Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Unafikiri YULE umpendaye kwa UZURI ni MZURI?

>> Sunday, June 13, 2010

Uzuri ni kitu cha AJABU ,...

.... LABDA ndio maana kuna APENDWAYE kwa kuwa anavutia FANTASI za sehemu zake zisiri kwa AMVUTIWAYE kwa kuwa tu ETI  ana  MATEGE.:-(


Uzuri ni kitu cha ajabu,....
.... ndio maana kuna ampendaye ujuaye kwa uhakika ni  mwenye PENGO  ila AMPENDAYE  anaamini hilo pengo ni MWANYA na  akihisi huoni avutiwacho anawezafanya siri na KUKIRI KWAKE hilo labda ni mpaka UMTEGE.:-(


Na uzuri wa MWANYA kama tu MATEGE YA MPENZI kimaajabu,...
....inawezekana kuwa ni kuwa HAKUNA kinacho kusaidia wewe MHESHIMIWA kama lengo na MAHITAJI YAKO YA MSHAWASHA  litafanikiwa zaidi KIFARAJA kama ukilenga MCHOCHEO katika LIMWILI LA MTU kwenye KIKOJOLEO hata cha ambaye hana MATEGE .:-(


Swali:

  • Hivi wewe MHESHIMIWA unahisi wewe ni MZURI uchi?

NI WAZO TU HILI la JUMAPILI!
JUMAPILI NJEMA MHESHIMIWA!

Hebu BOB MALYA arudie- BAD CARD



Au tu hebu  BURNING Spear naye asisistizie- SHE is MINE


Read more...

Wakati MTO ni ULEULE,....

>> Saturday, June 12, 2010

... unaweza kufikiria maji yaliyopita jana siyo yapitayo LEO,...


...ILA kama ni mfikiriaji unaweza kustukia asilimia kubwa ya MAJI  YATUMIWAYO na BINADAMU ni YALEYALE,.....

.... kwa kuwa mzunguko wa maji hapa DUNIANI chini ya anga ni ULEULE.:-(


Kwa hiyo  MAJI hata ya MKOJO wa mbuzi  ni yaleyale,...
....ambayo yakigeuka mvuke ndiyo yatakayo dondoka kama MVUA ambayo usipoichunguza vianzo VYA MAJI YAKE  waweza kufikiria maji yote ya mvua ni masafi kama ulivyo aminishwa kuna BINADAMU anamwili msafi kisa kaoga VILEVILE.:-(

Swali:

  • Si unakumbuka mawingu yanaweza kuwa na vumbi au tu hata  kemikali za sumu kama tu mabaki ya mikojo  mtaroni vilevile hasa ukikumbuka JAPANI baada ya bomu la nyukilia walio kunywa maji ya mvua walizurika  kama tu ULAYA walivyowahi kuzurika miaka fulani kutokana na kunyeshewa na maji yaliyoathiriwa na mlipuko wa volkano ya ICELAND enzi hizo vilevile?

  • SI unakumbuka  KATIKA MZUNGUKO hata udongo uukanyagao labda ni mabaki ya  MAITI fulani ambayo miaka fulani marehemu  au hata HAYATI chura alioza na kugeuka udongo katika mzunguko ambao leo ni udongo tu VILEVILE?

Ndio,...
... labda maji yaliyokudondokea  leo  MTONI baadhi ya matone yake ni yaleyale yaliyokudondokea JANA.:-(

NAWAZA tu MKUU na NIMEACHA wazolinalotapatapa hili!:-(

Hebu MRISHO MPOTO na MAUNDA walete kitu- Samahani Wanangu





Au tu MRISHO MPOTO na Banana ZORO wanyambulishe kitu katika -NIKIPATA NAULI


Au tu na REMMY ONGALA anyuke tu ndude-PESA

Read more...

MATATIZO ya MAHUSIANO ya ustadi wa KUCHAMBA UCHI na UCHI ikiwa ajuaye vizuri MATOKEO ni CHUPI na wala sio UCHI!:-(

Kuna vitu vihusianishwavyo ambavyo labda UKIFIKIRI,....

.....NI KITU kingine katika huo uhusiano ndicho  KITIWACHO  doa la chupi katika  KIPENGELE.:-(



Swali:
  • Unauhakika CHAKULA kinajua unanjaa?



Uzuri wa KIFANYIKACHO   ,....
... labda  KIHITAJIWACHO  KUAMINIWA sio  KFANYIWACHO.....
... kwa  kuwa LABDA ajuaye vizuri  umakini  wa KILICHOFANYIKA sio ALIYEFANYA au ALIYEFANYIWA,....

.... kwa kuwa labda kwa kawaida KILICHOFANYA  hakina uhusiano wa moja kwa moja na matokeo ya KILICHOFANYIKA.:-(


NI HILO TU KIJEBA! 
Na ni wazo tu HILI ambalo kuliendelezea vipengele hata vya kunajisi ni  RUKSA Mheshimiwa!

Hebu Bob MALYA atupe pambio -Mix UP mix up



AU tu Burning Spear arudie naye pia pambio- THIS Experience

Read more...

MSHINDI wa uhakika KABLA YA MECHI labda ni yule MSHABIKI wa REFA.:-(

Ukimshabikia REFA,....
.....haki ya sehemu za siri za mjusi vile,....
.... labda SI kweli huna TIMU!:-(

Na haki ya MAMA YAKE  naniliu vile,....
..... uwafahamuo wadaio wana ushabiki wa timu ,....
...kunaambao KAMA UNAUELEWA MSHUGHULIKO  waweza kuona waziwazi kama tu uonavyo chupi ya mwalimu aliyekaa vibaya darasani kuwa hao  ni VITIMUTIMU!:-(


Swali:
  • AU?
  • Kitimutimu si unajua hajatulia na anaweza KUTIMUKA?


Kwa bahati MBAYA inasemekana HATA katika kitimutimu  ,...
....kuna wajisikiao wana TIMU.:-(


Swali kitindamimba:
  • Umeshawahi kumshabikia refa wakati timu mbili  USIZOJUA KAMA ZINAUHUSIANO NA REFA zinabinyana ?

Samahani kwa tararila hii hasa nikiamini unakumbuka ni RUKSA KUTOELEWA!:-(

Hebu  tudungwe na amdungaye kikubwa Rais  OBAMA  katika kubadili HALI YA HEWA KIJIWENI  ajulikanaye kama Michelle Obama alete taralila iitwayo-My parents sacrificed for US



Au ngojea Q Tip na kundi zima la Tribe CALLED QUEST wadunge -Stressed out



Au tu TribecalledQUESt ft PHARELL waongezee tu MDUNGO tena unukuliwao kimaandishi kama - Can I kick it like that


Au tuachie tu mdungo orijino wa TribeCALLED QUEST kabla wajanja hawajajipendekeza katika-Can I kick it

Read more...

Tukiudeku UKAKAMAVU wa uzuri wa NDOTO za kumpata MWAJUMA , usioambatana na MIKAKATI na LENGO la kumpata MWAJUMA!

>> Thursday, June 10, 2010





NDOTO  kwa BAHATI MBAYA zipo,....
.....na  labda NDIO MAANA  kwa bahati NZURI   kila mtu ana mpaka MAJINAMIZI yake .:-(


Swali:

  • AU?

Na ndoto kama MAWAZO tu zipo,...
....na UZURI wa NDOTO kama kilema cha  MAWAZO TU  bila VITENDO  unaweza ukashindwa kumpa mimba mtu kwa kumuota TU au UKASHINDWA HATA  kufanikisha kuwa MWIZI  ingawa kwa NDOTO za wizi hata za magwaguro ya watu WEYE ni  kubwa lao.:-(


Swali:
  • AU?
  • Si unajua kwa kumuota tu  MWAJUMA kuwa ni  MCHUMBA wako haifanyi MWAJUMA ageuke MCHUMBA wako?


Ndio,....
... kunauwezekano NDOTO bila MIKAKATI na LENGO unaweza usitimize ndoto yako ya kuwa MWIZI.:-(


NI WAZO TU HILI na nakutakia kila la kheri  angalau uwe na uhakika wakupata CHOO MHESHIMIWA!

Au ngojea J DILLA atulize kwa kitu- Think Twice




Au tu Q-Tip aendelee kubadili hali ya hewa hapa kijiweni kwa kunyuka mkung'uto - Things U Do

Read more...

Tangazo la MSIBA!

>> Wednesday, June 09, 2010

Ndugu yetu Ben Kakengi amefiwa na Baba yake mzazi jana mchana nyumbani Tanzania. Kwa walio FINLAND watakutana leo  jumatano 9.6.2010 saa kumi na mbili jioni (6:00pm) katika ukumbi wa (Clubroom) Kilo kutoa pole kwa Ben., adress ni kilonrinne 10. Espoo.
Tafadhali wape ujumbe huu wote wanaohusika.

Namba ya simu ya Ben Kakengi ni: +358414329794


Our Brother Ben Kakengi has lost his father yesterday in Tanzania. Today wednesday   9.6.2010    6:00pm those in FINLAND  will pay a visit of condolence to Ben at Clubroom Kilo.
Adress is: kilonrinne 10. Espoo.

Please pass this message to everyone of us.

Ben´s telephone number is +358414329794.

Read more...

Labda ni kweli kuwa USO MZURI uonekanao UNAWEZA kumsingizia KIBWENGO afikiriwe ana sehemu za siri NZURI pia!:-(

NI jambo lijulikanalo,...
..... kuwa HAKUNA UHUSIANO kati ya sura nzuri na sehemu za siri nzuri hata  kama ambaye hajachunguliwa ni  MBWA.:-(


Na jambo lisilojulikana,....
.... ni pamoja na kwamba LABDA  moja ya tamu ya UHISICHO  NI KITAMU ni hisia tu ndio maana  hata CHAKULA ukitamanicho kwa utamu kuna MTU kakichoka  ladha na ukimpa nafasi anaweza akakilisha MBWA.:-(
Swali:

  • AU?
  • Unauhakika UMPENDAYE kwa sura hasababishi kukuchelewesha kustukia ana roho MBAYA kisa unapenda tu mwanya wake kama kitobo cha maji machafu ya choo na bafu la  gesti bubu  mitaa fulani?
Kuna uwezekano,....
...... ni  kumbukumbu za paja LA KUKU lifanyalo KUKU azaniwe anasura nzuri.:-(

Na kuna uwezekano ,....
..... ni paja lisababishalo  MTU MWINGINE asichunguze LIMSICHANA lake  sura vizuri.:-(


Lakini PIA labda  kunauwezekano,......
.......vifanywavyo siri  ndio siri usistukie sio vizuri na uuziwacho NI SURA  ili ujenge hisia vilivyo siri  sio vitamu vizuri.:-(

Swali:

  • AU?






NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA na nimeliacha.:-(

Hebu NAS na DAMIAN Junior Gong Marley wanyuke mkuno-FRIENDS




Au tu ngojea NAS ,Damian MARLEY na Knaan wanyuke pia ndude- Africa must wake UP

Read more...

Katika stori TUSIZOZIJUA za BIBLIA za ADAMU na EVA labda ni kweli MKUNGA alikuwa ADAMU wakati EVA ANAJIFUNGUA!:-(

>> Tuesday, June 08, 2010






Kuna ufanyayo TUSIPOFIKIRIA hatuwezi KUSTUKIA unafanya.:-(



Swali:


  • Si unajua ni kawaida kutowaoanisha waheshimiwa na  matatizo ya kujikuta chooni wakati hakuna kitawazio?:-(
  • Si unajua kuna MAPADRE wa kanisa la KIROMANI KATOLIKI ambao tunaweza tusiwe tunajua ni kwanini wanashauri sana kutotumia silaha za kuzui HADIJA asipate mimba kwa kuwa labda wanajua matumizi vizuri yazuiayo HADIJA asipate miba?


Kuna KAZI  mtu AFANYAZO ambazo HUWA HAZIONGELEWI,....
.....na hapa siongelei KAZI zile za  KUSAIDIA shimo fulani la CHOO kujaa.:-(



Na LABDA ndio maana mengi ya ujifunzayo SHULENI HUYASTUKII kwa kuwa darasani  HAYAONGELEWI,...
......na kwa  kuwa  katika MASOMO SHULENI  kunaujifunzacho na kukifanyia mazoezi mwenyewe BILA USIMAMIZI WA MWALIMU labda ndio maana kuna MWANAFUNZI ambaye angalau katika kujifunza kwa bidii mwenyewe MIMBA humjaa.:-(


Swali:

  • SI kuna uwezekano moja ya kazi  ya AMSIKILIZAYE RAIS akihutubia ni kumfanya RAIS  ahutubiaye kujisikia KUNAWANAO MSIKILIZA ingawa wamsikilizao hawakufunzwa kustukia hilo  wakati wamsikilizapo ALOLOMAYE?
  • SI unajua labda moja ya kazi ya walipa kodi wasioijua ni kusababaisha tuwe na MAFISADI ambao  cha kufisadi ni pesa za kodi?


NDIO,...
.... labda moja ya kazi ya MIAKILI yako ni kutufanya siye wengine tujisikie WAJINGA ingawa hujastukia.:-(

LIONE VILE!:-(

NIMEACHA WAZO Mheshimiwa !:-(

Hebu twende UGANDA tujifunze jinsi ya kujitetea OBAMA akitaka kuleta USENGE katika busara zenye kichwa cha habari -EAT DA POO POO



Au tu Jake Benson afanye ujumbe uwe dansabo katika kitu -EAT DA POO POO remix

Read more...

Labda NYOKA MWENYE SUMU hana sumu MWILI MZIMA!:-(

Ndio,...
... katika kuzinguliwa na sifa za NYOKA ASIFIWAYE KWA SUMU,....


.... unaweza ukamuogopa  mpaka NYOKA MTU MZIMA mwenye sumu KICHWANI TU,....
.... ingawa labda SHIDA YAKO inatibabu kwenye NYOKA HUYOHUYO  MKIANI ,...



.....halafu INAWEZA KUWA NI UKWELI  kuwa NYOKA umuogopaye sumu yake iko eneo moja tu LA MWILI na kama sumu iko KICHWANI kuogopa mpaka matako yake mazuri  LABDA  hakuna faida KWAKO.:-(

Swali:
  • SI labda  MWALIMU umuogopaye kama uwezo wake haukufelishi MTIHANI  TU  ingawa kakufanya MJINGA,  kipengele alichokusaidia kuwa mjinga kinaweza kutogundulika kwa sababu hakiko katika MWILI MZIMA wa FUNDISHO ustukiwao?:-(

  • Si kuna uwezekano UTAKATIFU wa MTAKATIFU labda hauko katika mwili MZIMA na labda kuanzia KICHWA mpaka MATAKO YA MTAKATIFU labda sio MATAKATIFU kwa kuwa  utakatifu wake uko kwenye mapaja tu ambayo hayana uke na ubongo?:-(


Ndio,...
..... labda MALAYA sio MALAYA mwili MZIMA.:-(

NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA usitishike!:-(


Hebu tupewe mizinga BAAB KUBWA kutoka KOLUMBIA kwa CHOC QUIB TOWN   kama tatika mshwasha -Somos Pacifico




Au tu  CHOC QUIB TOWNwanyuke kisawasawa kwa ndude-Toquemen EL BOMBO

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP