Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ed Bradley

>> Friday, November 10, 2006

Ed Bradley








Huyu mwanahabari Ed Bradley amefariki Alhamisi hii.Leukemia imemuondoa hapa duniani. Huyu ndie aliyekuwa ananipamotisha sana hasa nikiwa namcheki katika kipindi cha 60 minutes. Ni miongoni mwa watu weusi wachache walioweza kuingia katika vipindi vya televisheni vilivyo maini strimu kabla mambo ya cable tele hayajavinjari Marekani. Kuna kauli moja aliyowaikusema iliniingia sana. Alisema kisa cha yeye kuingia sehemu ambazo watu weusi walikuwa wanaamini haiwezekani ilitokana na wazazi wake kuwa wanamwambia tokea utotoni kuwa:mtu unaweza kuwa chochote utakacho. Akamalizia kwa kusema :unajua ukiwa unaambiwa kila siku jambo hilo unaanza kuamini katika hilo. Mimi nakubaliana kabisa na hilo. Sisemi kuwa ni rahisi lakini ni jambo lenye ukweli ndani yake. Sasa mara ngapi unasikia katika bongo yetu mzazi anakazana kumwiita mtoto wake pumbavu , huna akili, nk?Mimi nilichojifunza kutoka kwa Ed ni kwamba mtoto huanza kuamini katika hilo na kuanza kukosa kujiamini. Ni sawasawa tu na jinsi watu wengi weusi wasivyojiamini hasa watu wa rangi nyingine wakiwa katika anga kutokana na kuitwa pumbafu hujuikitu.
Pumnzika ED!


1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 1:10 pm  

Custo,

Umenistua na taarifa hii ya kifo cha Ed Bladrey. Mungu ampumzishe kwa amani, Amen.

F MtiMkubwa Tungaraza.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP