Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama HUPENDI magimbi jaribu VIAZI ingawa MAGIMBI yanazoeleka!

>> Tuesday, February 03, 2009

Ni kweli....
......hata UGUMU unazoeleka baada ya KUJILAZIMISHA kama haukuui.:-(

Tatizo ni....
...... maisha ni mafupi na usipoangalia unaweza kujikuta unatumia muda KEDEKEDE kujaribu kuzoea HATA kula MAGIMBI kwa MLENDA wakati labda ungeweza tu kuishi zaidi kwa kula VIAZI kwa CHUNGA.

Kama vile tu USTADH na MLOKOLE awezavyo kuzoea kutukana baada ya kufanyia mazoezi KUTUKANA, mheshimiwa unaweza kuacha MATUSI kwa kujinyima MATUSI.

Kumbuka tu.....
....... utamu wa kujaribu KUZOEA kitu unaweza usiustukie kwa kutogundua HATA ni siku gani hasa ULIYOHITIMU kuzoea.

Swali:

  • SI unakumbuka unaweza kuzoea hata mpaka KUPIGWA kama unabidii ya KUJIZOELESHA ingawa MHESHIMIWA MZOEFU umesahau ni siku gani uliyoanza kuzoea KIPIGO?
  • Unafikiri hujazoea kutukanwa kama siku hizi husikii matusi?


Tatizo ni.....
  • UNAFIKIRI unamuda wa KUJIZOELESHA wakati unaweza kuishi na ulivyovizoea TAYARI?

NI kweli.....
...... VIAZI vipo kama huhitaji kujizoelesha MAGIMBI.

Na pia ni kweli....
......MBWA ni chakula kama tu PANYA ukilazimika KULA.

NA.....
....... kama unafaidi zaidi MAISHA kwa kufanyia mazoezi kuzoea MAGIMBI ingawa VIAZI vipo, ......KULA MAGIMBI mwanawane!

NAACHA!
SIkuNJEma!
Tulia na LEADBELLY katika- IRENE GOODNIGHT

AU tu Ivete Sangalo alete za - Chica Chica Boom Chic

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP