Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Richard Bona Eeeh!! Mimi mshabiki !

>> Tuesday, November 14, 2006


Katika vyombo vya muziki nivizimiavyo ni Bezi gitaa. Halafu si siri miziki ya jazz ni moja ya miziki niitumiayo kusafiri katika ndoto za mchana(day dreams) na pia nikiwemo ndani ya treni ya mawazo.Nisikufiche Majazz yanapanda hata wakati nafanya kimbunga cha ubongo(brain Storming). Sasa huyu Mkameruni ni miongoni mwa wanamuziki wa kiafrika ambao wanatambaa katika miziki niipendayo kisawasawa.Anatambaa kuanzia Afro mpaka kwenya klasiko Jazz bila shaka.Hebu msikilize kwenye solo hii hapa chini:




Kama nilivyosema huyu katika wapiga Bezi gitaa waafrika huyu Richard Bona ni miongoni mwa naowahusudu. Tarehe saba mwezi huu nilifanikiwa kuona shoo yake na kuongea naye. Alichonizingua alipojua tu natokea Tanzania akaniauliza unatokea Bagamoyo? Swali hilo ingawafupi lilinidhihirishia kuendelea kutambulika kwa wasanii watokao Bagamoyo. Kwa maana sasa ni mara nyingi nikikutana na wasanii waaminikao katika fani kutoka nchi kibao tu wanakuwa wanajua kuhusu Bagamoyo. Bahati nzuri safari hii nikikutana na Richard Bona, nilikuwa na Msanii mahiri wakibongo, ambaye najua ipo siku Tanzania itamjua aitwaye Menard Mponda , hivyo halikuaribika jambo.



Richard Bona akikupa kile kibao kiitwacho 'Engingilaye'

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP