Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

VIKOROKOCHO katika STORI za UKUMBUKACHO!

>> Monday, December 28, 2009

Jinsi ukikumbukavyo UKUMBUKACHO hata kile ambacho unafikiria ni kwa kuwa NI KWA UTOFAUTI WAKE ndio maana UNAKIKUMBUKA ,.....

....kwa kawaida UKIKUMBUKACHO utakikumbuka kinamna au kivitu ambavyo UBONGO wako umezoea kuvistukia katika vitu na ndio maana kwa kawaida WEWE utastukia HIVYO kwa staili hiyo , kitu ambacho kitatofautisha UKUMBUKAVYO wewe kitu na WENGINE ambao kwa pamoja MLISHUHUDIA kwa pamoja KITU.


Swali:

  • Si unajua WASHUHUDIAO KITU HICHO KIMOJA wakiongezeka utapata STORI tofautitofauti za KITU au tukio hilohilo MOJA kutokana hasa na staili tofauti za watu za kukumbuka kitu?



Kwa kifupi:

JINSI usimuliavyo UKUMBUKACHO kwa kawaida HUJAA jinsi UTAKAVYO na kistaili tu ya ULIVYOZOEA tu kukumbuka VITU na wala sio KIUKWELI wa jinsi kilivyotokea KITU.:-(



KUNA jinsi tu ULIVYOJIZOESHA HATA BILA KUJUA kukumbuka jinsi ya UKUMBUKAVYO KITU kisababishacho kama ni MSICHANA kwa ko WEWE kirahisi unaweza kumkumbuka kirahisi kwa saizi ya TITI wakati Mwenzio MMOJA anaweza kumkumbuka kwa alivyokuwa na UPELE USONI kama ZEGE na MWENZAKO MWINGINE kirahisi awezavyo kumkumbuka kirahisi MSICHANA HUYOHUYO kwa jinsi alivyo kuwa na BONGE LA TAKO.:-(



Swali:

  • Unauhakika kilichotokea ulichowahi kukishuhudia kikitokea ndivyo jinsi UKIKUMBUKAVYO?


  • UNAFIKIRI ni kwanini KUNDI la watu lishuhudialo KITU KWA PAMOJA kwa kawaida huwa na STORI tofautitofauti za hicho kitu?

  • Kwani wewe unafikiri huwa unakumbukaje baadhi tu ya vitu?


NI WAZO TU HILI Mkuu na WALA usikonde!:-(


Na hebu Oliver N'goma arudishe -Nge


Au tu Oliver N'goma na Bhonos warudishe tena -Alphonsine



Au tu Oliver N'goma aachie na -Bané



0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP