Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ya DUNIA: -Flexisexuality!

>> Thursday, March 31, 2011

Wakati nafikiria  WABONGO  tupendavyo kuiga WAMAGHARIBI,.....

.......NA wakati nafikiria ya DUNIA,...

Mie yangu MACHO TU kwa tunakoelekea hapa DUNIANI.:-(

Kwa kifupi inasemekana:
More Western Women Reject Heterosexuality
Some studies indicate almost 1 in 4 females are not heterosexual.
Kwa Kilugha:

Wanawake wengi nchi za magharibi wanazidi kunanihii wanawake wenzao na ze mtalimbo wa wanaume  NO kuvutiwa nao aka no kuhusudu wanaume.


Kwa mchezo zaidi kongoli HUKU



Siku hizi kwa wajanja walao kotekote hawajiiti tena Bisexual aiseee.

 Au deku kideo upate swala la kisagaji LENYE jina KUBWA  mitaani  -Flexisexuality  .....









Au ...




Swali:
  • Waigaji MPOOO?

Read more...

LAFUDHI- hebu wasikilize Main Street SINGERS wakiimba-MUNGU ni PENDO!

Kuna rafiki yangu eti hasikii kuwa kiimbwacho ni kiswahili eti katika wimbo huu....



Read more...

Kwa kuwa KIWAZWACHO chooni LABDA kinawazika hata CHUMBANI!:-(

Ila bado kuna ambayo huwazika zaidi CHOONI kwa kuwa,...
... ni rahisi kuyakumbuka ukiwa MSALANI.:-(




Swali:
  • Si unakumbuka kuna mambo unayakumbuka tu kirahisi ukiwa na NJAA?
Ndio,...
...kuna MAMBO  ni labda ni mpaka UKIONA MGONGO  ndio unakumbuka  mfereji wa mwanzo wa   TAKO au tu ni UKIONA  kitanda ndio kikumbushayo hata ya MASHUKA bado MACHAFU ,...
....ingawa LABDA ni  ukweli  PIA kimawazo  ya kitandani labda yanafanyika hata CHOONI  kiwazo na wala tu sio kweli WAZO hilo  lawazika tu huko MSALANI!:-(

NI hilo tu na NI WAZO tu hili MHESHIMIWA!:-(

Tutulize maswala na manyanga yasiyo na fujo kwa WATU wasiotaka FUJO kwa kubakia Brazil ili Gilberto Gil alainishe kwa - Estrela


Twende UFARANSA ili Henri Salvador arudie - Jardin d'hiver



Henri Salvador arudie-Jazz Méditerranée




Alainishe zaidi kwa - Chambre Avec Vue



Au turudi tu Brazil ili Elis Regina arudie- Madalena

Read more...

Si unakumbuka MWALIMU wa NANIHII labda naye ana MWALIMU?:-(

Ndio ,...

... pamoja na kuwa  KUNA wajifunzao KUDOKOA MBOGA WENYEWE  bila kufundishwa na MTU,...
....au tu  KUNA wale warekebishao mpaka  JINSI YA  KUSALI au tu STAILI ya kufanya MATUSI    ili iwe  sio MPAPASO    kwa mafanikio kwa kuhangaikia hilo WAO WENYEWE,...


.... na  kwa kurekebisha STAILI  kwa KUJIFUNZA wao wenyewe kwa hata  kwa KURUDIARUDIA mpaka  kitendo HICHO  kwa BINADAMU WENGINE washuhudiao kuwa lijamaa mpaka kwa kuuza MAAANDAZI linafanikiwa  na kwa hilo lina cha   KUADIMAYWA kama wale  jinsi idaiwavyo  WAMEJIFUNZA WENYEWE,....
.... labda BADO ukweli uko palepale  kuwa MENGI ,...
..... watu hujifunza kutoka kwa WENGINE,...
.... na mengi wafundishayo WALIMU wa KITU ,...
... hayo walijifunza kutoka kwa MWALIMU wao hata wasio muita au kustukia ni MWALIMU.:-(


Swali:
  • Unabisha?
  • Kwani unafikiri WALIMU wengi hata tukiruka wale waliofundisha MTU  kuvaa chupi huwa wanaitwa WALIMU?
  • Na siinasemekana asilimia kubwa ya MAISHA ya MTU - mtu huitumia kujifunza kitu hata kama hastukii anavyojifunza ?

Ndio,...
... labda MWALIMU ana MWALIMU.:-(

NI HILO TU na ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu WAZIRI  wa UTAMADUNI  wa zamani wa BRAZIL yule  Gilberto Gil aanzishe upya kwa -Toda menina baiana




Au tu Gilberto Gil adinye tu na  -Aquele Abraço

Read more...

Kwa kuwa SHOMBO ya SAMAKI si PAFYUMU ila inazoeleka ukiishi pembeni ya SOKO la SAMAKI!:-(

Ndio,...
..... SAMAKI ni MTAMU  hasa  kama wewe sio MMASAI ajulikanaye kuwa ni upendaye NYAMA TU ,...

... lakini hata HIVYO  apendaye SAMAKI bado kwake kuna SAMAKI wenye MIBA aisee!:-(


Swali:
  • Au?

Kwa hiyo kwa kuwa SAMAKI ni MTAMU kwa apendaye SAMAKI,...
... bado labda TAFUNA kwa UANGALIFU usichokiona MIBA usijechomwa MIBA aisee!:-(

Swali:
  • SI nasikia SAMAKI kibao WENYE MIBA CHOMACHOMA  kwa nje hawaonekani  kuwa wana MIBA?

NI wazo tu hili MHESHIMIWA,...
....na  NENO  SAMAKI ukilioanisha na KIRUKA NJIA au tu LIMTU LAKO  udhanialo ni shwari kwa kuwa KWA NJE LIMENONA   kimtazamo wako ,....
.....   MIYE SIMO!:-(





Hebu twende BRAZIL ili  Gilberto Gil abadili wazo hili nyoko kwa kurudia-Waiting in vain




Gilberto Gil aje na Stevie Wonder wazingue..





Au tu Gilberto Gil azime sesheni HII kwa - Buffalo Soldier


Read more...

Wakati MTU halisi UNAYEKUTANA NAYE na AKUCHEKEAYE kajificha nyuma ya KITU!

>> Wednesday, March 30, 2011

Kuna wajifichao nyuma ya UREMBO,....

.... na kama ni wajinga utachelewa kujua kwa kuwa UREMBO ndio uustukiao.:-(

Kuna wajifichao nyuma ya HARAKATI,...
..... na  wanachofanya ni kufanya uoanishe UTU wao na HARAKATI zao  wakati  wao kama WATU kuwa ni ambalo hawataki liwe ni jambo listukiwalo.

Na kuna wajifichao katika DINI,...
....na wanaweza kuwa wafanyalo ni kutumia DINI na hata MUNGU ili kukurusha kustukia  yao BINAFSi ambayo  yanatisha  kama yakiwa ndiyo moja ya ambalo USTUKIALO

Kuna wajifichao nyuma ya KAZI,...
..... na ukitaka kuwaudhi ruka kutamka ni MAMENEJA wa kitu fulani  kwa kuwa ukiondoa UMENEJA WAO na UONGOZI wao wa  CHAMA labda hakuna lao BINAFSI kama WATU BINAFSi  wajivunialo.:-(


Kuna wajifichao nyuma ya SHULE zao,...
.... na ni tusi kwao kutowaita MADAKTARI hata kama NI UDAKTARI WA KUPEWA  kwa kuwa hicho ndio kithibitisho tu kuwa pamoja na yao yakijinga angalau waliwahi kwenda SHULE au wanaheshimiwa KISHULESHULE  ingawa labda ni vigumu  kwenye hilo kama ni BUSARA za USOMI wao ndilo kustukia  ulengalo .:-(


Kuna  wajifichao nyuma ya WATOTO , mme au WAUME zao,...
.... kwa kuwa yao ili wajisikie MAISHA yana maaana  ni WAUME, watoto, WAZAZI   au WAUME zao waaminikao kuna kitu wamefanikiwa ndio watakalo liwe listukiwalo.:-(


Swali:
  • Umeshawahi kukutana na mtu ambaye hatumii kitu KUJIFICHA nyuma yake ili angalau  kukujengea jinsi UMTAFSIRIVYO?

Ndio,...
.... labda kila mtu kajificha nyuma ya kitu fulani  ,....
... na ukijua ukweli juu ya MTU ,...
.....kiutu labda MALAYA ndiye MLOKOLE na MLOKOLE ndiye MALAYA !:-(


NI wazo tu hili MHESHIMIWA!


Hebu ghafla Loketo waingilie shughuli kwa -Extra Ball



Las-Ketchup wahamishe mashambulizi kwa -Asereje



Au tu Don Omar arudie - Danza Kuduro

Read more...

Safari ndefu ya kujifunza LADHA kwa BINADAMU kutoka kwenye ladha ya TITI la MAMA mpaka kufikia kuamini ladha ya MAGIMBI na SEHEMU za siri ni TAMU!!

Ndio,...

...watu wengi wapendao kula nyama hawakuzaliwa na TESTI ya NYAMA bomba ILIYOIVA ,....
....kama tu ilivyokuwa ni kweli LADHA ya SUKARI kwenye chai ni yakujifunza tu kwa kuwa kuna SUKARI!:-(

Swali:
  • SI unajua CHAI inanyweka bila sukari na kama unatumia SUKARI kurembesha chai yako hilo ni jambo la kujifunza tu kama iwezekanavyo TU kwa aliyezoea chai ya sukari kujifunza kuinywa bila sukari?

Ndio,...
.... labda BINADAMU ni MWANAFUNZI by nature na hata tukiacha maswala ya LADHA,...
... ila labda pia hata mapenzi ya MATAKO na vyote vilivyomo kwenye TAKO ya BINADAMU mpenda MATAKO ni ya kujifunza tu pia ,...
..... na cha kutisha ni kwamba LABDA uwezo huo wa kupenda MATAKO anao hata BINADAMU ambaye kwa sasa sio MPENDA matako!:-(


Swali:
  • SI inasemekana karibu wengi wapenda BIA ilibidi wajifunze kupenda ladha ya BIA?
Ndio,...
....labda kuna SUKARI ,....
... ndio hasa kisababishacho ULIPATA NAFASI YA KUJIFUNZA LADHA na unajua ladha ya SUKARI ,...
....na kama kungekuwa hakuna SUKARI kama CHUMVI tu vile,...
... MSOSI unalika bila CHUMVI wala SUKARI!:-(


Swali:
  • AU?
  • SI inasemekana aliyezaliwa maeneo ya walao MBWA na PAKA  ndiye rahisi kujua nyama ya paka ni tamu vipi?

 

Ndio,...
.... labda ukichunguza ,...
....utastukia mengi uyapendayo ,...
... umejifunzia tu kuyapenda UKUBWANI,...
...na kama usingejifunza ladha LABDA  wala HAYANOGI!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(


Hebu Kanda Bongoman aanzishe upya kwa-Wallow




Kanda Bongoman aendelee...-Isambe





Kanda Bongoman aendelee...



Aendelee...






BAADAYE BASI!

Read more...

Labda WATANZANIA walio wengi hawajali SIASA za CCM , za MCHUNGAJI MTIKILA, za CHADEMA , CUF au hata siasa zangu MTAKATIFU simon KITURURU za NANIHII zakujitakia !:-(

Ndio,...
...... wengi TANZANIA  kama wanamgao  nanihii , na wanaaamini serikali yao inawatekelezea wayahitajio hasa KATIKA WAHISICHO NCHI YAO ndio itoacho na yenye UWEZO NACHO  ufanyao maisha yao wakitaka kitumbua wanatumbua,..
...LABDA hawatajali GADDAFI anaibaje,...
-SAMAHANI! -
... namaanisha HAWATAJALI SANA viongozi  wa TANZANIA wanaibaje ,...
... na LABDA kama tu CCM ingeweza kutoa KITUMBUA,...
....labda CHADEMA na CUF visingekuwa vyama visumbufu kwa kutoa tu stori za MAANDAZI -maandazi  ambayo haVIjagawa bado.:-(



Na haki ya nani  INASEMEKANA  kwa aliyetibiwa HAMU  vizuri  si rahisi KURUBUNIWA na MTU kwa  kutumia  STORI TU  za KITIBU HAMU   kilichobenjuka tayari KIDUDE kama kionekanavyo KITAMU KATIKA STORI ZA WENGINE wadaio KINATIBU HAMU   kuwafanya WARUBUNIWE na wawe na MUNKARI au tu hamu yaVITU ambavyo UWEPO wake bado ni STORI tu!

Swali:
  • SI inasemekana aliyeridhika  na yake  aliyo na UHAKIKA NAYO  si rahisi kukubali kuhatarisha maisha yake yenye uhakika kwa kukimbilia ambavyo havina UHAKIKA na vyenye tetesi za hatari?
  • SI aliyeridhika kuwa MOTO unaunguza hahitaji kugusa MOTO ili kuhakikisha UNAUNGUZA?
Ndio nawaza tu ,...
... nafasi ya vyama vya UPINZANI  kwenye siasa ya TANZANIA kama CCM ingekuwa inatimiza KWELI  porojo za kwenye harakati za UCHAGUZI,...
...NA ni wazo tu HILI!:-(

....SAMAHANI  ,...
...nabadili ndude,...






Hebu Main Street Singers wanipe msaaada kwa KUDINYA kitu.......-MUNGU NI PENDO



Ngojea ghafla Black Ice abadili mdinyo na KATIKA KUBADILI  aongelee The music industry's exploitation of artists kwa kugusia ndude katika-Or DIE



Amir Sulaiman adunge nanihii - Spiting Truth




Au tu Notorious BIG aje tu na R.KELLY walainishe ZAIDI kwa kuongelea kula ngoma AMBACHO HAKI YA NANI NI KITU RAHISI yasemekana kwa wasioogopa dhambi au UKIMWI  kwa ndude-Fuck U Tonight





Ndio hili ni wazo tu MHESHIMIWA!:-(

Read more...

Wakati nawasiwasi na udhibiti wa MADAWA feki TANZANIA ,cheki hii kuhusu madawa feki NIGERIA !

>> Tuesday, March 29, 2011

Read more...

SHULE kidogo Zaidi ya AFRO BEAT kutoka kwa FELA KUTI!:-(

>> Monday, March 28, 2011

Ndio,...
...labda cheki tu kama ni mpenzi wa AFRO BEAT ...




Sehemu ya KWANZA....




Mnuno wa pili...



Mnuno ki MKUNO wa NANIHII wa tatu...






Mnuno wa nne...






Mnuno wa tano....




Fela kuti anunishwe mnuno wa sita...




Au tu Fela kuti akumbushie kitu kwa-Teacher Don't teach Me No Nonsense



Read more...

Kama unataka kuelewa MSHAHARA wa WALIMU msikilize Taylor Mali katika - "What Teachers Make"

Nahusudu SHAIRI hili la TAYLOR MALI ,...
.... ambalo nafikiri linadaka maswala ya fanyayo Prof. Mbele , Mwalimu Nyerere, Mwalimu Kheri Kitururu,  Prof. Matondo na Mtakatifu N.N. MHANGO  ...

....bila kumsahau akaribiaye kufikia uprofesa   MALKIORY .W. MATIYA  enzi zake  za KUTICHI na,...
...na WALIMU WENGINE wote WENGI  niwaheshimuo ,...
...ni walimu  na pia kuendelea  kufanya kazi muhimu HII  ya kufunndisha ya UALIMU ,...


....HEBU  tudake tu mpekecho wake ki MADUNGURUDU .....


Read more...

Kama vile mtazamo wangu mimi MJINGA MIE uhusuo BABU wa LOLIONDO NA DAWA ZAKE na hata ULE uhusuo madhumuni ya wampigao GADDAFI kwa KISINGIZIO wanalinda RAIA wa LIBYA unahitajika VILE katika JAMII!:-(

Ndio,....


...SIAMINI katika DAWA ya BABU wa LOLIONDO,...
... na siamini PIA kuwa UN aka UMOJA wa MATAIFA  ambao ni wenyepesa WAAMUZI ,...
....na WOTE wampigao GADDAFI wafanyavyo ni kwa ajili ya kulinda RAIA wa LIBYA  wasiuawe na GADDAFI wakati tunaona wakaavyo kimya mahali pengine RAIA wakiuawa na kufanya mchezo wa Ze KUFA!.:-(



Just SAYIN'!:-(


Hebu tubadili WAZO ......

...kwa kupata mashairi zaidi,....

....na hebu ngojea BLACK  ICE aanzishe kwa ......


Black ICE asisitizie kitu kwa -Truth is




GEMINI asawazishe kitu kwa-What are you fighting for



Au tu Julian Curry azime manyanga kwa - Niggers , Niggas and Niggaz


Read more...

Ikibidi uende KUKOJOA,...

>> Sunday, March 27, 2011

... labda lazima UMEBANWA  na kitakacho kukojolewa.:-(





Lakini ,....
... ukweli ni kwamba BADO sio kila akojoaye NI KWELI  alibanwa na MKOJO!:-(






Swali:
  • AU?

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!:
JUMAPILI njema!



Hebu Saadiq akiwa na LUCY PEARL aongelee ghafla kidude-Without U




Saadiq aguseguse- Its a shame



Saadiq ambaye ni Raphael Saadiq arudishe LUCY PEARL katika mdinyo kimlalamiko wa demu aonyaye demu kuwa-Don't mess with my man



Basi bwana hebu Raphael Saadiq mwenyewe amalizie tu kwa - 100 Yard Dash

Read more...

Mmmmmh!

MGUNO mmmmH!,...
.... ni kukubali.

MGUNO ni kiashirio kwa umpendaye kuwa afanyavyo vinakusikilizisha UTAMU.

MGUNO ni sauti  katika kustuka.:-(

MGUNO   ni TAARIFA hata KINYAMA kuwa  inauma,...
.....kwa hiyo MGUNO ni MAUMIVU.:-(

KUGUNA ni kukataa!
MGUNO ni  SENTENSI katika  TAARIFA hata kama kimaandishi yawezachukuliwa KAMA sio sentensi.:-(!

Swali:
  • Unafikiri mara ya MWISHO ulivyoguna ulikuwa unamaanisha nini?
  • Kwani unafikiri ulistukia mara ya mwisho ulivyoguna au ni wengine LABDA  ndio walisikia  na kustukia uliguna kwa kuwa labda ni wengine ndio ambao wanajua nakusikia yako?

Ndio,...
...inasemekana kunakuguna bila sauti,...
......na hili ni WAZO tu MHESHIMIWA!:-(


Hebu Raphael Saadiq aanzishe tena upya- Good Man





Brick warudie - Fun


Ndio India Arie na AKINYELE wali sampo BRICKS katika biti hili ingawa AKINYELE anamatusi kama hivi kwenye BITI HILIHILI kikidude-Put It in Your Mouth



Wakati eti  India Arie biti HILIHILI aliliweka mdomo safi katika-VIDEO





Sijui kwanini lakini ,...
...ila labda hebu  Brick wazime manyanga kwa - Ain't Gonna Hurt Nobody


Read more...

Ingewezekana-LABDA ningejisahaulisha kuwa nina matatizo ya zaidi ya NYEGE au hata UJINGA na KWA HILO labda sina MATATIZO aisee!:-(

Tatizo ni,...
.....HAKI ya nani TENA,...
....hata MTU ajisahaulisheje kuwa HANA MATATIZO,...
... hakuondoi UKWELI kuwa ana hayo MATATIZO na haki ya nani tena MATATIZO kama YAPO ,...
....kujisahaulisha hakuondoi UKWELI matatizo HAYO utakayo kuyasahau BADO yako PALEPALE.:-(


Swali:
  • Si nasikia hata ulisifieje TOTO lenye sura kama MATAKO ya bata kuwa lina sura kama  MALAIKA bado HAKUGEUZI UKWELI kuwa toto lenye sura kama matako ya BATA hilo lina sura kama MATAKO ya BATA na haki yanani  tena kimuonekano halionekani kama MALAIKA?

Ndio,...
...labda hata ujisahaulishe vipi hata  KAMA NI kwa hata  KULEWA POMBE , elimu  au hata kulewa tu  DINI kama wafanyavyo WENYE DINI , wapagani, walokole na waswahilina katika kujaribu kujisahaulisha machungu ya DUNIA,...
.... labda BADO HUKO   hakuondoi TATIZO aisee!:-(



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(


Hebu King Sunny Ade abadili ghafla kwa -Oluwa No'o Jeun Kan / Sijuade




Notorious BIG abadili kabisa kwa-Suicidal Thoughts





Notorious BIG akumbushe-Niggas Bleed






Biggie Smalls aanze kulainisha kwa-Sky's The Limit





Au tu a- Hypnotize

Read more...

Wakati inadhaniwa na BINADAMU kuwa NYANI haoni KUNDULE,......

.......labda kiendeleacho hasahasa kama asemaye hilo/HUO MSEMO ni BINADAMU ni kuwa,....
.... hivyo ni ADHANIAVYO tu  na idhaniwavyo tu na BINADAMU,...


....... kwa kuwa KIHALIHALISI labda  NYANI  hatafsiri KUNDU la MWENZIYE  kama KUNDU hata kama aonalo tu ni KUNDU LA mwenzie  kwa mtazamo wa BINADAMU wawaangaliao nyani kwa pembeni,...
... kwa kuwa labda kimawazo ya NYANI labda KUNDULE  ni KIKALIO au tu  sio KITU KIFIKIRIWACHO  kama idhaniwao na BINADAMU wenye akili mpaka wanatumia akili kutafiti mikundu hiyo mpaka KUJIPATIA mpaka MSEMO huo  ``Nyani haoni KUNDULE´´ .:-(

Swali:
  • Si labda ni kweli kuwa  kuna uwezekano lakini  tetesi ya kuwa ``NYANI HAONI KUNDULE´´ ni tafsiri tu ya BINADAMU aliyewahi tu kuwa pembeni ya NYANI akaona MKUNDU wa NYANI  afikiriaye anaelewa NYANI WANATAFAKARI NINI kuhusu MIKUNDU -  kitu ambacho labda  sio kitu BINADAMU awezacho kuelewa -na kutumia afikiriacho NYANI WANAFIKIRIA katika kujaribu tu  kuelewesha MTU yale ya  KIBINADAMU?:-(




Ni wazo tu hili  dhaifu  MHESHIMIWA na wala usikonde!:-(






Hebu Al Green abadili mkao kwa -I'm Glad You're Mine



D'Angelo achokoze kwa kurudia - So Glad You're Mine (Al Green cover)



D'angelo asogeze chupi pembeni kidogo kwa - How does it feel



Hebu D'Angelo, Spanky, Saadiq, Ali Shaheed na ?uestlove wadinye -Lady

Read more...

Mambo yote MBEYA! -Babu wa LOLIONDO who? Kijana wa Miaka 17 aibuka na Dawa Jijini Mbeya.

>> Saturday, March 26, 2011




Pata Picha za MCHEZO mzima:













Maelezo ya PICHA:

1.Mganga mwingine wa tiba za magonjwa Sugu aliyefahamika kwa jina la Jafar  Welino(17) mkazi wa mtaa wa Mianzini Kitongoji cha Mabatini jijini Mbeya ameibuka na kutoa tiba kwa mamia ya wakazi wa jiji la Mbeya na viotongoji vyake.

2. Umati wa watu ulionekana katika nyumba anayoishi kijana huyo wakisubiri kupatiwa tiba hiyo huku wakiwa na vikombe vyao mikononi. Baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo walidai kuwa wamefika hapo kutokana na taarifa za kuwa kijana huyo anatibu magonjwa Sugu bure kama vile ambavyo anatibu Mchungaji mstaafu wa Loliondo Mzee Ambilikile Mwasapila.

3. Akizungumza  kwa niaba ya kijana huyo mama mkubwa wa mganga huyo aliyejitambulisha kwa jina la Edina Sanga alisema kuwa kijana huyo alianza tiba hiyo wiki mbili zilizopita ambapo kabla ya kuanza kutibu alimueleza mama yake huyo kuwa alitokewa na mama yake mzazi a,mbaye kwa sasa ni marehemu akimuelekeza kurithi mikoba yake.

4. Bi.Sanga alisema kuwa mama yake kijana huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ni mtu mwenye maruhani ambapo kwa kutumia maruhani hayo alikuwa akitoa tiba kwa wakazi mbalimbali mjini Mbeya.Alisema kijana huyo ambaye wamezaliwa mapacha na dada yake aliyemtambulisha kwa jina la Hadija Welino kwamba yeye anasoma kidato cha Nne katika shule ya sekondari Itende.

5. Hata hivyo Bi.Sanga alisema kuwa kijana huyo aliitwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji ili kutoa maelezo ya namna ambavyo anaendesha tiba hiyo na kuwa hata hivyo anaendelea kutoa tiba kwa watu kwa kunywa vikombe viwili kwa muda wa siku mbili. Alisema kuwa dawa hiyo aliifuata katika kijiji cha  Iyula kilichopo wilayani Mbozi na kuwa mara alipofika alianza kuichemsha na kuwagawia wananchi wanaosumbuliwa na maradhi sugu. Aidha umati wa watu walikuwa wamejipanga katika mistari kusubiri tiba hiyo ambapo

6. Mwenyekiti wa mtaa wa Mianzini Bi.Elizabethy Mwakabungu aliweka utaratibu wa wananchi kupata tiba ikiwa ni pamoja na kuchangia fedha kidogo kwa ajili ya kununulia kuni za kuchemshia dawa hiyo.Akizungumza na umati wa watu waliokuja kujipatia tiba hiyo Mwenyekiti huyo wa mtaa alisema kuwa kila ambaye atapata kikombe kimoja cha dawa anatakiwa kupata kikombe cha pili siku inayofuata.

7. ‘’Mganga katuagiza kuwa kila anayekunywa kikombe kimoja anatakiwa kunywa kikombe cha pili siku inayofuata…yeyote atakayekunywa hatakiwi kunywa pombe kwa muda wa siku saba,’’alisema Bi. Mwakabungu

8. wakipata kikombe

9.maelekezo ya kufika eneo hilo

Pamoja tunaendeleza kupashana Habari








Ndio haya mavituz yanaletwa na MBEYA yetu BLOG ,...
...yaliyonifikia na ujumbe :
``Nimekutumia habari hii kutoka Jijini Mbeya .
Kuna kijana ameibuka nae anatoa dawa .
Hizo ni picha tulichukua eneo la tukio na pia na kila namba ya picha naambatanisha maelezo hapa chini.´´

Kumbuka  katika sentensi  iishiayo na maneno ``MAELEZO hapa chini´´  - maelezo yenyewe  na picha ndiyo hayo,..  ....HAPO JUU.




Hebu Chico Debarge aanzishe upya kwa kubadili mkao wa firigisi kwenye kikaango kwa ndude- Trouble Man


Chico Debarge adadavue kwa kuweka grisi kwenye belingi kwa - Love Jones



Hebu Chico DeBarge amuongelee kidogo BIKIRA katika - Virgin





Au tu Chico DeBarge ajaribu zaidi kuzima tu manyanga kwa ndude - Iggin' Me



Read more...

LABDA huwezi KUPONYA HOFU YA NANIHII au tu YA unachokihofia bila KUKIKABILI unachokihofia!

Kwa hiyo LABDA  kama uogopacho ni NYOKA,  mende, KUTUKANA  au tu KUNYA -samahani-  kujisaidia vichakani,....

.... DAWA NI,...
....kumkabili  huyo NYOKA ,...
......huyo MENDE ,..



....kufanyia mazoezi  KUTUKANA kwa kutusi MTU angalau kiadoadao ,....
.....na kwenda tu  KUJISAIDIA  mara moja moja vichakani mpaka uzoee,....
... kama nia yako ni  kweli kuponya HOFU ya  UNACHOHOFIA.:-(

Swali:
  • Unabisha?
Kwahiyo LABDA tafuta PAKUANZIA kukabili uyaogopayo,...
....mkabili hata kwa  angalau hata kwa KUMSABAHI basi  umpendaye ambaye kumtongoza bado UNAHOFIA,...
....fanya mazoezi hata kwenye blogu yake na sio uso kwa uso KUMTUKANA utakaye kumtukana TOKEA SIKU NYINGI kwa kutumia jina lako halisi NA KAMILI  ikiwa bado kufanya hivyo uso kwa USO unahofia,....
.....au tu  jifunze kumkabili MUNGU hata kwa maombi kama ndiye UNAYEMHOFIA,...
...isije kufanya UMUOGOPE TU ingawa inasemekana ni MUNGU wa upendo na apenda watu kwa hiyo labda sio wa KUHOFIA.:-(



Swali:
  • Si hata MAJAMBAZI na MAFISADI labda huanza kuua hofu ya kuiba kwa KUPATA PAKUANZIA KUONDOA HOFU -pale kwenye wizi mdogomdogo kabla hawajafikia kukosa hofu katika WIZI mkubwa uhitajio watu wafe kwa kupigwa risasi au tu kwa kuwa dawa za hospitali  YA SERIKALI ambazo zingewaponya BOSI kazitumia kumjengea kimada nyumba ya pili?

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
SAMAHANI!

Hebu SAMY DIKO aingilie shughuli ghafla kwa- Je Vous Aime



Au tu Samy Diko aendeleze tu mpekecho  kwa -EYAE'E EYA

Read more...

Unafikiri kama usingejua umezaliwa tarehe gani ikusaidiayo kuhesabu MIAKA,...

.... unafikiri ungedhania una UMRI GANI ?

Ndio ,...
... kwa kawaida siku hizi  tunahesabu MIAKA  kwa kuhesabu siku ambazo hugeuka MIAKA  ,...
.....lakini kuna umri wa KIBAOLOJIA ambao hutokana na ni jinsi gani tumejitunza KIAFYA na ndio uwezao  kufanya  saa nyingine  kuna MIMTU ufikiriayo ni MIZEE  na uipayo BONGE ZA  shikamoo kumbe ni MIDOGO kwako ,.....
....na  UMRI ambao ni mtu anavyojisikia ambao unamisingi yake KISAIKOLOJIA zaidi ambayo huweza kusababisha kufanya LIMAMA  au LIBABA zima  kuonekana linamitabia au linavaa kitoto.:-(


Lakini,...

Swali liko pale pale kuwa:
  • Unafikiri  USINGEJUA tarehe uliyozaliwa WEYE  ungedhania una umri gani?
  • SI labda UMRI na MIAKA ya mtu ni vitu tofauti?


Nawaza NAKUJIULIZA  tu kwa sauti MHESHIMIWA na wala usibanwe chupi!:-(


Hebu Lágbájá aanzishe upya kwa - Did I?







Lágbájá arudie-Skentele Skontolo




Lágbájá au amalizie tu kwa mdinyo-Sobolation




Read more...

Eee BWANA eeh!

>> Friday, March 25, 2011






Ijumaa na WIKIENDI njema MDAU!


Kaujumbe  KALEO pembeni kidogo ya tundu kwa ung'eng'e uliopinda:

``The only PERSON anyone should be JUDGING,...
.....is THEMSELVES!´´

Swali:
  • AU?
  • Kwani hujanielewa?



TUKO PAMOJA!
Ni hilo tu !






Hebu Culture Musical Club of Zanzibar waingilie kati na kushusha maswala Kidumbak kwa ndude-Mpewa HAPOKONYEKI





Au tu Culture Musical Club ngojea waendeleze tu KIDUMBAK kimmalizio wa NGOMA ILEILE ila part``BE´´ .... sasa kwani tutafanyaje?


Au tu hebu Mariam Khamis alainishe zaidi kwa-Huliwezi BIFU

Read more...

Kama tu KITU kizuri tusivyoridhikanacho na kukitafutia KASORO,....


....katika KUFANYA yawezekanayo ambayo HATUYAFANYI ,...
......labda  wengi wetu tutafutacho ni VIZINGITI na VIPINGAMIZI!:-(



Na wakati ili tupate NGUVU ya kuchukua HATUA na kuanza KUTEKELEZA,....
.....tufikiriacho KUFANYA,....
......tutakacho KUFANYA,....
......labda kihitajikacho ni  MTAZAMO chanya na MATUMAINI katika ya  dalili za WEZEKANO na yawezekanayo na kuanza kufanya kwa kuwa LABDA   hakuna chochote ambacho  kitakosa VIZINGITI na kitakosa VIKATISHAVYO TAMAA kuanza  kama  ukivisaka hivyo,....
.... hasa kwa kuwa kwa kuwaza tu sana KIMTAZAMO HASI na woga wa nini  ni pungufu katika HALIHALISI  YA MTU kabla YA KUFANYA ,...
....yaweza kuwa ndio kitengenezacho KIZUIZI kikubwa cha kutatua matatizo ya mtu na ambacho ndicho hasa  BREKI ya cha kufanya kitu ili kujikomboa- KIPINGAMIZI!:-(


Swali:
  • Au?
  • Kuna mangapi unafikiri HUFANYI  kwa kuwa umejitafutia tu mwenyewe VIZINGITI na vipingamizi na labda hata UDHAIFU ili kuhalalisha HAVIWEZEKANI hata kujaribu  KUANZA pambano la kujikomboa?
Ndio,...
... labda kitu KIZURI ,....
... wengi wetu tunakitafuta KASORO na udhaifu ili kujizuia kitu,....
.... na kwa bahati mbaya labda hakuna kitu ambacho ukikichambua ili kusaka KASORO na  ,....
..... utakosa udhaifu na  KASORO!:-(

Swali:
  • Si unajua  hata MREMBO usiyemuona kasoro kwa kuwa ananukia vizuri bado ukimsachi mpaka utumboni bado utamkuta anatembea na mavi kwenye utumbo?
Ndio,....
.... kama unataka KUFANYA kitu  ,...
... ukitaka kupata vizingiti na vipingamizi vya kufanya hivyo vitu ,...
.... utavipata tu MHESHIMIWA!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA lilengalo WOTE wenye MAAIDIA  ya kufanya MAVITU babu kubwa  ila WANASITA kuchukua hatua ya KUANZA KUFANYA MAVITU hayo MAKUBWA!:-(



Hebu TATUNANE waanzishe vita mpya kwa-Msewe



Tatunane waendeleze...

Read more...

R.I.P Asifiwe!

>> Thursday, March 24, 2011

Mdogo wa Bloga mwenzetu  na RAFIKI yetu Yasinta Ngonyani ,...

... kwa jina ASIFIWE ametutoka!:-(


R.I.P Asifiwe!
Poleni  sana Yasinta na familia nzima ya Mzee Ngonyani!


Na MUNGU akupumzishe mahali pema Asifiwe!

Read more...

Ukichunguza wasikilizao maneno yaliyo kwenye NYIMBO ZA DINI na MAHUBIRI au tu hata MANENO yaliyotumika kutongozea waliokubali utagundua,...

.....SIO kila asikilizaye NENO anatafakari ayasikiayo MANENO,...
..... na ndio maana unaweza kukuta MZINZI yuko bize anasikiliza nyimbo zikatazazo UZINZI bila hata kustukia zinamsuta ,...
... MWIZI fisadi kakaa kanisani mbele kabisa huku akimsikiliza ASKOFU akikemea ufisadi na wizi bila kuguswa,...
... na MSWALIHINA ajuaye maneno yakatazayo  nyama ya NGURUWE kwa kuiita  ni haramu akiagizia KITIMOTO bila kustukia maneno KITIMOTO na NYAMA YA NGURUWE yanamaanisha kitu kilekile kinamna ambacho ni haramu ,...
.... na bila kusahau UWEZAVYO KUSTUKIA mpaka  adanganywaye wakati anatongozwa kwa MANENO ayaliyowazi ni UONGO hakutafakari MANENO ayasikiayo  ya  kuwa KIDUME  asiye na BESENI  anadai kila  akioga anamuona KIGOLI kwenye BESENI ,...
....au akidai  kila wakati ANAMUWAZA YEYE TU  wakati yeye atongozwaye na mtaa mzima  inajulikana kauli hiyo anamuambia kila KIGOLI na wamwisho kuambiwa hivyo ni shoga ya atongozwaye ,...
..... kitu ambacho kuna wakati humshangaza mpaka mtongozaji mwenyewe   AKISHAKUBALIWA.:-(

Swali:
  • Si unajua MANENO YAKUTISHAYO kwa mtu bila kuyatafakari labda wala hayasemi kitu na nisawa tu na MLIO wa NGOMA kwa asiyejua MLIO wa ngoma waaina hiyo UNAASHIRIA nini hata katika enzi zile ambazo ngoma aka Talking Drums ndio zilipeleka mawasiliano mbali kuwa kwa jirani kuna MSIBA?
  • Huwa unatafakari MANENO uyasikiayo lakini -au yameshageuka kuwa ni maneno tu kama WATANZANIA wapendao nyimbo za KIKONGO  za KOFFI OLOMIDE walivyoridhika  kwa kutokuelewa KOFI Olomide katika nyimbo zake MANENO  ayasemayo yanamaana gani? 
  • Na si nasikia mpaka WASAINIO mikataba ya TANZANIA huwa hawatafakari maneno ya MIKATABA yanasema na yanamaana gani na ndio maana VITA ya Tanzania na IDI AMIN  mikataba ya silaha karibia ifilisi nchi chini ya Nyerere na  baada ya Nyerere  labda sio siri  KUANZIA RADA mpaka mikataba ya MADINI kinachoendelea  chamoto twakiona ?

Ndio,...
.... wengi hatutafakari MANENO yana maana gani,.....
... ndio maana labda usishangae ukikuta waimba kwaya , wenye  N.G.O za kueneza jinsi ya KUJIKINGA na UKIMWI na WAHUBIRI wakatazao waumini kitu kwa maneno ya nyimbo na MAHUBIRI yao ,...
....wakiongoza KUFANYA yaleyale WAKATAZAYO katika yaliyopo katika MANENO yao wayatumiayo KUKATAZA na kufunza wengine!:-(



Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na wala usikonde!:-(
SHIKAMOO basi,...

...Sasa nini kama hata SHIKAMOO hailainishi  kitu ili angalau utabasamu? 

Lione lile!:-(


Hebu Gelly na AT wabadili tu ili tusikonde zaidi kwa -Binti Yenu



Au tu USWAZI na Shirko wapige-Mwizi


Sijui kwanini lakini hebu tu tena NINA SIMONE arudishe usiriasi katika-I wish I knew how

Read more...

MAPUMBU aka makende/KORODANI ndio SOMO la leo la CHAPUCHAPU hasa kwa WANAWAKE hapa kijiweni!

Tahadhari :SOMO linagusa swala kwa JUUJUU !:-(


Habari zenu WADADA!
Aah jamani nawasabahi JAMANI  mbona mmenuna namna hiyo?
Naomba TABASAMU kidogo basi!

AKSANTEEEE Dada zangu,....
... na moja kwa moja ngojea tuongelee mapumbu.!:-(

Ndio,...
...najua  kati yenu kuna watundu ambao TAYARI  mshawahi  kuona hii kitu wakati toto la KIUME linaogeshwa au hata kupapasa hiki KIFAA ,...
....tukiachilia mbali na hata kujua kuwa HII NDUDE  ikigongwa inauma kweli  kwa hiyo tayari ni wastaarabu na hamjaribu kubinya  au hata wakati wa ugomvi kupiga teke hiki kifaa  MAKENDE  kwa kuhurumia mchango wake kwa vizazi vijavyo.

Na nashukuru kwa hilo yani!

Ila bado ,...
...wanawake WENGI ni miongoni mwa watu wengi  wasiostukia kwanini  WANAUME wanajihadhari kubinywa KORODANI ,...
...na pia wasiostukia hiki kifaa hakiko kwa ajili ya UZALISHAJI TU  wa malighafi shahawa aka MBEGU za KIUME ambazo ni maarufu sana  kwa kuchafua mashuka kama tu kusababisha mimba zikilengwa kwenye tundu lenye yai  lihitajilo rutuba.:-(



 Hiki kifaa kina kazi zaidi ya UZAZI  aisee,...
..... kwa kuwa ni chombo kitengenezacho pia HORMONES aka HOMONI  ambazo hutumika kurekebisha mwili wa BINADAMU  kutokana pia na kuwa na mfumo  ujulikanao kama endocrine system au System of Glands  ambazo hutengeneza hizi Hormones na kuzimwaga kwenye damu ya mtu ambazo hurekebisha kuanzia UKUAJI wa MTU, anavyojisikia mtu (MOODS) , mpaka jinsi ni kwa spidi gani unasikia njaa kutokana na hizi HORMONES  kucheza na ndude METABOLISM ya mwili,...


....ingawa NDIO ,...
...kifaa HIKI hujulikana zaidi labda kwa mchango wake wa sperms au kwa lugha ya kitaalamu SHAHAWA na kwa homoni moja zaidi ya aina ya TESTOSTERONE  ambayo inafanya DUME akae kidume ,...
.... yani  fulu MIDEVU  na minywelenywele bwelele mwilini isababishayo hata gizani kama mjanja ukipapasa ustukie ulipapasalo ni dume RIJALI , misuli mikubwa na mpaka bonge za mifupa kiujazo pia,..
....kitu isababishayo BODE la njemba liwe tofauti kidogo na BODE la kimwana mrembo mwenye kiuno kama nyigu,...
...ikiwa na maana inasaidia DUME lisikae  KIJIKE - ki fulu bonge za titi.

Na ukitaka kuijua zaidi hii ndude ninliyopapasa mpaka hapa   ,...
....Testicle,....
.....Testosterone ,....
.......kitu kizima ENDOCRINE SYSTEM,.....
.......hormones ,....
.....au hata kitu Sperm aka Shahawa ,...

.....gugo aka GOOGLE tu hizo MSAMIATIZ,...
....ambazo ndizo nimechezanazo katika somo mpaka hapa MKUU kwa shule zaidi isiyo ya juujuu kama ya vidokezo tu niistuayo hapa KIADOADO.:-(

Lakini kwa kifupi ,....
... nafikiri tutakubaliana kuwa MAPUMBU ni muhimu aisee mdada!:-(




 Hebu tupate kwanza kielelezo cha hiki kifaa :





Hiki kifaa hutunzwa katika kifuko kilichoumbwa kwa mchanganyiko wa ngozi na misuli  ``SCROTUM´´  ambacho kazi yake kubwa ijulikanayo ni kuweka KORODANI kijoto chini ya joto la mwili kwa  kuwa  KENDEZ zikiwa na joto kama la mwili  mbegu za kiume zitengenezwazo huingia udhaifu na kufanya kidume  sio kila goli  lake  lina afya na nguvu  kwa kutokana na joto kuathiri  kitu kiitwacho na wabongao ung'eng'e - Sperm Count.

Na kutokana na hilo mpaka kuna wadaio bila USHAHIDI WA KITAALAMU kuwa labda  MIDUME ijihadhari na chupi aka VIFICHA NYETI vibadavyo sana na kuzuia kazi  ya  kifuko ya kusogeza makende mbali na mwili joto likizidi na kuyarudisha karibu na mwili kama kipupwe kimezidi  kushusha joto za pumbuz .


Hebu tukideku kipicha  kifaa:
Hapa ni kitu kikivutwa juu ikiwa kinabaridi iathiriyo joto litakiwalo katika kiwanda cha shahawa na na kikishushwa chini kidogo  kimnig'inio ikiwa joto la mwili ni kubwa zaidi kidogo kuliko lihitajiwalo kiwandani.

  • Na nadhani  unakiona wakati kimesogeza   BALLS karibu na mwili hapo kulia .


  • Na kikiachanisha KORODANI na mwili huteremka kama ionekanavyo hapo kushoto.



Kazi hii ya kupandisha na kushusha GOLOLI hufanywa zaidi na Misuli ya cremester aka Cremaster muscle ambayo huvuta  pia makende juu kama MHESHIMIWA KIDUME ananyege na kitu kimesimama ,...
... kazi ifanywayo PIA  ili kulinda shehena za aina ya KORODANI zisiathiriwe  KATIKA KURUPUSHANI  hasa  wakati mheshimiwa anakula ngoma aka ANANGONOKA.



Mpaka hapa nimepapasa,...
....Cremaster muscle,...
.....Scrotum,....
....na Sperm Count ,...
,....ambazo kwa shule zaidi wewe ZIGUGO tu  ukizingati katika taralila hii nazigusia kwa juujuu.:-(


Na kifuko aka KITUNZA MAKENDE  HIKI kinasemekana kuwa na undugu sana na Labia Majora kwa wanawake.



Asanteni  WADADA,....
... na nimatumaini  kuna angalau jambo MOJA  ili taralila hii ifanikiwe labda mtalifanya na hilo ni angalau kujiuliza kitu kimoja ambacho kitazalisha  angalau MGUGO aka M-Google kitu kimoja zaidi KUTOKANA na TARALILA HIII  na kujua angalau kitu kimoja zaidi kuhusu hizi KENDEZI ambazo historia yake kwa UZALISHAJI na hata yakufanya MIDUME iote NDEVU  na kuwa na TITI ndogo ukilinganisha na NYONYO za WANAWAKE ,...
....  ni tokea enzi za ADAMU na HAWA.




SASA TARALILA inaegemea  kwa WANAUME zaidi ,...
..... na hii,...
.... ni KITU siriasi zaidi  hasa kwa kuwa inagusa zaidi  SARATANI ya Ze PUMBUZ!:-(

Hebu tuanze upya na  twende shule kuhusu MAPUMBU,...
...kwa msaada wa MWANADADA,...
..... Dr. Susan Jewell  kwa .....




Mdada SUSAN aendelee..



Somo zaidi  kwa wanaume kuhusu kucheki hiki kifaa hasa kutokana na saratani ya kiaina ichezayo maeneo kwa kumdeku huyu MDADA akizidi kufunza katika hii-Testicle exam






Kabla sijaacha labda tucheki SHULE MCHANGANYIKO ,...
...hasa kwa  wazazi ambao wamepata mtoto wa KIUME  ambao labda inabidi wajue tu pia  kuna kitu kiitwacho-Undescended Testicle kwa kumsikiliza Dr Steven Friedman






Mpaka hapa kwa shule zaidi unaweza KUGUGO,....

....Undescended testicle,....
...Testicular cancer,..
... ambavyo nimevigusa kwa juujuu .:-(


NIMEACHA!
Samahani tunakumbushana tu  SWALA na  madhumuni ilikuwa nikuchokoza udadisi wako ili udadisi zaidi kujua zaidi kuhusu hii kitu  MHESHIMIWA,...

.....na kama umekwazika au hukujifunza kitu  KATIKA PROSESI  ya KUDAKA USHUSHAJI wangu wa HII ishu KI-UjingaBUSARA maana yake mlengwa wa TARALILA HII haikuwa wewe,...
... na kwa hilo SAMAHANI!!:-(!

Read more...

UKICHUNGUZA utastukia watu BADO hupenda kujihusisha zaidi na wawafikiriao ni WASHINDI aisee!

 .... na kama inaaminika UNASHINDA,...
... tegemea wakuchekeao na watakao URAFIKI kuongezeka!:-(




Swali:
  • Au?

Kwa mara nyingine TUNAKUMBUSHANA TU  wazo  hili MHESHIMIWA!





Hebu Maxi Priest aanzishe tena upya kwa kitu tofauti kwa -Field



Maxi Priest aendeleze kidogo kwa - Believe In Love




Maxi Priest aendeleze tena kidogo tena zaidi kiduchu kwa -Should I



Au tu Lady Jay DEE aturudishe BONGO NYOSO kwa -Sirimba

Read more...

MAISHANI - kuna kujifunzia KATIKATI ya kitu pia!

>> Wednesday, March 23, 2011

Ndio,...
.... labda ANZA tu,....
.... mengine utajifunzia na kuyajulia MBELE ya SAFARI!:-(




Swali:
  • AU?
  • SI maishani hakuna aliyeanza kitu akijua?
Ndio,...
..... wajuzi wengi,....
... siri ya KUJULIA KWAO VITU ni kurudiarudia kitu mbele ya safari!:-(

 MAISHAAAAAAAAAAAA!:-(
 Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu  Israel Vibration waguseguse zaidi tu eneo anuai  ili wabadilishe WAZO  na ile ndude-Rude BOY shufflin'




Au tu Capleton na SIZZLA wajaribu kuzima manyanga tu tena kwa-Jah Jah City



Na sijui kwanini hebu na SIZZLA na Garnett Silk ndio wafanikiwe kuzima manyanga kwa -Bless ME

Read more...

NDIO -ntasogeza SIKIO ukitaka KUNINONG'ONEZA!:-(

Lakini  UKINONG'ONA ikasikika na utakaye UNONG'ONAYO asisikie,...

... kunakasheshe zake aiseee!:-(

Swali:
  • Si unajua ukinong'ona ukasikika kuna NOMA aka NISHAI zake hasa kama unong'onacho ni UMBEYA?

Lakini,..
.... kwa kuwa DUNIANI bado  kuna MENGI TU labda sio busara KUYAPAYUKA ingawa inajulikana DUNIANI hakuna siri,...

NONG'ONA tu AISEE!

Ila  labda
.... ni muhimu kuzingatia ukishapayuka  UKASIKIKA labda ndio inaweza kuwa IMETOKA HIYO kama tu maji yaliyomwagika mchangani yasivyozoleka,...
... na itakuwa ni JUHUDI zisizo za msingi kujaribu kuyameza yaliyopayukwa na kusikiwa nakujifanya huyajui kwa UMMA uliokusikia,...

...na kama unakumbuka hilo,...
..... basi ukinistua mie ntasogea UNINONG'ONEZE ,...
...na kwa wengine labda kwa UHURU,...

NONG'ONA TU AISEEE!

Swali :
  • Si unajua asilimia kubwa ya YANONG'ONEZWAYO ili watu wengine wasisikie huwa KWA KAWAIDA  ni ya kawaida sana na labda wala hayastaili KUNONG'ONWA?

Ndio,...
... kama huna uhakika na harufu ya mdomo wako,...
... kumbuka  WAKATI UNAMSOGEZEA MTU LIMDOMO LAKO  inaweza kuwa unanuka mdomo aisee ,...
...na wakati  unamnong'oneza mtu HARUFU YA  kitu DOMO  ikafanya ANONG'ONEZWAYE  aweze kukumbuka UNANUKA DOMO kuliko bonge la UDAKU  kuwa Rais MWINYI unadhani aliwahi KUKUKONYEZA ambacho ndicho ULICHOBUNI na ndicho  unachonong'ona aisee!:-(


NI wazo tu hili lililokaa kushoto zaidi ya kulia  MHESHIMIWA!:-(


DUH labda tubadili kabisaaa ili tuondoke kwenye hili WAZO nishai
NA ,...
....hebu Burning Spear aanzishe upya kwa -Driver


Burning Spear aje NAIROBI kudai-Jah no DEAD



Joseph Hill aje naye hapa hapa NAIROBI na kuongelea tatizo la kuwa-She want Money






Israel Vibration watoneshe kwa -Vultures

Read more...

R.I.P wasanii 13 wa FIVE STARS Modern TAARAB!

>> Tuesday, March 22, 2011

Poleni sana MAJERUHI na wote mlioguswa na tukio hili!
MUNGU  awapumzishe marehemu  KWEMA!




Habari zaidi za tukio:



Read more...

Unafikiri MWALIMU NYERERE angekuwa hai na kaanzisha BLOGU angekuwa na wamfuatiliao WANGAPI?

Ndio,...

..... kuna BAADHI ya MASWALI labda hayana jibu  la UHAKIKA KIBINADAMU  hata kama kuna watakao jibu  na majibu yao kuchukuliwa kama ndio jibu lakusadikika,....
... ndio maana hata kama SASA HIVI kuna wajaribuo kufikiria  kuwa wana JIBU la  labda YESU angekuwepo KARNE hii angekuwa na BLOGU na angekuwa anafuatiliwa na MTUZ kadhaa wa kadhaa ambao  kwenye KIBOXI cha MAONI aka COMMENT wangekuwa wanatoa maoni BWELELE hata ya kumtusi na WAKAAMINIKA kwa kuwa wamedai wameoteshwa kama BABU wa LOLIONDO,...
..... bado wafanyacho sasa hivi KWA MAJIBU YAO  HAYO kirahisi LABDA  itakuwa ni KUBUNIA TU .:-(

Swali:
  • SI unajua kuna MAMBO labda yana JIBU ila JIBU lake  sio lazima awe nalo MTU?
  • Si unajuwa jibu la tatizo la  KUBUNIA na KUOTESHWA  kama la BABU wa LOLIONDO linaweza kuwa ni sawa kama HUNA IMANI na maswala ya KUOTESHWA?

Ndio,...
... labda bado ni kweli kila kitu hata kisichomuhusu MWALIMU NYERERE kina JIBU,...
... ila  haki ya nani  HAKUNA  mtu  ajuaye   kwa usahihi NA UHAKIKA  hilo JIBU .:-(

Swali:
  • AU?
  • Na kukosa jibu na kukiri ``HAKUNA JIBU´´- si labda ndio  aina moja wapo ya JIBU aka ndio jibu LENYEWE?
Na najua ,...
.... ni silika ya BINADAMU kutafuta MAJIBU,....
..... lakini labda kuna mambo KUTOYAJUA ndio  chanzo cha FURAHA maishani ,...
.... kwa kuwa labda KUJUA kila kitu sio UBINADAMU na  wala hakuboreshi  UBINADAMU,...
.... ukizingatia kuwa hata tukijua kama NYERERE angeanzisha BLOGU angekuwa anafuatiliwa na watu wangapi isingesaidia kuweka tonge mezani  mwetu na wala isingetusaidia sana kupata hata kificha nyeti kwa wengi wetu!:-(

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu tumfuate tena hko Kameruni mdada SANDRA NKAKÉ arudie -I miss my LAND



Sandra amwage kitu kiushauri kuwa -Stay True




Au anikune tu tena kwa sindimba-Higher

Read more...

Nachofikiria WAKATI naangalia UNACHOANGALIA,....

.... ndio ,...
.... kinaweza kuwa TOFAUTI.:-(

Swali:
  • SI unajua kuna aangaliaye mdada  KIBONGE kama njemba tu yenye bonge ya KITAMBI na kuwaza uzuri na ULIMBWENDE  wa huyo TIPWATIPWA wakati  kuna mwingine wakati huohuo akimuangalia huyohuyo  BWANYENYE bonyebonye na afikiriacho kwa UNENE WAKE ni magonjwa na sio ULIMBWENDE wala uzuri wa huyo AJUZA -kitu kimfanyacho afikirie jinsi ya kumshauri apunguze UNENE  ili awe na afya njema?




Ndio,...
.....wapigao chabo mchezo huohuo wa unyumba hawafikirii SAWA,....
..... na ndio maana ajali ikitokea BONGO sio wote wakimbiliao palipotokea ajali wanakwenda kuokoa watu  ukizingatia wengine wafikiriacho ni DILI LA  kusachi maiti mawaleti  tayari wakiwa na mipango ya kutanua baadaye BAA kama ikitokea waliofariki ni wengi na walikuwa wanasafiri na NGAWIRA pesa za kutosha kwenda kwao huko uswekeni .:-(


NI wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(



Hebu tubadili wazo hili nishai kwa kuangalia mazoezi ya mchezo wa  GOLF  kiduchu.....




Au tukadeku tu tena Aerobics



Kama vile ujinga haukutosha vile....:-(



OK imetosha sasa!

SIKU NJEMA!:-(

Read more...

The one and only -JOHN KITIME!

>> Monday, March 21, 2011

Kuna dogodogo wa engo za BONGO FLEVA na hata za SINDIMBA  wasahauo kuna MTUZ kimiziki kama JOHN KITIME ,...

... ndio waliowahi mpaka kupata GRAMMY katika wanamuziki wa TANZANIA,....

GRAMMY kwa MFAFANUO kiduchu  ambayo JOHN KITIME kashawahi kupata kwa kutambublika KIMATAIFA kwa UMAHIRI -kwa kibena ni:

A Grammy Award (originally called Gramophone Award) — or Grammy — is an accolade by the National Academy of Recording Arts and Sciences of the United States to recognize outstanding achievement in the music industry. The annual awards ceremony features performances by prominent artists, and some of the awards of more popular interest are presented in a widely viewed televised ceremony. It is the music equivalent to the Emmy Awards for television, and the Academy Awards for film.

The first Grammy Awards ceremony was held on May 4, 1959, to honor musical accomplishments by performers for the year 1958. The most recent ceremony, the 53rd Grammy Awards, was held on February 13, 2011, at the Staples Center in Los Angeles.




Mtembelee ujifunze miziki ya TANZANIA ,...
... HAPA kwa zamani ,...
.... au hata HUKU  kupya kiduchu kama mdadisi.



Hebu Anania Ngoliga ambaye ni NGULI MWINGINE mwenye kidude Grammy kutoka TZ aka BONGO NYOSO  atekenye NENO na kifaa,....




ANANIA adinye zaidi nanihii chini kidogo karibu kabisa na nanihii kwa....



Au tu John KITIME aturudishe kwenye NJENJE ambako anatekenya maswala kwa GITAA na SAUTI katika bendi ya THE KILIMANJARO BAND kama kawa ashambulie jukwaa kwa-Masafa MAREFU




Sijui kwanini ila ngojea tu King Kiki  arudie tu naye-MASANTULA

Read more...

Kuna FARAJA za KUZEMBEA na KIFARAJA uzembe labda ndio unifanyao pia MIMI na MALAYA WANGU tusiendelee KUJITAHIDI!:-(

Tahadhari: Taralila hii si nzuri kwa MFANYAKAZI BORA!:-(





Ndio,....
... pamoja nakuwa KUJITAHIDI, kuhangaikia vitu na KUJITUMA kwa wenye busara FARAJA ZAKE ndio huzisifia hata kuzitukuza kwa kubobea katika wadaivyo ni malipo manono mtu upatayo BAADA YA KUJITAHIDI na kuhangaikia,...
.... lakini labda tusisahau kuwa labda kuna FARAJA pia za UVIVU na kuzembea ,...
.... na ndio maana labda kuna MIJITU kibao inazembea na ni fulu KULA kulala.:-(

Swali:

  • Na si inasemekana kwa hata kwa WAFANYA KAZI kwa BIDII wakishapata wanachohangaikia FARAJA waipatayo kwa hilo haidumu na kwa hiyo itabidi waanze tena upya kuhangaikia kitu kingine ili kufukuzia FARAJA kama hiyo tena?:-(



Ndio,...
....Labda UZEMBE na UVIVU vinafaraja zake pia aisee,...
.... na ndio maana si kila mtu anafuata busara za hata mpaka vifichwavyo na chupi za malaya kuvihangaikia.:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Jumatatu NJEMA  na KUJISHUGHULISHA kwenye faraja kwema MKUU!


Hebu twende Kameruni ili Sandra Nkaké arudie kuomba mtu awe-Sex Friend





The Hypnotic Brass Ensemble warudie-Planet Gibbous



Au tu Hypnotic Brass Ensemble wamalizie tu kwa - Balicky Bon

Read more...

Inajulikana kuwa SIRI kubwa ya KUANDIKA ni kuanza tu KUANDIKA!

>> Sunday, March 20, 2011

Tatizo linalojitokeza tu  ni kuwa ,....

...ukianza kuandika,....
... unastukia kwa UWAZI zaidi kuwa  kuna KUANDIKA VIZURI  pia kuhitajikako katika UANDISHI haki ya nani tena ,...
... ambako kwa WENGI WETU  kunahitaji mazoezi kwa kuwa kwa bahati mbaya  hakuji tu HIVIHIVI !:-(



Swali:
  • SI umestukia kuna waandikao na KUNA WAANDIKAO vizuri hapa DUNIANI?
MAANDISHI ni muhimu,....
.....ingawa labda kuna umuhimu pia waujuao WAANDIKAO vizuri  wakaeleweka niwaoneao WIVU!:-(


Nawaza tu kwa sauti MHESHIMIWA,...
.....wakati naendelea kufanyia mazoezi UANDISHI  wa kiaina fulani!:-(





Hebu Mos Def arudie mahesabu kwa-Mathematics



Busta Rhymes ajaribu kulainisha zaidi  kwa-I Love My Chick


Au hebu NYAMA YA BATA isimuliwe vizuri kinyamunyamu iifanyayo NYAMA HI kuwa NYAMUNYAMU  katika ndude ya Off Side Trick akiwa na Mzee Yusuf na Sella wakimuongelea-BATA...

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP