Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UKISTUKIA umekanyaga MAVI. Samahani! KINYESI.

>> Wednesday, October 31, 2007

Katika pitapita za kuendeleza libeneke, unaweza ukastukia umedakwa na harufu mbaya.
Wengi wetu hatuhusudu harufu mbaya na hatukawii kukiri hilo kwa nguvu zote!

Cha ajabu....

.. asilimia kubwa ya wakimbiao kitu au harufu mbaya, hujistukia wamegeuka kujaribu kucheki ni wapi harufu mbaya inatokea.

Swali:

  • Ukisikia kijambo, haujawahi kutaka kujua ni nani kajamba?
Sasaaaa......

Baada ya kushuhudia ni mzoga gani unatoa harufu na kuona yale mafunza yakifurahia kitoweo , hapo ndio binadamu huendeleza madoido, kama vile ya kutema mate , kubana pua , kujipepea na kadhalika kadhaa.Unaweza mpaka kumshangaa kwanini mdau alijaribu kukitafuta hata kwa macho tu hicho kitu kitoacho harufu kama kinamchefua namna hiyo.

Lakini....

.... wadau wabanao pua na kutema mate kwa sana wastukiapo kitu kichefuacho roho , ni wakali wa kukausha wakijamba kwa bahati mbaya hadharani au pale waachiapo ushuzi chobisi wakitarajia hakuna atakayetokea mida hiyo.

DUH!

Swali:
  • Ushastukia ukikanyaga kinyesi kikutiacho kinyaa, baadaye unaweza ukakishika kwa kisingizio cha kusafisha viatu?
  • Au ulifikiri ulipoburuza viatu mchangani na pale kwenye majani vimavimavi viliondoka vyote?
DUH!
Naacha !

Tulia na RICHIE STEPHENS na COCOA TEA

Read more...

Ratiba YA kujifunza KUMJUA Mpenzi!

Tokea kuzaliwa binadamu yuko katika ratiba ya kujua vitu fulani.
Kwa bahati mbaya binadamu atakufa bila kujua vitu vyote.

Lakini ukimuuliza mtu kajifunza nini tokea azaliwe, atakuwa na majibu mengi sana ya mambo aliyomaliza kujifunza, mpaka ataweza kukusimulia jinsi alivyoanguka wakati anamalizia ratiba ya kujifunza kuijua baiskeli.

Kama ni mdau wa kushushua , atakustua ; acha cha hizo wewe!
Swali gani hilo?

Lakini....

Swali:

  • Hakuna jipya unalojifunza kuhusu mama yako mzazi mpaka leo?
Sasaaaa....

...inaaminika kuwa mtu akijua kuendesha baiskeli , ndio imetoka hiyo. Yaani, hana cha zaidi cha kujifunza kuhusu baiskeli. Kitu hiki kinaweza kukushangaza sana ukistukia waendeshaji baiskeli maarufu, huwa wanafanya mazoezi kila siku yakuendesha baiskeli kabla hawajaingia Tour de France.Unaweza kubisha lakini kuwa hawa jamaa wafanyacho hakiko katika ratiba ya kujifunza kuijua baiskeli na miili yao waliyozaliwanayo!

AU?

Lakini...

...mimi naamini unaweza ukajifunza kitu kipya katika mikono yako mwenyewe kama utaiangalia kila siku kwa makini wakati mawazo yako yamekaa mkao wa kujifunza kuijua.


Kama ulianzia tumboni kwa mama, na inawezekana mpaka leo unaendelea kugundua mambo mapya kuhusu mama huyo huyo mpenzi aliyekuzaa, inawezekana mjumbe wa nyumba kumi kumi humjui kabisa.

Swali:
  • Unafikiri unamjua nani vile?
Ni rahisi kwa baba kudhani anamjua mtoto wake au mtoto kudhani amemaliza kumjua mama yake , hivyo kuacha kukaa mkao wa kujifunza.

Kwa wapenzi ndio kabisaa, mkao wa kuacha kujifunza kuhusu mwenzio , unakwisha mpenzi akisha kukubalia!

AU?

DUH!

Swali:
  • Si ulishamaliza kumjua rafiki yako tayari?
Nimtazamo tu mawazoni!
Usitishike!

Siku njema!

Nakuacha na SIMPLY RED wakinibishia katika swala na wimbo IF YOU DONT KNOW ME BY NOW.

Read more...

Binadamu Akicheza Muziki, hustukii KAKICHAA kiduchu?

>> Tuesday, October 30, 2007

Moja kati ya mahusiano kibao binadamu aliyojikutanayo au kujitafutia, ni uhusiano wake na muziki.

Jaribu kumuangalia binadamu achezaye mziki, halafu wakati anaendelea kusakata ngoma, mtazame tu huku umefuta sauti ya mziki.

Anachekesha eeh?

Napenda sana mziki, lakini ushafikiria ni nini kinakufanya utikise mguu ukinogewa na wimbo wa wa Kabasele ya Mpanya?

Miziki kiboko, kuna mingine kama ya kwenye makanisa fulani ya watu waughaibuni, inabidi uimbe au usikilize huku unaonyesha sura ya upole kana kwamba unapata utukufu.

Halafu kuna ile miziki ambayo ikipigwa, wajanja wakagundua kuwa staili nzuri ili wewe usifike unajua kucheza , ni lazima umkatie kiuno mwenzio mpaka ukirudi nyumbani cha kwanza ni kufua gwaguro au kificha faragha, kutokana na kuingia madoa yatokanayo na unyevunyevu uhusianao na sehemu za kuzalishia watoto.

DUH!

Swali:

  • Unafikiri kwanini mcheza sindimba maarufu ni yule akatikaye kiuno sana na Morani wakimasai ajulikanaye kama dansa mzuri ni anayeruka juu zaidi!

  • Wewe unajua kucheza muziki?
  • Kucheza mziki maana yake ni nini?

Binadamu kiboko kwa kujitafutia madoido ya kuongeza chachandu katika ladha ya maisha aishiyo. Ladha ya muziki ni kama ladha ya chakula ! Muziki uupendao waweza kutomfikisha mwingine kule kunako.

Katika utamu wa muziki, wengine hawakawii kuanza kulia kutokana na muziki kuwahuzunisha.

Swali:
  • Ushawahi kuona mtu anacheza mziki huku analia?

DUH!

Usitishike nawaza tu!

SIKU NJEMA!

Nakuacha na MATTAFIX wakikupa LIVING DARFUR

Read more...

KUHUSU MTAZAMO WAKO KATIKA SWALA!

>> Monday, October 29, 2007

Nikisema, utanikatalia!
Kisa, mtazamo wako na wangu vinatofautiana.

Katika mtazamo, king'ang'anizi anawezakuonekana kashinda, ingawa ashindwaye hoja bado inawezekana kashinda kimtazamo wa tikitaka.

Katika mtazamo mmoja Papa ni baba mtakatifu ,wakati mwingine unafikiria nje ya mtazamo, kama, hivi watakatifu wasio na wake au wanaume wanatibuje hamu takatifu za kibinadamu za uroda?

DUH!

  • Nakubali kabisa kwa mtazamo fulani Afrika ni maskini na kuna magonjwa kibao kama tuonavyo kwenye televisheni fulani.

  • Nakubali kwa mtazamo fulani inabidi niache hata kufikiria swala hili la mtazamo.

Swali:
  • Kwa mtazamo wako unafikiri mtazamo wa mwenzio ni bomba kuliko wako?
  • Kwa mtazamo wako, hivi ni nani anaenda mbinguni vile?

Duh!

Kwa mtazamo wangu ngojea niachie hapa hapa, kabla mtazamo wako haujaanza kufikiria kwanini naandika kuhusu swala la mtazamo ambalo inawezekana kama umesoma mpaka mstari huu , ukawa umejipotezea muda wako bure kwa mtazamo fulani.

DUH!
Nimtazamo tu ndugu yangu !
AU?
Tulia na Bendi ya Kisauzi SOUL BROTHERS

Read more...

Tukutane Kwenye Pombe Mshikaji!



  • Kila sehemu ni sehemu ya kukutana.Sehemu watu ambazo wanapanga au kunuia kukutana ndio hutofautiana.

Napenda kukutana na watu karibu kila sehemu, lakini mkutano wenye pombe ya kutosha unakasheshe zake ambazo sijafanikiwa kuziona nikikutana na binadamu, ofisini, kwenye michezo .........au hata chumbani.

Nazinguka sana na matokeo yapatikanayo baada ya kuchanganya ubongo wa binadamu na pombe au hata vilevi vingine kama.................na....................au......

  • Kikao chenye pombe kina digrii fulani za unafiki zitofautianazo na kikao cha binadamu akiwa katika anga ambazo hana kisingizio cha kwanini anafanya mambo ya ajabu.
Kikao chenye pombe unaweza ukasingizia ulilewa wakati unamtukana mheshimiwa , ingawa wote tunajua kisiri kuwa unachoongea kimetoka moyoni , hakuna cha pombe wala nini.

Kikao chenye pombe unaweza kustukia kubwa zima lile lijifanyalo babe, linalia!

Lakini.....

  • Tukikutana kwenye sinema, si tutaharibu utamu wa sinema kama nia yetu nikuongea?
  • Tukikutana msikitini au kwenye sinagogi , si itabidi tulazimike kumsikiliza mtu mwingine ambaye atakuwa anatushushia mitazamo yake akiihalalisha kwa kunukuu vitabu vya busara kama vile torati, wakati hatuna uwezo wa kumbishia kiaina?

Najua mikutano mingine inabidi tukutane faraghani, ili angalau na miili iongee mazungumzo yasiyo hitaji sana sauti, ingawa ukweli bado upo palepale, kuwa tukitazamana tu, mwili wako unaweza kunistua kama unajisikia kichefuchefu kuniona.

DUH!


Swali:
  • Si unakumbuka Kanisani si mahali pazuri sana kupanga kukutana na Zubeda ukiwa na nia na madhumuni ya kumtaka unyumba kabla ya ndoa?(utajisikia unafanya dhambi bure, ingawa nakukubalia unaweza ukawa unafanya hivyo kutokana na ukweli , Zubeda ni mtoto wa geti kali.)

DUH!

Sasaaaa....

Utamu wa kukutana kwenye pombe, ni jinsi kikao kiwezavyo kushirikisha waliolewa sana, wanaoanza kulewa , wenye uwezo wakuhimili kilevi na wale maji mara moja kama yale maharage ya......bila kuwasahau wale niwaheshimuo sana ambao wanauwezo wa kuja kuongea na mlevi wakati wao hawagusi kilevi wala sumu yoyote izinguayo akili.

Katika kikao cha pombe, starehe nyingine, ni jinsi wengine wanavyokuja kujiliwaza, wengine kutafuta ugomvi , kustarehe mpaka sababu za kutafuta ......nk.

Ukiwa na matatizo yako kichwani na pombe haikubaliani kiaina na kichwa, hukawii kunyanyua watu vitini kwa maswala unayoweza kufanya ambayo kesho yake hutapenda uyakumbuke.

Watu tunakutana vilabuni kwa sababu nyingi.
Moja wapo ikiwa ni moja ya sehemu ambazo ukiwa nchi fulani fulani ndio sehemu za kukutania kutokana na uhuru wake wa kuwezesha mtu kuonyesha ukichaa wake kiduchu.Au hata kwa sababu wengine tusingiziazo kuwa pale ndio marafiki zetu walipo.

Swali:
  • Hivi kilabu ni nini?(Hivi chumbani hapawezi kuwa kilabu?)

Lakini.......

..... kukutana kwa fundi viatu kunastarehe zake pia ,ingawa ni wanaume hupendelea kona hii.
Kukutana kwa muuza nyanya, pale kwenye genge, mali sana pia .
Kama muuza genge ni mwanaume na wewe ni binti mzuri , hukawii kupewa nyongeza.


Ukinuia kukutana na mtu bomba ,ni sawasawa tu na ukikutana na mdau unayemhusudu kibahatibahati pale uchochoroni ukitoka.......

Lakini.....
Kukutana si jambo zuri mara zote!

Swali:
  • Unapenda kukutana na jamaa anayekudai wakati umechacha?
  • Ungependa kukutana na Mama Mkwe wako Jikoni wakati unadokoa mboga?

Duh!

Najua tutakutana tu hata kama hutaki !

Tukutane kimawazo basi!

  • SI INAWEZEKANA KUKUTANA NA MTU KIMAWAZO TU?( Najua inasemekana wengine tunakutana kimwili hata kama tumeshindwa kukutana kimawazo.AU?)

Tukutane tu na tucheze nguti basi!

HONGERA KAMA WEWE SI MLEVI NA UNANGUVU YA KUKUTANA na KUONGEA NA WALEVI WAKIWA KATIKA KILEVI!

Baadaye basi, naacha kukuzingua!
Lakini hivi kumbe POMBE SI CHAI?

Namrudia Miriam Makeba akitukumbusha YUKO HIVI KWASABABU YA POMBE!

Read more...

Usanii wa KUMCHEKEA ADUI!

>> Sunday, October 28, 2007

Tatizo la binadamu mara nyingi, ni kuamini adui anamapembe.
Adui mzuri akiitiwa mwizi sokoni, atakayepigwa ni wapembeni yake kwa sababu anaonekana kibaka.

Adui tunamjua kwa sababu tuna marafiki.
Kama huna rafiki naamini huna adui!

Swali:

  • Kama hauna marafiki utajuaje kinyume cha urafiki?
  • Hivi una marafiki kikweli?
  • Hivi rafiki maana yake nini vile?

DUH!

Ukiwa na muda unaweza ukajifunza kumchukia rafiki.

Lakini....
... ukimchukia rafiki kwa sababu tu fulani ambazo unazijua au zinaleta maana sasa hivi , utajistukia tu baadaye kuwa ulikosea, ingawa hautakiri kirahisi mpaka akisha kufa ambapo utarudia msemo maarufu; MAREHEMU ALIKUWA MTU MZURI SANA, alishawahi kuninunulia juisi ya ukwaju!

DUH!

Wengi hufikiria kuwa wanamnunia adui!
Mimi naamini adui mkubwa huwa ndio rahisi kumchekea.

Swali:
  • Ushastukia katika maadui wakubwa ulionao mmoja wapo ni wewe mwenyewe?
DUH!

Staili yakutafuta marafiki ni ileile ambayo inasaidia kukujengea maadui.
Uzuri wa swala la maisha ni kale kaswala ka ubongo wa binadamu kutofikiria mambo yote na watu wote kila wakati.

Swali:
  • Kama ungekuwa unakumbuka ukali wa maswala yote uliyokutanayo maishani mpaka sasa hivi, unafikiri ungekuwa unacheka muda huu au unalia?
  • Ungekuwa unamchekea rafiki gani?
DUH!

NAACHA!

Samahani wote niliowakosea!

Kwa mara nyingine nashukuru kwa yote MARAFIKI zangu!

Nakutakieni kila la kheri katika KUMCHEKEA ADUI!

Tulia na Rick James anikumbushaye enzi za kabla ya Bongo Fleva kabla hauja angalia baadhi za picha zangu na marafiki.....Anakupa COLD BLOODED




Tuendelee na picha.....
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Lakini kabla ya picha zaidi ngojea Mdau Marcos aonyeshe madairo...


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Marcos
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Paullina
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
T na N
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Wax na ..
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee wa Zanzibar Nasibu na Steve
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Marasta mnanitenga lakini!:-)


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Timu imekamilika:-)
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
RumPunch aka Mtoto wa Kariakoo!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ngojea ni ziloop baadhi ya picha zangu nyingine nilizodakwa na kudaka wadau kadhaa ambao hawajanitenga bado !

Wadau ambao sijatumbukiza picha sijawasahau!

Tuko pamoja!

DUH!
Tulia na zilipendwa nyingine ya Shaba Ranks akiwa na Maxi Priest!
Si utakuja tena hapa baadaye?
AU?

Read more...

SWALA LA MUAFRIKA KUOA MZUNGU!

Swali:

  • Kuoa au kuolewa maana yake ni nini?
  • Ushastukia kuwa mtu umlengaye nitofauti na wewe?(Ukiwa wewe ni mwanamke, unaweza ukawa unamlenga mwanaume.)
  • Muafrika ni tofauti na Mchina au haya ni maneno tu?

Kuoa au kuolewa ni jambo la ajabu sana binadamu mwenye akili alifanikiwa kugundua.

Katika kuheshimu ndoa na kufanya yote jamii ikubaliyo kuwa yanaruhusiwa ndani ya ndoa, binadamu akagundua kuachana na kuachika hata kama wengine nje ya chumba hatustukii swala.

Staili ya kuacha au kuachika,(hapa na maanisha ifikiapo mpenzi kageuka mshea chumba kama unaaibu ya kukikimbia chumba) ni noma. Kwa sababu maana yake ni kutukana ile fikira uliyokuwa nayo wakati unataka kuoa au kuolewa kwa kisingizio umempenda kweli nanihino na unataka uishinaye milele.

Nakubali kuwa unaweza ukawa umeoa au kuolewa kwa sababu nyingine na sio kuwa unapenda harufu ya kikwapa ya mpenzi.


Ndoa kitu kizuri, inatunzika tu vizuri kama kikojozi awezavyo kutuza siri ya godoro alilokojolea.
Ndoa inatamanika sana tu kama walioko ndani ya ndoa wamtamanivyo kisiri hausigeli/hausiboi bomba wa nyumba ya jirani(ikiwa wa ndani havutii)

DUH!
Ngojea niache utani!(hivi unafikiri natania?)

Naamini ndoa nyingi na jamiii nyingi zihusishazo jamaa waliofunga ndoa, huendeshwa kwa janja ya mwanaume iliyo jificha ndani ya dini, mila desturi, ndani ya suruali na.......

DUH!

Hebu msikilize tena Harry Enfield akitania kuhusu baadhi ya mitazamo ya wanauume juu ya wasionauume....


DUH!

Napenda hadithi za ndoa kwasababu nyingi zimekaa kinamna ya kwamba aliyeoa au kuolewa na Mchina anajifanya hakustukia kuwa inabidi ajifunze kula kwa vijiti mara nyingine kama sio zote.

Halafu hadithi nyingine za ndoa, ni zile jamaa ajifanyapo hakustukia kuwa kwa kuoa au kuolewa hakujiingiza tu kwa mtu mmoja bila familia au jamii yake ambayo daima hukumbuka kuwa yeye ni wakuja tu hapo chobosi ya mjanja aliyemdaka.( ingawa kisiri anajua kuwa ni yeye kadakwa)

DUH!

Swali:
  • Unaposema unaheshimu ndoa yako, inamana unajinyima nini vile?
DUH!

Samahani naacha basi!
Siunajua niko mawazoni tu?
Nisamehe basi!
AU?

Lakini...

.......Naamini wewe kama Muafrika au Mgagagigikoko, umeoa au kuolewa na Mzungu, Mtanzania, Kibaka, Zeruzeru, Mweusi tiii, Muarabu fulani au yule ambaye uzuri wake unaonekana vizuri mpaka mkisogeleana umbali sifuri, ujue tu umeoa au kuolewa na haka kamchezo ni kaubunifu ka kidunia tu.

Naamini kama mbinguni ni kuzuri kama baadhi ya vitabu (biblia na...) vya ujanja uwakilishwavyo utundu uitwao dini vituambiavyo, sidhani kama kutakuwa na msamiati uitwao ndoa hapo HEVENI.
AU?

Swali:
  • Hivi si unakumbuka hisia za binadamu hutengenezwa na mchanganyiko wa kemikali tu mwilini mwa binadamu?

  • Halafu si unakumbuka ni mjanja fulani tu aliyetuambia TELEVISHENI kwa kiswahili inaitwa LUNINGA?

DUH!

Ngoja niache basi,Nisije kukosa mke bure!

Nawatakia maisha ya kutafuta au kuwa ndani ya ndoa mema!

Tulia na Samim akija na Heater

Read more...

KWA MPENDWA MWANANGU MSENGE!

>> Saturday, October 27, 2007


Swali:

  • Ngono kwako ni kiburudisho au unataka kutengeneza mtoto?
  • Hivi wasenge na Wasagaji wana kasoro?
Mchezo uhusianao na kutengeneza watoto unautamu wake, ikiwa umenuia na hujabakwa.

Pamoja na kufurahia na kuguna kwa utamu wa kuzalisha, (hasa ikiwa sio wewe uko leba wodi) wengi tunabunia tu, na kujihakikishia mtoto aliye mimbishwa atakuwa kama tumnuiavyo

Atakuwa.....
  • Bomba..
  • Ana akili huyo!We acha tu!
  • Daktari hapo baadaye
  • mwanaume au mwanamke.., (kama ni mwanaume ,hakawii kukuletea kesi homu za kumimbisha kuanzia hausigeli mpaka mtoto wa padri , halafu humaindi sana!).....
  • Anacheza sana basketi boli
  • ......... nk kadhaa zisababishazo unamtambulisha kila chobisi......nk.

Kwa ujumla , mwenye mtoto hawezi kunuia kirahisi toto lake liwe na kasoro fulani.
Mtu unajikuta tu umezaa mtoto kilema au yuko dakika kadhaa nyuma katika idara ya kufikiria.

Huwezi kuwa umechagua kirahisi kutengeneza toto usilojivunia.
Ingawa wengi wakati tunacheza kamchezo, hatukumbuki kuwa ni kamchezo kawezako kumimbisha mtu.(hapa ni kama wewe sio basha ahusuduo saresare maua au yule.....ndani ya kale kamchezomchezo)

DUH!

Ukiachana na mengine mengi ambayo yatajitokeza katika mtoto wako yakusikitishayo, hasa kutokana na tabia za binadamu kujenga mategemeo ya kutegemea toto lako litakuwaje au litafanya nini hapo baadaye....,naamini kuna mengi ya kushukuru tu kuwa, angalau umefanikiwa kulipata toto lako.

Sasa ukishalipata toto lako zuri na lina akili hilo, na halisahau kukuletea mlenda na kale kagari fulani liliko kununulia na kuhakikisha unapata mafuta na.....

DUH!
Naacha Basi!

Mcheki kidogo Harry Enfield akichekesha katika kugusia swala la mtoto wa kiume akimleta bwana wake wakiume nyumbani...


Swali:
  • Utafanyaje mtoto wako mpenzi akikustua kuwa anahusudu nanihii za faragha zifananazo na zake?( namaanisha, akiPENDA SARESARE MAUA?)
Usitishike!
Sina mtoto bado!
Inawezekana nawazia jambo nisilolijua!

Naaacha basi!
Tulia na Los Lonely Boys wakikupa kibao MBINGUNI

Read more...

Katika Kuchagua Nani wa Kumuua.

>> Friday, October 26, 2007

Kuua ni dhambi kwa wengine.
Kuua pia wengine huita adhabu au njia ya kuabudu.

Kuua ni rahisi hasa kwa binadamu aliyefanikiwa kujidanganya kuwa kitendo chake cha kuua si kuua.

Swali:

  • Ushawahi kupiga au kutamani kupiga mwizi?(Si unakumbuka ngumi moja yaweza kuua?)

  • Ushawahi kula nyama au samaki?


Staili ya kuua ni madoido tu.
Unaweza kuua kwa kutomjulia hali mtu.

Katika ajali....
......unaweza ukajikuta unachagua nani wakumuokoa kwanza.
Wakati unachagua wa kumuokoa kwanza, inawezekana umechagua nani afe

Usitishike!

Binadamu ni mtu mzuri, mara nyingi huchagua kufa yeye mwenyewe .
Hakawii kucheza peku kiwanja chenye miba!
Akiwanazo hakawii kula mpaka augue.

DUH!

Wiki mwisho Njema! Wadau!
Nakuacha na kaka Freddy Macha

Read more...

USHAWAHI KUNYIMWA?

>> Saturday, October 13, 2007

  • Mkubwa , ukinyimwa kitu baada ya kukiomba, unakifanyia kazi. Ukikifanyia kazi , lazima ukipate kama kilekile ulichonyimwa,hapo ni kama imeshindikana kupata ulichonyimwa.

Ukizaliwa tu, unaanza kunyimwa kitu fulani.
Unanyimwa hata chuchu, kwa faida yako mara nyingine.

Ukiwa unakua lazima ukutanane sana na sentensi kama; ``WEE ACHA ! au, Nani kakupa pipi, utaoza meno wewe, hebu tema hiyo lawalawa sasa hivi!´´

Lakini....

Ukiwa mdogo , baada ya kunyimwa chuchu, unaruhusiwa kuililia.
Ukiililia mara nyingine unapewa.
Baada ya kuililia na kunyimwa zaidi unalala.

Lakini.....

Kuna watu wanasema kuwa , ukifanyiwa kitu fulani mara nyingi, utazoea.
Ukweli ni kwamba, kukubaliana na kunyimwa au kuzoea kunyimwa ni vigumu.

Mara nyingi mtu akinyimwa lazima anyong'onyee.
Ukinyimwa unaweza pia ukaanza kuogopa kuomba tena ,kutokana na machungu uyakumbukayo au uliyopata baada ya kunyimwa..

Swali:
  • Unahisi unaweza kunyimwa kuingia mbinguni pamoja na kuomba kwako huku?

  • Ushawahi kunyimwa salamu na uliyehisi angekusalimia?
  • Ushawahi kunyimwa............na ..................?

USITISHIKE!

Kunyimwa ni kawaida!
Kunyimwa inaweza ikawa ni changamoto kwako, ambayo itakupeleka mbele na sio kukudumaza.

NAKUTAKIA WIKIENDI njema NA kila la kheri katika KUGEUZA machungu ya kunyimwa, YAZAE MATUNDA yatakayo msababisha AKUNYIMAYE akuombe urafiki!

Nakuacha na nyimbo mbili kutoka kwa SOLOMON BURKE na 2Face Idibia ,zikusindikize kwa muda wa siku kadhaa ambao sitakuwa mtandaoni kwa sana!

Solomon Burke...

2Face IDIBIA


TUKO PAMOJA!

Read more...

Nakupenda KWA HARUFU YAKO ya KIKWAPA, pamoja na HARUFU ya PILAU kunizingu Wakati wa EID HII!

>> Friday, October 12, 2007

NAWATAKIA HERI YA EID WAISLAMU WOTE na Wadau wote wa BLOGU HII!


Ngoja nikuzingue kwa nyepesi nyepesi basi.........

Wakati huu wa EID , ni rahisi pua kunusa harufu nzuri za mapochopocho.
Kile chakula kizuri kizuri, ndio hutawala majumbani na kikichelewa kuiva, unaweza kushiba kwa harufu tu!

Lakini ningependa kukukumbusha harufu binadamu azitoazo , ambazo ni vigumu kuzinusa wakati huu wa EID , ingawa zipo.

Kazi ya Proffesor Winston, ichambuayo machale ya binadamu(HUMAN INSTINCT) inagusia mpaka jinsi hata umpendaye wakati huu wa EID ,upendo wako unaweza ukawa umesababishwa na anavyo nukia kiasili(Bila Perfumes).Unaweza ukawa unamzimia baada ya kunusa harufu ya kikwapa chake.


Napenda kukukumbusha kuwa kikwapa hutoa aina mbili za harufu zinukiazo kama chakula. Kama unabisha , soma hapa usikie jamaa aliyefanya kauchambuzi.

Kumbuka pia , wanawake wapendao wanaume na wanaume wasenge ,huvutiwa na harufu sawa za homani za ngono. Ila wataalamu hawa bado hawajagundua wanawake wasagaji wanavutiwa na harufu gani.

Si basi ujisomee hapa mwenyewe wakati unasubiri pilau la EID?

Ningependa kugusia mpaka maswala ya jinsi ya kugeuza harufu ya kikwapa iwe harufu nzuri, harufu za uvundo za sehemu za faragha au zile harufu zipatikanazo katika sehemu za faragha mara nyingine zinukiazo kama samaki, lakini najua tunasherehekea EID, kwa hiyo nafikiri niache hilo kwa sasa:-(

Lakini usitishike, harufu asilimia kubwa zitokazo kwa binadamu , zinanukia vizuri puani mwa binadamu na zinamaana nzuri kwa binadamu. Tunazistukia harufu tuziitazo mbaya kwa sababu ni chache na ni rahisi kuzistukia.

DUH!

TURUDI kwenye EID basi.............!

NAWATAKIENI wote msherehekeao EID, harufu NZURI za MAPOCHOPOCHO hapo mlipo!

DONDOO:

  • Tukumbuke tu na kutowasahau wengi ambao watalala njaa katika EID hii, kutokana na kukosa chakula. :-(


Duh!

Naacha kukuzingua basi!:-)


Ngoja nirudi anga fulani za miziki. Kwa bahati bado MAXI PRIEST yuko kichwani.....

Read more...

MUDA DOMO KAYA! Siri yako yaweza kuwa nje baada ya muda!

>> Thursday, October 11, 2007

Fanya ufanyalo, sema usemalo, baada ya muda fulani ukweli utajulikana.

Kudanganya kwangu leo ni kuzuri.

Tatizo ni kwamba, baada ya muda, unaweza ukastukia hako kakitu nilikokudanganya sikapendi kuwa kananinogea.

Mimi naaamini kuwa, kitu chochote usicho na uhakika nacho , baada ya muda fulani utahakikishiwa,

Samahani!
......Hili swala linagusa mpaka maswala ya kama kuna Mbinguni au hakuna.

DUH!

Ukiwa huna uhakika, subiri , muda utakuhakikishia kuwa:

  • Jamaa hajali
  • Mbinguni na Jehanamu kweli kupo
  • Kweli Yesu ni Mwana wa MUNGU
  • Kuwa jamaa mjinga
  • Nanihino alidanganya

  • Kweli anakupenda.

  • Jamaa Mwerevu
  • Na kadhalika kadhaa...



Tatizo la kusubiri muda, ni kwamba ; kusubiri hakuna mpango!
Kusubiri kunaboa!

Tatizo jingine ni kwamba, muda hausubiri, unakwenda tu.

Leo yule dogo aliyekuwa anakusalimia kwa heshima wakati fulani, anaweza akawa anakuangalia kwa jicho la kukutaka. Inamaana tayari anajilinganisha kinamna na wewe, au sehemu zako fulani za faragha ashajua kuwa anaweza kuzihimili.Hapo ujue muda ndio umeanza hivyo! Si unakumbuka ulipoanza kupewa shikamoo, au mawazo yako kuhitajika kimchezo mchezo tu?

DUH!

Swali fulani:
  • Hivi muda unakwenda wapi?

Lakini....

Binadamu wengi hujenga ukweli wa mambo kichwani mwao, hata kama jina halisi la ukweli wao huo ni uongo. Watu wa namna hii , hata uwape muda, watautumia kutafuka jinsi ya kuhalalisha kaukweli wakaaminiko kuwa ni ukweli.

Wakati wakikuambia wanajaribu kutafuta ukweli wa jambo, huwa wanajaribu kutafuta vigezo vya kujihakikishia kuwa wanachoamini tayari akilini mwao kuwa ndio ukweli.

Hivyo ndani ya ka-Muda fulani...
  • Wakristo, Waislamu, Wabwiti, Wachawi,nk; wanapata vigezo kuwa wanafuata dini ya ukweli.
  • Walevi , watumia madawaya kulevya, walafi, nk; wanapata vigezo kuwa , hawadhuriki.
  • Wanafunzi , wanajisikia kuwa wanaakili baada ya kustukia kirahisi jambo waliloambiwa gumu.
  • Hausigeli na Hausiboi wanawezakujisikia nyumbani, katika nyumba ya bosi wao, na ikawa ni ukweli kwao, mpaka watakapostukia mshahara unachelewa.

  • Wakereketwa fulani hustukia kuwa wanaweza kuibadili dunia , na kuifanya iwe nzuri zaidi.
  • wa......wana....

DUH!

Ngojea nikupe MUDA ili ugundue kama nilichoandika ni upumbavu au sio!

DUH!


Naacha hili swala basi!

-----------------------------------------------------------
Ngojea basi nikutembeze katika mabadiliko yangu binafsi ,
....katika kona, kwa kutumia picha, wakati nikiendelea kuwajibu wadau kadhaa wanaoniuliza sana maswali fulani kwa muda sasa hivi.



SAMAHANI KWA Quality mbovu kidogo za picha ambazo nimeziscan midamida ili, kunisaidia kukusimulia hadithi inihusuyo kama nilivyoathiriwa na MUDA.

Kabla sijaanza , Unamkumbuka MAXI PRIEST?



Tuanze basi........


Hadithi Hadithi!

Simon enzi hizo......



Maisha yalikuwa matamu. Ukitaka kitu unakililia. Chakula kikichelewa unalalamika .Hujui kuwa wazazi wanatoa wapi pesa wala thamani ya pesa nini, wakati unauhakika wa kupata pipi gololi.


Muda Ukaenda wee, ukaenda weee...
Nikajikuta niko Sekondari /A-levo, nikisumbuliwa na matatizo mengine tofauti yaliyojitokeza....
....

Ni vigumu kuyataja yote, mpaka ya chakula kibaya shuleni. Ila kipindi hiki nakikumbuka sana kwa jinsi nilivyomtafuta Mungu , kitu ambacho bado naendelea kufanya. Mpaka kufikia kipindi hiki , nilifanikiwa, kuokoka, Baada ya kupata msaada wa Moses Kulola, Kuslim, baada yakukutana na mafundisho ya Korani, na kuwa Rasta. Mpaka sasa hivi ukinisoma hapa MAWAZONI , utastukia kuwa bado nafuatilia sana maswala ya dini maswala ya dini , nakujiuliza sana kuhusu Mungu , Shetani na .....

Lakini....

Katika kipindi hiki nilifanikiwa pia kupigwa buti na mwanadada niliyempenda.Na ndio ilikuwa mwanzo wa kustukia ugumu wa kuwa na mpenzi mbali nawe , hasa kutokana na kuwa mwanafunzi wa bweni, katika shule ya Wavulana watupu.

Tulikuwa tunatembelewa na akina dada wa MSALATO lakini, kama...


Duh!
....Sijui mdau wangu Godwin Mabagala ambaye tulikuwa tunashea chumba Mazengo na Mdau Kusirie ,wako wapi siku hizi.


Ngojea nikutonye kidogo kuhusu enzi zangu za URASTA...
DUH!
Sijui JAH Kimbuteh na Ras Pompidou wako wapi siku hizi....


Nachojaribu kusema....
.....nafikiri tungekutana na Rasta Luihamu enzi hizo, tusingekuwa tunabishana sana mitazamo, ingawa nakiri kuwa mimi ni mgumu kuaminishwa kitu ambacho akili yangu inashindwa kukubaliana na majibu kinipayo.

Nasikitika kukiri kuwa, nimejiuliza maswali mengi sana, wakati niko ndani ya dini zote nilizowahi kuwepo ndani yake , huku nikipima majibu dini hizi zinipayo, na kujiuliza tena zaidi kama majibu haya yananifikisha katika mridhiko au la.
Nasikitika tena kukiri, mara nyingi nimefikia kuaambiwa, dini haihitaji utumie sana akili kufikiria majibu upatayo ndani yake, la sivyo ,utajikuta huna dini.

Lakini.....

Katika Ukristo, niliweza kuwa bingwa wa mahudhuriao mazuri, muimba kwaya, na hata mcheza maigizo ya kanisani , kama hapa nionekanavyo, ndani ya kanisa la BUNGO , MOROGORO...





DUh!

Kuna kitu kingine wadau fulani hupenda kuuniuliza sana .
Hasa swala lakutochana nywele .

Kwanza napenda kukumbushia kuwa mimi kiimani sio RASTA kama wengi waaminivyo kuwa ukiwa na nywele kama zangu , basi wewe ni RASTA.

Pili , naamini unaweza kuwa na nywele za staili yeyote ,ingawa kumbuka kuwa dunia imejaa watu wepesi kuweka watu katika mafungu. Kwahiyo unaweza kukosa kazi sehemu kwa sababu tu unavaa lubega na sio jeans.

Mimi mwenyewe, mpaka leo hii, ukikutana na Baba yangu, ingawa ni mtu mwenye diplomasia, kama umesuka au Huchani nywele kama mimi, ujue kabisa kuwa atakuwa na mashaka nawe.

Dingi yangu anaamini , kijana nadhifu na waheshima, ni lazima atakuwa amekata nywele vizuri. Hawezi kukuelewa , kama wewe ni mwanaume halafu umesuka nywele. hawezi kukuelewa , kama huchani nywele kama mimi.

Kwa bahati mbaya, mimi nimepitia katika vyote vitatu. Kukata nywele, kusuka, na kuwa na locks kama nilivyo hivi sasa.
Unaweza ukastukia mionekano yangu kadhaa tofauti na mpaka mdingi wangu katika picha hizi...


Vilevile...
kuna jamaa wengi huniuliza kama mimi ni msanii au la!
Naweza kukiri kuwa mimi ni mpenzi wa sanaa. Nimefanya sana miaka kibao , ingawa sijasomea hii kitu wala sijawahi kujiita Msanii. Nimefuata sana mdundiko, kuigiza mpaka vijijini, na pia kupanda majukwaa kibao tu.
Baadhi ya viwanja enzi hizo....

Lakini...
Mimi , tokea nianze kuuza magari ya waya na ya makopo SONGEA, halafu nihamie kwenye uchumi , kimasomo High School, na Biashara kabisaaa, katika vyuo kadhaa., nakiri kuwa mimi ni MFANYABIASHARA.Usistuke kustukia siandiki maswala ya biashara humu.

USITISHIKE na NYWELE!

........Mwisho wa hadithi!

Naamini kuna baadhi ya wadau, mliokuwa mnanilenga mara kenda fulani na maswali fulani, nimewajibu kiasi.

MUDA UTAJIBU MAMBO MENGINE!
AU?



TUKO PAMOJA!
Samahani nawarudia KASSAV wakija na kitu SAMMI

Read more...

KATIKA kukwepa HALI HALISI igusayo MAISHA YETU!

>> Wednesday, October 10, 2007

Hali halisi haiwezekani ikawa na utamu tu bila chachu pembeni yake.

Hali halisi, wakati inakupa utamu dakika hii , inaweza ikawa inakukumbusha ni nini kitafuata baada ya utamu, ambacho kinaweza kikawa ni utamu zaidi au ikawa ni kukukumbusha kuwa kutokana na utamu huu uupatao sasa , ushaharibu kesho au nusu saa ijayo.


Sisi watu, hujitahidi kukwepa hali halisi, nakuiwekea mipaka izungukayo hali tuzipendazo tu.
Tunapenda fenesi lakini sio mbegu zake.

Katika kukwepa hali halisi ya dunia...

  • Matajiri...
... wanajifanya hawaoni maskini. Ni rahisi hata kujirungushia ukuta katika nyumba yako ili hao maskini wakae huko huko nje.

  • Wanadini kama Marasta, Walokole, Wabwiti, Wakristo , wa.....nk...
....wengi wao wanakwepa hali halisi kwa kutuambia wamegundua ukweli , ilikujilinda ndani ya huo watuambiao kuwa ni ukweli, ili wengine wote wasije leta za kuleta na kusababisha hali halisi wanayojiaminisha nayo, iwe ngumu zaidi kueleweka.

Swali:
  • Umefanikiwa kuweza kusababisha watu wengine wasijue hali halisi yako kwa jinsi ulivyokwepa hali halisi leo?


Hali halisi nishai!

Ndio maana watu tunajifanya tunamsikitikia marehemu ili kuja kula ubwabwa msibani, kutokana na kushindwa kusema hatuna msosi nyumbani.

Kukwepa hali halisi , ni sanaa kali!

Inaweza kukufanya uonekane bomba la mchekeshaji ,kumbe unaficha tu huzuni iliyokujaa moyoni.

Hukawii kumsifia demu au bwana yako , kuwa ni mzuri kubwa kuliko, wakati unajua watu wengine wote wanakujua kuwa unamuona hawala yako ndio bomba zaidi.(Si ndio maana ukawa na wapembeni?)

Kukwepa hali halisi si mdhaa!

Inaweza ikakufanya ushinde baa na na kupigana na wanaume wenzako ,kumbe ni kwa sababu unapigwa na mke wako nyumbani.

Inaweza ikakufanya usifike kwa manukato na kunukia vizuri, kumbe ni kwa sababu tu unakidonda ndugu kunako.

Unaweza kuokoka, kumbe kwasababu umechacha tu. Si unajua maisha ya kilokole yanasemekana gharama zake ni za chini kidogo?

Swali:
  • Ushastukia msemo wa serikali yetu wa kwamba ;uchumi umepaa, ni sanaa ya kukwepa hali halisi?


Lakini ....

Yote ni maisha!

Si unajua tena!...
.... kama kila mtu angejua hali halisi yako, ingekuwa usumbufu pia.

Si unajua tena....



  • Jamaa wakijua unazo, utakopwa mpaka ukome?AU?

  • Jamaa wakijua umechacha, wengi ambao mara nyingi ndio wajitangazao kuwa marafiki zako , watakukimbia

  • Jamaa wakijua unamdudu , kuna anga wataanza kukukwepa , ingawa wanajua huwaambukizi.

Swali:
  • Unaamini viongozi wetu walivyopima Mdudu juzijuzi kisiasa, wakiongozwa na Raisi wetu Kikwete , wote matokeo yao yalikuwa safi kama matokeo ya Kikwete?

  • Hali halisi yako ikoje? (Na maanisha , ukipima Mdudu ukajikuta unao, utatutangazia?)
  • Hali halisi yako ikoje?( Na maanisha, unaogopa kupima UKIMWI eeh?)

Lakini .....

Kitu kizuri katika maswala ya hali halisi,.....
......... hakuna ambaye anajua hali halisi ya mwenzake, hata kama wako wengi wajifanyao wanajua ya wenzao.


Naamini kila mtu anajua hali halisi aliyo kuwa nayo ki binafsi.
AU?


Na...
......Mchezo huu tushirikiyo, wa kujaribu kukwepa hali halisi, ndio unaitwa
MAISHA.

AU?

Nakutakia kila la KHERI katika KUJARIBU kukwepa au kutufanya tusijue HALI HALISI yako!


--------------------------------------------------------------------------------------------
Ngoja nikuache na picha fulani nililizozidaka hivi karibuni....


Picha za baadhi ya waliohudhuria Mkutano wa Watanzania, siku kadhaa zilizopita ....



DUH!
PATRA yuko kichwani na wimbo wake wa longi hizoooo... Msikilize kidogo kabla hujaendelea...


Picha za Shughuli ya COBRA

Naanza na Cobra mwenyewe

..

Cobra Vibes


Picha nyinginezo ndani ya Party ya Cobra:

Bobby Culture , Super ONE , Simon .....



Mzee wa A-Town aka Musical Blak


BONANZA the GREAT! Samahani nilikutenga kiwanja....!
Tuko Pamoja lakini!


Kikao cha Kwa Raymond aka MKUU wa KIKAO!

Naanza na MKUU wa KIKAO..

Ngojea CHACHA atuambie...!




Baadhi ya niliyowadaka kwa Mkuu WA KIKAO...



Hebu Ronaldo atukumbushe ile miondoko ...


Kwa wadau ambao sijaingiza picha, TUKO PAMOJA! Nimeziingiza haraka haraka na , hii kitu mara nyingine haina Baraka.
Hapa tu wakati naandika nimemkumbuka Mzee DEO!
Tumalizie na enzi hizo hizo...
Unamkumbuka MC Hammer?

Read more...

BAHATI na BARAKA zijazo kwa kukosa AKILI!

>> Tuesday, October 09, 2007

Kuwa na akili ni usumbufu mtupu!

Kama ujinga ni sawasawa na kutokuwa na akili, basi.......:

  • Ujinga unastarehe zake ,...
.... kwa mfano starehe kubwa yakutosumbuliwa na kufikiria maswala yaumizayo akili.

Kufikiria mambo muhimu ni noma sana!
Hukawii kuanza kujaribu kutatua matatizo hata yale usiyojua hata pakuanzia.

  • Uzuri wa kuwa mjinga , ...
.....ni pale unapoweza kuuhisi na kuufurahia utamu kisawasawa, kama tu wenye akili wanogewavyo pale watulizapo akili na kuziruhusu hisia zao kuonja utamu.

Swali:
  1. Nani kasema kuwa mwenye akili lazima afaulu mitihani?
  2. Hivi UJINGA ni kukosa akili?


  • Ujinga wa mwenye akili,....
.... ni pale atumiapo akili kufikia kujilamba, kitu ambacho mwerevu mjinga, bila kufikiria wala nini, anauwezo wakustukia lawalawa ,hata kama mwenye akili anadai kabahatisha, na kumumunya utamu mpaka kisogoni.

POLENI sana WADAU, kwa kuwa na akili!

SASA MTAFANYAJE?


DUH!

Naacha!

Siku njema!

Lakini ngojea LINTON KWESI JOHNSON , atukumbushe yaliyomkuta alipofika UINGEREZA.

Basi bwana endelea tu na Linton KWESI

Read more...

HIVI ni NANI anapata MADEMU zaidi?

Kabla sijasema, ngojea nijikumbushe mahesabu ya kubwa kuliko, ndogo kuliko na.....

DEMU= Mwanamke.

Na inawezekana ikawa matumizi ya jina DEMU <UTU wa mwanamke

DUH!

Samahani!
Haya turudi kwenye hoja .........

  • Dunia kama itawaliwavyo na wanaume kwa asilimia kubwa, mtu anaweza kuingia upofu wakutoweza kutazama nguvu za wanawake.

Dunia ionekanayo kirahisi,utastukia...

....Kwenye dini maarufu kama za Kikristo, Kiislamu,mpaka zile akina Babu Shogholo walikuwa wanafuata, kuna ka-sehemu fulani kakubwa ambako mwanamke amepewa, kasehemu kakuwa msikilizaji na sio mtoa hoja.

Mwanamke wa shoka mtoa hoja, katika kumbukumbu nyingi kuanzia zilizoko kwenye maandishi au hata za masimulizi ya mdomo, ni yule anayetengenezwa kama vile alibahatisha nguvu au anatokea kwenye familia iliyoko na nguvu kiasi cha kupenya mpaka katika kiti cha mtoa hoja kwa njia ya kusaidiwa na mfumo uliomzunguka kutokana na familia kujulikana.

Watu weusi hulalamika kuwa , hadithi nyingi zilizo tawala zionyeshayo mapungufu yao, zimetokana nakuandikwa na watu wa rangi tofauti na nyeusi.

Lakini...


Unaweza kusema pia, kutokana na wanaume kuhusika sana na usambazaji na uhifadhi wa stori za mwanamke, ndio maana kuna mambo mengi yamuhusuyo mwanamke dunia imenyimwa kuyajua. Na kwa bahati mbaya wenye kumbukumbu za stori hizo wanazidi kuondoka na kutuachia kazi ya kubunia, ambayo inasaidia kuendeleza mtazamo tulionao hivi sasa, ambao mmoja wapo, ni huu usemao; mwanamke ni msaidizi tu wa mwanamume.

Dondoo:
Nafikiri unakumbuka hata maswala ya sensa za watu , wanawake walikuwa hawa hesabiwi mpaka miaka isiyo mingi iiyopita.

Swali:
  • Hivi demu(jina sahihi mwanamke) gani anapata wanaume zaidi?

  • KWA nini unafikiri MWANAMKE mwenye kujisifia kutembea na wanaume kadhaa wa kadhaa, anaitwa MALAYA katika jamii nyingi duniani, halafu mwanamume atembeaye na wanawake wengi, huonekana mjanja, dume la mbegu, rijali...nk?

  • AU mwanaume atembeaye na wanawake wengi naye ni malaya?

DUH!

Inasemekana mitazamo ya wanawake na wanaume ni tofauti.
Kwa hiyo, ayaonayo mwanamke katika kipengele , yanatofautiana na jinsi mwanaume ayaonavyo katika kipengele hicho hicho.Ukichanganya na jicho lijengwalo na tamaduni mbalimbali kuongeza maluweluwe, basi unaweza kufikiri kuwa maswala ya wanaume na wanawake kama yalivyo sasa katika jamii mbalimbali ndio jinsi yanavyotakiwa kuwa.


Lakini...

Pamoja na yote ambayo kwa asilimia kubwa naamini kuwa mimi na wewe hatuyajui kwa asilimia za kutosha, tutakubaliana angalau kwa machache kuwa ..
  • Mahusiano kati ya wanawake na wanaume bado siyo murwa
Ingawaa...
  • Wanawake na wanaume wanahitajiana hapa duniani.
Bado kuna vita ya kijinsia , ambayo inaendelea , kutokana na mwanaume anayetawala kung'ang'ania kiti cha utawala ,wakati mwanamke kachoshwa na kutawaliwa,....

.... halafu na yule mwanamke aliyefanikiwa kutawala kutumia nguvu zaidi kushikilia kiti cha utawala, kutokana na mwanamume kukuzwa katika mazingira yamtengenezeayo saikolojia ya kudhani yeye ndio apaswaye kutawala.


Swali:
  • Hivi unafikiri ni kweli wanawake na wanaume wanatakiwa wawe na usawa?
  • Usawa nini?
Ni rahisi kuongelea tofauti,....
..... kutokana na kujua tofauti za kimaumbile, kisaikoloji, kifikira, kikusikia utamu, kinyume cha kuhisi utamu naki ........nk ; kati ya wanawake na wanaume.

Ni rahisi kuruka baadhi ya mambo ambayo yanaleta usawa kati ya wanawake na wanaume, kimaumbile, kisaikoloji, kifikira , kiakili,kikusikia utamu, kinyume cha kusikia utamu naki.......nk.

Swali:
  • Ushawahi kukutana na wanaume wawili walio sawa?
  • Ushawahi kukutana na wanawake wawili walio sawa?
  • Usawa ni nini?

Naamini, kama jamii haina hata tafsiri moja inayokubalika na wote ya usawa, hii jamii mpaka kesho ya kizazi cha mwisho, itakuwa inajadili haki ziambatanazo na usawa kati ya jinsia hizi mbili zenye sehemu za siri zisizofanana.

Ukiingia katika kudai haki za usawa wa wanaume wajisikiao kuwa ni wanawake na wanawake wajisikiao kuwa ni wanaume kutokana na kemikali za mwilini, hapo ndio kasheshe!

DONDOO:
  • Unakumbuka kujisikia kwako kuwa ni mwanamke au mwanaume ni mchezo wa kemikali mwilini mwako zikuzinguazo mpaka siku nyingine unaamini maswala ya ajabu ajabu kama vile kupenda, kuchukia,njaa, uchoyo ...nk?

  • Kamchezo kakemikali kakibadilika , si unakumbuka, dume zima utaota MATITI?
Halafu na haya maswala ya sayansi, ambayo yanaweza kukubadili kidude,....

....... usishangae kujua kuwa yule Demu umzimiaye, juzi alikuwa MWANAUME, na yule Mwanaume uliyempenda baada ya kuona picha yake kwenye gazeti, bado anasehemu za faragha za kike , mpaka akipata mshahara wa kumalizia operesheni yakumwekea kidude mwezi ujao .

DUH!

KUMBUKA MAMA ZETU WAZAZI NI WANAWAKE!

  • Naamini wote tunahusika katika kuhakikisha haki za watu wote zinaheshimika.

  • Naamini kuwa, wanawake bado wako na mapambano zaidi ya wanaume katika kudai haki zao za angalau kutoa hoja na kusikika.
  • Naamini unayesoma hapa , utajaribu kustukia na kusawazisha pale ugunduapo, mimi na wewe tunachangia kuongezea tatizo na sio utatuzi wa tatizo.

Ngojea nijaribu kuacha!

Lakini ngojea tupewe shule kidogo tena na Ahmed Deedat ......



Tuendelee na utani ambao unamgusa Warren Jeff , nabii wa WAMORMONI katika jambo lisilo utani lihusianalo na janja yetu WANAUME ya kupata KALE KAKITU mara kadhaa zaidi ya WANAWAKE.






Naacha basi DUH!

Burudika na Blues(halisi na sio ile ya disco la...) kama ipigwavyo na MUDDY WATERS

Read more...

Tuko Pamoja!

>> Friday, October 05, 2007

Nakukumbusha tu hili swala....

Ngojea nirudie kusema...


Duh!
Ngojea niache kukuzingua!:-)

Wiki Mwisho njema!

Badili kidogo mawazo kwa wimbo Dr Kitch ,ambao wadau kadhaa wa blogu hii waliomba niurudie kama ulivyopigwa na Marehemu Lord Kitchener


Nimekusikia mdau uliyestukia kuwa mara ya kwanza nilikuwa nimemposti Craig Mack hapa. Nimemrudisha...huyooo...

Read more...

HAKUNA JIPYA, yote yako MUKICHWA!

Pamoja na yote..

Binadamu tunaamsha tu yaliyoko ubongoni.Tunajaribu kufanya yaliyo ndotoni , mawazoni, yaonekane mbele ya macho yetu!Ukionacho mbele yako, ambacho binadamu mwingine amefanya, inawezekana ikawa ni jinsi alivyokosea kukitoa ubongoni au mawazoni na kukiwasilisha duniani.

Machache binadamu kafanikiwa kuyatoa ubongoni na yakawa kitu halisi ulingoni.
Ni machache zaidi binadamu aliyofanikiwa kuyatoa ubongoni na kuyaweka kama alivyoyaona ndotoni au katika kimbunga cha ubongo(brain storm)

Swali:

  • Si ushawahi kutoridhika na ladha ya togwa baada ya kuionja na kustukia haifanani na ilivyokuwa mawazoni mwako kabla ya kuionja?
Si ushawahi kustukia!
Mtu aliyevaa nguo, anaweza aasionekane kama jicho la ubongo lilivyokustua ndio maumbile yake yalivyo, baada ya kumchungulia akiwa bila nguo.

Duh!

Lakini sisi binadamu....

....tunajaribu kufanya yaliyo ubongoni, ndotoni, mawazoni ,ili yawe mbele ya macho yetu , ladha zetu nk.

Tunatofautiana tu, katika ujanja wa kuyatoa mukichwa , nia na umuhimu wa kuhangaikia kuyaleta yale tuyawazayo, tuyawezayo; yaonekane , yahisiwe au kubadili kitu fulani kama tukionavyo kwenye jicho la ubongo, kijiweni.

Swali:
  • Unakumbuka mambo yote yatokeayo ndani ya ndoto uziotazo?
  • Mangapi yaliyotokea kwenye ndoto zako, ulishawahi kuyashuhudia, kuyasikia au kuyatenda, kabla hayajajitokeza kwenye ndoto zako?
  • Hivi , unakumbuka de javue?

Mengi tuyaonayo, ambayo ni matokeo ya utundu wa binadamu , ni mrahisisho wa yale mambo ambayo yalionwa na jicho la ubongo la binadamu.Tunarahisisha yaliyo ubongoni kutokana na kutojua jinsi ya kufanya yote yaliyo ubongoni yawe ndio hali halisi kirahisi.Unajua, binadamu kwa asili ni mvivu.


Kumbuka hata majinamizi(ndoto mbaya) ukiyaamini , ni hali halisi. Ni kitu halisi kikuzinguacho na kukukosesha usingizi, kitu ambacho nikikuona kesho yake nitashuhudia hali halisi yako wewe baada ya kukosa usingizi.
AU?

Swali:
  • Wenye imani , si ndio wanakuambia, imani yako ndio itakayokuponya?

Nikirudi kwenye hoja...

Tuvionavyo sasa hivi si jambo jipya zaidi ya yale yale yaliyomo ndani ya vichwa vya watu hata kama hatuvistukii.

Tatizo mojawapo la ubinadamu , ni kutostukia baadhi ya mambo yaliyomo ubongoni mwetu.

Swali:
  • Ushawahi kuingia katika mtihani ukiamini hujui utafanyaje kutokana na kutojiandaa vizuri , halafu mtihani ukawekwa mbele yako , ukaona maswali na kuanza kushuka pointi mpaka unajistukia; kumbe nalijua swala?


Tatizo jingine la ubinadamu ni kuambukizana mitazamo na jinsi ya kutafsiri ya dunia.

MITAZAMO ya WAJANJA na TAFSIRI ZA YA DUNIA za WAJANJA , ndio binadamu wengine wanashikilia kuwa ni ukweli, MPAKA ATOKEE MJANJA MWINGINE mwenye mtazamo na uwakilishaji wa tafsiri ambao watu wengine wengi wanashindwa kuubishia.

Ushastukia !

Dunia ya leo iendeshwavyo kwa mafuta, karibu kila mjanja anajua imeharibu mazingira ya dunia na kushindwa kumuongezea binadamu raha wala furaha.Ila wajanja waliotupeleka katika njia hii bado ndio wameshikilia dunia.

Swali:
  • Unafikiri mababu zetu wa kale walikuwa hawali maisha ingawa hawakujua gorofa wala baiskeli?
  • Au, unafikiri , technology na maisha yaaminikayo kama bomba leo ni timilifu?
  • Au unasubiri mambo yatimilike ukifika mbinguni?

DUH!
Naacha!

Siku na Wiki Mwisho Njema!

Nakuacha na EVERLAST , wakija na kibao YESU MWEUSI.

Read more...

BAADA ya kumsikiliza na kuangalia kazi zake GURU wa YOGA, B.K.S. LYENGAR.......

>> Thursday, October 04, 2007

Baada ya kufuatilia kazi za GURU LYENGAR , sikuacha kujiuliza; ni kazi ngapi za Kiafrika ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi ili kueleweka au kufundishika kirahisi?

Huyu Guru, alifanikiwa kuchukua tamaduni ya YOGA na kuipanga kinamna ambayo watu wengi wanaweza kuielewa na kujifunza. Na uhakika kuwa kuna watu wengi wenye taaluma za asili za Afrika, ambao wangeweza kuzijenga kinamna ambayo tunaweza wote kuelewa kirahisi, zinafanyikaje.

Swali:
Hivi kwa nini taaluma ya Uchawi Afrika, tunafundishana kinyemela?
Hivi nani anafuatilia na kuturahisishia uchezaji wa sindimba?

DUH!

Tukiachana na Guru kidogo....

Nimefurahi kuona kazi za Bi Kidude na historia yake.
Naombea sisi wote, pamoja na wasanii waliokubuhu na wajuzi wa mambo yetu yafanyayo tutambulike kama Waafrika , wote kwa pamoja tuendelee kufanyia kazi za kuhifadhi na kuendeleza tamaduni zetu.


Hebu tumcheki GURU B.K.S LYENGAR

Mwaka 1938 akifanya vitu vyake...

Mwaka 1991 akiendeleza...


Akiongea...


Tumalizie kidogo na BI KIDUDE ,ambaye anaenda MIAKA MIA MOJA na hajaacha fani, aendeleze!(Ukitaka kumjua zaidi tafuta kazi imuhusuyo iitwayo AS OLD AS MY TONGUE)

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP