Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Mwanamama Cesaria Evora azidi kunizingua

>> Wednesday, November 01, 2006

Cesaria Evora hufanya maonyesho yake bila viatu akiashiria kukumbuka akina mama na watoto masikini waishio kisiwa atokacho cha Cape Verde








Siku chache zilizopita nilifanikiwa kumuonatena Cesaria Evora akifanyaonyesho lake maridadi kama kawaida yake. Huyu mama ajulikanaye kama DIVA MTEMBEA PEKU(The Barefoot Diva), ananiua sana awezavyo kudaka watu kwa sauti na uimbaji wake , nakuwafanya wakae chini kimya kusikiliza wakati hakuna anayejua anasema nini. Zamani wakati wa ndombolo,nyimbo za kihindi na hata za magharibi, nilikuwa bingwa wakuzitungia maneno ya kiswahili. Nakumbuka wengi tu tulikuwa tunaimba nyimbo kama: Maiko Jaksoni njooo, sitakiiii, kama hutaki nenda!Nyimbo ambazo tulikuwa hatuelewi zinaongelea nini , lakini zinachezeka. Kwa sababu zinachezeka basi maswala ya ujumbe yalikuwa si muhimu. Ila huyu mama anachonizingua ni uwezo wake wakukukalisha chini hata kwa masaa mawili akikuimbia na ukatulia na kuingiwa tafakari za kila aina mpaka unastukia anawaaga.Akiaga hapo ndio unastukia kuwa kumbe alikumeza na muziki zaidi ya masaa mawili. Kutokana na hilo husafiri duniani kote na kuimba akipokelewa kwa mikono miwili bila tatizo.

Sasa nani alisema kuwa kwa kuimba kiswahili tutashindwa kuwa na wasanii ambao wanaeleweka duniani? Naamini kama Cesaria anaweza kwa kushikilia nyimbo na midundo ya ki Cape Verde, basi na Watanzania tunaweza kwa kushikilia miziki yenye midundo yetu. Basi hata ambapo wasanii sasa hivi wanapotaka kubobea kwenye midundo ikaribianayo na ya Marekani tukumbuke kuwa bado tunaweza kufanikiwa kwa kuendeleza midundo yetu.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP