Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUNA NYIMBO MAMILIONI za MAPENZI DUNIANI ,....

>> Sunday, February 21, 2010

....HASA ukilinganisha NA wingi wa NYIMBO ZILE za UMUHIMU wa jinsi ya KUBWIA UGORO!:-(


 [Tahadhari: Taralila hii ina neno KUNYA!:-(]



Naanza;....

Kwa kuwa kuna NYIMBO MILIONI zizungumziazo MAPENZI  katika kila wimbo mmoja uzungumziao KUNYA,....

... haina maana KUNYA hakuna sifa ziwezazo kutungiwa NYIMBO MILIONI katika kila wimbo mmoja UUSIKIAO wa MAPENZI.



Swali:
  • Si unakumbuka watu hufikiria KWENDA kunya mara nyingi maishani kuliko wafikiriavyo MAPENZI au wampendavyo MTU?
  • Unauhakika ingawa huwezi kulazimisha watu waimbe NYIMBO ZA KILIMO  wakulima wenyewe  UKIWAACHIA WACHAGUE unadhani watasikiliza ZAIDI nyimbo zizungumziazo KILIMO?


Ndio...
... usidanganyike na usikiacho kwa kuwa KINATAMKWA MARA NYINGI HADHARANI  na kutungiwa nyimbo NYINGI ,...
... NA UKAAMINI na  kufikiri HICHO ndicho chenye umuhimu zaidi kuliko vingine kwa WATU.:-(


Ndio,...
... usidanganyike na USIKIACHO kwa kuwa KINATAMKWA mara nyingi na kutungiwa NYIMBO nyingi,...
.... MPAKA UKAAMINI KWA KUSAHAU  kuwa usichokisikia mara nyingi kina sifa nyingi tu za kutungiwa NYIMBO MARA NYINGI kama hichohicho ukisikiacho MARA NYINGI ,na  watunzi HAOHAO watu.:-(



Swali;
  • Si unajua unaweza kuishi  bila kupendwa lakini huwezi kuishi bila KUNYA ingawa nyimbo za HAJA KUBWA huzisikii vyakutosha REDIONI?
  • Katika kuangalia  ni kwanini kuna aina nyingi za nyimbo zenye neno  HALELUYA kuliko zenye sentensi ``kudokoa MBOGA´´  , unafikiri wewe sio usababishaye hakuna nyimbo nyingi ziongeleazo umuhimu wa kunya vizuri kwa KUWA unasikiliza KIRAHISI  zaidi  nyimbo za ``Mpenzi nakupenda zaidi maungo yako´´?



NIMEMALIZA.:-(




NI WAZO TU hili MKUU na unaruhusiwa kulitukania mama!:-(
JUMAPILI NJEMA MHESHIMIWA!






Au ngojea Peter Tosh akumbushie-U can't BLAME the YOUTH


Peter Tosh adai - ARISE Blackman



King YELLOWMAN anyambulishe kwa kitu- Fools go to church on Sunday


Au EEK a MOUSE abadili kwa kulainisha MSHAWASHA  kwa stori ya -The man and the mouse

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 4:16 pm  

Dominika njema kwako pia Mt.Simon.

Simon Kitururu 5:11 pm  

Asante Dada Yasinta!

Fadhy Mtanga 5:18 pm  

Mtakatifu Simon, kila siku unanifanya kufikiria sana hizi taralila zako. Ila nashukuru u always make my days!
Pamoja sana.

Simon Kitururu 5:29 pm  

@Askofu Fadhy: Nami nashukuru tena sana kwa wewe kutochoka kunitembelea hapa Mkuu!

Tuko Pamoja Sana tu Mkuu!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP