Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUJARIBU ni dawa ya KUISHI huku ukiridhika kwa kujua hata kama HUKUOPOA NGOMA angalau ULIJARIBU!

>> Wednesday, August 31, 2011

Kujaribu  ni DAWA,...
..... kwa kuwa  kwa weza kukuhakikishia ni jinsi gani UNAJUA hata kile uaminicho unajua,....
.... kwa kuwa labda bila KUJARIBU hutajua kwa uhakika ni kweli UNAWEZA uaminiyo unajua!:-(

Swali:
  • SI unajua bila MDADA  KUJARIBU labda hakitafanyika kitu kihiari katika DUNIA ya leo ya KISASA?
  • Na siunajua bila kufanya labda hakuna atakaye gewa mimba?



Ndio,..
... labda JARIBU,...
... kwa kuwa angalau KISAIKOLOJIA,...
.......bado ni tiba PIA ya yale ambayo ungeweza kuja KUJILAUMU hata UZEENI  kisa HUKUJARIBU wakati KIUJANA ungeweza!:-(


NI wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu OSHO aongelee- Behave As if You Are the First Here




OSHO aendeleze shule kimtazamo wake kwa- Anybody Who Gives You a Belief System is Your Enemy.



OSHO aongezee dozi ya shule kwa- Love and Hate Are One



Krishnamurti angilie kati darasa na kuuliza - Who am I?



J. Krishnamurti amalizie darasa kwa- Why don't You Change?








Read more...

Tatizo la KUDHANIA Askofu anajua BIBLIA na SISTA hajui MAPENZI ,....



..... vyakudhania hasa VISIVYOTHIBITISHWA ,...
..... huwezageuzwa ndio UKWELI WENYEWE!:-(

Swali:
  • SI unakumbuka UDHANIACHO- hata kama  kidhaniwacho ni mheshimiwa hajavaa chupi - hasa kama huna USHAHIDI na UHAKIKA labda bado hicho SIO KWELI?

Ndio,...
.... kuna vyakudhania mpaka kuwa MAREHEMU KAENDA MBINGUNI,...
..... lakini kama hakuna ushahidi,....
....... labda KUDHANIA ni KUDHANIA TU  na  haki ya nani tena labda bado  SIO KWELI HICHO!:-(

Swali:
  • Kwani kuna mtu anauhakika kwa asilimia MIA hata ya  Marehemu alikuwa MTU Mzuri hasa kwa kuwa inasemekana MTU MZURI kwako kama GADDAFI labda kwa MWINGINE ni MBAYA na hafai bila kuruka kipengele cha hatujui mtu anafikiriaga nini na nasikia mambo mengine hata  KIFIKIRA ni dhambi au tu misingi ya UTU UBAYA? 
  • Kwa kudhania kila MAMA WA KAMBO ni MBAYA si unaweza kuruka MAMA wa KAMBO wazuri kabisaa?
  • Si inasemekana hata WACHAWI ni washikaji tu wakawaida kiutu uzuri  MCHANA ila usiku fulu KUKUWANGIA au kipopobawa kunajisi watu kitu ambacho kwa KUDHANIA kama wewe hupainao UNGO usiku unawezafikiri ni WATU wazuri tu?

Ndio,...
... mie NADHANIA ni bora niachie HAPA hii taralila!:-(
Na ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
SIKU NJEMA!:-(




Hebu mutoto wa Afrika KEZIAH JONES ambaye nimiongoni mwa wanamuziki watokao AFRIKA niliowahikugongana nao mitaani nchi za magharibi ambaye haachi kunikosha roho aanzishe upya kwa kurudia-Million Miles from Home



KEZIAH JONES adinye tena pia - MY KINDA GIRL




Keziah JONES a -Familiarize



Keziah Jones amwage tena  - So Much Trouble in the World





Ndio huyu huyu mdau akumbubshie- Blufunk Is a ALIVE



Kabla  tu hajamalizia tena  kwa-Beautiful Emilie




Read more...

Kama MWEUSI na uko LIBYA chamoto utakiona sasa hivi!:-(

>> Tuesday, August 30, 2011

Ukionekana MWEUSI LIBYA,...

.....maana yake ni kuwa UNAMFAGILIA  papaa GADDAFI,...
.... na tafsiri yake ni kifo njenje chini ya  hawa wanaosaidiwa na NATO!:-(

Deku KIDUCHU waliokumbwa,...


Read more...

Kuna wanunao na HAWAJUI wamenunia nini,....

.... kama tu kuna WAMCHEKEAO MTU lakini labda ukweli,....
.... ASEMAVYO huyo MTU havichekeshi,...
... hawajui kiwachekeshacho ni nini!:-(

Swali:
  • Unauhakika mtu akianguka wachekao wanauhakika kiwachekeshacho ni ninni?
  • Kwani hujawahi kuamka umenuna na HUNA UHAKIKA na  sababu ikununishayo na unadai tu umeamka vibaya?


Wait aminute,...
..... kumbuka tu ujisikiavyo UKIWA na FURAHA, unahuzuni, unajisikia UMEPENDA eti MWENYEWE limtu fulani,..
....au tu swala la kuwa pamoja na kuwa kuna  MINUSO ya EID wewe husikii njaa,.....
..... jua tu kuwa YOTE ajisikiayo MTU ni matokeo tu ya MAKEMIKALI mwilini yalivyo JIPANGA hata kama hayo utayaita MAHOMONI, tindikali,.....


....au samahani tuangalie MAKEMIKALI kwa ung'eng'e  hata katika mfano wa ni kwanini JIMBWA la POLISI likitokea unaweza kujikuta umetoka BARUTI bado ni mchezo wa kemikali ambao hata ukiutafuta kwenye nukuu hata zile zisizoza  vyanzo vya uhakika sana utakuta wanakusimulia jinsi ni MAKEMIKALI yafanyayo ujisikie kutoka BARUTI au KUBAKI tu chumbani na limtu LILILOKUTISHA na KITU katika ndude ziunganishwazo na ADRENALINE RUSH ikimaanisha :

Adrenaline rush refers to an activity of the adrenal gland in a fight-or-flight response, when it is releasing adrenaline (epinephrine). When releasing adrenaline, one's body releases dopamine and can act as a natural pain killer. A chronic hyper-adrenaline is a common symptom of an anxiety disorder, but in some cases, it may be due to pheochromocytoma, a tumour in the adrenal medulla. An adrenaline rush causes the muscles to perform respiration at an increased rate improving strength. It also works with the nervous system to interpret impulses that trigger selective glands.

Ndio,...
.... kaung'eng'e hapo juu ni kakustua tu jinsi gani ukiogopa mpaka unaogopa tayari kuna mpaka adrenaline  na dopamine katika mfumo wa mwili wako ambazo ni baadhi tu  ya  kemikali vimiminika vigusavyo jinsi unavyo jisikia ingawa kwa undani  swala hili ni la kitabu kizima na sio sentensi moja.

Sasaa :
  •  Si unajua hata ili uote titi  pia ni MAKEMIKALI yanahusika na MWANAMKE  unaweza kumuotesha NDEVU kwa makemikali tu aka HOMONI kama utacheza nazo vyema ?
  • Si unajua kuwa hata hasira, nyege au tu uume wa beberu kudinda yote ni michezo ifanikiswayo na  makemikali ndani ya mwili wa kiumbe hicho?
  • Kwani unafikiri hata hisia zako katika dini hasa zile za ni jinsi gani unaweza kubadilishwa dini kirahisi kuliko wengine hazina uhusiano na UWIANo wa makemikali hata kwenye ubongo wako uwezao kufanya kama yafanyikao kwa wale ambao katika mtongozo ni maji mara moja?


Ndio,...
...... kuna WAKUCHEKEAO bila sababu ,...
..... ingawa pia inawezekana unajua KUCHEKESHA hata kwa kuwa uongeayo ukiwa siriasi ndio KICHEKESHO kama unashangazwa na wachekao wakati wewe uko siriasi!:-(



Na ndio,...
.... ni makemikali MWILINI mwa MTU yasaidiayo kufanya anayependa ajisikie anavyojisikia AKIPENDA.:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na wala USIKONDE!:-(



Hebu Offside Trick na Hammer Q warudishe -Dege




Franco na T.P. OK Jazz waingilie kati kidogo kwa-Simba Nkoni



Eddie Murphy na Shabba Ranks waingilie nakubadili muelekeo wa mchezo mzima kwa- I Was A King



Shabba Ranks na KRS One wabadilishe muelekeo zaidi kwa - The Jam



Au tu KRS 1 amalizie tu kwa -Sound of da police

Read more...

EID MUBARAK kwenu WOTE! Inshaallah kuleni EID MWANANA waislamu WOTE!



Awatakieni KHERI,...
.... ni mie SIMON KITURURU.

Read more...

Unavyokifikiria UNACHOKIFIKIRIA sasa hivi hata kama ni MKE wa JIRANI,....

>> Monday, August 29, 2011

.... labda  hutakifikiria hivyo tena MAISHANI,...
.... hata kama KIJINA unachokifikiria ukikifikiria tena kesho ni HICHOHICHO,...
.... mwendo wake kama bata!:-(

Swali:
  • AU?
  • Si unajua labda wakati unafikiria huwa unasahau kustukia jinsi unavyofikiria?


Ndio,....
.... labda kama hujastukia  kustukia ufanyacho ni KUFIKIRIA,....
...... wengi hawastuki kuwa wanafikiria  na kwa hilo hata waufikiriavyo MLENDA MWAKA juzi hawatastukia ni tofauti na waufikiriavyo MLENDA  leo!

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu tu Miguel arudie ghafla  - Quicke



Musiq SoulCHILD arudie - Halfcrazy



Musiq Soulchild aongezee dozi kwa-BUDDY





Dwele aingilie kati kwa kudai tena-I'm Cheatin´



Au tu tena Slum Village wamalizie kwa - Tainted


Read more...

EMU THREE aka Muzee wa STORI katika kuhojiwa!



Karibuni katika mahojiano yetu ya kila week. Week hii nimepata bahati kufanya mahojiano na Emu Three ktoka blog ya Diary Yangu. Kama wewe ni mpenzi wa riwaya natumaini mara ukiifahamu hii blog kila siku utajikuta utarudi kusoma hadithi moto moto anazoziandika Emu Three.

Karibu hapa na tunafurahi kuweza kufanya mahojiano na wewe. Unaweza kutueleza kidogo kuhusu wewe na blog yako?
Mimi naitwa emu-three, na nimetumia emu-three kama ufupisho wa majina yangu matatu yaani jina la kwangu la baba na la ukoo yote yakianzia na herufi M. Na wakati naanzisha hii blog, nilikuwa nawaza niweje jina gani , na mara likanjia jina hilo la miram3. Mira ikiwa ni jina langu halisi kwa kifupi na m3, ikiwa M.M.M.

Je blog yako unatumia jina lako kamili au unablog kwa kutumia kivuli kingine na watu wanasoma na kuenjoy blog yako lakini hawajui wewe ni nani?
Blog yangu situmii jina langu kamili, natumia jina la kubuni tu `nick-name’, na watu wananitambua kama emu-three, kama nilivyosema awali kuwa ni kifupisho cha majina yangu matatu. Sina nia mbaya kutojiweka jina kamili na picha yangu, ila nililenga kuwa ninachokiandika ndicho kinieleze mimi. Nia ni kutoa kile nilichokuwa nacho, lakini ikiwa ni muhimu sana nitaweka picha yangu na kujielezea zaidi, hapo wapenzi wa blog hii watakapokuwa wengi na kupendekeza hivyo.!

Ni miaka mingapi sasa umekua ukiblog?
Nina miaka mitatu sasa tangu blog hii ianzee kuwa hewani, mwanzoni na nilituma nianze kublog, kwani nilituma maelezo ya mwanzo kabisa kama utambulisho tarehe 14-7-2009.

Ni nini kilikufanya uanzishe blog?
Mimi ni mpenzi sana wa kuandika hadithi, kuweka kumbukumbu za matukio(diary) na napenda sana kusoma vitabu vya hadithi, hasa riwaya(novels) , tamithiliya nk. Nikawa naandika visa, au hadithi katika makatasi, na mwisho wa siku hayo makaratasi yanapotea au kuharibika, nikawa naandika kwenye computa za ofisini, nazo zinakumbana na virusi, au unaondoka kwenye hiyo kampuni na ina maana kila kitu kinamepotea. Nikaja kugundua kuwa kumbe kwenye blog unaweza ukaweka hizi kumbukumbu, za visa, hadithi nk na sio kuweka tu, bali unaweza kupata watu wakazisoma, na mkachangiana mawazo. Na kwa vile nia yangu ilikuwa sio kuandika tu, bali pia kutoa maoni yangu, kushauri,nk kuhusu hili na lile, nikaona blog ni sehemu nzuri kabisa. Kwa mfano mimi ninaamini kuwa kuwa kila tukio lazima lina na sababu, basi kwanini nisiweke hayo matukio na kuanisha nionavyo mimi ni sababu gani likatokea kwa kupekenyua chanzo chake, na hatimaye iwe kama kisa ambacho sio burudisho tu, bali kiwe na mafundisho ndani yake!

Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby?
Kwakeli kublog niliichukulia kama Hobby, na nina kazi nyingine inayonifanya niishi mjini, na kama utachunguza blog yangu haina hata matangazo ya kibiashara, sio kwamba sipendi, bali sijawapata watu wa kutangaza biashara zao. Kama kuna atakayependa kuweka tangazo lake namkaribisha sana. Kwa ujumla natumia muda wangu wa ziada, gharama zangu mwenyewe, na nashukuru kuwa naweza kutumia vitendea kazi vya muajiri wangu kuweza kufanikisha hili, ingawaje ni kwa shida, na vinginevyo nategemea sana internet cafe.

Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog?
Changamoto ni nyingi, kwanza kama nilivyosema awali muda mwingine nategemea sana vitendea kazi vya muajiri wangu, kama computa na internet ingawaje najitahis sana kutokutumia muda wake wa kazi, ninachofanya nikuwahi asubuhii sana na kuandika kile nilichokusudia kabla ya muda wa kazi, na zaidi sana natumia internet cafe. Kwahiyo swala la muda, gharama na vitendea kazi ni changamoto kubwa kwangu kwa sasa. 

Ni nani wasomaji wa blog yako?
Ni wote hasa wale wanaoutumia lugha ya kiswahili, ingawaje wengine wanaweza kutumia nyezo zilizopo kwenye blogs, kutafsiri kwa lugha zao. Matarajio kama ningeliweza, nilitaka iwe kwa lugha mbili ya Kiswahili na Kiingereza, ili wengine waweze kutafsiri kwa kirahisi kwenye lugha zao kwa kupitia kwenye lugha ya Kiingereza.

Ni nini imekuwa mkakati wako kwa ajili ya kujenga kujulikana kwa mwenyewe na blog yako zaidi?
Hilo pia limekuwa ni moja ya changamoto kwangu, kwani nimejulikana labda kwa kupitia kwenye blog nyingine ambazo wamenisaidia kuniweka kama blog rafiki, na wengine wamekuwa wakiambizana, na kuweza kuwavuta marafiki zao kuja kusoma visa kwenye blog hii, nawashukuru sana kwa hilo. Kama ujuavyo, watu wengi sasa hivi hawapendi kusoma, wanapenda zaidi kutizama, na kwahiyo mtu akiona umeandika taarifa ndefu, na haina hata kivutio kama picha anaghairi. Kwahiyo mkakati wangu ni kuiboresha hii blog, iwe ya kisasa zaidi, iwe sio tu kusoma, bali hata kutizama pia. 

Je unatumia mitandao mingine kama Twitter au Facebook kuitangza blog yako? Kama unazo unaweza kutuambia ili wasiofahamu waweze kufahamu na kukufuata?
Ndio natumia Facebook, hata Twitter, kwenye Twitter unaweza kunitafuta kama `emu-three’ lakini kwenye face book unaweza kunipata kama `diary yangu’
 au http://miram3.blogspot.com/

Je ni nini mkakati wako na blog yako kwa ujumla?
Mkakati wangu ni kuiboresha hii blog kuwa ya kisasa zaidi, na kuweza kuingiza e-book, kweny hii blog, nikipata wataalamu wa kunisaidia nitashukuru sana, na kwa vile leng ni kuwa mtunzi wa vitabu, basi blog hii itakuwa sehemu ya kujitangaza pia. Na ikiwezekana nisiifanye blog tu kama hobby, lakini iwe kazi yenye kuleta manufaa, sio kwangu tu hata kwa jamii kwa ujumla. 

Ni jinsi gani (mtu) anaweza kuelezea style/theme ya yako unavyo blog?
Mtindo wangu wa kublog unaweza kuelezewa kama blog ya visa vya kusisimua kutokana na matukio halisia. Ni kumbukumbu za kimaisha, kwani visa ninavyotunga ni vitu vilivyotokea na mimi naviboresha tu ili viweze kumsisimua msomaji.

• Je ni bloggers wapi ambao wewe unawaangalia na kufuata nyayo zao? Na kwanini?
Kwakweli kublog kwangu siwezi kusema nafuata nyayo za mtu fulani, sikumbuki kuwa nimeblg kwasababu ya mtu fulani, hapana, mimi nilipogundua tu kuwa kuna kitu kama hiki na unaweza kuweka vitu vyako bure, nikajimwaga, sio kwa ushawishi wa mtu, lakini wengi tu napenda blog zao, ikiwemo hii yako, na mimii huwa napenda sana kusoma walichoandika wenzangu, na nina imani kuwa kitu kipya ni kile hujakiona, kwahiyo kila blog ambayo sijaiona kwangu inanisismua kuisoma,na kuona mwenzangu ana nini katika mawazo yake! 

Je unafikiria kuwa unadaiwa na mtu akiacha comment/s kwenye blog yako?
Kuna jambo moja tuliweke akilini, mfano mtu akiweka comment kwenye blog yako, lazima atakuwa na shauku fulani, hasa iwe ya kuulizwa swali, ...au hata kama inakukwaza yeye atakuwa na matarajio fulani kuwa wewe mwenye blog unaweza kwa kutumia blog yako kumsaidia au kumsikia. Kwahiyo ni bora ukasema lolote, au usiitie kapuni, kwani ukifanya hivyo bila kuiweka hewani au bila kusema lolote, utakuona kama umemdharau, kwakweli ni deni...utakuwa hujamtendea haki mpenzi wa blog yako. Na pia kwa wale wanaosoma habari kwenye blog, ni busara pia ukasema lolote, kwani ni kama mtu kakupa kitu ukae kimiya,..ni busara kusema ahsante ...kwahiyo.unaweza hata ukaandika neno dogo tu la kushukurui au ukaandika `mmmh’ inatosha kabisa, ni maoni yangu tu.

Je kuna thamani kujibu comment iliyoachwa kwenye blog yako wakati ukijua kuwa huyo aliyeiandika labda hatarudi kusoma jibu lake tena?
Ukiulizwa swali ni vyema kulijibu, kwasababu mara nyingi ukikaa kimya unatafsiriwa kuwa umezarau au sio, kwahiyo kinachotakiwa ni kulijibu lile swali, kwani muulizaji anaweza kuwa aliuliza hilo swali kwa maslahi yake, lakini swali hilo linaweza likawa limesomwa na watu wengi na hata kuwagusa watu wengine, kwahiyo kama yeye hakurudi kusoma majibu ya hilo swali watafaidika wengine, walioguswa nalo.

• Je wewe ni mtu ambaye uko rahisi kukata tamaa?
Hapana mimi spendi kukata tamaa, kwasababu sisi tunaishi na kilichokukatisha tamaa kinaweza ikawa sababu ya kukupambanua ubongo wako ili ufikiri zaidi. Cha muhimu ni kutafuta kwanini, na baadaye utagundua hata kile usichokitarajia kwani wanasema tukio hutokea ili iwe sababu, na hicho kinachmfanya mtu ajisikia kukata tamaa, ni moja ya jambo, ambalo halijatokea hivi hivi, ushauri ni kupambana hadipumzi ya mwisho!

Ni nini baadhi ya malengo yako ya mwaka huu kwa ajili ya blogu yako au unaonaje mwenyewe kwa kipindi cha mwaka mmoja ua mitano toka sasa hivi blog ya itakuaje?
Malengo ni mengi, lakini unapoigusa blog, utagundua hii ni nyanja inayokuwa, kila siku kunatokea mabadiliko, ni kama mwanablog unatakiwa kujifunza kwenda na wakati. Tatizo ndio hilo utafanyaje... Kwahiyo lengo mojawapo ni kuiboresha blog hii, ili niweze pia kutoka kwenye hobby tu, na kuingia kwenye kublog kama kazi, na ili nitoke kwenye kumtegemea muajiri nifikie kwenye kujitegemea mwenyewe kwani kuna kesho na leo. Na nina matumaini makubwa kuwa kwa kupitia blog hii niweze kuwa mtunzi bora, na hata blog hii kuwa miongoni mwa blog..

• Je upi ujumbe wako kwa wale watu wanaotaka kuanza kublog?
Kwa wale wanaoanza kublog, ushauri wangu ni kuwa kublog ni rahisi sana, kwani ni bure, muhimu ni muda wako tu, na kupangilia nini unachotaka kuwaambia wenzako, na unapoutoa ujumbe wako pia ufikiri mara mbili ,usiweke ujumbe wenye madhara, kwani watakaosoma ni wengi, wa rika tofauti, dini na mataifa mengine, kwahiyo ujaribu kublog ukiwa na uoni kuwa haitaishia tu kwa wale uliowalenga, itafikia hata wale usiotarajia kuwa wataisoma blog yako.

• Je kwa maoni yako ni lipi lengo kubwa kwa mwanablogger?
Lengo kubwa kwa mwanablog ni nini unachotaka kukitoa kwa jamii, nini ulichokusudia na ukijua hilo wewe anza kuweka hoja zako, kwani hoja huzaa hoja. Blog sasa ni kama vijiweni, ukiwa na jambo lako jema, litoe, huwezi jua, ukiwa na matatizo yako yatoe, huwezi jua...unaweza ukapata msaada mkubwa sana, kwahiyo lengo ni wewe mwenyewe tu!.

Kuna jambo lolote ambalo hatukuliuliza na ungependa kuwaeleza wasomaji wa blog yako?
Labda maoni tu kwa wanablog mbalimbali. Mimi kama mzazi limekuwa likiniuma sana, ni sawa kila mmoja ana malengo yake, kila mmoja ana utashi wake, lakini lazima mtu ufikie na kujiuliza kwa kina faida na hasara kwa anachokifanya., lazima ujiulize hivi hiki ninachokifanya kitajenga au kitabomoa.
Kizazi kinachokuja kinategemea sana msingi wa kizazi kilichopo, na busara yako ndiyo itakayojenga, kama tutasema hewala, kila mtu ana akili yake, tutakosea, wapo watoto wadogo ambao hawaajui jema na baya, wanapupa ya kuiga, sasa ni vyema lile tutakaloliweka hewani liangale hiki kizazi,....natumaini ujumbe huu utaeleweka bila kutafsiri zaidi.

Nakushukuru sana kwa kunitupa fursa hii na sina cha kukupa zaidi ya kukuombea heri na fanaka katika utendaji wako, kwani wewe umekuwa mtu wa watu. Kujali wengine, ni kazi kubwa sana, inahitaji moyo, wewe hili umeliweza hilo, shukurani sana.

Asante sana Emu Three Kwa kufanya mahojiano haya na sisis na tunakutakia mafanikio mema katika blog yako.



Waliomuhoji ni hawa huku TANZANIAN BLOG AWARDS,..
..... nakiri nahusudu sana tu kazi zake  huyu MKUU!

Read more...

Umuhimu wa MTU mmoja utegemeavyo angalau MTU wa PILI hata katika yale ya utunzi wa MIMBA!

>> Sunday, August 28, 2011

Na hata katika swala la ``Kwaniniiii?´´katika  MTU MMOJA ,....

........mara nyingi JIBU LAKE labda sio lile  ``Kwa sababu´´ ila ni lile mbele ya SABABU za mtu zaidi ya MMOJA!!:-(


Na ya MTU mmoja,....
.... hata kiulevi, udokozi wa mboga ,USHIRIKINA  au tu hata ULOKOLE ukiyafuatilia,....
..... unaweza kukutana na yazaidi ya ya MTU mmoja yaliyofanya au KUMJENGA huyo mtu MMOJA,...
.... kuwa MWALIMU mzuri au  hata MCHIMBA makaburi vizuri!.



Swali:
  • SI unajua labda wadaio wamejifunza kitu peke yao labda kuna BAADHI ya misifa wamejizidishia tu?
  • SI unajua labda kuna sababu inahitajika MIJUSI  angalau miwili ili MIMBA  YA MJUSI itungwe?

Na kwa kuwa hata katika ya MTU MMOJA yake binafsi,....
.....``UNAJUA?´´ jibu lake  ZURI  labda  sio lile ``NAJUA ´´ au ``SIJUI´´ bila kuhusisha ujuzi wayaliyofunzwa na WATU wengine...

......... labda bado ni lile mbele ya AJUAYE na ASIYEJUA hasa mbele ya neno `` NAJUA au SIJUI,...
.... ambalo laweza kutoasiri hata ya MJUZI mzuri wa hata kupika MAGIMBI ,....
.... unatokana na hata ambacho hakikiri,...
....kile alichostukia kwenye uchemshaji wa MAGIMBI wa WACHEMSHAJI wengine ambao kivyake ni KIBAYA.:-(


Swali:
  • SI umestukia  kirahisi unaweza kuchukulia   neno kama ``NAJUA´´ kama ndio ujuzi kikweli wa adaiye KUJUA wakati kujua au kutojua ni zaidi ya NENO na labda hata hilo neno ni matokeo ya kujifunza neno  hata hilo ``NAJUA´´ kutoka kwa MTU MWINGINE?

Ndio,...
..... labda jihadhari na adaie haraka anajitegemea katika  KUTOJUA au KUJUA,...
.... kwa sababu kuna NENO na  kuna TENDO lirahisishalo UMAHIRI wa MTU hata katika yakudai tu  ujuaji au tu utojua,.....


...........kwa kuwa MTU HUYO hapo inawezekana anajiamini UJUAJI ni kitu ndani ya MTU MMOJA na ndio maana kikujitegemea NENO ni rahisi kutamkwa ,...

..... ingawa hata UPISHI wa WALI wenye MPISHI mmoja kumbuka ukifuatilia mchele mpaka MPUNGA,chumvi, maji mpaka MAFUTA YA KUPIKIA  kama tu ukifuatilia  NDEGE IPAAYO yenye mpaka KIYOYOZI na bonge la MUZIKI ndani ya SAFARI ijengwavyo waweza kukuta yahitaji ujuaji wa zaidi ya MTU MMOJA ambao labda ulichangiwa na baadhi ya wasiojua pia.:-(

Swali:
  • SI unajua hata siasa ya KUJITEGEMEA ya RAIS NYERERE ilihitaji uwepo wa zaidi ya MTU MMOJA?


Asanteni wote ambao kwa kuwa UWEPO wenu hata hapa kwenye BLOGU hii,....
.... ndio hasa kisa labda hata UJINGA WANGU  kuna ambaye mchango wake ni kustukia,..
....  ee bwana hili lijamaa SIMON KITURURU, ....
......JINGA KWELI!:-(



Ndio,....
.....MKUU labda lakini hata ukuu wako ni kwa sababu kuna zaidi ya mtu MMOJA hapa DUNIANI,.....
.... na ni kweli MTU mmoja ni MUHIMU ila labda hilo haliondoi ukweli ya MMOJA labda huhitaji uwezeshwaji na MTU mwingine!:-(




NI WAZO tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu twende MSUMBIJI ili TOFO TOFO wacheze muziki kidogo,...
....



Au tu TOFO TOFO waendelee kwa kumfundisha MKE wa JAY Z   jinsi MSUMBIJI ngoma inavyochezwa,...





 Vitali Maembe arudishe usiriasi wakati akidai-AFRIKA ni SHILINGI TANO




 Vitali Maembe amalizie kwa kuongele hizi-Hotuba





Kabla REMMY ONGALA hajadinya tena-CAROLLA



Read more...

MOYO labda WASINGIZIWA mengi na WATU ,....

..... kwa kuwa ni UBONGO hasaa ndio kisa,...
..... watu WAMEJIPENDEA /jifia  hata yule umuonaye kuwa ni FALA ,mbaya halafu ananuka  ananuka kinyesi  pia kwa mbaali!:-(

Swali:
  • SI inajulikana ni UBONGO ambao ndio wenye mchezo MZIMA karibu kivyote hata katika kuelewa na KUJIELEWA kitu ambacho chaweza kuchangia mpaka kwanini unafikiri NGURUWE ni mzuri ila nyama yake HARAMU?


Ndio ,...
.....labda MOYO wasingiziwa tu,...
.... kwa kuwa akupendaye anaweza akawa anakupenda kwa kutumia UBONGO na sio MOYO,...
.... na UBONGO unastukia POCHI , ufala wa afaaye kuchunwa BUZI mpaka yule atakaye saidia wakati MSAADA hata wakuwa ndugu ya Rais NYERERE kisiasa  utakavyo hitajika.

Swali:
  • Unabisha?
  • Kwani hujui kuna wapendwao na wachukiao matege kama NYUMBA, cheo na MAGARI yao hao walengwao kwa kuambiwa ``WANAPENDWA KWA MOYO WOTE ´´ hao ambao ni  wenye MATEGE ?

Ndio,...
... inawezekana hata kwa WATANZANIA,...
...... Tanzania hupendwa kwa akili na sio MOYO,...
.... na ikibidi  wataiita AFRIKA MASHARIKI kirahisi tu KIAKILI!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA !
JUMAPILI NJEMA!


Hebu Lupe Fiasco aingilie kati kwa- Daydreamin'



BWANA abadili kidogo kwa-Take It Slow



Au tu Safari Sound Band warudie tu kuturudisha KENYA kusiko na matata kwa ndude - Jambo


Read more...

Kilichonigusa kunako leo: SO U are from TANZANIA !Do U still kill albinos THERE?

>> Saturday, August 27, 2011

Ni swali ambalo,...
..... nilidungwa leo na MDAU wakati nasubiri msosi kwenye KIMGAHAWA cha WASURINAME /wadau watokao Republic of Suriname hapa mjini Amsterdam na MMAREKANI ambaye akumbukacho kutoka TANZANIA sio SERENGETI wala kuna DHAHABU ,...
.... bali ni kuwa TANZANIA wanaua MAALIBINO,...
.... Uganda wanaua WASENGE,...
.... na Mlima KILIMANJARO uko KENYA.

Naendelea KUWAZISHWA kidogo na SWALA HILI!

Swali:
  • Ushawahi kukutana na SWALI ambalo ukajistukia katika kulijibu UNAJIELEZEA SANA  katika kuelezea HALIHALISI  kuliko  kawaida?
Mambo mengine ila ni SHWARI mitaa hii ,...
.....hasa nikiifananisha na MIJI lukuki MINGINE niliyowahi kuitembelea ULAYA..
...hasa katika kutojali rangi za watu  kitu kifanyacho kirahisi unaweza kujisikia uko nyumba ndogo.:-(


SIKU NJEMA!


Hebu ALBINO FULANI aongezee dozi kwa - Barua Kwa Mama



Au tu Albino Fulani arudie  tu na panga-NAFASI




Read more...

``Halafu nikajisikia vibaya kwa kuonja TAMU ila ni ile HARAMU´´-hata KISTORI!

Kuna wajisikiao VIBAYA kwa kuwa tu WAMEJISIKIA vizuri,...
..... kwa kufanya au KUONJA waliyojifunza kuwa ni MABAYA.

Swali:
  • SI unajua ASIYEPENDA hata UGALI WA MUHOGO anaweza kufunza mtu mwingine kuamini UGALI wa MUHOGO ni MBAYA?

NDIO,...
..... labda yawezekana ni MUHIMU kukumbuka labda mengi yawafanyao WAPENDAO kujisikia vibaya baada ya KUONJA hata kama hapa hatuongelei wale waonjao KIDUDE haramu kisa hakijabarikiwa bado na SHEKHE ,mchungaji au ASKOFU ,....
.... yasemekana MABAYA na imani ya nini KIBAYA mara nyingi ni MASWALA tu ya KUJIFUNZA hasa kama hayo mabaya ni yale yasiyo sumu kikuua MTU.:-(

Swali:
  • Unafikiriri ni vitu vingapi kwako ni VIBAYA kisa tu UMEFUNZWA kuamini ni VIBAYA bila kushuhudia UBAYA wake?
  • Na sinasikia pia BANIANI ni MBAYA ila kiatu chake ni DAWA kitu ambacho kinaweza kutetewa na kufikia kumfanya mtu afikirie labda BANIANI sio mbaya hivyo kama kiatu chake kwako ni ASPIRINI?


Ndio,...
.... kuna waonjao hapa DUNIANI na kufurahia LADHA ya WAONJACHO,....
..... ingawa hujisikia vibaya baadaye hasa kwa kuwa wamependa walichoonja ,...
... ila bdo hata kama LADHA ya hicho KINANILII ni TAMU ,...
.... bado ni HARAMU.:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
JUMAMOSI NJEMA!







Hebu Hawa Pullo abadili kwa - Pulaku



Salif Keita na Cesaria Evora wasibadili sana mwelekeo aliotupeleka HAWA kwa-Yomore





Baaba Maal arudishe ndude- Niiwa




Kabla Salif Keita hajamalizia kwa ndude - Africa



Read more...

Wengi wenye uwezo wa KUSIKIA VIZURI ndio waongozao kwa KUTOSIKILIZA MTU hata wakitongozwa!:-(

WENYE uwezo wa  KITU,...
.... yasemekana HUJIAMINI  ZAIDI kitu kifanyacho,.....

..... mara nyingi  wanaingia UDHAIFU wa kutotumia kipaji walicho nacho vizuri kama wale ambao  wana UWEZO MDOGO na ili wawe MAHIRI na KITU inabidi wafanyie kazi  sana kumasta hicho KITU!

Swali:
  • SI umewahi kusikia KIPOFU kama STEVE WONDER akiongelea hata kwenye nyimbo zake yale asiyoyaona kama vile ya uzuri wa MSICHANA MZURI awezavyo kuwa mahiri wa hata wa kusimulia UZURI  wakati unajua hajawahi KUONA?




Ndio,....
.... na kwa kuwa pia UNAONA VIZURI,...
..... labda hicho ni moja ya KITU kikigezo kifanyacho HUANGALIII VIZURI VITU,...
.... kitu kiwezeshacho kuna uwezekano utafutacho hata LEO umekipita kwa kuwa HUANGALII VIZURI kwa kuwa tu unaamini UNAONA VIZURI.:-(

Swali:

  • Kwani huamini kuwa ni kweli WASIOONA VIZURI ndio hasaaa wenye jitihada zaidi ya KUANGALIA VIZURI hata uzuri wa PKIPENGELE ambacho kinaweza kuwa sio PAJA?

NDIO,...
.... tukiacha mengine,....
......labda ni KUJIAMINI  kwa WAONAO na WASIKIAO VIZURI,....
... ndiko ambako kunachangia WAONAO kutoangalia na WASIKIAO kutosikiliza WANAAMBIWA NINI.:-(

Swali:
  • Si unajua KUSIKIA na KUSIKILIZA ni vitu viwili TOFAUTI?
  • Na si unajua KUONA na KUANGALIA ni vitu viwili TOFAUTI?

Ndio,...
....ni wazo  TU HILI MKUU!


Hebu Gregory Isaacs aingilie kwa -Dance This Reggae Music



Gregory Isaacs akumbushie ya - Slave Master




Gregory aingizie ya -Night Nurse



Gregory Isaacs asiondoke bila kuachia - My Only Lover




AU tu hebu MAKASSY abadili mchezo mzima kwa kuturudisha Tanzania kwa ndude -MAMBO BADO



Ndio bado,...
... nakatiza hapahapa Amsterdam!:-(







































Read more...

Ukikaa sana na walio UCHI hata kama wewe umevaa kificha nyeti/ NGUO,....


... yasemekana utaanza kuonekana kama hao WALIO UCHI ,....
......utaanza KUFIKIRIA kama haohao unaokaanao ambao wako UCHI,...
.......na mwisho utaanza KUJISIKIA  kama walio uchi kabla ya wewe mwenyewe kuanza nawe kukaa UCHI!:-(

Swali:
  • Si unajua hata ukikaa sana na walio MALAYA unaweza kujikuta umeuzoea UMALAYA na labda kuanza kufanya UMALAYA wewe mwenyewe bila kustukia ufanyacho ni UMALAYA?
  • Na si inajulikana kama unataka MOTO wako wa KILOKOLE uendelee kuwa kilokole labda ni busara kujichanganya zaidi na WALOKOLE kwa kuwa unaweza kuyeyusha hata USWAHILINA kama wewe ni MSWALIHINA ila ni yule ashindaye na wasioamini ya KISWAHILINA?


Ndio,...
...... labda kama unataka sana KUELIMIKA,...
..... labda jichanganye SANA na WALIOELIMIKA,...
.........na kama unataka usijizoeshe DHAMBI au tu kukaa uchi kwepa kujichanganya sana na waliodhoea kufanya dhambi au tu kukaa uchi,...
.... kwa kuwa hata yale UYAONAYO NI ya AJABU huzoeleka ukijichanganya sana na walioyazoea.

Swali:
  • Si yasemekana hata KUUA kunazoeleka na aliyewahi kuua MARAMOJA kurudia kuua mtu sio shughuli kubwa sana kama ilivyokuwa mwanzo?


Ndio,...
.... ukikaa sana hata JALALANI,...
..........nasikia jalala litaanza kuzoeleka pia AISEE!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!





Hebu  Israel Vibration waingilie kati kwa kudai-System not working




Burning Spear arudie-AFRICAN POSTMAN



Burning Spear aongezee dozi kwa-African Teacher




Au tu Culture wabadili tu kwa - Peace, Love & Harmony



Ndio nipo AMSTERDAM ,Uholanzi ..
.... na kwa bahati mbaya nakatizia denge maeneo pia :-(







































Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP