Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

MFANYAKAZI na MFANYIWAKAZI wakati inasadikiwa KWA WOTE KAZI ni tamu!

>> Wednesday, December 16, 2009

Kila mtu hata kabla hajazaliwa HUANZA kwanza kufanyisha watu KAZI.:-(

Na akizaliwa tu MTU huendeleza kufanyisha watu kazi ,....


... na miongoni mwa moja ya KAZI ZA KWANZAKWANZA aitoayo MTU kwa watu ni ile ya KUCHAMBWA a.k.a KUBADILISHWA NEPI yenye choo laini na ujazo fulani wa mkojo , na kumbuka kazi hiyo ya KUCHEZA na KINYESI mhusika TOTO huitoa bila kujali kuwa apewaye hiyo shughuli kwake ni KAZI.:-(


Swali:
  • Sasa umegundua ni wapi akupaye kazi bila KUJALI unajisikiaje alitoa wapi hiyo hulka ?

Na ni baada ya miaka MICHACHE tu baadaye MTOTO aliyeingia duniani huanza naye kufanyishwa KAZI,.....


..... ingawa kazi za MWANZOMWANZO ni kama tu zile za kusakiziwa kwenda mlangoni MTU AKIGONGA HODI ili kudanganya `` MAMA KANIAMBIA KUWA niseme WENYE NYUMBA HAWAPO!´´ yote ikiwa ni moja tu ya shughuli na mafunzo ya mwazomwazo HATA YAKO ya KUDANGANYA KAZINI hata kabla hujafikiria ya kulipwa mshahara KAZI.:-(


NDIO , ni muhimu KAZI,...
..... lakini kwenye kazi kuna WATENDEWAO kazi.:-(


Na katika KAZI,....
.... tukumbuke kuna MFANYAKAZI ambaye kuridhika kwake kuko katika kufanyia WENGINE KAZI. :-)



Lakini pia katika KAZI,....
.... kuna WAAJIRIWA ambao ingekuwa BOMBA a.k.a BORA sana wangekuwa wao ndio WAAJIRI wa watu katika AJIRA a.k.a hizo KAZI.


Na KWA BAHATI MBAYA mara kibao katika tuzifanyazo kazi ,.....
....tunazifanya tu kwa kuwa hatufikirii tunamfanyia nani kazi.:-(



Swali:
  • Unauhakika humfanyiii adui yako au tu MHESHIMIWA SHETANI ufanyayo hiyo KAZI?
  • Si unajua wengi wawaajirio watu ni NYOKO?


Na haki ya nani inazingua yoyote uifanyayo KAZI,...
.... hasa kama wewe ni miongoni mwa ambao hunogewa zaidi KUAJIRI watu wengine a.k.a KUFANYISHA WENGINE KAZI kwa kuwa unajijua ni mbunifu zaidi wa kazi na kwa sababu MOJA MBILi huwezi hata mwenyewe kuanza kwa KUJIAJIRI MWENYEWE kazi.:-(


Na nikiongea kama MTANZANIA kuhusu kazi,...
.... naweza kukuambia kuwa elimu ya TANZANIA mara karibu zote hulenga tu kumjenga MTANZANIA asijiajiri kwa kuwa inalenga kumuandaa kujisikia inabidi AAJIRIWE MAENEO siku akihitaji KAZI.:-(


Na ukichunguzaTanzania utastukia wengi wajiajirio kuanzia kwenye KILIMO vijijini mpaka mijini KIKAZI,...
.... wengi wao ni wale wenye sifa AMBAZO KWAKO NI za kuwa hawakwenda sana SHULE KAMA WEWE ULIYEAJIRIWA NA UNAMSHAHARA BONGE LA MSHIKAKI , na kwa HILO unaamini ilibidi walazimike KUJIBUNIA KAZI.




Swali:
  • Unabisha?
  • Lakini si unakumbuka ajibuniaye kazi leo akifanikiwa kesho anaweza kuwa muajiri WAKO?


MFANYAKAZI na MFANYIWAKAZI,....
,..... ni kweli wote labda KWAO ni tamu KAZI.


Lakini kama unafanyishwa KAZI,.....
.... ingawa nia YAKO IFANYAYO UFANYISHWE KAZI labda ni MSHAHARA au hata STATASI a.k.a MSHEBEDUO ukuwezeshao KUJISHEBEDUA kuwa wewe ni kiboko kwa kuwa UMEAJIRIWA na UNAKAZi,....

...... LABDA fikiria pia hivi kikweli unafanyanini katika hiyo kazi na kikweli unamfanyia nani hiyo KAZI.:-(




TUNAJUA,...
.....katika kazi za unyumba chumbani WATOTO WAKILALA ni rahisi kujua unamfanyia nani kazi,....
.... au ni nani mvivu katika kukufanyia kazi KAMA NI YA ufundi wa tendo la ndoa ndio KAZi.



Lakini ulimwenguni KIKAZI,......
... unaweza kujikuta wakati unafikiri unafanyiwa kazi IKAWA UKWELI wenyewe ni wewe UFANYISHWAYE KAZI.:-(



Na ina weza PIA ikawa UNAFIKIRI ni kwa ajili tu ya mshahara ndio maana UNAFANYA KAZI!



KWA BAHATI MBAYA ,....
.....ukweli wenyewe unaweza kuwa hata kwa utulivu wa UBONGO WAKO tu bila hata kuhitaji mshahara WEYE unahitaji KAZI.:-(

Swali:
  • Unafikiri ni kweli unaweza kuishi bila kazi ?

NAKATIZA WAZO KIDUCHU!:-(



Hebu KEM alete tena-WHEN LOVE CALLS[REMIX - Ft FLOETRY]


Floetry walete- Fantasize


Floetry walete -Floetic



Au tu Faith Evans amalizie kwa -Mesmerized

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa 11:11 am  

inafikirisha hii kazi

Simon Kitururu 3:20 pm  

@Komandoo Kamala: Si utani!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP