Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

JINSI ya kumbembeleza WAZIRI mkuu AKILIA!

>> Friday, February 20, 2009

Wakati katibu MKUU au mtoto analia,.....
...... kumbuka KUFARIJIKA kwa kujua kwa vyovyote vile hawawezi kulia DAIMA hata kama hawatapewa nyonyo.

Tukumbuke pia,....
...... kuna watu wako kimya ila wanalia KWA NDANI!:-(

Pamoja na mwiko wa jamii usababishao kubwa zima kuogopa kulia hadharani, KULIA NI MUHIMU.

Na USIDANGANYIKE....
... kuwa sababu za watu kulia MSIBANI ni kweli wanasikitika marehemu katutoka.

Kuna watu walikuwa wanatembea na KILIO tokea jana na MSIBA wa leo umewawezesha kuangua kilio HADHARANI au nyuma ya mbuyu, na wala walikuwa hawamjui marehemu na kama walikuwa wanamjua MAREHEMU, ...
......WALIKUWA HAWAMPENDI.:-(




Swali:

  • Unafikiri kubwa zima wakati linalia msibani ni dakika ngapi wakati linalia ndani ya dakika linafikiria jambo jingine lisilo husiana na kilio msibani?

  • Unafikiri toto wakati linalilia pipi likiona lawalawa nyama halianzi kufikiria labda ligeuze kilio cha pipi kielekee kwenye lawalawa nyama?
  • Unafikiri wakati mtu ANALIA anakuwa ameshaanza kufikiria jinsi atakavyo malizia gia ya KULIA?


Kumbuka wakati KATIBU MKUU analia, bado kunyonya kidole ni RUKSA.

Na, ....
.... DAIMA kumbuka watu wanatembea na VISIRANI vyao na wanaonekana wanatembea kwa maringo tu na VILIO vyao ingawa unaweza usistukie na ukiwapa sababu ya KUKULILIA WEWE wanaweza wakachukua nafasi hiyo KUJILILIA WAO na YA KWAO.

Na usipoangalia UNAWEZA kupigwa kibao kwa kumchekea mtu halafu usielewe KWA NINI , kumbe mwenzio alikuwa anavisirani vyake anavifuga tokea MWAKA JUZI na SIKU HIZI kwake KUTABASAMU kwa wengine na KUNG'ONG'A ni saresare MAUA.

Swali:
  • AU?
  • Hivi unafikiri hakuna kitu ambacho wewe ni Rais au angalau ni Waziri MKUU kabla hujalia?
JARIBU.....
........ kujipa ruhusa KULIA leo kama unachakulia LEO, utafaidika kwa kulenga kulilia kilichokuliza na kinachohusika katika ULIZI leo. Ukitunza kilio cha leo unaweza kujikuta UNACHANGANYA VILIO na unalia ya marehemu wa leo na yakuaibishwa mwaka juzi ,wakati sasa hivi unatakiwa ulie kwa sababu ya utamu wa penzi.

Na ikibidi kukasirika leo ,.....
.......KASIRIKA leo yaishe leo!
Usije ukaanza kutukasirikia na sisi leo wakati hasira zako zilipewa ujauzito na bosi wako juzi na pia na LIMPENZI lako mwaka JUZI na sisi hatuhusiki:-(

Na ni kweli,...
....Mila , Desturi na Miiko mingine mingi hata ya kijinga inatusaidia kusababisha tunatunza maumivu na vilio mpaka inakuwa vigumu, mambo yakiwa magumu kujua tulilie lipi.

Wakati unamalizia kulia,....
..... jaribu kukumbuka kujiangalia kama ulifanikiwa kutoa KAMASI ili ulifute kamasi kama lilikutoka katika miondoko yako ya kulia.

NAACHA!
Topiki imenishinda!:-(

Hebu tubadili hali ya hewa kwa kukutana na Michael Leahy labda na kwa mbaaali Mtaalamu RON JEREMY, ili kuuliza-How did you get hooked on Porn?...


Au turudi tu Congo na kukutana na Tshala Muana atukumbushe - Mbombo..

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 9:13 am  

amakweli simon uko mawazoni.

rasta hapa.

Simon Kitururu 9:26 am  

@Rasta: :-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP