Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KAWAIDA- kwa kuwa ni kawaida kupitisha siku bila KUFANYA matusi!:-(

>> Saturday, July 31, 2010

[Tahadhari: Katika tararila HII neno matusi halina uhusiano na vitendo vitendewavyo sehemu za siri.:-(]




NDIO,...
... kwa kuwa ni kawaida kupitisha siku bila kufanya MATUSI,....
... bado hilo halibadili kuwa ni kawaida PIA kama siku ikipitishwa kwa kufanya MATUSI.:-(



Swali:
  • Unabisha?

KAWAIDA ni KIDUDE bonge la kigeugeu kwa kuwa labda KAWAIDA,....
..... huhitaji tu UNAVYOTAFSIRI nini ni KAWAIDA na uzoefu wako wa KURUDIARUDIA KITU ,....
.... kitu kifanyacho kumuwezesha BINADAMU MWINGINE kwenda CHOONI kabla hajabanwa kwa kuwa ni kawaida kwake akiamka tu cha kwanza ambacho kwake ni kawaida ni kwenda kunya.:-(


Swali:
  • SI mpaka kuna atakaye kula NANIHII wakati hana njaa ya NANIHII kisa kazoea tu na kwake akiona tu KINONO anafikiri ni lazima aonje?

  • Umewahi kuchunguza UWEZEKANO kuwa labda KAWAIDA kwako inaweza ikamchubua uchi wa FIKIRA mwenzio?


Na kama kwako ni KAWAIDA kupitisha siku bila kula kwa kuwa UMEZOEA,....
... unaweza usimuelewe aliye FUNGA hata RAMADHANI kwa kutafsiri kutokula ni KUFUNGA.:-(

NIMEACHA!
NA ni wazo tu hili MHESHIMIWA wala usikonde!:-(

Hebu RICHIE SPICE  akiwa na CLINARK walete kitu - Living In A Concrete Jungle



Richie Spice na J BOOG wanyokolishe pambio-Got to be STRONG



Au tu RICHIE SPICE amalizie mkuno kwa ndude- MORE LIFE




Au tu J Boog alainishe ujumbe kwa -LETS do it again

Read more...

Tatizo liwezalo KUJITOKEZA kwa kuwa NYOKA huwa HAWAKOJOI,......

>> Friday, July 30, 2010

.....labda ni kuwafanya WASISTUKIE viumbe  wengine wanakojoa na kwao KUKOJOA ni muhimu.:-(





Na labda ni kweli  kwakuwa NYOKA hawakojoi,...
.....labda kwao sio muhimu kujua kama ni kweli kwa BINADAMU kukojoa ni muhimu.


Swali:
  • Kwani huwa unakumbuka YASIYOKUHUSU labda NI MUHIMU kweli kwa WENGINE?

  • SI unajua ya WENGINE  yanaweza kuwa ni MUHIMU SANA tu KWAKO ingawa hujastukia UHUSIANO wa YA WENGINE na WEWE?

  • SI unajua kama wewe ni mpenda MAUA ingawa HUWAHUSUDU NYUKI labda nyuki ndio wasababishao furaha zako za MAUA ya pendezayo hasa ukikumbuka halihalisi kuwa LIBWANA lako LINA SURA mbaya na halipendezeshi NYUMBA?



Na kwa kuwa BINADAMU anaweza kuhisi ya NYOKA hayamuhusu,....
.....kitendo hicho kinaweza kusababisha BINADAMU aishi bila kustukia NYOKA hakojoi.:-(

Na wakati unafikiri  BINADAMU WENYE MAJI YA KUNYWA  ya watu  yanawahusu,....
..... kumbuka BINADAMU huyohuyo anaweza kusahau kuwa MTU mwenzie kwa kuwa hana MAJI ya kunywa  leo anaweza kuwa anakosa  FARAJA KAMA ZAKE za  kutoa mkojo kwa kuwa  KUTOKANA NA UHABA wa maji , hakojoi.:-(

Swali:
  • Wakati BONGO FLEVA inakuhusu  unauhakika BONGO FLEVA haina uhusiano na MDUNDIKO?

  • SI unajua UFIKIRIAYO hayakuhusu LABDA yanauhusiano  nawe na kukuhusu kuliko UFIKIRIAVYO ?
  • SI unajua labda hata kilimo cha PAMBAufikiriacho kuwa hakikuhusu kwa kuwa HULIMI PAMBA labda kinauhusiano wa karibu sana na CHUPI YAKO uipendayo ambayo kwa inavyo kuhusu  unaivaa siku  maalumu tu ambayo unahisi utachunguliwa kwa kupenda mwenyewe?


  • SI una JUA labda URAIS wa Rais KIKWETE una uhusiano na wasukuma MKOKOTENI wasababishao URAIS wa RAIS KIKWETE uwezekana kwa kuwa tu  azungumziavyo vya wasukuma MIKOKOTENI vinakuhusu?

NI WAZO TU HILI na ni ruksa kutolielewa!:-(

MIE naanza kivyangu na nakutakia IJUMAA  na wikiendi KIBONGE!


Hebu twende Ivory Coast mtoto mdogo  BB DJ waanzishe siku kwa -Enfant POLI



 Hebu tupitie Guinea ili  Mory Kante arudie mkuno-Touma




Au tu twende Senegal ili  Daara J Family walete ndude- Bayi Yoon

Read more...

Kuna watu KULALAMIKA hiyo ni tabia yao,....

..... ndio maana kulalamika BILA SABABU kupo pia.:-(

Na tamutamu ya KULALAMIKA labda ndio siri ya kuzoeao kujisikia kulala kwao,....
..... LABDA ndio maana hukawii kustukia hata KWENYE GAZETI LA UDAKU eti ndani ya siku RAIS na HAUSIGELI wote kunakitu wanalalamikia na eti hicho kidude kinaweza kuwa ni UGUMU WA MAISHA yaleyele ambayo kwa tafsiri ya MAISHA labda ugumu ni sehemu yake na labda hakuna sababu ya kuuulalamikia kama ni siku yako ya kutosikilizia utamu katika maisha kitu ambacho labda ni HALIHALISI YA MAISHA pia.:-(


Swali:
  • SI unajua hata uwe tajiri au MLOKOLE vipi tamu na CHUNGU za maisha bado utakutananazo tu zikipeana zamu?

  • Kwani hujawahikukutana na MTU ambaye KULALAMIKA ni tabia yake na hata UUMPE YOYOTE nanihiii bado atatafuta sababu angalau alalamikie ulivyomgawia KIDUDE?


SAMAHANI nimekutana leo na MTU ambaye kila nikikutananaye kunakitu ANALALAMIKIA.:-(

NIMEACHA topiki MKUU  !

Hebu  The Beatles warudie ndude- DRIVE my CAR



Au tu Bobby McFerrin arudie kukumbusha watu kama unakipaji huhitaji chombo cha mziki kunyokolisha katika ndude-Drive


Au tu Bobby McFerrin arudie kukumbusha -Dont WORRY be HAPPY

Read more...

Katika KUJIULIZA MASWALI labda kila MTU ana UPROFESA , ila tatizo liko kwenye kupata MAJIBU!:-(

>> Thursday, July 29, 2010

Na uhusiano wa SWALI na JIBU,....
.... inawezekana sio SWALI na JIBU  ikiwa kuna ukweli labda uhusiano wa SWALI na JIBU ni MTU MWENYEWE tu  ndiye astukiaye SWALI  na anadhani lazima liwe na JIBU.:-(


Swali:

  • AU?

Na kwa bahati mbaya inawezekana MAJIBU,....
.... kuna mpaka mtu ambaye wakati anafuatilia MASWALI  ya gono akajikuta kapata MAJIBU yakuwa ana UKIMWI pia.:-(

Swali:

  • Unafikiri UKIKOSA JIBU kukosa kwako  JIBU kwenyewe sio JIBU?

Kumbuka,...
....duniani kuna mpaka WATU wasicho kijua  na KISICHO WAPA MAJIBU,...
.... wamefanikiwa kukiita MUNGU yote ikiwa ni katika jitihada za MWENYE SWALI kufikiria ni lazima kuwe na JIBU.:-(

Swali:
  • SI unajua  ukiuliza unaweza kupata jibu kuwa hata  NG'OMBE  usiyemuabudu  ni MUNGU  katika baadhi ya IMANI na DINI  za watu wenye akili tu za kutosha?

NI HILO TU!:-(


Hebu LAGBAJA abadili hali ya hewa kijiweni kwa kushusha AFRO BEAT ambalo halijakaa kitoto liitwalo-Sobolation


Hebu LAGBAJA arudie tu pia mkito -Feyin e



DUH au tu aachie na kitu-Rock me Gentle


Basi bwana labda jifunze tu LAGBAJA ni nani kama muda unakuruhusu::-(


Read more...

ASIYETUKANA ukimsachi unaweza kustukia naye anamatusi tu NDANI YAKE!

>> Wednesday, July 28, 2010

Uwezo wa  WATU kusema chochote kile UPO,.....
..... ingawa sio kila MTU mwenye kibezi cha kusema chochote kile ANACHO kifikiria.


Na ingawa kuna WATU lukuki  wasingiziao KUJIHESHIMU, walivyooshwa ubongo na dini au tu tabia nzuri ndio kiwasababishao washindwe kupata FARAJA ya kukutukana  au KUKUSENGENYA hadharani wapo,...
.... ukichunguza unaweza kustukia WAPO PIA WASIO SEMA  kwa kuwa hawajui tu jinsi kuwakilisha MLOLOMO  kimswano HADHARANI  ingawa wanavyo kufananisha na watu watengenezacho MSALANI bado ndivyo wanavyo kufikiria.:-(




Swali:
  • Si unajua labda LEO asilimia kubwa ya ULIYOYAFIKIRIA hujayasema?
  • Umewahi kujichunguza JINSI wewe mwenyewe unavyojinyima FARAJA ziletwazo na kusema chochote kile?


Ndio,....
.....hata PADRE au SHEKHE anayekutolea macho ukimsachi anacho kifikiria unaweza kustukia ANACHOKUSEMESHA sio anachokifikiria kwa kuwa labda anacho kifikiria kikitendwa kuna atakaye pata ujauzito.:-(


Ndio,...
..... unaweza KUFUKUZWA kazi kisa umesema chochote kile na hata kama KIBUSARA kina bonge la tani kiuzito.:-(

KWA bahati mbaya naachia hapa WAZO!:-(

Hebu The Kilimanjaro Band walete -Kachiri



Au tu JACOB F. DESVARIEUX anlete ndude -Goree



Au tu Jacob Desvarieux , Jocelyne Labylle & Cheela warudie mdinyo -Laisse parler les gens


Read more...

KULIA ni MUHIMU kweli kama tu KUCHEKA!:-(

....na labda ni zisizo BUSARA za wahenga zisababishazo ANAYELIALIA kuonekana nishai hasa kama KITENDO HICHO hakifanyiii msibani.:-(


Swali:
  • Ushawahi kujikuta uko msibani halafu huna huzuni kitu kikufanyacho ushindwe KULIA KIMADHUBUTI na matokeo yake uanze kusikiliza watu wanaliaje na katika mkao wakulia wanakunjaje SURA kitu kifanyacho ufanye kazi ya ziada kujizuia kucheka?

  • SI kunauwezekano wengi wakenuao meno labda hawacheki kutoka moyoni kwa kuwa moyo unalia wakati wanajitahidi kufanya JAMII ifikiri wanakuchekea?

  • SI unajua KUKENUA meno labda ni sehemu kiduchu tu ya KUCHEKA?



Tukiachia longolongo hilo,....
.... MHESHIMIWA labda lia tu kama umefanikiwa kujisikia KULIA;...
.... kwa kuwa haki ya nani tena baada ya kulia utajisikia vizuri MKUU.



NI HILO tu MHESHIMIWA , na nakutakia kila la KHERI LEO na ikiwa ni msichana utakaye MTOTO nakutakia kila kheri ili upewe ujauzito leo!

BAADAYE basi BINGWA!
AU?


Hebu Safari Sound Band warudie mkuno-Lala Salama



Au tu Mombasa Roots wanyuke- Mezea tu


Au tu Jean-Claude Naimro atulize



Au tu ngojea Jean-Claude Naimro aendelee tu kunyokolisha

Read more...

Umuhimu wa CHUCHU kwenye TITI.

>> Tuesday, July 27, 2010

Tahadhari: Labda TARALILA hii ina WAZO ambalo halijaenda shule hasa kama UHESHIMIWA wako unakuponza kuchokozwa wazo na UJINGA.:-(








Labda TITI zima halistaili sifa,...
... kama  kishikilia MNYONYO  kwa mtoto ni CHUCHU.:-(



Swali:
  • Si ukifikiria unaweza kuhisi labda MATAKO yanasifiwa zaidi kuliko yastailivyo sifa kama  kaziyenyewe inafanywa na mkundu?
  • Unafikiri CHUCHU inahitaji TITI?
Ndio,...
....labda ni titi ndio sehemu ya CHUCHU kama ukizidisha kufikiria.:-(
Samahani kwa LUGHA na NIMEACHA wazo hili MHESHIMIWA!

Hebu  niwaache MADEMU watatu wanikunao roho..
Nikianza na...
Sheila E ambaye wengi wanamjua kwa kuwa anakaanga chipsi Prince akipiga mziki kwenye ngoma




Au tu Cindy Blackman ambaye wengi wanamjua tu kwa kuwa anampigia ngoma Lenny Kravitz akaange naye chipsi . DUh Santana kamdaka juzijuzi kiuchumba eti.:-(





Au hebu Me´shell Ndegeocello atekenye bezi tena


Au tu Me´shell Ndegeocello aendelee kwenye bezi na vokoz katika mnyokolisho unikumbushao mbali uitwao -Stay



Au tu atoeshule kama wewe unahusudu kujifunza nanihiii



Au tu niachie tu PIA baadhi ya  picha za juzi ya jana...

Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket






Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket




Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP