Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

NIA na MADHUMUNI ya BARUA hii MPENZI ni kukujulisha kuwa UKISINZIA huwa unajamba!:-(

>> Saturday, May 29, 2010

Ukipenda ,...
.....KIJAMBO cha mpenzi kinukacho sio BUGHUDHA.:-(

Swali:

  • AU?
Ukipenda  NI kama tu UKIAMINI dini yako ndio ya kweli,....
.....utamu wa  kibano chake   kwa wapendao burudani za sehemu za siri  watadai kiwepo hata mbinguni ingawa ukikifikiria baada ya kumchoka mpenzi  LABDA ni BUGHUDHA.:-(





Kwa kifupi nilitaka kukuuliza MHESHIMIWA :
  • Hivi ni mangapi unamficha MPENZI?
  • Huwa unamstua mpenzi kuwa ananuka?
  • Si unajua kunavitu unavifanya wakati umelala na washuhudiao ni watu WENGINE?
NDIO,....
... kuna uwezekano UKISINZIA  kunavitu unafanya na huvistukii tu  ndio maana UKIZINDUKA unashangaa jirani  yako ana BENZI uitakayo halafu wewe bado hata Corolla YAKISHIKAJI  huna.:-(


Ndio,...
.... ukisinzia KUNA KITU unafanya zaidi ya KUSINZIA na kimojawapo ni  kuachia  vyako WENGINE  bila kujijua  na LABDA  ukijiuliza MWENYEWE  unaweza kudhani hivyo vyako wavishuhudiavyo kwako WATU wengine kuwa HUNA.:-(

NI WAZO TU  a.k.a UjingaBUSARA HUU  na nimeukatizia MHESHIMIWA ili usitishike!:-(
JUMAMOSI na WIKIENDI NJEMA  Mkurugenzi!

Hebu twende KONGO STAFF BENDA BILILI wanyuke-Je t'aime


Au jifunze tu  STAFF BENDA BILILI

Read more...

Kwa bahati mbaya HATA kwenye limwili la LIBINADAMU zuri.....!

Mdomo wa kulia ndio huohuo wa KUTAPIKIA kilichoingizwa MWILINI.


Sehemu za siri zenye kiburudisho KWA WASIO MAPADRE ndizo hizo hizo zenye kutoa Uchafu mwilini au ndizo zilizo karibu na chakutolea uchafu a.k.a kimba/timba  MWILINI.


Tako zuri ulipendalo wakati linatikiswa mtu akitembea eti ndilo hilohilo tumizi lake kubwa ni kukaliwa au tu kuficha kijambio mwilini.

Swali:

  • Kama unadharau kazi ya tako , unafikiri ni rahisi kukaliwa au kutunza kijambio?

Halafu eti mikono ya kuchambia ndio hiyohiyo isaidiayo kupeleka chakula mdomoni ili kiende Mwilini.:-(

    Halafu eti Kitovu na Mavuzi KWA WA KUBWA  zaidi tu yakuwatia madoa WATU  kunauwezekano havina kazi MWILINI.:-(


    Swali:

    • Hivi mkuu bado unanisoma tu?
    • Unauhakika usomi ujinga ?
    • Si unakumbuka kusoma ujinga ni mazoezi ya akili pia?

    Ndio,...
    ... eti limwili la binadamu lina KICHWA na moja ya tumizi la KICHWA sio kusoma NA wala sio kutumia akili!:-(

    NIMEACHA wazo MHESHIMIWA!:-(








    Hebu Alpha Blondy akite-LES CHIENS


    Au ngojea tu tubakie Ivory Coast ili Alpha Blondy akune kwa- Brigadier sabari





    Au tuhamie Ufaransa kidogo katika kubadili ili DAFT PUNK wanyuke katika kupoza mshawasha kwa ushauri- Make love



    Au tubakie hapahapa Ufaransa  ili St Germain wafankifai kwa mara nyingine kwa ndude- Sure Thing

    Read more...

    Chaguo la LEO: Katika kutibiwa NANIHII, ungependa NESI kipofu au DAKITARI kipofu ?

    >> Wednesday, May 26, 2010

    [Tahadhari:Kuna uwezekano wazo limepindia kushoto zaidi ya kulia katika taralila hii!]


    Katika kuchagua,...
    ... unaweza kuwa unatishika NA MAJINA yaambatanao na wenye taaluma kuliko hata TAALUMA yenyewe waliyonayo kwa kuwa ukifikiria UNAWEZAKUSTUKIA ,...

    .... kuna uwezekano NESI na DAKTARI vipofu wenye utaalamu na GOVI wanaweza wakawa wazuri katika tibabu lako LA KUKATWA JANDO kuliko NESI na DAKTARI waonao lakini utaalamu wa kucheza na GOVI kimatibabu hawana.:-(


    Swali :
    • Si unaweza kutishika tu kwa kusikia NESI na DAKTARI watakaokutibu ni vipofu wakati gonjwa lako  linahitaji ajuliaye kupapasa na wala sio aonaye?
    • Unauhakika ni asilimia ngapi ya magonjwa uliyowahitibiwa  NESI au DAKTARI alikuwa anatumia macho kuyaona ili upewe KLOROKWINI?

    Ndio,....
    .... labda MAHUBIRI mazuri ambayo yatakufanya uende mbinguni  MWENYE NAYO ni yule umkwepaye kumsikiliza ukiwa na nyege za kutishwa kuhusu JEHANAMU  au SHETANI kisa KIUTAMBULISHO  anaitwa tu  KIBAKA , kiruka njia, MPAGANI  au tu  KIDUME anajulikana kwa kupenda kukuna sehemu za siri wakati anaongea na WATU hadharani kitu ufikiriacho kuwa si sahihi kufanyika kwa akuhubiriaye kuhusu MUNGU hadharani.:-(

    Ndio,...
    ... inawezekana moja ya kimsaidiacho MGONJWA kupona ni imani yake tu  kuwa ANATIBIWA  vizuri na MTU au  MADAWA yanayoaminika  kitu ambacho kinasababisha  pia KWA IMANI  hata manabii wa uongo wanao watu LUKUKI wakirio kuwa waliponywa nao HADHARANI .:-(


    Swali:
    • Si unajua nesi akuchomaye sindano aliyevaa glovu anaweza akahatarisha imani yako ya kupona ugonjwa kwa VIDONGE alivyokupa ukigundua wakati anakupa vidonge alitoka haja kubwa na hakunawa mikono vizuri baada ya MTAWAZO  ingawa mikono yake haijagusa vidonge kwa kuwa kavaa gloves?
    • Si umeshawahi kusikia eti hata YESU alikuwa anasema ``IMANI YAKO IMEKUPONYA´´? 
    • Sitanii, wewe kwako ni afadhali Nesi au Daktari wako ndio awe KIPOFU?
    • Kama wewe sio kipofu umeshawahi kufikiria KIPOFU anakuaminije wewe bila kukuona au tu anastukiaje unabonge la makalio?

    IMANI nishai,...
    .... inaweza kusababisha uamini mke wako ulimkuta bikira wakati unamjua mtoto wake ULIYEMKUTA NAYE  alelewaye na wazazi wake.:-(

    Imani NISHAI,....
    .....kwa kuwa inawezajengwa bila USHAHIDI kama vile tu UDEKUVYO KWENYE MASWALA YA  DINI ila kwa imani tu UKAAMINI  UNESI au UDAKTARI haumfai KIPOFU   kwa kuwa kwa imani unaamini ILI DAKTARI akutibu malaria inahitajika AKUONE  ili ustukie kama anakuelewa hasa kwa jinsi wakati anakudadisi ili kujua ni GONO au MALARIA ndicho kinachokusumbua UMDEKU anavyokuuzia kwa huruma na upendo LISURA lake.:-(

    NI wazo tu hili  USINUNE Mheshimiwa!
    Cheka basi kidogo !AU?

    Basi bwana NIMEACHA!:-(




    Au tu tupate mnyumbulisho kutoka kwa GILBERTO SANTA ROSA anyuke kwa - VUELA LA PALOMA



    Au tu Machel Montano na Xtatik wanyuke tena - Big Truck



    FIKIRIA hii spichi ingekuwa ni ya RAIS mmoja wa TANZANIA na asemacho hapa Martin Luther King Jr kiwe kinamaa kuwa huyo Rais wetu MTUKUFU kashaona TANZANIA ielekeapo KUNAUNAFUU kwa MTANZANIA MNYONGE na kunanukia bonge la pilau[hasa kama wewe ni mpenda pilau] hebu sikiliza kwa mkao wakumtafakari HUYO Rais wa TANZANIA kuwa anaongea kuwapamoyo WATANZANIA

    Read more...

    Tukiangalia uwezekano kwanini WIZI , uuzaji uchi au tu UCHAWI kwa kawaida INASEMEKANA auwezaye HUWA ni mtu MWINGINE na sio WEWE!:-(

    [Tahadhari: Wazo katika taralila HII  limepinda !:-(]


    Ukifikiria utastukia kuwa  katika kila uliogopalo kuna MWINGINE  anashamiri katika hilo bila UOGA uliokuwa nao KUHUSU HILO  wewe.:-(


    Swali:
    • AU?
    Ndio maana,...
    ..... uchochoro UUOGOPAO  kuupita  kuna ambaye hauogopi na kageuza hapo makao a.k.a OFISI  yake ya KUKABIA watu ambaye kwa jina la kitaalamu huyo ni mjanja kwako.:-(


    Ndio maana,....
    .... kwa  uogopaye WACHAWI  unajua kuwa kuna watu ambao hawaogopi uchawi  kitu ambacho kimewasaidia zaidi ya kutoogopa uchawi kuliko aogopaye uchawi wamekuwa wenyewe WACHAWI  labda HATA katika eneo lako.:-(

    Ndio maana,....
    .... katika ujasilimiamali weye ukichacha hata kama ulishawahi kujichungulia ukastukia unasehemu nyeti kisura ambazo zinauzika MTAANI na unawajua  waliojenga nyumba na kupandishwa vyeo kwa UFUNDI wa tumizi la NYETI  waweza kujikuta unaogopa kufanya mauzo ya NYETI ZAKO NONO kama wengine ambao walitatua tatizo lako  katika eneo lako kwa mauzo ya kiungo kitu ambacho unaamini hakiwezekani kwako.

    Swali:
    • Sasa kwanini wengine na sio wewe?
    • Unafikiri wengine wanakuzidi nini mpaka wanafanikiwa kuwa mafisadi  katika UFISADI uushindwao , wakati wewe unadai unamuogopa Mungu hata kuonjesha watu uzinzi kama wenzio wafanyao UZINZI ambao vifaa vyake vya tumizi kama hamu na pembejeo za kazi unazo?


    Ndio,....
    .... inasemekana MAKUZI ya mtu yanaweza kumsaidia mtu kutokuwa na tabia ya kudokoa MBOGA JIKONI hasa akihisi hakuna watu.


    Ndio,...
    .....inasemekana  MAZINGIRA yanasaidia  kurahisisha baadhi ya MDADAZ  kutoa nyonyo kwenye umati KIRAHISI ZAIDI katika swala muhimu la kucheza SINDIMBA KIFUA WAZI  hata kama tukiachilia mbali lile swala la KUTOA NYONYO  kirahisi zaidi kwa baadhi ya mdadaz HADHARANI katika kunyonyesha TU toto  lenye njaa ambalo limeanza kulilia NYONYO a.k.a HOTELI YA MTOTO mbele za watu.:-(


    Ndio,...
    ....inasemekana ELIMU inaweza kusababisha MTINDIO WA AKILI usababishao  TOFAUTI YA WASOMI WAWILI  usababishao aliyeelimishwa KIKRISTO akubaliane na MTINDIO WA AKILI wakuwa UKIPIGWA KIBAO SHAVU MOJA geuza na jingine UBWENGWE TENA na aliyeelimishwa KIISLAMU au KIYAHUDI  apate MTINDIO WAAKILI umsababishao UKIMBWENGA KOFI SHAVU la kulia  akurukie kichwa halafu kabla hujatulia akukabekabali ifuatwayo na gonge la ngwala  na kama unamakende labda ayasigine wakati  anakutukana PAMBAFU WEYE mbele za watu.:-(


    Swali:
    • Unabisha?

    Cha kusikitisha ni kwamba,....

    .... labda weye kisa sio MWIZI, malaya na UNAOGOPA WACHAWI,  giza na unatabia pia ya KUTOPENDA ukitoka tu chooni mtu MWINGINE aingie baada yako kwa kuwa unajua unautaalamu mkubwa wa kunukisha choo HARUFU MBAYA  kitu ambacho hupendi watu wajue,...

    ... tabia zote hizo  labda ni zako tu kwa kuwa kama ni MALEZI , mazingira  hata elimu , vyote vinalingana na wengine kwenye familia yako BABA mmoja na MAMA mmoja  mliokulia nyumba moja mkaenda shule moja   WASIO NA TABIA HIZO  na pia hata katika  MTAA WENU pale kijijini  JANGILI, mwizi wa mapera  na FISADI wote ni ndugu zako wa damu ingawa baba aliwazaa nje NA WEYE eti  ni ASKOFU ambaye mtoto wako wa pili wakike atakuwa mchawi baadaye akikua vizuri baada ya jitihada zako zote za MALEZI mazuri ya staili za kumfunza kumuogopa MUNGU vizuri.:-(


    Cha kusikitisha ni kwamba,....

    .....labda WENGINE wanaonekana wanaweza ndio maana ni MAPROFESA siku hizi ingawa wewe ulikuwa unawazidi akili darasani na  bado weye ni mesenja kwa kuwa tu HUJARIBU KITU  hata katika kusawazisha tu maisha yako kitu ambacho kimekusaidia kutogeuka MALAYA au mchawi  au tu kisababishacho watu usiue,...

    .....ingawa pia kimesababisha usijaribu kwenda shule  ANGALAU YA MASWALA YA JANDO zaidi angalau ikusaidie kumridhisha umjaliye zaidi hapa duniani ambaye ni MKE WAKO angalau katika tendo lililobarikiwa na SHEKHE liwasaidie kuujaza ulimwengu hata wakati lengo la tendo ilikuwa liwe ni KIBURUDISHO MURUA TU, wakati MKEO ANARIDHIKA  vizuri.:-(



    Swali:

    • AU?

    NDIO,...
    ..... ni kweli KADODA sio KADALA,.....

    ......na labda hiyo ndio sababu kubwa ingawa GIZA lisilo mdhuru  KADALA  hilo halimdhuru KADODA,...

    ...ila KADODA anaweza geuka JAMBAZI ajifichaye GIZANI na KADALA akageuka aogopaye GIZA kwa kuhofia ajifichaye gizani ingawa kiukweli KADALA hamuogopi KADODA  mchana.


    Swali:
    • Ushawahi kujiuliza kwanini aogopaye MAJINI  hajiulizi inakuaje kuna mwingine kazi yake ni kwenda kwenye wenye MAJINI ili kuyaagua na kuyafukuzilia mbali?

    • Ushawahi kujiuliza kwanini UOGOPACHO kukifanya na hapa siongelei swala la kujamba hadharani wengine wanakifanya hilo KIRAHISI kama wanafyonza AISHIKIRIMU YA UKWAJU vile kitu ambacho weye huwezi?


    Ndio,...
    ..... WEWE sio WAO na labda ndio maana LIMPENZI lako baya NA HULIPENDI VIZURI  ingawa lenyewe LINAKUPENDA SANA kitu kilichorahisisha ukonalo  kwa kuwa ulipendalo kikweli lile ZURI  KINOMA UNALIOGOPA KULIAMBIA kitu ambacho wenzio wanafanikiwa KUFANYA ndio maana wana LIMPENZI ZURI ingawa limpenzi lenyewe eti HALIWAPENDI VIZURI.:-(

    Ndio,...
    .... labda MALEZI, elimu, MAZINGIRA na.......
    .... vyote vinategemea wewe ulizaliwa ni MTU WA AINA GANI na kuna uwezekano pamoja na KUKULIA MAZINGIRA ambayo UZINZI ni DHAMBI ukifanya mazoezi vya kutosha unaweza kujikuta weye ni PROFESA WA UZINZI kama tu wengine ambao wamefanyia mazoezi UFISADI, KABUMBU, au hata kubulogi walivyogeuka MAHIRI ingawa hawakuzaliwa  kukiwa na KOMPYUTA na wala BLOGU hazikuwepo.:-(


    Swali:
    • Hivi si kuna uwezekano kila mtu kazaliwa na chembechembe za UFISADI kwa hiyo klihitajikacho ni NAFASI ya KUFISADI na MAZOEZI ya kunoa jinsi ya KUFISADI vizuri bila kudakwa kama MAFISADI mahiri wajulikano ila ushahidi hakuna?

    • Unauhakika kwanini ni WENGINE na sio wewe MALAYA wakati mchakato wa maisha ni uleule kwako na kwao?
    Ndio,...
    ....Nakubaliana na WEWE,...
    ...kunyoshea wengine vidole KUNA utamu wake.:-(


    NAACHA WAZO hili nikishukuru uwepo wa MIMI na WEWE, wao na WALE kitu kisaidiacho uwepo wa MAFISADI kwa kila uwepo waogopao KUFISADI, uwepo wa MALAYA kwa kila awapo mchoyo wa kuuza tendo la unyumba, UWEPO wa WENYE IMANI KALI kwa kila WAWAPO WASIO AMINI kitu ambacho kinaifanya DUNIA HII iko ilivyo kitu ambacho naaamini  hakiko HIVI au HAKIKUUMBWA KIWE HIVI KIBAHATI MBAYA  !:-(

    Nakutakia SIKU KIBONGE Mheshimiwa hasa ukikumbuka hili NI WAZO TU!:-(

    Tubadili MUSHKELI kwa kumsikiliza YOUSSOU N'DOUR anyuke mkito-Bamba



    Afroman abadili kidogo kwa -Because I got High



    Au tu Warrior King aje live katikakurudisha ustaarabu mkuno -Education

    Read more...

    Sehemu ZA SIRI!

    >> Sunday, May 23, 2010

    Sehemu za siri maana yake sio KIJAMBIO,...
    ...na kama ni siri kuwa una kula uyoga  mbele ya wanywao mbege  kisiri labda hiyo si siri.:-(

    Na kuna wenye sehemu za siri ambazo zinanuka kwa kuwa wanazichukulia ni sehemu za siri na sio KIJAMBIO,...

    ......kitu ambacho kinafanya KUNA waaminio leo hawatasababisha mtu akazinusa  SEHEMU AMBAZO LABDA NI  siri.:-(


    Swali:

    • Unauhakika  unakumbuka sehemu za siri labda hazikuumbwa ili zinuswe?
    • Unafikiri una sehemu za siri wakati  Binadamu  hana siri?

    Ndio ,...
    ...kuna uwezekano hata jasho la tako sio siri ya akimbiaye hasa kama anaonekana  kwenye mbio ana KIKWAPA..:-(


    NAACHA HII TOPIKI!:-(

    Hebu DDC Mlimani  Park wanyuke-SHEMEJI ISSA





    Au ngojea Di Gaza na Vybz Kartel waongee kitu katika BICHI PATI



    Au tu Vybz kartel aje na Popcaan & Vannessa BLING katika MNYUKO- Clarkes

    Read more...

    LEO ukiwa na hamu!

    >> Friday, May 21, 2010

    ....na mwenye HAMU,...
    ... inasemekana ni kawaida anataka.:-(


    LEO na HAMU...
    ... na mwenye HAMU,...
    ....kama tu wasio hamu ukiwachunguza nyuma ya kitunza kinyeo labda wana TAKA.:-(



    Leo na HAMU...
    ...taka na TAKATAKA na kwa kuwa LEO laweza kuwa jina la MTU labda ni taka ,.....
    .....katika kitakiwacho KWA WATAKAO LABDA ni TAKATAKA.:-(

    Leo katka tamu ya HAMU,...
    ... labda vyote VITAKIWAVYO kwa ASIYETAKA ni takataka.:-(


    Swali:
    •  Ushawahi kuwa na hamu NA KITU  halafu wakati hupendi mabiringanya ukaona biringanya na kufikiria labda BIRINGANYA tamu?
    • Umeelewa?
    • Si unajua si lazima uelewe?
    Wazo la leo NI HAMU  na hamu inawezekana ikawa ni ya BAGIA katika siku ya tamanio la mishikaki kwa mwenye chachandu  ambaye ukimpa MSHIKAKI  kwa kujivunga anaweza kusema anataka ingawa atakacho sio CHACHANDU wala MSHIKAKI.:-(




    NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA KIFALSAFA na usijali kama huelewi hii KINDEGATENI!:-(
    NI wazo tu hili kwako AJUZA!:-(
    Ndio NI WAZO TU HILI  MKUU WA WAJANJA  na sitaniii hata kwako  Mdada mwenye HAMU UIFICHAYO KIJANJA  na PAPAA mwenye HAMU ambayo ina kufanya uchovye cha hausigeli KIJANJA !:-(
    NIMEACHA!:-(

    Hebu nibadili kwa kumpata The great MIKE TYSON atukumbushe ni nini waheshimiwa wasio wajanja wakumbukavyo katika ya -Mike Tyson's




    Au tu Richie Spice anyutrolaizi lawalawa na MKITO - Uptown Girl




    Au tu Richie Spice akiwa ni miongoni wa watu wavutao wakisifiao na hakuna siku nimekutananaye kimemzingua avutachokimemzingua aendelee halafu jiulize ni wangapi UWAJUAO  watumiao wako fiti hivi kuanzia kutunga vyombo mpaka kuimba  walivyovitunga kama afanyavyo huyu katika ndude- MVUKE



    Au tu nimuachie huyu hyu Richie Spice asifie  katika kitu -Brown Girl

    Read more...

    Labda PENYE NIA pana NJIA MBOVU pia.:-(

    >> Thursday, May 20, 2010

    Ndio inasemekana ,....
    ... PENYE NIA pana njia,...
    ....ndio maana MALAYA na MLOKOLE wote wanafanikisha wakilengancho kidude walichokinuia kukipandisha mzuka.:-(



    CHA KUJIULIZA:
    • Hivi Tanzania na RWANDA kama ni nchi zenye NIA kwa nini RWANDA inasemekana sasa hivi kupatia njia wakati Tanzania bado tokea ipate uhuru kwenye nia zake hapapatikani njia au ikipatikana inabonge la makorongo na kama unatakakuelekea Kigoma unaweza jikuta Mbinga?
    • Hujastukia ni kwanini naanza kufikiri PENYE nia pana njia MBOVU pia?


    Nalikatiza hapa hili wazo nyoko a.k.a shenzi kiduchu!:-(
    BAADAYE!


    Hebu tuburudike kwa kudeku maswala ya Wazungu na Watu weusi bila kuwasahau wenye rangi nyingine mwanana katika kidude kitafitiwacho kwa watoto -STUDY shows how children view race bias




    Au tuendelee tu na burudani hiihii katika-








    Au hebu tu Jocelyn Beroad abadili kidude kwa -Ti tak isi



    Au na  Malaika nao walete katika kubadili mkuno  ndude-Destiny

    Read more...

    Tangazo kwa walio Morogoro- PAUKWA!

     





    Ngoma Afrika Performing Arts Co.

    Performances
By Primary School Children
On 20th & 21st May 2010
Bwalo la Umwema, Morogoro
2:00pm to 5:30pm
Karibu!Proudly presents
    PAUKWA
Children
Art
Festival
2010












    PAUKWA is to enable the children to be creative, 
express their imaginations and develop their talents
Kukuza uelewa, kujenga uwezo wa kubuni mambo 
na kufikiri, kuibua na kukuza vipaji





    For more information Contact: napactz@yahoo.com Phone: 0787 292982/0714 679162




    The EVENT will involve Music, Traditional dance; Modern dance (choreography), Storytelling, Drama,
     Poetry recitations, Fashion and designs, Paintings/handcrafts, Singing, Children monologs

    Read more...

    MAONYO ya kileo kwa adhaniwaye anatafuta POOZEO au MCHUMBA !

    >> Wednesday, May 19, 2010



    ``SIMON eeh, MSICHANA ana kesi huyo!´´- ni moja ya onyo hasa marafiki zangu wa MOROGORO hunipa pale wakihisi kuna ZALI aka MTOTO MZURI ananilenga au tu kinamna imetokea mie mwenyewe nimelisifia ZALI kitu nikimaanisha labda mwendo, dimpozi au tu miakili ya kimwana katika kunyambulisha hoja za kitu zikatokea kustua marafiki zangu kuna kunafununu ya kaudhaifu napandikiza kwa ZALI  ,....

    .... kitu ambacho kinawafanya wawe na wasiwasi nini kitatokea bila miye kuijua HISTORIA ya KIMWANA.

    Na wakisema MTU ana kesi MAANA YAKE huwa kuwa inajulikana kashafiwa labda na MME wake, Mke wake, poozeo, au tu shughuli zake vitani wengi wanamuhusisha na mauaji ya MPENDWA mtoto wa mtu ambaye anaitwa marehemu siku hizi kutokana na gonjwa wajanja walihisio lilipewa ujanja na busti ya mashambulizi kwa kuwa mwilini alikuwa hana KINGA YA MWILI.:-(


    Kwa kifupi,...
    ... katika pitapita zangu hasa MOROGORO na ARUSHA nimekutana na mazingira yanikumbushayo stori nilizokuwa nasikia kutoka kwa BABU upareni jinsi utafiti ulivyokuwa unafanywa katika kuhakikisha KIDUME anaopoa ZALI lililotafitiwa ili kuhakikisha KIDUME huingii zali katika kujipatia KIMWANA.


    Kwa kifupi zaidi hasa kama wewe hujatokea BONGo kwa muda mrefu,....
    ......siku hizi SI JAMBO LA AJABU  ukimchekea mtu wakujalio KUKUSHUSHIA BONGE la historia ya UMCHEKEAYE hasa katika mrengo wa  ana KESI NGAPI.:-(

    Swali:
    • Unafikiri leo hapa BONGO kama hupuuzii mambo unaweza kujiamini KUPENDA mtu?

    Samahani NAANZA UPYA taralila hii kwa mwendo wa kusuasua!

    UKIMWI UPO!

    ....Ila UKIMWI wa watu kumtungia mtu nao UMESHAMIRI maeneo kibao niliyokatiza TANZANIA na KENYA mpaka sasa.


    Lakini MAPENZI yapo!

    ... labda pia ni kitu kizuri HICHO kuwa bado MAPENZI YANASHAMIRI hata kwa wale ambao kwa kuwa WAMEWAHI KUFIWA basi ukiwachekea WANAOKUJALI hata kwa sauti ya zaidi ya ile ya TISHA TOTO watakustua kuwa TOTO ZURI lina kesi a.k.a LIMESHAFIWA tayari na limpenzi lake.:-(



    NA ile sifa ya PESA kuwa ni sabuni ya roho bado IPO!

    ... na PESA  katika uwajibikaji wake hasa UKIDHANIWA UNA PESA unaweza kujikuta kuwa kuanzia MALAYA, wababaikaji wa kawaida au mpaka mchumba wa ASKOFU  wote wamekulenga na kama unajali TAMUTAMU ZA GHAFLA unaweza kujikuta umejitafutia kesi KILAINI wakati wala hupendwi wewe ila ni POCHI lako tu ambalo wala halina kitu kihivyo hasa ukizingatia pesa zilizotunisha POCHI labda ni kodi ya nyumba kwa kuwa kujenga NYUMBA  pesa huna.:-(


    Swali:
    • Unafikiri ni wangapi wametungiwa kuwa wanamdudu BONGO nyoso na wapiga taralila tu?
    • Hivi wewe hujawahi kutishika na LIMTU  zuri kisa maonyo ya watu ?
    • Unafikiri watu wanatoa wapi historia na siri  za watu ukizingatia  ukiulizia unaweza ambiwa mapaka ya chumbani kwa watu  na watu ambao hata sebuleni kwa huyo mtu hawajawahi kuingia?

    Ni STORI FUPI tu nazokutananazo safarini MHESHIMIWA na wala usijali kwa kuwa NAACHIA HAPA.
    Ngojea miye niende zangu BAA kufanya mazoezi ya kuacha kunywa POMBE unajua tena wikiendi bado.:-(
    BAADAYE!

    Hebu tujikumbushe Loon wa enzi za Badboy akiwa na Mario Winans katika mnyuko- Down For Me


    Au ngojea tujikumbushe Loon aongeleye UISLAMU na Allah baada ya kugeuka

    Read more...

    MIPANGO ya NCHI IITWAYO TANZANIA kama aiendeshayo angekuwa ni yule aandaaye KICHENI PATI!:-(

    >> Monday, May 17, 2010

    Mipango ya HARUSI,...
    ......ambao wanaandaa HARUSI hufanikisha HARUSI TANZANIA.:-(


    Aandaaye bajeti ya KICHENI PATI Tanzania kabla ya HARUSI,....

    .....  bonge la profesa wa bajeti za KITANZANIA kwa kuwa KICHENI PATI  zina tako kubwa kweli kwa mpenda matako makubwa  KIUFANIKISHAJI   katika mtikiso  TANZANIA.

    Swali:
    • AU?
    • Si unajua Harusi hufanikiwa  BONGO ila kujenga zahanati ni shughuli TANZANIA kama tu kutafuta hela za kuchangia ada  ya shule?


    Ndio,..
    ... kuna walipa kodi BONGO.:-(

    Ndio ,...
    ...tuna RAIS , wabunge, diwani  na mpaka .... BONGO.:-(

    Swali:

    • Hujawahi kufikiria  kama TANZANIA ingeendeshwa kwa umakini wa waaandaa HARUSI  wa TANZANIA hata kama ITAENDESHWA kama kile  kikao    cha kuhusu chupi ya bibi harusi haijalipiwa  labda TANZANIA ingeshakuwa imefanikiwa  kwa kuwa kufanikiwa kwa tendo linuiwalo KWENYE HARUSI huwa  ni muhimu kuliko  chupi YA BIBI HARUSI ni bei gani katika kulifanikisha?


    • Si unajua kutonielewa ni RUKSA?
    NIMEACHA!

    Hebu SADIKI arudie - Do You Hear What I Hear

    Read more...

    MAANA katika MAISHA isababishayo BIN LADEN na RAIS KIKWETE wote hawataki kujiua.:-(

    Kuna sababu NYOKO zisababishazo MWALIMU ajisikie MAISHA YAKE yanaleta MAANA kwa kufundisha,...
    .....kama tu MALAYA ajisikiavyo MAISHA YAKE yanaleta maana baada ya kurizisha mtu kwa ufundi  na UMAHIRI WAKE  katika  kazi yake muhimu ya kusaidia watu katika MGAO wa utupu.:-(

    Swali:
    • SI kunauwezekano maana ya maisha ni nyoko ndio maana MENEJA na MESENJA wanaweza wakawa wanaridhika na kazi zao ndani ya ofisi moja?


    NAACHA HII TOPIKI  HAPA ila ruksa kwako kuiendeleza kimawazo hata kama KWA USTAARABU WAKO  unahisi nimetukana .:-(

    Hebu  tukutane na Mzimbabwe  Prudence


    Au tu tuendelee kusikia kuhusu Prudence

    Read more...

    KUNA uwezekano MJANJA sio YULE AJAMBAYE KISIRI!

    KWA binadamu,...
    .....kitendo kidogo ambacho kila mtu anajua kila mtu anakifanya inaweza kuwa ni ujanja kukifanya siri.:-(



    KWA binadamu,...
    ... haki ya nani hata KUJAMBA kama nia na malengo yako huna uhakika na wakuzungukao wana kuathiri vipi inawezekana kama umejaliwa USHUZI WAKATI HUO  na ukautoa kwa neema na furaha labda weye ni MJANJA na unaweza kutajirika kwa kuwauzia waliokusikia ukijamba kwa furaha mbele za watu hiyo SIRI.:-(



    Swali:
    • Unabisha?

    Ndio,...
    ... kuna ambao walistukia tokea UTOTONI kuwa kujamba HADHARANI SIO USTAARABU na wakaanza hapohapo mazoezi ya KUJAMBA kwa siri.

    Swali
    • SI unajua sikuzungumzii wewe?

    .....na HAKI YA NANI TENA,...
    ... kama hao watu kama WANANUKIA PAFYUMU NZURI unaweza usistukie wakati umekutananao WAKINUKIA VIZURI kuwa wakati huo labda wametoka KUJAMBA au kwa lugha ya kitaaalamu ,...

    ....wametokea kuachia USHUZI.


    Swali:

    • Unauhakika ni mara ngapi katika uwaaminio kama vile , PADRE, mchungaji , SHEKHE, RAIS ... wakati wanakupa hoja zinukiazo vizuri bila wewe kustukia walikua wanaachia ushuzi  wakati huo WAKIKUPA HOJA MWANANA au walitoka kuachia ushuzi wenye undugu na mayai yaliyooza kitu ambacho huwahusianishinacho wakati msikilivu  na wakati huo una busara?

    • Si unajua kuna uwezekano hapa siongelei KUJAMBA aka USHUZI ?
    • Unauhakika wewe MJANJA?

    NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA.:-(


    Hebu tusikilize ya Valentin Abe



    Au ngojea watu wajaribu kutuchekesha..

    Read more...

    Kuna maelezo ya MPENZI ambayo labda SHANGAZI hatakiwi asikie.:-(

    Kikukunacho kueleza wengine labda ni BOMBA,...
    ... lakini  kuna MAELEZO  kwa MPENZI labda sio busara MAMA YAKO  ajue  .:-(


    Ndio hata katika MTONGOZO bomba,...
    .... ambao unasababisha  mahausiboi wote mtaani wanafikiri dili ni MAMA MWENYE nyumba WEYE ya kwenye kona ndio unalipa zaidi katika  siri za ushujaa huo wa mama mwenye nyumba,...
    ....si lazima  SIE WENGINE tujue.:-(



    Swali:
    • AU?

    Na wakati MJOMBA anasikiliza MAONGEZI alengwayo SHANGAZI,....
    ....inaweza sababisha MPAKA MJOMBA  AKATWE mizizi ya UTAMU wa SHANGAZI kama nia ni kuokoa uwezekano  hata wa uwezekano  ZILIPENDWA YA SHANGAZI inaamsha anasa ZILIPENDWA za MJOMBA kisa kasikia tu aambiwacho shangazi hasa kama kiokolewacho ni UJOMBA TU.:-(

    Swali:
    • Kwani humjui MTU ambaye anataka KUSIKILIZWA ili tu aeleze wengine kisa kagundua kusikilizwa  ndio tamu yake ilipo na KWA HIYO ANAHISI ITABIDI  aongee tu  hata ya chupi wakati kikao ni cha sidilia?

    • SI unajua kuna uelezwayo mengi ambayo hutaki kusikia ila kwa kuyasikiliza kuna watu siku hiyo walilala vizuri kisa wamehisi wamesikilizwa?
    • Unafikiri aelezaye yasiyokuhusu hafanyi hicho katika kujitafutia shughuli kama tu afanyaye mtu bila kuwa na hamu?

    NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA samahani!.:-(

    Hebu tubadili kwa ndude ya Gil Scott Heron ,Jay Z asaidie ili watu fulani wasikie iitwayo - Home Is Where the Praying Is



    Au tu GIl Scott Heron ailete kavukavu ndude katika -Home is where HATRED is



    Au tu ngoje Gil Scott anyuke kwa-Dont give up

    Read more...

    NGUVU ya KUJISAIDIA!

    NGUVU,...
    ... ina sura kama TAKO kwa kuwa TAKO KATIKA SWALA ZIMA LA KUJISAIDIA kinamna ni NENO TU.:-(


    NGUVU,....
    .... inaweza kuwa UCHOCHEZI kama imeelekezwa kwa ambaye NGUVU YAKE ni ile ambayo haina nguvu kwa kuwa HAJIAMINI NA AFANYACHO CHENYE NGUVU na  hata KABLA HAJAKIRI afanyacho ni kupiga KELELE  KATIKA MFANYO UHITAJIO VITENDO   kitu ambacho kinguvu kinahitaji vitendo na sio kukivulia chupi kitaralila TU.:-(

    NGUVU,...
    ...ukiwanayo UNAWEZA usijue nini ni NGUVU kwa kuwa  katika dunia ya sasa unaweza usijue mwenye nguvu ni RAISI au FISADI MESENJA WA RAIS AMBAYE  ni jirani yako  katika kuhakikisha kwa shilingi ngapi una pata choo  kinamna ambayo unaweza ukawa unamlaumu mpaka mama yako  ambaye katika mchezo mzima alicho kifanya ni kukuzaa tu.:-(


    Swali:
    • Unauhakika nguvu ni nini?
    • Unauhakika naongelea nini?

    NI WAZO TU HILI!:-(

    Hebu Frankie Paul aje live kwa kurudia kumsifia mtoto mzuri-SARAH



    Au tu turudi studio Frankie Paul amsifie tena -Sarah

    Read more...

    Kwa MPENZI KINUKA mkojo!

    Ni kweli,....

    ... sijali harufu na labda wewe hujagundua tu bado  kuwa pamoja na harufu kuwa ni moja ya kifanyacho pilau kwako inavutia BILA KUIONJA ila hujali harufu ndio maana  labda hata kuna choo fulani ushawahi kukikimbilia ingawa kinanuka  KIHARUFU.:-(


    Ni kweli,....
    ...tamu ukionja kama kwako ni tamu kweli  kimgido ,...
    ...kama inanuka,.....
    .....cha mwisho kusumbua MUONJO WAKO si harufu.:-(



    Swali:
    • AU?

    Swali kwa MPENZI kinuka MKOJO;....
    •  SI unajua anogewaye na CHAKULA wakati wa njaa huyo hana njaa vizuri?

    • Si unakumbuka mwenye njaa umuhimu ni kushiba na sio kushughulika na  swala la maharage yanajambishaje?

    Ndio,...
    ....kuna uwezekano mkubwa anogewaye na CHAKULA wakati kinanuka ukitaka kumgawia tena chakula katika KIBAKULI KILEKILE akakubali kwa nguvu zote KUGIDA tena,....


    .....maana yake ANAUMWA na njaa VIZURI huyo,  zile njaa za kumgeuza asiye penda kugida akagida tu hata ukoko wa mlenda wa jana kwa kuwa KULA  CHAKULA ni tofauti kama ulaji wako  ni katika staili ya kusikilizia utamu  au tu ni kwa kuwa  unakula kwa kuwa una njaa.:-(



    NI WAZO TU HILI ambalo lina UTAFITI HAFIFU NYUMA YAKE mheshimiwa  .:-(

    NAACHA WAZO!

    Hebu Twende SenegaliViviane Ndour abadili kwa mfinyo- Fima Tollu







    Au tu AFFO LOVE alete alete tena coupe decale katika -INFIDELITE Sexy Boulance

    Read more...

    Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


    Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

    Partner

    save mt. Kenya campaign
    In partnership with africapoint.com

    Taswira BANANGENGE

      © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

    Back to TOP