Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Matunda ya MSICHANA kufanana na BABA na MAFRUTI ya MVULANA aliyefanana na MAMA!

>> Saturday, January 31, 2009

Msichana asemekanaye kufanana na BABA yake na si MAMA, labda ni yule aliyekaa KIJIKEJIKE!

Mvulana asemekanaye kufanana na MAMA yake kuliko BABA , labda ni yule aliyekaa KIDUMEDUME!

Swali:

  • SI inawezekana MSICHANA anafanana na BABA aliyefanana na MAMA yake ndio maana KISURA, na MVULANA anafanana na MAMA kwa sababu kanyoa ndevu?
  • AU?

Mvulana aliyefanana na mama labda ni yule wasichana wanajisahau na kumwita SHOGA wakati wanataka kujua kama chupi imekaa vizuri KATIKA MUONEKANO au pindo za KINING'INIO hazichori ramani za vichochoro juu ya kibwaya au suruali ya PEKOSI iliyobana MAKALIO.

Msichana aliyefanana na BABA labda ni yule WANAUME wanasahau kuwa anafaa katika shughuli za faragha au MCHEZO zilaumiwazo nyumbani kwa akina ZUBEDA kwa kusababisha ZUBEDA ANA mimba.


Swali:
  • Hivi si katika jamii ni ujanja kufumbia macho wasagaji wasiovutiwa kukoboa kama tu mabasha wasiokubali wafanyacho ni usenge?
  • Si unakumbuka kuna VISURA huvutiwa na VISURA na VIJEBA wavutiwao na VIJEBA katika shughuli za NANIHII?


Lakini tatizo la KUFANANISHA linaletwa na KUFANANA tu,
....Ingawa,...
................wakati unafananisha unaweza ukachochea KUSHINDANISHA wafananishwa.


Wakati ukweli ni kwamba,...
... KAMA wewe ni BINADAMU lazima kwa namna fulani unafanana na MTU,
.....na labda ni kweli ....
.... wewe ni binadamu na unafanana na BABA NA MAMA ambao ni BINADAMU kama hupendi jina, WATU .

Na....
...UKIKOSEA na kudhani MVULANA ni MSICHANA, labda kuna mvulana unamfurahisha atambuaye UHENDISAMU ni kuonekana kama mwanamke kama tu yule msichana ajisifiaye kwa kuitwa dume jike kutokana na kujua VIJEBA wanajua kuwa wakiingia kichwakichwa DOZI ya KIPIGO watapata na kujisikia kama wamevalishwa gauni AMBALO sio kama la PADRE, bali kama la MWANASESERE aliyechezewa tayari na hana KICHWA.

Swali:
  • SI kuna wavulana wanaosahau hata mwanamke aonekanaye laini anaweza kuruka KICHWA?
  • Unamkumbuka mtoto mzuri kama msichana wa Kizungu kwa jina la Michael Jackson?
  • Hivi kuna mwiko wa DUME ZIMA kuitwa ZURI na DUME?

NAACHA wazo!
SAMAHANI kwa WAZO lakini!
BAADAYE!
Tutulie na DerrickCOMEDY katika NATIONAL SPELLING BEE[ Tahadhari :lugha si nzuri kwa mtu mweusi na anayependa sehemusehemu za watu wa jinsia moja katika NANIHII:-(]


Nakuacha na MANU CHAO katika - Bongo Bong




Au tu Tevin Campbell alete tena ukubwa katika-Break it Down( Tahadhari:wimbo wa kikubwa kama msikilizaji wa neno)

Read more...

TANGAZO na kijulisho!

  • Malkia, Your once in a LIFETIME INDULGENCE



VISIT THE WEBSITE
Mustafa Hassanali HAUTE COUTURE P.O.BOX 10684, 105 Kilimani Road, Opposite Patricia Metzger health and Beauty Clinic, Next to Embassy of France, Kinondoni, Dar es salaam,Tanzania.
Telephone:+255-76-7303880
+255-78-4303880
+255-22-2668555
Website:http://www.mustafahassanali.net/











  • TANZANIAN SONGBIRD NAKAAYA SIGNED TO SONY MUSIC ENTERTAINMENT


An icon of contemporary Tanzanian music, Nakaaya, has been signed to Sony Music Entertainment. Among the record label’s well-known subsidiaries are Columbia Records, RCA Records and Epic records, just to mention a few.

Nakaaya, who has acquired a large following and growing fan base across the region, now makes history by being the first East African artist ever to be signed to the second largest record company in the world.

The company’s roster includes internationally-acclaimed artists such as Alicia Keys, Beyonce, Britney Spears, Celine Dion, Chris Brown, Sean Kingston and many more.

The signing took place when Nakaaya was attending the "Music’s Relevance in Third World Countries" Conference, in Copenhagen, Denmark, in late 2008. Sony Music Entertainment spotted the Tanzanian artist during an interview with "Deadline," on the prominent Danish television channel, "DR2," and immediately sought to sign her up for a recording deal.

"We are very excited by having signed Nakaaya to our company. She’s an extremely talented artist and we look forward to working with her in the future", comments Peter Groenbaek, Sony Music, on the signing.

After having burst onto the Tanzanian and East African music scene just two years ago, Nakaaya’s popularity and recognition as one of the Region’s top artists continues to grow, and her being signed by a major player in the international music business is a milestone for her career and the East African music industry as a whole. This historic signing is also a testimony to her talent and capability.

The lyrical content of Nakaaya’s music is inspired by social issues that have on-the-ground relevance to Tanzanian, East African and indeed African audiences, with a particular skew towards women and the plights of their everyday lives.
Her musical style is influenced largely by Hip Hop, R&B and some Afro flavour, and is essentially a well-rounded depiction of Bongo Flava.

VISIT the website:http://www.nakaaya.com/

Read more...

Kama BINADAMU atafikiria hata MALALAMIKO ya mbu MJAMZITO , atafutaye PROTINI kwa kunyonya DAMU hata ya MJAMZITO!

>> Friday, January 30, 2009

Na labda Mbu jike tunayempiga na kang'atuka,
...... mchango wa nguvu za mwili katugea.

Katika dunia ambayo wadhaifu hutoweka ,
...... si binadamu wadhaifu wakesho watakao ilea.

Maringo ya viumbe vingine kwa binadamu MHUSIKA,
.......... hakuna kingine zaidi ya chanzo TU cha magonjwa kuenea.:-(

Lakini nguvu ya binadamu kuhimili magonjwa husika ,
................ si huhitaji mazoezi ya kuhimili maradhi yaliyoenea?

Nipe nikupe ni mchezo wachezao WANYAMA na MIMEA husika,
....ingawa binadamu huchukua bila kutoa hata katika KUMEA.

Wadudu, minyoo wapata shida wahangaika,
.......kwa binadamu kuhangaikia kughairi kufa tofauti na mimea.

Binadamu sumu ajifunza kutokuila ninahakika,
............ingawa apulizia SUMU mpaka HEWA.

Alalamika kama vile BINADAMU yamuumizayo kichwa akilalamika,
....... hayasaidii akili au hata umbea.

Yajulikana lakini akili za kijeba zamjulisha kama sio hata ya malaika,
.............basi angalau ajue baada ya YA kutambaa kuna ya kutembea.

Akili zamjulisha mbu AUMAYE ni protini kwaajili ya mimba zimfanyazo anahangaika,
.........zifanyayo DAMU anainyemelea.

Mbu ajishughulisha MPAKA kwenye giza anaimba akishughulika,
......mimba kuilelea.

Cha ajabu binadamu kuhusu ya mbu yanayomshughulisha nauhakika,
........ si ya MBU bali ya MTU kumtetea.

Aua MBU mhusika,
...... kwa kukwepa denge na malaria.

Lakini....

Mnyoo Binadamu amshughulisha kuhakikisha ikibidi anarutubika,
...... ili udongo wa rutuba aendelee kuulea.

Kasitukia kinyesi cha mnyoo aliyeumbika,
.... kwa udongo BINADAMU autegemeao ni mbolea.

Twakumbuka JONGOO na viumbe vingine HUSIKA ,
.....dunia vyailea?


Na kama binadamu DUNIANI ndio kiumbe pekee husika,
........ bila viumbe vingine duniani BINADAMU pekee aweza kuilea?
__________________________________________________________

NAACHA!
NAWAZA tu hapa kuhusu viumbe vingine ambavyo vinalazimika kuishi na binadamu hapa DUNIANI.
Swali:

  • Unafikiria KIBANO na hali ya viumbe vingine zaidi ya binadamu WENZAKO hapa DUNIANI ingawa sisi binadamu wenyewe maisha magumu halafu tunakufa?
  • Si ulishawahi kujiuliza kwanini ni mbu jike ahitajiye damu akupaye malaria?

Tutulie na LABI SIFFRE akisema - SOMEthing inside SO Strong.

Au LABI SIFFRE aendeleze kwa kusema tena -WATCH ME...

DUH!

WikieNDI NjeMa!
Turudi Tanzania kwa PAPI KOCHA na NGUZA VIKING waseme ya mpenzi -SEA

Read more...

KAMA hutamani WAKATI UKO katika MAZINGIRA ya KIBINADAMU yenye vimtamanishavyo BINADAMU!

Labda....
.....Matendo yote afanyayo binadamu ni ya KIBINADAMU hata yale yahusuyo MUNGU yafanywayo na BINADAMU kibinadamu.

Swali:

  • Unafikiri MIJUSI haina dini na haiendi mbinguni?
  • Unafikiri Binadamu anaweza kufanya wafanyayo MALAIKA ?

Pamoja na UBINADAMU ni kuwa BINADAMU, binadamu ana BAADHI ya chaguo la aina ya UBINADAMU afanyao kabla ya kuwaachia walimwengu WENGINE waendeleze na mengine BINADAMU asiyoweza KUCHAGUA katika muda husika.

Labda pia....
....kama Upendo ni sifa ya kimalaika , kuna binadamu wapendao HILI , na kwa HILO wanafanya ya Kimalaika kabla hawajastukia kuna Simon wamchukiaye, tendo ambalo pia ni la KIMALAIKA, lakini la MALAIKA mwovu au kibaka.

Tatizo ni ...
.....matendo mengine yafanyikayo nyumbani kwako WEWE au MIMI sasa hivi wakati tuko sokoni muda huu, HAYO ya nyumbani ndio yametoka kwa muda huu, hayo HAYAFANYIKI mpaka baadaye kwa sababu inamaana katika muda huu tulioko sokoni tunafanya YA SOKONI.

Kuna mengi hayawezi kufanyika ndani ya muda mmoja kwa uwezo wa kibinadamu mwenye kichwa kimoja, na ujanja UKO KATIKA uchaguzi wa BINADAMU MUHUSIKA kuwa uwe JUU ya MTI au CHINI ya mti wakati unakula EMBE BOLIBO litokalo mtini , kama unafanya kihusianacho na MTI hai wa embe BOLIBO au hata NG'ONG'O.


LABDA...
.... tusikie AIBU kwa kutofanya ya kibinadamu wakati WEWE na MIMI ni BINADAMU.
Labda pia hata...
...kama huzini WAKATI UKO katika MAZINGIRA ya kuzini, SIKIA AIBU kwa kwenda kinyume na UBINADAMU ingawa ukifanya ni dhambi!:-(

Na NI kweli pia,....
....kujizuia kufanya vyakibinadamu bado ni UBINADAMU.

Na...
....Binadamu akijizuia kukupa ,inawezekana anafanya tendo la kibinadamu la UCHOYO, ingawa
akikupa YOTEYOTE kwa juhudi bila kuumiza akili, anaweza akaitwa malaya pia.

Swali :
  • Mazingira yako sasa hivi hayakutii majaribu katika tamanio la kibinadamu?

Usionje , SHAURI YAKO!

Naacha!
Mwenzio NAWAZA tu HAPA YA KIBINADAMU usistuke sana!
BAADAYE!

Tutulie na OSIBISA wakija na kibao- WOYAYA

Au Saul Williams ashushe USHAIRI katika - Black Stacey

Read more...

BADO huwezi kuwalaumu BINADAMU wenye nguvu za kiMTU katika kujaribu kumtetea MUNGU!

Bado...
.....UNAWEZA kufikiri BINADAMU huhitaji dini kama muongozo wa kwenda MBINGUNI mpaka ugunduapo jinsi binadamu watumiavyo ZAIDI DINI katika kumtetea MUNGU WAO hata kwa chuki na KUUA labda hata zaidi ya DINI iwafanyavyo wafanye ya Mungu ambayo ni ya UPENDO.
mfano:

  • Umewahi kusikia Ukristo, Uislamu , Usingasinga, Uhindu ,.....au hata Upagani usababishavyo BIN-ADAMU apiganie nani yuko sahihi zaidi ya NINI ni SAHIHI?

Lakini....
.....PAMOJA na uwezekano humuombi MUNGU msaada wakati unaenda kuiba , kuna uwezekano pia hatushukuru MUNGU kwa kutuachia kufanikisha KUIBA na kubakia natulichoiba.
Ndio...
.....BINADAMU ni wagumu kurudisha hata SADAKA walizoiba.

Na...
...kuna wenye kufuata DINI zikatazazo kumtamani jirani yako, wawezao kujaribu kujisahaulisha kwa dakika kadha kabla ya kukiri MATAMANIO au kutubu kuwa NANIHII inatamanisha ,na ikibidi hawasiti kutoa sadaka kwa kutumia walivyoiba.


Swali:
  • Ushawahi kujistukia wewe au mimi binadamu NISIYEWEZA YOTE nikimtetea MUNGU AWEZAYE YOTE?
Au niseme,....
......Binadamu ni MTETEZI kwa AKITETEACHO!

Ni binadamu wachache ambao hata wakifeli mtihani ukawaambia wajitetee kwanini wamefeli wanaweza kushindwa kujitetea hata zile sababu za kuwa sikuwa na kitabu na nilikuwa naumwa kichwa au chini ya KITOVU kidooogo siku ya MTIHANI kama ndio sababu KUU ya kufeli!

BINADAMU ni MTETEZI hata wa maswala yasiyowezatetewa, na akishindwa atakuambia kuwa NIMAPENZI YA MUNGU ndio maana haiwezekani KUTETEA!

Ndio maana hakuna tofauti kama:.....
  • Ukimkuta muhubiri DODOMA karibu na IKWETA anawezakukuambia kuwa ;ikawa usiku ikawa mchana, MUNGU aliumba kitu gani siku ya kwanza .

  • Na mhubiri wa dini hiyohiyo aishie katika maeneo ya kaskazini ya DUNIA ambako karibu miezi mitatu ni giza tupu kila mwaka , ATATETEA maana ya siku kwa kukuambia jinsi gani ; ikawa usiku ikawa mchana, MUNGU aliumba kitu gani siku ya kwanza, wakati siku yake ya mchana au usiku yatofautiana na DODOMA kwa miezi KADHAA ya giza tupu au mwanga mtupu, lakini atatetea BADO SIKU ni SIKU na katika kitabu kitakatifu ataelezea SIKU MOJA inaweza kumaanisha siku elfu moja.

Swali:
  • AU?
  • Unauhakika lakini usemavyo ''TUMSIFU Yesu Kristo ''kuwa Yesu anataka kusifiwa au unatetea sifa?
  • Usemapo MUNGU ni MKUU unauhakika kuwa MUNGU hajui kuwa ni MKUU au unajitetea kwa WATU wakusikiao unasifu na sio unayempa SIFA?

Inasemekana kuwa ni kweli......
.....tusipokumbushana YA MUNGU , ya Mungu husahaulika , ndio maana ni ujanja kwa wapendao kuendelea kuabudu hata MTI kukutana mara kwa mara CHINI YA MTI ili wasije sahau staili za kusujudia MTI.

BASI ngojea tujikumbushe:
  • UNAJUA unaweza ukawa unahangaikia kumtetea MUNGU asiye HITAJI UMTETEE?

Na....
......Kama unanguvu za KIMTU au KIBINADAMU, muombe MUNGU kama BINADAMU na naamini mbele ya MUNGU hakuna MTAKATIFU asitailiye sifa .


Ndio...
... najua kuna dini zishaurizo waumini wake KUMPIGANIA MUNGU na ya MUNGU na hilo sipingani nalo kwa sababu ni juu ya waaminio dini hio ya MUNGU. Ila hakikisha kuwa ni kweli ni MUNGU ASEMAYE umpige BINADAMU MWENZIO katika kupigania ya MUNGU na sio Muhubiri TU wa dini ya MUNGU au ya NANIHII uifuatayo asemaye hivyo nakuhatarisha walimwengu kwa asiyojua na afanyayo kwa kutaka sifa.:-(

CHA kujiuliza tu ni kwamba:
....Unauhakika ni kweli Mungu muweza yote anahitaji msaada wa BINADAMU katika kueneza neno LAKE TUKUFU?

TUBU au MUOMBE MUNGU WAKO usipotoke lakini!
Niombee na mimi kama sio MVIVU au kama nakukwaza kwa kutaka sifa!

PAMOJA na yote,.....
...... kuna BINADAMU anaye MLAUMU binadamu ajaribuye kumtetea MUNGU wakati ya MUNGU ni fumbo na adaie anajua jibu LA FUMBO labda afanya hivyo bila kujua fumbo kwa kutaka sifa?


BAADAYE!
NAWAZA tu hapa MKUU na MUNGU yuko MAWAZONI leo hii!
Tubadili HALI YA HEWA na kuwapata ZE COMEDY katika.....


Au tujivunie tu TANZANIA....

Read more...

Kama PENZI limekufa ,HUWEZI lifufua MOCHWARI!:-(

>> Thursday, January 29, 2009

Kama Mapenzi hufa,
............kabla ya kuzikwa labda yako MOCHWARI.


Maiti kabla haijazikwa bado imekufa,
.........kabla ya GEST-KABURI hupelekwa MOCHWARI


Na penzi huanza kufa,
.........pale wapendanao WAPUMZIKAPO kwa kudhania mambo yako shwari.


Kama unaPENZI ndio mwenye penzi liwezalo kufa,
......kwa kujisahau kulihudumia, usishangae kulikuta MOCHWARI.


Hivi twasubiri mpaka UMATI ujue penzi limekufa,
.......ndio tujifanye kupeleka penzi gereji au tuamini mambo si shwari?


Tibu penzi wakati lina dalili ya kifafa,
....... halitibiki tena kama lishafika MOCHWARI.
---------------------------------------------------------------------------------
Swali:

  • Si unahitajika kuwa na MPENZI kabla ya kuachana na MPENZI?
  • Si inawezekana hukuwa na MPENZI wakati unafikiria kumuacha MPENZI?
SIKU NJEMA!
NAWAZA tu MKUU!
Nakuacha na ISLEY Brothers wazungumzie penzi .....(tahadhari:wimbo wa kikubwa)

Read more...

TANGAZO: Fest Africa Winter Jam 7.2.09 @ Klubi (Tre)‏

FEST AFRIKA WINTER JAM ( The only African Festival )
SAT:07.02.09 @KLUBI-TAMPERE TIME: 20-04

PRESENTS TO YOU:

JAH KIMBUTE-REGGAE(Live band-Tznia)
TABIA MWANJELWA-AFRO RUMBA(Live solo-Tnia based in Germany)
THE NGOMA AFRICA BAND&RAS MAKUNJA-(Live band-Tnia+Congo)Afro beat,ndombolo,Zuku and much more
TOOTHPASTE BAND-WORLD MUSIC
THE MPONDA´S-DRUMING&BODY MOVEMENTS

DJ´S
George-MTV,NESTAR,JAHGUN-Bongo&ALTUNES

Tickets 10€,advince at Klubi,Swamp Music&Epe´s

YOU ARE MOST WELCOM!!!

MENARD AND THE CREW

Read more...

Kwani UNAFIKIRIA unavyokojoa WAKATI UNAKOJOA?

>> Wednesday, January 28, 2009

WENGI tu ni WATAALAMU wa kujilaumu badaye kidogo BAADA ya kufanya JAMBO wakati ni kawaida kwa jambo kutofikiriwa sana wakati JAMBO LINAFANYIKA.
Swali:

  • Si ni kawaida kwa MTAALAMU kufikiria KUNYA kabla ya KUNYA na si wakati ANAKUNYA?
  • Kichambio si ni muhimu baada ya kunya NA hakifikiriwi sana kabla ya faragha?
(Samahani kwa lugha chafu na naahidi kujaribu kuifua iwe safi siku nyingine)

NA...
... Nikawaida kujikuna KIPELE bila kufikiria tunajikuna kipele kama shughuli yenyewe ni KUFINYANGA TONGE la UGALI.

KAMA...
...shughuli ni kusubiri JAMAA litoke MSALANI , labda hatufikirii tunavyosubiria JAMAA LITOKE CHOONI wakati shughuli yenyewe TUILENGAYO ni HAJA NDOGO, au kwa lugha ya kigeni KUKOJOA:


Swali:
  • SI mwenye NJAA wakati anakula anaweza kuwa anafikiria ALALE WAPI?

NAACHA!

Tupumzike na WATAALAMU WA MATUSI mtandaoni watuimbie madhumuni ya mtandao.(USIANGALIE au kusikiliza kama UTAKWAZIKA)...

AU tuwasikilize washabiki wa YESU katika.....Yesu kele Nzambi...

Read more...

UMEJIULIZA ukweli wa WASEMAYO wamjuaye MAREHEMU baada ya MAREHEMU kuwa MAREHEMU?

WOTE tunajua ni UUNGWANA au KAWAIDA kwa wahudhuria MSIBA kusema MAREHEMU alikuwa MTU mzuri.

Lakini....
... kuna WAJUZI wadaio kumjua MAREHEMU kwa kuwa walikuwa naye SEBULENI ,wasimuliao MPAKA jinsi WALIVYOMJUA MAREHEMU chooni ambako hawakuwa naye.

Na...
... pia kwa sababu MAREHEMU alikuwa na DODOKI bafuni, kuna WADAIO KUJUA au wachukuliao kuwa ni kweli MAREHEMU hakuwa na UKURUTU kwenye NYETI katika simulizi zao hata ambazo MAREHEMU angechukulia kuwa ni simulizi za ishu NYETI.

Labda ni kweli .....
....TUJUACHO ambacho NI KWELI, ni kwamba MAREHEMU alikuwa MTU ingawa LABDA HATA hatukusikia akiJAMBA!:-(

Swali:

  • Kama unaogopa MAITI unauhakika MAREHEMU alikuwa MTU mzuri?
  • Unakumbuka labda leo kabla hatujanya NINA WEZA au UNAWEZA kufa?
  • Wakati uko hai hujawahi kufa MOYO?

Kwa bahati mbaya....

......MAREHEMU akifanikiwa kuwapa uhakika washabikiao MAREHEMU msibani kuwa MAREHEMU amekuwa MAREHEMU , marehemu HANA KAULI yakujitetea ingawa bado MAREHEMU ana UJUMBE.

Kama unamjua MAREHEMU, marehemu bado anasema na anakupa au ananipa UJUMBE ingawa ni MAREHEMU.

INAWEZEKANA...
...labda Marehemu anaweza kukukumbusha MPAKA kuhusu alivyotoa au ulivyotaka akutoe BIKIRA hasa kama ndiye yeye aliyekuwa chaguo LAKO au hata kama pia ndio yeye ambaye HAKUWA chaguo LAKO la KUPULIZIA KIDONDA.

Swali:
  • SI unakumbuka si wanawake tu wenye BIKIRA?
  • Kama wewe ni MTANZANIA , hivi MAREHEMU NYENYERE , samahani NYERERE, hakukumbushi Tanzania haina DINI ingawa ni Marehemu?


NA ...

....kama WEWE au MIMI ni mpenda KUSIKILIZWA , tunaweza KULAZIMISHA tusikilizwe hata MSIBANI ingawa tuongeayo hayahusiani na Marehemu.

NA...
....STAILI yako au YANGU yakuzungumza kwa MAJONZI inaweza KUSABABISHA upendwe au kupewa SENENE waliotunzwa kwa ajili ya WAHESHIMIWA msibani.:-(

Na ni kweli...
...Pamoja na wote wenye simulizi TAMU au CHUNGU kuhusu Marehemu MSIBANI au NYUMA ya CHOO , .......HAKUNA AMJUAYE MAREHEMU kama marehemu alivyomjua MAREHEMU.

Swali:
  • Au unafikiri unamjua MAREHEMU?
  • Unauhakika UNAJIJUA?

NAACHA!
KUMBUKA NAWAZA tu HAPA!:-(
ISHI ingawa kama unaishi si lazima ni kwa sababu ni kweli WEWE au MIMI ni BINGWA wa kuwa HAI:
JAMBA basi uhakikishe kama UKO HAI!

SIku njeMA !

Ngojea HOMER SIMPSON ajaribu kubadilisha HALI YA HEWA katika BEER SONG.....


AU ngojea RED HOT CHILI PEPPERS waendelee kubadilisha hali ya HEWA.. katika DANI CALIFORNIA


AU CULTURE wamalizie kusema nijitahidivyo kueleweka ingawa sieleweki katika shoo yao ya South AFRICA katika - I TRIED....

Read more...

Starehe ya KUJISIKIA NAFUU ukiungwa MKONO!

>> Tuesday, January 27, 2009

KUBISHIWA nishai kama hujui!

Kubishiwa kwaweza kukujulisha kuwa ni kweli unajua .

Kama hujui...

Unaweza ukabisha ili ujulishwe usichojua.
Unaweza pia ukabisha na kuachwa hujui!:-(

Kuna wajuao wasiojua kujieleza NIKIBISHA wananiacha nifikirie hawajui.

Lakini.....
Pamoja na UBISHI, mwenzio sijui!
Nikikuunga mkono, kumbuka labda ni kwa sababu SIJUI!:-(

Swali:

  • Wewe unajua?
  • Wajuao hujisikia pia nafuu wakiungwa MGUU?

SIKU NJEMA!


Ngojea Malcom X aseme : Who Taught You To Hate Yourself?


AU mwanafunzi wa Malcom X ambaye baadhi wanamlaumu kwa mauaji ya Malcom X kwa jina Farrakhan aseme katika Charges of anti-Semitism ....


Au tu THE ARCHIES wabadili hali ya hewa kwa kusema- Sugar Sugar...

Read more...

Kwa jina la WAZIRI MKUU , waganga wa KIENYEJI TOKA!

Tokea enzi za kale mpaka leo kulikuwa na USHIRIKINA na UCHAWI na huwezi kuuUA ushirikina au uchawi kwa kutunga sheria.

Palipo na USHIRIKINA na UCHAWI , waganga wa KIENYEJI wana nafasi yake hata kama HUTAKI
.
Na ukweli ni.....

.....katika TANZANIA ,ushirikina na uchawi kama vile tu UDINI , uko kwenye chati.

Swali:

  • SI mpaka leo uchawi unavutia ndio maana kitabu cha HARRY POTTER mtoto mwenye nguvu za kichawi, ndio maarufu kuliko Biblia na Korani katika nchi zilizoendelea?
Kwa nia njema...
...kuna wasemao pia ;'' KWA JINA LA YESU shetani TOKA''!
  • Ingawa inasemekana shetani hao huwa hawatoki kama utolewaye shetani huamini ya mtoa shetani.

Na ..
...kuna watumiao KORANI kusomea mtu ALBADILI katika kufanikisha.

  • Ingawa bado Wayahudi wanaendelea kuwapo na kuendeleza !

Mauaji ya Maalbino na wakongwe kwa sababu za kishirikina yanasikitisha sana!

MAUAJI ya MAALIBINO na WAKONGWE JICHO NYAYA ,inabidi yapigwe vita sana !
  • Na tusipoangalia NA kwa kuingilia SHUGHULI kichwakichwa ,haya MAUAJI YATAENDELEA KUWEPO kinamna .

Ila....
... naamini Maalbino hawajaanza leo kuuawa.:-(
Kama unakumbuka vizuri na ni kijana wa zamani, utakumbuka ilikuwa kawaida kabisa kwa watu wengi kuamini Maalbino hawafi ila wanapotea tu . Pia mpaka kulikuwa na waaminio hawapigiki picha.

Nakumbuka pia mpaka kuna watu walikuwa wanabishana kuhusu kama kuna mtu kaona kaburi la albino sio miaka mingi iliyopita. Hili ni jambo nalolisema nikiwa mimi mwenyewe MSHUHUDA wakusikia kwa masikio yangu watu ambao wanaelimu zao wakibishana kuhusu hili jambo.

Hii inaonyesha jinsi gani Watanzania wengi hatuwaelewi ndugu zetu Maalbino na sio tu Waganga wa kienyeji ambao tunawalaumu ndio WANASTAHILI KULAUMIWA.

Na...
.....Mganga wa kienyeji hawezi kufanikisha kitu kama sisi wateja tunaelewa nini kinaendelea na tunawaelewa ndugu zetu Maalbino na Wakongwe JICHO NYANYA .


Haiwezekani kufuta waganga wa kienyeji wakati jamii ukijumuisha na viongozi wenyewe ambao wanatakiwa kusimamia ufutaji wa waganga wa kienyeji, wana aamini katika waganga wa kienyeji.

Ukiwanyang'anya vibali waganga wa kienyeji, unachofanya ni kuwafanya waendeshe shughuli zao chini kwa chini kwa sababu wateja wapo.

Na kama unakumbuka.....
.....Uchawi na taaluma ya uganga wa kienyeji ni moja ya vitu tokea enzi hizo vimeshamiri na hushamiri zaidi chini kwa chini .Ndio maana mpaka leo bado tupo tusiojua kuruka na ungo.


Naelewa kuwa WAZIRI MKUU anasema waganga wa tiba ya jadi ambao wataweza kuhakikishia wanataaluma kuwa wagonjwa wao wanatibika watarudishiwa leseni.Lakini tukumbuke tu kuwa kuna watu wengi wanaugua kisaikolojia tu hata katika hospitali zetu za KWAIDA , na afanyacho mganga WA KIENYEJI kama MGANGA HOSPITALI FULANI ni kuwapa nguvu tu WAGONJWA. Nguvu ya kujiamini na NI kwelikweli KUNA WAGONJWA WENG TU warudipo nyumbani,SHUGHULI itajipa na Zubeda mwenyewe MIMBA ataipata kutokana na nguvu mpya na hari mpya aliyokuja nayo Simon Kitururu iliofanikisha mbwembwe za Simon Kitururu mdogo abanwe na chupi kabla yakuonyesha maringo yake.

Nachojaribu kusema ni;.....
.....''Kwa waaminio Mganga wa kienyeji , Mganga wa kienyeji anaponya kama TU katika waaminio maombezi Kanisani kuna watakaoshuhudia wamepona ''.


Tatuzi la swala hili zima ni elimu.

Tatizo la elimu yetu Tanzania, maswala kama haya hayafanyiwi utafiti wa kitaaluma na Vyuo Vyetu Vikuuu au hata Vyuo Vyetu Vikuukuu ili kuwa na njia iliyotafitiwa kitaalamu ya kutatua swala.Matatizo yetu katika jamii yanarukwa na elimu yetu na hata sheria zetu zenye misingi kutoka kwa elimu na sheria za kikoloni na labda zenye uhusiano na matatizo ya nchi za nje kuliko matatizo ya nchi yetu.

Kama dawa itakuwa kama aliyoshauri Waziri Mkuu PINDA kuwa auaye auawe bila kufikishwa Mahakamani, kuna watu ambao watauawa kwa kusingiziwa kisivyo halali .

Na...
....Vitendo vya kuua au hata kubagua Maalbino na Vikongwe ni vitendo vya kinyama .
Na...
....Vitendo vya kujichukulia sheria mkononi na kuua binadamu yoyote kwa kuhisi yeye kaua na labda kasingiziwa ni vya KINYAMA pia.

Ni jukumu la kila mtu kuelimisha jamii na sio kukuza CHUKI.
Vitisho sio dawa kama atishwaye kwa sheria anaogopa zaidi uchawi.


Swali:
  • Unafikiri ni wanasiasa wangapi maarufu ambao ni wateja wa waganga wa KIENYEJI?
  • Hivi wewe haufai kuuawa?


NAacha!
Na NAWAZA tu hapa MKUU!

Au ngojea tujifunze historia ya Marekani kwa mtazamo fulani.....katika AMERICAN HISTORY


Au tu Dru Hill waseme.....HOW DEEP IS UR LOVE

Read more...

LABDA shetani ASIFIWE!

>> Sunday, January 25, 2009

Pamoja na yote....
Labda shetani asifiwe kama:...

  • Waaminio MUNGU wanafanya ya SHETANI.
  • Kwa waaminio MUNGU , vitamu vingi kama sio VYOTE ni vishawisi na nyuma ya YOTE unogewayo ya kidunia kama NANIHII au labda MBATATA, ni propaganda za SHETANI.
  • MUNGU wako waupendo anasababisha UMCHUKIE aaminiye MUNGU KWA STAILI TOFAUTI NA YAKO ya kumtukuza MUNGU.
Swali:
  • Unadhani wasiojua MUNGU wanamatatizo na SHETANI umjuaye?
  • Kwanza unamjua SHETANI?
  • SI waaminio MUNGU ndio wajuao kuna kitu kinaitwa MUNGU au SHETANI?

Unaweza kubisha !

Lakini...
.... labda SHETANI ASIFIWE kama:

  • Wanasiasa uwaaminio wanaapishwa kwa vitabu vya MUNGU na wanafanya ya SHETANI kwa kuiba na kutojali WANA watesekao wa MUNGU.

  • WEWE uaminiye MUNGU unakwazika na mimi BINADAMU hata LABDA kwa HATA kuongea niongeacho,na badala ya kufikiria MUNGU unachukia, unakasirika , unataka kugombana au unakumbuka maswala ya kishetani zaidi ya YAMUNGU kwa sababu unanichukia.

Swali:
  • Hivi unanichukia?
  • Wakati unamuamini na kumuabudu MUNGU, unafikiri SHETANI pamoja na mafanikio yake yote yakukudaka na KUNIDAKA mara kiduchu nakadhalika, hasitahili SIFA?
  • Unafikiri mpaka JUMAPILI hii ni SHETANI au MUNGU aliyefanikiwa kukudaka MARA NYINGI?

TUBU kama unahisi mrembo SHETANI bado anakuvutia zaidi kidogo ingawa unaongea ya MUNGU.

Kaza BUTI katika ya MUNGU kama UNAAMINI MUNGU na unataka usidakwe na mtoto wa mjini a.k.a SHETANI.

Niombee kama nakutia majaribuni au unahisi nimepotea zaidi kuliko wewe na nahitaji KUOMBEWA!

NAACHA!
Bwana , Bibi na MTOTO wasifiwe!
jumAPIli njeMA!

Niko katika JAZZ na Bongo Flava ya SOMALIA Mukichwa!
Tulia basi na DUKE ELLINGTON katika shoo yake ya mwaka 1942 katika C Jam BLUES...

AU twende tu SOMALIA kwa K'naan katika kibao -SOMALIA

Read more...

UNAUHAKIKA kwanini UKO MTANDAONI kwenye kurasa za AJABU au za busara SASA HIVI au SASA ya BAADAYE?

Unauhakika una marafiki wakutosha watoshelezao NANIHII au kona zote za NANIHII na AMBAO ukitaka unaweza HATA kuwagusa au kucheza UNGEDERE au UTUMBILI na kuwakagua CHAWA ukitumia vidole au NANIHII?

Labda...
... wenye marafiki sasa hivi ambapo wewe na mimi tuko MTANDAONI ni wale wamaliziao kutengeneza mtoto au BADO wanacheza KIKUBWA au KITOTO.
Swali:

  • Unafikiri ni kwanini katika mambo yote BIN-ADAMU awezayo kufanya sasa hivi MIMI , WEWE au YULE labda bado tuko MTANDAONI na LABDA si kikazi na SI kikuwa na MArafiKI?
  • Hivi wewe unahitaji marafiki kila wakati?
NAACHA!

Hebu Homer Simpson alainishe kwa msaada wa Sisqo katika kusifia tena chupi....


Au tu Barrington Levy asifie UA ROZI BUSTANINI kama unaamini anaongelea UA katika -Black Rose....

Read more...

UDHAIFU wa BLOGU uipendayo ni; UNAIPENDA!

>> Saturday, January 24, 2009

Usichokipenda LABDA ni shule zaidi ya UPENDACHO.

Tatizo ni...
.... binadamu si wavumilivu katika KUCHUJA NA KUDAKA MAZURI KATIKATI YA MABAYA.

Kizuri jujuu hukimbiliwa ndio maana UTUMBO husamehewa kwa mpenda nyama ya utumbo hata kama bado kwa ndani UTUMBO una chembechembe za mavi. (Samahani kwa kutamka tusi a.k.a mavi. Namaanisha kinyesi)


Tunadakwa na tufikiriayo ni mazuri hata kama kwa ndani ni mabaya.

Ukipenda unaweza kusamehe UDHAIFU.
Ukichukizwa na kitu , INAWEZEKANA kuna kitu utakikosa cha muhimu katika kikuchukizacho.

NA ni kweli....
....Labda kikuchukizacho kuna kitu kinagusa ndani yako na inawezekana kinagusa kaudhaifu kako maeneo.

Swali:

  • Kwani kuna kitu ukipendacho kisicho na udhaifu?
  • Unauhakika MUNGU hana udhaifu au umehakikishiwa TU na wahubiri kuwa Mungu anaweza yote na hana udhaifu?
  • Katika maisha usiowapenda sio MUHIMU?
  • Unauhakika uko kwenye BLOGU ikuhusuyo?


NAACHA!
Samahani kama nimekukwaza!:-(
NAWAZA TU HAPA MKUU!
NAKUTAKIA mafanikio chooni leo!

Tutulie na EDDY MURPHY aongelee ya Rais wa kwanza mweusi Marekani.....(Usisikilize kama unakwazika na lugha za sehemu za siri:-()


Au tutulie na IVOR Biggun katika wimbo Msichana wangu ana paka...(usisikilize kama utakwazika)...


Au nimuachie Zain Bhikha featuring Dawud Wharnsby waseme -ALLAH KNOWS...

Read more...

TUMAINI LA KESHO lisilo NA uhakika, baada ya YAJANA tusiyoyakumbuka kwa UHAKIKA !

KUNA wafikiriao wanauhakika na yaliyopita wakati ya leo yanapita bila UHAKIKA.

Wote tunajua ya kesho hayana UHAKIKA.:-(

Kuona ya LEO ni TAALUMA ikiwa labda leo hata sehemu zako nyeti hujaziangalia kwa UHAKIKA.

Katika kujaribu kufikiria ya jana, unaweza usikumbuke kama ulimfurahisha mpendwa, adui au hata MUNGU kwa UHAKIKA.

Wakati ya jana tuyakumbukayo YANAHESABIKA, labda ya leo tumeanza kusahau hesabu zake NAHAKIKA.

Na pamoja na kuomba MUNGU , mwenzio hata ya KESHO kuhusu mimi na wewe sina UHAKIKA!


Lakini.....
....NAKUTAKIA KILA LA KHERI Mdau NA Adui na kwa hilo NINAUHAKIKA!

SIKU NJEMA!

Tutulie kwa kupata mtazamo wa Rashid Bhikha featuring Abdul-Malik Ahmad katika BANGI na Madawa ya kulevya.....katika Can't U see?


Au tupate mtazamo mwingine wa BANGI kutoka kwa Daddy Rings & Cocoa Tea wakisema- Herb fi bun


AU tu tupate mtazamo wa chupi kutoka kwa Sisqo....katika Thong Song

Read more...

Weka AKIBA ya MAUMIVU NDANI YA ROHO kwa KULIA kwa MADOIDO!:-(

>> Friday, January 23, 2009

NI BUSARA kwa ajisikiaye kulia , KULIA.

KULIA ni muhimu ingawa kwenye FASHENI ni KUCHEKA NA TABASAMU ambavyo viko kwenye chati.

Na,...
...KICHEKO na TABASAMU vyaweza kusifiwa zaidi MPAKA kwa kusaidia kuamsha MSHAWASHA wa liMTU kukustukia UPO,mwenye tabia fulani kufikiria kama UNAFAA kulawiti au KUKUPENDA tu kwa mvuto wako wa DIMPOZI zako kwenye SHAVU la kumimina wakati unakenua meno kwa kufurahia zaidi KIDOGO ya wakati UNALIA ingawa unavutia UKILIA.

KULIA ni bomba la shoo!
Unaweza kupata UMAARUFU kwa jinsi uliliavyo pipi au uliavyo msibani.

Ila,...
....KULIA PEKE YAKO ni muhimu zaidi ya kucheka peke yako.

AJALIYE jinsi AONEKANAVYO akilia, atafanikisha kuchelewesha kupunguza maumivu ya roho YALIZAYO.

Katika fasheni za kulia,...
... ..kuna vikorombwezo na MAZAGAZAGA kama vile ya...
............kuongezea MSISITIZO wakulia kwa kutoa kamasi, kujamba kidogo au kuongezea na chachandu ya KWIKWI kwa mbaaaaali, viwezavyo kukusaidia KUPAMBA jinsi ya MUONEKANO WAKO UKILIA.

Lakini.....
...... wakuonao ukilia pamoja na kujisikia vibaya au vizuri kwakua BINGWA unalia, LABDA MISINGI YA MAUMIVU bado iko ndani yako uliyeanzisha KULIA.

KUNA wajaribuo PIA kuchanganya kulia na kucheka katika jitihada za KUTUNZA MUONEKANO, kitu ambacho MARA ZOTE hufanikisha utengenezaji wa sura ya TISHA TOTO.

Labda....
.....LIA kama unajisikia KULIA hata kama ni mbele ya WATOTO ambao labda watalia wakikuona unalia.

Kuwaliza watoto kwa kuwa unalia , inaweza kuwasaidia KUKUA wakijua kuwa kulia ni kitu cha kawaida na labda watakua bila kufanikiwa kutunza maumivu ya moyo kwa kukwepa KULIA.

Kulia ni bomba la KAULI isemayo na kufikisha ujumbe kwa NGUVU zaidi ya MLIO.
Swali:

  • AU?
  • Katika UTANI , ukimtania mtu ni lazima uwe na wasikilizaji?
NAACHA!

AU ngojea tupumzike kwa kumuangalia Bill Clinton akiwa inspired KULALA na Martin Luther King Jr......


Basi Mkuu, ngojea tu Mr Nice aseme katika - RAFIKI
WIkienDI NjeMA!

Read more...

BINADAMU katikati ya MAPENZI ya PUA NA KAMASI!

Labda SI kitu rahisi kuwa PUA au KAMASI.
Masikini PUA mpaka HUBINYWA atoe KAMASI.

PUA, pamoja na yote , ni nyumba ya KAMASI...
....ingawa mwenye MAFUA pua haina krisiMASI.

Kwa WALIMWENGU wasiothaminisha PENZI kama tu wathamanishavyo KAMASI.......
......Pua ni TUNDU la kupumulia na si nyumba ya KAMASI.

Kama kupumulia PUA ni muhimu kwa PUA kuliko KAMASI,.....
....apumuliaye MDOMO hapendwi na PUA yenye KAMASI.

Pamoja na yote....
....Kitu cha tatu AMBACHO NI MTU ndio KIINGILIACHO PENZI la pua na KAMASI.

....Kitu cha tatu hiki HUINGILIA hata PENZI LA BINADAMU wawili wapendanao kwa sababu wako nasi na hawana KAMASI.


Katika wawili WAPENDANAO kama pua na KAMASI....
.....Ni MIMI au WEWE tumpengeshaye mmoja PENZI lake kwa mwenziye na kulitoa kama PUA kutoa KAMASI.
PENZI lao likiisha na chuki kunawili, bado twajifanya tunashughuli na hatutaki wale nasi.

Kama WAWILI wamependana kama PUA na KAMASI......
....Kwa nini tusihemee mdomo na kumuachia pua KAMASI?

----------------------------------------------------------------------------------

Nawaza tu MKUU na NIMEACHA!
Swali:

  • Unakumbuka penzi lako na mpenzi linaweza kufa kwa msaada wa mtu wa tatu asiyehusika katika shughuli zako na PENZI?

  • Ushawahi kuwa na hamu ya kupata mafua ili ufanye mazoezi ya KUPENGA?


Au kama unamuda, mpate ZE FRANK azungumzie tukutananayo kwenye WEB katika jitihada za kuchekesha ingawa sina uhakika kama inachekesha ,katika What's so funny about the Web?....


Au mtoto anune....

Read more...

KUNA kipele MWANAWANE!

>> Thursday, January 22, 2009

LAKINI kabla HUJAKUNA,.....
Swali:

  • Ushawahi kukuna KIPELE?

Labda.....
..... KIPELE kimenuna!

Labda....
....KIPELE kinajipendekeza machoni mwako kwa kukununia!


Ukikiangalia vizuri KIPELE, unaweza mpaka ukakistukia kimekukodolea kwa jicho jekundu!

Na unaweza kukikomoa KIPELE kwa kutokiKUNA au kutoKIBINYA ingawa kinawasha.

Na .....
...baada ya kukishikashika ,
..........UKIKIBINYA KIPELE kilicho kununia, kinaweza kukuharishia ujiuji wa rangi ya CHAI YA MAZIWA.


DUH!

LABDA ....
.....KIPELE kama MAISHA , inabidi tufikirie kwanza kabla ya KUKUNA ingawa muwasho unatoa dondoo kuwa JAWABU la tatizo la KUWASHWA ni KUKUNA !

Inawezekana kabisa pia KIPELE kitapona tu chenyewe kama kilivyo jileta tu chenyewe maishani mwako bila kukihitaji kama vile tu ukurutu wako au wangu ujiletavyo wenyewe, kisa UVIVU wa kusugua MGONGO.


Tatizo ni....

....katika maisha kuna tunaodhani tunalazimika kuharakisha kuamua TATUZI la tatizo ni nini.

Labda kwa wengi ...
.....SABABU ya kuchukua hatua ya kutatua TATIZO ni hali tu ya kujisikia kuwa unaTATUA na sio kweli KITENDO kichukuliwacho katika kutatua ni kweli TATUZI.

Na katika KIPELE hiki labda TATUZI sio kukuna ingawa ndio UAMUZI wa MWANAWANE alioufikia , bali tatuzi NI kukiachia KIPELE kionyeshe maringo yake ,KIIVE na KUCHEUA chenyewe asali-usaha au KICHEUE kwa msaada wa MBINYO.

Tatizo ni....
.....uamuzi katika jinsi ya kukiliwaza KIPELE au MAISHA ni lazima uchukuliwe,
......INGAWA pia,kutochukua hatua yoyote pia ni UAMUZI.


Katika HADITHI hii,....
......HAPO zamani za kale mpaka leo kulikuwa na KIPELE.

Na labda katika hadithi hii.....
..... SI lazima UKUNE au KUBINYA kipele kama TATUZI ingawa KINAWASHA .

Swali:

  • Si unakumbuka kubinya kipele na ngono vyote hutatua haja za aina moja kwa binadamu katika harakati za kutafuta kauAHUENI?
  • SI tunakumbuka kuwa hatuhitaji KIPELE ili KUJIKUNA?
  • Si tunakumbushwa, binadamu huweza kujitengenezea KIPELE?

NAACHA!
NAWAZA TU MKUU HAPA!

SIku njeMA!

TUTULIE kwa mara nyingine na MBILIA BELL & AFRISA wanisaidie katika- La beauté d'une femme

Au tu mwanadada mwingine au JANET JACKSON amalizie kwa - That's the way love goes

Read more...

TANGAZO:Mchango wa MSIBA!

>> Wednesday, January 21, 2009



SALAAM,
DEVELOPMENTS YA MIPANGO YA MAZISHI TAMPERE 24.JANUARI 2009 ya Mtoto mpendwa wa Calister Kagali, baby Abigail Marja.

Account ya mchango wa msiba ni LINUS KAGALI 139535-114611 Nordea.
WASALAAM

Read more...

PONGEZI Barrack OBAMA ingawa tupo WATAALAMU wakunogewa wakati CHUNGU!

>> Tuesday, January 20, 2009

Tunaishi katika dunia ya mshindi kusifiwa ingawa aliyeshindwa hajakatwa makende !

Tunaishi katika dunia ambayo hata TUSIMULIWAYE kwa umaarufu wa KUPENDWA hawezi kutembea bila kulindwa asiuawe na binadamu wajisifiao kuwa sio wanyama na wenye busara kuliko Kuku mzazi achungaye vifaranga.

Binadamu wavaao nguo kusitiri nyeti kwa sababu wanatunza utu, huweza kumcheka nyani-MNYAMA ambaye bado hajastukia fasheni za vibwaya au busara za kumvalisha pete mchumba Ngedere wakati wakimuua mpaka NABII ISSA a.k.a YESU kwa kosa la kuhubiri UPENDO .

Binadamu kiumbe wa ajabu na anakatisha tamaa wakati mwingine!:-(

Labda tuendekeze udhaifu wa kibinadamu kwa;

  • Kunogewa na tamu ili itusaidie kukabili chungu.
  • Kuhitaji kiongozi ilitumfuate bila kuhoji.
  • Kumsifia Rais kwa hotuba ASIYOANDIKA na iliyoandikwa na muandika hotuba tusiyemjua kwa jina ambaye hatumpendi.
AU...
  • Tuchunguze hali halisi ya uwezo wa binadamu na kutomzidishia sifa binadamu zikazidi sifa za binadamu.
  • Tuhoji mchango wetu katika jambo tuhitajilo KIONGOZI

Lakini labda....
.....t
uwe na matumaini tu kuwa inawezekana ingawa ngumu!
Na kwa kuwa LEO NI SIKU YA OBAMA kuapishwa URAIS;
  • NA TUWE na matumaini basi kama OBAMA aletavyo MATUMAINI!

Asante OBAMA kwa kuleta matumaini kuwa inawezekana!
HONGERA OBAMA!

Tutafika tu INGAWA hali halisi CHUNGU ingawa tunahangaikia KUNOGEWA kwa kujaribu kukwepa MACHUNGU kwa sababu kwa muda angalau mfupi INANOGA!

Swali:
  • Huhisi RAIS Mugabe wa Zimbabwe pamoja na Marais fulani .....hawahisi RAIS Bush ni mjinga kwa kuachia ulaji Marekani?

NAACHA!

---------------------------------------------------------------------------------
Tutulie kidogo na kujikumbusha waliomdharau OBAMA kama katika hotuba ya Rudy Giuliani ionyeshavyo.


Tufikirie na THE LAST POETS waongelee WHEN REVOLUTION COMES....


AU tu tufurahie pamoja na COCO TEA akiimba Barrack OBAMA....


SIKU NJEMA!

Read more...

KAMA kuna umpendaye, UNAUPENDELEO weye!

Ni kweli kwako au kwangu .....
.....BINADAMU hawako sawasawa kama unahisi kuna UMPENDAYE!

Kama kuna umpendaye , basi kuna umchukiaye.
Swali:

  • Kwa asemaye hanachuki na mtu kajuaje anapenda watu wote na sio kuwachukia watu wote kama kwake binadamu wote ni sawa?
  • Kama unampenda mtu inawezekana unajua HIVYO kwa sababu unamchukia mtu, na chuki si ni dhambi?[shauri yako , unaweza kushindwa kwenda kunywa togwa mbinguni kwa sababu ya dhambi!:-(]

Labda...
....hakuna usawa katika binadamu ndio maana unastukia kuwa katika BINADAMU kuna UMPENDAYE!:-(

Unaweza kujisikia mpaka kumpa KIDUDE umpendaye UMPENDELEAYE asiye hitaji kidude chako na kumruka ahitajiye kidude chako ambaye angekiliwaza kidude ingawa ndiye AMBAYE hajabahatika kufarijika na wako UPENDELEO.

Chakushangaza...
.....katika binadamu apiganiaye USAWA, hakawii kujihifadhia AMPENDAYE kwa kuwa ANAMPENDELEA kwa UTOFAUTI WAKE asemao ndio kidaka pendo ambacho ananyimia nyie wengine KUGAWIWA kwa sababu ni wake MPENZI na ni chake kidude!:-(

Ni kweli....
....WAPENDAO, sifa yao kubwa ni UCHOYO wa kumgawia mtu mwingine WAMPENDAO au kidude wakipendacho.

Labda...
....kama unagawiwa kidude umo miongoni mwawapendelewao katika dunia hii isiyo na USAWA.

Swali:
  • Kwani hujui KUNA WADAIO katika binadamu hakuna upendeleo katika kugawiana kidude kwa sababu WOTE tumeumbwa kwa mfano wa MUNGU?
  • Ushawahi kunyimwa kidude cha kuchezea?
Tatizo ni.....
.....labda ukimuondoa Mungu wa upendo ACHOMAYE au kukupa MBINGU, ampendaye na amchukiaye BINADAMU mkubwa ni BINADAMU.
Na labda....
......aninyimaye KIDUDE ni BINADAMU niliye mnyima KIDUDE!

Na tukumbuke tu kuwa....
......umuhimu wa vidude kibao ni wa muda mfupi tu, na wote tutakufa baadaye kidogo na kuacha au kuoza na vidude ambavyo labda tusinge kuwa na UPENDELEO labda vingekuwa na manufaa zaidi au vingetumika zaidi kuongezea chachandu za WAISHIO .

NA....
.....Sina uhakika sana na busara ya BINADAMU KUTUNZA SANA VIDUDE ikiwa binadamu mwenyewe HATUNZIKI na atafanikisha KUZEEKA au KUFA baadaye kidogo pamoja nakujinyima kula ANGALAU nyama ya paka.

NAACHA!
Ninawaza tu hapa MKUU!

Siku njema!

Hebu twende NAMIBIA tukutane na Tate Buti katika- Super Focus (Drive Slow)


Au tu U2 wazungumzie The Sweetest Thing...

Read more...

Baadhi ya pesa hupitia mpaka kwenye TITI!

>> Monday, January 19, 2009

Sidilia ni pochi mwanadada akiamua!

Kuna waogopao ukoma lakini wakajivunia pesa wasiyo jua ni pesa KIRUKA NJIA!

Na....
.... ukiichunguza sana noti unaweza kustukia labda imewahi kuchambiwa KIDOOOOOGO!:-(

Na ni kweli...
... Ukimfuatilia nyuki katika matembezi yake, unaweza kustukia kinyesi kwenye kachumbari ya ASALI.
Swali:

  • Kwani hutumii noti na mashilingi kwa sababu kibonge una kadi ya benki?

Kwa chekibobu na sista du msafi....
...kumbuka labda pesa ujivuniayo wa mwisho kuishika ni ombaomba mwenye ukoma.
Na...
.... kutokana na kuingia na kutoka kwa pesa kwenye WALETI a.k.a pochi,KUNUKA kwa choo cha stendi na POCHI a.k.a waleti vinatofautiana kwa ujazo tu wa HARUFU!:-(



NAACHA!
Nawaza tu hapa MKUU!

Kwa sababu leo ni siku ya watu fulani kumkumbuka Martin Luther King Jr... tupate tena kidogo...I have a dream...


Au tu Nyerere aongee tusichoelewa kwa hisani ya Suby production.......

Read more...

Swala la KUONGEA kirefu katika KUFIKISHA ujumbe MFUPI!

>> Sunday, January 18, 2009

Karibu mara zote UJUMBE ni mfupi ingawa kuna wasifiwao kwa kuongea kirefu!

Binadamu alivyokuwa mvivu, angekuwa mahiri wa lugha kila atakalo kusema lingekuwa na UREFU wa herufi moja.

Na labda....
.....ninajieleza kirefu kwa sababu NINAJARIBU kujieleza na si MTAALAMU WA KUELEZEA.

Na....
......Unabahati kama bado kuna wasikilizao kila neno lako katika hadithi YAKO ndefu yenye ujumbe CHEMBE MOJA, hasa kutokana na ujuavyo kupigisha tikitaka maneno na sentensi, katika kumkwaza hata Sista wa Kikatoliki kuanza kufikiria labda ngono NI muhimu au Padre wa Kipagani kuanza kufikiria labda ni kweli ulawiti ni dhambi na sio tabia mbaya tu isiyo na uhusiano na dini ya WAHESHIMIWA wenye dini.

Swali:

  • Katika hadithi yangu ndefu kwani ni nani anafikiri nafikisha hata ujumbe mmoja?
Na.....
.....Katika kufikisha ujumbe kuwa jamaa limekaa vibaya kuna walioimba wimbo wenye maneno;.....
''DUKA LA MZUNGU liwazi. LAUZA mchele na NAZI.Kaniona mimi kafunga.......''


Na labda....
.....kama neno moja lingetosha kuelezea KUNYA tusingetakiwa kuleta maneno mengi yaharibuyo ustaarabu wa SIMULIZI za HAJA KUBWA uwezao kudakwa kwa neno moja lisomekalo au kutamkwa; ''KUNYA''

Na labda pia,....
.....ingawa binadamu wanasifiwa kwa kujua kuongea mpaka KICHINA, tukumbuke mpaka SISIMIZI wanajua kufikisha ujumbe KWA MPENZI SISIMIZI kuwa wapi kuna chakula-kibonge cha sukari na kuhakikisha TAIFA LA SISIMIZI halikumbwi na janga la njaa kama liwakumbavyo BINADAMU wenye maneno KEDEKEDE , WAVIVUUU, halafu wanasikia njaa haraka.


Lakini....
......Ongea tu KIREFU kama inalipa au inakusaidia kutonuka MDOMO.
Swali:
  • Si unasikilizwa?
NAACHA!



Ngojea tena Martin Luther King Jr ajaribu kufikisha ujumbe kwa kumuongelea Malcom X....




Au tu Rick James azungumzie ya COLD Blooded....





Pata baadhi ya picha zangu na wadau tuliokuwepo maeneo juzi ya jana...ASANTENI WOTE!
Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Read more...

Labda ALIYEPENDA ashaurikaye, HAJAPENDA HUYO!

Kipenda roho hunusa vilivyooza!

Vilivyooza kwa apendaye vitahalalishwa kwa kuitwa kuwa vimeiva sana tu ndio maana kuna MAFINYOFINYO, minyoo na nakadhalika tatu .

Na....
...Labda kilichopendwa hakikosoleki mpaka PENZI LIPUNGUE kidogo ustukie JAMAA halipigi mswaki ingawa tokea ukutane nalo LILIKUWA linanuka MDOMO.

UZURI wa penzi hata la chupi, INGAWA utajitahidi kuisifia kwa uzuri, CHUPI ILIYOTOBOKA bado haibadili ukweli kuwa IMETOBOKA na labda haishikilii vizuri MATAKO.

IKITOBOKA hata kama ni mpya,bado IMETOBOKA.

Swali:

  • Ushawahi kupenda KUPENDA?

Ni kweli....
...... inawezekana ukawa unapenda KUPENDA na sio unapenda kitu usemacho UNAKIPENDA.
Na...
....kama unahamu ya kupenda , CHOCHOTE HUPENDEKA.


Swali:
  • AU?
NAACHA!

Ngojea TONY HENRY ambaye ni miongone mwa wanamuziki weusi katika Opera wanizinguao aseme ya .....


Au tu David Hines,Bunny Rugs,Joseph Hill,Maxi Priest,Ras Shilo warudie kusema .....

Unaweza kuziruka au kutulia tena na picha zangu na wadau za juzi ya jana...
Kwa mara nyingine ASANTENI WADAU WOTE ambao hamkunitenga.....


Photobucket



Photobucket

Photobucket





Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket


Photobucket



Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP