Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Heri ya Mwaka mpya wa Kalenda ya Kirumi!

>> Sunday, December 31, 2006



Katika siku hii heshima yangu kwa wanawake wote!Mama yangu Zilpah Asante kwa yote! Namuachia Shaggy aelezee kwenye wimbo Strength of a woman....


Kwa wengine nawaaga mwaka huu kwa wimbo huu wa Capleton...

Read more...

Dini au Utaifa kwanza?

>> Saturday, December 30, 2006


Hivi wewe ni Muislamu au Mkristo kwanza halafu ndio Mtanzania au ni Mtanzania kwanza halafu ndio mpagani?
Nauliza tu, usitishike!

Read more...

Chakula cha Mawazo-Biblia !


Katika vitabu ninavyovipenda kimoja wapo ni biblia. Leo naendelea kusoma historia ya kitabu hiki kama nilivyosema kwenye video hapo juu.Nitaandika zaidi siku nyingine lakini kwa kifupi historia ya kitabu hiki huwa inanizingua sana .Najaribu kukisoma na kuendelea kujifunza kutoka kwa watu wengine wengi . Na kila mara nakutana na watu wengi wenye maelezo tofautitofauti wakiwamo hawa hapa chini...

na mwingine huyu hapa..


Pia ningeomba mtu mwenye data nzuri za kuaminika kuhusu historia ya Kuran zaidi ya hii hapa anisaidie dondoo za vitabu au sehemu nayoweza kujenga picha zaidi ya jinsi kilivyoandikwa na kutunzwa mpaka sasa.Ningependa zaidi kujua histori ya jinsi maandishi yalivyokuwa yanaandikwa au kukaririwa katika kipindi Quran ilipoandikwa.
Nakuacha na Injili ya Yuda hapo chini, wakati nikiendelea kutafakari kasoro na upungufu wa kiubinadamu unaotukabili sisi wanadamu.

Read more...

Wakati tukondani ya KWANZAA na tukisubiri Mwaka mpya wa Kalenda ya Kirumi...

>> Thursday, December 28, 2006


Kabla sijasema sana ningependa kuachia The Last Poets wamwage shairi....


Watu weusi bado tumegawanyika sana.Moja ya mgawanyiko ni ule wa Weusi wa Afrika na weusi wenye asili ya Afrika ambao kuwako kwao mbali na Afrika ni matunda ya utumwa, na wengine ambao walihama wenyewe. Waafrika ndani ya Afrika bado tumegawanyika sana pia, kimakabila , kidini,kiutajiri au umaskini na mambo mengine kemukemu ikiwa mpaka rangi.Unakumbuka katika kundi la watu weusi bado tunabaguana kwa rangi , nani mweupe na nani mweusi? Watu weusi waishio mabara mengine nao wamegawanyika kwa hali ya mali,elimu na hata jinsi ya toni za mwonekano wa rangi ya weusi wao . Marekani na sehemu nyingi bado ile hali iliofanya watumwa weupeweupe kupewa kazi za ndani na wale weusi kabisa kazi za nje bado upo.Hivyo bado wale weupe weupe mara nyingi huonekana wazuri kuliko weusi kabisa. Hiki kitu ndio kile kile kinachofanya akina dada kujichubua Afrika katika kutafuta kuwa weupe weupe kwa imani ya kuwa ndio uzuri. Hivi uzuri ndio nini?Haya mambo ambayo binadamu anajitengenezea akilini na kutengeneza mazingira ya kuhalalisha mtazamo yanazingua sana.

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana! Kila wakati na kila siku yuko shuleni. Anajifunza ladha na anajifunza kuishi katika mazingira yake. Ndio maana kila siku utasikia, alah! Hiyo fasheni imepitwa na wakati! Halafu ghafla atakuambia nilipoonja bia kwa mara ya kwanza sikupenda ladha yake.Wakati yeye ndiye ajulikanaye kwa unywaji wa bia. Binadamu huyo huyo katika kutafuta kujiridhisha huwa anapenda kujifananisha na wenzake na kujipima kupitia wenzake. Hii pamoja na kujipatia furaha pia huleta mikwaruzo ndani ya jamii.Mikwazuzo hii hutugawa lakini pia kutujenga.Tatizo letu watu weusi bado tumeshindwa kuunganisha nguvu zetu na mikwaruzo yetu inatubomoa zaidi yakutuletea changa moto zakutujenga.


Tukirudi kwenye KWANZAA, mimi naona ni moja ya jambo ambalo pamoja na mengine linajaribu kuunganisha watu weusi. Na nafikiri jambo lolote liunganishalo watu weusi wenye asili ya Afrika ni jambo muhimu kwa sababu umoja tuna uhitaji sana sisi kama watu weusi.Vizazi vijavyo vya watu weusi vitashindwa kutuelewa ni namna gani Afrika pamoja na mali zetu bado tumefanikiwa kuwa masikini na wanyonge hivi.Kizazi chetu hiki tu bado tuna maswali ilikuwaje wakoloni wachache waliweza kututawala .Unakumbuka tulikuwa tunawabeba kuwasafirisha maporini? Unakumbuka mara nyingi ilikuwa waafrika wanne wanambeba mzungu mmoja na anatoa amri hata huko msituni, huku watu wakitii?Sasa fikiria baada ya miaka kadhaa sisi ndio tutakuwa somo.Vizazi vijavyo watajiuliza, hivi hawajamaa vipi? Kila siku kugombana tu huku wakijua maugomvi yao yananufaisha wengine.

Sasa hivi kuna Wamarekani weusi watambuao umuhimu wa Afrika katika maisha yao lakini wapo wengi wachukiao Afrika na waafrika.Wao kwa wao hawana umoja , wamegawanyika hadi kwenye maadili.Waangalie wengine hawa hapa wakijielezea....


Nasi Afrika hatujakuwa mfano mzuri wakujivunia. Na katika hili na kubaliana na wale wanaoenzi nguzo saba za kwanzaa ambao wanatafuta maadili kutoka Afrika ilikujisikia kamili.Kwani hata kwa hili kuna kaumoja kanajengeka. Kumbukeni kama watu weusi ni miaka mingi imepita bila kula raha na kufurahia uweusi wetu.Ngoja Mighty Diamond wakukumbushe hapa chini...



Sasa mimi na wewe tunafanyanini katika kuleta mikwaruzo yetu na tofauti zetu kama watu weusi iwe inatujenga zaidi ya kutubomoa?

Samahani nilisahau kuwa bado tuko katika shamra shamra za KWANZAA, kusubiri mwaka mpya na kadhalika nyingi!Haya basi tuendelee kufurahi. Nakuacha na Lagbaja hapa chini.


Heri ya KWANZAA!

Read more...

Bado Mawazoni!

>> Tuesday, December 26, 2006




Leo nasikiliza sana Zouk, kama za Kassav hawa hapa chini.....



lakini pia mdundiko na nyimbo mbalimbali nazipitia pia ingawa wimbo huu hapa chini uitwao Kiuno Viuno unanifikirisha kidogo!Hii sio kutiana majaribuni?

Read more...

Nafikiria nini kuhusu Krismasi na Mwaka Mpya!

>> Monday, December 25, 2006


Nafikiri binadamu mara nyingi hutafuta sababu ya kusherehekea.Hii ni kawaida.Tanzania katika mila zetu utakuta sherehe hizi nyingi tu. Kuhusu Krismas kama siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa yesu ni tarehe iliyo buniwa tu. Tafiti nyingi zinadai kuwa kwa kufuata kalenda tuitumiayo na mambo mengi yaliotokea kipindi cha kuzaliwa kwa yesu inawezekana kabisa ikawa Aprili ndio kipindi.Hata hivyo hakuna uhakika asilimia mia wa siku hiyo.Na nukuu nyingi hizi zilizoko kwenye biblia ziliandikwa miaka mingi baada ya kufariki kwa yesu.

Kuhusu mwaka mpya ndio hivyo tena ukifuatilia historia ya kalenda na ukajiuliza kwanini watu wengi walikuwa na kalenda tofautitofauti, na bado wana kalenda tofautitofauti utapata jibu.

Kuhusu Santa Klaus au Saint Nicholaus- askofu wa mji wa Myra,Uturuki na kuibiwa na Waitaliano waliomhamishia mji wa Bari na kuingia dili na kanisa ilikukuza utalii kwa kumtangaza. NAfikiri unajua nafikiria nini. Lakini Cocacola Kampani ilimtafutia vazi zuri ilikupendeza akitangaza Coca cola.

Tukiachana na hilo, nadhani asilimia kubwa yetu tunapenda sherehe na tunapenda zawadi.Nafikiri hakuna haja ya kufuatilia sana mambo haya maana utaondoa utamu wa sherehe yako. Heri ya Krismas na Mwaka Mpya, lakini kumbuka siku ya krismas na mwaka mpya zaweza kuwa ni siku yoyote ile uamkapo, na hizi siku tusheherekeazo ni binadamu kama mimi na wewe waliozitunga.

Read more...

Wakati bado Soul na Funk ikiniburudisha- Hello Brother Curtis Mayfield!

Brother Curtis Mayfield Semanaye basi!

Superfly!




Move on Up!

Read more...

James Brown afariki!


Mzee James Brown ndio kaanza hivyo. Mimi kama mpenzi wa Soul , Funk amekuwa akiniburudisha muda mzefu tu. Uwezi pia kusahau mchango wake kwenye Hiphop na miziki mingine.Mzee kafariki akiwa na umri wa miaka 73 baada ya kupata nimonia.Pumzika Mzee!

Hapa Chini mwaka 1966 akikupa zile nyimbo zake. Baba ana mkoba mpya na pia ule wimbo najisikia vizuri


Hapa chini katika mwaka 1966 vilevile akinipa nyimbo kadhaa ukiwamo ule utukumbushao kuwa leo inawezekana ikawa ni siku yetu ya mwisho kuwasiliana ,kusalimiana, kushikana mikono na kadhalika. Duh unajua hii leo inawezakuwa siku ya mwisho kwetu wote?Samahani nilio wakosea na nimewasamehe mlionikosea.Kama hatukutani tena bye bye!

Read more...

Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya!


Read more...

Leo Mawazoni-Tanzania hali ni mbaya haikubaliki

>> Wednesday, December 20, 2006


Sitaki hata kuongelea hili swala kwasababu Mwandani kaliongelea vyema na yeyote ambaye hajamsoma Eldridge Cleaver namshauri amsome.Lakini ukitaka kufaidi anayosema usiishie kusoma historia yake Eldridge tu.

Read more...

Sanaa Babu kubwa!

>> Tuesday, December 19, 2006

Ijumaa iliyopita nilipata kushuhudia bomba ya kazi ya sanaa iliyofanikishwa na Wasanii wa kitanzania Arnord Chiwalala, Menard Mponda na Aliko Mwakanjuki. Hii kazi ya kimataifa ilihusisha Tanzania na Umataifa kwa namna ambayo ukitaka kuelewa kongoli hapa. Nitaipandisha kwenye blogu baadaye.Kutokana na matatizo ya kitekinolojia ndio maana haijapanda bado.Halafu kongoli watch the recorded broadcast in Real Player

Read more...

Cola za Kiislam VS Coca Cola.

>> Tuesday, December 12, 2006

Inanizingua sana mara nyingine ninavyostukia jinsi gani mazingira ya vita yanavyoweza kuzua aidia za biashara.Leo nimeamua kuangalia jinsi mazingira ya vita yanavyo neemesha biashara za cola.

Miaka ya themani mpaka tisini kulikuwa na vita ya Cola (Cola War) ambayo ilihusisha Coca Cola na Pepsi. Hii ilisababisha Cola hizi mbili kutangazwa kupita kiasi, hivyo kuuzwa sana.

Sasa hivi kuna vita ya Cola ambayo inaibuka ihusishazo Cola ziuzwazo kwa malengo ya kupiga vita utawala wa vinywaji vya Cola kutoka Marekani na pia maadili yake. Vinywaji kama Qibla Cola , Mecca Cola na Zam Zam Cola ambavyo vimeanzishwa na kuwalenga zaidi waislamu ni miongoni tu mwa vinywaji hivi.Nawasifu wabunifu wa miradi hii ambayo inakusudia kutumia asilimia kadhaa ya faida itokanayo na mauzo ya vinywaji hivi kusaidia Jamii zao.

Coca Cola katika tangazo mwaka 1917






Ukifuatilia kinywaji cha Coca Cola utagundua jinsi asilimia kubwa ya ukuaji na utawanyikaji wa kinywaji hiki ulivyo saidiwa na vita. Kinywaji hiki ambacho mwanzo wake kilitumia malighafi kadhaa ikiwamo cocaine hapo kitambo , ndio kinywaji cha kola maarufu kupita vyote mpaka sasa. Vita kuu ya pili ya dunia ilisaidia kukitawanya kinywaji hiki baada ya mwenye kiwanda kukubaliana na serikali ya marekani ku peleka kinywaji hiki kwa wanajeshi wakimarekani popote walipo duniani na kwa kufanya hivyo kiwanda hakitahusishwa katika mgao maalumu wa sukari ambao ulikuwepo Marekani kutokana na upungufu wa sukari.


Vita vilisababisha uanzishaji wa viwanda sehemu mbalimbali duniani ilikukidhi mahitaji ya kinywaji hiki kwa wanajeshi.Na pale vita vilivyozua kasheshe nchini Ujerumani hivyo Kiwanda cha Coca Cola kikaanzisha Fanta pale Ujerumani. Hivyo utaona kuwa kutokana na vita Fanta ikazaliwa.


Mecca Cola na muanzilishi wake Mr Tawfik Mathlouthi












Sasa leo hii tuko katika vita vyingine ambavyo vinaleta msuguano kati ya nchi za magharibi na za Kiislam.Na hii vita inaonyesha kuzalisha wanunuzi wapya wa vinywaji vipya na kwa asilimia kubwa si kwa sababu ya utamu wa vinywaji hivi, bali maadili yahusishwayo na vinywaji hivi.
Qibla Cola

















Vinywaji hivi kama Mecca Cola, Qibla Cola , Zam Zam Cola nk, vinafanikiwa sana katika jamii wazilengazo. Inasemekana watengenezaji wa Mecca Cola walishawahi kulalamika kuwa katika soko la Uingereza wanapata tabu kutokana na kuwepo kwa Wapakistani wengi ambao hupendelea Qibla Cola ambayo hutengenezwa na Wapakistani.

Zam Zam Cola














Nachojiuliza tu ni kwamba je hii staili ya kuvitangaza kwa kuvihusisha na dini itafaa katika muda mrefu?Nashangaa kwanini kampuni zitengenezavyo vinywaji hivi haviungani ilikuwa na nguvu zaidi ya kupambana na Coca cola?Au ndio ushindani wa kibiashara utakaoleta ubora katika kampuni hizi?Kama ndio hivyo hii si ndio ileile filosofia ya kimagharibi ambayo Coca Cola inaindeleza?


Je, na Afrika tunahitaji kinywaji chetu cha Cola ambacho kwa kukinywa tutakuwa tunajua kuwa pasenti fulani inaenda kusaidia Afrika?

Read more...

Kutoka mdomoni mwa Spika wa Bunge la Tanzania

>> Tuesday, December 05, 2006

Wiki kadhaa zilizopita nilipata kusikia hoja moja kwa moja kutoka mdomoni mwa Spika wa Bunge, Mzee Samwel Sitta. Kuna mengi aliongelea. Ingawa pia kuna mengi hakuweza kuyaongelea kutokana na muda mdogo uliokuwepo na maswala na maswali kuwa mengi.

Aliongelea umeme. Akasema kuwa sasa hivi ndani ya Tanzania kuna mpango wakutumia nyanja tatu za uzalishaji wa umeme. Kuna Wachina ambao wataanza kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe katika sehemu mbili tofauti Tanzania.Pia kuna mpango wa kuongeza sehemu moja ya uzalishaji wa umeme kwa maji.Umeme wa gesi unafanyiwa mpango kuingizwa katika mfumo pia. Kwa kifupi kuhusu mashine mpya za dharura ziletazo majadiliano mengi mtandaoni amesema zinahitajika na pia kuwa bila mashine hizi za muda sehemu kama za Mwanza zingekuwa zinakosa umeme masaa ishirini na nne.

Kuhusu matatizo ya Zanzibar alisema tatizo kubwa liko katika uhasama uliojengeka kabla na baada ya mapinduzi. Asilimia kubwa ya wenye asili ya kiarabu au kipeshia ndio waliokimbia visiwa baada ya mapinduzi. Na wengi wao ,takribani laki tatu wako Uarabuni. Hawa na ndugu zao ndio wenye pesa na elimu. Maana hawa ndio walioweza kuwasomesha ndugu zao visiwani na hata nje. Lakini hawa ndio ambao wanachuki juu ya yaliyotendeka baada ya mapinduzi. Baadhi yao walilazimika kuolewa na wasiowapenda hata kuzalishwa na wasiowapenda. Sasa hivi wengi wao ndio wako katika upinzani visiwani.Kwa mtazamo wa Spika hawa jamaa hatakama wanaona ukweli wa mambo hawawezi kuukubali kwani bado yale machungu yayaliowatokea bado yapo ndani ya jamii yao. Hivyo ni vigumu kudili nao kwani mara nyingi ni machungu ya kihistoria ya wapandishayo mori na sio hali halisi ya mambo.

Kuhusu Umoja wa Afrika Mashariki , yeye anaona hakuna haja ya Watanzania kuuogopa muungano. Alisema kunanjia nyingi za kisheria ambazo zitawalinda Watanzania katika mambo mengi. Anasema kuwa kwa mfano ndani ya muungano kutakuwa na sheria kama za kuzuia asiyekuwa Mtanzannia kumiliki ardhi Tanzania nk.Alisisitizia kuwa tunahitaji kuungana ililikukuza soko la Afrika Mashariki kwani tukijitenga ni vigumu kuvutia wawekezaji wenye kuvutiwa na soko na pia itasaidia kujengea wanaafrika mashariki soko kubwa zaidi la bidhaa zao.

Aligusia pia maswala ya Watanzania waishio ughaibuni na maswala ya usalama wao. Anasemakuwa serekali inajua matatizo ya Watanzania Ughaibuni na inayafanyia kazi. Anasema baadhi ya misiba iliyotokea Ughaibuni ilipewa hadhi iliyokaribia ya msiba wa kitaifa Tanzania. Alisisitiza watu kujisajili kwenye mabalozi yao ilikuwezesha baadhi ya mambo yawe rahisi kwa balozi kushughulikia.Alisema serikali inafuatilia vifo na matatizo ya Watanzania ughaibuni.

Kuhusu wawekezaji wa Kiafrika kusini alidai kuwa si kweli kuwa wao ni wabaya. Alidai matatizo mengi ya kibiashara na dhuluma za kibiashara hufanywa na wahindi.Alisema kuwa kwanza mfumo uingizwawo na waafrika kusini unasaidia kurekebisha biashara. Kwa mara ya kwanza unaweza kupata uhakika wa bei za vitu na pia wameleta utumiaji wa viwango vya ubora wa bidhaa ndani ya biashara Tanzania. Anasema si kweli kuwa Waafrika kusini hawanunui bidhaa za Tanzania. Anasema wao hutoa viwango vya ubora wa bidhaa watakazo kuzinunua. Katika mazao hutoa mpaka aina za mbegu za vyakula watakavyo kuviuza. Na watanzania wote wafikiao viwango vitakiwavyo ,bidhaa zao huingizwa dukani.Alisema kuna tatizo sana kwa wahindi kufanya biashara chini ya meza na kupeleka pesa nchi za nje.

Haya ni baadhi tu ya aliyo yasema muheshimiwa.Maswali mengi hakujibu kutokana na muda.Nikikumbuka mengine aliyoongelea nitayaandika hapa.

Read more...

Baada ya mafanikio ya Asia je, ni Afrika iatakayofuata?


Hakuna ujanja, baada ya Asia itakuwa ni zamu ya Afrika.Huu ndio mtazamo wangu.Kwa jinsi uchumi wa Asia unavyokua ni rahisi kujua kuwa na gharama za uzalishaji wa bidhaa zifanyazo makampuni mengi yaende Asia kuongezeka. Na kama kawaida ya mfumo wa biashara ulioshamiri duniani lifuatalo ni wawekezaji kukimbilia katika sehemu ambazo wanaweza kuzalisha bidhaa zao kwa bei ya chini. Sehemu ambayo haijatumiwa kisawasawa katika uzalishaji mali ni Afrika. Asia ilipata umaarufu kama sehemu ya kuzalisha mali kwa sababu kubwa mbili,unafuu wa gharama za uzalishaji na pili, uwepo wa wafanyakazi wenye taaluma za kazi.Ingawa pia huwezi kupuuzia nguvu ya idadi ya watu waishio Asia ivutiayo wawekezaji kwa sababu ya soko kubwa.

Tatizo kubwa la Afrika ni ukosekanaji wa wafanyakazi wenye taaluma za kazi.Ukosefu wa mfumo uelewekao uwezeshao mambo kufanyika. Hapa na maanisha udhaifu wa institutions na mifumo iwezeshayo mambo kufanyika. Tatizo la nishati za umeme ziwezeshazo uendeshaji wa viwanda.Ukosefu wa nguvu za ununuzi kutokana na umasikini wa watu.Haya ni baadhi tu ya mambo yatatizayo. Lakini, bado kila kukicha utakutakuwa inakaribia siku ambayo dunia haitakuwa naujanja wa kukwepa Afrika kwani ,Afrika inazidi kuwa ndio sehemu itakayo kuwa inatoa faida zaidi katika mitaji ya wawekezaji.

Inashangaza jinsi viongozi wetu Afrika wanavyoweka umuhimu wa mambo gani yatendeke ili kuboresha nchi zao. Unakuta kiongozi anazunguka dunia kutafuta wawekezaji katika viwanda wakati anajua wawekezaji hao hawawezi kufanya lolote bila ya nishati ya umeme. Mifano ipo mingi tu ambayo hata haileweki kuwa hawa viongozi wetu wanafikiria nini.

Si ajabu sasa hivi kuona Wachina wakihamia Tanzania ingawa kwao Uchina ndio wawekezaji wengi wa kimataifa bado wanakimbilia. Hii ni moja tu ya kidokezo kuwa tabaka la wenye navyo Uchina linazidi kuongezeka hivyo wengine inabidi wakimbilie sehemu ambazo wanaweza kujishamirisha bila kuwa na mtaji mkubwa.Pamoja na sera za serikali kusababisha hili kuwezekana sasa, lakini ukweli kwamba hili ni jambo ambalo imefikia kipindi chake kutokea hasa ukiangalia mwelekeo wa uchumi dunia nzima.Ukiangalia hata mwelekeo wa nguvu za nchi ziendeshazo mifumo iliyojengeka duniani zinavyobadilika utapata dondoo nyingine.

Sitaki kuusifu huu mfumo wa kibepari ambao umetunyonya kwa mamia ya miaka, lakini najua mfumo huu unakasumba moja, nayo ni kwamba hufikia wakati mewnye nguvu anakuwa hana uwezo tena wa kutawala mwelekeo wa mfumo. Kwa mfano kuna savei nyingi zioneshazo kuwa asilimia mpaka 60% za Waulaya na Wamarekani wanatishika na ukuaji wa uchumi wa nchi kama Uchina, lakini hakuna ujanja wawezao kuufanya kujitoa katika mahusiano na na nchi hizi sasa hivi. Kwani Wachina wameweza kuwazidi kete katika mchezo wao wenyewe.

Mifumo iundwayo na binadamu mimi naamini huweza kuchezewa kete na binadamu. Ukiangalia maswala ya demokrasia, imedhihirika mara kibao kuwa ilikuwa sio nia ya waihubiriyo baada ya walengwa kuitumia kwa kuchaga kidemokrasia maswala ambayo wahubiri hawakuya dhamiria.Mfano kidemokrasia , Wapalestina wakachagua Hamas jambo ambalo ilikuwa si nia ya Marekani kuhubiri demokrasia itakayo chagua maadui zao. Hili limetokea Venezuela pia baada ya Chavez kushinda tena. Naamini sio demokrasi tu zinaweza kutoa jawabu kinyume bali hata maswala mengine. HAPA NA MAANISHA INGAWA WANAOTULENGA AFRIKA WANATULENGA ILIKUTUNYONYA TWAWEZA KUWAGEUZIA KIBAO WAKAJAKUJIKUTA KUWA SISI NDIO TUMEWAZIDI TUKITUMIA AKILI.Itafurahisha siku tukifikia sehemu China waliyofikia ambapo hakuna ujanja nchi nyingine zawezakuwaletea bali kudili nao tu, hata ikiwa kwa shingo upande.

Afrika na pamoja na umasikini wa serekali zetu hatuwezi kujitoa kirahisi katika mfumo.Bado asilimia kubwa za pesa ziendeshayo shughuli Afrika ni tupewazo na wamagharibi. Mpaka uendeshaji wa Afrika Union unashindikana kutokana na ukosefu wa pesa na kila ukifanikiwa ni kwasababu kunamfadhili katoa pesa.Sasa tuna taratibu gani au strateji gani zitakazo tupa nguvu ya kuja kuzishika nyenzo za kiuchumi za nchi zetu?Je , mipango hii tuwekayo inatazama mbele? Au ndio kama maswala ya umeme?Kwa maana maswala yaumeme hayakupewa mstari wa mbele kama maswala ya rada na ndege ya Raisi. Je, Viongozi wetu wanaona mbele?

Read more...

Vyakula vipo duniani, mbona twafa njaa?-----Na .1



Konokono huyu kanona!









Konokono huliwa sehemu nyingi lakini ni maarufu zaidi Ufaransa , Uspain ,Italy na Ureno. Afrika kusini kwa sasa ndio inaongoza katika nchi za Afrika katika biashara ya kimataifa ya konokono. Ushawasikia wakinamama hawa wa Western Cape township walivyojiajiri katika maswala ya kukusanya konokono?Kwa habari zaidi kuhusu kama unadhurika (allergy) kivyovyote kuhusu msosi huu soma hapa

Chura aliye nona kabla ya kuingizwa jikoni.










Kwa habari zaidi kuhusu msosi wa chura na kama unazurika naye (allergy) soma hapa






Chura hawa washaiva , karibuni mezani.









Panzi ni msosi babu kubwa











Nyoka ni msosi mahali pengi.King Cobra pichani ni miongoni mwa nyoka ambao katika mitaa ya nchi kama Thailand, damu yake pia ni kinywaji kiaminiwacho kuongeza nguvu za tendo la mapenzi na pia dawa kwa magonjwa














Bado najiuliza, nini kinasababisha tufe njaa Tanzania ?Kwa maana sidhani hata inahitaji kuangaika sana kutafuta mnyama, mdudu, ndege nk ambaye analika.

Read more...

Tufurahi tufurahi Wikiendi eh!

>> Saturday, November 25, 2006

Duh ingekuwa poa kuwa binadamu wangekuwa wanfuraha siku zote. Unamkumbuka The Cool Ruler?


Gregory Isaacs katika baadhi za nyimbo zake zinazonikumbusha mbali sana.

Read more...

Kikao na Spika Wa Bunge la Tanzania

Nikiwa na Spika , Balozi wa Tanzania mwenye makazi Sweden na mbunge









Jana tulikuwa tukimsikiliza Spika wa bunge. Nikipata nafasi nitaleta dondoo zilizotoka kinywani mwake.

Read more...

Chakula cha Mawazo!- Ukimwi!

>> Friday, November 24, 2006


Jacob Zuma alidai alioga kuzuia virusi baada ya kufanya mapenzi na mwanadada mwenye ukimwi.











Kwa nini binadamu anauwezo wakufanya mapenzi na mtu mwenye ukimwi kwa hiari yake mwenyewe hata kama anajua kuna kufa?Je unamkumbuka Jacob Zuma?

Niliwahi kuulizwa maisha ni nini? Swali hili nikashindwa kulijibu kwani lili nisababishia maswali mengine mengi sana. Naamini binadamu mara nyingi anaishi akitafuta maana ya au uthamani wa maisha! Kwa wengine maisha yanaanza kuwa na maana pale anapo kuwa na watoto. Hivyo watoto wake wana kamilisha au kutoa jibu la kwanini aamke asubuhi kwenda kazini au hata ajitunze. Wengine maisha kwake yanakamilika kupitia mitazamo ya kidini. Anaamini yuko hapa kwa mpango wa Mungu na hivyo basi moja ya mambo yaletayo maana kwake ni pamoja na kumtukuza Mwenyezi Mungu. Anautunza mwili wake kwa sababu mwili ni hekalu la Mwenyezi Mungu. Kuna mwingine maisha hayana jibu sahihi. Hivyo ni lazima awe katika hali ambayo inamsahaulisha machungu ya maisha ambayo yanaonekana ndio pekee yana tawala maisha.Wengine wanaishi maisha yakutokujali lakini wakijua kuwa hawajali. Wengine wanaishi maisha ya kutojali lakini kwa sababu hawajui wamejiingiza kwenye nini.

Hivi ushawahi kujiuliza kwanini unataka kuishi muda mrefu?Hivi ushawahi kutamani maisha waishio Wazee wa miaka mingi? Hivi ukikumba ukimwi na maisha yako yakafupika na labda ukafa kwa kuteseka sana inakutisha? Je, ukikumba mdudu utawatesa watu wa karibu yako?


Lakini hayo yote ni maswala ambayo wewe mtu mzima unaweza kuyatafakari. Kwa watoto ambao wanakumbwa katika janga hawana chaguo kubwa. Hawana uwezo wa kuelewa hata wamekumbwa na nini!Hawajui ngono wala nini! Je unawakumbuka hawa watoto wanao kumbwa katika janga kama hili?Mimi sijui mengi lakini nafikiri angalau viumbe wasio na hatia wasiingizwe katika kasheshe litokanalo na chaguo mtu mzima mwenye akili timamu achagualo kufanya.Tujaribu kuwafikiria watoto. Tujaribu kuwafikiria watu tunao wajali. Hivi wewe unamjali nani?Je, uko tayari kivyako au ukishakufa ndio imetoka hiyo ndugu na jamaa watafanya mambo?

Angalia nyumba hii ya Rehema hapo Kenya:

Read more...

Tulijifunza nini kutoka Kwa akina Khmer Rouge na Mao Tse-Tung

Baadhi ya Mafuvu ya waliokufa baada ya Khmer Rouge kuamua watu wote wawe wakulima.








Nimejikuta katika siku za karibuni nikiingia katika mijadala ya kilimo. Baadhi ya watu wamekuwa wakifikiri kuwa nabisha kuwa kilimo si muhimu hasa baada ya kusema kwamba siamini kuwa matatizo ya Tanzania yana jibu moja kama baadhi ya watu wapendavyo kutaja kilimo kama ndio jawabu pekee. Mwanablogu Luihamu alifikia mpaka kutunga shairi akitaja jina langu na la Ndesanjo kuhusiana na maswala haya ya kusisitizia umuhimu wa kujali umuhimu wa nyenzo nyingine katika kutatua matatizo ya Tanzania. Bado hapa napenda kukazia kuwa tunahitaji kila ujuzi ilikuweza kufanikiwa Tanzania. Mkulima alivyo muhimu ndio hata mwana tekinolojia, mwana sayansi ya jamii, mfanyabiashara, nesi , dakitari na taaluma zote zilivyo muhimu katika kujenga nchi yetu.

Nimeona labda nikumbushe watu historia kidogo igusayo maswala yawezayo kutokea kama mkazo wa mambo ukiwa katika eneo moja liaminikalo kuwa hilo pekee ndio njia. Naamini kuwa binadamu kama angeweza kujifunza kutoka katika makosa basi kunauwezekano wakutopoteza muda katika kutafuta matatuzi mengi tu. Siamini kuwa ni lazima kila mtu apitie katika makosa hayohayo wakati unaweza kujifunza kwa makosa wengine waliofanya. Sidhani ni mpaka ushike moto iliujue unaunguza.Naamini mambo mengi tunaweza kujifunza kutokana na kutafakari mafanikio na makosa yetu na yale ya wenzetu hapa duniani. Naamini kwa kufahamu vikwazo na virahisisha mambo ambavyo twaweza kujifunza kutoka kwa wengine tunapata muda wa kuweza kukwepa kurudia makosa na kukazia miundo mbinu ituwezeshayo kuyakabili mazingira yetu na matatizo yetu. Naamini kama Watanzania tunamengi tumefanikiwa na mengi tumekosea na tunazidi kukosea. Ni kweli kama Watanzania si kweli majawabu yote au njia zote walizopita watu wengine basi nasi zitatufikisha paradiso.Ila naamini kuwa kuna mengi twaweza kujifunza kupitia machambuzi ya ni nini wenzetu walifanya na wanafanya katika kutatua matatizo yao. Mara nyingi tunakazanina kujifuza kutoka katika nchi zisemekanazo kuwa zimeendele. Mara nyingi tunasahau kuangalia nchi nyingine ,hasa hatutaki kujifunza kupitia makosa ya wengine. Ili Tanzania iendelee tunahitaji busara zitokazo kila pande na sio tu zile tu ambazo twafikiri ni za nchi zisemekanazo ziko dunia ya kwanza. Leo hii nimechagua Cambodya na China katika historia .

Tukiachilia mbali siasa na mambo mengi yaliyo izunguka Cambodia, utakutakuwa kitu ambacho uongozi wa Khmer Rouge ulitakakufanya ilikuwa ni kuikomboa Cambodia. Walifikia hatua ya kulazimisha watu kwenda vijijini, na kuwa lazimisha wawe wakulima. Ili kuhakikisha kuwa wanapata tabaka la wakulima walitengeza sera zitakazo wapa watu wapya wenye misingi ya kazi ya ukulima au kwa Kiingereza "New People" through agricultural labor. Wakafanikiwa kufuta pesa na mabenki. Wakafuta maswala ya shule na kulazimisha watoto wa mjini wawe wakulima kijijini. Wale wenye elimu walionekana wameambukizwa fikira potofu hivyo wakauawa na wengine kwenda jela. Lakini kwa ujumla walichokuwa wanajaribu kufanya ilikuwa ni kuikomboa nchi wakiamini kuwa kilimo tu ndio njia pekee. Sishangai kuona jinsi gani walishindwa. Lakini kitu nachokistukia ni kwamba mpaka kwenye blogu zetu nakutana mara nyingine na hoja ambazo zinaonyesha kuwa kuna watu bado wanaamini kabisa katika hoja ambazo zina fanana fanana na Khmer Rouge. Nadhani tunakumbuka hata maswala ya vijiji vya ujamaa. Sasa wakati tunajadili kuwa kilimo ndio jibu pekee kama Mzee Luihamu asemavyo tukumbuke basi na baadhi ya mambo yaliyotushindwisha kufanikisha vijiji vya ujamaa . Tukumbuke basi na mambo yaliyoishindwisha Khmer Rouge kuwabakiza watu vijijini . Kwa maana mara nyingi tunawanyoshea watu vidole wakiwa vijiweni mijini bila kukumbuka kuwa kuwapo kwao vijiweni ni matokeo ya tatizo na sio kiini cha tatizo.

Tukienda China, ni vizuri kumkumbuka Mao Tse Tung na kitu chake alichokiita Hatua Kubwa Mbele(The great leap Forward).Yeye aliamini kuwa ilikwenda mbele basi lazima kuingilia maswala ya viwanda kwa nguvu zote. Watu wakalazimishwa kutengeneza chuma majikoni mwao.Chuma ilikuwa ndio ufunguo wa maendeleo.

Posta la propaganda za Mao likikwa mbia ujanja katika kutatua uchumi ni chuma. "Take steel as the key link, leap forward in all fields".








Hatua nzima aliifanyia kazi bila kuwa na ukweli wa mambo ya jinsi gani mambo yafanyike. Hivyo asilimia kubwa ya mambo watu waliolazimishwa kufanya hayakuzaa matunda. Mashamba hayakutosheleza chakula kwa watu. Viwanda havikuweza kuzalisha bidhaa bora. Watu wakafa njaa. Inasemekana katika kipindi hiki hata ndege karibu waishe China kutokana na amri ya kuwaua kwa sababu ya kuamini wanakula mazao. Kutokana na kuua ndege wadudu kibao walizidi kutokana na kukosa maadui wakuwazuia kuzaliwa kwa wingi kupita kiasi. Haya yote huonyesha jinsi gani jambo moja laweza kuzua tatizo jingine kama mipango na utekelezaji wake ni holela.

Sasa kwa nini naongelea mambo yaliyopita? Si ni ukweli kuwa Tanzania sio Cambodia wala China? Jibu ni ndio. Lakini katika kipindi hiki ambacho ni lazima tuende mbele bado kuna mambo mengi yanayoamuliwa na viongozi wetu kienyejienyeji tu.Sasa matokeo yake ni kwamba tuna weza tukajikuta tunaendelea kufanya majaribio(experiments) na maisha ya watu na nchi ilimradi tu kesho inafika.Tukumbuke kuwa bado Tanzania tunahitaji kiongozi mwenye nguvu awezaye kufanya maamuzi kwa faida ya nchi . Lakini naombea kiongozi huyo asiwe kama wa Khmer Rouge au kama Mao ambaye pamoja na mengi kuna mambo mengi alikuwa anayaamua bila kujua athari zake zitakuwa ni nini. Je , unafikiri viongozi wetu wamejifunza kutoka kwa mapungufu ya Viongozi wa Tanzania waliopita? Au ndio mambo ya kutunza statasi quo? Je viongozi wetu wanajifunza jinsi gani nchi kama China ilistukia tatizo na kugeuza mwelekeo?Je tumejifunza kwanini hawakurukia ubeperi kama wa nchi za magharibi kama USA na Uingereza? Je, Kikwete ndio kiongozi wetu atakaye tatua tatizo?

Read more...

Kikao cha wanablogu wa Tanzania.

>> Thursday, November 23, 2006

Kutokana na kuchelewa mkutanoni kutokana na matatizo ya kiufundi nimeona niandike tena kile ni lichokuwa nimechelewa kukipa sauti yangu kuhusu mkutano wa wanablogu.
1. Mikakati ya Kufikisha Ujumbe wa Wanablogu kwa Watu Wengi Zaidi:
Nakubaliana na yaliyo jadiliwa kikaoni. Lakini ningeshauri kuwa kuwepo ndani ya jumuia kamati yenye kufuatilia yenye 2/3 ya watu walioko Tanzania wenye kazi ya kufuatilia nukuu zizungumzwazo katika magazeti redio na Televisheni ili wote wanablogu ambao hatutakuwa tuna jua wamenukuu nini nadani ya Tanzania tuweze kujua kuwa tumenukuliwa kisahihi. Pia kama tumenukuliwa vibaya au kutokueleweka tuweze kupata nafasi ya kujitetea au hata kusawazisha vyombo vya habari kwakutu nukuu vibaya.Member waliobaki watashughulikia maswala ya Wanablogu kama wanukuliwavyo nje ya Tanzania.

2. Maadili:
Nakubalia na na mawazo yaliyotolewa kikaoni.Lakini lazima uhuru wa mwanablogu kusema apendacho lazima ubakizwe. Lugha safi ni muhimu lakini itambulike watu tofauti huchukulia kuwa wametukanwa katika vigezo tofauti. Mimi nashauri lugha ambayo ikataliwe ni ile tu ijumuishayo matusi ya nguoni. Pia mtu yeyote ndani ya jumuiya atakaye fikia kumdhalilisha mtu au nchi kwa kutumia blogu yake bila sababu maalum ambayo anaweza kuzitetea atolewe kwenye aggregator na pia hoja zake zikanwe na kamati maalum ya maadili. Nashauri atolewe ndani ya aggregator kwa muda wa mwaka na ikiwezekana wanajumuiya kumtoa katika viunganishi vyao. Kurudi kwake katika jamii kutokane na kuomba kwake msamaha kwa aliye dhalilishwa kwa kuandika hivyo kwenye blogu yake.Pia lawama za adhalilishawe ziwekwe kwenye tovuti ya jumuiya.

Picha ziwezazo kumdhalilisha mtu pia ziangaliwe.Lakini kama zina ukweli wa hoja zinazoweza kutetewa kwa mtazamo wangu zinaruhusiwa.Ila maswala ya picha za ngono na wasiwasi yanaweza kuteteleza madhumuni ya jumuiya nzima kwa kusababisha kuhusisha na kupotosha mwelekeo wa jumuiya nzima.Sipingi kuwepo kwa blogu za ngono Tanzania kwa sababu ngono ni jambo linalotakiwa kuongelewa, lakini mpaka sasa sijaona blogu ya ngono ambayo inaelimisha Mtanzania maswala ya ngono. Nashauri blogu ya ngono itakayo kubalika ni ile tu ambayo hailengi udhalilishaji wa mtu yeyote na yenye ujumbe uhitajikao katika jamii. Kwa mfano mimi naweza kuikubali blogu ya ngono iwafundishao vijana uroda na madhara yake na jisi ya kuuvinjari kiusalama na kiafya. Blogu za ngono ziwekayo picha za watu ambao hawakutoa idhini ya kutolewa picha zao na kwa madhumuni ya kuwaletea washawasha na ashki wasoma blogu na isiyofundisha mimi nadhani zisikubalike kwenye jumuiya.

Kusiruhusiwe kutukania watu dini zao.Lakini isije tu ikafikia kuwa maswala ya dini ni mwiko kuyaongelea.

Kamati ya ushauri wa maadili iwe inatoa mawazo ambayo wanajumuia watayapigia kura . Kwa mfano ili mtu kutolewa kwenye jumuia ingekuwa vyema kuwe na wiki nzima ya wanablogu kupigia kura uamuzi.Hii ingefanyika kama tulivyo pigia kura tarehe ya siku ya blogu.
3. Jumuiya:

Naunga mkono swala lakuwa na jumuiya iliyo sajiliwa. Naamini itatoa nguvu zaidi kwa wanajumuiya hasa katika maswala ya haki za wanablogu na kazi zao na pia maswala ya kuaminika.(credibility).
Katika tovuti ya jumuiya kuwepo na muhtahsari wa yaliyosemwa katika vyombo vya habari kutoka blogini.Pia kuwe na nyumba ya kuchat na forum ambayo itawezesha wanablogu kukutana mara kwa mara ikiwezekana wakitumia majina watumiayo kwenye blogu zao.Kuwepo na ukurasa wa maoni ya wanablogu na chumba cha ushauri kwa jumuiya ya wanablogu. katika chumba hiki mambo mbali mbali ambayo yanapendekezwa kufanyiwa kazi na kamati ya jumuia yatawekwa wazi.

4. Uongozi:
Nakubaliana na Uongozi wa muda ulioteuliwa .Ningependa jina uongozi lisitumike bali tutumia jina la wawakilishi.Tuwe na kamati ya wawakilishi katika kamati mbalimbali.Kwa mfano tuwe na kamati ya maadili. hii itafuatilia kuwa tunafuata miongozo tunayopanga yakutuongoza kuendelea kuwa huru lakini sio kuwa vyomo vya chuki na kashfa kwa watu. Tuwe na msemaji mkuu ambaye ndio atakuwa anahakikisha kuwa hata katika mikutano yetu hatupitilizi kupita wakati. Tuwe na kamati ya ustawi wa blogu za kitanzania. Hii itahakikisha maswala ya muonekano wetu na ni kwa jinsi gani tunawakilishwa katika vyombo vingine vya habari. Kamati zote ziwe na watu watano. Kwa sababu ni kawaida kwa wanablogu kuzidiwa na shughuli wakati mwingine hivyo kukosa muda wa kufuatilia mambo au kuandika mambo . Tuwe na kamati ishughulikiayo maswala ya elimu ya teknolojia hii ya kublogu na jinsi gani wanablogu na wananchi wataweza kujiboresha zaidi katika matumizi yake. Hapa na maana maswala ya uboreshaji wa blogu zetu na pia maswala ya ufundishaji au uelimishaji wa maswala ya blogu.Kuwena msemaji mkuu wa jumuiya ambaye yeye kwa kupitia ushauri wa jumuia nzima anaweza kuisemea jumuiya ibidipo.
Kuwe na kamati maalumu inayofuatilia jumuiya kama NGO. Hii itakuwa inafuatilia pia jinsi gani tunaweza kujenga akauti ya Jumuiya itakayo wezesha maswala yatakayo hitaji pesa . Mfano, ikiwa mwanablogu yuko matatizoni kutokana na mambo aliyo wakilisha bloguni.Mfano ikiwa tutahitaji kuwa na fund yetu kama wanablogu ya kusaidia maendeleo ya kitu tukubalianacho.Iwe ni watoto yatima au uhuru wa habari nk.

Kuhusu Jina ningependa katika kila kitu tutumie majina ya Kiswahili. Jina la jumuiya mimi na shauri liwe:
Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania(JYWT).

jina la Aggregator, mimi ningepenga jina liwe la Kiswahili au Kifupi cha jina la Kiswahili
Mfano wa majina niyafikiriayo ni:
Bloguni Wasemaje(BW)
Sauti za Watanzania Bloguni(SWB)
Kipya Katika Blogu za Watanzania(KKBW)

Kuhusu muda wa wawakilishi kuwepo katika kamati ningeshauri muda wa miaka miwili . Kila baada ya miaka miwili tungepiga kura kuchagua wanakamati wapiya au kuwabakiza wale ambao tunaona mchango wao una umuhimu wakuendelea kwa muda mwingine.Kuwepo na uwezekano wa kuitisha kikao cha dharura cha kutengua uwakilishi wa mtu katika kamati. Kwa ujumla jumuiya ibakie kuwa ya wanablogu wote hakuna kiongozi wala afuataye bali wote kwa pamoja tukienda mbele. Wawakilishi wanapewadhamana kuwakilisha wanablogu kurahisisha ufanisi wa jumuiya tu. Ila ni wajibu wa jumuiya nzima kuhakikisha kuwa tunakuwa nguvu ya kuelimisha , kuhabarisha, na ya kujikomboa.

Read more...

Chakula cha Mawazo!- Is U Coloured?

>> Friday, November 17, 2006


Read more...

PIKINIKI MAKABURINI! Je ukimchungulia mtu mzima Utapofuka macho?

>> Wednesday, November 15, 2006

Naamini mila na desturi zetu wabongo bado zina nguvu sana ingawa watu wanadai hizi ni zama ya bongo fleva. Naamini kuwa katika shule zetu za jadi mbinu mbalimbali zilitumika kuwezesha mambo fulani katika jamii kwenda shwari na kulindwa kwa nguvu zote na jamii. Mimi ni mchanganyiko wa Kipare na Kijita na katika makabila yote haya mawili njia za kuelimisha zilitumia mbinu nyingi ikiwa pia na vitisho. Mfano kwa Wapare maswala ya kufundishwa kuwa mwanamume wa shoka yaliendana na vitisho na maumivu. Kama wewe ni mwanamume basi lazima uweze kuvumilia maumivu .Nadhani kwa walioenda jando watakumbuka! Kulikuwa mpaka kuna simba wamsituni akumezaye ukishindwa kufanikisha mambo fulani ya kidume. Hii maana yake ulikuwa unauawa ingawa ilidaiwa umeliwa na Simba. Sasa njia hizi za kutufundisha heshima , maisha na hekima nyingine nyingi zikajakuuawa na wakoloni na wengine walioleta tamaduni mpya. Basi unaweza kudhani kwa sababu Wakoloni waliua shule za jadi basi na baadhi ya mambo tuliyokuwa tunatishiana yamekwisha!Utadhani mpaka sasa tumeweza kuelewa au hata kujiuliza ni kwanini mambo mengine yalitishalo kabila moja, hayalitishi jingine hata hivi sasa baada ya makabila ya Tanzania kuchanganyika na kutawanyika katika mikoa mbalimbali . Jibu bado tukopalepale. Tunaamini wachawi wanapaa na ungo ingawa hata kushuhudia hatuja shuhudia. Tunaamini kibibi fulani kichawi kwasababu macho yake mekundu bila kushuhudia aliyelogwa. Tuna chanja na kuvaa hirizi kibao bila ya uhakika hata wa ni nini hasa tunakiogopa.

Sitaki kukataa kuwa hakuna uchawi kwa sababu hili ni jambo lililorekodiwa miaka mingi tu na vitabu vingi vimelizungumzia. Lakini mimi ninachoamini ni kwamba uchawi mkubwa ni hofu ya kibinadamu itokanayo naupungufu wa kibinadamu wakutokujua. Na upungufu huu kwa bahati mbaya hauna dawa. Upungufu huu umefanya wengine waabudu miti ili kuujazia, wengine Yesu, na Wengine Mtume Mohamedi. Tatizo jingine la upungufu huu uko kama njaa, kila siku unahitaji kupewa chakula ilikujazilizia pengo la upungufu wa kibinadamu ilikupata uhaueni. Mimi naamini pamoja na kuwepo wachawi, moto wa ahera na mambo yote hayo, lakini upungufu wa kibinadamu wenyewe hulenga binadamu kitofauti kutokana na binadamu mwenyewe alivyo na mazingira yake katika kumuelekeza binadamu huyu kuamini nini kinampa ujazo na uhaueni. Basi utakuta huku wanaogopa makaburi, kule wanaogopa mbuyu na hata wengine kukimbia vifuu vya nazi kutokana na mazingira yao. Basi unaweza ukakuta kutokana na mlengwa hirizi ikajazia na kuziba hofu hiyo, dini au hata kujinyonga. Naamini ubongo wa binadamu unanguvu kiasi kwamba hufanyia kazi hofu za binadamu na kuzipa uhai na uhalisi.Na naamini asilimia kubwa ya wajulikanao kama wachawi, waganga wa kienyeji au hata uchawi wenyewe haukuthibitika ingawa una uhalisi. Halafu si kweli zote ni zakufundisha maana nyingine ni zakutishana kwa madhumuni yakutishana tu.Na nyingi za mila na desturi hizi hatakama zilikuwa zinafundisha zamani hazina mchango mkubwa sasa hivi katika kuifundisha jamii ya leo.Na kama kuna sababu zakuzikubali hizi dini za kuletwa moja ni kwamba kwa sasa ndio zimeshikilia ukanda katika kuipa jamii muelekeo, ingawa hata kwa hili sina uhakika zitaweza jukumu hili mpaka lini kama jamii haifumbui macho nakuelewa mchango wake bila ya kukariri na kufuata kiulimbukeni.

Lakini hizi mila za kutishana kwa dhumuni la kufundisha kitu haziko afrika pekee. Na rafiki yangu Myahudi alikuwa anatishwa na wazazi wake asiweke Tattoo kwa sababu hata weza kuzikwa kiyahudi akiwa na tattoo, kitu ambacho baadaye akagundua hakina ukweli. Nakumbuka pia nilipotembelea Russia mitaa ya Viborg nishawahi kuwatisha wenyeji wangu kwa kuwa nilipiga mluzi ndani ya nyumba na wao waliamini kabisa kwa kupiga mluzi ndani ya nyumba unaleta bomba la balaa. Kitu ambacho mimi siamini, kwani mimi nilifundishwa usipige miluzi porini. Hivyo hizi mila na desturi ambazo zina mambo haya ya kutishana haziko Afrika tu. Duh !Unakumbuka kitabu kiuzacho kuliko vyote siku hizi cha Harry Potter kinastori gani za kichawi?

Sasa ngojea nikupe stori fupi kuhusu uoga wangu wa makaburi.
Nakumbuka tokea utotoni nilizoea kusikia habari za kutisha kuhusu maeneo ya makaburini. Nakumbuka kunakipindi nilikuwa nang'ang'ania kutokwenda kulala mapema ilikuendelea kusikiliza stori za wakubwa, basi ilikutaka kunifanya niondoke wanaanza kusimulia stori za kutishatisha. Sehemu kubwa za stori hizi zilikuwa zinalenga maswala ya majini mashetanishetani na maeneo ya stori yanakuwa makaburini. Basi nisitake kukuongopea mara nyingi ilivyokuwa inaingia giza nilikuwa natishika kukatizia njia yoyote inayokatizia makaburini.Kilichokuja kunishinda ni pale nilipokuwa natembelea Upareni kwani kule ni kawaida kabisa marehemu kuzikwa katika eneo la nyumba. Sasa kutokana na kukulia mikoani ambako kunatamaduni za kuogopa maeneo ya makaruri ilinichukua muda kidogo kuzoe mpaka kuona ni kawaida.Kama nakumbuka vizuri Wachaga nao hawana uoga sana na makaburi hivyo nadhani kwa waogopa makaburi wanaweza kupata taabu sana uchagani na Upareni pia. Lakini akipata tabu Uchagani atatokwa na jasho akikatiza katika anga kama za Ufini ambako kuna mpaka siku katika mitaa ya krismasi ambapo makaburini ndio pakwenda sio kikilio bali kimatembezi.

Mila na desturi zetu nyingi ni nzuri lakini hatuzisomi na kuzielewa sasa hivi tunapo ingia katika tamaduni za bongo fleva. Tatizo linalojitokeza ni kwamba mila nyingi nzuri zitapotea, halafu na zipo mila na desturi nyingi zisizo na manufaa sana kwetu tutaendelea kuzitunza. Bahati mbaya mila ambazo zitatunzika ni zile tuziogopazo! Je ukimchungulia mtu mzima utapofuka macho?Je , utakwenda pikiniki makaburini?

Read more...

Richard Bona Eeeh!! Mimi mshabiki !

>> Tuesday, November 14, 2006


Katika vyombo vya muziki nivizimiavyo ni Bezi gitaa. Halafu si siri miziki ya jazz ni moja ya miziki niitumiayo kusafiri katika ndoto za mchana(day dreams) na pia nikiwemo ndani ya treni ya mawazo.Nisikufiche Majazz yanapanda hata wakati nafanya kimbunga cha ubongo(brain Storming). Sasa huyu Mkameruni ni miongoni mwa wanamuziki wa kiafrika ambao wanatambaa katika miziki niipendayo kisawasawa.Anatambaa kuanzia Afro mpaka kwenya klasiko Jazz bila shaka.Hebu msikilize kwenye solo hii hapa chini:




Kama nilivyosema huyu katika wapiga Bezi gitaa waafrika huyu Richard Bona ni miongoni mwa naowahusudu. Tarehe saba mwezi huu nilifanikiwa kuona shoo yake na kuongea naye. Alichonizingua alipojua tu natokea Tanzania akaniauliza unatokea Bagamoyo? Swali hilo ingawafupi lilinidhihirishia kuendelea kutambulika kwa wasanii watokao Bagamoyo. Kwa maana sasa ni mara nyingi nikikutana na wasanii waaminikao katika fani kutoka nchi kibao tu wanakuwa wanajua kuhusu Bagamoyo. Bahati nzuri safari hii nikikutana na Richard Bona, nilikuwa na Msanii mahiri wakibongo, ambaye najua ipo siku Tanzania itamjua aitwaye Menard Mponda , hivyo halikuaribika jambo.



Richard Bona akikupa kile kibao kiitwacho 'Engingilaye'

Read more...

Kwa wapendao mpira wa vikapu, mnamkumbuka Dr. James Naismith?

Dr James Naismith akipozi na gozi la mpira wa kikapu enzi hizo








Kwa wapenda michezo naamini mnamkumbuka huyu daktari aliyebuni mchezo wa Basketi Boli. Ninachojiuliza ni kwamba katika mazingira ya kwetu tumetosheka na michezo iliyopo ambayo mingine hata kutokana na umasikini hatuwezi kushiriki? Nakubali tunamichezo mingi Tanzania. Nakubali tuna michezo kuanzia bao mpaka mieleka ya asili. Je, katika shule zetu bado kunaruhusiwa ubunifu wa michezo ili kukidhi matakwa ya mazoezi ya viungo ya Wanafunzi? Nakubali kuwa tuendelee kuipa kipaumbele michezo hii ambayo inashindaniwa kimataifa duniani. Nakubali kuwa huyu Dr J Naismith alibuni mchezo huu kuwaondoa wanafunzi kuboreka wakati wa kipindi cha baridi(winter) ambapo wanafunzi walifanya mazoezi ndani ya maholi. Lakini kwa Tanzania naamini kuboreka kwa wanafunzi katika maswala ya mazoezi kupo sana.Je hii sio changamoto ya kuchochea haja ya mchezo mpya? Na sasa hivi vijana wengi wanaacha kabisa kufanya mazoezi na kubobea mbele ya Luninga kujadili mechi za Uingereza. Sawa, inawezekana hawa ni wachache wafanyao hivyo. Lakini unaonaje muelekeo wa vijana kwa ujumla ukiweka mazoezi ya viungo kama kigezo?Labda hatuhitaji mchezo mpya!Labda ni kibano cha maisha kisababishacho kushuka kwa ushiriki kikamilifu katika michezo kwa vijana! Lakini nchi nyingi ni hasa wenye kibano ndio wanaibuka kuwa kiboko katika michezo. Ukienda Brazili akina Pele ni ushahidi.Inabidi kuangalia tena uhamasishaji wa michezo, mfumo mzima na streteji za kufanikisha michezo bongo. Naona Raisi Kikwete anapenda michezo sio kama Mwalimu Nyerere ambaye pamoja yake mazuri mengi aliyofanya, alishindwa kuona umuhimu wa michezo kama silaha moja wapo ya kujenga Utaifa. Labda hatuhitaji Dr Naismith wa kibongo!Nawaza tu usiogope!

Read more...

Dini ni za amani na upendo?

>> Monday, November 13, 2006

Kila siku ukitazama au kusoma habari utasikia kasheshe za mikwaruzano duniani. Mambo mengi ya vita na majanga utayaona yakiwa kurasa za mbele za magazeti. Cha kushangaza ni kwamba baadhi ya mikwaruzo hii utaiona inaendeshwa na watu wanaosema ni wanadini zipendazo amani. Kinachoshangaza ni jinsi gani hizi dini zisemekanazo ni za amani zilivyokuwa na misingi ya utenganishi. Au hivi ni hawa wanadini tu ambao uzigeuza hizi dini kuwa chanzo cha utenganishi?

Hebu tuangalie baadhi ya chokochoko hizi:

Israeli na Wapalestina ni kawaida kabisa kuwakuta msitari wa mbele katika kupigana. Hawa pamoja na mambo mengine tofauti za dini zao ni moja ya jambo kubwa lifanyalo wabwengane. Hivyo hapa tunawakuta wale wenye dini ya kiyahudi wanabwengana na waislamu. Na wameanza zamani! Je, unawakumbuka Falashas au Beta Israel?Hawa ni wale Wahahudi Wakiethiopia. Kuna theori zinaeleza uondokaji wao baada ya ufalme wa Judah kugawanyika mara mbili na baada ya Jeroboam kumrithi Mfalme Solomon.Na baadhi ya mambo anukuliwayo ni pamoja na dini yao. Nilipenda kuwagusia kidogo Waisraeli hawa weusi hapa kwasababu mpaka leo wana mikwaruzo ya kidini Ethiopia.Na pia mzungukowao wakukimbia Israel mpaka sasa hivi warudishwapo Israel umejaa mikwaruzo ya kidini. Wako bado mafalasha kwa maelfu ndani ya Ethiopia ambao wanasubiri kuchukuliwa kwenda Uisraeli.

Waisraeli weusi ndani ya Ethiopia walikuwa na mikwaruzo na wakristo na waislamu pia. Wako ambao walilazimika kubadili dini na sasa wanarudia uyahudi ambao wanaitwa Falash Mura. Lakini wapo wanaoamini kuwa baadhi ya Falash Mura wanarudia Uyahudi ilikuweza kurudi Irael. Chaajabu ndani ya Israel wanabaguliwa kwa rangi na hata kidini na Wayahudi wa kiothodoksi.Wayahudi wakiothodoksi wanaamini Mafalashas kuwa sio wayahudi kamili.

Tukiondoka mashariki ya kati ambapo kasheshe liko wazi tunaweza kukatua mitaa ya Marekani kusini. Ukienda nchi kama Brazili , mikwaruzo ipo kati ya Wakatoliki na Maprotestanti. Hili utalikuta kwa Waairishi pia ndani ya Ulaya.
Ukienda India utakuta kasheshe iko kwenye Wahindu na Waislamu, Wahindu na Wakristo, Waislamu na wakristo bila kuwasahau Wahindu na Masikh. Ukidondoka Pakistani utakuta kasheshe kati ya Waislamu na Wakristo, Waislamu wa Sunni na Shia.

Ukienda Australia utakuta mikwaruzano kati ya Wakristo na dini za Kiaborijini na pia na waislamu pia.

Kwa haraka haraka utakuta kila kona ya dunia kuna mikwaruzo ambayo waiendeshao wanadai wako ndani ya dini zipendazo amani. Sasa ni nini kiko ndani ya dini hizi ambazo zafanya wanadini wakwaruzane bila upendo?

Sijaisahau Tanzania katika hili. Dini inayoonyesha kutulia kuliko zote ni ya kipagani ndani ya Tanzania. Sijawahikusikia wasio kwenye dini za amani zilizoletwa wakichimbiana mikwala na wenye dini. Sijawasikia wakilalamika kutoalikwa kwenye ubwabwa na Raisi Jakaya kikwete. Tanzania kuna chokochoko kati ya Waislamu na Wakristo.Kuna misingi ya chikochoko ndani ya makanisa mbalimbali. Kila thehebu hutakakuhalalisha ukweli wake kwa kujenga hoja za kukosoa jingine.Hivyo timu zipo umekosekana uwanjatu na mashabiki.

Ukirudi Israeli , Mafalasha wanabagulia na wanadini wenzao wayahudi wakiothodoksi. Ukirudi Iraq waislamu kwa waislamu wanabwengana kwa misingi ya nani ni msunni na nani Mshia. Kunakipindi ilinishangaza mitaa ya Kilimanjaro kukazuka mpaka ugomvi kati ya Waluteri na Waluteri wenzao.Kisa wanagombania dayosisi iliwaendelee kumtukuza Mungu wa amani. Sasa sababu zinasemekana kuwa ziko nyingi! Sasa sitashangaa kasheshe likizushwa kutokana na sababu hizi zisemekanazo kuwa nyingi!Chakusikitisha ni kwamba watu tunashindwa kujifunza kutokana na mikwaruzo hii ambayo mingine ni ya maelfu ya miaka. Pale Juu niligusia zaidi swala la Beta Israel kwasababu unaweza kustukia jinsi gani misingi ya amani ikawa inakuletea mikwaruzo anga zote za dunia uamiako.Nazidi kujiuliza, kwanini dini zetu za amani zinaleta utenganishi namna hii? Je Tanzania tutaponyeka kuingia katika kasheshe kubwa zaidi ya tuliyonayo sasa kutokana na dini hizi za amani?Sijui , niko bado ndani ya Treni hii ya mawazo

Read more...

Oliver Mtukudzi na Manu Dibango mawazoni!

>> Friday, November 10, 2006

Wakati najiandaa kwenda kumuona Oliver Mtukudzi leo hii, nimejikuta napitia miziki ya kiafrika kibao ambayo imenisaidia kupitisha siku za shida na raha. Bado napooza kichwa katika behewa hili la mawazo kwa kuwasikiliza zaidi Oliver na pia Manu Dibango. Hivi, unakumbuka ile Soul Makossa?Mimi nilikuwa naiimba kiswahili yote.



Oliver Mtukudzi akikupa Ndakuvara




Manu Dibango akikupa Soul Makossa

Read more...

Ed Bradley

Ed Bradley








Huyu mwanahabari Ed Bradley amefariki Alhamisi hii.Leukemia imemuondoa hapa duniani. Huyu ndie aliyekuwa ananipamotisha sana hasa nikiwa namcheki katika kipindi cha 60 minutes. Ni miongoni mwa watu weusi wachache walioweza kuingia katika vipindi vya televisheni vilivyo maini strimu kabla mambo ya cable tele hayajavinjari Marekani. Kuna kauli moja aliyowaikusema iliniingia sana. Alisema kisa cha yeye kuingia sehemu ambazo watu weusi walikuwa wanaamini haiwezekani ilitokana na wazazi wake kuwa wanamwambia tokea utotoni kuwa:mtu unaweza kuwa chochote utakacho. Akamalizia kwa kusema :unajua ukiwa unaambiwa kila siku jambo hilo unaanza kuamini katika hilo. Mimi nakubaliana kabisa na hilo. Sisemi kuwa ni rahisi lakini ni jambo lenye ukweli ndani yake. Sasa mara ngapi unasikia katika bongo yetu mzazi anakazana kumwiita mtoto wake pumbavu , huna akili, nk?Mimi nilichojifunza kutoka kwa Ed ni kwamba mtoto huanza kuamini katika hilo na kuanza kukosa kujiamini. Ni sawasawa tu na jinsi watu wengi weusi wasivyojiamini hasa watu wa rangi nyingine wakiwa katika anga kutokana na kuitwa pumbafu hujuikitu.
Pumnzika ED!


Read more...

Unawakumbuka Uhuru Mweusi?



Najiuliza ktu kwanini watu tunapenda kuonyeshana meno tukidai kuwa ni tabasamu? Unafiki mkubwa umejaa na chuki ambazo zinafichwa nyuma ya meno yaliyokenuliwa.Lakini Je kila anayetuchukia angekuwa anatuonyesha dunnia ingekuwaje?
Nasikiliza Uhuru Mweusi wakikwambia Dont show me your Meno Plastic smile can't work



Black Uhuru 1981

Read more...

Kuhusu kwanini Simon hatuoni Blogu nyingine zikikuunganisha

>> Thursday, November 02, 2006



Mimi sina jibu hilo. Waulizeni ambao unahisi wangeniunganisha katika blogu zao. Lakini hata katika blogu yangu sijamuunga kila mtu.Lakini si umenipata?Kumbuka hapa ni katika treni ya mawazo. Maana yake hakuna majibu sana.Kama maswali tu!Utayapata.

Read more...

Yesu Mweusi

>> Wednesday, November 01, 2006

Moja ya picha imuonyeshayo yesu kama mtu mweusi.










Hivi karibuni sinema mpya ya kimarekani imetoka ikimuonyeshaYesu kama mtu mweusi. Sinema hii inaitwa The Color Of The Cross. Kuhusu swala la kwamba Yesu alifananaje ni swali ambalo limeulizwa na kuchambuliwa kwa miaka kedekede. Nachojiuliza ni kwamba , hivi kwanini watu wanahangaika sana kujua Yesu alifanana vipi? Hivi hii sio hali ileile ya watu kutaka kujifananisha na waliofanikiwa? Hivi hali ya watu kutaka kujulikana wanauhusiano na mtu maarufu, au wanafanana na mtu maarufu sio dalili ya udhaifu katika idara ya kujiamini?
Katika sinema hii kunakipengele kihusishacho rangi ya Yesu kama sababu nyingine yakumthulubu.Sijaiona hii sinema bado.Wewe je?

Read more...

Mwanamama Cesaria Evora azidi kunizingua

Cesaria Evora hufanya maonyesho yake bila viatu akiashiria kukumbuka akina mama na watoto masikini waishio kisiwa atokacho cha Cape Verde








Siku chache zilizopita nilifanikiwa kumuonatena Cesaria Evora akifanyaonyesho lake maridadi kama kawaida yake. Huyu mama ajulikanaye kama DIVA MTEMBEA PEKU(The Barefoot Diva), ananiua sana awezavyo kudaka watu kwa sauti na uimbaji wake , nakuwafanya wakae chini kimya kusikiliza wakati hakuna anayejua anasema nini. Zamani wakati wa ndombolo,nyimbo za kihindi na hata za magharibi, nilikuwa bingwa wakuzitungia maneno ya kiswahili. Nakumbuka wengi tu tulikuwa tunaimba nyimbo kama: Maiko Jaksoni njooo, sitakiiii, kama hutaki nenda!Nyimbo ambazo tulikuwa hatuelewi zinaongelea nini , lakini zinachezeka. Kwa sababu zinachezeka basi maswala ya ujumbe yalikuwa si muhimu. Ila huyu mama anachonizingua ni uwezo wake wakukukalisha chini hata kwa masaa mawili akikuimbia na ukatulia na kuingiwa tafakari za kila aina mpaka unastukia anawaaga.Akiaga hapo ndio unastukia kuwa kumbe alikumeza na muziki zaidi ya masaa mawili. Kutokana na hilo husafiri duniani kote na kuimba akipokelewa kwa mikono miwili bila tatizo.

Sasa nani alisema kuwa kwa kuimba kiswahili tutashindwa kuwa na wasanii ambao wanaeleweka duniani? Naamini kama Cesaria anaweza kwa kushikilia nyimbo na midundo ya ki Cape Verde, basi na Watanzania tunaweza kwa kushikilia miziki yenye midundo yetu. Basi hata ambapo wasanii sasa hivi wanapotaka kubobea kwenye midundo ikaribianayo na ya Marekani tukumbuke kuwa bado tunaweza kufanikiwa kwa kuendeleza midundo yetu.

Read more...

P.W. Botha afariki



P.W Botha-The great Crocodile












Mamba mkubwa , ndivyo alivyoitwa P.W. Botha. Huyu Mzee mpaka kufa kwake hajawahi kukiri wala kuomba msamaha kwa uhalifu wa serikali yake kwa watu weusi Afrika kusini. Pia alivyo ulizwa ingekuwaje kama watu weusi wangechukua nchi mwaka 1948 wakati chama chake kilichukua hatamu akasema nchi ingeharibika. Mpaka anafariki hakuamini katika kipaji cha uongozi wa mtu mweusi. Lakini je kwa mifano ya viongozi wetu Afrika na rekodi zao za uongozi unaweza kumlaumu huyu Mzee kwa kufikia kuamini watu weusi hawawezi uongozi? Amefariki akiwa na miaka 90. Natumaini kuwa karibu Afrika itaanza kupata viongozi ambao wataturudishia heshima yetu Waafrika na wote wenye rangi nyeusi. Kabla hawajatokea changamoto aliyoacha P.W. Botha ni kwamba: je, si ni kweli mpaka sasa viongozi wetu weusi ndio wanazidi kuchangia kuporomoka kwa nchi zetu za Afrika?Kama viongozi wanabisha Botha hakuwa anasema ukweli kuhusu uongozi mbovu wa viongozi wa kiafrika basi wafanyekazi na kutukwamua katika matatizo yetu Waafrika. Haya naona hata Mo Ibrahim anataka mpaka kuwalipa pensheni ilimfanyekazi.Fanyeni kazi basi, AlaaH!Habari zaidi hapa

Read more...

Unamjua Sunday Adelaja?

>> Wednesday, October 25, 2006

Pastor Sunday Adelaja akishusha kauli katika kanisa lake la Embassy of the Blessed Kingdom of God for all Nations.







Katika Wanageria ambao nimewasikiliza hivi karibuni huyu Sunday Adelaja ni jamaa ambaye amenifikirisha kidogo siku za karibuni. Huyu Mnigeria ni miongoni mwa Wanageria waliofanikiwa katika biashara ya dini hivi sasa. Akiwa Ukraina , aliaamua kuanzisha kanisa ambalo kwa sasa hivi lina watu zaidi ya 20,000. Anachonizingua ni jinsi alivyoweza kuanzisha kanisa katika mazingira magumu kama ya Ukraina hasa akiwa Muafrika. Ubaguzi katika nchi zilizokuwepo ndani ya Soviet Union ni mkubwa mara nyingi zaidi ya zile za magharibi. Halafu mifumo ya nchi hizi ni dhaifu hivyo ni vigumu kwa wageni kupata usalama. Kwa hilo tu, naweza kumvulia kofia kwa kuweza kutumia udhaifu huo huo na umasikini uliozidi baada ya kuvunjika kwa Soviet Unioni kusimama kivyake. Kuhusu ukweli wa kanisa lake,hilo mimi sijui. Changamoto anayonipa ni kuwa penye nia pana njia.

Hivi hili hapa chini ni kweli? :
"Nigeria's Christians have a prophetic mandate," says Matthew Ashimolowo, a former Muslim who now leads England's largest church, the Kingsway International Christian Centre in east London. "God gave us a prophetic word that his servants will go out from our nation and shake the world." The 15,000-strong Word of Faith Bible Church, Ukraine's largest church, was founded by Sunday Adelaja, also a Nigerian, and the largest churches in Kenya, Tanzania, Ghana, Zimbabwe and Jamaica are also led by Nigerians.

Read more...

Chakula cha mawazo!

Hivi tutawalalamikia Wazungu na Waasia kwa kutunyonya na kuendelea kutufanya watumwa mpaka lini?Mwanzo tulisema kuwa hatukuwajua hawa watu na hila zao.Sasa asilimia kubwa ya wasomi wetu ambao wamewasoma hawa watu wanajua hila zao.Sasa tunafanya nini na ugunduzi huu wa hila zao? Tunafanya nini kukabiliana na mifumo yao ambayo sasa hivi tunao wasomi wengi tu Afrika waliobobea katika taaluma za mifumo yao?Hivi wasomi wetu wa Afrika walio wengi siku hizi si wamesoma shule hizi hizi za hawa wamagharibi waongozao nchi hizi?Hata akina Sumaye , Malima nk si baadhi tu ya hawa ambao vikorido vya vyuo vikuu kama Harvard, nk, wanavijua kama nyuma ya viganja vya mikono yao?

Sasa swali ni kwamba, kama tunajua wanafanya nini hawa wamagharibi kwanini tunashindwa kujikwamua au hata kuwa na laghai zitakazotufaidisha sisi?Wachina walivyostuka wakaamua kubadili mtazamo na kutumia mpaka laghai ilikujifaidisha.Wajapani, Wakorea nk walifanya laghai kulingana na mazingira yao.Sasa sisi je?


500 YEARS LATER: AFRICA AND SLAVERY Dr Kimani Nehusi akilalamika.Nakubaliana naye lakini najiuliza hivi tutafanya hivi mpaka lini?

Read more...

Behewa la mawazo: kwa nini Tanzania imechelewa kufanikiwa?...-N.1

#UTAIFA
Naamini Raisi Nyerere na uongozi wa kwanza ulibidi kutumia muda mwingi kujenga utaifa.Kuweka misingi ambayo ingeweza kutufanya taifa.Lugha ya kiswahili na kujenga mfumo mzima ambao ungetuwezesha kujiendesha kama taifa huru.

Swali: Je, Utaifa tunao hivi sasa?Kama tunao unatuweka katika nafasi gani nzuri ya kuendelea mbele kupita mataifa mengine ya jirani ambayo hayana Utaifa?Je kama Nyerere alikuwa anatumia baadhi ya muda kuhakikisha maswala mbalimabli ya utaifa yanaendeleaje akiwa chini ya upungufu wa viongozi wasomi, je, Raisi wa leo anatumia muda huo kufanya nini ikiwa idadi ya wasomi imeongezeka kupita ya kipindi cha Nyerere? Je , wasomi wetu wameelimika au wamekwenda shule tu na kuwa na vyeti babu kubwa?

Usistuke kama unasoma hapa maana yake uko ndani ya treni ya mawazo.
Katika behewa hili namba moja najiuliza tu kwamba kama utaifa ulikuwa lazima kujengwa hivyo lazima muda ulitumika kuujenga.Hii inaweza ikawa sababu ya kuchelewa kuendelea. Sasa kama huu utaifa umejengeka basi muda huu ni wa kuutunza Utaifa na kuutumia Utaifa wetu kama chanzo kimojawapo cha kwenda mbele.Je, mikakati ya nchi yetu inatumia faida zote ziletwazo na utaifa? Najaribu kufikiria kwanini tunajisifia sana Watanzanina kwa amani wakati sioni kama amani imetusaidia sana kupiga hatua kimaendeleo? Ukiwa unawasikiliza watu kama akina Jared Diamond, hasa katika kitabu chake cha Guns, Germs and Steel, utamsikia akikueleza ni jinsi gani Wazungu waliweza kufanikiwa . Atakupa jiografia, atakupa jinsi hata uwezo wa kugundua kilimo , kufuga wanyama mapema kulivyowezesha jamii mbalimbali duniani kuendelea mapema na kutawala nyingine.
Sasa hayo yalikuwa zamani lakini kikubwa ni kwamba jamii zote zilizo piga hatua ziliweza kutumia faida zilizoletwa na mambo ambayo wameyamasta tayari. Je sisi kama Tanzania na utaifa wetu na amani yetu , tumepungukiwa nini sasa hivi ambacho kinatufanya tusiwe Taifa lililofanikiwa kufaidika na yale tuliyoyamasta tayari? Mapungufu yapo, lakini tunajifunza nini kutokana na mapungufu hayo?Kwanini tokea enzi hizo za uhuru mpaka sasa bado tunazungukwa na magonjwa,mfumo dhaifu wa elimu,mfumo wa uongozi hata mori mbaya wa kazi?

Sasa siri ya kutatua jambo hili ni nini? Je, ni mpaka Taifa zima lielimike ili tuweze kuwa na mabadiliko?Je, hivi historia inatufundisha kitu kweli?

Naendelea kusafiri katika Treni hii ya mawazo........

Read more...

Simon , kwa nini?

>> Tuesday, October 24, 2006


Rasta Luihamu na baadhi ya wadau wamekuwa wananipiga maswali kibao hivi karibuni. Najaribu kujibu hapa baadhi ya maswali ambayo yanazidi kujirudia.

Kuhusu Waafrika kuogopa kurudi Afrika
Mimi sidhani kwamba ni vigumu kuelewa kwa nini Waafrika wengi wanavyowezakuogopa kurudi nyumbani. Pia siwezi kusema kuwa Waafrika wengi ni ukweli kuwa ni woga uwafanyao waishi mabara mengine. Mpaka sasa hivi elimu itawalayo Afrika ipo katika vitabu vya wageni kutoka nchi nyingine. Luninga watazamazo zimetawaliwa na maonyesho yaelezwayo na watu wengine na kwa mtazamo mkubwa usioupa sura nzuri Afrika. Kama uijuavyo tabia ya binadamu, ni rahisi kuelewa kwanini atajaribu kutembelea sehemu zisifiwazo ilikujionea mwenyewe. Kila muafriaka aliyeko nje ana stori yake. Wengine walishakata tamaa na Afrika. Kwa sababu hakuna wanachokiona ambacho kina wapa moyo kuwa wanamchango wowote wakutoa.Hii hasa ni kutokana nakuamini mfumo ambao upo ni vigumumu kuwapa nafasi ya kutoa mchango wao. Wapo ambao wamekwama nje ya bara. Maisha ni magumu, lakini bado wameweza kutunza hali ya utu wao kwa kujificha mbali na Afrika ambako ndugu na jamaa hawatashuhudia kasheshe ya maisha waishiyo. Wako ambao maisha yao na ujuzi wao hawawezi kuutimiza ndani ya Afrika kutokana na kukosekana mfumo uwianayo na elimu ambayo msingi wake wameupata tokea shule zetu za Afrika zinavyotuandaa. Wako wanaodhalilishwa kila siku. Wapo ambao wanaheshimika na kuthaminiwa. Kuhusu kujiandaa kabla ya kuvamia jambokwangu naona ni jambo ambalo kila mtu anatakiwa kufanya kwanza. Hivyo kwa wale walioishi muda mrefu nje ni lazima waliangalie hili swala. Hata kwa wale amabo wanaamini vijana wote wa mijini warudi vijijini, kama aaminivyo Mzee Luihamu,si busara tu ukaamua kwenda tu huko kijijini na jembe lako begani bila kujiandaa na hali halisi ya maisha ya kijijini. Maisha ni mchezo wa ajabu. Ukikua unastukia maamuzi yako kimaisha haya kuhusu wewe peke yako.Maamuzi yako hugusa ndugu na jamaa hadi jamii nzima. Maamuzi yasiyokuwa na mipangilio maalumu mara nyingi hayana nguvu ya majawabu ya kudumu.Kuna maamuzi yenye majina matamu lakini sio ukweli kuwa ni ya matatuzi ya kudumu.


Kuhusu nani atavaa viatu vya Martin Luther King Jr au Malcom X

Mimi binafsi sidhani kuwa kuna mtu atavaa tena kiatu cha Martin Luther King wala Malcom X. Kwa sababu sidhani kuwa kuna mtu yeyote amabaye anaweza kuwa kama mwingine. Nacho amini kila muda katika historia una matatuzi yake yalinganayo na muda huo. Hivyo yeyote mwenye busara atajifunza kutoka kwa akina Martin Luther Jr,Malcom X, Mwalimu Nyerere, babu, bibi, msaidizi wa kazi za nyumbani, na jamii kwa ujumla ilikufikia busara zimwezeshazo kutatua matatizo yamkabiliayo . Kumwezesha kutabiri mwelekeo wa mambo ilikuepuka au kuweza kukabili matatizo yatarajiwayo nk.

Kuhusu imani
Imani ni ya mtu binafsi na naamini kuwa mtu hawezi kulazimishwa kwamba aamini nini. Naulizwa sana mambo ya Urasta na Mzee Luihamu ameniambia kuwa tusiogope Urasta na Marasta , kwa kuwa ni wana wa Yosefu wa Israeli. Namuelewa kwanini anasema hivyo. Lakini chakujiuliza ni kwamba dini nyingi hizi watu wafuatazo sasa hivi zimekuwepo muda mfupi sana ukizingatia historia ya uwepo wa binadamu duniani. Je, kabla ya Yosefu Waafrika si walikuwepo? Je siinakumbukwa mikutano ya kujadili ni vitabu gani viingizwe kwenye biblia? Je ina maana Mwenyezi Mungu kabla ya dini na vitabu hivi vitakatifu viongozavyo imani karne hii alikuwa hana mapenzi na viumbe wake?Kwa mtazamo wangu ni kwamba imani ni kitu cha mtu pekee. Mtu akifa anaanza kivyake mwenyewe hivyo haya maswala ya imani za watu sitaki kuyaingilia. Kwa rasta Luihamu, mimi binafsi siogopi kuwa Rasta. Nilishawahi kuwa Rasta na kujikuta na pingana sana na baadhi ya misigi ya imani hiyo.Kwa kifupi, nilizaliwa katika familia ya kikristo.Nikawa Muislamu kwa muda, nikaokolewa na Mozesi Kulola, Nikarudi kwenye Ulutheri, na nikaendelea kujiuliza maswalali na naendelea kujifunza kuhusu imani.Hivi sasa naamini Mungu bila kufungamana na mfumo au institution yeyote.

Kuhusu vilevi

Mimi simshauri mtu yeyote atumie vilevi. Madhara yake hujulikana vizuri tu. Sidhani kuwa kuna kilevi hata kimoja ambacho hakina madhara. Pia, hili swala kila mtu anakichwa chake. Kwa ujumla sidhani kuna mtu anweza kupinga madhara ambayo yanaweza yakajitokeza na kumharibia mtu maisha. Lakini kumbuka hata chakula kina weza kukudhuru pia kama unakila bila mpango.Hivyo maswala haya ya vitu tuviwekavyo kinywani si yakuharakisha majibu kirahisirahisi. Sasa, mimi sivuti bangi wala kutumia madawa yoyote. Ndio nakunywa pombe za aina kadhaa. Simshauri mtu kuwa akiniona nakunywa basi naye aanze?Hapana hilo sifanyi.


Kuhusu muonekano wa kiafrika
Kwanini huwa najibu sana kuwa mimi ni muafrika lakini wakati mingine navaa suti? Mimi siamini Uafrika ni mavazi. Sidhani ukivaa Kichina basi unahalali yakuitwa Mchina. Napenda mavazi ya kiafrika. Huvaa mavazi ya kiafrika. Napenda kuvaa navyojisikia na siamini kuwa Uafrika wangu unapungua kwa kuvaa hivyo. Sidhani kuwa Mandela kwa kuvaa Kiindonesia amepunguza Uafrika kusini wake.Halafu sioni kwanini muonekano wa nywele zangu uwe ni tatizo . Siamini kuwa muonekano wa nywele ni kipimo cha ubinadamu wa mtu.Muonekano wa nywele zangu mimi kama Muafrika naona ni wa kawaida tu.Na naamini ni wa kiafrika sana ambao isingekuwa wamagharibi kuunganisha na tafsiri mbalimbali ungeweza kuwa wakawaida sana katika maofisi ya Afrika. Nashangaa sana kuona kuwa bado watu huchukua muda sana kufikiria swala hili. Je na wewe ufuge nywele kama zangu?Hilo ni juu yako. Je, wewe unavaa nguo za Kiafrika zipi? Jinsi au lubega?

Sidhani kuwa nimepungukiwa Uafrika kwa kuwa hapa sijavaa nguo zitafsiriwazo kama ni za Kiafrika. Ila sikushauri unywe pombe, unajua mwenyewe :pombe si chai

Read more...

Jerry Rawlings , Babangida wanarudi, Mwinyi Je?



Mzee Jerry







Kama Jerry Rawlings anataka kurudi, hii inatuambia nini kuhusu imani ya Wazee wa Kiafrika kuhusu damu mpya katika ukombozi wa Afrika? Nigeria,Ibrahim Babangida anataka kurudi.Soma hapa habari za tetesi za kwamba Jerry anataka kurudi. Jambo hili kwanza likanifanya nifikirie kuwa sisi Tanzania tuna bahati, kwani sijasikia tetesi za viongozi waliopita wakitaka kurudi. Lakini nikaanza kujiuliza, hivi hawa Wazee wetu Tanzania waliondoka kweli? Tanzania ndio hivyo hata kama Raisi Mwinyi hajasema anataka kugombea tena Uraisi ili kuongeza ruksa, bado tumefanikiwa kutunza utamaduni wetu potofu wa kuwatunza viongozi ambao washaonyesha kushindwa kazi. Tabia ambayo labda wakati wa Nyerere ungeeleweka kuwa unatokana na nchi kutokuwa na wasomi wakutosha kushika uongozi, inazidi kuneemeka katika kipindi cha Muheshimiwa Raisi Kikwete. Na hii ni ya kuwaamisha viongozi walioonyesha mapungufu kutoka katika ofisi moja kwenda kwenye nyingine. Naamini kitendo hiki ndicho kimesababisha maraisi waliopita Tanzania kutosema wanataka kurudi kwa sababu kwa ujumla hakuna kilichobadilika.Natumaini jambo hili litakemewa na sisi wana jamii ya Tanzania mpaka lionekane ni la aibu kwa viongozi wetu. Au labda Raisi Mwinyi atataka kurudi tena na kuwa na waziri wake mkuu John Malecela.Tusubiri tutaona!
Kwa kuandika hivi simaanishi kuwa Wazee mchango wao hautusaidii bali ningependa wajaribu kuelewa kuwa pale ambapo mtu mwingine anaweza kutoa mchango zaidi basi apewe nafasi. Busara ya Wazee inahitajika. Hawa Wazee wangekuwa na mchango mkubwa sana katika kutambulisha ni mambo gani na njia gani walipita ambazo zimekuwa ni kikwazo cha maendeleo. Ingekuwa bora wawewakweli na makosa yafanyikayo na hii ndio busara ambayo inahitajika. Kuhusu kung'ang'ania ofisi na kushauriana jinsi ya kubaki ofisini sidhani ndio busara tuihitajio kutoka kwa Wazee wetu. Basi Wazee mlioshindwa ondokeni , mpishe damu mpya yenye mtazamo mpya. Au andikei basi hata vitabu kuelezea undani wa kiini cha kushindwa kwenu kututoa katika hali hii mbaya tuliyonayo Tanzania.Mkitoka kuweni washauri wema kwa kuwa wazi na jinsi kirahisi mzunguko wa makosa unavyoweza kujirudia.Ingefurahisha kuona heshima za shikamoo viongozi wetu mpewazo zingelingana na hekima na busara ambazo mnaziangaza kwa Taifa. Shikamooni Wazee!

Read more...

Watu maarufu wachukuapo Watoto Yatima Afrika

>> Wednesday, October 18, 2006

Hivi karibuni swala la watoto yatima Afrika limekuwa jambo kubwa katika vyombo vya habari vya magharibi. Hasa ni baada ya Madonna kwenda Malawi na kuchukua mtoto mmoja wa kiyatima hapo. Nimekuwa nafuatilia mambo mengi yaliyozuka katika mjadala kuhusu kwanini ni sahihi au sio sahihi jambo hilo alilofanya Madonna. Wengi walisema kuwa mtoto wa kiafrika anapaswa alelewe na familia ya kiafrika ili awezekukua katika maadili ya kiafrika. Wengine wakasema kuwa mtoto ambaye hana ndugu wanaoweza kumlelea ,hana kwake ni afadhali apate tu pakuishi kuliko kutokuwa na sehemu aitayo nyumbani. Wako wengi wakasema, hawa watu wanatumia hii njia ya kudhamini watoto ilikujitengenezea jina zuri.Mimi ninakubaliana na wote. LAKINI NINGEPENDA WATU WOTE WASEMAO, WASEME ZAIDI YA MANENO MATUPU WAO WANAFANYA NINI KIVITENDO KUSAIDIA WATOTO YATIMA?Isije ikawa kuwa sio hawa watu maarufu kuwa wanajitafutia umaarufu, bali ikawa ni hao wawasemao akina Madonna ndio wakawa wanatafuta umaarufu.Chakujiuliza ni kwamba tunavyodai watoto wa kiafrika wanapochukuliwa kwenda nchi za magharibi wanapoteza Uafrika wao, je ni nini kinachotunza Uafrika wamtoto wa kiafrika Afrika kitamaduni sasa hivi? Kwa maana ni ukweli asilimia kubwa za mambo yanayozidi kumzunguka mtoto wa kiafrika Afrika yanamizinguo ya kimagharibi.Yaonyeshwayo kwenye televisheni ya asilimia kubwa ni ya kimagharibi.Shule zetu zinashinikiza elimu ya kimagharibi.Dini zetu ndio hizo zakutoka nje. Sasa tunafanya nini kumtunza mtoto wa Kiafrika abakie na maadili ya kiafrika? Halafu sisi Waafrika tunafanyanini kumfanya mtoto wa Kiafrika aliye nche ya bara la Afrika kujivunia Afrika? Je tunaendeleza vita na njaa+ je tunaendelea kujidharau wenyewe?

Nachoshukuru moja ya jambo lililojitokeza katika mshawasha huu ni kuwekwa hili swala la watoto yatima kwa siku kadhaa katika kurasa za mbele za vyombo vingi vya habari duniani. Natumaini kama umaarufu basi uwe katika swala zima la tatizo hili na sio kwa watu binafsi.Kwani inajulikana kwa miaka mimi wako watu binafsi ambao wanafaidika na miradi ya watoto yatima zaidi ya watoto yatima wenyewe.Tatizo hili ni kubwa.Na ninawapapongezi wale wote wajitoleao kwa moyo kusaidia kwa lolote wawezalo kutatua swala hili.

Hivi unahisi Michael Jackson angetaka kuadapti mtoto angeadapti kutoka wapi?

Read more...

Chakula cha Mawazo!- Dume Jike!

>> Tuesday, October 17, 2006

Nakumbuka nilipokuwa mdogo katika jitihada za kuhakikisha kuwa mimi naitwa dume ilibidi nipitie mambo kibao. Nishakula pilipili kali , kupigana na mengine mengi tu ili mradi nipasi kama dume. Sasa hivi karibuni nilipata kuongea na Mbongo ambaye alikuwa anauelezea utamaduni wa ubasha na usagaji ulivyo neemeka katika baadhi ya sehemu Tanzania. Hili swala ingawa mara nyingi haliongelewi sana ni jambo ambalo liko sehemu kibao. Katika kipindi hiki cha karibuni, hasa baada ya Louis Farrakhan kuzidi kuugua nimekuwa nikipitia kazi zake. Yeye analake la kuongea, hasa mtazamo wake juu ya wanaume kama akina Michael Jackson na Prince, unanifikirisha. Kwa kuonekana kikekike anaamini si mfano mzuri kwa wanawake, kwani wnaanza kupotoka kuwa mwanamume halisi ni yupi.
Je unasaidia wanaume kuwa kama wanawake?


Read more...

Mtazamo wa Kiafrika

Kuna kipindi hapo nyuma niliongelea kuhusu jinsi Watanzania tunavyoweza kutoa heshima zote kwa wageni katika nchi mambo hambayo hatupeani wenyewe. Nilisoma habari moja iliyotoka kwenye tovuti ya The Black Star News, ambayo ilinigusa pia. Hii habari ilikuwa inaongelea jambo la kuenzi wageni kuliko wazawa nchini Kenya. Inasemekana Seneta Barak Obama, alipata muda wa vyombo vya habari kuliko mwanasiasa yeyote mwingine Kenya . Lakini kilichoniua ni kwamba inasemekana hata timu ya mpira wa miguu ya Kameruni ilipofika Kenya ,maafisa wa Kenya wakaiondoa timu ya Taifa ya Kenya kwenye uwanja mzuri iliiipishe ya Kameruni. Kumbuka ni katika kipindi ambacho timu ya Kenya ilipokuwa inajiandaa kucheza mechi ya kimataifa. Soma habari hii mwenyewe:
African Inferiority Complexes. Mtazamo huu wa kimawazo nimeushuhudia sana Tanzania.

Sawa watu wengi husema sisi Watanzania ni wakarimu. Lakini mimi nahisi ukarimu wa kuufanya tu kwa kuwa tu mgeni kutoka nchi za nje anahusika hautatupeleka mbali.

Read more...

Tanzania gizani!

Kila nikisikia juhudi za viongozi wetu kufanya ziara duniani hujiuliza hivi ni wawekezaji gani ambao ni walengwa? Karibu wawekezaji wote hawataweza kufanya mengi ikiwa hakuna umeme wakuendeshea shughuli. Labda ikiwa walengwa sasa ni wale wawekezaji ambao watasaidia kutatua matatizo ya umeme au safari hizi zenye gharama za kutafuta wawekezaji hazitakuwa na manufaa sana.

Chakujiuliza tu ni kwamba:inawezekanaje katika nchi za Afrika Mashariki ni sisi tu tunaathirika sana na swala hili la umeme mara nyingi kuliko wengine?
Je, kwanini hakuna mipango ya muda mrefu ya kujua jinsi ya kukabiliana na swala hili la umeme?
Hivi katika maswala ya kupewa kipaumbele, ndege ya raisi, radar ya jeshi au umeme uwezeshao viwanda kufanyakazi ni nini muhimu sasa hivi?
Je umeme kuwepo siku za mapumziko na kukatwa siku za kazi sio dalili kuwa wahusika wanatoa kipaumbele potofu?

Natumani siku moja taifa letu litafikia uwezo wakutabiri maswala yafaayo kupewa kipaumbele katika wakati ufaao kuandaa matatuzi.Kwa maana kama ilikuwa haijulikani kuwa taifa litaingia katika kisa hiki kabla basi sishangai Tanzania ikijikuta inakabiliana na kasheshe nyingine kama hii kienyejienyeji tu.

Read more...

Chakula cha Mawazo!

>> Tuesday, October 10, 2006

Dini yako ni ipi?

Je wewe ni mkristo au muislamu?
Hivi kwanini siasa ya Taifa kama Tanzania haichezi mbali na maswala ya dini?
Kwanini dini ni muhimu Marekani na siyo Japani?
Hivi Louis Farrakhan unamkumbuka?Naona naye anasubiri kufa kwa kansa sasa hivi.


Duh hivi kweli asilimia kubwa ya Wachina, Wahindi , na Waafrika ambao hawako kwenye Ukristo au Uislamu kwao ni motoni tu? Hivi Wayahudi wasio wakristo au waislamu kwao ni motoni? Hivi Uislam wa Wamarekani weusi ni sawa na Uislamu wa Uarabuni?Hivi Ukristo wa Afrika ni sawa na wa nchi za mgharibi?

Hivi wewe ni mdini wa kweli?

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP