Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ombi la msaada kwa Mgonjwa NURDIN LULANGA !

>> Thursday, February 04, 2010

Habari,

Naomba umtoe huyu kijana katika blog yao ili apate msaada kwa watanzania wenzake , anasumbuliwa na ugonjwa wa ajabu, mguu unavimba kila siku na hospital wamemshauri aende akatibiwe nje ya nchi na familia yake hainauwezo wa kumpeleka huyu kijana tunaomba MSAADA kwa Watanzania woote wenye moyo na uwezo wakumsaidia huyu kijana















Hiii ni historia fupi ya huyu kijana:

ANAITWA NURDIN LULANGA AMEZALIWA MWAKA 1990 DAR ES SALAAM TANZANIA, HIVYO ANA MIAKA 19.

HISTORIA YA UGONJWA HUU ILIANZA WAKATI KIJANA HUYU AKIWA DARASA LA 6 (SITA NA ILIKUWA NI MAUMIVU YA KAWAIDA TU YA MGUU JUU YA GOTI NA INAFIKIA MDA MWINGINE ANASHINDWA HATA KUTEMBEA.



MAUMIVU HAYO YALIKUWA YANAENDELEA NA KUACHA NA BAADA YA MDA UKAANZA KUVIMBA TARATIBU NA BAADA YA KWENDA KUCHUKUA VIPIMO VYA X-RAY IKAONEKANA KAMA MFUPA ULIKUWA UNALIKA TARATIBU.

BAADA YA KUFIKA FORM SIX (2009 MAY) TERM YA KWANZA MGUU ULIVIMBA GHAFLA KWA KASI YA AJABU NA NDIO IMESABABUSHA ASHINDWE KABISA KUTEMBEA HUU SASA NI MWENZI WA 9 YUKO TU NYUMBANI.

AMESHAPIMA FULL BLOOD PICTURE,ABSOMEN, BONE SCAN (OCEAN ROAD) N.K LAKINI HAKUNA KIPIMO KILICHOONYESHA DIRECT ANAUMWA UGONJWA GANI MADAKTARI WAMETUSHAURI TUMPELEKE NJEE YA NCHI NA FAMILIA HAINA UWEZO HUO .


JAMANI NDUNGU WATANZANIA TUNAOMBA MSAADA WENU ILI TUMSAIDIE HUYU KIJANA KATIKA UGONJWA HUU!

NATANGULIZA SHUKURANI ZANGU ZA DHATI!













KWA YEYOTE ATAKAE GUSWA NA HILI TATIZO NAMBA ZA SIMU NI:

0712 677 977 -NURDIN (MGONJWA MWENYEWE)
0715 247 460 -MAMA WA NURDIN
0754 247 460
0784 753 312 NA
0773 464 833 KAONEKA (MJOMBA WA MGONJWA)



Asanteni,
-Shamsa Kaoneka



4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 10:34 am  

MASIKIN POLE SANA KIJANA MUNGU ATAKUSAIDIA ILA MIE NASHANGAA SANA HAYA MASHIRIKA MAKUBWA KAMA NMB HUYO SHYROSE BANJI MWAMVITA MAKAMBA TIGO ZAIN HAWENGINE HIVI NDIO VITU VYA KUSAIDIA JAMANI TUMSAIDIE HUYU KIJA MIE NTATOA 100 LAKI MOJA NITUME KUPITIA KWA NANI NAOMBA ACCOUNT NAMBA

Mija Shija Sayi 12:12 am  

Asante kwa tangazo tutajitahidi kadiri ya uwezo wetu.

Lakini kwa nini serikali haina fungu la kusaidia wananchi wake katika mambo ya dharura kama haya?

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! 11:04 am  

Anony na Da Mija: hivo si vipengele vya serikali wala hayo makampuni :-(

Mija Shija Sayi 12:13 pm  

Chacha kivipi si kipengele cha serikali? Naomba utete hoja yako..

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP