Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kwa MPENZI sura ya MALAIKA! Tupande KIBAJAJI mwenzio BENZI sina!:-(

>> Friday, February 06, 2009

Kwa mpenzi Midomo Mizuri!

Dhumuni la barua hii si kukujulia hali tu , bali na kutaka kuharakisha safari ya penzi letu ifikie pale niaminipo nimelipata penzi lako kiuhakika ili mwenzio niache KUKUDANGANYA.

Mpenzi Midomo Mizuri kama ya bata, ni kweli nikikuona moyo unapiga mdundiko na kwa jinsi macho yako malegevu yanavyoniwashia indiketa kuwa ni zamu yangu kupita, napata mshawasha wa ari mpya na nguvu mpya yakufika nawe faragha tukafanye ya faragha. Lakini pia indiketa ziniambiazo hii ni zamu yangu kupita zanikumbusha kuwa labda aliyetangulia alizionja zabibu hizo kwa mitindo ambayo mimi siwezi kuchuma zabibu.:-(

Mpenzi naombea ningezaliwa enzi zile wazazi na kijiji kizima wangekujua zaidi kuliko mimi na kazi yangu ingekuwa ni kusikilizia ni lini wazazi wangu watakutana na wazazi wako katika kunirahisishia ujio wako maishani mwangu tule zabibu.

Mpenzi midomo mizuri, mwenzio na wasiwasi pia kuwa hupandi baiskeli, ingawa Phoneksi yangu iko pimped na nyuma imeandikwa maandishi kwa lugha ya kisasa ''NO SWEAT''! Tetesi hizo nimezipata baada ya kusikia hata VIBAJAJI hupandi na ulishawahi kumtukana Kamanda aliyekuja kichwakichwa kukuchukua na PICK UP kwa kudai kuwa kaja na gari la kubebea majani ya ng'ombe na sio kumpakia Kisura Midomo Mizuri.:-(

Mpenzi katika barua hii naomba kukiri kuwa nahitaji huruma yako ili niache kukudanganya. Nafikiri inabidi nikiri tu kuwa hii misuli sio ya gym bali ni ya kugonga kokoto. Na suti yangu ya Kaunda sio fasheni bali ni kweli ilikuwa ya Kaunda na nilipewa na hausiboi wa Kaunda tuliyekutana na kuzoeana katika mikutano na semina za mahausiboi za kuboresha jinsi ya kumnyenyekea akupaye kazi kubwa kwa mshahara mdogo.

Na nimeshauriwa niendelee kukudanganya kwa kuwa inajulikana kuwa WEWE unafurahia sana mdanganyo kwa dhati, na wenye busara wanaendelea kudai kuwa nikikuambia ukweli hatua ya ndoa hatutafikia . Na unajua tena mwenyewe dunia tuishiyo kwa wastaarabu kama sisi wa dini za kupokea kutoka kwa wageni kistaarabu , tendo la ndoa linahitaji refa au libarikiwe na Padre au Sheikh kabla hatuja likokotoa kistaarabu.

Mpenzi Midomo Mizuri, wakati najisikia kukuambia ukweli, ngojea nikiri pia kuwa ni kweli sio kila siku unapendeza na ukiniuliza kuhusu nguo zako nijuazo unazipenda kuwa zimekupendeza ,nalazimika kukudanganya kuwa ni kweli zimekupendeza. Ni kweli pia unanuka sana mdomo nikigongana na wewe asubuhi na tako lako halitingishiki ukitembea kama nikusifiavyo. Samahani kwa kukiri PIA kuwa hizo ni baadhi za vitu vinivutiavyo kwako sana tu ingawa nasikitika kujua unavikimbia kwa kupiga mswaki na kujaribu kwa nguvu na nusu ya ustadi kutingisha makalio.

Kabla sijamaliza barua hii ningependa kukuomba angalau leo nijitahidi kuja kukuchukua kazini mwako na BAJAJI. Ni matumaini yangu utachukulia huu ni utani na utapanda bajaji twende kwenye nyumba husika karibu na Shekhe alipo nikiwa na tumaini labda tutafumaniwa kwenye mkeka na kufungishwa ndoa ya mkeka maana hela za kitchen pati , begi pati na hata Fweza za harusi ya kuhalalishia watu au kujulisha umati tendo la ndoa RUKSA na labda tunalifanya KIMANDINGO sina !:-(

Nimatumaini yangu kabisa baada ya kusoma barua hii utatabasamu kwa kuzani si kweli ni kwenye BAJAJI na sio kwenye BENZI ndio matarajio yangu tutaanzisha ukurasa mpya wa PENZI. Hali halisi MPENZI ni kwamba bado niko kwenye hatua ya BAJAJI ya kukodi ingawa nina PENZI LA KWELI pamoja na kwamba nilikudanganya ilikupata sikio lako lililozoea kusikia utamu wa asali kuliko wa ndimu. Nasita pia kukiri ukweli mwingine kuwa mwenzio hata ndoto za Benzi sijafikia Mpenzi.

NAKUPENDA Mpenzi Midomo Mizuri Cheusi Dawa Mwanambilimbi!
Nakupenda sana na naahidi kukupenda kwenye CHEUSI na hata kwenye MKOROGO!
Pata basi busu la kikohozi cha bata MPENZI na kwa mapenzi usiteme!
Nakuahidi nitakuwa mwenye juhudi za kujitolea kwenye shughuli za faragha mpaka kitengo kitapata ujauzito tu Mpenzi!

Nitunzie nafasi angalau ya kigoda kwenye moyo wako Mpenzi!
Tutaonana basi mbele ya ofisi yako ukitoka ofisini tukaendeleze ule mpango vipi!
Au vipi Mpenzi!

Wako katika penzi ,
MPENZI.
--------------------------------------------------------------------------------
Swali:
  • Unauhakika Mpenzi ni nini?
  • Unauhakika husemi tu na ukweli ni kwamba huelewi penzi wala hujui kupenda ni nini ingawa unadai kwa juhudi mbele za UMATI unampenda hata Yesu au Mungu?
  • Unauhakika ni kwanini umeisoma hadithi hii ambayo labda ni ya kijinga mpaka sentensi hii hapa Mkuu?
Loh !Lione vile!:-(

Au twende tu na Kibajaji maeneo...:-)

AU?
Photobucket

Photobucket
NIMEACHA!
NAWAZA tu Mkuu hapa !
WiKIenDI njeMA!

Tutulie na NANKO arudie kusema.....-.LUCKY U


AU tu Pepe Kalle aseme....-HIDAYA..


AU tu Pepe Kalle aendeleze kwa kusema- Milla....

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 10:57 pm  

Kuhusu mpenzi Midomo Mizuri...hehe, nimesoma hadi mwisho lakini siwezi sema kwa nini...tuseme mie mdaku tu! Kisha kama kawaida mzik nao umenirudisha mbali tena sana,,,nikiwakumbuka wazazi wangu wakiusikiliza mziki wa kina Marehemu Franco, Pepe, Tabu Ley,na wengine wengi...kisha mwenyewe na marafiki angu tukisakata viuno kule Tents eneo la Buruburu Nairobi huko 90's...siku ambazo Lingala ilikuwa imevuma...tukiskiza Arlus Mabele...Koffi Olomide...weh...raha ile tukicheza kochokocho DUH! Nisije nikaema mengi hapa:)

Simon Kitururu 3:50 am  

@Serina: DUH!:-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP