Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Matatizo YALIYOJITOKEZA baada ya WATANZANIA kufunzwa kufuata GREGORIAN KALENDA ambayo inadai leo ni MWISHO WA MWAKA!:-(

>> Thursday, December 31, 2009

GHAFLA Mzee akumbukaye kuwa alizaliwa wakati KIBAHA kulikuwa na SENENE wengi,...

....huanza kuonekana HAJAELIMIKA kwa kuwa hajui tarehe aliyo zaliwa.:-(


GHAFLA Kigoli mwenye bonge la TITI kuna ushahidi ni MTOTO,..
...kwa kuwa kuna vyeti vidaivyo ana miaka kumi na NNE tu na hafai KUOA.:-(



GHAFLA Mheshimiwa MTANZANIA anajisikia MZEE ,...

.. kwa kuwa kastukia kuwa eti miaka ya WASTANI wa MTANZANIA KUFA,...

... DUME ni miaka 51 na JIKE la KITANZANIA ni - miaka 54


Ghafla KUBWA JINGA lenye mambo ya KITOTO,...
... linakabiliwa na KUHESHIMIWA kama KUBWA kwa kuwa kuna uhakika lina miaka SABINI.:-(




Swali:

  • Unafikiri kwanini TANZANIA haifuati KALENDA ya KIISLAMU wakati walioleta UISLAMU walikuja na KALENDA ya KIISLAMU?

  • Unafikiri ni kwanini ETHIOPIA ni nchi pekee karibu na TANZANIA yenye KALENDA yake yenyewe?

  • Unafikiri ni kwanini BC na AD a.k.a "Anno Domini" na "Before Christ" havijulikani na wengi kuwa ni "CE" na "BCE" a.k. a "Common Era" na "Before Common Era" ?

  • Unazijua KALENDA NGAPI zitumikazo sasa hivi duniani ambazo leo sio MWISHO wa MWAKA?






Photobucket

NAKATIZA HILI wazo NYOKO hapa!

NAKUTAKIA HERI katika MWAKA MPYA Mheshimiwa!

ASANTE SANA kwa KUNITEMBELEA HAPA KIJIWENI MKUU!




Moja kwa moja tubadili kwa kumuachia AFANDE SELE arudishe- DARUBINI KALI



Au tu Mr EBO acheki uzoefu wake katika kukujulisha wewe- MBADO

Read more...

Unafikiri ni VICHAA wangapi WAMEKUPANDISHA JAZBA , au tu WANAONUKA NYETI waliosababisha ufikiri wanajua KUJISWAFI NYETI mwaka 2009 MTANDAONI?

Mtandao KIBOKO!

Na MTANDAO ulivyo kiboko,...

...usipoangalia unaweza hata kudhania KITUMBUA ni KEKI au kummendea DADA YAKO mtandaoni halafu siri ikafichuka kwenye familia yenu kuwa ni kweli WEYE msagaji.:-(




Siriasli kwa KISWANGLISH:

  • Unafikiri nini wakati unapandishwa JAZBA na ANONYMOUS mtandaoni?
  • Huwa unafikiria nini wakati unapandishwa nyege, - SAMAHANI- wakati unapandishwa JAZBA na USIOWAJUA mtandaoni?

  • Si unakumbuka LABDA usiyemjua MTANDAONI NI KICHAA na ukigombana na kichaa WAHENGA WANADAI ni vigumu kwa wengine kukutofautisha weye na aliye KICHAA?

  • Unauhakika wewe sio kichaa kwa wengine kisa kuna kitu chako unogewacho nacho na kukiona ni MUHIMU SANA PAMOJA NA MIAKILI YAKO kama vile tu VIATU au CHUPI GUCCI wakati unajua kuna WALIMWENGU wanakufa NJAA , hawakielewi?





NI WAZO tu hili MHESHIMIWA Kalumekenge!:-(




Hebu Miriam Makeba aingie DEEP kwa - When I've PASSED on




Marvin Gaye akumbushie kuwa dawa ya michecheto na kuwashwa kwingine ni- Sexual Healing




Tukiachana na hilo ngojea tukumbushane:

Read more...

PETE YA HARUSI, msalaba KIFUANI /jengoni, PICHA YA Rais NYERERE ukutani,.... vyote kialama vikifanana na HERENI imtambulishayo MSENGE!:-(

>> Wednesday, December 30, 2009


[Tahadhari MHESHIMIWA: Tararila hii ina ZIGZAG katika Mtiririko ,Lugha iliyotumika, na Mifano pia. Kwa hiyo kama weye ni mtoto , Mavi kwako ni rahisi kuyaita Kinyesi na Matako unadhani ni ustaarabu kuyaita makalio- unaweza usielewe naongelea nini au kwa kifupi hii tararila haikufai.:-(]







Kwa kuwa YASIYOTUHUSU,...


...kuna wanaopenda tujue,...



.....YAWAHUSUVYO.....


... binadamu hutumia mpaka ALAMA katika vielelezo ili tu YASIYOTUHUSU nayo TUYAJUE.:-(


MATOKEO yake,....
.. mpaka PENDO BINAFSI LA watu wawili,......

..MME na MKE hulazimika katika jamii fulani fulani kama YA WATANZANIA kulivalia PETE ili kutuhakikishia siye KISICHOTUHUSU ,....


....kuwa wako katika NDOA na MPENZI wakati SIRI YAO YA MOYONI kuhusu HIYO NDOA ambayo ndio JAMBO LA muhimu KATIKA NDOA,..

... inapiga kelele;..

  • HII sio NDOA

  • Napenda pesa zako na sikupendi wewe.

  • Wazazi wasingenilazimisha usingenipata, na jamii isingetegemea nipate mimba NIKIOLEWA nisingekupa kidude ng'o labda unileweshe.

  • Niko nawe kwa kuwa nilipata mimba kwa bahati mbaya na nikakosa wakumsakizia mimba kabla WEWE hujajiingiza kichwakichwa katika zile TAIMINGI kwa ung'eng'e ziitwazo ;``just at the right time´´.

  • Wewe Msichana INGAWA NIMEKUOA ni kweli unasura kama SAFARI BUTI iliyochakaa nisiyoipenda na inukayo uvundo . Lakini BABA yako tajiri kama MENGI na nazimia sana hilo MPENZI ingawa ASANTE NYINGI ZIENDE katika jinsi ulivyoniachia kazi ya kuchagua mahausigeli hapa nyumbani kitu ambacho kimenisaidia kuajiri mapoozeo yanisaidiayo kujisikia KURUDI nyumbani na hata kulala chumba kimoja na wewe. Na kuhusu sekretari wangu ofisini asaidiavyo kunifanya nikuvumiliea kwa kuwa hujamstukia BADO ngojea hiyo iwe siri yangu kwa sasa.


  • NK. :-(


Swali:

  • Si unajua pamoja na PETE KUVALIWA bado kuna wapendao na kuvutiwa na WAUME au WAKE ZA WATU na wakikuona na PETE ndio wanajua wamempata wa KUMTONGOZA?


  • Kwani unafikiri kwa mpenda MUME au MKE wa mtu ANAKWAZIKA NA PETE mpaka ahitaji PETE IVULIWE saa na wakati wa kufanikisha UASHERATI a.ka KUZINI a.k.a KUCHOKONOA DAFU ikifika?



-Tuendelee...-




KWA kuwa YASIYOTUHUSU;....

...kuna wanaopenda tujue,....

... YAWAHUSUVYO,....




MATOKEO YAKE,....

.... kuna WAKRISTO wafikiao kuvaa MSALABA ili kuwahakikishia yasiyowahusu UISLAMU au tu UBUDHA haupandi kwao,...

....KITU ambacho LABDA wangejisikiliza MOYONI wasingehitaji kuhakikishia WENGINE ukristo wao SASA HIVI kwa kuwa WANGESTUKIA kuwa hata UKRISTO wenyewe MOYONI MWAO hawauelewi na bado kiimani HAUJAPANDA VIZURI:-(



Swali:

  • Unauhakika wahubiri wahubiriao wengine INJILI wangetumia busara wasingestukia wao ndio wahitajio zaidi injili ya Mheshimiwa YESU?

  • Unafikiri alama ya MSALABA kwa wengi sio PAMBO tu kama KINYAGO cha Kigoli mcheza SINDIMBA cha Mmakonde?

  • Unafikiri vyako vya MOYONI ni DHAIFU KIASI GANI mpaka wajanja kama akina PAPA WA KANISA LA KIKATOLIKI ikabidi wavalishwe bomba la GAUNI na KOFIA ukubwa KIKAPU , Mchungaji wa KILOKOLE Morogoro akalazimika kuhubiri kwa sauti ya Kizungu, SHEKHE wa KIBENA akalazimika kuwa na lafudhi ya Kiarabu katika kushuka neno,.... ILI tu kudaka utulivuwako ULAINIKE wakati unapewa NENO la MOLA?


  • Unafikiri vyako vya MOYONI ni DHAIFU KIASI GANI mpaka ukitaka kujaribu TUVIJUE WEWE MWENYEWE HAUTOSHI mpaka inabidi utafute msaada wa ALAMA FULANI FULANI kama vile MSALABA au tu HERENI SIKIONI ili tu tujue PENDO lako ni la KISENGE?



-Tuendelee,...-



KWa kuwa YASIYOTUHUSU,....

... kuna wanaopenda tujue,....

.... YAWAHUSUVYO,...



MATOKEO yake,...

.... ndani ya TANZANIA kuna MABEPARI na MAFISADI kibao ambao katika kuta za ofisi au nyumba zao kuna PICHA YA Rais NYERERE,...


... kitu ambacho LABDA HAKITUHUSU ingawa hakiachi kushangaza hasa ukifikiria imekuwaje MHASISI wa SIASA YA UJAMAA na KUJITEGEMEA asiyehusudu UBEPARI anafanya nini katika ukuta wa FISADI BEPARI ambaye anaamini UBEPARI kama tu UBIKIRA wa BIKIRA MARIA ni kitu kinachoeleweka kirahisi na ni KITUKUFU!:-(




Swali:
  • Unakumbuka lakini Siasa ya UJAMAA na KUJITEGEMEA kuna iliyowafanya wawe WATEGEMEZI na inazidi kufa leo hii chini ya walewale waliokuwa WANADAI wanaamini hiyo SIASA na pia waliitikia sana ZIDUMU FIKIRA za MWENYEKITI ambaye moja ya fikira zake ilikuwa ni AZIMIO LA ARUSHA na SIASA ya KUJITEGEMEA?

  • Unauhakika kwa MAFISADI MABEPARI, picha ya Rais Nyerere hawaitumii kama ALAMA ya;`` UJAMAA ZIII na UJANJA NI KULIA OFISINI OYEEE!´´?

  • Unauhakika kama wewe MTANZANIA una picha ya RAIS NYERERE ukutani mwako, MZUKA /Mzimu wa MWALIMU NYERERE ukipitia NYUMBANI KWAKO hausikii KICHEFUCHEFU?




NDIO,...

....tukiachana na VINDUMBWENDUBWE kibao katika HOJA ZANGU kibao HAPA ZENYE KIBIONGO,...



.....labda bado kuna UKWELI kuwa,...

... ALAMA KIBAO,...

... kama tu ilivyo MISALABA kwenye makaburi ya WAKRISTO kwa wengi,...
.... ni MAPAMBO TU.:-(






NDIO,...


....ALAMA,...


....kama tu madoadoa usoni kwa KISURA,....


.....inaweza tu kumaanisha KISURA aliwahi kuwa na VIPELE VYA UCHAFU na wala ALAMA ZA madoa HAYO hazimaanishi kuwa KISURA aliwahi kuugua TETEKUWANGA utotoni ,...



....kama tu ile alama ufikiriayo ni ya NDUI ukweli wenyewe ni KWAMBA hapo alikuwa na BONGE LA JIPU.:-(





Swali zaidi kiduchu:
  • Si unakumbuka KUTONIELEWA hasa kama tu kuna kitu umefikirishwa kwa kunisoma katika tararila hii RUKSA?




NIMEACHA WAZO Mheshimiwa na KUMBUKA hili ni wazo tu MKUU wa KITENGO!:-(


Hebu Michael Jackson kama Spike Lee alivyo Direct atupe- This IS IT




Sijui kwanini bado -JULIE naye ananitekenya kichwani kama tu adaivyo Oliver N'goma



Read more...

Ujumbe kutoka kwa BABA GASTON kwa WATANZANIA WOTE Waheshimiwa NA wasio Waheshimiwa WALIOKO UGHAIBUNI!

[Tahadhari: Kama uko Tanzania au uko ughaibuni na unajisikia uko nyumbani huko UJUMBE HUU HAUKUHUSU:-(]


Kabla BABA GASTON hajaleta ujumbe, .....
.....ngojea nilalamike nilivyowahi kulalamika kipindi fulani..









Ujumbe wenyewe kutoka kwa BABA GASTON kwa akina Simon Kitururu ni huu...






-RUDI NYUMBANI AFRICA-

Read more...

LADHA!

>> Tuesday, December 29, 2009



Kuwa na LADHA,...
... ni uwezo wa kustukia kitu BORA, kwa kuwa unajua ni nini UBORA.


Lakini LADHA,....
....ni UTAMU hata wa ile CHACHU isiyo BORA.:-(


Ladha,...
... ndio IUAYO watu KWA HIARI kwa kuwa tu wamejizoesha ladha ,...
....ya UTAMU wa visivyo BORA.:-(


Kizuri na kibaya katika LADHA,....
... kwa bahati mbaya HUFUNDISHIKA kama tu afundishikavyo MTU kujua ni viatu gani BORA.


CHAKUSIKITISHA kuhusu LADHA,...
...ni kwamba mengi ambayo WATU huangaikia kufudhu KATIKA ujuaji wa LADHA ,....
.... ili waipende LADHA,...

.... mara karibu zote kwao hayo si BORA.:-(








Swali:

  • Unafikiri una LADHA?

  • Si unajua adhaniaye ladha ya CHAI YA SUKARI ni tamu anafundishika kupenda ladha ya CHAI BILA SUKARI hasa akistukia chai isiyo na sukari ndio BORA?

  • SI unajua apendaye LADHA ya ASALI anafundishika kupenda ladha ya BIA?


  • Si unajua MUME au MKE apendaye ladha ya jamii kuhusu NDOA aliye kwenye NDOA anafundishika kupenda ladha ya MAPENZI YA KULIPIA ya MALAYA?


NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA na Usikonde!:-(



Hebu katika kubadili somo tusikilize Chef akiulizwa swali -Chef what's a prostitute?




Au tu TONY TUFF alete ustaarabu kijiweni kwa kitu- Mix ME Down

Read more...

Ujifunzacho kirahisi CHOONI!

>> Monday, December 28, 2009

CHOONI ni mahali pazuri PA kujifunzia kirahisi kuwa MAISHANI kuna vya lazima VINUKAVYO,....

..... na maishani HARUFU ya vitu VILEVILE vyenye jina LILELILE hutofautiana DIGIRII za MNUKO hata kama chanzo cha harufu kina jina LILELILE .:-(





SWALI:
  • Au?

Na ukitoka chooni waweza kujikuta umestukia kuwa SI VIBAYA mara kwa mara kukatiza SHUGHULI nyingine muhimu kama vile kazi kwa ajili ya shughuli nyingine NDOGO NDOGO za muhimu kama vile KWENDA MSALANI kwa ajili ya KUTATUA haja ndogo kwa manufaa yako au tu ya MWILI WAKO .



Na ukitoka CHOONI ,....
.....kwa mafanikio ya chooni hasa kama ulibanwa sana KABLA YA KWENDA chooni, waweza stukia kirahisi na kuelewa KIRAHISI nadharia nzima ya ``BAADA ya KAZI NZITO kuna FARAJA´´, hasa kama kilichokupeleka chooni kilihitaji juhudi na kilikuwa na uzito angalau katika JINSI ulivyokuwa unajisikia kabla ya kukifanikisha huko msalani,..
.... NA kwa MAFANIKIO YAKO hayo CHOONI wajisikia FARAJA na ahueni katika HALI YAKO.



Swali:

  • AU?
  • SI unajua ingawa matunda ya shughuli za chooni hudumbukizwa chooni hudhani moja ya funzo la hilo ni kwamba si lazima matunda ya kazi yako yaliwe au watu wengine wayaone?
  • Mheshimiwa kama ulifanikiwa LEO kwenda CHOONI ,umejifunza nini leo huko chooni?
  • Si unajua mahali popote kwa mjanja ni SHULE YA MAISHA kama unania ya kujifunza?






NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA na NIMELIACHA!


Hebu basi mshairi LINTON KWESI JOHNSON arudie kishairi kuzungumzia- New world ORDER


Mshairi Linton Kwesi Johnson arudie pia shairi-Sonny 's Letter


Au tu Linton Kwesi amwage na shairi-Want FI go Rave?

Read more...

VIKOROKOCHO katika STORI za UKUMBUKACHO!

Jinsi ukikumbukavyo UKUMBUKACHO hata kile ambacho unafikiria ni kwa kuwa NI KWA UTOFAUTI WAKE ndio maana UNAKIKUMBUKA ,.....

....kwa kawaida UKIKUMBUKACHO utakikumbuka kinamna au kivitu ambavyo UBONGO wako umezoea kuvistukia katika vitu na ndio maana kwa kawaida WEWE utastukia HIVYO kwa staili hiyo , kitu ambacho kitatofautisha UKUMBUKAVYO wewe kitu na WENGINE ambao kwa pamoja MLISHUHUDIA kwa pamoja KITU.


Swali:

  • Si unajua WASHUHUDIAO KITU HICHO KIMOJA wakiongezeka utapata STORI tofautitofauti za KITU au tukio hilohilo MOJA kutokana hasa na staili tofauti za watu za kukumbuka kitu?



Kwa kifupi:

JINSI usimuliavyo UKUMBUKACHO kwa kawaida HUJAA jinsi UTAKAVYO na kistaili tu ya ULIVYOZOEA tu kukumbuka VITU na wala sio KIUKWELI wa jinsi kilivyotokea KITU.:-(



KUNA jinsi tu ULIVYOJIZOESHA HATA BILA KUJUA kukumbuka jinsi ya UKUMBUKAVYO KITU kisababishacho kama ni MSICHANA kwa ko WEWE kirahisi unaweza kumkumbuka kirahisi kwa saizi ya TITI wakati Mwenzio MMOJA anaweza kumkumbuka kwa alivyokuwa na UPELE USONI kama ZEGE na MWENZAKO MWINGINE kirahisi awezavyo kumkumbuka kirahisi MSICHANA HUYOHUYO kwa jinsi alivyo kuwa na BONGE LA TAKO.:-(



Swali:

  • Unauhakika kilichotokea ulichowahi kukishuhudia kikitokea ndivyo jinsi UKIKUMBUKAVYO?


  • UNAFIKIRI ni kwanini KUNDI la watu lishuhudialo KITU KWA PAMOJA kwa kawaida huwa na STORI tofautitofauti za hicho kitu?

  • Kwani wewe unafikiri huwa unakumbukaje baadhi tu ya vitu?


NI WAZO TU HILI Mkuu na WALA usikonde!:-(


Na hebu Oliver N'goma arudishe -Nge


Au tu Oliver N'goma na Bhonos warudishe tena -Alphonsine



Au tu Oliver N'goma aachie na -Bané



Read more...

Msaada TUTANI!

>> Sunday, December 27, 2009

Read more...

Kwa kuwa BINADAMU hukosea MPAKA kwenda HAJA KUBWA!::-(

[Tahadhari: Lugha ya tararila inaweza kumkwaza Mheshimiwa ATAFSIRIYE USTAARABU kinamna FULANI, kwa kuwa haijavalishwa chupi!:-(]





Kuna siku MHESHIMIWA achambaye,....

.... hustukia ANAHITAJI kuchamba KIREFU au tu kwa JUHUDI zaidi katika KUJISWAFI kwa kuwa Mheshimiwa pamoja na uzoefu WOTE siku hiyo kwa bahati mbaya hajapatia kunya VIZURI.:-(



Na kwa kuwa BINADAMU achambaye,...

... kuna siku hukosea mpaka KUNYA [ au kwa lugha ya kistaarabu:``hukosea kuachanisha mwili na kinyesi´´],....

.... jiulize ni nini basi BINADAMU mahiri asichoweza kukikosea ambacho anajulikana kwa kukifanya VIZURI. :-(






Swali:

  • Si unajua hata mzoefu wa kukata tonge la UGALI kuna siku katika staili ya kula hudondosha tonge?
  • Huwa unajipa ruksa kujisamee ukikosea kwa kuwa unajua kuwa taka usitake weye kama binadamu kila siku unakosea?
  • Si unajua kila siku ya Mungu kuna kitu unakosea ingawa ni baadhi ya mambo ambayo unayashupalia ukistukia UMEYAKOSEA?

  • Si unajua ni baadhi tu ya mambo ndio uchaguayo kuyastukia au tu tuseme ndio uyastukiayo TU kuwa umeyakosea wakati kila siku ni mambo kibao unayakosea?

  • SI unajua kuna wakati unapatia zaidi KUNYA kuliko WAKATI MWINGINE ingawa wakati uhitajio TISHU a.k.a MAKOKONEO zaidi au tu MAJI zaidi katika kufanikisha KUCHAMBA hutafsiri kuwa ni kwa sababu tu ulikosea KUNYA?


NDIO,...
..... unaweza KUNIBISHIA katika yote niliyosema lakini amini KILA siku ni baadhi tu ya mambo uyastukiayo UKIKOSEA wakati kila siku ni mambo kibao UNAYAKOSEA.:-(



Na pia kama tu swala la - nini ustukiacho ukikosea lilivyo kama tu swala ZIMA la nini kwa kawaida HULIKUMBUKA KILA SIKU- nikiwa na maana : ni mambo machache sana MTU KIBINADAMU huwa unayakumbuka kila siku ingawa katika siku ni mambo kibao huwa unayashuhudia, kuyafanya au kufanyiwa.:-(



Nimeacha NA KUMBUKA ni wazo TU hili MKUU na nia na madhumuni sio KUKUKWAZA Mheshimiwa!:-(


Namuachia Isaac HAYES arudishe ustaarabu kwa- I stand ACCUSED


Au tu Isaac HAYES amalize kwa kitu-SHAFT

Read more...

Namtafuta Dada Renatha BENEDICTO!




H
eshima kwako NDUGU.


Namtafuta Dada Mdogo RENATHA BENEDICTO ambaye tumepoteana kwa takriban miaka 7 sasa.



Renatha alikuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kibasila jijini Dar kati ya mwaka 1998 - 2001 na baada ya hapo alienda Songea TTC kujiunga na masomo ya ualimu.



Pia alikuwa kati ya wahanga wa ajali mbaya ya Tawfiq iliyotokea tarehe kama ya leo mwaka 1999 ambapo alikuwa msaada mkubwa saana kuokoa maisha yangu.

Maelezo kamili yako:


http://changamotoyetu.blogspot.com/2009/04/namtafuta-renatha-benedicto.html




Niliwasiliana naye kwa miaka miwili iliyofuata mpaka alipoenda chuoni Songea nami nikaondoka nchini mwaka uliofuata na kwa miaka mingi sasa nimekuwa nikijitahidi saana kumtafuta bila mafanikio.


Naomba kama anaweza kusoma ama kuna anayesoma na kumfahamu anisaidie kuwasiliana naye.



Email yangu ni: changamoto@gmail.com


Blessings,

Mubelwa Bandio









Read more...

WAKATI na wasiwasi KUNA asilimia YA UKWELI katika kila UONGO!





Ukinuia KUDANGANYA,...


.... kwa kuwa WEWE na MIMI tunajua kuwa KUDANGANYA ,...
.....kama tu KUZINI, kudokoa MBOGA au tu kupika UBWABWA ,....

.... kuna WAPATIAO VIZURI kuliko wengine,....





Swali:

  • Unafikiri katika kila ufanikiwavyo KUDANGANYA uongo wako ulioutumia ni 100 % uongo ?

  • Kwanza unauhakika kila uliponuia KUDANGANYA ni mara ngapi ULIFANIKIWA KUDANGANYA 100% ?


Na labda moja ya rasilimali ITUMIWAYO HOVYO NA BINADAMU ni ile ya UONGO kwa sababu ya UWEZEKANO MKUBWA kuwa watu wengi huzidisha UONGO katika kudanganya HATA wakati UONGO kidogo ungetosha KUDANGANYA na usingeumiza MTU.:-(









Swali zaidi kiduchu:

  • Si unajua PIA KUWA HATA kila mzazi , moja ya tendo afanyalo KWA UFANISI ZAIDI ni kumdanganya MTOTO wake hata kama nia YAKE ANAFIKIRI ni kukwepa kujibu tu swali la mtoto la; `` Hivi kwanini ghafla MAMA KAOTA kitambi?´´ ?

  • Huwa unaifikiria dozi utoayo ya UONGO kwa uwadanganyao katika danganya yako au ni kawaida yako kugawa dozi ya uongo bila vipimo WAKATI UNADANGANYA?


Nalikatizia WAZO hapa MHESHIMIWA!

Hebu tukumbushwe jinsi ya KUDANGANYA katika somo la kudanganya la- Why do kids lie?


Au Bjork atulize kwa- It's Oh So Quiet



Au tu Vumbi-Dekula arudishe kitu- Makumbele

Read more...

Wakati MWENZIO Mpenzi MAULANA ana HAMU,....

>> Saturday, December 26, 2009

...... wote TWAJUA sio lazima na WEWE wakati huo uwe na HAMU.:-(





Ila HAMU yako ikistukiwa na MTU yawezapandisha mtu HAMU!
Ila HAMU yako ikistukiwa na MTU yawezapandisha PIA kinyume cha HAMU YAKO mtu!:-(





Na IKIWA tatizo NI huruma YAKO kwa MWENYE HAMU,...

.....ndiyo ikufanyayo UFIKIRIE ili umtibu HAMU ZAKE mwenye hamu ,....

...inabidi UJIANZISHIE au KUJIPANDISHA yako hamu ili uwe kama MWENYE HAMU,...

.... huyo MWENZIO utakaye KUMTIBU au TU kumuigilizia kuwa na HAMU,....

...waweza kumtesa MWENZIO kwa kumpa matumaini UTAPANDWA HAMU kwa kuonyesha dalili unajitahidi kupandisha HAMU ,....


... HASA kwa kuonyesha JUHUDI zako za KUJIPANDISHA HAMU,...

.....halafu UKASHINDWA kufanikisha KUJIPANDISHA hamu,...

...IKADHIHIRIKA , hasa kama ULIMUONYESHA kuwa nia yako ilikuwa NAWE UPANDWE NA HAMU ili KWA PAMOJA msaidiane KUZITIBU KWA PAMOJA zenu HAMU.:-(


NDIO,...
....hamu kibao za watu HASA ZA ``KUNA - NIKUKUNE a.k.a TUKUNANE´´ siri ya TIBABU inaaminika ni ushirikiano wa PAMOJA wa WENYE HAMU katika kuzitibu HAMU.



NDIO,...
....sio wote HUPANDWA na HAMU kwa kustukia tu MWANAKWETU una HAMU.:-(


NDIO,....
... Kuna wachukizwao na hata KUONDOKWA na HAMU wakistukia tu Mwanakwetu UNA HAMU.:-(


Na YASEMEKANA moja ya KOSA tufanyalo SIYE watu ni kutia moyo watu kuwa katika tibabu lao la HAMU nasi kwanza tutapandwa HAMU kabla ya kuwatibu yao HAMU.:-(




Na kwa bahati mbaya INASEMEKANA katika KUMTIBU MWENZIO hamu zake wakati wewe mwenyewe huna hamu ,....
....mchezo MZURI hata wa matusi HUWA HAUNOGI na waweza hata kumuumiza asiye na HAMU.:-(





Tukiachana na kucheza na maneno:
....

....Siriasli a.k.a Swali KIDUCHU:

  • Ushawahi kupandishwa hamu ya kitu hata kama ni hamu ya kucheza netiboli kisa umeshuhudia umzimiaye apandwavyo HAMU a.k.a mzuka wa Netiboli?
  • Kwani HUJUI MAFANIKIO YA WENGINE kuna YAWAFANYAO waingiwe na HAMU ya KUFANIKIWA lakini pia kuna YAWAFANYAO watake KULOGA MTUHUYO ALIYEFANIKIWA kwa kuwa tu AMEFANIKIWA?
  • Ukistukia MWENZIO anahamu kwani kila mwenzio au kila wakati ushuhudiao hicho weye hupandwa hamu?
  • Kwani ukistukia hamu ya mwenzio ya MCHICHA huwezi pandwa hamu ya MISHIKAKI?

NI wazo tu MHESHIMIWA HILI na RUKSA KUTOLIELEWA ingawa SHUKRANI ZA DHATI kama likikufanya ufikirie KITU.:-(


Ngojea St Germain wabadili hali ya hewa kwa kurudisha KITU CHA UHAKIKA au tu - SURE THING

Read more...

'Christmas Recipes / Mapishi ya Noeli'

>> Friday, December 25, 2009

A Taste of Tanzania has posted a new item,....

..... 'Christmas Recipes / Mapishi ya Noeli'


I have put together a pdf of simple recipes from Tanzania that many people will
be preparing this weekend back in Tanzania. Traditionaly Pilau is the number one
recipe to think of during the holidays. I wish you a VERY MERRY CHRISTMAS.


You may view the latest post at:

http://tasteoftanzania.com/blog/2009/12/24/christmas-recipes-mapishi-ya-noeli/





Best regards,
Miriam Rose














Read more...

MNONG'ONEZO kwa APOKEAYE au afanikiwaye kutarajia ZAWADI!

>> Thursday, December 24, 2009

NI KWELI,....


.....WAUNGWANA hudai ZAWADI ni kitu chochote,...


.....INGAWA waungwana WASICHOSEMA ni kwamba,...


...hata VISIVYO KIUNGWANA wakipewa MAVI hawaiti au hawataita MAVI zawadi,.....:-(





Swali la KIUNGWANA:
  • Unauhakika aliyepewa zawadi huwa mara zote hustukia hiyo sio ZAWADI?

  • Si unakumbuka kuna WENZETU kule TANZANIA watokao katika MAENEO YA MADINI kama ALMASI walitoa ALMASI kwa zawadi ya PIPI?

  • SI kuna machifu waliosaidia maeneo yao yachukulliwe na WAKOLONI kwa zawadi ya ZE WHISKEY?

  • Si unakumbuka katika awezavyopewa mtu vingine ni LAANA hata kama sio MAVI?

  • Unafikiri zawadi yako sio kujidhalilisha UTU wakati ufikiriacho ni kwamba unamzawadia tu mtu UCHI?



NDIO,...
......Haki ya nani sikubishii kama wewe ni miongoni wa waaminio kuwa ZAWADI ni ZAWADI,...
.....na KUTOONA kuwa,....

..... mara kibao SIO ZAWADI ndio ZAWADI!:-(




NI wazo TU hili MHESHIMIWA na NIMELIACHA,....

...... ingawa NI MATUMAINI YANGU waweza kulikumbuka wakati UNACHEKELEA UDHANIACHO upewacho ni ZAWADI!:-(




MWISHO wa TARARILA .


Au ngojea Tantra ZAWADI atupe zawadi ya -``GIRL´´

Read more...

Siku ukistukia MALAYA WAKO kaanza kukupenda KIKWELI kama MAMA WATOTO/Baba WATOTO!

>> Wednesday, December 23, 2009

[Tahadhari: Labda tararila hii haikuhusu na ni ya kwa ajili ya wanaochanganyachanganya au kubadilibadili siagi:-(]


Kumbuka tu kuwa katika dini KUNAUWEZEKANO kuwa uvutiwavyo na UISLAMU kikuvutiacho ni 100% UISLAMU .





Swali:
  • Unafikiri UKRISTO hubakia UKRISTO kama katika ukristo wako unaruhusu na UISLAMU?




Ngojea nifanye majaribio tena ya kutoa AU KURUDIA hoja HII HII au hiyo hapo juu!:-(




KUMBUKA tu kuwa KUNAUWEZEKANO,...
.... akuvutiavyo MALAYA ni kwa sababu tu YEYE ni MALAYA na sio MME au MKE wako. :-(





Maswali ZAIDI yenye uhusiano au KUJARIBU kuelewesha HOJA hii nyoko ni:

  • Kwani hujastukia STORI za jinsi MME au MKE wa mtu alivyostushwa AU TU kutopenda mabadiliko ya MME kutoka katika alivyokuwa BOIFRENDI au MKE kutoka kwa kuwa KIMADA kisa wamefunga ndoa?



  • Unauhakika USIPOBADILIBADILI tamu ya jana, NI KWELI tamu ya jana ilivyo kuwa tamu kwa staili ile itadumu milele?



Swali zaidi ZILEZILE kwa kifupi:

  • Unauhakika KASHATA upewayo unaipenda VILEVILE kila siku na KAHAWA au IKIBADILISHWABADILISHWA LADHA YA TAMU yasababisha usichoke angalau ileile GAHAWA?

  • Unauhakika kwa kuwa unapenda chupi nyeusi NYUPI nyekundu hazihitajiki kurudisha kuendeleza hamu yako ya kuendelea KUJISIKIA VIZURI kutembea na chupi tu chumbani hata kama uko peke yako?

SINA UHAKIKA KAMA NIMEELEWEKA au NAWEZA KUELEWEKA na NAACHA WAZO hili nyoko MHESHIMIWA!




-------------------------

Hebu tupate angalau Pambio zielewekazo kutoka EL GATO Taquillero -I LOVE YOU TOO






Au tu Mrs Etienne atusaidie Pambio zielewekazo ZAIDI ujumbe katika -Amezaliwa MWANA WA MUNGU

Read more...

Merry somethin' EVERYBODY!

Send your own ElfYourself eCards

Read more...

Kama swala tumeelewa kuwa ni UIGIZAJI SINEMA, hatutashangaa kushuhudia MKE WA MTU akipigwa busu la wazi na TUSIYEMJUA!

BINADAMU kisaikolojia,....

... huwa hajisikii hata kuwa ni MUUAJI hata kama anajua MWIZI aliyempiga baada ya kumkuta anamuibia KAFA kwa kuwa jamii hata SWALA LA NANI NI MUUAJI hulijaji KISTAILI .:-(




Na tukiachana na JAMII isiyowashangaa WAUAJI kama akina Rais Obama ,NYERERE au tu WAHESHIMIWA WENGINE MARAIS watoao amri watu wauawe kwa kuwa jamii imeaminishwa kuna watu wanastaili kufa na pia kutowastukia wauao KISTAILI,......



....JAMII haishangai MHESHIMIWA muigizaji katika SINEMA akiwa UCHI kama STORI ya MOVIE jamii imeikubali kuwa GUMZO lake LINAFUNDISHO ZITO KWA JAMII na ni LA KIHESHIMA kwa kuwa katika sinema hiyo WAIGIZAJI kUWA KWAO UCHI ni katika kuonyesha MADHARA ya UKIMWI au tu HIYO ni STORI ya MHESHIMIWA Rais MANDELA na WINNIE MANDELA ila katika hicho kipengele cha sinema wanaonyesha JINSI Mheshimiwa huyo na MKE wake huyo aliyekuja kumshindwa BAADAYE walivyokuwa wanatengeneza watoto KISTAILI.





Swali:

  • Unabisha?
  • Unafikiri Rais SADDAM HUSEIN na GEORGE BUSH ni nani kaua watu wengi zaidi?
  • Unafikiri ungeandaliwa kimawazo kitofauti usingefikiria JOHO la PAPA BENEDICT ni aina tu ya GAUNI YA MATENITE ambayo PAPA kamuazima Ashura MJAMZITO?


Kwa kifupi TUKIRUDI KWENYE HOJA:

Kama umewahi kuangalia SINEMA ambayo ina MUIGIZAJI umheshimuye:

.......utastukiaKUWA HUWA hushangai au wala kupunguza heshima kwake ukimuona TITI a.k.a NYONYO kama sio mpaka CHINI KIDOGO ya KITOVU iwapo tu unaamini kuwa kwake UCHI ni muhimu katika kukufikishia UJUMBE muhimu KIHESHIMA au tu KISTAILI.





Swali:
  • Unabisha?
  • Unafikiri Rais OBAMA anajisikia MUUAJI kwa kuamuru watu waue VITANI?
  • Unafikiri ni wakati gani akili yako kisaikolojia hugeuka na kukufanya ukiona NYONYO hufikirii kuwa kazi muhimu ya NYONYO ni kuwa Hoteli ya MTOTO?
  • Si unajua karibu kila mme wa mtu MWENYE KUPIGWA DENDA kwenye SINEMA za HOLLYWOOD huwa anapigwa denda na mke wa mtu mwingine au tu Binti ya Mtu ambaye Padre hajahalalisha matamanio ?
  • Na unafikiri ni wangapi denda wawapigalo waume AU wake zao katika maisha yao ya kweli mtaani ni MAIGIZO?


HITIMISHO la hili wazo nyoko:

Ukiandaliwa vizuri na jamii kisaikolojia na hata tu kistaili ya kuona ni nini kawaida ,....

.....labda KUNAUWEZEKANO mkubwa ,...

.....mheshimiwa HATA wewe KWAKO hata NYAMA YA MTU INGELIKALIKA tu kama Njegere.:-(







NI WAZO TU HILI na mwenye kuelewa kashaelewa na kulibishia RUKSA!:-(





Hebu CHARLIE CHAPLIN akumbushie-SMILE



NENEH CHERRY amzungumzie tena -WOMAN



Au tu Angelique Kidjo arudishe- Agolo








NIMEACHA!

Read more...

Kwa KIFUPI,...

>> Tuesday, December 22, 2009

.... ujumbe HUFIKA.:-(



Na mara nyingi kwa KIREFU,....
..... kuna uwezekano ni staili tu ya KUZIDISHA tu katika UJUMBE MANENO tena katika ujumbe tayari ULIOFIKA.:-(








Swali:

  • Unauhakika na ujuzi wako wa lugha kama UJUMBE WAKO MFUPI unahisi wahitaji kuelezewa KIREFU?

  • Unauhakika ni maneno mangapi ndio mwisho wa kuandika kifupi?
  • Kama hujanielewa hapa kifupi, wafikiri nikizidisha maneno ndio ungenielewa?



NI WAZO TU HILI MKUU!


Hebu FELA KUTI aongee kirefu katika- OPPOSITE PEOPLE






Au tu Neneh Cherry & Youssou N'Dour warudie - SEKUNDE SABA

Read more...

Kwa kuwa YEYOTE akihisi kibano aweza KUBADILI au KUNAKSHI STORI.

Karibu kila umjuaye KAFUDHU,....
.....katika sanaa ya kubadili STORI.



......na kwa sababu HIYO ukweli wa HALI HALISI ya SHENZI usimuliwao na aliyefudhu,....


..... yaweza ikawa IMEPENDEZESHWA au kutoongelewa KABISAAA kwa kuwa SHENZI KIHALIHALISI NI SHENZI KWELI na hilo ndilo UDHAIFU katika upewayo STORI kama ni kweli umepewa hiyo STORI.:-(



Swali:

  • Wewe sio miongoni mwa WANADILIO STORI au hata KUNAKSHI SHENZI kwa kuwa tu HALIHALISI ni CHUNGU na UKWELI WAUMA ?

  • Unauhakika stori zako kwa kawaida zinadaka hali halisi au huwa zinanaksh tu zaidi SHENZI isionekane kwa wake ushenzi?


NI MOJA YA WAZO na kama umenielewa DOUBLE CHECK upewazo STORIZ!


Hebu twende Senegal Youssou N'Dour adai - Birima




Au tu Youssou N'Dour alete - Salaam

Read more...

BUSARA na USTAARABU!

Ukichunguza waweza kustukia kuna BINADAMU wengi ,.....
...... wasahauo kuwa BUSARA MARA NYINGI haijali lihitajikalo kibusara liwe LA KISTAARABU.




Na kwa USTAARABU wa wengi,.....
......lihitajikalo hata kujikwamua katika tatizo liwasumbualo sana HALIFANYIWI KAZI kwa kuwa kitafsiri yao sio la KISTAARABU.:-(




Swali :

  • Si unajua KISTAARABU kuna wachambiao TISHU /makaratasi hata kama kwa busara zao ni maji ambayo wanayo msalani ambayo yangethibiti vizuri usafi wa kitobo cha tako?




Ndio,...
..... KISTAARABU waweza kufa na NJAA hata kama kibusara suluhisho la tatizo unajua ingebidi udokoe MBOGA.:-(





NI wazo tu HILI Mheshimiwa na NALIACHA!


Au ngojea tu R.Kelly arudie-I believe I can FLY

Read more...

Ukishamalizia KUJILAUMU!

Kama wewe ni MFANYAJI kitu ,....
.... jua kwa vyovyote maishani UTAKOSEA KITU!:-(


Na ukikosea kitu,....
..... ni kawaida ukiweza PIA kirahisi KUJILAUMU kitu.:-(





Swali:
  • Lakini si unajua tu kuwa jambo muhimu wakati UNAJILAUMU mara karibu zote sio huko kujilaumu, bali UMUHIMU MUHIMU katika SWALA UJILAUMULO UKO KATIKA utafanya nini KUHUSU ulilofanikiwa KUJILAUMU?
  • Si unajua kujilaumu kama tu maneno matupu hakutoi mtu mimba?


Ni hilo TU na NI WAZO TU MHESHIMIWA!:-(

Hebu Los LONELY BOYS warudie kibao - How FAR IS HEAVEN


Read more...

Ili UACHE,....

>> Monday, December 21, 2009

......anza!

Read more...

UKIFANIKIWA kuchungulia mawazo ya MTU!

......,jamaa lenye pozi la KUFIKIRIA sana mpaka unaweza ukatishika kwa kudhani linafikiria jambo gumu sana na JIPYA ,.....


......KUNA UWEZEKANO hilo KUBWA ZIMA likifikiriacho saa hiyo ni UBWABWA .:-(









Swali:
  • SI unajua afikiriaye UBWABWA na MTAFITI afikiriaye kugundua DAWA YA UKIMWI kimuonekano wa pozi la kufikiria inaweza ikawa ngoma sare?

  • Hivi KIMUONEKANO unajua pozi lako wakati unafikiria UGALI utofauti wake na wakati unafikiria kitu KINGINE?



NI HILO TU Muzee wa KUTISHIKA na MAPOZI na ni WAZO TU!

Read more...

E-mail ya wazi kwa YESU!

>> Sunday, December 20, 2009

Kwa .....




Mheshimiwa mwokozi YESU,...

...... si UNASTUKIA na UNAJUA kuwa kuna WAJANJA wameivalia njuga siku fulani na KUIUZA kama ndiyo uliyozaliwa MPAKA usipokuwa MJANJA waweza kuamini ni kweli hiyo ndio tarehe na siku ULIYOZALIWA?

Ni hilo tu Mheshimiwa YESU.:-(








P.S:

Baizewei vipi lakini huko MBINGUNI maswala?

Si unacheki mwenyewe idadi ya waogopao kufa hasa kwa kutokuwa na jibu tu kama ni kweli huko mbinguni maswala ni MSWANO ZAIDI kuliko kule JEHANAMU kwa yule mshikaji wako wa zamani SHETANI?


BAADAYE BASI Mheshimiwa YESU kama nikipatia upendayo ilinijichanganye kwenye kijiwe chako huko uliko MKUU!

Si unajua mwenyewe MASHARTI ya PATI YAKO yalivyo magumu kwa BINADAMU akijaribu kuishi KIBINADAMU?:-(







.......AU tukiacha hili WAZO NYOKO , ngojea BOBBY McFERRIN atupe kitu - AVE MARIA



Au tu Mr PREGNANT alie tu kama hivi...

Read more...

KUHUSU nafasi uipayo UPUUZI MAISHANI mwako!:-(






PAMOJA
na ukweli NI KWAMBA unaweza na UNARUHUSIWA kunibishia,...

... bado taka usitake UPUUZI NI MUHIMU pia MAISHANI MWAKO na labda ndio maana unajisikia vizuri hata kwa kujitahidi KWAKO usionekane MPUUZI.:-(





Swali

  • Unabisha?


Tatizo ni:

  • Je unajua nafasi ya UPUUZI MAISHANI MWAKO inatosha au ni kweli umezidisha tu angalau kidogo UPUUZI?
  • Si unajua upuuzi ukizidi ndio mpuuzi anakua MPUUZI na hilo mara nyingi sio wakati WEWE unadhani umeshamtambua au kustukia MPUUZI kwa kuwa kinamna unadhani unajua ni nini UPUUZI na nani MPUUZI?


Tukiachana nahilo:

  • Unauhakika unajua ni nini UPUUZI na kwa hilo uligundua mwenyewe na sio kwa kufundishwa na wajanja hata kama ni WAZAZI WAKO kuwa ni NINI upuuzi?




NIMEACHA!:-(




Hebu Bobby McFERRIN a -DRIVE

Read more...

Jinsi ya kumpenda SIMON KITURURU,....

......wakati huna UHAKIKA na SIMON KITURURU ,....


....na KWA HILO USILO NA UHAKIKA NALO sio tu NI ule MSHEBEDUO wa SIMON KITURURU!:-(








Swali:

  • Unauhakika ulishawahi KUJIPENDA?
  • Unahakika UNAJIPENDA?
  • Na unauhakika wewe UNAPENDEKA?



:-(


NIMEACHA wazo hili NYOKO!:-(








Ngojea tu PEPE KALLE abadili hali ya hewa kwa kitu- HUGE SUCCESS




Ajivunie - Roger MILLA






Au tu aongelee alivyotafuta kidude ARUSHA kwa simulizi aliyoiita-HIDAYA

Read more...

UKISHAtombwa,....

..... ,



...... katika FARAJA HIYO,....


..... unawezakustukia ULIJIPENDEKEZA MWENYEWE ili UTOMBWE ingawa KIRAHISI TUKIFAFANUA MBINUKO WA WAZO ulilokuwanalo WAKATI HUO ,..


labda WAKATI HUO MAWAZONI kutombwa sio ulilokuwa unafikiria,....

.... na KWA HILO wala haibadili UJANJA hata kama hukusikia UTAMU KIJANJA kwa kuwa ni kweli hata ufanyenini ;...


...... UMESHATOMBWA.:-(








Swali:

  • Au?
  • Lakini si unajua hata baada ya kutombwa unaweza usistukie ULITOMBWA?:-(




[Tahadhari: Katika tararila hii , kirahisi NENO halina uhusiano na ufikirialo kirahisi NENO.:-(]

NI HILO TU!:-(








Au tu ngojea PRODIGY washindwe na kuamua ku- Smack MY BITCH up




Au tu waanzishe kwa -FIRE STARTER





Au tu waongelee pumuzi katika-BREATH

Read more...

Kama Rais BARACK OBAMA angedakwa wakati bado ANAVUTA BANGI na kutumia madawa ya KULEVYA!:-(

>> Saturday, December 19, 2009






Kama wewe ni MALAYA,...
... au tu kama wewe BADO ni MALAYA!




:-(








Swali:
  • Si unajua kama tukikuachia utusimulie jinsi ujambavyo vizuri unaweza kusababisha tufikiri una jamba PAFYUMU?


  • Unajua kunauwezekano UKIACHA KITU KAMA TU ULIVYOACHA KUWA MLOKOLE na ukajua jinsi ya kuongelea HILO kuna uwezekano MKUBWA tutakusamehe?

  • Unajua kunauwezekano UKIACHA KITU KAMA TU ULIVYOACHA KUWA MLOKOLE na ukajua jinsi ya kuongelea HILO WEWE MALAYA hata jinsi ULIVYO KUWA MALAYA ukiongelea hilo la UMALAYA WAKO kivyako tunaweza kufikiria kuwa weye si MALAYA KAMA MALAYA WENGINE na hata ukizaa bila MUME kama MAMA MARIA mama ya YESU tutaamini tu KAMA WAKRISTO WAMINIVYO MIMBA YA MAMA MARIA ni kweli ulipata mimba KAMA UKIPATA MIMBA kwa kuwa ulivyoonjwa UMETUAMINISHA KUWA ulionjwa kitukufu?
  • Si unajua nikifanikiwa utanisamehe NA mpaka hili niandikalo hapa ambalo labda ni NYOKO na WAWEZA MPAKA ukashauri ndani ya TANZANIA nisomwe KWA HILI mpaka shule za CHEKECHEA?





Unajua,...

... pamoja na MADOIDO yote ya sentesi HIZI kadhaa bado niongeleacho kinauhusiano na jinsi ambavyo ungejisikia kuhusu BARACK OBAMA kama kichwa cha habari cha tararila hii kiulizavyo ;...


.... `` Barack Obama angekiri ni kweli alishawahi kuonjwa TAKO kabla hujawa MSHABIKI WAKE ungeshabki nini katika lake yuleyule ambaye ni huyu?:-(´´







SWAli:
  • Umenielewa?
  • Unauhakika Rais Barack OBAMA kama tu Waziri msaafu WARIOBA wameacha kuvuta BANGI kama adaivyo RAIS mstaafu BILL CLINTON?






NIMEACHA na haki ya nani MIMI Simon KITURURU SIVUTI bange!:-(

Hebu nimuache BOB MARLEY arudi kukukumbusha unafiki katika-Hypocrites

Au tu BOB MARLEY aongelee swala hili kimarudio ili ufikirie kama hata wewe sio MNAFIKI:-(..

Read more...

Wakati kunahisia za MTU kuwa ni kweli : ``HUNA HAMU ya KUTOMBWA leo!:-(´´





K
ama una HAMU mpaka ya kwenda MBINGUNI LEO ukifikiria vizuri,...

.... HIYO HAMU yaweza KUWA yafanana na jinsi ufikiriavyo KUJIUA leo.:-(






Swali:
  • Unauhakika ni kweli huna hamu ya kutombwa leo, kama ni kweli hata unajua na HUWA unapatia KUTOMBWA weye?

  • Unabisha au unafikiria tu kwa kuandika KWANGU neno kutombwa katika kichwa cha HABARI labda kwa hilo huna uhakika bado sijatukana?:-(



Na WAKATI tuangaliacho mpaka katika zaidi ya sentensi ni ; ``SINA HAMU ya kukutomba´´....


...... labda bado ni kweli KUNAUWEZEKANO katika ujuayo ya kutombwa katika hilo WEYE huna KITOMBEO na,...

..... labda pia NI KWELI hamu ya kwenda MBINGUNI kama tu hamu yako ya KUTOMBWA ukiisikilizia vizuri ,...

...LABDA,....


....

WAKATI HUO usikiliziavyo unaisikia au kuihisi ,....


.....WAKATI HUO ladha yake ihitajiyo BINZARI wakati haina BINZARI.:-(





Swali :

  • AU?


Na wakati una HAMU ya KUKATAA TU KULA VIZURI,....
......kama wakati unakataa CHAKULA ulikuwa na njaa vizuri ,..
.
... KUNAUWEZEKANO MKUBWA wakati HUO unakataa kula UKATAACHO KULA wakati huo sio hicho CHAKULA.:-(





Swali :
  • Si unajua kunauwezekano MKUBWA huelewi naongelea nini?:-(

Ngojea tu NIACHE WAZO na ni RUKSA kufikiri kunatusi katika NENO. Mheshimiwa!:-(


Ngojea basi JOSEPH COTTON abadili kwa kudai -Things RUNNING SLOW.






Au tu MAXI PRIEST amzungumzie-TEMPTRESS




Au tu SHABA RANKS amrudishe dokta katika-Champion Lover

Read more...

Lol !

Kama ``LOL´´ kwa ung'eng'e ni;

.....-``Laughing Out Loud!´´












SWALI:

  • UNAFIKIRI ni kweli waandikao LOL ni kweli wana LOL wakati wanaandika LOL?







Kwa kuwa OMFG sio tusi kwa wadhaniao ni MSHANGAO,...



,,,, katika TUSU itusulizwayo ki TUSU kama tafsiri yake BANANGENGE ni TUSU,.....

.... labda ``OH MAI FAKEN GODI {omfg}´´.....


.... labda kwa Mheshimiwa OMFG ni TUSI kilugha OMFG ....


.....,


:-(





Swali:

  • Unafikiri niwangapi WAANDIKAO KIFUPI ni kweli wanacheka wakati wanadai WANACHEKA kwa kuwa waliyoandika kwa HERUFI KIFUPI kwa kuwa RASILIMALI YA MNYONGE ni UNYONGE katika UMOJA ,.....unawezakusingiziwa BASI katika ya wachekeleao kanyau SI hawachekeshwi hata katika iaminikayo INACHEKESHA?




OMFG NIMEACHA!:-(...



SWALI:
....Mheshimiwa ``KAJMB N.ni´´ IKIHITAJIKA KUELEWEKA ilipohitajika apumue.,...

.....mtu AKIHITAJI APUMULIE TAKO unadhani ni LAZIMA AOMBEE WATU WASISIKIKE akipumua kistaili iitwayo KUJAMBA ki kifupisho; KJMB N.na.i?:-(









NIMEACHA WAZO!:-(

Omfg na NAACHA kulazimisha KITU !:-(




LAKINI SI MHESHIMIWA,....

...... unajua hili ni wazo tu ndio maana labda wakati umejifunza kuandika LOL si LAZIMA ni kweli UNACHEKELEA KANYAU kwa SAUTI ki -``LOL´´ kama ulivyojifunza IMAANISHAVYO ``LÖL´´ :-(?





.:-(





NIMEACHA WAZO na RUKSA kutoelewa MHESHIMIWA hasa kama unakumbuka HILI NI WAZO TU MKUU!:-(






Ngojea GEORGE MICHAEL anung'unike kwaa kitu - Careless Whisper




AU tu CULTURE warudie kitu- I tried




Au tu niachie picha zaidi za juzijuzi za WANZABANGA....


Photobucket



Photobucket














Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP