Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

BAADA ya kuamka na KABLA ya kwenda KUKOJOA!

>> Friday, February 13, 2009

SIKUBISHII....
...... ukisema ASUBUHI katikati ya muda kati ya ULIPOAMKA tu na muda ulipoenda chooni KUFANIKISHA kwa mara ya kwanza, hakuna ulichofikiri.

Ingawa naweza KUJARIBU kukubishia kwa hoja angalau ya kwamba baada ya kuamka na kabla ya kwenda chooni angalau ulifikiria kwenda kukojoa,.....

...... unaweza ......
.....kudai kawaida yako ukiamka tu hubanwa na kiu ya maji na sio KUBANWA na shehena ya HAJA-msalani, hata zisizohitaji maji!:-(


Lakini .....
.......labda kuna kitu huwa unafikiria katikati ya safari ya kutoka kitandani kwenda choooni ukiamka TU , ingawa unahisi huwa unapiga MMMMHH-ayo TU ,bila kufikiri kwa sababu umeamka na umekenua MDOMO katika miondoko ya kujinyosha.


Kumbuka lakini kuwa ,.....
..... baada ya kuamka UKIKOJOA, umekojoa mkojo uhitajikao na daktari , DAKITARI akitaka kujua AFYA YAKO kupitia wako MKOJO kama sio kucheki chako kinyesi ambacho kama WEWE ni mbunifu wa kibebeo ,KINYESI huwezabebeka kwenye kiberiti.

Lakini asubuhi pia,....
......kuna wenye bidii mpaka ya kutaka kukipa KITENGO ujauzito ingawa ni kweli hawajaAMKA vizuri na kwa maajabu ya Musa, KIUNGO NANIHII cha mwili kimeamka na kinafikiria VIZURI ingawa hakina ubongo wenye akili.


NA ni kweli kuwa ....
.... akili yako kabla HUJAAMKA sawasawa inajua zaidi KULIKO ukiamka VIZURI na kuanza KUDHANI unafikiria zaidi kwa kuwa umeanza kufikiria:
  • Shule
  • Utakula wapi
  • Mnuno wa Bosi
  • Utakavyo mchekea mesenja
  • Kubeba maboksi
  • Hawala sijui atapiga simu?
  • Mchezo sijui utakuaje.
AU......
  • hata utachambia nini na nakadhalika tatu na nusu.:-(


Swali:
  • Lakini si umeamka?

Endeleza tu Mkuu kama umeamka na sio mzuka wako tu ndio UMEAMKA!

Kumbuka lakini kwa kuwa macho unapunguza uwezo wako wa kufikiria mengi kwa sababu KUNA ambayo unayapa kipaumbele kwa kuwa macho.

Labda.....
....... wakati UMEAMKA na uko MACHO kwa kuchunga POCHI, mwanawani unasahau kuchunga CHUPI.:-(


NAACHA!
MIe NAWAZA TU HAPA!
Tuko Pamoja!
WikiENDI njeMA!

Nakuacha na Mr VEGAS akisema -Nuh Want No Fren From Dem na Tek Weh Yuself..(Tahadhari kama mkwazikaji au mtoto halafu msikilizaji ,kuna mambo ni ya wakubwa:-()



Au tu Eminem ft. Dr.Dre & 50 Cent wadai - Crack A Bottle....(Tahadhari lugha kama mtoto au mkubwa akwazikaye na lugha.Kuna mambo ni ya wakubwa:-()

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Mzee wa Changamoto 2:47 pm  

Kaka. Nimerejea. Nimeweka Firefox na nakupata bila kale kadubwana kalikokuwa kananibania.
Sasa tuko pamoja na nashukuru kwa ziara zako zote.
Amani kwetu

Simon Kitururu 8:34 pm  

@Mzee wa ChangaMoto:Asante kwamba ziara hazina Mzuizi Mkuu!Tuko Pamoja!

Anonymous 9:44 am  

amani mkuu.
rasta hapa.

Simon Kitururu 10:15 am  

@Rasta: Asante Mkuu!tuko Pamoja!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP