Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati MTO ni ULEULE,....

>> Saturday, June 12, 2010

... unaweza kufikiria maji yaliyopita jana siyo yapitayo LEO,...


...ILA kama ni mfikiriaji unaweza kustukia asilimia kubwa ya MAJI  YATUMIWAYO na BINADAMU ni YALEYALE,.....

.... kwa kuwa mzunguko wa maji hapa DUNIANI chini ya anga ni ULEULE.:-(


Kwa hiyo  MAJI hata ya MKOJO wa mbuzi  ni yaleyale,...
....ambayo yakigeuka mvuke ndiyo yatakayo dondoka kama MVUA ambayo usipoichunguza vianzo VYA MAJI YAKE  waweza kufikiria maji yote ya mvua ni masafi kama ulivyo aminishwa kuna BINADAMU anamwili msafi kisa kaoga VILEVILE.:-(

Swali:

  • Si unakumbuka mawingu yanaweza kuwa na vumbi au tu hata  kemikali za sumu kama tu mabaki ya mikojo  mtaroni vilevile hasa ukikumbuka JAPANI baada ya bomu la nyukilia walio kunywa maji ya mvua walizurika  kama tu ULAYA walivyowahi kuzurika miaka fulani kutokana na kunyeshewa na maji yaliyoathiriwa na mlipuko wa volkano ya ICELAND enzi hizo vilevile?

  • SI unakumbuka  KATIKA MZUNGUKO hata udongo uukanyagao labda ni mabaki ya  MAITI fulani ambayo miaka fulani marehemu  au hata HAYATI chura alioza na kugeuka udongo katika mzunguko ambao leo ni udongo tu VILEVILE?

Ndio,...
... labda maji yaliyokudondokea  leo  MTONI baadhi ya matone yake ni yaleyale yaliyokudondokea JANA.:-(

NAWAZA tu MKUU na NIMEACHA wazolinalotapatapa hili!:-(

Hebu MRISHO MPOTO na MAUNDA walete kitu- Samahani Wanangu





Au tu MRISHO MPOTO na Banana ZORO wanyambulishe kitu katika -NIKIPATA NAULI


Au tu na REMMY ONGALA anyuke tu ndude-PESA

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP