na KASSAV wabadili tena kwa-Ave'w Doudou



Au tu JOCELYNE BEROARD wa KASSAV alete -Kay Manman




Au tu Jacob Desvarieux  na   KASSAV  wapoze pia zaidi kwa -Malad aw

Read more...

SHOGA njoo pembeni TUMSENGENYE MAMA MWENYE NYUMBA kwa kuwa HAUSIGELI ni kibonde , TUTAMSUTA uso kwa USO!:-(

 Katika dunia yenye  WENYE mabavu,...
.... kwa kawaida WABABE HUSENGENYWA kwa SIRI ili wasije kubwenga MTU bure  wakisutwa USO kwa USO,....

....na ASUTWAYE uso kwa uso ni ambaye inaaminika katika tukio  hana MABAVU na akileta za kuleta wakati anapandishiwa sketi a.k.a ANASUTWA hata  MBATA na KONZI anawezabwengwa  kama nyongeza juu ya MSUTO.:-(





Swali:

  • SI unakumbuka mara nyingi  HATA WEWE ufanikiwaye KUMSUTA uso kwa uso   KWA KAWAIDA ni YULE ambaye humuogopi VIZURI?

  • SI unakumbuka UMSENGENYAYE  na KUMTETA na MASHOGA ZAKO  hasa yule rafiki yako bado  ni ISHARA ya KUOGOPA KUZUNGUMZA NAYE UFIKIRIACHO  na ndio sababu INGAWA UNAMSENGENYA NA MASHOGA ZAKO WENGINE  bado KWA KUMUOGOPA una kahofu kakutotaka ajue ni wewe UMTETAYE  kisa  unajua ana mimba ya PADRE  na wala si ya HAUSIBOI kama walivyohisi   WAMBEYA wa nyumba ya jirani  waliovalia njuga ufala wa MUME wa rafikiyo kabla huja waongezea MSENGENYO kwa kuwa tonya ishu?

  • Si unakumbuka kuna WAPINZANI wengi wa Rais KIKWETE ambao ni mabingwa tu ya KUMSENGENYA na KUMTETA wakati hayupo lakini akitokea KIJIWENI kumsuta HAWAWEZI?



Kwa mtazamo huo usishangae mahusiano YA ASUTWAYE  na ASENGENYWAYE na KUTETWA yakiwa na MWALIKO uliokaa mkawai :

Njoo tumsute MLALAHOI,...
... kwa kuwa FISADI  inabitumsengenye tu na kumteta kwa siri kwa kuwa mpaka POLISI ni hawala zake.


Njoo tumsute, KUMTETA  na kumpiga makonzi MSENGE,...
... kwa kuwa NJEMBA RIJALI yenye wake wengi hata  kuisengenya tu kwa hilo KIMILA nyingi za KIAFRIKA bado haiwezekani.


Njoo  tumsengenye MAMA MWENYE NYUMBA na sio HAUSIGELI,...
..... si unajua  kumsuta MAMA MWENYE NYUMBA unaweza kuchochea kubwengwa na mpaka BABA MWENYE NYUMBA ingawa kwa kumsuta HAUSIGELI  yaweza kuonekana sawa TU  ingawa HAUSIGELI na wala sio MAMA MWENYE NYUMBA ndiye kiburudisho cha  Baba Watoto.




Swali:
  • Lakini si unakumbuka asengenywaye kama hastukii asengenywacho  MSENGENYAJI labda anapoteza tu MUDA?
  • Si ulishawahi kufikiria kuwa mara nyingi UMSUTAYE unaweza pia kumsengenya lakini si kila UMSENGENYAYE unaubavu wa kumsuta kwa kuwa kusuta mtu huhitaji umuangalie machoni?



Ndio,...
....labda hata katika  ya  VIONGOZI wako  MAFISADI kuna uwezekano yote uyasikiayo ni MISENGENYO na kuteta tu kwa wasio na MABAVU ,...
....kwa kuwa hakuna wa KUWASUTA uso kwa USO.:-(

CHA ajabu ni kwamba,...
....wengi waogopwao KUSUTWA uso kwa USO mabavu yao  MISINGI YAKE  inatokana na  kitu hicho hicho ``KUOGOPWA´´.:-(

Swali:
  • Unauhakika weye MTANZANIA  Rais Lowasa Mkapa akiwa mbele zako utaongelea Richmondi kama utetavyo kijiweni na washikaji?

Ni wazo tu DHAIFU HILI Mheshimiwa lakini pamoja na yote NI  WAZO!



Hebu FALLY IPUPA abadili kwa -Cadenas





au tu tulia na Awilo Longomba - Awa Imani - African Tonic katika- C'est pas Complique

Read more...

KUNA NYIMBO MAMILIONI za MAPENZI DUNIANI ,....

>> Sunday, February 21, 2010

....HASA ukilinganisha NA wingi wa NYIMBO ZILE za UMUHIMU wa jinsi ya KUBWIA UGORO!:-(


 [Tahadhari: Taralila hii ina neno KUNYA!:-(]



Naanza;....

Kwa kuwa kuna NYIMBO MILIONI zizungumziazo MAPENZI  katika kila wimbo mmoja uzungumziao KUNYA,....

... haina maana KUNYA hakuna sifa ziwezazo kutungiwa NYIMBO MILIONI katika kila wimbo mmoja UUSIKIAO wa MAPENZI.



Swali:
  • Si unakumbuka watu hufikiria KWENDA kunya mara nyingi maishani kuliko wafikiriavyo MAPENZI au wampendavyo MTU?
  • Unauhakika ingawa huwezi kulazimisha watu waimbe NYIMBO ZA KILIMO  wakulima wenyewe  UKIWAACHIA WACHAGUE unadhani watasikiliza ZAIDI nyimbo zizungumziazo KILIMO?


Ndio...
... usidanganyike na usikiacho kwa kuwa KINATAMKWA MARA NYINGI HADHARANI  na kutungiwa nyimbo NYINGI ,...
... NA UKAAMINI na  kufikiri HICHO ndicho chenye umuhimu zaidi kuliko vingine kwa WATU.:-(


Ndio,...
... usidanganyike na USIKIACHO kwa kuwa KINATAMKWA mara nyingi na kutungiwa NYIMBO nyingi,...
.... MPAKA UKAAMINI KWA KUSAHAU  kuwa usichokisikia mara nyingi kina sifa nyingi tu za kutungiwa NYIMBO MARA NYINGI kama hichohicho ukisikiacho MARA NYINGI ,na  watunzi HAOHAO watu.:-(



Swali;
  • Si unajua unaweza kuishi  bila kupendwa lakini huwezi kuishi bila KUNYA ingawa nyimbo za HAJA KUBWA huzisikii vyakutosha REDIONI?
  • Katika kuangalia  ni kwanini kuna aina nyingi za nyimbo zenye neno  HALELUYA kuliko zenye sentensi ``kudokoa MBOGA´´  , unafikiri wewe sio usababishaye hakuna nyimbo nyingi ziongeleazo umuhimu wa kunya vizuri kwa KUWA unasikiliza KIRAHISI  zaidi  nyimbo za ``Mpenzi nakupenda zaidi maungo yako´´?



NIMEMALIZA.:-(




NI WAZO TU hili MKUU na unaruhusiwa kulitukania mama!:-(
JUMAPILI NJEMA MHESHIMIWA!






Au ngojea Peter Tosh akumbushie-U can't BLAME the YOUTH


Peter Tosh adai - ARISE Blackman



King YELLOWMAN anyambulishe kwa kitu- Fools go to church on Sunday


Au EEK a MOUSE abadili kwa kulainisha MSHAWASHA  kwa stori ya -The man and the mouse

Read more...

KWA kuwa njia NZURI ya KUTUNZA AHADI hata kwa MPENZI ni kutoahidi!

AHADI ni faraja ya KITU kwa muda mfupi,....
.... kwa kuwa hata UKITIMIZA  ahadi  LEO hata bila KUDENGUA  ,.....
.... huo ni mwanzo TU  wa kumuandaa mtu ULIYEMTIMIZIA AHADI kukaa mkao wa kuhitaji  AHADI mpya UPYA .:-(






Swali:
  • AU?
  • Kwani ulichoahidiwa kikitimizwa UNADHANI HUO ndio mwisho wako wa KUTAKA  kuahidiwa TENA kidude?



AHADI mpya ni tamu KWELI,...
.....kwa kuwa inatia faraja UPYA!

AHADI hujenga tegemeo la kuwa ingawa sasa hivi huna KIDUDE ,....
... ni muda tu kidogo ambao ndio tatizo kwa kuwa utakacho utakipata  BAADA YA MUDA kwa kuwa UMEAHIDIWA tayari KIDUDE.



Swali:

  • AU?


NA AHADI  ni tamu tu wakati IMEAHIDIWA,.....
.... kwa kuwa utamu wa AHADI ni AHADI yenyewe ,....

...... hasa KWA SABABU  ulichoahidi UKIKITIMIZA HUGEUKA KWA KUTIMIZWA  na kuwa  sio  AHADI  TENA ,...
...na KWA HILO  ladha yake ni tofauti na AHADI ndio maana   bado kuna WADAIO walinogewa na KILICHOAHIDIWA zaidi ya AHADI .:-(


NDIO,...
.....uhakika wa ladha ya AHADI uko  zaidi  katika AHADI tu na sio KILICHOAHIDIWA ,.....
..... kwa kuwa KITU ulichoahidiwa  CHENYEWE ,....


.... kinaweza kuwa KINANUKA uvundo wa MKOJO  au tu KIMEZIDI SUKARI kuliko ulivyoahidiwa na uifikiriavyo AHADI.:-(


Swali:
  • Unafikiri AHADI ya BUSU a.k.a kula denda ina utamu kama kula mate  a.k.a KULA DENDA?

  • Si unakumbuka utamu wa KUHISI UNAPENDWA ni tofauti na kitendo cha KUPENDWA CHENYEWE ndio maana  uhisiye anakupenda wakati anakupa KIDUDE    ili akuaambukize GONO  na MDUDU  unaweza kumpenda zaidi kuliko AKUPENDAYE na kukunyima KIDUDE kwa kukujali  ili asikuambukize HERPES au tu FUNGUS ya kunako hata kabla hana GONO na MDUDU?

NDIO,....
.... KUAHIDI ni kujenga misingi ya KUVUNJA ahadi ,....
.....kwa kuwa KUAHIDI ni mimba ya MATEGEMEO ya ALIYEAHIDIWA ,....
.... na kitegemewacho KWA KUWA NI AHADI  ndicho  chenye  misingi ya MAUMIVU yatakayopewa MOTISHA au  kuvunjwa kwa AHADI hasa kwa kuwa wewe NI BINADAMU na hakuna BINADAMU mwenye uhakika na BAADAYE kiasi cha kuwa na uhakika asilimia MIA atatimiza AHADI.:-(


Na KWA BAHATI MBAYA  kama HUJAAHIDI ,...
.... MKUU kumbuka kuwa haina maana kuwa,...
... HAKUNA MTU aaminiye weye huna AHADI ya KUVUNJA kwake .:-(


Swali:

  • Si unajua kuna watu hata  MSICHANA AKIOLEWA TU ni kama vile KAWAAHIDI na  kahakikishia ukoo kuwa atapata mimba hivi karibuni kwa hiyo ni wakati wakumuangalia ujazo wa tumbo au tu katika mwendo anatikisaje matako , LA SIVYO itabidi  kumuuliza MUME wake kuwa nini kinaendelea mbona KIMWANA HAJISIKII KICHEFUCHEFU ,kitambi hakikui, hali udongo, habanwi haja ndogo mara kwa mara au tu hatema mate ovyo?

  • Si unajua PIA kumchekeachekea mtu ingawa ni kwa kuwa NI  mcheshi  TU kunaweza kumfanya MHESHIMIWA  ACHEKEWAYE afikiri akitongoza atapewa kwa kuwa kicheko chako kimetafsiriwa ni KUJIGONGA na unaahadi kukubali?

Tahadhari,...
....tafsiri za AHADI ziko nyingi kwa wengi na wala HIZO TAFSIRI hazitokani na  sentensi - `` NA AHIDI´´.:-(






Lakini ,....
.....KUMBUKA  kama hujaahidi ,...
... wewe HUJATOA AHADI.




NA kama HUJAAHIDI ,...
.... MKUU kunauwezekano MKUBWA weye huna AHADI ya KUVUNJA,...
..... ingawa TU usisahau UWEPO wako tu labda unawapa watu AHADI ambazo usipoangalia unaweza mpaka KUJILAUMU kwa kudhani ULIAHIDI MTU kitu.:-(



Swali:
  • Unabisha?

 Lakini  kama unajua tatizo  na SILIKA  za MTU ,....
.....TIMIZA usivyoahidi,....

...kwa kuwa hakuna kitu kitamu  KWA MTU  kama kupata kitatuacho TATIZO LAKE  ambacho hakutegemea na HAKUAHIDIWA!


Swali:
  • Si unajua jinsi gani utamu wa shilingi  ulivyo mtamu zaidi ya shilingi kama ukigawiwa shilingi uliyokuwa na shida nayo bila kutegemea hilo?

  • Ushawahi kusikilizia utamu wa kidude ulichopewa ghafla bila kutegemea wakati unahamu na kidude ulivyo tofauti?

NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA !

Hebu King Yellowman abadili kwa - Wrong Girl To Play With



Au tu King Yellowman alete tena-Reggae Calypso



Au tu KING YELLOWMAN amalizie na pambio-Gimme vagina

Read more...

WALI uliokula JANA kama tu PENZI la msichana kipenzi ALIYEKUACHA JANA!:-(

>> Friday, February 19, 2010

[Tahadhari: Taralila hii inatafakari iliyopinda kidogo maeneo!:-(]







Hiii ni STORI ya WALI  ulioula JANA, uulao LEO na utakaoula KESHO.

Wali kwa mlenda ULIOULA jana  LEO ni stori TU.

Wali uulao leo ndio nguvu yako LEO .:-(

Wali utakao kula kesho NI WAKUFIKIRIKA TU  kwa kuwa unaweza kukojolewa KWA BAHATI MBAYA  na MBUZI kabla huja-UGIDA kesho.:-(





Swali:
  • AU?



Hii ni STORI ya MSICHANA KIPENZI  wako wewe MSAGAJI  aliyekuacha JANA, umfikiriaye LEO na utakaye mfikiria KESHO.

Alivyokuacha jana ,...
.....mengi utakayoyazungumzia kuhusu yeye LEO  ni ZILIPENDWA TU  za kabla ya jana na JANA.:-(

Leo kama unahamu KAMA tu VIDUME wapweke wamkumbukao KIPENZI ZILIPENDWA ALIYE WAACHA SOLEMBA JANA ,...
....KWA BAHATI MBAYA leo kilichobaki ni KUJIGALAGAZA na  kumbukumbu tu za JANA ambazo zinaudhaifu  KIMPEKECHO katika kukuna  ya LEO.:-(

Kesho,  kama hutafuti tibabu   ndani ya HIYOHIYO  KESHO,...
... na  kuachilia mbali ya JANA,....
....kwa bahati mbaya  kama hutaendelea na MAISHA yako kivyako  aliyekuacha JANA bado hatibu  NG'O mshawasha wako hasa kwakuwa HAYUPO hiyo KESHO.:-(





Swali:
  • AU?



Samahani naanza upya hiii taralila...:-(





Nachojaribu kusema ni;....

-HATA kama WALI kwa ROJO  uliula JANA,....
......kama  una njaa leo, WALI MZURI JANA ni stori tu LEO.:-(


Na hata usimulieje  jinsi ulivyowahi kufaidi sana tokea ZILIPENDWA za kabla ya JANA,....
..... kwa mwenye njaa leo bado  UJANJA ni kula LEO.:-(


Na KAMA UNAWASHWA LEO,...
.....kumbuka stori za jana za ULIVYOKUNWA mara nyingi ni za JANA ,....
.... na ni kawaida kuwa  MATIBABU ya kipele leo huhitaji KUKUNA na mkunaji kipele LEO:-(.





Swali:
  • Unafikiri simulizi za nilivyowahi faidi bonge la UKOKO mwaka jana kama NA  njaa sasa hivi inanisaidia kitu MIMI sasa hivi katika kutibu njaa?
  • Unafikiri  simulizi  ZANGU  za nilivyofaidi bonge la UKOKO na UTANDU kwa mbali lililomwagiwa ROJO TAMU bila kusahau CHACHANDU na KACHUMBARI pembeni    mwaka juzi , ambazo hazinipozi  NJAA leo mie mwenye njaa leo hazikufunzi kitu  tu weye LEO ambaye huna njaa,  .... kuhusu ya KESHO?





LABDA niseme:

Tunza cha leo, ....
... JANA na ya jana YAMEPITA  na kwa leo  YA JANA kwa zaidi ni STORI tu LEO.:-(

.
NA ya KESHO,....
.....kama wewe ni BINADAMU ,....
....BASI hayo bado ni ya kufikirika TU.:-(





Swali:

  • AU?





Lakini pia,...
.... kumbuka tu kuwa PAMOJA na ALIYEKUACHA JANA  kukuacha  na hahusiki katika TATUZI lako la  hamu yako ya kusikia tamu LEO,....

..... usisahau lakini kuwa YA JANA BADO NI SHULE,....


...na staili ya ulivyong'ata kidude au SENENE  jana yaweza kuwa  FUNDISHO , na inafundisho katika staili yako ya kulamba KIDUDE  au kugida tu  KUMBIKUMBI kesho katika ukabilivyo vyenye uwiano na kilichobakia kuwa ni ZILIPENDWA MUKICHWA ,....

.....kwa kuwa KWA LEO hata ufanyeje bado KILIFANYIKA , kilionjwa au tu kilikuwa chako JANA hata ya dakika tano zilizopita na ndio IMETOKA HIYO!:-(




Kumbuka tu  pia ,....
.... pamoja na YOTE ,....
..... wali uliokula  jana huwa ndio uumpao MTU NGUVU ya kuweza kukata tonge LEO.:-(




NIMEACHA!

NI Tafakari tu  HII MHISHIMIWA Bwana MKUBWA jaribu hilo KUKUMBUKA !

IJUMAA na WIKIENDI NJEMA MKUU!




Hebu TPok JAZZ wajaribu kutusaidia kubadili hali ya hewa kijiweni kwa kitu- MAMOU




Au tu Kassav warudie tena -Zouk La Ce Sel Medicament Nou Ni

Read more...

Manufaa MAKUBWA ya RAIS au KIONGOZI MJINGA!

>> Thursday, February 18, 2010

 [Tahadhari: Tafakari imepinda na ni fupi a.k.a imekatiziwa denge!:-(]


Kama KIONGOZI  mjinga si mjinga vyakutosha kuharibu kabisa,......
...BASI labda ....
....KILA NCHI ili ijengwe na kuimarishwa MISINGI YAKE KIBUSARA labda inahitaji mara kwa mara kuongozwa na RAIS au Kiongozi MJINGA!


Kiongozi  MJINGA hata wa KAMATI   YA KIJIJI na SIO  NCHI  ionekanayo inahitaji KIONGOZI asiye MJINGA kama TANZANIA ana manufaa yake katika kuamusha MORI WA WANANCHI  katika kustukia NA KUHESHIMU  ni nini umuhimu wa VIONGOZI BORA wajuao wanafanyanini na si WAJINGA katika UONGOZI  WAO  ambao matunda yake ndio kielelezo bora cha ubora wao wa kutoongoza mambo KIJINGA..



Na Rais MJINGA ni msaada sana hasa akifuatiwa na RAIS MWENYE MIAKILI ya uongozi na bingwa wa  UTEKELEZAJI  kwa  BUSARA  ZAKE hasa katika kusaidia kukubalika kwake na SERA ZAKE baada ya WANAVIJIJI kuchoshwa na YALE YALE  ya danganya toto za KIJINGA..



Swali:

  • AU?
  • Unafikiri HITLER hakuwa msaada kwa KIONGOZI aliyemfuatia UJERUMANI baada ya wananchi kushtukia alichemsha?
  • Unafikiri UONGOZI wa CCM  kama UNAKOSEA sio msaada na  funzo kwa CHAMA chochote kingine kitakacho ingia MADARAKANI Tanzania baadaye?



Lakini.....

  • Hivi katika shughuli, KIONGOZI MJINGA na mtekelezaji swala na KIONGOZI MWENYE MIAKILI a.k.a SIO MJINGA  lakini PIA  si mtekelezaji unafikiri watoto watafanana na nani  kama uzalishaji watoto unahitaji MTEKELEZAJI wa shughuli?



NIMEACHA!

SAMAHANI ni wazo tu fupi hili MHESHIMIWA na ni ruksa kulipinga!

SIKU NJEMA!


Au badili kwa kupata stori ya ndoa na penzi kiduchu....



The LAST POETS warudie tena -Take Your Time



Au tu Fu-Schnickens na Shaquille O'Neal wabadili tena kwa -What's up DOC

Read more...

Chandarua CHENYE manufaa NA CHA BUSARA kwako katika KUZUIA MBU ni nyavu nzuri za KUVULIA SAMAKI kwa MWENZIO!:-(

Wewe katika MAISHA sio WAO,...
..... kitu hicho hicho kikabiliwacho na swala la kuwa MIMI sio WEWE na  nipendacho MIMI ni kutokana na nikabilianavyo mimi KITU KISABABISHACHO  kwangu  kupenda upendacho wewe yawezekano inahitaji NIJIFUNZE.:-(

Na kujifunza inahitaji SABABU,.....
... na tatizo linarudi pale pale kuwa SABABU ZAKO zilizokufunza  KUTOPENDA hata SINDIMBA na ujanja kwako ni BONGO FLEVA labda yabidi nikuelewe kwanini katika NGOMA nzito zote TANZANIA  wewe ikudakayo DAR es SALAAM kirahisi sio MDUNDIKO na ni KWASAKWASA ya kutoka kwa BABA MOBUTU ambaye ndio juzijuzi WANASIASA wetu TANZANIA wanastukia KUMUIGA katika UFISADI.


Swali:

  • AU?
 Tukiachana na hilo, kumbuka tu .....

Kwa aaminiye katika KUCHEZA peku  hata uumpe KONDOMU za BURE,....
......kama staili ya UMUHIMU uuonao hauangalii kwa jicho na ujuzi wa kunogewa UTAMU  kama wewe uchezaye MAMBO KWA SOKSI,....
.....hata kama ATAKUFA atakufa wakati  anachezea kinjegele  PEKU kwa raha zake wakati UJUMBE wa UDAICHO NI MUHIMU alikusikiliza..

Swali:
  • Kwani unafikiri  wangapi waambukizwapo UKIMWI walikuwa na KONDOMU na hawakuamua kuitumia tu?

Na NDIO,...
.....chenye manufaa kwako hata ukigawe bure kama wagawavyo VYANDARUA kuzuia MBU na MALARIA ,...


.... CHANDARUA kinaweza geuzwa TU  kuwa ni nyavu za kuvulia SAMAKI ingawa ulihubiri na kupigiwa makofi  ukiongelea  CHA MUHIMU KWAKO ambacho  NI KUZUIA MALARIA wakati CHA MUHIMU KWA UWALENGAO NA MSAADA ni nyavu kama za CHANDARUA ambazo ni muhimu zaidi kwao KWA kuvulia SAMAKI.:-(


Swali:
  • Unafikiri  ni kwanini kuna WANAWAKE wateteao umuhimu wa KUKEKETWA wakati wanogewao maswala kwa kuwa na kinjegere wanasimulia tamu za kutokeketwa?


Ndio,...
...mwisho wa siku  LABDA ,...

... cha muhimu kwako  na ambacho unaamini kina umuhimu kwa wengine bado ni CHENYE manufaa ZAIDI  kwako kwa kuwa UMUHIMU WAKE una  MTAZAMO WAKO.:-(


Na kama chako UAMINICHO kinamanufaa kwa wengine ,....
..... ukitaka WENGINE waambukizwe kunogewa kwako  katika hicho,...
... labda kabla hujachukua HATUA YOYOTE ,....
...FIKIRIA wanogewavyo wengine kabla ya kuwapanulia hicho wengine WATU na  kufaidisha NZI  tu wakati uliotaka waonje ni WATU,...
...na wala sio hao INZI  wenye kunogewa na upanuacho vingine.:-(




Swali:

  • Si unajua kuna uwezekano kabisa UFIKIRIACHO NI MSAADA KWA WENGINE ni kwa kuwa tu kwa kufikiria hivyo hicho ni msaada kwako?



NI TAFAKARI tu HII Mheshimiwa! 

Na MSOME,...
.....Kadinali Chacha o'Wambura NG'WANAMBITI  aliyeiotesha TAFAKURI HII  kwa kuzungumzia jinsi VYANDARUA VIGEUZWAVYO    sehemu za kupoozea maisha magumu KUKU HAPA









Au HEBU Mr.CHEEKS na STEPHEN MARLEY wabadili kabisa hali ya hewa kijiweni kwa kitu  - Guiltiness


Mr CHEEKS alete-Double B Flow



Au tu Mr.Cheeks amalizie kwa - Lights, Camera, Action

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP