Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Swala la KAMA huna PAPARA usihofie TUSI!

>> Friday, February 27, 2009

Lakini,...
....LABDA KAMA HUNA papara, TUSI utukanwalo kama KWELI ni tusi na sio sifa, TUSI utukanwalo HUNUNA zaidi.

Swali:

  • BADO unamshangaa APAPARIKAYE na TUSI wakati nyuma ya tusi kuna SIFA ya mtu?


WIkienDI NJema!
Tutulie na Aaliyah- At Ur Best.


Au ngojea Inner Circle wazungumzie - Sweat

Read more...

Wakati UNAENDELEA kupenda sehemu za SIRI za mwenzio!

>> Thursday, February 26, 2009

TATIZO ...
...... la afanyaye SIRI ni kufikiri au KUDHANIA kifikiriwacho ni siri ni kweli NI SIRI, au labda NI SIRI.

WAKATI....
.... unaficha siri, KUMBUKA unawaficha wasio na JUHUDI za kutaka kujua SIRI yako ni, NI nini, au TU unajaribu kuficha ambacho si siri kwako ili kiwe kwa wengine SIRI.

KUNAUWEZEKANO,...
... siri yako wanajua ambao HAWAJUI unafikiria kuwa HIYO ni SIRI.


LABDA,...
... siri yako si SIRI ndio maana wewe MWENYEWE umeistukia na kuipa jina SIRI au kufikiria LABDA KWELI ni SIRI.

WAKATI...
.....unaficha SEHEMU za siri , kumbuka kuwa ni ukweli asilimia kubwa YA ambao hujui sehemu zao za siri unajua WANAZAA au KUZALISHA na labda unajua watoto wao , NA si SIRI.
Swali:

  • Ukiona watoto wa MWENYE siri ,SI unajua kuna MTU anajua sehemu zake za SIRI?
  • Unauhakika una siri au hujui ajuaye yako SIRI?

Naacha!
Hebu twende tena GABON kwa Oliver N'goma katika - BANE

AU ngojea tu Will Smith azungumzie - Miami..

Photobucket


Photobucket


Photobucket


Nipo na kama upo Stockholm labda tutakutana.
Nipo kama baadhi za picha zisemavyo....

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Nipo na usafiri upo kama wewe sio MNENE.
Photobucket

Read more...

LINI Tanzania kutakuwa na CHAMA CHA MAPINDUZI?

>> Wednesday, February 25, 2009

Inasemekana TANZANIA ina WANAMAPINDUZI!

Na,...
....TANZANIA kuna WANAMAPINDUZI.
Swali:

  • Unajua chama CHAO?
  • Unauhakika wanamapinduzi wanahitaji CHAMA?


NAACHA!
Tulia twende Brazil kutulia na Zé Renato na Milton Nascimento

Au ngojea BUGLE aseme- WHAT WE GONNA DO...

Read more...

Kama kuna BUSARA za KUJILAUMU!

>> Tuesday, February 24, 2009

Labda,....
.... kama bado unakumbuka kujilaumu kuna uwezekano una UTU!

Kama,....
..... unajilaumu , si lazima lakini kuwa ni wewe wa KULAUMU.
Lakini wakati UNALAUMIWA labda ni kweli kuna kilichofanyika.

Swali:

  • Tokea uzaliwe unafikiri umesahau kujilaumu mara ngapi?
  • Wakati unalaumiwa ni mara ngapi unajua ukweli si wewe ustahilie lawama?


Siku Njema!

Au kama una muda tulia na Faya Tess katika kibao -GINA

Read more...

Labda BASHA ni MSENGE!

>> Monday, February 23, 2009

LABDA,...
....basha MSENGE kwa sababu anakula unacho ONJA!.


Lakini,...
.... kumbuka ukionja maana yake UMEKULA.

Inawezekana unakumbuka bado BASHA na MSENGE wanakula UGALI kama tu asiye TALIBANI.

Wakati....
.... unafikiria kwanini Msenge hajaoa BASHA ,kuna uwezekano unafikiri unajua ndoa.

Na,...
....kunauwezekano kama umefikia kujua ndoa NI nini ,....

.....basi....
....ndoa YAKO imeanza kuharibika au imeshaharibika ndio maana una utaalamu wa ndoa.
Swali:
  • AU?

Lakini,...
.... kabla basha hajaonja bado ni BASHA.

Msenge anapendwa kulalamikiwa kwa sababu ya roho nzuri ya kutoa , ila ukweli ni kwamba hakuna basha kama msenge hayupo.
Swali:
  • Si unakumbuka kuna watu wanahangaikia sana KITU wakati LABDA wahangaikiacho kama hakijaoshwa labda kinanuka Mkojo au mavi?
  • Unakumbuka PADRE, Shekhe na MSENGE ni watu ambao wamebobea kwenye ZAO wafikiriazo waziweza fani?
  • AU?

NAACHA!
Kumbuka NAWAZA tu!
siKU NJema!


Tumtembelee mtoto wa Bob Marley kwa jina Steve Marley azungumzie.. - Rebel In Disguise

Au Ngojea Snoop Dogg na Butchy Cassidy wamalizie kwa kusema - Loosen Control..

ASANTENI WADAU WOTE!
Asante pia kwa wadau ambao tulikuwa wote JUZI ya JANA na kamera yangu ilibahatika kuwadaka kama hawa.....

Photobucket
Papaa Ray a.k.a Raymond Mutafungwa , a.k.a Mkuu wa kikao, ASANTE!


Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket



Photobucket






Photobucket







Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Papaa Ronaldo, ASANTE!

Photobucket





Photobucket

Photobucket

Read more...

INASEMEKANA kuna siri ya KUJUA kama UGALI UMEIVA kabla ya KUUTOMASATOMASA, kuubonyeza au KUUONJA!

>> Friday, February 20, 2009

LABDA,....
......binadamu ni MALIMBUKENI!:-(

Baada ya binadamu kugundua kuna uwezekano wa kupika, wamesahau kuwa MBICHI NYINGI hulika.:-(


Lakini,...
.. ....inasemekana UGALI hujisikia vizuri ukiliwa kwa mkono , na maswala ya kula kwa UMMA au KIJIKO yana uparura tu ugali na kuutia majeruhi ya dondoshayo njiaani utamu, katika safari ya utamu wa ugali kutoka kwenye sinia kwenda mdomoni.

Na....
.....wakati unajiandaa kufinyanga TONGE la UGALI ni muhimu ujue UNAUNYEMELEA ugali wa aina gani.

Kila aina ya ugali, kuanzia wa mahindi, muhogo, ulezi , BILA KUUSAHAU ugali wa unga wa magimbi, kumbuka UNAHITAJI mbinu tofauti ya mashambulizi hata katika KUUTOMASATOMASA, kuushikashika au tu katika KUUTUMBULIA MACHO ugali, hata KAMA safari hii ni katika kutaka kujua tu kama ugali umeiva au bado bila KUUONJA!

Swali:

  • AU?

Lakini,...
...... nisikudanganye kwa kukataa kuwa hakuna WAZOEFU wa ugali hata wa Mbatata ambao wanajua UGALI WA MBATATA umeiva bila KUUSHIKASHIKA, KUUTOMASA au hata KUUONJA. Na sina uhakika kama hawa WAZOEFU huwa wanatumia harufu au ni mbinu gani zaidi katika utaalamu ,na labda hiyo ndio siri ya UZOEFU katika taaluma.

NA TATIZO....
.... la wote wahangaikiao staili za kutaka kujua IMEIVA au BADO, mara nyingi WAMESAHAU tu kuwa WAHANGAIKIAVYO vinalika vikiwa VIBICHI.

Ni kweli kabisa nakwambia kuwa kuanzia;
  • Nyama
  • Nyanya mshumaa
  • Mchele
  • Wali
  • Unga wa mahindi
  • Ugali

AU
  • Nakadhalika kadhaaa,.....
......VYOTE huweza kulika vibichi hata kama huna ujazo wa njaa WAKUTOSHA.

Swali:
  • Si kuna uwezekano bikira mdogo yuko tayari ingawa mkubwa ndio inaaminika kaandaliwa na yuko tayari ingawa naye hayuko tayari ingawa yuko tayari?
  • Unakumbuka kuna mpaka wataalamu wajawazito walao mpaka UDONGO?


SIKUKATAZI!

Endelea tu KUTOMASATOMASA , kubonyeza au KUONJA kama ni kweli HUZIJUI MBIVU HIZI kuwa ni MBIVU hata ukiwa kona ya saba KULE katika mkao wa KUNYEMELEA huku ukiwa na wasiwasi labda ni MBICHI!

Kumbuka kijiweni kuna KIPINDUPINDU lakini, kabla hujafinyanga tonge !

Na nimesikia kuna wenye busara wadaio ukinawa mikono kabla, INASAIDIA hata kwa kuonyesha umejaribu kujiandaa angalau kwa kunawa kabla ya mashambulizi ya tonge.

Labda,...
..... tutumie tu kijiko!
Swali:
  • SI labda ni kweli ukila vibichi utaumwa tumbo?
  • Hivi sijui tutumie tu kijiko?
  • Si utaumwa tu tumbo au kuharisha kama vibichi vinakuumiza hata ukitumia kijiko?

Lakini,....
... Labda endelea kula vibichi kama vilivyoiva hujazoea, USIJEUMWA TUMBO buuure!

Mimi simo!

NAACHA!
Kumbuka NAWAZA tu hapa!



wiKIENdi njEMa!
Twende kidogo kwa Wakyuba kukutana na Orishas wakidai - 537 CUBA



Au tu tupitie tena Jamaica kwa Admiral Tibet, Shabba Ranks & Ninja man enzi hizo , watupunguzie spidi kwa kitu - Serious times

Read more...

JINSI ya kumbembeleza WAZIRI mkuu AKILIA!

Wakati katibu MKUU au mtoto analia,.....
...... kumbuka KUFARIJIKA kwa kujua kwa vyovyote vile hawawezi kulia DAIMA hata kama hawatapewa nyonyo.

Tukumbuke pia,....
...... kuna watu wako kimya ila wanalia KWA NDANI!:-(

Pamoja na mwiko wa jamii usababishao kubwa zima kuogopa kulia hadharani, KULIA NI MUHIMU.

Na USIDANGANYIKE....
... kuwa sababu za watu kulia MSIBANI ni kweli wanasikitika marehemu katutoka.

Kuna watu walikuwa wanatembea na KILIO tokea jana na MSIBA wa leo umewawezesha kuangua kilio HADHARANI au nyuma ya mbuyu, na wala walikuwa hawamjui marehemu na kama walikuwa wanamjua MAREHEMU, ...
......WALIKUWA HAWAMPENDI.:-(




Swali:

  • Unafikiri kubwa zima wakati linalia msibani ni dakika ngapi wakati linalia ndani ya dakika linafikiria jambo jingine lisilo husiana na kilio msibani?

  • Unafikiri toto wakati linalilia pipi likiona lawalawa nyama halianzi kufikiria labda ligeuze kilio cha pipi kielekee kwenye lawalawa nyama?
  • Unafikiri wakati mtu ANALIA anakuwa ameshaanza kufikiria jinsi atakavyo malizia gia ya KULIA?


Kumbuka wakati KATIBU MKUU analia, bado kunyonya kidole ni RUKSA.

Na, ....
.... DAIMA kumbuka watu wanatembea na VISIRANI vyao na wanaonekana wanatembea kwa maringo tu na VILIO vyao ingawa unaweza usistukie na ukiwapa sababu ya KUKULILIA WEWE wanaweza wakachukua nafasi hiyo KUJILILIA WAO na YA KWAO.

Na usipoangalia UNAWEZA kupigwa kibao kwa kumchekea mtu halafu usielewe KWA NINI , kumbe mwenzio alikuwa anavisirani vyake anavifuga tokea MWAKA JUZI na SIKU HIZI kwake KUTABASAMU kwa wengine na KUNG'ONG'A ni saresare MAUA.

Swali:
  • AU?
  • Hivi unafikiri hakuna kitu ambacho wewe ni Rais au angalau ni Waziri MKUU kabla hujalia?
JARIBU.....
........ kujipa ruhusa KULIA leo kama unachakulia LEO, utafaidika kwa kulenga kulilia kilichokuliza na kinachohusika katika ULIZI leo. Ukitunza kilio cha leo unaweza kujikuta UNACHANGANYA VILIO na unalia ya marehemu wa leo na yakuaibishwa mwaka juzi ,wakati sasa hivi unatakiwa ulie kwa sababu ya utamu wa penzi.

Na ikibidi kukasirika leo ,.....
.......KASIRIKA leo yaishe leo!
Usije ukaanza kutukasirikia na sisi leo wakati hasira zako zilipewa ujauzito na bosi wako juzi na pia na LIMPENZI lako mwaka JUZI na sisi hatuhusiki:-(

Na ni kweli,...
....Mila , Desturi na Miiko mingine mingi hata ya kijinga inatusaidia kusababisha tunatunza maumivu na vilio mpaka inakuwa vigumu, mambo yakiwa magumu kujua tulilie lipi.

Wakati unamalizia kulia,....
..... jaribu kukumbuka kujiangalia kama ulifanikiwa kutoa KAMASI ili ulifute kamasi kama lilikutoka katika miondoko yako ya kulia.

NAACHA!
Topiki imenishinda!:-(

Hebu tubadili hali ya hewa kwa kukutana na Michael Leahy labda na kwa mbaaali Mtaalamu RON JEREMY, ili kuuliza-How did you get hooked on Porn?...


Au turudi tu Congo na kukutana na Tshala Muana atukumbushe - Mbombo..

Read more...

Katika kutembelea SHULE ya VIDUDU!

>> Thursday, February 19, 2009

Shikamooo Watoto!

Swali kwa wakubwa:

  • Hivi kwenye SHULE YA VIDUDU umeshawahi kuona WATU?
  • Hivi kwenye shule ya watu kukiwa na VIDUDU Mwalimu MKUU atatoa UAMUZI gani?

Naacha!

Leo nimebanwa kidogo kujazia muda ndani ya siku iliojaa mambo mengi kwa kuandika kirefu-kifupi UjingaBUSARA kama kawaida!:-)

Kesho Basi kama Hatujafa!

Ngojea tupumzike kwa kupata mtazamo na swali katika fantasi ya Mwanadada katika....-Woman's fantasy(Tahadhari kama mtoto au mtoto mkubwa na utakwazika katika topiki)

Au ngojea FAYA TESS atukumbushe kwenda Kenya katika kibao -Nairobi.....

Read more...

STAILI ya kuongea IMSAIDIAYO mhubiri wa dini , labda INA MSAADA pia kwa mtongozaji!

>> Wednesday, February 18, 2009

Katika kila fani wanafani wanastaili zao za kuongea au kushusha kauli KATIKA FANI.

Kama wewe Mkristu, Mkristo ,Mlokole, Muislamu,......., au unatumia tu Waganga wa kienyeji , nafikiri unajua staili ya WAHESHIMIWA WASIKILIZWA katika kumwagia wafuasi KAULI zao hasa za vitisho kabla ya KUAHIDI tamutamu katika FANI.

Mimi binafsi napenda staili ya uongeaji wa kitakatifu wa MAPAPA wa kikatoliki ndani ya fani , na nakiri kuwa huwa wananifanya nijaribu kusikiliza wasemacho ingawa sielewi Kilatini , Kiitali au hata lugha yoyote watumiayo katika kumwaga KAULI kutokana na staili za kumwaga neno kitakatifu zitumikazo katika fani .

Na,...
......katika staili ya kumfanya msichana ajikute anavuta majani au anajikanyaga katika mkao wa nataka-sitaki wa kusikilizia kauli TAMU anazopatiwa na Mtongozaji, inasemekana ukimrekodi anayetongoza utastukia haongei kwa sauti yake ya kawaida.Yuko katika fani.

Na katika fani, hata ukiwa mbali lazima utajua nini kinaendelea watu wawili wakiwa wanapeana kauli hata kama mara hii ni Kijeba anacheza mchezo wa nataka-sitaki wakati MWANADADA anamwaga kauli ya mtongozo ndani ya fani.

Lakini,...
....... binadamu tuko tofauti!:-(


Wengine tumezaliwa tunapenda MDUNDIKO wakati wengine wamezaliwa wanasikia kelele tu kwenye MDUNDIKO.

Nawasiwasi staili ya wahubiri wa kilokole, hata kabla ya KUSIKIA WANAONGELEA NINI kuna watu inawatuliza roho na hao kuna uwezekano wakaokoka kirahisi labda kwa kuogopeshwa zaidi kutokana na staili ya mzungumzaji iwaingiavyo au kwa kuelewa zaidi kutokana na mhubiri kuto waboa kwa staili na kabla ya kwa neno, na kwa hilo labda mhubiri anakuna kipele kwa KAULI kwenye fani.

Kuna wengine ni staili ya mashekhe ya kushusha neno a.k.a KAULI iongezayo uelewa wao wa Kitabu Kitakatifu na ya ALLAH.


Tukirudi kwa mganga wa kienyeji au hata mtongozaji , staili yake inaweza kumfanya mtu akubali jambo ingawa aliyepewa KAULI wakati amejilaza kwenye kitanda chake cha teremka tukaze BAADAYE, atakuwa bado haelewi ni kwanini mambo kama; ya mtongozaji ya;Aisee dada nakupenda sana na kila nikikuona nabanwa mkojo AU ya mganga ya;Lete kijambio cha njiwa jike msenge na mzizi wa jiwe, vilikuwa vinaleta maana sana wakati anapokea kauli.

Bado tatizo ni;...
....tunaamini STAILI ya ashushavyo kauli Mmarekani ni tofauti na ya ashushavyo Mfaransa, na labda ni KWELI ! Lakini ukweli ni kuwa kuna Mgogo wa DODOMA anayeweza akawa anakuna Mfaransa kwa STAILI na kauli za Kigogo kuliko Mfaransa akunavyo Mfaransa mwenzake, kama tu Mmarekani awezavyo kuvutia Mpare wa Mwanga kwa Msuya , kwa staili na UNG'ENG'E labda kuliko awezavyo kulainisha Mmarekani mwenzake mtaa wa jirani kwa kauli , kisa anaongea na ana STAILI za Mmarekani mweusi katika kumwaga KAULI ya fani.

Swali:

  • Ushastukia hata mjinga akiwa anaongea kwa sauti au staili uioanishayo na mwerevu, mjinga haonekani mjinga sana ingawa unajua pointi zake zote hazikuni pointi ingawa anamwaga KAULI?

  • Ushawahi kutofautisha staili na sauti yako ya kuombea msamaha ilivyotofauti na ya kutongozea ingawa zote ni za utulivu na zinamwaga kauli?
  • Si unajua kutongoza maana yake kuomba kwa kubembeleza na sio lazima uwe unaomba nanihii?
Labda ni kweli ,.....
.... staili ya kuongea imsaidiayo MGANGA WAKIENYEJI, ina msaada kwa mtongozaji!
Na labda,....
... Staili ya muhubiri huyu UAMINIYE anahubiri ya nabii wa UONGO haiwezi kutumika kukuokoa kwa kutumiwa na muhubiri mwingine kukuokoa WEWE hata kama inashusha ya NABII wa kweli yenye UKWELI katika staili ya kukugawia KAULI.

Lakini,....
......HATA kama hutaki , ukweli ni kwamba Mtongozaji na Mtongozwaji wapo na staili za kumwaga kauli ZIPO na zina afya kama MNYOO na binamu yake FINYOFINYO!:-(
NAACHA!
Kumbuka nawaza tu hapa!:-(
siKU Njema!


Tulia na Harry Belafonte katika -Man Smart, Woman Smarter....



Au ngojea turudi tena Guadeloupe kukutana na FUCKLY katika kibao -Doudou....

Read more...

SINA MAJIBU!

Katika hali halisi ya kuumbwa kibinadamu Simon Kitururu kama Chakubanga tu , bado ni MTU.


CHAKUSIKITISHA....
......katika ubinadamu wa baadhi ya binadamu kutafuta mkao wa kuheshimika katika jamii ya kibinadamu, MHESHIMIWA MTU huweza hata KUAHIDI MAJIBU yawezwayo na MALAIKA kama si MUNGU PEKEE.

Mie sina majibu ingawa napenda kuuliza!:-(

Swali:

  • Hivi Mungu kama yuko pekee na hapendi dhambi, unafikiri sio mpweke sana kwa kuwa pekee na labda kwa miaka milioni kadhaa KANUNA kutokana na kujua ataumba binadamu halafu watafanya dhambi?
  • Hivi wewe unajua mangapi kama mjuaji yaliyokufanya uweHAI jana?
  • Sina majibu lakini si kuuliza RUKSA?
NAACHA!
BAADAYE!
Hebu tubadili hali ya hewa kwa kucheki uhusiano wa binadamu katika kufuatilia
Mapping migration with genes katika -phonecian gene.


Au ngojea tena Billy Taylor, Duke Ellington and Willie the Lion waJAZZfai katika kibao -Perdido..

Read more...

KAMA wewe huandiki historia yako kama uijuavyo wewe!

>> Tuesday, February 17, 2009

Labda...
.... hatujui hata USAHIHI wa historia ya juhudi za binadamu kugundua choo cha shimo ,hata baada ya miaka yote hii baada ya baadhi ya BIN-ADAMU kuchoshwa na safari za kwenda kichakani ambako ukikosea unaweza kujikuta kichaka kimoja na Mama Mkwe mnachimba DAWA.


Na historia yako kama si wewe uiandikayo, inaweza kusimuliwa na ajuaye CHEMBE kuhusu wewe akiwa katika mkao wa kudai anajua mwili wako mzima hata ile chunusi yako KUNAKO.

Tatizo pia ni kwamba chochote kisemwacho juu yako hukutana MPAKA na masikio yenye UDHAIFU wa kuvumilia UONGO uliopo kwa kutopenda kuhangaikia ukweli mpaka UJITOKEZE kuhusu hata ubikira wa Bikira Maria baada ya kujifungua Yesu.

NAACHA!
Kumbuka Nawaza tu hapa MKUU!

SIku Njema!

Tulia na moja ya bendi nizipendazo sana kwa jina NUTTIN but STRINGZ katika kibao -Thunder..

AU ngojea wamalizie na Broken Sorrow

Read more...

MBWA MWITU aliyeshiba kaonekana akicheza na MBUZI! (hadithi ya KIJINGA- kisogo cha pili)

Hapo zamani kulikuwa na MBUZI aitwaye KIBEZI DUME, na mbwa mwitu aitwaye BINTI TITI!

Kibezi na Titi walikuwa marafiki wakubwa wapendao kucheza katika kijiwe cha jamii bila viatu.Lakini jamiii iliishi na hofu ya ukweli kuwa Binti Titi anaweza kumla Kibezi Dume.

Hofu ya jamii ilizidi kukua hasa mbwa mwitu- BINTI TITI alivyo kuwa anazidi kukua na mbuzi- KIBEZI DUME alivyozidi kunawili katika safari ya kukua pamoja na ilivyozidi kuwa vigumu kuwatenganisha wasicheze pamoja bila viatu.

Jamii ilikuwa roho juujuu kwa kuamini mbuzi wa jamii ataliwa tu akiachiwa aendelee kucheza na mbwa.

Swali:

  • Hivi chui si huwinda akiwa na njaa tu?

Lakini....
... ni kweli labda mbwa mwitu huwa na hamu na mbuzi.

Tatizo...
.... hatujui apitaiti au mshawasho wa hamu ya MBWA MWITU huyu ya KULA, katika kumuachia mbuzi huyu achezee mpaka gololi zake.


Swali:
  • Si kuna chui walafi?

  • Hivi si nasikia kuna mbuzi wapendao kuliwa?

Lakini ...
.... Mbwa mwitu kama anaendelea kuishi maeneo yenye mbuzi labda kuna ukweli Mbuzi wanaendelea kuliwa.:-(

Tatizo KUBWA katika swala hili la msichana na mvulana linaweza likawa linajengwa zaidi NA hofu ya jamii ifanyayo Mbuzi ajisikie KULIWA zaidi na Mbwa Mwitu ajisikie kula zaidi kwa sababu jamii imekaa mkao wakufikiri chakula kiko tayari kila wakati.:-(

HADITHI imeisha !

DUH!

Hadithi imeisha na ujumbe hakuna!:-(


NAACHA!
Swali:
  • Sasa jamii itafanyaje wakati jamii lazima iwe na Mbwa Mwitu na Mbuzi katika jamii?
  • Hivi katika stori hii ya kijinga mbuzi anaweza akawa ndiye Mbwa Mwitu eeh?

  • Hivi wewe hujawahi kutaka kula wakati umeshiba?



Tutulie na Just for Laughs - Don Juan


Au ngojea BENNY BENASSI acheze na wimbo wa Eurythimics watukumbushe kila mtu kuna kitu anatafuta katika -SWEET DREAMS....

Read more...

Mr KIBEBERU ndani ya siku! (Hadithi ya KIJINGA -kisogo cha kwanza)

ILIKUWA jumamosi kama jumamosi nyingine kwa Mr Kibeberu na siku ilianza kwa CHAI na KIPORO cha wali na maharage cha juzi.

Pamoja na kwamba kiporo kilikuwa kimeanza kuchacha kwa mbali, hii haikuacha kumfanya Kibeberu ale huku akiachia tabasamu kwa mbaaaaali huku akisema kimoyomoyo hii ni siku ya kujirusha hasa kwa mtu kama mimi niaminiye katika DINI ya KAZI KWA SANA na baada ya kazi ni KUTOA STIMU KWA SANA tu.


Wakati anamalizia kufunga zipu ya suruali na wakati akijiuliza kuwa kwa nini suruali yake ina zipu badala ya vifungo, Kibeberu aliendelea kutabasamu kwa kukumbuka kuwa jioni hii BENDI aipendayo ya Ochestra MSULI PEKECHAPEKECHA ndio itamiliki mirindimo ya mioyo ya watu mjini katika KUPEKECHA.

...............Kama kawaida saa za kikubwa hazikawii kuwadia na jioni ikamkuta Kibeberu akitumia kujulikana katika mchezo aliozoea wa kutaka kuingia kwenye shoo bure ingawa leo hii bila mafanikio.

Lakini kwa uzoefu wa nyoka alijikuta akijinyonganyonga katika foleni na kwa uzoefu alifanikiwa kuwa miongoni mwa washabiki wa Ochestra MSULI PEKECHAPEKECHA waliokuwa ndani ya ukumbi mapeeema!

Kibeberu ndani ya nyumba alienda na miondoko ya kusalimia awajuao na kuchekea VIMWALI wazuri asiowajua katika kujaribu kuweka jeduali likae katika mtindo wa kurahisisha mtongozo hapo baadaye, yote ni katika KUANDAA matibabu ya kujihami na upweke ujao baada ya shoo ili Kidume asijejikuta yuko pekee ghetto.

Kibeberu kwa unyenyekevu aliisogelea BAA yenye kuonekana kuvutiwa na ushabiki wa wajao kula KILAJI na kuipunguzia bugudha ya kujaa pombe. Wakati Kibeberu anatafakari bei za pombe mawazo ya POMBE SI CHAI na uharamu wa pombe yalimkatiza akilini mara mbili na nusu ,kwa kukumbuka makaripio ya SHEKHE na hata Mchungaji wa kanisa la kijiweni kuhusu madhara ya ulevi.

Wakati anaanza kukumbuka pia maoni ya wazazi kuhusu mambo ya anasa , KIMWANA MWANANA aliyekaa kwenye stuli ndefu pembeni ya baa akifyonza KILAJI akafanikiwa kurudisha ari mpya ya KIMIMINIKA na kilaji kikaagiziwa huku akikumbuka lakini sasa hivi NI kwa mbaali kuwa ; POMBE si CHAI.


Dakika chache baada ya kuwa akijaribu kutatua swala la hivi KIGOLI aliyempita yuko NUSU-uchi au uchi-nusu , akasikia sauti ya PAPAA MSULI ambaye ni kiongozi wa bendi ya MSULI PEKECHAPEKECHA akifoka kwenye KIFOKEO kwa msemo wake uliopo kwenye wimbo wake maarufu mpya,- alisikika akisema; ''GRISI kiunoni weka, MBINUKO pakua!'' na umati ukasikika ukijibu; ''MSULI pekechapekecha na MAkalio BINUA!'''
Mr Kibeberu akatabasamu mtabasamu wa kujua sasa shughuli imeanza!



Mr Kibeberu alifumbua macho na kuiona silingibodi anayoitambua kitu ambacho kilimfanya akenue meno kwa tabasamu la kujua alifanikiwa kurudi nyumbani SHWARI baada ya kimiminika a.k.a KILAJI cha kutosha jana usiku. Wakati anajaribu kukumbuka jinsi alivyofurahia jana usiku akashtuliwa na sauti ya kijambo pembeni yake na ndipo alipo kumbuka hakuja nyumbani peke yake.

Kwa haraka alistukia mpaka yuko uchi na kwa kawaida huwa halali uchi. Kwa mbali akakumbuka jana alikuwa anadansi na kimwana mwenye mwanya wenye ujazo mwanana.Na tabasamu likarudi baada ya akili yake kurudi katika mkao wa tamaa za fisi.

Lakini alipofunua shuka kumshuhudia KIGOLI, alipigwa na butwaa kugundua aliyelala pembeni yake bila nguo ni bibi kizee na hana meno. Wakati anajaribu kutafakari imekuaje yuko uchi na bibi kizee, akastukia gauni jekundu lililoko sakafuni linafanana na la yule kigoli aliyekuwa naye kwenye taa dimu mwenye bonge la mwanya mwanana na denda lenye uzito wa FRESH mtindi.

Ghafla moyo ukaanza kumdunda kwa spidi za sungura wafanyao mapenzi kwa kukumbuka jana usiku hakuwa hata na condom, huku akishindwa kuelewa ilikuwaje mapengo yalikuwa yanaonekana kama mwanya mwanana jana usiku!:-(


HADITHI IMEISHA!

Swali:

  • Unakumbuka pombe si chai?
  • Unakumbuka kumlinda na kujilinda ingawa wote tumekusikia ukitangazia umati HUFANYI uasherati?
  • Bado huongelei ngono na kondomu kwa sababu si utamaduni wetu ingawa uwapendao wanaendelea kufa kwa kutokujua?
  • Unauhakika kama umesoma mpaka hapa, huu sio ujinga ulioandikwa hapa?


BAADAYE!.....
Hebu tutulie kwa kushuhudia mtazamo wa HARUSI ya dada na dada katika- SOAP'S FIRST LESBIAN WEDDING..


Au ngojea CYPRESS HILL wazungumzie wao mtazamo katika - Under Mi Sleng Teng

Read more...

NI KAZI YAKO au chaguo lako?

>> Monday, February 16, 2009

NAJUA uko kazini hata kama huna kazi!


WAKATI unafikiria hiyo kazi ya kuwazia kazi, ....
..... kuna uwezekano bado kuna chaguo la KUENDELEA NAYO au KUENDELEZWA NAYO.


Kuna uwezekano kabisa ni KAZI INAKUFANYA wakati wewe unafikiri unaIfanya kazi!:-(



Narudia swali:

  • Hiyo ni kazi yako ILIYOKUCHAGUA au ni chaguo lako la KAZI?


Labda hiyo kazi sio chaguo lako kama tu lisivyokuwa chaguo lako kuwa wewe ni mtoto wa RAIS MANDELA na lingekuwa chaguo lako ungetaka uwe mtoto wa RAIS LOWASA.:-(

Lakini kama sio chaguo lako katika mkao wa HALI HALISI uliyonayo , bado naomba tena kukuuliza SWALI:
  • Unauhakika hiyo ni kazi yako au haikua chaguo lako na ni kazi kwako?

  • Unauhakika ingekuwa ni chaguo lako ungetaka uzaliwe katika dunia hii yenye mpaka gono?

NAACHA!
Ngojea Mory Kante aendeleze tena katika- Yeke Yeke

Read more...

Nimecheki jana na UKWELI ni kwamba nina UKIMWI!

>> Sunday, February 15, 2009

Ukweli ni kwamba sijacheki jana ingawa nacheki mara kwa mara labda kwa kuhisi nipewavyo katika kupakua MARA NYINGINE labda NINAPAKUA zaidi kama WEWE katika staili ya KUJIJAZIA.:-(


Swali:

  • Hivi kama KESHO nikicheki tena halafu ikawa ni KWELI kuwa NIna UKIMWI kama MHESHIMIWA naNIhii, UTAJIANDAA KUKATAA kunipa ingawa sitarajii KUKUOMBA unisaidie NANIHII?

  • SI unakumbuka kuwa UKIMWI ni ugonjwa tu kama BERIBERI na kwa ujanja wako unaweza UKAWA umeishi SANA kwa kukwepa mpaka ugonjwa wa MDONDO halafu ukawa huoni NISHAI kujinyea ingawa NI KWELI kwa ujanja wako umeishi mpaka UKAzeeka SANA na hukumbuki choo wakati UNAJINYEA na si mjanja?
  • Hivi ulikumbuka kucheki jana?
Nakushauri ucheki hasa kama umepata LIMPENZi jiPYA na unahisi mnaweza kutaka kuishughulikia SHUGHULI bila VIATU.

Cheki pia kama ulishakuwa hata katika ajali ya mkokoteni ambayo ulijeruiwa wakati uko na MAJERUHI.

Cheki pia kama katika uteja wako wa magonjwa unawasiwasi na sindano zilizotumiwa kukupa ugoro.

Wakati unacheki kumbuka mtoto wa mjini HIV ukimdaka leo kwa kawaida hata mwezi ujao na mbili haonekani, kwa hiyo rudia tena kabla hujajinoma bila viatu angalau baada ya miezi mitatu.


CHEKI TU ila jiandae kabla ya kucheki kwa sababu jamii imezoea hata kutisha watu kuhusu KIFO mpaka imetisha watu kucheki MDUDU, wakati ukijua mapema unaweza mpaka kupanga maisha yako vizuri na labda badala ya kuhangaika na maboksi ungeweza kurudi kijijini kwenu MVOMERO ukacheze mkulanga katika kufurahia maisha kivyako.

Inasemekana wengi wasambazao UKIMWI kwa makusudi ni kutokana na kwamba hawakujiandaa na baada ya kujua wanafanya yao ya udhaifu ambayo ni kufikiri inalipa kufa na watu.

Kumbuka aliyedaka UKIMWI sio lazima maana yake kafikia mwisho wa maisha na HAJINOMI.
Swali:
  • Unafikiri kwanini kuna aogopaye kucheki mdudu kwa kudhani ATAJUA atakufa wakati kuna wajitoleao kufa kwa ajili ya dini ambazo cha maana zifanyazo ni kuahidi YASIYOJULIKANA?
  • Unajua inawezekana unao kama ni kweli bado hujacheki ?
NAACHA!
Baadaye basi kama SIJAFA au HUJAFA!

Au ngojea tena Tender Mavundla atusaidie tena...

Read more...

NIPE KIDOGO NIchangamshe DAMU!

Lakini.....
.....kabla hujatoa SI lazima ulipata wakati unafikiria labda unipe!:-(


Na....
..... WAKATI unatoa ni kweli ULIKUWA NACHO ndio maana unanipa na sio KWELI unanipa kwa UKARIMU tu.

Wakati unanipa UKWELI ,......
........chakusikitisha ni kwamba hakuna UHAKIKA unanipa NINI na kwamba ni kweli ni UKWELI kama siamini ni UKWELI.

Na ni kweli,....
.....LABDA wakati unafikiri unanipa KITENGO labda ni kweli unatembea huku umebeba mzigo wa MAUNGO kitumbua.


Kumbuka,....
....KUNA busara za kutua mzigo hata kama mzigo wako ni moja ya KIUNGO kwenye mwili.


Swali:

  • Hivi ni kweli unafikiri damu inahitaji kuchangamshwa?


Na,...
.... wakati damu INACHANGAMKA,...

............. jaribu kuwa na uhakika uko na watu wenye undugu na ADAMU na EVA katika ya KIBINADAMU na ya MUNGU muachie MUNGU uchangamke.

Swali:
  • AU?


JUMAkumi NJEMA!

Ngojea Michael Jackson na Britney Spears waseme....

AU tu RICHIE SPICE amzungumzie -GHETTO GIRL....

SAMAHANI ngojea basi SHABBA RANKS amalizie na -COOL COOL......


ASANTENI TENA WADAU WOTE!

Au ngojea niwaache TENA na picha zangu na baadhi ya WADAU niliofanikiwa kuwadaka hivi karibuni ya JUZI YA JANA....

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP