Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Labda YULE NI mjanja kwa kuanza JUZI na sio MWAKA JUZI!

>> Friday, February 06, 2009

Moja ya TATIZO la walioanza zamani ni KUZOEA SHUGHULI!

Na....
..... shughuli IKIZOELEKA afanyaye husahau kuwa wakati alivyokuwa anajifunza KUIKATIKIA SHUGHULI, ni kweli shughuli ilikuwa ni UJANJA.

Ni kweli....
...... walioanza MWAKA JUZI wengi wako kimya ingawa wanafanya SHUGHULI ingawa unayemsikia ZAIDI ni aliyeanza JANA.


Na ALIYEZOEA tokea karne ya juzi.....
.... anaweza kusahau unamsubiri kwenye FARAGHA akupakulie MAUNGO wakati hisia zako za KIUNGO zimeiva.

Na AANZAYE juzi....
......anaweza akakereketwa na alichoonja kwa MARA YA KWANZA JUZI mpaka akakusimulia visivyo simuliwa kuwa KAONJA visivyoonjwa.:-(

Lakini Swali:

  • Hivi aliyejua MWAKA JUZI unauhakika bado anajua utamu wa ILE KITU leo?
  • Hivi aliyeonja ile kitu MWAKA JUZI akionja tena leo, hivi HII KITU haina LADHA mpya?

Inasikitisha kukiri,.....
..... labda ajuaye juzi pamoja na MCHECHE WAKE WA ULENA, anasikilizia zaidi UTAMU WA JUZI aliouonja kwa SIKIO JIPYA na kwa mara ya kwanza kuliko MZOEFU ajuaye A,B,C za utamu tokea karne ya MWAKA JUZI!:-(

Tusisahau lakini kuwa kuna aina za utamu kama UTAMU WA BIA ambao huongezeka kwa jinsi UZOEAVYO BIA ,
......na labda pia,....
....... BIKIRA aliyeonja kwa MARA YA KWANZA JUZI katika kumbukumbu za utamu ni MAUMIVU au AIBU za aliyofanya BILA UZOEFU kwa mara ya kwanza JUZI!:-(

Swali:
  • AU?
  • Kwani unakumbuka UTAMU wa MAZIWA YA MAMA kama ulivyoonjeshwa miaka ya karne ya juzi?


KWAHIYO,.....
.... labda tusiMCHEKE aliyeanza juzi kwa kuwa msemaji MKUU WA ULICHOKIZOEA tokea KARNE YA JUZI kwa kuwa mwenzio labda bado ANAKISIKILIZIA USIVYOKISIKILIZIA tokea karne ya juzi , kwa kuwa kakionja kwa mara ya kwanza JUZI.

NA labda MUONJA juzi,....
.... utamu wa chakula cha juzi bado UPOUPO na ni utamu FRESHI, na kama WEWE hukula tokea mwaka juzi , wewe ni MFU nanikweli hujaonja vya JUZI kwa ulimi wa JUZI.

NAACHA!
Ngojea tena tujifunze kufungua SIDILIA katika -How To Undo Her Bra With One Hand...


Au niwaachie Ray Parker Jr. & Bobby Brown katika - Ghostbusters

Au turudi tu kwa Mtanzania a.k.a Freddy Macha atukumbushe Kilimanjaro na kuleta nguvu mpya ya kuendeleza siku....

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP