Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TATIZO la kuogopa KUONGELEA nanihii!

>> Tuesday, February 10, 2009

Labda BADO unasema na kuongea kwa KUKAA kimya!
CHAKUSIKITISHA ni ukweli kuwa hata wasemao hawaeleweki NDIO MAANA kuna BINADAMU wakagundua KUJIELEZEA.


TATIZO la kuogopa kuongelea laweza kusababisha watu kudhania KIJEBA ni BASHA kumbe ukweli wenyewe ni kwamba KIJEBA ni MSENGE!

Na katika kuogopa kuongelea,......
.....unaweza kusababisha MUISLAMU aendelee kuwa MUISLAMU na MKRISTO aendeleze UKRISTO kwa kushindwa kwako kutetea uishivyo KIPAGANI wakati unajina la KIHINDU.



USIPOANGALIA unaweza mpaka KUFA NA NJAA kwa kogopa KUONGELEA NJAA!

Swali:

  • Hivi unaogopa kuongelea tu au hata KUSIKILIZA HUSIKILIZI?

  • Kama UNACHAKUONGELEA unauhakika UNAWASIKILIZAJI?



USITISHIKE!

Labda unaamini huna cha KUONGELEA ndio maana UKO KIMYA!


Kumbuka tu kuwa hata PADRE , ASKOFU, SHEKHE na hata mganga wa kienyeji HAWAKOSI cha KUONGELEA kwa kustukia tu kama ulivyoSTUKIA kuwa kama huna vyako vya kuongelea unaweza ukaongelea vya MUNGU na kuna vitabu unaweza kukariri mistari ilikuongezea UAMINIKAJI wako katika KUONGELEA STORI uwashauriyo wengine wasifanye ingawa wewe bado unayafanya au angalau dhamira yako YAKUFANYA ipo na inakusumbua.

Na wakati hutaki kumuongelea MALAYA ,bado kama unavutiwa na uzuri wa MALAYA twaweza kustukia unavutiwa na MALAYA kwa sababu MALAYA mhusika ANAVUTIA hata labda si kwa UMALAYA ndio maana UNAVUTIWA.


Kumbuka tu kama UNAPUMUA ukipenda unaweza kuanzia kuzungumzia PUMZI katika KUONGELEA.


KUMBUKA tu;.....
......CHOCHOTE ni STORI kama unataka kiwe STORI.

Swali:
  • SI kama una roho nzuri utapenda kujua kama wengine watasaidiwa kuendelea HATA kupumua kwa kuwa UMEONGELEA SWALA ingawa unasita kuongelea Swala au NGURUWE?
  • Unauhakika huna tatizo la KUONGELEA ingawa laweza kutafusiriwa kwa neno UMBEA kama bidiii ZAKO za kuongelea zimezidi?

NAACHA!
NA kumbuka NAWAZA tu hapa nachojaribu KUONGELEA ingawa kinaweza kisieleweke ingawa NAKIONGELEA!:-(

Tuburudike kwa kuangalia HABARI MUHIMU kama ya Rais Obama kujigonga kama ni burudani , kama iletwavyo na chombo cha habari za maana cha CNN........


Au ngojea Sluggy Ranks azungumzie - Sodom & Gomorrah

Au ngojea tu Papa San alie tena .....katika - maddy maddy cry ... (sikiliza kwa hiari yako mwenyewe mie simo....!)

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP