Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati karibu kila mtu ANAJUA kuwa NIPE KIDOGO NICHANGAMSHE DAMU kwa kawaida hugeuka ''NIPE YOTEYOTE, yote tu JAMANI!'':-(

>> Saturday, October 31, 2009

[Tahadhari: Katika kichwa cha habari sentensi ''NIPE YOTEYOTE, yote tu JAMANI!'' imebaniwa pua na Limdada zuuuri!:-(]


KIDOGO ni chachandu,....
.... na ikizidi kwa kawaida utavimbiwa.:-(


KIDOGO ni utundu,....
..... ikizidi maana yake huweza kutafsirika kuwa umeharibikiwa.:-(


Na kijuacho ukubwa kwa kawaida KAMA ni tundu,....
....basi kwa hilo si lazima mpaka tundu liwe KUINGIZWA limejaribiwa.:-(

Ila kwa kuwa Binadamu ni watundu,...
....DUNIA INAHARIBIKA SASA HIVI kwa kuwa TU mpaka binadamu wakijuacho kidogo wanakitaka kwa ukubwa na MAKUBWA YOTE KILAFI , na ndio maana wanaonja mpaka VYENYE SUMU VILIVYO tayari JARIBIWA.:-(

NALIKATIZIA HILI WAZO HAPA na unaruhusiwa kuliendeleza KIVYAKO MHESHIMIWA!:-(
Lakini swali KIDUCHU:

  • Unafikiri si kweli kuwa WALIOONJA KIDOGO na kujua ni tamu kwa kawaida hutaka makubwa yote ingawa wanajua kuwa hata asali ingawa tamu kuinywa, KUNYWA LITA kwa kawaida ni tofauti na kuilamba asali kidogo katika ujazo na KWALITI wa uupendao utamu?
  • SI unajua siri ya kilele cha utamu hupatikana kwa kuonja kidogo tu?
NIMEACHA na kumbuka hili ni wazo tu!
KUMBUKA PIA kuwa KIJIWE HIKI cha MTAKATIFU Simon Kitururu sio YESU wala NYERERE kikukorokochoa!:-(


JUMAMOSI NJEMA Mheshimiwa OTHRONG'ONG'O!


Hebu basi tusukutue uchafu wa wazo kwa kumsikiliza M-Ivory Coast mdada Monique Seka akilainisha kwa ndude iitwayo-Okaman

Au tubaki naye tu Monique Seka afanye matusi katika kitu -Missounwa

Read more...

Katika kufuatilia HISTORIA ya BINADAMU NA lugha, unadhani ADAMU na EVA walikuwa wanaiita ngono jina GANI wakati wanaitana chobisi ili KUNANIHII?

[Tahadhari: Kama unajiheshimu unaruhusiwa kutosoma hii taralira!:-(]

Fumba macho ,....
.....halafu tafakari kama ungetaka kumuomba KIZALISHIO mtu kwa tumizi la burudani au la kuzalisha MGAGAGIGIKOKO msiyeelewana lugha, uhisi ni sauti NA NENO gani ungelitumia kumuelewesha katika mtongozo MGAGAGIGIKOKO asiye wa KIMANDENGO utakacho kitumbua SIO binamu ya andazi KITUMBUA.

Halafu fungua macho,....
.... na jaribu kutafakari kama unanjaa halafu ni ombaomba, ni sauti au vitendo GANI utatumia kuomba chakula KUTOKA KWA mtu msiyeelewana lugha hata kama chakula chenyewe UOMBACHO ni kitumbua KITUMBUA.

Swali:
  • Unafikiri UNAHITAJI YENYE MANENO lugha kama unahitaji kuwasiliana na ujuaye hamuelewani lugha ZA MANENO hata kama ujumbe ukupao nyege ya kutamka ni kumtusi tu Mwalimu Nyerere '' BICHWA kama mbwa''?



OK!
NIMEACHA hili WAZO Mheshimiwa!

Ngojea tu ABETI MASIKINI arudishe utulivu na ustaarabu kwa kitu-Yamba Yamba



Au tu tena ABETI MASIKINI adunge kitu-Je suis fache

Read more...

CHA AJABU ni kwamba, WENYE AKILI WENGI bado husomea ambavyo wangeweza KUVIJUA WENYEWE BILA KWENDA SHULE!:-(

>> Friday, October 30, 2009

Na ni kweli,...
...wengi wasifiwao kwa akili NI kwa sababu TU wanasomea ambayo kwao kirahisi wangeyajua tu bila MWALIMU!:-(

Na ni kweli,....
.... karibu kila mtu kuna kitu KWAKE ni rahisi kama KUNYA TU na wala si vigumu kama KIWASUMBUAVYO WENGI CHA kujulia jinsi ya KUTAWADHA VIZURI baada ya kuachia TIMBA , ingawa haki ya nani hata katika hilo la STAILI YA KUCHAMBA VIZURI wengi hufikia UGWIJI bila msaada wa MWALIMU!:-(

Swali:
  • Unabisha?
  • Kwani unataka kusema BADO hujastukia KUWA mpaka wenye vipaji vya asili vya kusukuma mkokoteni wapotezavyo muda kusomea kusukuma mkokoteni hata kama UDHAIFU wao uhitajio SHULE uko katika kumridhisha mama watoto na KWA HILO hata siku moja haistukiwi labda SHULE bora kwao ingekuwa ni ya kuridhisha mke na sio ile waahangaikayo nayo wakati hawaihitaji SANA ya kusukuma mkokoteni?

  • Kwani hujastukia kama MFUMO usingekuwa UNA VYETI vihakikishiavyo watu kuwa KIBONGE KAENDA SHULE kuna wengi wenye DIGIRII za VYUO VIKUU elimu yao katika swala ni BOMBA LA KINDEGATENI?

HILI NI wazo tu KISHTOBE na wala usitishike!
Ijumaa NA wikiendi njema MHESHIMIWA!

Hebu tupate tena ambacho kwa MAFISADI labda NI burudani kutoka TANZANIA kama iletwavyo na ile kitu -DARWIN's NIGHTMARE


Au tu hebu huyu Mbenini WALLY BADAROU atupe ile NDUDE roho ilipenda iitwayo - HI LIFE




Au tu Mkameruni BEBE MANGA amwage tena ndude roho ilipenda kwa jina-AMIO

Read more...

Samahani naiachia hii NYOKO ibinjuke kwa UNG'ENG'E!:-(

>> Thursday, October 29, 2009

Nenda HAPA ,...


......UJIKONDESHE kama huwa unakunwa na HIZI VITU NYOKO za kitafiti AMBAZO saa nyingine ni NYOKO kuzifuatilia na kuziamini....










What is prosperity, and how is it achieved?


Following a turbulent year marked by a global economic crisis, the Legatum Prosperity Index seeks to answer these two fundamental questions. It defines prosperity as both wealth and wellbeing, and finds that the most prosperous nations in the world are not necessarily those that have only a high GDP, but are those that also have happy, healthy, and free citizens.

How we created the Index

The Prosperity Index accounts for 90% of the world’s population and is based on years of statistical analysis and research of objective data and subjective responses to surveys. The data comprises 79 different variables organised into nine sub indexes – each identified as a foundation of long-term prosperity. A country’s performance in each sub-index is given a score, and the overall Prosperity Index rankings are produced by averaging the scores of the nine sub-indexes for each country. Those countries that perform well across each sub-index do best in the overall rankings.

The nine sub-indexes are:

  • Economic Fundamentals – a growing, sound economy that provides opportunities for wealth creation
  • Entrepreneurship and Innovation – an environment friendly to new enterprises and the commercialisation of new ideas
  • Democratic Institutions – transparent and accountable governing institutions that promote economic growth
  • Education – an accessible, high-quality educational system that fosters human development

  • Health – the physical wellbeing of the populace
  • Safety and Security – a safe environment in which people can pursue opportunity
  • Governance – an honest and effective government that preserves order and encourages productive citizenship
  • Personal Freedom – the degree to which individuals can choose the course of their lives
  • Social Capital – trustworthiness in relationships and strong communities

Rankings

Finland tops this year’s Index, with the United States ranking ninth, ahead of large European nations such as Britain, Germany and France, which all still make the top 20. Finland is narrowly ahead of Switzerland, Sweden and Denmark. Zimbabwe ranks last, following Yemen and Sudan.












TANZANIA kwa kuwa TOP TENI ya takoni OYEEE!:-(

AU tujibaraguze hatujali kwa kuangalia akinadada wakifundishwa GOLF na kudakwa na SEXY CAM katika- The Golf Course

Read more...

katika KUJARIBU KUZICHUNGULIA tamutamu ZIOANISHWAZO na ETI KWASABABU TU JAMAA ni la kwanza KUFANYA!

Kuna wajivuniao KWELI kwa kuwa ni WA KWANZA,.....
......mpaka usipokuwa mfikiriaji waweza kutostukia DUNIANI kuna mengi ukitaka kufaidi MGIDO basi weye usiwe wa KWANZA.

Kwa mfano, ukiwa wa pili na sio WA KWANZA,....
.....kama wewe ni mdadisi na unajua kuandaa shughuli kwa kumchunguza ALIYENANILII kwanza, UNAWEZA kujikuta shughuli nzima za ALIYEENDA MWEZINI KWANZA, kuwa Rais wa TANZANIA kwanza, KUTOLEWA bikira ya mbele ya NYUMA kwanza,KUPATA UKIMWI KWANZA,.......nk. wewe unazihimili vizuri kama huna mchecheto kwa kuwa kuna wa kumuangalia yaliyomkuta kwa KUNANILIHI kabla YAKO kwanza.:-(


Na nikijaribu kukuambia ukweli hasa wewe ujivuniaye kwa kuwa WA KWANZA,....
......kumbuka kila mtu hata kwa kuonja mwisho, hiyo ni KWANZA YAKE kama ndio anaionja hata ikiwa ni EMBE BOLIBO TU lakini NI kwa mara ya KWANZA.


Swali:
  • Hujastukia furaha nzima imfurahishayo mtu kwa kuonja KWANZA ni ya kisaikolojia tu na kama ingekuwa kionjwacho kinahisiwa kuwa na sumu , MTU KIBAO zingekwepa kuwa wakwanza kulamba NDUDE?
  • Lakini umestukia kuwa kama nia yako ni uwe wa kwanza halafu ukawa wa pili inauma kweli ingawa ukweli ni kwamba MAUMIVU YOTE HAYO yanaponzwa tu na tafsiri ya maana yake ni nini kwako kuwa WA KWANZA?

Kumbuka NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA na wala sikushauri kama nia yako ni KUONJA KWANZA usubiri mpaka mabingwa wakuonjee NANIHII ILE KITU UNAPENDA uitakayo iweyako yoteyote hata kabla hujaionja KWANZA!


DUH Ngojea NIACHE!

Lakini hebu twende KAMERUNI Sandra NKAKE akiwa na BOOSTER watusaidie kubadili hali ya hewa HAPA kijiweni kwa kitu-Sex FRIEND


Au tu SANDRA NKAKE aje tu live akikumbuka Kameruni kwa kitu-I Miss My Land

Read more...

AKILI sio NYWELE na LABDA si kila mtu ANATUMIA zake!

Na ni kawaida kukosea MATUMIZI ya akili,.....
....hasa kwa kuwa SIYE MTU KIBAO tunasahau kuwa ndani ya siku LABDA akili zetu hutumika zaidi SIO KWA KUBUNI na KUFANYA YA KWETU WENYEWE KIAKILI , bali kifanyikacho NI kutumia akili zetu ili kutumia yaliyoanzishwa na kufanywa na AKILI ZA WENGINE.

Na haki ya nani kuna WENGI tuishio bila kutatua yetu ya KIAKILI ZETU kwa kuwa zetu akili,....
.....zijuacho TU hata katika kuelewa ya KWETU, hakikamiliki bila kutumia akili za WENGINE.:-(

Kama unabisha:
  • Unafikiri kama wewe ni MKRISTO huhitaji kutumia yaliyokokotolewa na akili za YESU ili umwelewe YESU anamaanisha nini kwenye hata la kubatizwa ni kuzaliwa tena , au tu KWA UJUMLA UKRISTO WENYEWE hata kama huamini hii ANDUNJE NI kitu ambayo kwa kuwa INATEGEMEWA TAYARI KUNA AMBAYO HUTAELEWA, yabidi katika kukihalalisha KITENDO CHA KUWA MARA NYINGI KIDUCHU DINI HAZIELEWEKI, unaandaliwa uelewe yasiyoeleweka YA kufuata dini bila kuelewa KWA KUFUNZWA YASIYOELEWEKA KWA KUTUMIA AKILI ZA KIBINADAMU ni IMANI au yanaeleweka UKIWA NA IMANI TU?
  • Si ushawahi kusikia kwa imani utaponywa na kama imani yako mkweche hutapona HATA ukoma wa nanihii?

  • Na kama wewe ni MUISLAMU, unafikiri huazimi akili mpaka za SHEKHE ili tu uelewe utakacho kukielewa katika UISLAMU?
  • NA si unajua kama sasa hivi unatumia KOMPYUTA labda unatumia akili za wengine kama sio wewe uliyegundua KOMPYUTA?


Ok MKUU!

Labda kama kila mtu ana akili zake basi akili za watu ni OMBAOMBA kwa jinsi tu zilivyodoezi katika hata watatuayo idaiwao WANAAKILI inasahaulika labda walitatua kwa kudoea AKILI ZA WENGINE!:-(

WAZO nalikatizia hapa na UNARUHUSIWA KUNIBISHIA MUUNGWANA na katika SPIRITI ya kutokusahau KUTONIELEWA NI BOMBA LA Ruksa!






Au ngojea nikiri yamenishinda katika hoja hii kwa kusema...


Basi bwana mie ngojea nirudie kumsikiliza tena ASA akilalamika tena kuhusu-JAILER




Au tu Jimmy DluDLU arudishe tena JAZZ kutoka AFRICA.....

Read more...

Umefanikiwa KUDANGANYA MTU leo ?

[Tahadhari: Katika taralira HII Sentensi NI ndefu na pointi ujazo wake NI nukta!:-(]

Dunia imejaa uongo na dalili zenyewe waweza kuzistukia kama umestukia kuna WATU wanajipodoa,...
......kwa kuwa TUKITAFSIRI KINAMNA , ajipodoaye anataka tu kukudanganya kuhusu halihalisi ya UNYORORO wa yake NGOZI.

Na wengi kama mavazi yao UTAYAONDOA,....
...unaweza kustukia mpaka MREMBO KITOVU saizi KIBUYU , idaiwavyo KATIKA REDIO ZA MBAO ni kwamba ana KITOVU SAIZI YA JIPU DOGO , wakati labda HATHARI ZA KITOVU saizi KIBUYU ndio vimfanyavyo MHESHIMIWA JAMAA mpaka LINAVAA jeans aina DENGRISI, yote IKIWA ni katika kubana ukubwa wa ngumi wa KITOVU , na kwa hilo la SAIZI ya ngumi laweza mpaka kukufanya UKARIDHIKA NALO angalau ukisikia MHESHIMIWA mwenye KITOVU SAIZI NGUMI ,anakitetea kwa KUREMBA TETEZI kwa kudanganya LAKINI bila kupunguza ukubwa wa tovu MPAKA ufikie saizi ya jipu kwa kudai anakitovu SAIZI ya KONZI.


Na kwa kuwa jamii haipendi WAHESHIMIWA heshima zao tuzitie MADOA,....
....haki ya nani mpaka UBONGO unaweza usistukie Mheshimiwa anatudanganya tu na sketi ndefu tusione kwenye MIGUU ana BOMBA LA TEGE , na KIHESHIMA uongo wote wa matendo ya watu ili tusistukie ukweli twaweza kuuita ni MATENDO YA KUTUSAHAULISHA KUSTUKIA UKWELI , ingawa UKWELI uko palepale kuwa KWA ASHUHUDIAYE hata swala la kuwa MHESHIMIWA KABANJA , kumbuka tu KWAMBA kila abanjae hata awe maridadi kivipi huyo anajua utamu wa kamasi NI NINI hata kama kilichoshuhudiwa KWAKO baada ya yeye KUBANJA SIO KULAMBA KAMASI ila ni staili yake TU ya kutema KOOOZI.:-(

Swali:
  • Kwa hiyo sasa hivi MATENDO na MUONEKANO wako bado HUAMINI labda TU yana lengo LA kutudanganya TUSISTUKIE UDHAIFU WAKO NI NINI, au wewe ndio uridhikaye tukidai unajaribu kutusahaulisha tusistukie staili ya kunuka jasho kwako ni IPI kwa kuwa una bomba la PAFYUMU na kwa hiyo kwa HILO hutudanganyi?
  • Kwani UNATAKA KUSEMA hujui KUDANGANYA kwingi kwa watu hakutumiii maneno?

MHESHIMIWA nimeacha WAZO hili NYOKO!


Au tuliza mshawasha kwa Steel Drums wimbo- Sweat(A la la long)


Au tu Inner Circle wenyewe waje live na wimbo huo huo-Sweat(A lala long)


Au tu Big Mountain wadai tu nao-Baby I love Ur WAY

Read more...

Sala ya LEO: Miungu MKIUMBA TENA WANADAMU , labda wajalieni nywele za KIZUNGU AKINADADA ZETU Waafrika !

>> Wednesday, October 28, 2009

NA tufumbe macho TUOMBE! NA kupiga magoti ni RUKSA .;


Kwa MIUNGU wahusika!

Naamini mmestukia kwa nguvu zote asilimia kubwa ya akina dada wa KIAFRIKA wakomavyo na KIPILIPILI.

Na naamini mnashuhudia mpaka AKINA KAKA wa KIAFRIKA nao walivyoshindwa kuwa msaada kwa kukosa WABUNIFU wa jinsi ya kulainisha nywele za akina DADA WAKIAFRIKA ili wasisumbuke na MAWIGI au tu katika kujiandaa MPENDEZO iwe rahisi kidogo ili wasilazimike KUIGA WAZUNGU , kwa angalau kuvumbua MASHINE zielewazo mpaka cha MUAFRIKA kipilipili.

Halafu na hawa akina KAKA nyie MIUNGU wafumbueni macho ili akina dada bonge la figa , TABIA nzuri PANA, akili ujazo TANI, MASHAVU ya KUMIMINA mwanana , Macho ya GOLOLI za nguti, SANGARA wamo, KUJAMBA pafyumu, wasipikuliwe katika kudakwa PENZI na wenye kalikiti mpaka kwenye masharubu ya KWAPA kwa kisa tu eti STAILI YAO ya nywele KIPILIPILI!


AMEN!

MNAWEZA KUFUMBUA MACHO SASA!

Swali:
  • Unauhakika kuwa ni kweli sababu kubwa ya asilimia kubwa ya Wasichana wa Kiafrika isemekanao wamefanikiwa kuwa na nywele zifanananazo na za Malkia Elizabeth ni kwakuwa tu ni vigumu kuhudumia NYWELE KIPILIPILI?

HILI NI wazo tu MHESHIMIWA na wala USITISHIKE !:-(

Ngojea Oliver N'goma na Bhonos wamsifie Mwanadada ambaye nahisi labda anakipilipili na twende kilioni imeanza kufumuka kwa mbaaaali aitwaye-Alphonsine



Au tu Oliver N'goma mwenyewe aendelee kumuongelea mwanadada mwingine kwa jina-Julie

Read more...

Punyeto ya UBONGO!

Kuna UWEZEKANO kabisa kuwa,....
.....kila mtu kwa siku hutumia asilimia MIA ya wake UBONGO!

Na inawezekana kuwa,....
.......kwa kuzimia UBONGO wa profesa wa MAPISHI kwa kuwa chakula chake ndicho tukionacho na ni kitamu, WATU hujisahau muosha SUFURIA labda kwa hilo NI PROFESA wa UOSHAJI na SI UPIKAJI na ni JINIASI kwa usuguaji SUFURIA/Chungu kwa kutumia majivu na katani kwa hilo UKIANGALIA atumiavyo UBONGO.


Na INAWEZEKANA kuwa,....
..... ni jinsi TU ya kubalansi MTU ATUMIAVYO ubongo kufanyako wengine wadhani kunawasiotumia UBONGO.
Ubongo NI kitu cha ajabu kwa kuwa,....
.....ndicho kikusababishacho ustukie una UBONGO.

Na kwa kuwa ,.....
.... UBONGO haulali, ndio maana ni kiranja MPAKA wa mapigo ya MOYO na yote afanyayo BINADAMU hata bila ya kujijua anatumia UBONGO..


Na kuna maswali MENGI kuhusu ni asilimia ngapi ya UBONGO binadamu atumiayo.....

Na tujuacho ni kwamba ni asilimia chache tu Binadamu tujuazo kuhusu UBONGO........
Na kunauwezekano kabisa Profesa wa HISABATI na Hausiboi KIBAKA anayekuonjea kwa siri mke wako bila wewe kujua kwa ufanisi WANATUMIA nguvu sawa KIUBONGO kufanikisha KALIKULESHENI za kufanikisha zao fani.....

....Endeleza Mental masturbation/Punyeto ya UBONGO kwa kumsoma ROBYNNE BOYD katika banangenge aiitayo -

Do People Only Use 10 Percent Of Their Brains?



....kama alivyoiandika kwenye http://www.scientificamerican.com kwa kukongoli HAPA


....astue hoja zenye mistari ijaziazo ndude ....
....Adding to that mystery is the contention that humans "only" employ 10 percent of their brain. If only regular folk could tap that other 90 percent, they too could become savants who remember π to the twenty-thousandth decimal place or perhaps even have telekinetic powers.


Au tu adai.....
.....Another mystery hidden within our crinkled cortices is that out of all the brain's cells, only 10 percent are neurons; the other 90 percent are glial cells, which encapsulate and support neurons, but whose function remains largely unknown.


SAMAHANI kwa kudesa MITAZAMO YA MTU MWINGINE katika kujaribu kukupigisha punyeto ya UBONGO kama wewe ni mpenda kutekenya UBONGO.:-(


Au tu tubadili hali ya hewa na kuwasikiliza Oliver Mtukudzi & Ringo Madlingozi wakileta kitu-Into Yami



AU tu unaweza kuangalia mazoezi kama yalivyodakwa na sexy cam katika-Sexy Aerobics

Read more...

KWA aelewaye neno BINDUKI hutumiwa na amaanishaye BUNDUKI!

>> Tuesday, October 27, 2009

Kwa waelewao BINDUKI ni BUNDUKI,....
..... bado CHAKUSIKITISHA tu ni kwamba wengi wasahihishao LUGHA hainamaana ni kweli wanaelewa katika lugha KINACHOONGELEWA.:-(



Na kama swala ni UJUMBE na si LUGHA wakati tunaongelea kwa nini binadamu kwa kumkabili BINADAMU wanahisi wanahitaji BUNDUKI,...
......kwa kawaida UJUMBE WA HOJA HUFIKA KWA MWENYE MACHALE hata kama lugha katika hilo hakuna mwenye kukumbuka KUIHARIRI KWA KUWA HICHO KWA KAWAIDA SI MUHIMU KAMA NI KWELI UNATATIZO na cha mwisho katika yote itakuwa ni kustukia kuwa mwenye BUNDUKI kaiita BINDUKI na kwa sababu hiyo wadai HUJAELEWA.:-(





Swali:

  • Si unajua kwa kukosea tumizi la neno katika lugha unaweza kujikuta unaongea kiitwacho lugha ya kisasa?
  • Si unajua kama unanjaa jinsi uelewavyo kirahisi umekaribishwa chakula hata kwa Kichina?

NI wazo tu hili Mheshimiwa OTHRONG'ONG'O na wala lisikutishe!

Hebu MANU CHAO atupe tena -BONGO BONG


Au tu adai-POLITIK KILLS

Read more...

Kama ni kweli UNAFIKIRIA unachokifikiria!

Unaweza KUSTUKIA ukifikiria,....
... kuwa kila mtu afikiriapo kitu maana yake WAKATI HUO hilo linawezekana KWA KUWA kuna ASICHOKIFIKIRIA!

Swali:
  • Kwani unauhakika kuna afikiriaye mambo mawili ndani ya sekunde HIYOHIYO moja?
  • Kwani unafikiri ni kawaida KUKIFIKIRIA unachokifikiria?
  • Unafikiri hupumzishi fikirio moja ndio maana la pili limeshamiri?


HILI Ni wazo tu MHESHIMIWA na KWA BAHATI MBAYA linaweza lisikusaidie mlo LEO!:-(



Au hebu MANU DIBANGO atupe kitu-African Battle



Au tu Manu DIBANGO adondoshe kitu alichokipiga mwaka1974-Super Koumba

Read more...

SIRI!

SIRI inamchezo wakutokuwa siri kwa jinsi tu uifanyavyo ni SIRI!:-(

Kunauwezekano,...
.....MWISHO wa SIRI YA KITU ni utambuapo unataka HICHO kiwe SIRI!:-(

Swali:
  • Kwani hujastukia watu wengi tabia zao na MPAKA muonekano wao ni MATOKEO ya vita zao tu na waliyoyatambua na kuamua hayo ni SIRI?

  • Unajua kuwa kama siri yenyewe ni sura mbaya mdada anaweza akahakikisha anabomba la staili ya nywele halafu mwendo wake ni wa tingisha tako ili usibobee kumchunguza sura?

  • Unauhakika kuwa tabia nzuri mbele za watu sio KIFICHA SIRI tu cha ajihisiye anasura mbaya mbele za watu ?
  • Hufikiri kwa kujifanya unaakili ni staili tu ya kuficha yako ya kijinga ufanyayo ni SIRI?

NI WAZO TU HILI Mheshimiwa!:-(

Hebu Lagbaja arudie ndude iitwayo-GRA GRA



Au tu arudie ndude iitwayo-Skentele Skontolo

Read more...

KAMA wafu a.k.a marehemu WANAONA!

>> Monday, October 26, 2009

Basi kunauwezekano kuwa,....
....BINADAMU lukuki wanachunguliwa na NDUGU ZAO WAFU /Marehemu katika ya FARAGHA ya chooni au mpaka TU yale yamjazayo mtu MIMBA!:-(

Swali:
  • Baada ya kujua hilo huhisi labda inahitajika uongeze MACHEJO ya kumwaga kitendo hata kama unahisi huchunguliwi kwa kuwa umejifungia chobisi wakati wa tendo dukinaa?
  • Wakati unafanikisha unafikiri utasumbuliwa zaidi ukihisi ni MUNGU au ni NDUGU ZAKO MAREHEMU ambao wakati wanakula bisi mbinguni burudani yao ni kukuangalia ukionyesha maringo yako wakati unahisi UNAFARAGHA?
  • Kama unaamini kuna MUNGU na anaona yote, unauhakika unatoawapi jeuri ya kutokuwa na haya wakati wa kitendo ufanyacho siri HASA ukihisi BINADAMU KIBAO zisizo muhimu kama MUNGU hazikuoni?

NI WAZO TU Mheshimiwa na WALA USITISHIKE MKUU!


Au tu ngojea Bobby McFERRIN akumbushie-DON'T worry be HAPPY

Read more...

PANUA ZAIDI KIDOGO basi mpenzi NIINGIZE!

[Tahadhari: Panuo katika hili wazo halina uhusiano na maungo.:-(]


MAPENZI ni kupanuliana,...
... kwa kuwa hasa kabla HUJAPANULIWA ndipo USTUKIAPO hata katika maisha YANAYOBANA ni KIBANO!:-(


NA katika PENZI hata liitwalo MAISHA kama wewe ni MUUNGWANA anayebana,....
...basi kama PENZI ni la KISWAHILI na hupanui wakati unakipanulio, KUNA uwezekano unalielewa PENZI kwa Kiitaliano na huelewi kwanini wengine PENZI = MAISHA na katika hilo labda HUHITAJI kujua KIRENO.:-(

Na ni kweli kwa apanuaye zaidi ajuacho huwa kinabana,......
......NI KWELI hupata zaidi MPAKA hata ujuzi wa ambavyo kwa kawaida INASEMEKANA hata malaya anabania, NA huyo NDIYE ASTUKIAYE mpaka kama WATANZANIA kabila ni WAPARE kuwa hata kwa WAPARE ili UELEWEKE wapo ambacho waongeacho KIPARE huitwa KIGWENO!:-(


NAACHA WAZO !
Kumbuka SI LAZIMA UELEWE kila kitu MAISHANI kama hata hiki HUELEWI, kwa kuwa KWA KAWAIDA kutoelewa ndio siri ya kuwa wewe NI BINADAMU!


Swali:
  • AU?

  • Si unajua UKIPANULIWA unaweza kuingiza au KUINGIA KIRAHISI ndio maana SI MAZINGAOMBWE mtoto wa KIKWETE ikiwa kirahisi kawa KIKWETE na mtoto wa MWALIMU NYERERE akashindwa kuwa NYERERE?
  • Unajua kunauwezekano kama umefanikisha kuna aliyekupanulia ingawa kijeba unataka tukusifie kuwa uliyofanikisha ni juhudi zako tu?

Hebu JIMI HENDRIX atoe dozi katika kitu kisicho mkao wa kitoto kigitaa....-THE SKY is CRYING



Au tu TINA TURNER akumbushie -BETTER be GOOD to ME


Au tu MwanaFA na LADY JAY DEE watulize boli KIBONGO kwa kitu-MSIACHE KUONGEA

Read more...

Ni UTAALAMU kwa mwenye MDOMO na awezaye KUFANYA MATENDO kufikia idaiwe ANAHESHIMA !

Haki YA NANI VILE , kama katika maisha unafikiria mpaka HESHIMA ,...
... ufanyacho ni ANASA ingawa unaruhusiwa MHESHIMIWA hata KWA HILO kunibishia tu!


Na HAKI YA NANI TENA VILE, kama katika yote wewe umefikia MPAKA kufikiria HESHIMA,....
....basi KUNAUWEZEKANO wewe maishani kuna MAMBO LUKUKI umetatua NAKUYAFIKIA na LABDA HATA kwa kuheshimu wengine, NI WEWE TU uliyefikia mpaka KUHITAJI uheshimiwe tu!:-(


HESHIMA na kukosa HESHIMA,...
..... vyote ni kutokana na MTU amjuavyo MHUSIKA tu!:-(

Na hata bisha USIBISHE, ukijua sana vya ajulikanaye kwa kuwa na HESHIMA,...
..... utakuwa tu unashangaa kwanini BWANYENYE anaitwa MHESHIMIWA, na kwa hilo halibadili kuwa AITWAYE MHESHIMIWA aheshimiwako LABDA sio alambako visivyolambwa CHOBISI tu!:-(

Na uheshimiwa NI bomba la nyoko HASA kama kukosa kwako HESHIMA,...
....KIBONGE hujastukia, NA eti NA WEYE BINGWA nawe WAJARIBU KUFANYA mpaka uvikoseavyo adabu visimi ETI navyo NI SIRI tu!


NI HILO TU MHESHIMIWA USTAHILIYE HESHIMA na HATA pia weye MHESHIMIWA Ajuza!

Swali:
  • Si unajua kama TU kuvulia mtu nguo si HESHIMA, mheshimiwa akijuliwa inawezekana ni bomba la mvuaji mpaka kondomu za tendo katikati ya tendo?

  • Unafikiri usingekuwa umekuja kiwanjani na fikira MHESHIMIWA anaheshimika, ungekumbuka MHESHIMIWA ni MHESHIMIWA?

  • SI unakumbuka udhaniaye hana HESHIMA kuna kitu anakiheshimu kweli na labda wala HICHO PIA pamoja na yote , BADO NACHO sio PILIPILI kichaa?

NIMEACHA WAZO Mheshimiwa!
Kumbuka kuchekelea KANYAU HAPA ni RUKSA ikibidi!

Hebu basi ETANA atupe busara katika kitu- Wrong ADDRESS


AU tu Tracy CHAPMAN atupe kitu-New Beginning






Nipo! Ingawa LABDA ngojea niombe msamaha kwa WOTE niliowatenga CHOBISI hivi karibuni:-(
....Ni kweli nipo kama tu picha zisizo na sababu muhimu ya kuwekwa hapa kijiweni zikodoleavyo maning'ining'i..


Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket










Au tu ngojea Gloria Estefan na CELINE DION wakune kipele kwa pambio iitwayo-Conga

Au tuovadozi tu kwa Gloria Estefan akiongezea kidonge-Rhythm is gonna GET U

Read more...

TOKEA tanzania IZALIWE unafikiri IMEBALEHE au KUVUNJA UNGO?

>> Saturday, October 24, 2009

[Tahadhari: Mahubiri ya leo yanatumia lugha chafu kwa watu fulani!:-(]




Leo navyoongea hapa , ....
......U.S.A imeonya WAMAREKANI wote kujiadhari na Tanzania hasa Zanzibar kwa kuwa wanatarajia kutakuwa na VURUGU tokea usajili tu wa wapiga kura KUHUSU UCHAGUZI UJAO ulivyonasa RATIBA.:-(

[Kama unabisha GOOGLE tu swala hili kwa UNG'ENG'E!]





Sasaaaa , katika kujaribu KUWEKA MAMBO CHANYA kuhusu NCHI YA AMANI niulize;-

  • Kama Tanzania ni BONGE la TOTOZ, hufikiri baada ya miaka yote hii kitabia HILI toto huhisi ndio labda limevunja ungo?

  • Huhisi labda Tanzania kama ni LIVULANA, labda limebalehe hivi karibuni ndio kisa cha mchecheto na kujiingiza kichwakichwa lihisipo tu kuna kiboxi manyoya na titi?


SAMAHANI kwa wazo chafu MUUNGWANA;....
......ILA NAJARIBU KUWA NA WAZO CHANYA KUHUSU NCHI IITWAYO YA AMANI AMBAYO DUNIA IMEANZAKUAMINI AMANI YAKE NI TARARILA TU zaidi ya mtombo ,...
.....lakini labda na wewe unaweza kutonishangaa kama umeshuhudia MICHECHETO ya aliyevunja ungo na KUBALEHE tu!:-(

Na MWENZIO najaribu TU kuamini TANZANIA kama ni DEMU basi ni bonge la TOTOZ halafu bado SHAMBA ndio kisa cha kushabikia Konyagi wakati Gongo ipo!:-(

Na LABDA MWENZIO naamini TANZANIA kama ni DUME kinaweza ZAA HOVYO sasa hivi kwa kuwa bado halijajua hata uzazi wa mpango NI NINI au kwanini linataka mtoto wakati kujaza dunia labda sio mara zote ni UJANJA!:-(


NIMEACHA wazo MKUU na HILI NI WAZO TU MHESHIMIWA na shauri yako kama umelisoma na LIMEKUKWAZA kinamna!:-(
MUNGU IBARIKI TANZANIA!

Hebu tupate SINDIMBA kidogo kutoka kwa First Lady MICHELLE



Au tu MYA na Ciara watukumbushe pambio iitwayo-My Love is Like Whoa


Au tu N.O.R.E watupe pambio izungumziayo-Nothin'



UPDATING HUBIRI
a.k.a Kitu kipya katika kipele / habari BIKIRA:
Dada CHEMI CHE MPONDA anaongelea kilichonipa nyege ya TOPIKI HAPA

Read more...

Katika USHINDANI si unajua ukishindanisha tutampata MPAKA ANYAYE VIZURI?

Haki ya nani katika kila kitu,....
..... ukishindanisha kuna BINGWA!:-(


Cha kukumbuka tu ni kwamba katika kila kishindaniwacho kitu,....
..... kuna watu kwa hilo HAWAKO KATIKA SHINDANO na kwa hilo WAO ni MABINGWA.


Na kwa bahati mbaya KWA vya kila siku vitu,....
..... KILA MTU kuna ashindwavyo kila siku ,....
....na unaweza kusahau hilo kwa kuwa HATA KWA umjuavyo wewe MAHIRI KATIKA kitu KABUMBU kwa kuwa KWAKO YEYE kusakata kabumbu ni MARADONA na kwa KUWA UNAPENDA KABUMBU,.....


.... basi KWA KIRAHISI unawezafikiri labda HUYO mpaka kwa kula ubwabwa msibani, KUKUJIBU MASWALI YAKO YA MUUNGANO WA EAST AFRICA , au tu matatizo yako na HAWALA , anaweza akawa kunakitu anajua kukuzidi, NA yote ni kwa kuwa unaudhaifu wa kufikiri yeye kwa kuwa ukipendacho KABUMBU NI MAHIRI, basi yote atetayo yanabusara na yeye ni BINGWA.:-(

Swali:
  • Kwani hushangai kuna watu waaminio KIKWETE au Obama maswali wajuayo labda ni Profesa Sarungi ndiye mtaalamu?
  • SI unajua profesa wa CHAPATI , biskuti na KEKI vinaweza kumshinda ingawa vyote ni MLO?
  • Si unajua hata katika kushindwa kunaidaiwao wanashindwa vizuri KISTAARABU?
  • Kwani hujawahi kushuhudia ASIYEBINGWA kupenga kamasi?

NIMEACHA WAZO MHESHIMIWA na kumbuka hili ni wazo tu na MIYE sio NYERER!E

Ngojea tupate pambio kutoka kwa Tshala MUANA akiongelea-Banda YANGO



Au tu LOKETO watupe pambio iitwayo-Extra BALL

Read more...

Kuhusu KICHWA cha MATAKO!

Haki ya nani UKIFIKIRIA labda kila kitu,....
...kina SHINA, mzizi na sio KICHWA tu!:-(

Na ni kweli watu,...
.... wengi , huoanisha KICHWA na kijulikanacho ni kichwa ingawa MTU KIBAO huelewa ukiongelea YA YALIYOMKUTA aliyepata mimba kwa kuingizwa kichwa tu!:-(


Na labda UKIPENDA , kichwa WAWEZA KUKIELEWA KAMA ni bomba la pua katika ya mtu,...
....hasa kama CHA MSINGI ni kunusa katika HILI na umuhimu wa anusacho MTU unahitajika katika HILI , na katika hili na lile HILI halikwepeki na KWA HILO limekuwa KICHWA tu!:-(

Na wakati sasa hivi unajiandaa kutonielewa kinamna tu,...
...Kumbuka PAMOJA na yote AMBAYO BADO unadhani HAYANA KICHWA HAPA , chakushangaza labda bado nikikuuliza kwanini unasoma TARALILA HII , Bulicheka naye hawezi kushtuka UKIJIBU kuwa kilichokuvutia kusoma hii NANIHINO nacho kinaitwa ni CHA HABARI kichwa tu!:-(

Swali:

  • Si unakumbuka MHESHIMIWA asingekuwa anafikiria MATAKO ni nyezo wakaliazo watu HUGUNDUA maana ya MATAKO kwa KISWAHILI ni MAHITAJI?
  • Unauhakika unajua nini ni KICHWA kama HABARI, mtu, KISIMI na mwenye akili tani kadhaa vyote unaelewa ikiongelewa vyao VICHWA?
  • Kwa hiyo bado unanibishia Tako , HABARI, kikojoleo, UJINGA kwa kuwa vyote kwa staili tu ya kuvielewa ni ndugu kwa kuwa kwa vyote ukitaka kuelewa kinamna vina VICHWA?

NIMEACHA wazo MKURUGENZI na kama itakufurahisha unaruhusiwa tu KUKASIRIKA!!

Hebu tufuate ushauri wa DAKITARI na kupata dozi tatu za kurudisha ustaarabu kijiweni hapa kutoka kwa TP OK JAZZ.....

Dozi #1.Tress Impoli




Dozi #2. Maya


Dozi #3.Makambo eza minene

Read more...

Kunauwezekano sababu kubwa ya kufuata KIONGOZI ni uvivu na ukosaji wa UBUNIFU wa MUELEKEO tofauti!:-(

>> Friday, October 23, 2009

Ndio,...
.... kuna mambo ni TAKO na sio KICHWA ndio kiongozi!
Swali:
  • Si unajua kuna mambo huhitaji tako ingawa una kichwa?
  • Kwani unafikiri kiongozi ni yule aliyetangulia?
  • Kwani hujastukia kuna vitu wewe ndiye mahiri na unajua hilo lakini wote tunajua sio wewe kwenye hilo ndiye atuongozaye kwa sababu bulicheka?
  • Lakini si unajua pamoja na yote kuna kitu utake usitake kwa watu fulani wewe ndiye KIONGOZI?
NI WAZO tu hili KIJEBA na wala usitishike USIPOELEWA!
IJUMAA na WIKIENDI NJEMA Mheshimiwa!

Hebu DOGO aonyeshe maringo yake dingilidingili mpaka chini kiduchu...


Au ngojea Dre na Snoop DOGG watupe tena pambio zilipendwa iitwayo -Still Dre



Au tu Usher atuimbie naye tena pambio zilipendwa-Pop ya Collar

Read more...

Midadi na MDADI, na MIDADI ya mdadi!

[Tahadhari: Taralila hii sina uhakika na maudhui yake kama yanakufaa!:-(]


Ukiwa na MIDADI ,...
.....unaweza mpaka kupiga teke mtu kisa kwa kuangalia mpira tu kupiga kona unaigilizia.

Na ukijua akuvutiaye kapandwa MDADI,....
.... nawe unaweza jikuta unapandisha MDADI kwa kuwa tu mwingine anamdadi na umestukia.

Na kama tunajua UNAMIDADI ,....
.....tutaogopa kuangalia NDONDI kwenye kideo nawe usije nawe ukarusha ngumi kwa kuigilizia.
Cha kusikitisha ni kwamba kama umepandwa na MDADI,....
... yawezabakia kuwa ni siri yako ukifanya siri na mpaka KIPENDA ROHO wako mwenye tibabu USIPOANGALIA naye anaweza kutostukia.:-(

Swali:
  • Hujastukia watu wana MIDADI ya MDADI na ukianzisha hata staili ya KUPENDA kama tu ukianzisha kwenda chooni tu pembeni ya barabara BASI likisimama kuna watakao jisikia pia kwenda haja ndogo kichakani kwa kuigilizia?
  • Unauhakika MDADI WAKO sio midadi tu?
NIMEACHA na kumbuka hili ni wazo tu na wala hii sio BIBLIA au KAMASUTRA!:-(



Samahani nafuata ushauri wa daktari wa leo WA kupata dozi tatu za Barrington Levy

Dozi #1.Dont throw it all away


Dozi #2.Too Experienced



Dozi #3. She is Mine





Kamusi kiduchu ya kijiwe ya lugha banangenge kama ilivyotumika:
MIDADI= mwenye mdadi kwa kutazama kitendo kifanywacho na mwingine anaigilizia bila kujijua.

MDADI=hamu mchecheto, nyege baruti, au hamu tu maridhawa.

Read more...

USHACHUNGUZA hasara za KUACHA UJINGA?

>> Thursday, October 22, 2009

Kumbuka,....

..... kuna pande tatu katika SHILINGI ndio maana unaweza UKAISIMAMISHA ikasimama ingawa pande moja huwa haizungumziwi kwa kuwa eti TU haina PICHA!:-(


Swali:
  • Lakini unafuraha kwa kujua au unafarijika TU na shughuli nzima ya kutaka kujua utakacho kujua?

NI HILO TU!
Ngojea lakini BLACK UHURU waongelee wahitajicho tu ni -Happiness


Au tudeku tu sura kadhaa za huzuni za Mtakatifu Simon Kitururu majuzi ya jana....


Photobucket




Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket

Read more...

Hasa kabla hujachunguza KAZI ya KIDAKA TONGE!

Kwa kuwa tunajua kwa kupiga MSWAKI kuna kitu UNAJUA ndio MAANA unashughulikia MENO na ULIMI kwa kuwa umestukia umuhimu wake kwenye KUGIDA mlo,...

... basi labda katika KUGIDA inabidi TUASHUMU a.k.a tuhisi unajua si muhimu sana kama tayari unajua utakacho kukila sio sumu KUKILAMBA.:-(
Swali:
  • AU?

Lakini kumbuka kama kwako ni muhimu kugida MLO,...
..... janja ya mdomo si kulainisha tu MGIDO ,bali pia NA kulengesha chakula tumboni na hapo ndio utastukia kuna MGAMBO kidaka tonge kama hutaki KUPALIWA a.k.a KUKOLISWA (kwa kilugha), kama umezidisha bugio zaidi katika shughuli ZA baada ya KULAMBA.

Swali:
  • Kwani hujastukia mara kibao janja ya MENEJA yaweza kuwa ni sekretari NA mesenja?
  • AU?
  • Wakati unafanya shopingi za mdomo ushawahi kufikiria yafanywayo na mdomo engi yanakihusu pia KIDAKA TONGE?
  • Hivi unakijua kidaka tonge ni NINI?

NI WAZO tu Mheshimiwa na labda ujumbe wake SAIZI KIPELE, kwa hiyo usitishike sana USIPOELEWA namaanisha nini HAPA katika hii DOZI!

Hebu Barrington Levy atupe kitu-Vice VERSA LOVE


Au tu Vybz Kartel aongelee tu -LOVE

Read more...

A Taste of TANZANIA!

Taro – Magimbi



I do feel very sad these days when I visit home (Dar Es Salaam). Because I have noticed that some of our staple foods are disappearing from the market. I do not see Taro (magimbi) in vegetable and food stands anymore,.....

....tekenya HAPA .....
........uendeleze kunogesha GIMBI.






KACHUMBARI



This is the one salad most Tanzanian kids know and love.Traditionally, raw cabbage is used for this dish. However, I prefer to first slightly fry the cabbage in a little extra virgin olive oil before using it in the.......

Kuendelea kunonesha KACHUMBARI tekenya HAPA





HAPA kwa,.....
....... DADA MIRIAM .....
...MIMI pananifundisha kweli kunogesha MSOSI






Dada Miriam Rose

















Au ngojea tuache swala la MSOSI ili tubadili nchi ili LETTA MBULU atupe kitu....
-NOT YET Uhuru


AU LETTA MBULU akiwa na CAIPHUS SEMENYA aongelee-NOMALIZO


Au tu tena LETTA MBULU ili niache atupe tu ile kitu-KILIMANJARO


SAMAHANI wana NDOMBOLO ,Mdumange, SEBENE , Mugongomugongo,Mdundiko, BUKUTA JUU, SENDEMA,Emba la SASA, TAKO Mchilili, CHAKACHA, Lubogobogo, BONGO FLEVA, .....nk.

........SAMAHANI hii ilikuwa zamu ya Mwanamama LETTA MBULU kijiweni kimiziki!

Read more...

Tatizo la BINADAMU liko katika wake UBINADAMU!

>> Wednesday, October 21, 2009

Na BADO kuna uwezekano SULUHISHO la MENGI matatizo ya KIBINADAMU,....
.... liko katika jinsi TU alifikiriavyo tatizo BINADAMU!:-(

Swali:
  • Si unakumbuka tatizo la HAUNA hutokana tu na kwa kuwa unafikiri UNATAKA?
  • Si unajua kama ishu ni WALI,kwanza kabisa MCHELE WENYEWE hutafunika mbichi na pia SUKARI na CHUMVI vyote ni viungo vya wali kutokana na afikiriavyo mwenye MCHELE?

  • SI unakumbuka ukijinyima NYAMA makusudi unaweza mpaka kufarijika kwa kujiita VEJETERIANI?

NI wazo tu HILI MHESHIMIWA na unaweza tu kuendeleza kula UGALI WA MUHOGO tu kwenye sikukuu kama hushibishwi na WALI!

Hebu Mwanadada AYO adai -Help is Coming


Au tu Mwanadada huyu huyu AYO adai-ONLY YOU

Read more...

Kwa kuwa bado Bin-ADAMU anastukia nani dumeJIKE !

Kwa kuwa tabia ni TABIA ,...
.... basi ni kweli tabia zenyewe hazina UUME au UKE!

Na ni tafsiri tu za tabia,...
..... zifanyazo watu wafikiri ni za KIUME au KIKE.


Mazoea mwanaharamu kweli kwenye tabia,....
.... ndio maana dume zima likitingisha kalio katika kutembea, ingawa mwendo hauna jinsia kuna watakaoapia lina mwendo wa KIKE.

Na mpaka shughuli tu zenyewe na si tabia,....
...... kuna wamuonao mwanamke hafai kuzifanya kwa kudai sio za KIKE.


Na kuhusu shughuli na tabia,...

....kirahisi wawezakuta ni RUKSA katika jamii fulani mwanamke kuwa NGANGARI shambani na nyumbani(hasa kwa watoto) na aonekane bonge la MAMA WATOTO , lakini mwanamke NGANGARI ofisini kirahisi aonekana analeta kibezi cha kiume na si mahali pake kwa kuwa yeye MAWANAMKE.:-(

Ngojea nilikatishe denge wazo:

Nacho jaribu kukokotoa hapa ni kuwa , kama jamii inastukia dumeJIKE,....
.... basi jamii inamtazamo wa KATIKA JINSIA nini ni SAWA na ni nini si SAWASAWA.

Na kama jamii inamtazamo ni nini cha kiume na nini ni cha KIKE,...
...... ni rahisi kwa jamii kuchanganya ni nini kati ya WANAWAKE na WANAUME ni muhimu kuwa sawa na ni nini ni baraka kuachwa viwe sio SAWASAWA.

Na kama HUJASTUKIA hasa katika maswala ya usawa wa WANAUME na WANAWAKE,....
..... kirahisi kuna watakao kila kitu , NA NAMAAANISHA kila kitu kiwe SAWA.

Na labda wakati unapigania usawa kati ya WANAUME na WANAWAKE,....
....kumbuka tu pia ni BOMBA la aidia kuwa BINADAMU WOTE NI SAWA kama ukikumbuka ukweli pia BINADAMU WOTE NI SAWA lakini SI SAWASAWA.

Swali:
  • Katika kupigania haki za binadamu unafikiri maana yake ni kufuta MWANAUME kuwa MWANAUME na MWANAMKE kuwa MWANAMKE?
  • Labda ni haki yako DUME zima kutaka nawe uwe na bonge la TITI, lakini bado si kuna starehe wanawake wakiwa na tabia za kike na wanaume wakiwa na tabia za kiume?
  • Umeshastukia dunia inaingia katika kipindi ambacho kirahisi unaweza usistukie ni nini tabia za KIUME au ni zipi zile za KIKE?

AU ngojea niseme:

NAKUWE na HAKI za binadamu kwa wote,.....
...... lakini tusichanganye kuwa hata kibaolojia MWANAUME ana uume na MWANAMKE ana UKE kwa hiyo KIUBINADAMU TUKO SAWA lakini vile vile hatuko SAWASAWA ambacho sio lazima kuwa ni TATIZO na kusema ukweli ndicho kiletacho starehe ya UNYUMBA.


Na ni vigumu kila mtu kujaribu kuwa yote,....
...... kwa kuwa KILA MTU ana ubingwa eneo lake na ni UTAMBUZI wa HILO ndio uletao ufanisi wa yafanikishwayo na MWANAMKE na MWANAUME wakiwa kwenye UNYUMBA.

NA wakati tunapigania haki za wanaume au wanawake katika yote,....
..... tukumbuke tu kuwa ni haki ya kila mtu kufanya yote awezayo lakini tutii pia kuwa MWANAMKE na MWANAUME tofauti zipo pia na zinajulikana hata KUNYUMBA.

NA tukumbuke tu WAKEREKETWA wa HAKI ZA BINADAMU kuwa si wakati wote,.....
..... ni vibaya kutambua kuna mambo ni WANAWAKE wamebarikiwa zaidi hata kuyastukia na si msuli tu wa kiume wenye suluhisho wa ya KUNYUMBA!

Na kwa kutambua tofauti zipo hata kama si kote,....
.....vita za haki za dume JIKE nazo zaweza eleweka ofisini mpaka KUNYUMBA.
Swali:
  • AU?

DUH NAACHA kwa maana topiki KUBWA na IMENISHINDA!:-(





Hebu Hugh Masekela ABADILI HALI YA HEWA akiwa na Paul Simon waje live


Au tu Miriam Makeba akiwa na Paul Simon waje nao live...

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP