Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UNAUHAKIKA unafikiria JIPYA leo AKILINI lililo TOFAUTI sana na Ulivyofikiria JUZI ?

>> Saturday, June 28, 2008

INAWEZEKANA hakuna JIPYA!:-(

Kuna mambo , ni staili yako ya kuyafikiria leo itofautishayo ULIVYOFIKiRI mwaka juzi!
Kwa ujumla inawezekana kila siku tokea uzaliwe kuna mambo yajirudiayo ambayo siku nyingine eti utanikuta nimenuna kana kwamba ni jambo jipya!

Sasaaa.....
Kutokana na taarifa bwelele kuhusu NANIHII zote watu wajuazo ,nikichezea moto nikaungua, na maswala ya ukicheza peku si lazima upate au umgawie mimba yule nanihii , SI ni jambo lijulikanalo na KWA HIYO nikipata UKIMWI au kwenda MOTONI au akipata mimba, pale nikifanikiwa kufa, si nisi- AU asi-shangae?

AU?

INAWEZEKANA tokea asubuhi mpaka jioni , ni chaguo lako tu la nini au nani UNATAKA kiuumize roho au kiangalie mnato katika makalio yako ili ustukie LEO ambacho KILIKUWEPO jana au walikuwepo tu tokea msimu wa UKWAJU.

Swali:

  • Unafikiri ni mangapi uyapitayo njiani bila kuyaona lakini unamstukia nanihii?
Samahani narudia mcheuo...
Nahisi labda fikira zako za jana zinaweza kuwa ndio hizo hizo zikuzinguazo leo ila staili tu ndio ya leo inaweza ikatofautisha MAPENZI yako kwa NYERERE , KIGOLi au RAis MUGABE.
Kwa mfano:

  • Kama una njaa leo , utafikiria kuhusu maswala ya kula kama juzi tu, labda staili ya kupata CHAKULA ndio itafanana na ya mtondogoo.
  • Kama wewe muhusika huna uhakika na wewe mwenyewe , watu wakicheka leo utahisi wana kucheka kama juzi tu ulivyofikiria.
  • Kama wewe mwanaumume , kuna kamuda kwa siku, fikira za UASHERATI ukiona au ukikosa nanihii zitakuja kama juzi tu , hasa kama mazingira ni ya kawaida na hufukuzwi na kicheche ndani ya muda .(Si ndio maana wenye busara wanashauri tuondokane na UKAPERA?)

Sasaa....
Ni mangapi umefikiria leo ni sawasawa na MWAKA JUZI?
  • Na ni kwanini leo au juzi ya wiki iliopita inawezekana ukawa unahisi UMEFIKIRIA ZAIDI na unakumbuka zaidi UBWABWA wakati jana katika yote uyakumbukayo ukipewa karatasi itachukua muda kuyaweka yote ndani ya kibwagizo?

  • Hivi si Ubongo wa binadamu unafanyiakazi mambo bilioni kwa sekunde?Sasa kwanini unakumbuka unachokumbuka na hukumbuki usichokumbuka?


DUH!
NAWaZA tu hapa na NAACHA topiki!
JUMA fulani NJEMA!

Mpate kidogo Youssou N'Dour na Neneh Cherry wa kupe maswala ya "7 Seconds"


AU ngoja Murray Gell-Mann achokonoe kiduchu hamu yako na yangu ya kudadisi kuhusu swala la:Do all languages have a common ancestor?

Read more...

Limtu LIKIFANYA vibaya BILA kukuambia unashuhudia MFANYO mbaya, UTASTUKIA kanyau?

>> Friday, June 27, 2008

Inasemekana unazaliwa na machale!
Kibaya wakistukia.

Inasemekana kitu kizuri hakihitaji kujitembeza iliutamani kukiiba.
Hata hukohuko chini ya uvungu, waweza kukistukia kama wewe muinamaji au muinamishwaji.

SIKATAI!
Labda ni kweli.

Lakini je ni kweli?


  • Wakoloni walipofika kututawala kuna waliostukia pipi na lawalawa nyama zao kuwa si bomba na kuna walozipenda kama KUBWA JINGA.Kuna waliofikiri wanakuwa wakarimu kwa wageni , wakati waliokuwa wanakarimiwa wakitafsiri ni UJINGA.

  • Kuna watu wakamuua YESU ingawa mpaka kesho ya mwaka fulani wapo watakaokiri YESU alikuwa anawafunza mazuri.

  • Kuna wanaona MFAlme MTUKUFU MUGABE anafanya mazuri kupigania kuikomboa nchi yake tukufu ya ZIMBABWE kutoka kwa wakoloni mwaka 2008 , wakati wengine wakimuona nikatili ingawa anabomba la mustachi kiduchu.


Lakini.....

HELLO TANZANIA !

MWALIMU Nyerere mzuri......

...... hivi mtoto azaliwaye leo, atakumbuka alifanya nini ikiwa wakirio kuwa alikuwa mwalimu wao hawakumbuki aliwafundisha nini?

RAIS Mwinyi mzuri.....
..... kwa aliyezaliwa miaka kadhaa iliyopita, anakumbuka aliruhusu nini kama hivi sasa mpaka UFISADI ruksa?

RAIS MKAPA mzuri...
......si tutakumbuka alijenga uwanja wa mpira kwa sababu sisi ni mashabiki wa mpira wa timu za UINGEREZA?

Rais KIKWETE mzuri....
... si nasikia anasura nzuri ?


SASAAA....

Swali:
  • Hivi ni kweli kila mtu anatamani akumbukwe?


Labda ni kweli waliosema TENDA mema na usingoje shukurani walikuwa wana busara ya kustukia kuwa MAOVU yako+ kutenda VIBAYA ndio vyaweza kuamsha MORI wa UMATI wa kutoshukuru .

AU

Labda tutende mema na twende zetu msalani, na kama tutakumbukwa basi isiwe kwa sauti tuzitengenezazo msalani. Si nasikia tuko wengi hatupendi kuonekana tukitoka msalani tukihisi kuna sauti zimesikika katika kuku wengi?


Lakini...
.....napenda jinsi TELEVISHENI a.k.a LUNINGA inavyo tusaidia kutukumbusha kitu kwa kututangazia matangazo yatukumbushayo ngwagulo au HATA NANIHII ni vizuri kwako kununua.SASA nasikia mpaka unaanza kununua mayayi ya kuku wakati mpango wako ulikuwa ni kula MAYAI ya BATA kama kawaida yako.

Nashukuru pia TELEVISHENI , magazeti NA bila kumsahau kipenzi wazamani REDIO vilivyotusaidia mpaka KUGUNDUA MSICHANA GANI NI MZURI kutokana na MASHINDANO ya UZURI ya MISS MBAGA MANKA. Labda sasa hata yule KIGOLI niliyekuwa nammezea mate, sitaki hata kuonekana naye tukifanya shopingi za mitumba.

CHAKUJIULIZA tu .....
  • ....ni vibaya vingapi twafikiri ni vizuri kwasababu tumevisoma kwenye KAMAsutra au tumeambiwa ni ujanja kula mshikaki?
  • Je kuna binadamu ambaye machale yake ni sahihi tu?

Lakini...

Naogopa wasomi!

COMMON SENSE yao ina kuja na shule na uonapo banda yeye anaona gorofa.

Naogopa walioenda shule!
Wanaweza wakafanya wanayofikiri waliyasoma shuleni hatakama hawakuelewa kitabu na mwalimu.


NAACHA
hapa hii topiki nisije nikaanza kukuambia blogu yangu nzuri ,halafu ukaanza kuamini kuwa ni kweli ina ladha ya NYANYA MSHUMAA:-(

DUH!
Nammisi kipenzi changu kingine katika BASS , Mwanadada MESHELL NDEGEOCELLO, msikilize kidogo kama FUNK inapanda akupe SLAP FUNK

Unaweza kumsikiliza Graham Norton kama hutatukanika kama maneno yanaweza kuwa si matusi kama yanaaminika kuwa si matusi(Usicheki kama matusi ni matusi kwako.Na unaweza usijifunze kitu katika kideohiki SAMAHANI!:-(

Read more...

UHAKIKA wa kununa KESHO!

Kesho yazaliwa leo
yakusubiri KESHO


Nyoka ujauzitoni
ajifunza panya KESHO kitoweo

Binadamu mitumbani
awezajua KESHO chupi yawezawasha

Tokea MTU leo azaliwe
tegemeo la KESHO

Anakula au kulala
ili nguvu zimsalani KESHO

Shuleni ajifunza ujinga
ili ikabilike KESHO

Apata mimba,
ili kumpa mimba TAIFA la KESHO

Njiwa sekundeni leo
Nani amuhakikishia ana KESHO?

Funzo ,
kesho uko hai.
Msuli upo kununa KESHO?

...........................XXXXX...................

Usitishike MDAU!
Nawaza tu ya KESHO, kwani sina uhakika na ya leo.

WEWE je?
Kila laKHERi kwa leo yako ili ikusaidie kesho yako iwe KULIA zaidi ya KUSHOTO!
HASA ikiwa fikira zako kuhusu kushoto ,ziko karibu na tafakari ya mchambia kono la shoto.

BASI Mkuu naacha topiki!

Tulia kidogo TAMANI KAONDO akukumbushe unaweza kuwa MPWEKE kesho.



AU kama MAJAZZ yanapanda, Mcheki kipenzi changu katika BASS na JAZZ kwa ujumla Mwanadada ESPERANZA SPALDING

Read more...

TAMUTAMU nyuma ya kauli;''JAMAA LINAPENDA SIFA HILO!''

>> Wednesday, June 25, 2008

TATIZO la kusifiwa ni jinsi utamu wa sifa uwezavyo kufanya ASIFIWAYE kuanza kusahau kuwa binadamu wote duniani kuna kitu washawahi kusifiwa hata kama ni sifa za jinsi wajuavyo kufunga breki ya baiskeli kwa KISIGINO.

Ni udhaifu tu usababishao KASTAREHE au KAUTAMU upatako UKISIFIWA.
NA...
.....ni vigumu kukutana na binadamu asiyependa kusifiwa.

Lakini.....
....INAWEZEKANA mimi na wewe ni wastaarabu ambao hatuwezi kukiri TUNAPENDA SIFA.
Lakini.....
... INAWEZEKANA, anayedai hapendi sifa, hajastukia afurahiavyo sifa hata kama sifa yenyewe ni ya mashavu yake murua kama embe dodo.
SWALI:

  • Hujawahi kufurahia ukisifiwa sifa za uongo?
  • Una uhakika sifa zako usifiwazo ni sifa?

Labda,....
... chochote afanyacho binadamu ni sifa.

Si ulokole, wizi , ufisadi au hata MENO KAMA NGIRI vyote ni sifa vikiwekwa kwenye sentensi fulani?

Chakusikitisha ni kwamba unaweza kujikuta unalazimika kuishi kwa kujaribu kujilinganisha na sifa usifiwazo ambazo hauna.

SAMAHANI!
Nawaza tu hapa!:-(
Hebu tumsikilize I -WAYNE akikiri katika CAN'T SATISFY HER

au tuwasikilize tu Bascom X ft I Wayne, Richie Spice, Chuck Fender & Capleton

Read more...

Maswala ya kitu MUHIMU kwa binadamu wakati ANASUBIRIA kuwa ''MAREHEMU Alikuwa MTU MZURI!

Tafsiri ya chochote kile yaweza kusababisha mtu awe kapata au kukosa.
Ukifeli mtihani inaweza kuwa ndio somo kubwa kwako la kufaulu mtihani.

Tafsiri ya kuishi miaka mingi, inaweza kuwa ni jinsi tu ya binadamu achelewavyo kufa.

Kuna vitu kibao mtu huweza kusema ni muhimu sana maishani mwake hasa kutokana na ubahiri wake au ukarimu wake kwa binadamu mwingine au hata dunia.

Vitu kama familia, ndugu, marafiki au staili ya kumzimia MWenyezi MUNGU ,ni moja au mbili tu ya baadhi ya yale yawezayo kuwa karibu katika fikira ,ukimuuliza yule au yeye kuwa ni nini muhimu maishani mwake, ingawa inawezeka KWA KULA mlafi kasingiziwa.

Lakini.....
......INAWEZEKANA, maadui, kutofanikiwa au hata shetani atusaidiaye kukumbuka kuabudu Mungu , vyaweza kuwa na umuhimu katika dakika hizi tuishizo au tuziitazo kuwa tuko hai.

Lakini.....

....INAWEZEKANA, naogopa kuamini kuwa kitu muhimu kwangu ni cha kijinga kwako.

Kumbuka tu, tafsiri yako ya kitu inaweza tu ndio ikawa imekufanya uwe na furaha au huzuni leo.
SWALI:

  • Kwa tafsiri yako leo, wewe umefanikiwa au umeshindwa ?
  • Unafikiri tafsiri zako za maisha zinaathiriwa vipi na mtazamo wa jamii kwako?
  • Ushawahi kufikiria tofauti za mtazamo wako kuhusu wewe binafsi UKIWA CHOONI na UKIWA STESHENI ya BASI zitofautianavyo?
NAWAZA TU hapa MDAU!
SIKU njema!


Unaweza kumsikiliza kidogo Matthieu Ricard ajaribu kukupa mtazamo wake wa TABIA za kuwa na FURAHA


Au wacheki wapenzi wapendao kuishi uchi , wakisaidia kutukumbusha mapenzi ya binadamu kwa binadamu ya kibinadamu

Au msikilize tu ABETI MASIKINI kama mimi, akukumbushe kabla ya ndombolo ya SOLO

DUH !Naacha ingawa natamani kukuacha na TPok JAzz

Read more...

SHENZI mimi au YULE!!

>> Tuesday, June 24, 2008

Mapenzi ya kutukana yako kichwani mwangu na kwako tu.
Lakini kuna maneno ambayo hutambulika kama matusi ambayo sijui yanatokea wapi mpaka mimi na yule tunaamini kuwa tumetukanwa.
AU?
Swali:

  • Unafikiri kutukana ni nini?
  • Ushawahi kukasirika baada ya kuamini umetukanwa?
  • Hivi matusi ni nini?

Samahani blogu yangu imezubaa siku hizi kutokana na ukweli kuwa niko kushoto.
Samahani kiduchu kuna haka kawimbo ka KASSAV kako kichwani kidogo:-(

Niko kushoto kidogo a.k.a nchi fulani ambayo kupata internet connection ni ujanja kidogo ndio maana blogu iko nanihii.

LAKINI Unaweza ku -search chochote kwenye blogu hii wakati unanisubiri niandike ujinga mpya tena ukipenda au kama wewe mdau wa kijiwe hiki.
Cheki baadhi ya picha zangu za Vilnius LITHUENIA na......
Photobucket

Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket






SAMAHANI kwa ambaye anaweza kuzinguka!
Kama una nafasi unaweza kusikiliza mziki naoendelea kusikiliza sasa hivi ingawa usiniulize muziki huu unafundisha nini:-(
Mpate basi Snoop DOGGKatika wimbo GO Girl


Usimuangalie hapa kama unamchezo wa kuogopa majini, shetani au mambo yawezayokuwa mbele KIDOGO ya kinyesi kwa KUCHEFUA..... katika wimbo KUUA ni KESI niliyoPEWA.


Pata busara au msikilize Michael Shermer akukumbushe kwa nini nikijaribu kukudanganya unastukia na......

Read more...

Kama BADO unataka kuanzisha KANISA, dini AU kutongoza ili ufaidi nanihii ,JIFUNZE saikolojia ya kitu fulani kiduchu!

>> Thursday, June 19, 2008

Udhaifu wa binadamu kichwani , unakautamukake katika swala zima la kuuchezea.
Tatizo ni kwamba , inawezekana anayechezewa MUKICHWA ni mimi na wewe , na ni yule mpendwa NANIHINO ndio anafanikiwa kutuchezea.

Utamu wa kuchezewa akili ni jinsi unavyopunguziwa mahangaiko ya kufikiria mwenyewe katika kufikia hatima ya kustukia kuwa inawezekana ni kweli Maisha ya amani na upendo yanakuwa rahisi zaidi kama katika UHUSIANO wenu na liMPENZI lako , mmoja wenu ni MJINGA .

Swali:

  • Si inasemekana mafahari wawili hawaishi zizi moja?
  • Si ni kweli kama ushaambiwa njia ya kwenda mbinguni ni nyembamba,huna haja ya kufuata njia pana ya ahera ingawa ushastukia njia pana imejaa nanii za kidunia tamutamu sana ingawa nyingine zinaweza zikawa zinanuka?

Sasaa....

Ngoja tujifunze kitu kidogo kutoka kwa James RANDI hasa kuhusu lile swala la kucheza na akili za watu hasa kama wewe unania kama yangu ya KUANZISHA dini....
cheki basi....


Tuendelee..


Nazimia kweli staili ya Peter Popoff ya kuwafisadi wafuasi fulani ambao kwa sababu za kisaikolojia fulani ukiwaelewa,nahisi wanaweza kukusaidia sana katika kupata wafuasi wa dini yako mpya mdau.
AU?

Hebu mcheki kazini....


Pata kidogo dondoo kuhusu BENNY HINN

Basi Mkuu, NAACHA hii topiki...
Lakini....

Swali:
  • Nani kakudanganya kuwa hupendi kudanganywa?
  • Unafikiri huchagui ukweli usiotaka kuusikia; kama ule wa labda umfikiriaye ni baba yako , ukweli ni kaka yako kutokana na kamchezo alikocheza babu?

DUH!
SAMAHANI!
Hebu tumsikilize huyu MVULANA tena akimsimulia mwenyeuke hali halisi...



Kwa wapenzi wa REGGAE MUSIC , jifunzeni ufanisi wa WAIMBA REGGAE kutoka kwa Clint THE DRUNK:-)

Read more...

Kama wewe ni MSHABIKI wa MCHEZO au timu ya MATOMBO STARS!

Napenda saikolojia ya washabiki au wanadini.

Unaweza kusahau!
Lakini....

Mshabiki wa timu fulani anauwezo mkubwa wa kufumbia macho mambo kibao katika kuendekeza tamutamu au chachu imnasishayo yeye na Litimu lake.

Mkristo akisha amini, HISTORIA nyingine nishai ambazo zinazunguka Ulutherani wake, zinafumbiwa macho ili kuendekeza mtazamo wa yale mazuri au yale yamtekenyao kwa mkao wa kukimbia kwenda motoni!
Nafikiri kamchezo haka , KISAIKOLOJIA, kanapatikana hata kwa wafuatao dini za kuabudu chooni.

Swali:

  • Wengi si tunajifanya hatukumbuki kuwa mpenzi huwa anajamba?
  • Unafikiri ni kwanini watu husimulia ushindi zaidi kuliko shule ya kushindwa?
SITANIIII !
Kama wewe mshabiki wa CHELSEA , Matombo stars,Mshabiki wa timu ya RUGBY afrika KUSINI......au mshabiki wa timu fulani tu na si lazima iwe kusini kwa mwili wa mtu,
UNAJUA HISTORIA YA TIMU UISHANGILIAYO?

Hebu tujikumbushe kakitu kidogo kutokana na vipengele viduchu kutoka katika historia za timu zifuatazo .....




DUH!
NAACHA naacha basi topiki!

Samahani natoka nje kidogo ya topiki , nikichukua nafasi kumshukuru MZEE MANENTO!
MANENTO eeh!
Asante kwa kutonitenga na sijasahau!
Hizi picha kali MKUU!
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

DUH!
SAMAHANI kwa wawezao KUZINGUKA!

Tulia na Montell Jordan akija na Get it on tonight

Read more...

NGUVU ya KICHWA kimoja KATIKA kuchokonoa NANIHII!

>> Wednesday, June 11, 2008

Katika dunia hii ambayo inaweza kukukatisha tamaa kila siku, ni vizuri tu kukumbuka kuwa ingawa KIDOLE kimoja hakiui chawa, lakini kichwa kimoja chaweza kugeuza mitazamo ya mamilioni au hata kusababisha idadi kadhaa ya watoto kibao mtaani!

Katika historia , ni vizuri kukumbuka kuwa kuna majina fulani unayajua na si vikundi ambavyo vilifanikisha mambo kugeuka.
Nahisi unafahamu mchango wa baadhi ya watu nyuma ya majina fulani katika dunia hii ya mamilioni ukoje.

Kuna majina kama...

  • YESU(samahani hapa namchukulia kama binadamu , nisameheni)
  • Martin Luther na ishu zake na UKATOLIKI
  • GANDHI
  • Nyerere
  • Baba yako
  • Nk....
Mchango wa mtu mmoja unaweza ukawa mara kumi ya mchango wa mamia kama unagusa swala katika kipele.
Tatizo ni pale mchango wangu au wako unapomtegemea Kikwete au RAY C


Inawezekana ni wewe , mimi au yeye ambaye atabadili staili ya Watanzania ya KUCHEKELEA kanyau!


Topiki inaendelea........Nisubiri kiduchu!

Mpate Chris de Burgh akija na LAdy in RED


SAMAHANI naweka tena Picha zangu na wadau za mchanganyiko! Naendelea kuwashukuru wadau wangu kwa yote niliyojifunza kwenu na mliyonisaidia, Wadau ambao tumekutana , Wadau niliowaweka picha hapa na pia wadau wote popote duniani!
ASANTE!

(Zinaweza zikawa zinajirudia kutokana na kuzipandisha haraka haraka)

Samahani kwa wawezao kuzinguka!

Photobucket
Photobucket
Photobucket


Photobucket
Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket
Photobucket
Powered by beta.joggle.com


Nakuacha na Queen Latifah akiwa na Al GREEN

Read more...

Inawezekana Unataka kushindana UKIHISI tu kuwa Unayeshindana naye KIBONDE!

Labda binadamu hata wakati anakuhurumia ni kwa sababu anahisi wewe kibonde!

Kuna watakaokubali kuwa binadamu hukwepa kuvamia anachoamini hakiwezekani .

Ni rahisi kumuonea KIBONDE kirahisi tu, hata kama hukiri au hukustukia ni kwanini nirahisi kwako kumpiga kibaka akikuibia pochi kwa kukutishia na kisu kuliko jambazi ambaye anaweza akapora nyumba yako nzima kwa bunduki isiyo na risasi na hata kunajisi kuku wako.


Swali:

  • Hukiri kuwa BARACK OBAMA kwa Watu weusi , amesaidia kutoa ka mwanga kuwa kale KAKIJEBA labda kanapigika ukikaa mkao wa ngwala?




Naacha Basi kwa sasa!

Topiki Inaendelea.. nipe muda kidogo!
Mpate JHIKOMAN kidogo....akikuambia SET ME FREE

SAMAHANI naweka tena Picha zangu na wadau za mchanganyiko! Naendelea kuwashukuru wadau wangu kwa yote niliyojifunza kwenu na mliyonisaidia, Wadau ambao tumekutana , Wadau niliowaweka picha hapa na pia wadau wote popote duniani!
ASANTE!

(Zinaweza zikawa zinajirudia kutokana na kuzipandisha haraka haraka)

Samahani kwa wawezao kuzinguka!



Photobucket

Photobucket
Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket

Photobucket

Powered by beta.joggle.com

Tulia na Tina Turner akisema BE GOOD TO ME

Read more...

UAFRIKA wako ni UARABU kama Asili yenu ni WAZUNGU!Unafikiri WaaFRIKA walijua lini kuwa pamoja nakuwa WAGOGO bado wanahitaji kutambulika kama WAAFRIKA?

Nafurahia sana kusikiliza mijadala ihusuyo UAFRIKA hasa pale Mpare au Mgogo aliyevaa JEANS afikiriapo MYAO achezaye sindimba Hoteli NYONYO nje, au Mmasai ambaye hajazoea chupi kuwa hachezi Uafrika.

Kuna wenye busara wanaodai kuwa wenye uke wavaao nguo fupi, hawafuati maadili ya Kiafrika.

Kuna Waafrika watumiao vitabu kama Biblia , au VITABU tu kwa ujumla ,kuhakikishia umati kuwa maadili yao ni kiboko na kuwa Uafrika wao hauna dosari kama ukilinganisha na wale Waafrika ambao kwao Uafrika ni neno la kujifunza tu na UCHAGA ndio asili waijuayo


Swali:

  • Uafrika ni nini?
  • Unafikiri ni lini ulistukia kuwa wewe si Mzungu au kwakua sehemu zako za siri tofauti , basi , unatambulika kama MwenyeUUME zaidi ya toto jinga katika jamii?
  • Unafikiri ni UAFRIKA kwa watu wenye asili ya Kiafrika kuongoza katika kuamini dini zisizo za asili ya Afrika ?




Naacha!Unajua niko mawazoni tu MKUU!

Nitaongelea zaidi topiki baadaye.......

Pata basi haka kawimbo ka Mighty Sparrow
ambako kalinisaidia kucheza muziki wakukumbatia(Dansi ya kushika kiuno kwa mwenye sehemu za siri hasi) na niliyekuwa na udhaifu naye kwa mara ya kwanza maishani, enzi hizo za karibu na kufikia umri wakuwezesha kumpa mimba asiyeficha nanihii!


SAMAHANI naweka tena Picha zangu na wadau za mchanganyiko! Naendelea kuwashukuru wadau wangu kwa yote niliyojifunza kwenu na mliyonisaidia, Wadau ambao tumekutana , Wadau niliowaweka picha hapa na pia wadau wote popote duniani!
ASANTE!

(Zinaweza zikawa zinajirudia kutokana na kuzipandisha haraka haraka)

Samahani kwa wawezao kuzinguka!

Photobucket
Photobucket
Photobucket

Photobucket


Photobucket
Photobucket
Photobucket
Photobucket

Powered by beta.joggle.com


DUH!
Tulia basi na CRAZY ataBIRI miaka ijayo itakuaje katika kibao IN TIME TO COME

Read more...

Samahani kwa Kupotea kiduchu!

Katika mtafuto wa kuweka maisha katika uzani ambao hauangaishi sana, nikajikuta niko uchochoroni kiasi kwamba, kuna maeneo hasa ya mawasiliano na ndugu, jamaa,maadui na marafiki , yakakaa kushoto kidogo.

Kwa wadau wa BLOGU hii, ..
Samahani kwa kutokuwepo hapa kijiweni kwa muda!:-(
Tuko Pamoja!
Au niseme......

Kabla sijasema zaidi, msikilize kidogo MOS DEF



SAMAHANI naweka tena Picha zangu na wadau za mchanganyiko! Naendelea kuwashukuru wadau wangu kwa yote niliyojifunza kwenu na mliyonisaidia, Wadau ambao tumekutana , Wadau niliowaweka picha hapa na pia wadau wote popote duniani!
ASANTE!

(Zinaweza zikawa zinajirudia kutokana na kuzipandisha haraka haraka)

Samahani kwa wawezao kuzinguka!


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket

Powered by beta.joggle.com

Basi Bwana!
Mpate tu Talib Kweli akikukumbusha KUSIKILIZA

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP