Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama kuna UWEZEKANO wa kujitahidi KUNYA bila KUKUNJA USO!:-(

>> Sunday, May 31, 2009

Kuna mambo UNAJITAHIDI bila kujua!:-(

Na wakati unajitahidi labda UMEKUNYA na kama unajitahidi kunya halafu mavi hayatoki .......OK ngojea nisiendelee na mrengo huu wa fikira.
Swali:

  • AU?


Lakini,...
... WAKATI unajitahidi labda kuna ambaye UNAMCHEKESHA ingawa sio kwa sitaili yako ya kuguna choooni.:-(


Na labda wakati unajitahidi ,....
... LABDA kuna ulikunjialo SURA!

Swali:

  • AU?

NIMEACHA!
Au ngojea MISTA KUUUL a.ka. GREGORY ISAACS ajiongelee katika nanihii iitwayo- -TEACHER's Plight....



Au nikuache tena na baadhi ya picha zangu JUZI ya JANA...

Photobucket




Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket











Photobucket








Photobucket





Photobucket


Photobucket













Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket






Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket





Photobucket



Photobucket


Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket






Photobucket



Photobucket






Photobucket









Photobucket




Photobucket



Photobucket


Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket









Photobucket



Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket

Read more...

JINSI ya kuendelea KUMPENDA MWANAMKE aliyeota NDEVU!

>> Friday, May 29, 2009

Penzi kiboko mpaka unaweza kuanza kulisingizia vitu!

Likinoga unalisingizia mpaka utamu lisionalo , likiingia uchachu mpaka saizi ya chuchu inakuwa ishu.:-(

Na mara nyingi kikuvutiacho kwa mtu sio kidevu ndio maana husiti ukipewa chansi gizani kuendelea kumpapasa umpendaye bila kumuona vizuri .Na ukipapasa labda hubobei kwenye kidevu.

Na haki ya nani tena, wakati unamtumbulia macho mpenzi, kama unampenda bado huoni kila kitu ingawa yuko mbele yako!:-(


Ndio!
Mapenzi sehemu nyingi hufanyika gizani au kwa kuyafumbia macho.
Na kama wewe unaweza kufanyapenzi huku unastukia utandu wa buibui kwenye silingibodi , basi ufanyalo sio penzi.

Narudia!
Mapenzi sehemu nyingi hufanyika gizani ndio maana mara zote UNAHITAJI MWANGA ili umjue MTU kabla HUJAMTEMA a.k.a KUMUACHA SOLEMBA!

Nachojaribu kusema ni; DAIMA PENZI HUNOGA ukiwa GIZANI na ukianza KUJUAJUA SANA kwa kuwa uko MWANGANI , kwa wengi hilo ndio misingi ya mwisho wa PENZI au kutonogewa na penzi kama juzi.
Swali:

  • AU?
Sikatai!
Labda utadai kuwa kwa kumjua sana mpenzi ndio msingi imara wa penzi.
Na labda ni kweli kama unaoanisha tafsiri ya PENZI na KUISHI PAMOJA bila MAKEKE na Limtu.

Ndio !
Nakubali kuwa kuna ukweli kuwa kuna aina nyingi ya mapenzi na labda moja ya tafsiri ya penzi ni hiyo yako na unasaidiwa na kutaka kujua kila kitu au kustukia mpaka NDEVU.

Sikufichi!

Inawezekana DEMU wako ana nywele za kutosha tu kifuani a.k.a LAVU GADENI , na sababu za WEYE kutojua hicho kama ni kweli hujifanyi hujui ni kwa sababu YEYE mwenyewe zinamkwaza kwa hiyo anazinyoa ndio kisa hajastukia mpaka leo mapenzi yako ya nywelenywele hata za kiboxi manyoya.

Swali:

  • Hivi unakumbuka binadamu ana nywele mwili mzima ndio maana limtu lako linatoka jasho mwili mzima na ukilipa chansi lanuka kikwapa?

Turudi kwenye Mwanamke Mwenye ndevu....

Naweza kusema,...
....UKIPENDA umependa na umpendaye akiwa na ndevu hizo ndevu kwako za mpendeza.
Swali:
  • Au?
  • Kwani UTU na UKE kwako havitoshi?

Kumbuka ,..
....KAMA WEWE nimtafutaji wa KASORO kila MTU ANA KASORO ingawa katika kasoro ;NDEVU SI KASORO!


Swali:
  • AU?

NIMEACHA wazo na samahani kama nimekukwaza na kumbuka HILI ni moja tu ya wazo!
Nakutakia WIKIENDI KIBONGE na kama unapumzika nakutakia MAPUMZIKO JEMADARI!


Tupumzike tena kwa kujifunza kunyoa sehemu sehemu kwa msaada wa Gillette..


Au turudi tu South Africa tupate Dikgomo REMIX..

Read more...

Woga wa ukubwa wa NANIHII!

Nasikia kuna waogopao kubwa!

Labda ni kweli KUBWA inatisha ingawa pia kubwa inaweza kupwaya!:-(

Saikoloji ya muogopa makubwa hutegemea kwa muogopaji dogo ni nini.

Ukubwa wa jambo KWAKO unategemea na UBONGO wako ulivyojengeka ili kustukia MADOGO ni nini.
Na kwa kawaida unaujenga mwenyewe UBONGO KUSTUKIA MAMBO ingawa pia MAZINGIRA na JAMII inamsaada mkubwa katika kukuponza kwa hilo.

Na sababu za kuhofia kwa kuwa unahisi ni kubwa basi itauma au kukushinda ni jambo lako ULILOJIFUNZA tu!

Na kumbuka,...
.... chochote ujifunzacho kinafundishika kukiacha.

Swali:

  • Unafikiri wakati umezaliwa ni vingapi vilikuwa vikubwa kwako na hukuviogopa kwa kuwa mtoto mwenye umbo dogo na vimekuzidi kimo?
  • Unafikiri ni kwanini kwa kukua na woga wako wa makubwa umekua?
  • Unafikiri makubwa ni yapi ikiwa ukweli ya yako makubwa kwa mwingine ni madogo?


Na ,...
....tunajifunza ukubwa wa mambo hata kwa kusikiliza tu wadaio yaliwaumiza.

Lakini katika mchezo wakuumiza labda na wewe ni muumizaji ndio maana mara kwa mara kuna mambo unayastukia kabla hujaumizwana sio kwa kuwa ni marudio ya maumivu.

Kumbuka tu,..
... TAFSIRI ya ukubwa wa jambo kwako labda kwa mwingine ndio saizi yake na inatosha kabisaaa!

Kumbuka tu,..
... LABDA ukubwa wa jambo kwa MWIZI ni kichekesho kwa JAMBAZI, ingawa duniani hapa kati ya wezi na majambazi waliotajirika zaidi ni wezi .

Swali:
  • Hujastukia wanasiasa wako uliowapigia kura?

Na USISAHAU,...
.... Udhaniapo ni UDOGO wa jambo ndivyo UMUUAO MWENZIO ambaye kwake SWALA ni kubwa na halina udogo kama tu maumivu USIVYOJUA ukubwa wa maumivu ya mkeo kujifungua au ya mjusi kutoa mimba.

Swali:

  • AU?

NIMEACHA!
Ngojea Rolling Stone wanipe- Satisfaction


Au tu Akon na Michael Jackson warudie-Wanna be Startin' Somethin'

Read more...

Honest scrap award á le Simon.

>> Thursday, May 28, 2009

My friend Serina forced me to do this!:-)















The Catch

You must brag about the award

You must include the name of the blogger who bestowed the award on you and link back to the blogger

You must choose a minimum of seven (7) blogs that you find brilliant in content or design.

Show their names and links and leave a comment informing them that they were prized with Honest Weblog.

List at least ten (10) honest things about yourself. Then pass it on with the instructions



1. Mapishi

I love cooking and I've been cooking for myself since 1996.

Sadly, I have never cooked for my mum yet!:-(
She still prefer doing everything for me her last-born.:-(


2. Mawazoni.

I think too much about everything.

When I am listening to Ur story, there is a possibility I might be paying more attention to the part of the story you don't intend to tell me with Ur story.


3. Anger

I don't easily get angry when provoked simply because I tend to find comedy in the strangest of places.

4. Appearance

Most people I meet are surprised that professionally I do business and I majored in economics since High School. I guess it is because I don't comb my hair which makes people automatically shift to the artistic mode when they see me.


Well, I do art too as a hobby though!
Another thing is, I think my father still struggle to accept my dreadlocks and hasn't forgiven me for not wanting to be a medical doctor because I was very good in science subjects.:-(



5. Wanawake wanaonikuna roho


I have a weakness for smart women.
A stupid lady always succeeds to turn me off!

I am polite and try to learn something through the experience though!


6. Technically I am a Muslim

I was once a Muslim and there those who say once a Muslim always a Muslim until death as there is no way out.

In short;

I was born in a family that attends Lutheran Church although my mum is of Mennonite denomination.

Nilifanikiwa kwenda Sunday School mpaka kupata mademu ndani ya shughuli za kanisa hili la Kilutheri
Well, niliimba kwaya pia sana tu pale Bungo, Morogoro .

I became a born again Christian through Moses Kulola.

Rastafarianism followed through my own curiosity.

Changed to Islam through my own curiosity.

Doubted God through my own curiosity.

Returned to beliving in God without ties to any religion through the same curiosity of mine and thats where I am right now.
Na labda ni kweli Curiosity iliua Paka!:-(


7. Creepy Crawler I hate

Of all the creepy crawlers , I hate scorpions!

I would easily have a sleepless night if U tell me U've seen a scorpion in my room.:-(

Anyway, a glass of Cognac , a shot of Tequila or.. always helps.:-(

8. Relationships

I have problem with love ,and I am not suggesting that I am not loved!:-(
The people who I love always think I take more than I give!:-(

I have been dumped once so far and that is when I was form three in Morogoro Secondary.



9. Uvaaji.
I tend to over -dress most of the time.:-(

10. Weakness for News


I watch news a lot while feeling guilty that I am wasting time because of loads of BS in what is considered news.:-(

11. How I talk

For a lot of people finds me talking very slow and I get teased a lot for that!:-)
.On top of that ....most people who know me find it funny when I rap fast or when I sing with a very low voice that they don't associate with me.:-)
Yes I do play music as a hobby everytime I find time....... and it has been Progressive Rock the style I do often for quite sometime now .

12. Inawezasemekana kuwa Mie Mjinga
I always think I have to improve on what I know!



Serina umefurahi sasa?
Basi ngojea nami niwaonee wengine hawa ambao ni baadhi ya Wanablogu nipitiao kazi zao kwenye zao blogu mara kwa mara, nao ni;

Koero

Edo Ndaki

Markus Mpangala


Digna Abrahamu



Shaban Kaluse

Chib

Muzee wa Taratibu


Aaah! Basi Ngojea tu Marilyn Manson awakwaze watu katika -Beautiful people


Read more...

(Tangazo)ALI KIBA ndani ya L.A hii JUMAMOSI!
















Au jikumbushe wimbo wake wa CINDERELLA

Read more...

LABDA kuhangaikia KUJUA UKWELI hakuna tofauti na kuhangaikia KUJUA KUDANGANYA vizuri!

>> Wednesday, May 27, 2009

Kafuraha kakujiridhisha NDIO CHANZO cha kuhangaikia uridhike!


Si UKWELI ndio ukusababishao utake kujua UKWELI , bali kafuraha KAKURIDHIKA na ahueni ya kuwa sasa unajua ndicho kikuhangaishacho na kukugalagaza utake kujua UKWELI.

Tatizo ni,...
... hata ukitaka kudanganya halafu ukafanikiwa kudanganya vizuri, mwili huachia kemikali a.k.a homoni a.ka kibaruti kile kile kilichokufanya uridhike kwa kujua UKWELI.

Kwa kifupi,..
.. labda KAFURAHA kakusema kweli tu kwa madoido KANA UTAMU sawa na KAFURAHA ukapatako kwa kumwaga bomba la uongo VIZURI!

Swali:

  • Hivi si bado kuna uwezekano KAUKWELI kako bado kana KAUONGO?
Na,...
... LABDA mpe tu shughuli BINADAMU ili umcheleweshe kufikiria ukweli au uongo wa lini ni siku yake ya kufa.

NA labda MTU akiwa bize na maisha , UKWELI hauna tofauti na UONGO katika umuhimu wakufanya wewe kama BINADAMU ustukie unaishi.

Na labda ndio maana,...
.....UONGO na ukweli vina mchezo wakufuatana hata mpaka chooni, ukizingatia vingi wadanganyanavyo watu huambatana na shughuli ziambatanazo na jinsi ya kupata uhakika wa maakuli usaidiao kumpatia mtu choo!:-(


DUH!


Swali:
  • AU?
NIMEACHA na samahani kama unastukia ujinga zaidi ya busara katika hili MHESHIMIWA!

Nakutakia siku Kibonge na mapumziko Bwanyenye!


Au ngojea CHRISETTE MICHELLE akuongelee katika- Love is U..


Au tu BAABA MAAL airudishe AFRICA kwa kibao-Souka Nayo(I will follow U)

Read more...

HONGERA kwa KUKOSEA MWANIWANI!

Labda unalazimishwa ujisikie vibaya UKIKOSEA!:-(

Na ukikosea unajisikia vibaya,...
... wakati UKIPATIA hata ukisifiwa kujisikia vizuri bado HAKUDUMU!

Na kumbuka;...
.. ..kama ulipatia juzi leo ni mpaka ujikumbushe kuhusu juzi ndio kumbukumbu ya ladha na sio ladha halisi ya ulivyopatia ndio hurudi na kukuchekelesha leo.

Na usisahau,..
.... kama ulikosea juzi ni mpaka ujikumbushe ya juzi ndio kukosea kwako juzi kunaweza kukuumiza tena leo.

Kwa hiyo kama ULIPATIA au KUKOSEA JUZI ndio ilitoka hiyo mchezo leo unaanza upya na KUKOSEA au KUPATIA sasa hivi kwenye umuhimu ni utakavyofanya leo.

UKIKOSEA bado watu watajifunza kutokan na makosa na kama unatumia akili usitishike na wababaishwao na KUSIFIA KUPATIA TU.

KUPATIA kwaweza kukawa ni CHANZO CHA UZEMBE hasa kwa vigezo vya kwa kuwa leo UMEPATIA!

KUKOSEA mara zote ni CHANZO CHA MAARIFA hasa kama UNAHIARI ya kujaribu tena hata kama UTAKOSEA TENA!

Swali:

  • Kwani wewe ni mara ngapi huwa unakosea makusudi?



Naweza kusema,..
....KOSEA mwanawani kama nia yako sio KUKOSEA!
Swali:
  • AU?

NIMEACHA na kumbuka MWANIWANI hili ni moja ya WAZO TU!

Ngojea No DOUBT waongelee -Underneath it All


Au tu Gregory Isaacs adai-My Only Lover

Read more...

Swala la busara za KUJIHAMI na MTONGOZO!

Labda,..
... kama unajihami na mtongozo basi weye UNATONGOZEKA!


Lakini,...
...inasemekana KUNA watu inabidi uwakwepe KUWASIKILIZA usipotaka kuwakubalia MTONGOZO!

Kuna watu hata kama hukubaliani nao kisiasa,...
.... ukiwapa muda wa kuwasikiliza unaweza kujikuta unawapigia kura wakati bado hukubaliani na siasa zao.

Kuna njemba mwanadada akijilogo alipe muda limng'ate sikio hukawii kustukia mwanadada anavuta majani kwa kukosa tikitaka ya maneno ya kukataa zaidi yakutoka mbio a.k.a baruti!

Nachojaribu kusema ni kuwa kuna watu unaudhaifu nao na ushakaa mkao wa kukubali na kikusitishasho ni woga wa kuwa ni dhambi, itauma, watu wengine watasemaje kama ukikubali kula bata wakati kwenu chakula ni nguruwe.

Nachojaribu kusema,..
... LABDA sio ukali wa kauli ya mtongozaji ikufanyayo upende CCM, bali ni mkao wako wa kuzimia CCM ndio usababishao hustukii hoja za Mchungji MTIKILA kama zina kuna KIPELE!


Na ukimkalia mkao wa kumkubali Mwanadada,...
... hata akibinya chunusi inavutia na kukutia mshawasha.

Swali:

  • AU?

Sikatai lakini kuwa kuna watoaji Mtongozo kama akina Nyerere ambao wakikukalisha chini na kukuambia a.k.a kukupiga siasa kuhusu UMUHIMU wa chama kimoja utakubali, na wakidai vyama vingi bomba unakubali na wakikaa kimya bila kukujibu unajazia mwenyewe wanafikiria nini hata kama hawafikirii kitu na fikira zimekwama!:-(

Narudia ,...
... LABDA ukijihami na mtongozo basi weye unatongozeka!

Na atongozekaye kunauwezekano alikaa mkao wa kutongozwa na atongozaye!


Swali:
  • AU?
NIMEACHA!

Ngojea Papa Wemba alete za-Ye TE OH


Au to tujikumbushe Geto BOYS waongelee - 6 feet Deep

Read more...

Kuhusu ule UHAKIKA wa HATA kumpa MIMBA mtu KESHO!

>> Tuesday, May 26, 2009

Uhakika wa ya vitendo vya binadamu LABDA ni kama wa mbegu za kiume mamilioni zipiganiazo yai moja la kike wakati mmoja na kwenye shahawa zenye mbegu mabilioni ,mbegu mshindi kwa kawaida ni moja.


Chakutia moyo ni kwamba,...
..... katika mbegu mamilioni moja ikifanyakazi yake binadamu tutasahau uzembe na bahati mbaya za mamilioni ya mbegu kwa sababu mbegu moja imehakikishia uhakika!


Chakutisha ni kwamba,...
..... mamilioni husahaulika kwa sababu tu ya vurugu ya moja na kama hilo moja lina pua kubwa kuliko sura ndio imetoka hiyo kwa UHAKIKA.

CHA KUTISHA ni kwamba,...
.... hata sasa hivi unavyonisoma , kunashughuli mamilioni lakini kuwa kwenye internet ndio iliowini na shughuli ya kwenda kumvizia SISTA wa KIKATOLIKI umgeuze awe mke wako kwa sasa hivi labda ndio imetoka hiyo kama hayuko mtandaoni , e-mail hana na gia za kumuingilia bado hazijaandikwa mtandaoni.:-(

DUH hivi nilikuwa natakakuongelea nini vile?

Ok turudi kwenye swala la UHAKIKA KESHO!

Na KUHUSU KESHO,..
...sina UHAKIKA!:-(

Uhakika wakumalizia leo yenyewe SINA UHAKIKA, ingawa ni mwepesi kudhania mipango ya kesho nimeimaliza.

Na KUHUSU MIPANGO YAKESHO,...
...sina UHAKIKA,...
.....Ingawa nasifiwa kwa hata mipango ya kesho kutwa kwa jinsi nilivyoipangia ratiba na kuisimulia kwa UHAKIKA!:-(

CHA ajabu NAANZA kuwa na wasiwasi na hili neno UHAKIKA kuwa labda lina kasoro kama likitumiwa na BIN-ADAMU kudai anauhakika!:-(

Swali:

  • Inawezekanaje Mtu akawa ni binadamu halafu anauhakika?
Sikubishii!

Labda,...
... unauhakika na hata wakwenda Mbinguni ingawa hupajui mbinguni ingawa hata kwa kulia utashuhudia kwetu siye walokole kuwa UNAUHAKIKA!

Na labda ni kweli ,....
.... ninauhakika sitakupa MIMBA, kwanza sikujui halafu labda weye TASA kama tu WEYE ulivyokuwa na uhakika kuwa sasa hivi hujabanwa mkojo!

Halafu HAPA labda wote tutabishania ni nini unauhakika na kipi unadhani kila mtu inahitajika awe anauhakika na lazima kuna uhakika , lakini MUHIMU KULIKO VYOTE;....
  • Unauhakika wewe ni kweli ni wewe na sio akili zako zinakuchezea akili na ukweli labda wewe ni yule?

Narudia;..
  • Unauhakika wewe ni wewe ?
  • Unauhakika wewe ni nini?
NIMEACHA wazo Kingunge na kumbuka ni moja ya wazo tu USIZINGUKE!
Nakutakia siku KIBONGE Mkurugenzi ndani ya lako LIBENEKE!

Ngojea Sade abadili hali ya hewa...-King of Sorrow..




AU tu Sade arudishe tena -Smooth Operator..

Read more...

Hamu ya KURUDIA kuonja!

Labda kama ungekuwa na uhakika na kitu usingehitaji KUKIONJA!

Kuonja maana yake huna uhakika.

Na ukirudia kuonja kuna uwezekano unaonja tena tu INGAWA unajua tayari kuwa NI TAMU!

Lakini,..
... madhumuni ya kuonja labda ni kujua ina UCHUNGU gani!

Cha kusikitisha ni kwamba ,...
.... TAMU YA JANA , leo inaweza kuwa ni CHUNGU!

Na nyege zako za kuonja jana zinaweza kuwa zilisababisha isiyo tamu ikaonjeka TAMU SANA!:-(


Swali:

  • Ushawahi kutofautisha utamu wa ukoko ukiwa na njaa ulivyotofauti na utamu wa ukoko wakati umeshiba?
  • Unauhakika ungekuwa na uhakika ungeonja badala ya kuila tu a.k.a KUBUGIA?
Ni wazo tu Mkurugenzi USITISHIKE na NIMEACHA!

Ngojea Makassy arudie ya -Mke WANGU

Read more...

Kama kuna KISASI, labda KISASI cha KUKU angetaga mayayi VIZA!

NDIO,....
..... labda unafikiri UMEMKOMESHA!

Swali:

  • Hivi utamu wa kisasi unadumu dakika ngapi?

NDIO,...
.....alikufanyia, na unafikiri roho haitatulia usipo mparura na utafaidi ukimfanyizia!
Swali:
  • Hivi tukibadili jina la KISASI na kuliita URODA ukimfanyia kama alivyokufanyia hivi nyie hamtazalisha MTOTO MAUMIVU ambaye atakuwa nimaumivu yenu wote wawili ?

NI kweli,..
....KISASI kwake ni KISASI kwako!

Na hata ukibisha ,...
... inasemekana kisasi kizuri ni KUSAMEHE!
Swali:
  • Unafikiri unaweza kujilazimisha kusamehe?
  • Unafikiri utamu wa kisasi ni nini?

Na,..
...kusamehe ni sanaa,kusamehe ni taaluma na kila mtu ni bingwa katika hii fani ingekuwa hatuchagui ni nini cha kusamehe!

NDIO,....
.....NAAMINI Bin-adamu huchagua vya kusamehe na mara nyingi hudai hawajasamehe leo baadhi ya vitu ambavyo walivisamehe tokea mwaka juzi ila hawajastukia tu kuwa walisamehe kwa kujiamisisha kuwa mpaka leo vina leta MAANA.


UKINIULIZA mimi ntakuambia KISASI NI UGONJWA WA AKILI na kama unabisha, hebu tazama kuanzia mkao wa alipizaye KIASASI hata kabla ya kushuhudia VITENDO vya alipizaye KISASI!:-(

Ni wazo TU Kingunge na kuna uwezekano nakudanganya!
KASIRIKA basi na tunza kisasi kama unadhani inalipa!:-(

NIMEACHA wazo KINGUNGE!

Ngojea Ali Kiba adai tena- NICHUM

Read more...

BINADAMU ananuka!(wazo lililopinda)

Bin- ADAMU hata baada ya kumaliza kuoga,...
..... huwa bado ANANUKA!

Kama unabisha muulize MBWA anamtambuaje mmiliki wake hata asiye na bahati ya kunuka kikwapa!


Na Bin-ADAMU akishakufa ,...
.... ndio huacha KUNUKA kama unaamini akigeuka udongo huacha KUNUKA!

TUKIACHANA NA HILO,...

....ni kweli ,...
....DUNIA INANUKA!

Kama hujastukia labda ni kwa sababu umeizoea ndio maana hushangai kwanini mtoto akizaliwa na kunusa dunia cha kwanza AKIPUMUA ni kulia!

Na labda moja ya visababishavyo DUNIA KUNUKA ni BINADAMU KUNUKA na uozo wa miili ya binadamu kabla haijaacha kunuka!

Swali:
  • AU?
  • Baada ya kunisoma BADO unauhakika umewahi kukutana na binadamu anayenukia na asiyenuka?

Ni wazo tu Kingunge, USITISHIKE!

Ngojea BEN WESTBEECH aongelee kuhusu kesho katika- So Good Today

Read more...

Kuwa MAARUFU watu wakustukie kama vile GHAFLA umekuwa GENIUS wa kila kitu /Una MIAKILI Kibao na MAJIBU BWELELE !

>> Thursday, May 21, 2009

Sikutanii,...
... hata kama ukipata umaarufu kwa kukaa uchi, GHAFLA mpaka hata maswala ya kilimo kuna watu wataanza kukuuliza wewe ushauri na sio BIBI KILIMO!:-(


Utashangaa nakwambia kuwa mpaka hata apataye UMAARUFU kwa kucheza FUTIBOLI a.k.a KABUMBU , kwa washabiki wake , yeye kafuzu na anafaa UBUNGE hata wa BIHARAMULO na kwao mpaka maswala ya KEMISTRI yeye Profesa.

(Ok, labda katika Uprofesa wa Kemistri hapo nimezidisha.)

Na ajulikanaye GHAFLA kwa sababu WAZAZI wake walikuwa wanajulikana KABLA, ndio kabisa kwa umaarufu wa ghafla leo , AKITAKA URAIS kuna watakaodai ANAKWALIFAI.

Swali:
  • Kwani wewe pia sio msikilizaji wa watu maarufu kuliko wale wajuao siri ya kitu umuulizacho maarufu?


Haki ya nani tena,...
... baadhi ya binadamu kwa kuzimia watu maarufu hawakawii kutosita hata kuwagawia sehemu zao za faragha a.k.a PIPI na wakataka mpaka kukushawishi na wewe uamini kuwa Lijamaa Maarufu wanauhakika likijamba hakitoi harufu! ( samahani kwa matumizi ya lugha ya faragha)


SIKATAI lakini,...
.... maarufu mjinga LABDA hujulikana na kumuuliza maswali kabla ya kumzoea ni bomba KWA SABABU ni BOMBA la staili nzuri ya KUJIGONGA kwake!

Tatizo ni pale kujigonga kukizidi na pamoja na kumgawia sehemu zako za faragha unaanza kuamini kuwa anafaa kukuongoza kama KAtibu KATA.
Halafu eti mara ghafla eti nalo LIMAARUFU linaanza kupandisha nyege MPAKA za Ubunge na hata Urais!:-(



Swali:
  • Au?
NIMEACHA wazo!
Nakutakia siku KIBONGE Kingunge na TUTAFIKA TU!


Ngojea Sammy Davis Jr amzungumzie- Mr Bojangles


Au tu Miles Davis azungumzie - Human Nature

Read more...

POPOBAWA, Kidudumtu, CHINJACHINJA, Ndondocha,... yote ndani ya STORI!

Hata kama ingekuwa ni YESU ndani ya stori, umuhimu wa stori bado ni imgusavyo mtu tu hiyo stori!

Na hata kama stori yako ni tamu namna gani lakini HAITEKENYI HALELUYA a.k.a kipengele muhimu, hiyo stori kwetu si muhimu ingawa ipo HATUKUBISHII!

Na kama ukikutana na bingwa wakutoa stori,...
... stori hata ya MENDE MJAMZITO ndio stori utakayodhani ni baba la stori.

Na aihitajiki stori iwe inahusu Mungu ili utishike,....
.. ukikaa mkao wa kutishwa stori ya viroboto inatosha kukufanya ughairi kufanya uasherati a.k.a ngono a.k.a uroda a.k.a KULA N'GE angalau kwa leo kama tu ya MUNGU, kama akushushiaye stori ya viroboto anaweza kuioanisha vizuri na wako mshawasha.

Ni kweli ,...
... ukikaa mkao wakutishwa SISIMIZI ni SIMBA!

Swali:

  • Ushawahi kustukia STORI ZOTE HUFUNDISHA na inategemea tu UNATAKA KUJIFUNZA NINI?


Hebu turudishe manyanga kwa POPO BAWA kiduchu;....
.... kwani hukustukia kilichokuwa kinatisha watu katika stori za popobawa ilikuwa sio POPOBAWA bali hofu ya kulawitiwa?

Mie mvivu kwa hiyo jazia mwenyewe kuhusu KIDUDU MTU , Chinjachinja, Ndondocha au tu demu umpendaye kwanini kuna stori anakutisha!:-(


Kumbuka tu,...
... ukitaka kujifunza, hata sentensi moja na wala sio stori nzima huhitajika ili ujifunze.

Na mara nyingi stori au hata kijitabu kimoja kinawadakisha watu UJUMBE TOFAUTI na pia huwafundisha watu mambo tofauti.
Swali:
  • Kwani hujawahi kukutana na mjanja atumiaye BIBLE au KORANI kutongozea ?

  • Kwani hujifunzi kwa kustukia stori ulioifuatilia kama hii ya POPOBAWA labda haina funzo ukitaka na wala haimhusu POPOBAWA?

NIMEACHA!
Kumbuka ni moja ya wazo tu KINGUNGE!


Au ngojea Clouds Production( Sindila , Njaidi, Kolumba , Pamela, Dj Bonnie Luv na Steve kwenye Keyboard.) enzi hizo Bongo Fleva inapewa mimba 1992 wazungumzie - MSELA

Au tu ngojea NURU the LIGHT amsifie tena- MSELA..

Read more...

Ukiamini, ''UONGO huwa ni UKWELI!'':-(

Kama unaamini,...
.... kwako hilo uaminio ni UKWELI.

Halafu ETI labda unashangaa kwa nini binadamu wanauana,...
... wakati kila kona a.k.a chobisi uipigiayo chabo, KILA MTU ana KWELI YAKE .

Na ukikutana na aaminiye kweli yake ukakosea staili ya kumstua ajuacho si kweli,...
... anaweza kukurukia kichwa, kabla haja kukaba roba, huku akikupiga ngwala halafu ni mpaka baadaye akienda kuoga ndio atastukia naye kachubuka halafu chakusikitisha pamoja na yote hatastukia ''UKWELI YAKE bado ni UONGO!'':-(

Swali:

  • Unauhakika KWELI yako sio UONGO?

Inasemekana na huu asemao JF Kennedy na.... ni Ukweli...



Na inasemekana asemacho I Jahman Levi nacho kwa watu fulani ni kweli katika- I want to be Free...


Au tu mwanadada kwa jina Truth Hurts ft Rakim aondelee kunasa labda nao ni kweli katika -Addictive

Read more...

NYUMBA hii inalindwa na MBWA KOKO!

>> Wednesday, May 20, 2009

Kama unafuga mbwa BONGO, ni kawaida KUMSINGIZIA kuwa ni MKALI.

Hukawii kukuta mpaka NYUMBANI kwa kijeba mpaka na kibao wamekuandikia;''JIHADHARI MBWA MKALI!'' kama vile ni kweli mwizi atumiaye akili ni tatizo mbwa mkali.

Lakini kama tu WAZAZI wa Libinadamu wadhaniavyo kuwa watoto wao ni spesho kuliko mtoto wa jirani, labda mbwa wa kwenye tangazo mbwa mkali ni mbwa koko na akibweka ni katika kujihami kwake tu na mapopo.

Swali:

  • Hivi bado hujawahi kufikiria kuwa labda kama Tanzania inalindwa na mbwa basi huyo mbwa ni KOKO?
Kumbuka lakini kwa wajanja nchi za magharibi jibwa koko kuwanalo ndio ujanja!

Na haki yanani tena utakuta Profesa wa lilesomo unaloamini linahitaji akili za hali ya juu ndio yuko bize anaongea na jibwa lake na anaamini linamuelewa kuliko binadamu na urafiki na bin-adamu haupi tena kipaumbele ukizingatiwa dogi linahitaji KWALITI TAIMU na usisahau linahitaji kwenda kutembezwa ili liende haja kubwa na lazima likijisaidia uzoe kinyesi.

Kumbuka tu tamaduni na mazoea ndio vyaweza vikawa vinasababisha hustukii mbwa koko ni koko .:-(

Na kama wewe ni miongoni mwa waogopa mbwa, LABDA mbwa koko ni MKALI!

NIMEACHA wazo!
Siku Njema!


Ngojea Tracy Chapman adai- Give me one reason



Au tu Lenny Kravitz adai-I belong to U

Read more...

UKIJUACHO ni kama tu jinsi ya kwenda haja ndogo, kama unakijua vyakutosha ULISHAACHA KUKIFIKIRIA wakati UNAKITENDA hicho!:-(

>> Tuesday, May 19, 2009

Kama kuna kitu unakijua, basi hicho kilishaacha kukuumiza kichwa!



Na labda,...
... kama kuna unachokifikiria, KUNA UWEZEKANO hukijui bado hicho!


Na kama unafikiri unakijua kitu,...
... lakini bado kinakufikirisha, LABDA labda kunamapungufu ya ukijuavyo au kinakasoro hicho .

Na kasoro ya udhaniacho unakijua inaweza kuwa ni mtazamo wako wa kudhani unakijua:-(


Na unachokijua unaweza kusahau kipo,...
... kwa kuwa hukifikirii tena hicho.

Na hata kama ukifikiriacho ni MUNGU,...
... kuna uwezekano unafikiria ya MUNGU kwa kuwa kuna kitu kuhusu MUNGU hujui bado hicho.

Na ungemjua MUNGU,labda SHETANI na vya shetani yasingevutia na kukudaka hivyo!:-(

Swali:

  • Unafikiri kuna mtu hapa duniani unauhakika anakujua?

  • Unauhakika hakuna limtu nyumba ya jirani zuuriii NA kwa kuwa unalijua unasahau kulistukia kuwa ni zuri na linafaa kwa matumizi yako ya kuumiza mtu roho?

Unaweza kunibishia,.....
.... LAKINI ni kweli mambo yako unayoyajua kama vile kutawaza, huwa unafanya bila kuyafikiria .

Na unachokifikiria, bado hujakimasta ndio maana kunasiku unajistukia mnyonge na katika kujaribu kusawazisha unyonge kuna WATUTISHAO na watakavyotudhaniye wanajua na katika prosesi wanatuboa.

Swali:
  • Au?
  • Unauhakika kwanini unafikiri unajua wakati wadaio kujua hata kufinyanga tonge la ugali kunasiku hudondosha tonge?

NIMEACHA!
Kumbuka ni moja tu ya mtazamo na wazo Kingunge , usitishike!
Ngojea Marvin Gaye abadili hali ya hewa kwa kibao - Lets get it on



Au tu aendeleze simulizi za uasherati katika- Sexual Healing

Read more...

KWA wanaojisahau na SIRI na kuendelea kuishi wakitunza SIRI ZILIZOEXIPAYA!:-(

Mara nyingi ni ghali kutunza siri yako hasa kwa kuwa asilimia kubwa za siri za watu zitunzwazo zilishaexipaya longitaimu!:-(

Na kwa kuwa wote tunajua jinsi gani watu ni wasahaulifu, labda siri yako isingekuwa wewe binafsi unaiendekeza iendelee kuwa siri , siye wengine tungelishasahau uhusiano wako na hiyo yako siri.

Siri kiboko!

Inaweza ikasababisha unogewe na hata visivyovitamu kwa kuwa tu unavilia migombani kisiri na kama ungetandikiwa mkeka ungelistukia zamani unogewavyonavyo vimechacha kwa mbaali na vinanuka kwa kuwa si siri kuwa ni kweli vinakosewa kuoshwa.


Na,...
.... umuhimu wa siri mara nyingi unazidishiwa sifa zaidi kuliko unavyostahili.
Matokeo yako unaweza kunogewa na kutunza siri huku kumbe kama tungeijua hiyo siri wala tusingeioanisha na huo udhaniao ni umuhimu.


Swali:

  • Unauhakika siri zako bado hazijaexipaya na unaendelea kuzitunza kwa mazoea tu?
  • Hivi weye sio miongoni mwa wadaio kwa kuwa siri yako anajua mtu mmoja tu a.k.a rafiki mpendwa, basi hiyo unadhani bado ni siri?

Kumbuka, kutunza siri ghali kinoma!

Inashangaza lakini kwa jinsi watu wasivyostukia ughali wa kutunza siri ingawa hao hao ni mabingwa wa kunyemelea vitu vya chee!:-(

Kumbuka kama siri yako ni kuwa unamakengeza, kama nakupenda basi wewe kwangu KAMWE HAUNA MAKENGEZA na ukiniuliza ntakuhakikishia kuwa hayo ni macho malegevu na kwa kurembua katika mahaba hauwezekani.

Swali:
  • AU?
  • BADO unauhakika na umuhimu wa siri yako?

NIMEACHA na kumbuka ni moja ya wazo tu Kingunge!
Nakutakia siku KIBONGE na kila la kheri kwa kupafekti sanaa ya kuficha siri!

BAADAYE basi KINGUNGE!

Ngojea tu Lupe FIASCO amkaribishe mtu katika - Welcome Back Chilly



Au tu Ricky James azungumzie -COLD BLOODED

Read more...

Ndani ya shule ijulikanayo kwa jina; BAA!

>> Monday, May 18, 2009

Unaweza kukataa,....
.... lakini baa ni shule.


Pamoja na BAA kulalamikiwa,....
..... ukitaka naweza kukuhakikishia kuna masomo ambayo baa ni Chuo Kikuu.

Na mara nyingi ni watu wasioijua baa huwa mstari wa mbele kuilalamikia baa!:-(

Siwalaumu lakini kama kwa kuwa kwako baa pamoja na mengine kama ya kujisomea hufanyi na tunaweza kujumlisha pia na tabia yako ya kuwa huwa Unalia NA Kujikojolea ukilewa, wakati mtoto wako anavaa midabwada na hajawahi kushiba.:-(


Lakini waweza kujifunza WATU na SILIKA ZA MTU baa zaidi ya uwezavyo kujifunza mtu Kanisani , Msikitini au Shuleni.



Ila BAA kama tu Msikitini au Kanisani,....
..... ukienda na ajenda zako zisizohusiana na kikao, ujumbe wa SHEKHE au PADRE unaweza usipande!:-(

Swali:

  • Au?
Ila baa kiboko , ...
.....usipoangalia unaweza ukanywa mpaka kodi ya nyumba na kuanza kuifikiria kuinywa pesa ya kununulia padi za mke kama tu ulivyowahi kunywa za mpenzi hausigeli.:-(

Swali:
  • Lakini si unakumbuka kila swala binadamu kaamua kuwa lina mahali pake?
  • Na kwani darasani huwa unaelewa kemistri wakati unamfikiria Khadija?

Nimeacha!

Au ngojea Bunny Wailer aongelee- Mellow Mood



Au tu Peter Tesha aongelee- Why Must I Cry


Au tu Bob Maliya aje katika- All in one medley mix


Nakuacha na baadhi ya picha zangu za juzi ya jana..
Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket





Photobucket







Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket

Photobucket





Photobucket



Photobucket


Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP