Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LABDA mpaka leo kila AFAYE na AISHIYE kashindwa KUMALIZIA kwa sababu hakuna KILICHOMALIZIKA.

>> Thursday, February 05, 2009

Kama wewe ni MTANZANIA unaweza kumshangaa hata NYERERE kwa kuishia katikati katika SIASA zake za UJAMAA NA KUJITEGEMEA, kwa kusahau INASEMEKANA hata aliyoanzisha YESU hayajamalizika kama tu ya MTUME na hata ya BUDDHA katika kutafuta NIRVANA au KUMALIZIA.

Na kama wewe unaishi, labda unaanzisha ambacho hakitamalizika au unaendeleza walichoanzisha MAREHEMU au MAREHEMU WATARAJIWA ambacho utafariki hakijaisha.

Swali:

  • Kwani kama marehemu walianzisha unafikiri waishio wanafanya nini kabla hawajaMAREHEMUKA?

  • Unauhakika MUNGU alimalizia kuiumba DUNIA kama mpaka leo bado inabadilika?


Unaweza kubisha!
Lakini....
.....LABDA alichoanzisha marehemu au aliyehai yeyote hakijaisha na kama kuna aaminiye kimeisha , anatafsiri nyingine ya kumalizika kwa kitu na SHUGHULI ZA kuondoa dosari aionayo katika adaicho KIMEMALIZIKA atadai hamalizii SHUGHULI ila au labda ANAFANYA UKARABATI.

Labda ....
......kwa aaminiye hata kuwa DUNIA na viumbe vyake MUNGU alimalizia kuviumba enzi hizo za zamani, basi mabadiliko ya DUNIA na VIUMBE vyake yaendeleayo kutokea KWAKE si matokeo ya MUNGU kuendelea KUMALIZIA na labda si UKARABATI.:-(

Swali:
  • Unauhakika ungekuwa unauwezo wa kuumba kiumbe chako ungetaka KIHANGAIKIE kula CHAKULA halafu KINYE?
  • Hivi inawezekana ni mbinguni ndiko Mungu atamalizia ukarabati wa liMTU MIMI kama sio MTU WEWE?
  • Unafikiri Kijeba na binti Halufani wakikamilika watahitaji kwenda MSALANI MBINGUNI?


Pamoja na kuwa kuna watakaodai :
  • Kwa sababu ulizaliwa , basi kuna Marehemu kadhaa walifanikiwa kumpa au kupewa mimba na kazi yao ilimalizika ndio maana leo hii kuna wanaoishi!

  • Simon Mkodo KITURURU kufikiria KAZI YA MUNGU YA KUUMBA HAIKUISHA ndio maana labda hata mpaka leo hii BINADAMU BADO TUNAKUNYA hapa mawazoni, ni KUKUFURU!
Unaweza ONGEZEA nakadhalika saba na nusu za mengine yote yawezayo kukupitia kichwani wakati unafikiria uendelee kunisoma au LA HASHA,.... kwasababu NI RUKSA udaicho na kuna watakaopingana na udaicho!


Swali:
  • SI wapo wajanja WADAIO wanaendeleza kazi ya YESU , Mtume MOHAMADI, BUDDHA, MRUNGU, hadi mpaka MBUYU MWANAMBILIMBI katika dunia hii ambayo kwa binadamu kila siku ni KUANZISHA , KUSHINDWA KUTUNZA na KUKARABATI kwa sababu HAIJAISHA?
  • Hivi kwa MCHORAJI kuna picha ILIYOISHA isiyofaa kupitishwa HATA BRASHI mbili-NNE ili kumalizia PICHA?


Sibishi!

Labda....
..... kazi za MAREHEMU walizoachia WALIMWENGU ni kuweka wazi tu nini kiendelee kufanyiwa KAZI na ndio sababu nyumba ILIYOMALIZIKA KUPAKWA RANGI inaendelea KUPAKWA tena RANGI , katika kuendeleza hata tudaicho MAREHEMU alimalizia KUPAKA RANGI!

Na unaruhusiwa kudai kila AFAYE na AIISHIYE kuna kitu ALIMALIZIA kama unauhakika HATA kwenye utumbo ukimsafisha MHESHIMIWA MAITI au KISURA ALIYE HAI hakuna makombo ya mavi ambayo hakumalizia kuyatoa katika SHUGHULI ambayo HAKUMALIZA:-(

DUH!

Swali:
  • Unafikiri umemalizia KUZEEKA?
  • Unafikiri maiti haimalizii KUZEEKA?

NAACHA!
NAwaZA tu HApa Mkuu USITISHIKE na samahani kama nimekukwaza!
Nakutakia kila la KHERI chooni!

Tutulie basi na mshabiki wa Yesu a.k.a ISSA , ROSE MUHANDO akumbushe waaminio- Baba nipe uvumirivu


Au twende tu tena Somalia kwa K'naan azungumzie -HARDCORE...

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP