Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

BUSARA zikizidi ni UJINGA na AKILI zikizidi ni UKICHAA!:-(

>> Friday, February 06, 2009

Kwa kawaida ni mwenye AKILI na BUSARA za wastani ndiye asifiwaye kwa kuwa na AKILI SANA au BUSARA SANA kwa sababu wenye AKILI SANA na BUSARA SANA hawaeleweki kwetu tuliozoea kutumia busara na akili ADOADO ilimradi siku inapita tukiwa katika majonzi au kufurahia NANIHII tuzipatazo kiADOADO!:-(

WENYE akili na busara sana hawaeleweki na wanaweza wakawa wameshajiua tayari au wanajiua sasa hivi kinamna kwa ajili yangu au yako kama sio kwa YALE tuyafanyayo.

Inawezekana lakini....
.... kama umezidiwa BUSARA , ukapunguza BUSARA ZAKO na usionekane kufanya UJINGA ingawa ukashindwa kupunguza AKILI ZAKO ambazo kwa bahati mbaya zinapungua zenyewe ukizipa MUDA WA KUTOSHA.


Swali:

  • Mtaalamu si unakumbuka kama utafanikiwa KUISHI VYA KUTOSHA akili zako za UPASUAJI WA UBONGO zitafikia kushindwa kukukumbusha KITANDANI si CHOONI?
  • Hivi labda si ni kweli unang'ang'ania AKILI na BUSARA hata zikupazo MAJONZI kwa kuogopa kuonekana HUNA BUSARA na MJINGA?


NA tatizo ni ukweli....
.... DUNIA INAENDESHWA na WENYE busara za wastani kama si za KIJINGA na WENYE akili za WASTANI kama sio chini ya wastani AMBAO KWA BAHATI MBAYA ndio wana eleweka NA WENGI.

Narudia....
... kwa mtazamo wangu,.....
.........WENYE BUSARA SANA huonekana WAJINGA na WENYE AKILI SANA huonekana VICHAA na kwa bahati mbaya hao wote hawako katika FASHENI YA KUSIKILIZWA wala KUELEWEKA.:-(

Swali:
  • Bado unaamini BINADAMU WOTE wameumbwa kwa mfano wa MUNGU?

NAACHA!
Kumbuka NAWAZA tu HAPA usitishike na wala sikuongelei WEWE!
Tutulie tena MTOTO ANUNE....

AU Ikiwezekana SAMBA MAPANGALA amalizie kwa kutukumbusha ...-Nyama CHOMA..

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP