Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

MCHEZO wa KUMIMBISHA au kupewa MIMBA!

>> Sunday, September 30, 2007

Swali:

  • Hivi unamjua mtu aliyepewa mimba?
  • Hivi nani anaamini kuna mtu anaweza kupewa hako kakitu?
  • Unajua nini maana ya kumpa na ni nini kinatumika kumpa yule.......?

Mwenye SAUTI KUBWA anaMIMBISHA mara NYINGI , ndio isemekavyo!

DUH!

Sijui ingekuwa mwanadada, ndiye anayeandika huu upuuzi, angesema kuwa mwenye sauti nyororo ,ndio anamimbishwa kirahisi?

AU?
  • Inasemekana wanaume wenye watoto wengi , wanakibezi!

Cheki hii stori ya wa Tanzania wa kabila la HADZA
, kabla hujaanza kunibishia.

Tuhame kwenye .... turudi kwenye sauti.....

Mwenye sauti kubwa asiposikika, atakuumiza masikio au kukusumbua.
Mnyonge mwenye kujaribu kusikika, ana uwezo wa kutatua katika anga fulani kuliko ambaye , anangojea huruma ya KIKWETE.

DONDOO:
Umestukia jinsi wenye sauti wanavyosikika kuliko WANYONGE?


Mpate huyu mchaga , aitwaye PITA TESHA. kabla sija kuacha na baadhi zangu kidizaini.






Wapate wadau wangu fulani wachezao timu ndogo..



Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Waangalie lakini wakiwa angazao...


Samahani kwa picha ifuatayo kama umefunga.

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Tuendelee!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
DUh!
Naacha basi!
Endelea na Peter tosh!

Read more...

HIVI KWANINI TUNAONGEA NA MAREHEMU?

>> Saturday, September 29, 2007

Najiuliza tu!
Kuna mwenye uhakika kuwa, Marehemu alikuwa MTU Mzuri, ANATUSIKIA?

DUH!

Naacha!

R.I.P wote mliotangulia!

Swali:

  • Hivi kwanini tunataka MAREHEMU WALIKUWA WATU WAZURI, wapumzike mahali fulani wakati wengine waliotutoka tuna jua walikuwa wanafurahia kuchakalika sehemu sehemu kuliko kupumzika?
DUH!
Tulia na Awilo wakati ukifikiria kama nilichoandika ni sahihi au sio...
AU?



Read more...

UMEDINDA?

  • Tatizo la kudindisha, ni kupooza, baada ya ujanja kufikiwa au kutofikiwa.
DUH!

Mheshimiwa Mwalimu Nyerere alidindisha na UJAMAA na CCM, mpaka baadaye kidogo .

AU?

Baadaye kidogo, akamruhusu Mheshimiwa MREMA avae raba , na wengine kadhaa waanzishe NGO KINYUME, ziitwazo VYAMA vya UPINZANI!

Inasemekana , hata Mheshimiwa Mandela, baada ya kudindisha kwa miaka kibao , sasa hivi ame.........

Duh!

Matatizo ya kushindwa kudindisha, yana dawa ndogo ndogo, kama VIAGRA.

Swali:
  • Nani kasema kuna mtu anashindwa kudinda?
  • Akishindwa ni tatizo?
Lakini......

Tatizo la dawa hizi zisaidiazo au kuongezea urefu wa kudinda, zinamsaada usiodumu kama nguvu zako za kuguna.

Huwezi kuguna muda wote.
AU?

Piga ua,..
...siku moja tu , hata usipo jitahidi kuikwepa..
itafikika, ambayo, nguvu ya kusimamia jambo uliaminilo kutoka chini na juu ya moyo wako, utaamua kulikodolea macho tu, kulaumu na kuguna kisirisiri, kutokana na MDINDO kusinyaa.

DUH!

Nisikutishe!

LAKINI KUMBUKA WEWE, MIMI NA Binti HALUFANI, NI BINADAMU TU!

Huwezi kufanikisha mambo yote.

AU unafikiri KAMBONA na NYERERE, wote wangefanikiwa katika muda mmoja kufika pale........., wewe unge....

DUH!

Naacha!

Pata wimbo wa Kevin Lyttle abadili somo.




Read more...

TAFADHALI! PIGA KURA KUISAIDIA KAZI ILENGAYO KUELIMISHA MATATIZO YA KINA MAMA na WATOTO

HABARI!

Naomba ubonyeze hapa http://www.funsahara.co.uk/zafaa_2007_award_nominees.htm AU www.zafaa.com halafu bonyeza link ya NOMINATE HERE. Ukifunguka huo ukurasa naomba uende kwenye category ya BEST DOCUMENTARY FEATURE, pale kuna filamu tatu, ya kwetu (ya Watanzania) ni PLAY YOUR PART - TANZANIA. Naomba uipigie kura ili ishinde tuzo za African Academy Awards. Naomba uwaambie na watu wengine wengi.

SAMBAZA HABARI HII KABLA GIZA HALIJAINGIA. Filamu ya PLAY YOUR PART inapambana na Filamu kutoka Zambia na moja kutoka Uganda. Hadi sasa PLAY YOUR PART inaongoza kwa kura.

Tafadhali ongeza idadi ya kura zile ili kilio cha wakina mama na watoto wanaopoteza maisha kwa sababu ya afya mbaya ya uzazi kisikike zaidi.

PIGA KURA kwa PLAY YOUR PART Asante sana.

To the English Speaking Friends:

Please visit www.zafaa.com or http://www.funsahara.co.uk/zafaa_2007_award_nominees.htm and on the category "BEST DOCUMENTARY FEATURE" vote for the film "PLAY YOUR PART" from Tanzania. Your vote will add to the voice of the mothers and children who are fighting for the better maternal health.

Tuko Pamoja!

Bob Sankofa

www.mwenyemacho.wordpress.com

Tukiachana na Tangazo.

Mimi namsikiliza Bill Withers sasa hivi....
Wewe Je?

Read more...

WAKATI , naikumbuka SikuKUU Ya Milleniamu ya Ethiopia....

>> Friday, September 28, 2007

Samahani !
Kabla sijaanza........,
.........angalia picha ya MTU aliyesababisha unaamini, tarehe uliyozaliwa ndiyo yenyewe.

Naamini unajua jina lake laki -PAPA alilojipa.
Si alivyozaliwa alikuwa anaitwa Ugo Boncompagni.
DUH!
Mcheki basi!























Swali:
  • Umezaliwa siku gani vile?

  • Hivi Ukiwa umezaliwa tarehe 29 mwezi wa pili, aka Februari 29. Bethidei zako unazifanyaje mwaka usiofikia februari, 29?
Nikiongelea tarehe ,
siongelei Maulidi wala Krismasi ,aliyoibadili au kugundua
MJANJA.

DUH!

Dondoo:

Naamini unajua kulikuwa na kalenda nyingine enzi za wanzabanga!

AU?



Binadamu ana mambo ya ajabu,
anayofikiri kuwa anayajua.

  • Kama wewe Binadamu, usibishe!

DUH!

  • Bisha!
Kwa sababu Simon, anasema, yaliyoko mawazoni mwake, ambayo ni wewe unauhakikanayo, kwasababu, shehe na mchungaji wako, bila kumsahau , baba, mama , mwalimu , au yule umuaminiyo, ambao wamejua maswala kutoka kwa .............amesema ingawa huko kwa... huna uhakika ni ukweli.


DUH!

Swali:
  • Waliokufundisha wayajuayo, wamejifunza kutoka wapi? (Au wameshushiwa ujumbe pale kilimani ambako hakuna aliye shuhudia?)

DUH!

Wakati nchi nyingi ziliacha kutumia Julian Kalenda baada ya makubaliano ya wajanja wakiongozwa na Papa Gregory , akisaidiwa na aliyeanzisha utundu wa kubadilisha , aitwaye Aloysius Lilius, kalenda ikabadilika kutoka ya ki- ROMA kwenda...

DUH!

Nisikufiche !

Narudia Swali:
  • Una miaka ufikiriayo unayo?
AU niulize .....
  • Hivi unafikiri unamiaka mingapi?
  • Hivi unafikiri utafanya nini ,ukijua uchovu wa kalenda ikufanyayo uamini leo ni ijumaa, na ......kuwa Waithiopia , Waroma, na Sisi, tumfuataye Papa Gregori na...... kuwa tunacheza pata po.... .......?
DUH!

Si endelezi!
Nimeacha!
AU?

Samahani kidogo naingia kwenye Ubudhisti....

Naamini wewe muislamu usiyefuata kalenda ya kiislamu, nakufuata ya Papa Gregori, isemayo leo ni tarehe 28, na wewe ufuataye kalenda ya Papa gegori ambayo ingekurusha miaka saba ndani ya siku moja, Papa na kikundi chake walivyoamua kubadili siku kutoka za kiJULIAN kwenda Kigregory,kuwa leo ni miaka saba zaidi, na wewe ufuatayo kalenda nyingine ambayo kama Muislamu umefunga, kama mimi , unaweza ukawa unafuturu sasa hivi, kwa mambo ambayo kama wewe ni Mkristo unaweza kuamini baraka fulani za utamu sijapewa na......

(Dondoo:

Umependa sentensi yangu ndefu hapo juu,isiyo nampangilio , bila kukwazwa?)

Samahani nagusia kwenye mwanamme na mwanamke...
DUH!

  • Uliyekuwa unaamini mvulana akidinda na binti akapata mimba kuwa walifanya utundu tarehe fulani....Hiviiiii....MNAFUATA KALENDA GANI na YA MJANJA GANI?
Ngoja tupate kwasababu gani wanaume hawatosheki na uhusiano na KIPENYO, mpaka wapate VIPENYO



SAMAHANI WANADADA!
DINAH!
Nipe mambo!
AU?

NIPENI Wanadada upande WENU uelezao KWANINI HAMUTUWEZI, TUKIWA WENGI TUKIwaSHEA?

SWALI :
HIVI KUnaukweli WANAWAKE, hamtujumlishi?


UKiRISTO
HAUJANIPA JIBU!




DUH!


Samahani nakuondoa katika maswala hapo juu, na....

Au Unayakumbuka?

Jisahaulishe basi...!

Swali
  • Hivi hizi ndombolo za solo aka ngwasuma, tuzipendazo Tanzania, tunaelewa wanasema nini? Hasa wakiimba vizuri kwa lugha za kingwasuma?
Nisikufiche ,!
Nanihii na...zinachezeka na najua tunaimbiwa kwa kiswahili nyimbo kedekede!

AU?

Turudi kwenye Kalenda...

  • Katika kubadili kutoka Juliani mpaka Gregori kalenda, ilichukua dakika moja ambayo inasababisha, Ethiopia iwe miaka saba nyuma leo hii kutoka katika miaka ambayo, Tanzania inafuata.
Swali:
Hivi Watanzania, wabudhisti, mbona hawastukii kila tarehe muhimu zisizo za kidini, hazifuati tarehe za kiislamu?

Kwasababu ,
naamini, wanadini, hasa Wakristo na waislamu, wana nyege za kufuatilia mambo fulani ambayo ukigusa kuongelea kinamna naongelea, lazima uungue.

AU?

Samahani lakini!

Kwenu wote Wanadini, hasa wakristo ,kwa kuwazingua !
MsiniSOKOINE BUREeee !
Kisa niko mawazoni,
wala hata gari la ubunge na ... sijapata.

DUH!

Naacha!

Nitaanzisha kalenda yangu karibuni.

Atakaye kuifuata anyoshe kidole juu!
DUH!

Ushawahi kufikiria utajisikiaje mara tu ukigundua miaka yako imeongezeka kwa miaka saba ndani ya siku moja, kama leo, kwasababu nimeamua, kutokana na ushauri wa muangalia anga?

DUH!

Usitishike!

Mpate Busta Rhymes atulize...
Samahani lakini!
Haongei lugha nzuri.

Read more...

Mtembelee FEDE.BLOGA MPYA kutoka TZ..



Msanii BABU K,nukta

Si umtembelee tu, uamue mwenyewe?

DUH!
Sisemi sana!

Kabla hujamtembelea FEDE
Nakuacha na Bill Withers wakati unamtembelea FEDE

Read more...

UTAMUACHAJE MGENI PEKE YAKE?

>> Tuesday, September 25, 2007

Utamaduni ni kitu cha ajabu!
Unaweza kukufanya umchinjie mgeni kuku, ingawa huli kuku kama mgeni hatokei.

Nakubaliana na wewe,
...........kuhusu swala la ngojea mgeni aje ili mwenyeji ale kuku.

Ushastukia?

Siku nyingine......
.......unataka kuwa peke yako ingawa ......
mwenyeji wako anaamua kutokukutenga.

DUH!

Sasa utafanyaje?

Nauliza kwasababu, ukifika nyumbani kwa mtu , huyo mtu ana ..amini ,umeenda kwake kwa sababu ,ulitaka kwenda kwake.

Swali:

  • Hivi, unajua unaweza kwenda kwa mtu kwasababu anapika dagaa wa nyasa na si wa Kigoma?

Hivi , si,
.....unaweza kwenda kwa mshikaji, kwasababu hukutaka tu, kwenda kwako.......?

DUH!...

....(
Samahani sentensiYa juu ya SWALI, inaendelea...)

Unaweza kwenda ....
kutokana na kupendwa sana nyumbani,
,,,,,, kiasi chakupewa chakula kikubwa,,,,,,
ambacho hukihitaji siku hiyo?

Swali:
  • Unafikiri kupendwa ni kitu kizuri?

  • Hivi , chakula kikubwa ni nini?
Naacha!
Tulia basi na Maxwell

Read more...

KUIVA ni MWANZO wa KUOZA kwa TUNDA!

>> Friday, September 21, 2007

Wengi wetu hufurahia tunda likiiva.

Tatizo la tunda likishaiva, ni muelekeo wake.

Lakini....

Tunda likiiva , hatua inayofuata ni kuiva sana, halafu kuoza.
Tunda lililooza wengi tunalikwepa ingawa ndio mimba ya mbegu zitubarikizo na mimea kedekede.

  • Kuiva ni kufikia katika kikomo cha kipengele.
Chakusikitisha ni kwamba ukifikia kikomo cha kipengele unaweza usistukie mwenyewe.
Halafu wanaostukia wanaweza wasiwe na uhakika na ulipofikia, kutokana na kukumbuka yale wayahusianisho na kipindi mambo yako yalipoiva.
  • Kuiva ni kufikia mwisho wa ngazi.
Ukifika mwisho wa ngazi kilichobakia ni kushuka.

Duh!

Ukifikia ngazi ya mwisho ,unaweza ukapaa, kama unamabawa au helkopta ya kukuchukua hapo ngazini na kukupaisha juu zaidi ya jengo ambalo kiurefu huzidi ngazi.

WIKI MWISHO NJEMA!
Burudika na Mr Nice

Read more...

Haja Ndogo!

>> Thursday, September 20, 2007

Haja ni haja!
Nani kasema haja ndogo , udogo si neno
Haja ndogo na kubwa ni maneno
Umuhimu wake haupimiki kwa neno

Haja hupindisha msumeno
Msumeno uwekao butu meno

Haja kubwa na ndogo si neno
Ni kitendo kiwakilishwacho na neno
Lakini sauti upatiwazo katika uroda ni maneno.
Yasemayo hufiki, unafikia au naumia kutokana na yako meno.

Kuuma na kupulizia huhitaji nanihino
Lakini haja kubwa au ndogo huhitaji maneno
Ingawa chooni bado panono

Kama unahaja...
pata hata kama siye hautatupatia neno
........................................



Usistuke usiponielewa!

Nakuacha na Erykah Badu na Blues Brothers Band

Read more...

ASANTE TOTO JINGA KWA KUTOENDA SHULE!

Swali:
Unajua unaweza kujua zaidi kutokana na kutofundishwa?

Wanadamu maishani ni wanafunzi.
Unaweza kumlaumu mtu kwa kitu ambacho wewe mwenyewe ulijifunza kwa kubahatisha, kutokana na nafasi uliyokuwa nayo kama mtoto wa mganga wa kienyeji.

Lakiniiiii.......

Kujua mizizi fulani na jinsi ya kupaa na ungo, ilikuchukua muda.

Kumfikisha kilele mtu.......,

....... cha kumdanganya, kumuambia ukweli,....... kimapenzi,.....
ndio kabisaaaaaa,..... ukibadili mtu, nukta za utamu unaendelea kujifunza upya.

Swali:

  • Ushastukia! Kumdanganya mtu, saa nyingine inabidi ubadili jinsi ya kudanganya?
  • Au, unaamini wanasiasa kutokana na kufanikiwa kwao kwa kutumia uongo uleule?

Kutokwenda shule, sioni ni ujinga mara nyingine!

Nashuhudia wasomi wanavyofanikiwa kufanya vizuri ujinga baada ya kwenda shule.
Wengi wanaotundika vyeti vyao sebuleni, ni kweli wameenda shule.

ILA.......


Tatizo la kwenda shule , ni kipimo chake!
Kipimo chake, ni cheti´chake , ambacho aliyeamua ndio kiwe kipimo, ndio mjanja, na aliye elimika.

Swali:
Shule ni nini?

Shule zetu za jando na kutairi wanadada, zilikuwa bomba.
Zilitufundisha jinsi ya kuishi katika mzani wa nani anaamua na nani anaitikia.


Kwa mwanamume, ilikuwa uroda sana katika tamaduni nyingi, kutokana na uwezo wao wakuamua kucheza bao, wakati mwanadada anakuchemshia maji yako ya kuoga nyumbani, na ile minofu ya nyama iliyonona, watoto wako wanakatazwa kuigusa, unaahifadhiwa.
(sijui kwanini naongea swala hili katika tensi iliyopita!)

Swali:
Hivi unafikiri Mwalimu wa kwanza duniani alikwenda shule gani?


DUH!


Ushastukia!

Mwalimu wako wa dini, si lazima alikuwa anajua jinsi ya kumloga nanihii....?

AU?

Shule ni kitu cha ajabu.
Kwa sababu ni kitu kigumu kiasi watu fulani wakaamua kurahisisha na kujenga majengo ili uweze kunyosha kidole nakusema; nilienda shule ileeee!

Shule kiboko , kwa sababu inaweza kukukaririsha vitabu kibao ambavyo utajisifia sana unapofanikiwa kufaulu mitihani fulani, na katika kikundi, kuonekana mkariri fulani, samahani, kuonekana unaakili.
(Samahani lakini kwa kukutambulisha! Nilikua sifeli darasani.Ila baada ya kulijua darasa nikastukia nafeli kila siku. DUH!)

Swali:
Shule ni nini?

Darasa je?

Ushastukia shule fulani, zinafanya watu fulani wajisikie kufakufa?

Samahani!

Siongelei shule za kidini hapa za kujilipua, ambazo nyingine Bin Laden Alifeli.

Si unajua tena!

Bin Laden hajajiua, ingawa wafuasi kadhaa wamefanikiwa kuji ......

Duh!


Naongelea shule hasa za kujiua ukishachoka kuwa hapa duniani sasa hivi.

Ukijisikia kufakufa, unaweza ku google shule hizi na kufundishwa.

Naamini unajua kuwa utakuwa unajiua ukifuata hizo shule ,kitu ambacho nitakushangaa kama unauhakika kuwa ni jambo la busara.

Swali:
Hivi kwanini watu wanajinyonga wakati kuna njia rahisi za kujiua?


Samahani kwa wote ambao darasa linachukua kitu kikubwa katika kujijua, mpaka hauwezi kua Zubeda au Halufani bila kujitambulisha kwa cheti fulani!

Lakini najua kuwa Marconi aliyerusha matangazo ya kwanza kutoka bara moja mpaka jingine, alikuwa mjinga darasani.

Namkumbuka Leornado Da Vinci, alikuwa mjinga katika wasomi waliokuwapo enzi zake.

Watu wameenda shule bwana!

Naweza kuwaongelea wengi kama akiana Albert Einstein ,bila kumsahau.....aliyegundua kujisaidia porini.


Duh!




Ningekuwa siwaogopi , ningewauliza shule Yesu na Mohamedi walizoenda.
Lakini najua hawa .....nitakua nimeenda mbali .
Si unajua
,ni vigumu kuelezea mahusiano yao na Mungu au Umungu wao
?


Metty najua wewe mdini:-)

Swali :
Hivi Mkwawa ,Zulu fulani na .........walienda shule gani?

Duh!

Nimeacha!
Samahani!

Lakini...

Shule au sio shule , wote tunatafuta kujazia kakitu fulani .
Kujazia kale kasehemu ambako kwa sababu sisi ni binadamu, hakazibiki.
Mzani tu ndio unaegemea upande ambao kaubongo kakibinadamu kanatuambia kunaupungufu.

Swali:
Si unajua ubongo unaweza kukushauri uchambe kwa maji kwa sababu makokoneo ya karatasi huacha vimavi fulani?


Duh!

Tulia na OSIBISA watukumbushe miaka ya sabini jinsi bendi za Afrika zilivyokuwa na wanamziki bomba.

DUH!
Najua wanamziki bomba kutoka Afrika wanatawala na miziki bomba sasa hivi pia:-)


Read more...

USISAHAU KUPITIA KATIKA JUMUWATA!

>> Tuesday, September 18, 2007

Tunaomba usisahau kupitia JUMUWATA kuchangia, kukosoa,kukemea,kushauri,kuondoa, kusogeza....ilikuchangia muelekeo wa Jumuiya ya wanablogu Tanzania.

Mchango wako unahitajika wewe mwenye blogu na hata usiye na blogu ilikujenga muelekeo uliochangiwa na wengi na sio kikundi cha watu wachache.

Kama unablogu tunaomba uweke tangazo hili ili liwezekuwafikia watu wengi.

KARIBUNI WOTE!
Uongozi.

Read more...

UNAWEZA KUPIGA NDEGE WAWILI KWA JIWE MOJA.

>> Saturday, September 15, 2007

Ukilenga ndege mmoja na kupiga wawili, kumbuka umepiga wawili tu na sio wote.

DUH!

Najaribu kusema....

Jambo moja ulifanyalo ,laweza kuwakilisha mambo mawili.

Unaweza kuongea ujinga na hekima katika sentensi moja.

Inawezekana ukiambiwa unaongea busara , ni kwasababu wasikilizaji hawajastukia jambo la pili liwakilishwalo katika hiyo busara , ambalo ni ujinga .

Swali:
Hekima na busara ni nini?

DUH!

Lakini ukipiga ndege wawili maana yake hujapiga wote, ila, kama ndege wawili ndio waliopo, basi unaweza ukawa umepiga ndege wote.

DUH!

Hii ni makala moja, lakini inaweza ikawa inawakilisha mambo mawili.
Umestukia eeh?

JUMAMOSI NJEMA!
Nakuacha na baadhi ya picha za jana baada ya kazi!

Powered by www.myfabrik.com


Tulia na Portishead wakikupa kile kibao kiitwacho Kiboksi cha Utukufu.

Read more...

USHASTUKIA !KIPINDUPINDU HUWARUKA VICHAA WALAO MAJALALANI.

>> Friday, September 14, 2007

Watu hukimbilia kusema kuwa Mungu anawalinda watu fulani, ndio maana hawapati kuharisha.

Mimi nafikiri kuna kitu zaidi ya hicho.

Naamini mwili wa binadamu unamambo yake. Mwili wako na wangu vinafanana jina tu. Wewe kama umekwepeshwa kukutana na uchafu fulani, mwili wako ukajifunza kupigana na vichina viletwavyo na uchafu huo, tunaweza tukashea sinia la ubwabwa lakini wewe ndio utakaye tembelea msalani mara kadhaa kwa tatizo la kuumwa tumbo au geti la haja kubwa kutokubali kufungwa kwa idhini yako.
Vichina , samahani virusi, vinaenda gym kila siku , hivyo kama mwili wako haujengi misuli ya kujikinga na virusi hivi, jasho litakutoka.

Kwa bahati mbaya baadhi ya misuli katika mwili wako inatokana na ulivyorithi kutoka katika kizazi chako. Kama kizazi chako hakikujenga kinga zitokanazo na mutation mbalimbali ndani ya mwili wako zikulindazo, ukicheza
peku hovyo, lazima UKIMWI ukuondoe.

DUH!
Sasaaaa....ngojea turudi kwa kichaa......

K
aribu katika kila miji kibao, katika nchi zinazoitwa zinaendelea, kulikuwa au kuna kichaa fulani maarufu mjini.Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo.

Swala hili tunaweza kushukuru serikali na jamii yetu nzima kwa jinsi ilivyofanikiwa kuwaacha ndugu na jamaa mtaani , baada ya kurukwa na akili.


Kwa kuwa jamii zetu zimefanikiwa pia kuacha majalala na uchafu kibao mtaani, mara kwa mara tumefanikiwa kutembelewa na ugonjwa wa kipindupindu mtaani. Inatambulika kuwa vijidudu vya kipindupindu hupenda kuishi katika sehemu chafu ,kama majalala watu watupapo makombo.

Kwa bahati mbaya huku majalalani pia vichaa hupapitia sana kufuatilia makombo ya vyakula kutokana na jamii kutofanikiwa kuwalisha. Hata wasipokula jalalani , ni makombo ya vyakula yaliyochezewa ngwasuma na nzi, ndio waambuliayo mara kwa mara.

Swali:
Sasa mbona kipindupindu kikija hawajamaa kinawakwepa na kumdaka jamaa anayekunywa maji yasiyochemshwa?(Labda ni seme maji yenye vijidudu , kwa maana kuna nchi kibao nimekatiza, maji yao ya bomba au yasiyochemshwa ni salama tu..)

Sasaaa......
Tukitoka kwenye sebule ya Kipindupindu na kuingia chumbani kwenye UKIMWI.........


Swali:
Je , unafikiri gonjwa kama UKIMWI linawapata watu wote baada ya kucheza mchezo wa baba na mama?

Duh!
Hata sihitaji kusema sana kwa hili. Ila nachojua ni.......

Dunia ina mwisho, lakini kuna watu wagumu kuiondoka dunia hii kwa yale tuliyo nauhakika ndio yatuuayo.

Imeshagundulika hata Nairobi kuna wadada hawashikwi na mdudu ingawa wanacheza kiwanja chenye mdudu.
Soma hapa.
Au turudi nyuma kidogo kwenye kastori haka, kalikotokea nchi kadhaa wa kadhaa duniani.

DUH!

Najaribu kusema kuwa, kila mtu na kila siku tunaijenga miili yetu kinamna tofauti. Miili yetu inakinga tofauti kutokana na mabadiliko yatokeayo ndani ya mwili kutokana na tunayo kutananayo kila siku.

Sasa maswala ya mutation ya CCR5 genes au delta 32 yanaonyesha jinsi gani baadhi ya watu wanaepuka magonjwa fulani kama UKIMWI.[Nisikutishe sijui sana maswala ya genetics:-)]

Mimi naamini.....
Mimi na wewe kunakitu kizazi chetu kiliepuka ndio maana bado tunaendeleza libeneke leo hii.
Lakini kumbuka sisi ndio tunaweza kuwa hitimisho la kizazi ingawa kizazi cha Ze Zubeda kikawa kina dunda kwa miaka maelfu fulani yajayo.

Duh!
Mara nyingine kukwepa sana kitu ni kujidhoofisha.Lakini kumbuka ukikumbwa na kabingwa fulani kama UKIMWI , hauna nafasi kubwa ya kupitisha zile jinsi zako kwa kizazi kijacho.

Kumbuka sehemu karibu zote duniani, bado hawahifadhi mbegu za kiume na washikaji zake, unajua tena, wale mayai ya kike ya binadamu yalioathiriwa na vichina vya UKIMWI kwa aajili ya taifa la kesho litakalo jua zaidi jinsi ya kuutekenya udhaifu huu wa UKIMWI na kadhalika kadhaa zitusumbuazo hivi sasa, halafu jamii ikacheka.

DUH!
Usitishike wote tutakufa!
Lakini cheza salama.

WIKI MWISHO NJEMA!
Burudika na Rikki Jai akija na miondoko ya Soca Chutney


Read more...

Jamaa wanachuki na mimi ,NDIO MAANA NIMEPANDISHWA CHEO KAZINI!

  • Shikamoo bosi!Ulaji unanizidi?

Wanaojiita wajanja fulani, hudai kuwa cheo kizuri ni kile kinachokupa ulaji wa haraka.
Unaweza ukakuta jamaa kachukia, anakuna kichwa, kisa amepandishwa cheo .
Katika mazingira ya kawaida unaweza kushanga ni kwanini jamaa hafurahii kupandishwa cheo!
Lakini , utapewa jibu hata pale kwa fundi viatu kwa kusikia porojo zisemazo ; tutaona sasa atamaliziaje nyumba ya kimada wake sasa ,wakati kaondolewa kwenye ulaji.

Naogopa ofisi zisizoeleweka na zisizo na taratibu ziwezeshazo kufuatilia nini kinaendelea.
Kwa bahati mbaya hizi ofisi ni nyingi na nyingine zinajulikana kwa jina Ikulu..
Katika ofisi ambayo haina mbele wala nyuma zaidi ya viini macho na majina ya vyeo vya wajipumzishao ofisini, unaweza kukuta ni dereva au mesenja wa bosi ndio mlaji na aendeshaye mambo kuliko yule Kikwete wa ofisi.

Mara nyingi tunamzungumzia bosi mambo yakienda vizuri au vibaya.
Lakini katika hizi ofisi
  • unaweza kukuta mesenja ndio tajiri, halafu haachi kazi ingawa ana hoteli kadhaa na teksi kibao pale kona.
  • Unaweza kukuta ni aitwaye dereva wa bosi, mwenye nguvu ofisini, anaamua misafara ya bosi na bosi anaitikia kasuku kasingiziwa.

Swali:
Hivi katika serikali ya Marekanni ni George Bush mwenye nguvu?

Nachojaribu kusema ni:
WAKATI unafikiria jinsi ya kumnyima bosi ulaji, kumbuka unaweza ukawa umelenga pembeni ya goli.Inawezekana hata bosi mwenyewe hajastukia kuwa hausiboi wake nyumbani ndio mjanja,kuna kaasali kanakosababisha anajilamba na kukubali mshahara mdogo.

Na pia tusisahau kutafakari haka kakitu ujanja, kwa maana janja nyingine mimi na wewe tunazifagilia lakini manufaa yake ni msamiati mgumu.
DUH!

Kuna kawimbo ka Jimmy Cliff kako mawazoni......
Kapate basi:

Read more...

HAKI ZA TOTO LA KUKU WA KIENYEJI ZIKO WAPI?

Tukumbuke:

  • Nchi kibao ni kama kibanda cha kuku wa kienyeji. Mmiliki wake hahitaji kumlisha kuku mapumba, ili amfaidi kuku na mimba yake.

Ngoja tumfuatilie kuku wa kienyeji....


Kuku wakienyeji hujitegemea.
DUH!
Asubuhi huenda kujitafutia na usiku anarudi kufungiwa.


Swali:
Unafikiria ni kwanini kuku aliyehuru anarudi kibandani jioni mwenyewe kwa hiari yake?

Lakini.....

Tunachojua ni kwamba:
  • Jioni, kuku wa kienyeji hurudi kibandani.
  • Asubuhi ukisahau kumfungulia ,jogoo atawika kukukumbusha kuwa kumekucha ukafungue mlango wa kibanda.

Sasaaa.....

Naamini kuwa, kuku hurudi kibandani jioni kwa sababu hutambua kibanda kama nyumba yake.

Tatizo ni kwamba;
  • mwenye kibanda naye anatambua kuwa anamiliki pale aishipo kuku.
  • mwenye kibanda humuita kuku , KUKU WANGU.
  • mwenye kibanda huita matokeo ya mimba ya kuku, MAYAI YANGU.
Mitazamo ya mwenye kibanda na kuku aishiye kibandani inatofautiana sana kiasi kwamba unaweza hata usihisi wana migogoro.

Lakini....

Mitazamo ni kitu cha ajabu sana!
Kwa mtazamo wangu toto la kuku wa kizungu linalelewa kama yatima, bila wazazi.
Mtazamo mwingine unaweza kubobea kwenye jinsi toto la kuku wa kizungu liletewavyo misosi chumbani na kunenepeshwa haraka.

Swali:
Hivi kwanini lile kuku jingine linaitwa la kizungu?

DUH!

Kuku wa kienyeji ni kiboko!
Kwa kuhaha humuwezi.
Kwa utamu ni balaa.
Matokeo ya mimba yake (mayai) ni matamu , ukiyakaanga hata kuchemsha.
Yakitamiwa na kutotolewa, watoto wake kwenye bustani yako ya mbogamboga utakutana nao.

Kuku wakienyeji kakomaa, misuli kwenye vigimbi miguuni utashuhudia kutokana na mahangaiko ya siku nzima chini ya jua kali.
Kuku wakienyeji huchuma halali kwa jasho lake.



Toto la bata , lazima lionee wivu toto la kuku wa kienyeji.
Toto la kuku, chakula latafutiwa na mama.
Mama pia ni mlonda au kwa jina maarufu, mlinzi.

Ukicheza karibu na wanae, waparuriwa.
Toto la kuku lina ustaarabu!

Ushastukia toto la kuku huchuchumaa likienda haja kubwa wakati toto la bata laweza harisha likitembea?

DUH!

Lakini.....

Tatizo ni kwamba :
  • ramani ya misafara ya kuku haiwekewi kumbukumbu.
  • kila siku , inaenda ilimradi chakula chafika tumboni .
  • kuku anadhani kibanda ni nyumba yake wakati mfugaji amuona kuku na kibanda chake kuwa ni mali zake.
Tatizo linalozidi kujitokeza ni kwamba, toto la kuku likikua linarithi mfumo lililoukuta kwa wazazi wake. Ni vigumu kustukia kuwa kilichomkuta baba yake(jogoo) baada ya mwenye kibanda kupata wageni, ndio kitakacho mkabili Kijeba aka Toto la Kuku, mfungo Ramadhani ukiisha.

DUH!

Swali:
Ushawahi kustukia waitwao wananchi mara nyingi ndio wasiomiliki nchi?

Sitaniiii!
Turudi kwenye hoja;

  • Kama mwananchi anajivunia nchi yake wakati akipatacho kwenye nchi ni sawa na uhuru wa kuku wa kienyeji, je, hiyo ni nchi yake?
  • Kama siyo nchi yake, ni nani anaimiliki ambaye wametofautiana mitazamo mpaka mwananchi anajidanganya kufikiria kuwa yeye ananchi?
  • Au tuamke tu na kufanya tufanyalo ilimradi chakula chafika tumboni na tuko huru kwenda kulia na kushoto, bila kujali tupaitapo nyumbani kuna mtu mwingine anapamiliki?
  • Unafikiri Tanzania inamilikiwa na Watanzania au Watanzania wanawakilisha mtazamo mmoja tu, kati ya mitazamo ya makundi mawili tofauti yatumiayo sentensi moja na kuiita Tanzania;nchi yangu?
Swali:
Nani anaathirika sana kati ya kuku au toto la kuku, kwa kosa la kutomstukia mwenye kibanda?

Sina uhakika lakini kama kuku anafaidika sana kwa kumstukia mwenye kibanda lakini bado kutokujua nia yake au hata jinsi ya kupambana naye.
Duh!
Naacha basi!


Tulia na Seal





Read more...

Pitia katika Ukurasa wa JUMUWATA!

>> Wednesday, September 12, 2007

JUMUWATA iko jikoni ingawa mambo fulani yanaweza kutafsiriwa kuwa yamechelewa kwa tafsiri fulani.
Aggregator iko jikoni ,Katiba na kila kitu.
Lakini pitia kwenye JUMUWATA upate muelekeo wake.
Sijapandisha kitu kizima.Lakini nilichopandisha unaweza kuchangia na kujua muelekeo.

Kemea, toa maoni,ongezea ,au ondoa mizinguo.....

Pitia hapa JUMUWATA basi!

DuH!

Kuna kawimbo lakini naendelea kukasikiliza.
Unapenda Lovers Rock?
Mpate Bobby Kray basi wakati una....

Read more...

Robert Mugabe VS Askofu PIUS NCUBE

Inajulikana kila binadamu ana udhaifu wake.
Na watu wakikufuatilia sana watakudaka katika kaudhaifu kako.
Inawezekana kaudhaifu kakawa ni kale kakulialia haraka mambo yakiwa magumu .Lakini kaudhaifu kanaweza pia kakawa ni kale kanakokupa sura tofauti na ile watu waijuayo kuhusu wewe.

Naona Askofu Pius Ncube, akina Mugabe walimstukia kaudhaifu kake ka ngono.
Ingawa anatakiwa awehajihusishi na maswala ya uroda hasa yeye kama Askofu wa kanisa la kikatoliki inasemeka alifanikiwa kujifariji kama wafanyavyo maaskofu na mapadre wengi tu .
Inasemekana lakini kuwa huyu Askofu alikuwa amespeshalaizi kwa wake za watu.

DUH!

Sasa haya ni mambo binafsi.
Hayatuhusu.

Lakini nimejikuta niko katika majadiliano na wadau ambao wamesisitiza kuwa huyu Askofu kama alikuwa anauwezo wakutomuogopa Mungu amuubiriyo na kuwa muongo na Mzinzi, inaawezekana hana tofauti na Mugabe ambaye amezidiwa utamu wa kuwa na nguvu.Hii hoja imetokana na baadhi ya watu kufikiria kuwa ni afadhali ahamie kwenye siasa baada ya kuenguliwa na Papa.

Najua jamaa wamempatia kasehemu kakumkata nguvu za kumpinga Mugabe kwa kuonyesha kuwa ni muongo na mdhaifu kama binadamu wengine.
Lakini haka kamchezo wakianza kukafuatilia bongo si itakuwa balaa?
Swali:
Si Bongo siasa inatafsiri sawasawa na uongo?

Tulia na Boney M

Read more...

Binadamu Kwa Mashindano!DUH!

>> Tuesday, September 11, 2007

DUH!
Nilipotea kidogo.
Nimerudi sasa!:-)

Ngoja niende kwenye kilicho mawazoni....

Tabia ya kutafuta nani zaidi , imezoeleka sana katika shughuli mbalimbali za binadamu.
Na kwa kweli huwa wanampata nani zaidi kwa kutumia vipimo kemukemu ambavyo mara nyingine ni vigumu kuelewa vipimo vyenyewe mara nyingi.


Swali:
Hivi ni nani Mzuri kuliko wote?
Nani anaakili kuliko wote?
DUH!
NANI ZAIDI?
Si wote ni binadamu?


  • Nashindwa kuelewa kwanini kuna mashindano ya wasanii.
  • Nashindwa kuelewa Kwanini kuna mashindano ya Uzuri!
  • Nashindwa ku....
Nirahisi kuuona ushindani kwenye sanaa, michezo ,siasa ,lakini uko kila kona.
Nirahisi kusikia watu wakijiuliza kuwa hivi:
  • Hi Hukwe Zawose au Moris Nyunyusa
  • Ni Mr Nice au Dudubaya ni zaidi?
  • Bob Marley au Peter Tosh ni zaidi?
  • Michael Jackson au Prince?
  • Miles Davis Au Louis Armstrong?
  • Ngwasuma au...............
  • Ni Richa Adhia au Hoyce Temu
Naamini kila msanii ni bomba.
Naamini kila mtu anapenda kitu fulani, ambacho masikioni au machoni mwake kinapendeza.
Naamini kitu kizuri kwangu sio lazima ni kizuri kwako.
Lakini!
Duh!


Tukienda kwenye michezo, inasemekana ushindani ni afya!
Lakini kuna michezo kama formula 1 ambayo pia nashindwa kuamini kuwa ,ingawa dereva ndio anasifika kuliko wote, kama ni kweli anastahili kuwa na sifa zote zile.


Kushindana labda ni ubinadamu.
Kwa sababu ninauona sana ubinadamu kwenye mashindano ya kisiasa.
Mwenye nguvu na hela mara nyingi ndio huibuka mshindi.

Nakutakia kila la heri katika ushindani!

Nawaza tu!
Usitishike!

Pata picha fulani ambazo hazija poa.
Lakini tulia na wadau wa senegali waliotuburudisha....

(Mtimkubwa unasalimiwa na Maissa na timu nzima ya Gallaxy)

PICHA ZA KIKAO CHA WADAU WA TIMU YA BONGO FC HELSINKI
Powered by www.myfabrik.com


Lakini ngojea tupate dondoo ya kitu fulani kiaandaliwacho...

AU hukustukia eeh!
Endelea kupata dondoo..


Tuendelee na picha....
Dj EZZA na Magonella
Powered by www.myfabrik.com


Niliowakata ni kwasababu tu sikuomba kuwapiga picha.Natumaini hakuna noma.Sijatoa sura nzima:-)
Powered by www.myfabrik.com

Picha mchanganyiko
Powered by www.myfabrik.com


Tuko pamoja!
Siku njema!
Tulia na Common

Read more...

KWA Jalala AFRIKA, NAJUA WEWE SI BIKIRA!

>> Thursday, September 06, 2007

Afrika imekuwa ni sehemu ambayo mataifa mengine yanailenga kuleta uchafu wao ambao wanaona si vizuri kuwa nao nchini mwao.
Mimi binafsi , natishika sana na tamaa za pesa ambazo zimesababisha viongozi wetu Afrika kuruhusu mataifa mengine kugeuza Afrika kuwa jalala.

Kidonda hiki kimefumuliwa na taarifa zilizojaa katika vyombo vya habari zionyeshazo jinsi gani mataifa mengi duniani yanarudisha mali zilizotengenezwa China huko huko Uchina kutokana na kuwa na sumu na pia kasoro chungu mbovu.

Nafikiri kama wewe ni mfuatiliaji wa habari, utastukia katika miezi hii michache, kuanzia vyakula mpaka madoli ya watoto yamerudishwa Uchina kutokana na kuwa na sumu. Kuanzia wanyama Marekani mpaka watoto wamedhurika kwa sumu au kwa vifaa kutotengenezwa kwa kuangalia usalama wa watoto

CHA KUJIULIZA:
Hivi ni nani anafuatilia vifaa , vyakula hivi hatari, vikirudishwa Uchina vinapelekwa wapi?

Kiniogopeshacho ni kwamba inawezekana vifaa hivi na vyakula hivi , haviharibiwi.
Vinauzwa kwetu sisi Waafrika kwa bei ya cheeee.
Sina ushahidi na hili, lakini naamini kabisa hili jambo linatokea na lishatokea.

Si unakumbuka:

  • Wamarekani wanamchezo wakutoa hata kwa msaada vile walivyostukia haviwafai kama vyakula au kwa nia nyingine zilizojificha zinufaizazo Marekani na sio Afrika . Unakumbuka hii?
  • Mambo mengine mengi yaliyogeuza Afrika kuwa jalala.

Sasaaaa...

  • Tuachie na Wachina wageuze Afrika jalala?
  • Kama hatutaki kuachia, nani anafuatilia hizi mali za kichina ambazo zimejaa Afrika?
  • AU ni mpaka tufe?

Afrika inabidi ijiadhari na mpenzi mpya huyu wa Kichina. Isije ikawa hata Uwanja mpya wa Tanzania ni moja ya jalala, maana nasikia ukijikwaa kwenye kiti kinaweza kung'oka.Ukifunga maji kwa nguvu unaweza ukaongoka na bomba zima la maji!

Tuwe macho na Afrika yetu hata kama katika swala hili haina bikira.

Duh!Naacha!
Baadaye basi!
Mpate Bilal akija na Soul Sista!

Read more...

Ratiba ya SIKU YA KUFA!

Baada ya taarifa za habari kujaa habari za kufariki kwa LUCIANO PAVAROTTI leo, na kumsikiliza Dr Remmy Ongala akiimba kuhusu siku ya kufa, nimeshindwa kujizuia kutafakari haka kamchezo ka-kufa na ratiba yake, ambako ni ka-lazima kwa binadamu wote kukacheza siku na mminyominyo ukifika.

Lakini.........

Ratiba, katika tamaduni nyingi ni kitu cha kawaida.
Tatizo ni kwamba , ratiba haina sura moja katika tamaduni tofauti.
Ratiba iaaminiwayo kuliko zote duniani, ni ile isiyo na vikolombwezo vingi ndani yake.
Ni ile isemayo kesho nitaamka, halafu nikichoka nitalala.
Hizi ratiba zenye sekunde, dakika ,saa , siku , mahala, zikiongezea na nitafanya nini katika muda huo, pamoja na kuwaletea mafanikio mengi wachache waliofanikiwa kwelikweli hapa duniani, kuna mambo mengine inacheza hola.

Lakini.....

  • Nisikufiche, ukiwa na ratiba na unauwezo wa kuifuata, kuna uwezekano ukafanikiwa sana.
  • Nasikitika , Tanzania , hatujafanikiwa kuweza kufuata ratiba kisawasawa.

DUH!

Siku zote ni tofauti.
Nikiwa na maana hakuna siku mbili zifananazo.
Hakuna mtu aliyeweza kuishi siku mbili akiwa ni binadamu yule yule.

Kila kiminyominyo, sekunde, dakika, siku....., binadamu anageuka, kuanzia chembechembe mwilini mpaka hamu yake na ujuzi wake wa utamu wa pipi.
Naamini unakumbuka, pipi uionjavyo mara ya kwanza ni tofauti na urudiapo kuimumunya baadaye.
(Kumbuka kiminyominyo au mminyominyo ni kipimo changu binafsi cha muda)

DUH!
Lakini....

Siku ya kufa , inaweza ikawa si leo, ingawa ni kama kesho!
Ratiba yake ni kama kesho tuifikiriavyo.

Swali:
Si unakumbuka hakuna siku mbili zifananazo?


DUH!

  • Unajua lakini, unaweza kupanga ufe saa na dakika ngapi? -nategemea ukifanya hivyo unajua utakuwa umejiua lakini.
  • Si unakumbuka mara nyingi wale wajilipuao kwa sababu ya kutetea dini, walioko kwenye fasheni siku hizi, huwa hawafanikiwi kujilipua katika dakika waliyopanga?

USISTUKE!
Kila siku , kuna watu magerezani na kwingineko waliopangiwa wafe dakika gani na ratiba inafuatwa kikamilifu.


Nawatakia wote waliofariki WAPUMZIKE MAHALI MEMA PEPONI!
Sijui lakini kama wote tuwaombeao wapumzike mahali mema peponi wataenda huko peponi.
Na kama wote wanaenda huko....... mmh!

DUH!
Kama unasoma hapa , inamaana wewe mzima, lakini haina maana mimi niliyeandika bado niko hai.

Ishi vyema, hatuna uhakika na ratiba!
SIKU NJEMA!
Nakuacha na marehemu aliyefariki jana, LUCIANO PAVAROTTI na marehemu aliye tutoka miezi kadhaa iliyopita. JAMES BROWN:

Read more...

Wadau EEH! ASANTENI! TUKO PAMOJA!

>> Wednesday, September 05, 2007

Kuna kitu rahisi sana kusahau!
Nacho nikuwashukuru washikaji wanaotupa kampani kila siku katika shida na raha.
Mimi kama Mdau ambaye kwa miaka zaidi ya Kumi na tatu nimekuwa naishi mbali na nyumbani,marafiki na wadau mbalimbali ninaokutana nao au kujuana nao ni muhimu sana kwangu, na wamekuwa msaada mkubwa kwangu kiakili na kimaisha.
Mnikosoavyo na mnifundishavyo ni muhimu sana kwangu.

Bila nyinyi nafikiri ingekuwa vigumu kuweza kuwa Simon mmjuaye.Na nafikiri ningekuwa mpweke sana katika maisha haya ambayo unapoishi, hata jirani humjui zaidi ya kupungiana, na hilo ni kwa bahati bahati hasa katika maisha haya tuishiyo yaendayo kwa spidi kali.

Nashukuru sana kwa yote!Ningependa kutaja majina lakini itashindikana kutokana na wingi wa washikaji zangu ambao wote ni muhimu.

ASANTENI SANA!
NA SAMAHANI KWA WOTE NILIOWAKWAZA NA KUWAKOSEA!
Unajua tena miye ni binadamu!

Ngojaniseme....

Usistuke hakuna sauti, nakuzingua tu mdau!

Lakini....
Ngoja niweke baadhi ya picha zangu na wadau niliokuwa nao ndani ya siku hizi chache zilizopita.

(WADAU WENGINE POPOTE DUNIANI NISAMEHENI! MNAWEZA KWENDA MOJA KWA MOJA KWENYE VIDEO YA X-plastaz , chini kabisa ya post hii.)

DUH!
Kabla ya picha wadau tuliokuwa pamoja mnakumbuka hii?:-)


Clemoo uliniua mbavu.

Mnakumbuka hii pia......?


Picha za baadhi ya washikaji wangu siku chache zilizopita na mimi...

Powered by www.myfabrik.com


Kwa mara nyingine:
ASANTENI WADAU WOTE!


Siku njema!
Na tulieni na X Plastaz

Read more...

IMENISIKITISHA KUGUNDUA ULE MRADI WA KAMUSI YA KISWAHILI UMEKUBWA NA MATATIZO!

Ukizingatia kuwa bado tunahitaji Kamusi nzuri za Kiswahili Mtandaoni, huu mradi wa Yale uliokuwa unapatikana katika anuani:http://www.yale.edu/swahili/, nilikuwa nauthamini sana.

Lakini...:

The Internet Living Swahili Dictionary has been taken offline.

The project has been ordered to remove all links to the sites that the project has relied on to raise revenue for project maintenance and improvement. Without these links, the project has no income source and cannot function; the project will have a negative account balance after outstanding debts are paid.

We sincerely regret this interruption. The Kamusi Project usually serves over one million pages per month to users around the world.

We are working to resolve the situation. However, the site will remain offline until the following issues have been resolved:

  • can the Kamusi Project raise funds through the sale of clocks and other merchandise?
  • can the Kamusi Project acknowledge gifts from major supporters?
  • can the Kamusi Project include passive advertising alongside search results and other pages?

The relevant section of University policy is the following:

ITS Appropriate Use Policy 1607.C.2 Use that is inconsistent with Yale's non-profit status. The University is a non-profit, tax-exempt organization and, as such, is subject to specific federal, state, and local laws regarding sources of income, political activities, use of property, and similar matters. As a result, commercial use of IT Systems for non-Yale purposes is generally prohibited, except if specifically authorized and permitted under University conflict-of-interest, outside employment, and other related policies. Prohibited commercial use does not include communications and exchange of data that furthers the University's educational, administrative, research, clinical, and other roles, regardless of whether it has an incidental financial or other benefit to an external organization.

The Kamusi Project was in the past granted authorization to raise funds through certain merchandising links. However, documentation for that authorization is no longer available. Therefore, the site must remain offline until all questions about whether the project has authorization to raise funds through passive revenue generation on the site have been resolved.

With sincere apologies,
The Editor

5 September, 2007

Read more...

UTAMU WA KUFANYA DHAMBI!

>> Tuesday, September 04, 2007

Watu wengi ingawa hawatakiri hadharani, hupenda kutenda wakatazwayo.
Wapo wengi wafurahio kuvunja sheria kwa sababu tu zimeitwa sheria.

Swali:
Unafikiri kwanini kuna sheria?

Ukikatazwa kudokoa mboga, halafu ukajikuta pekee jikoni mbele ya sufuria fulani , mdadi wa kudokoa unaweza kukupanda.

AU?

Ila, kumbuka kama hujakatazwa kudokoa mboga, ukajikuta jikoni mbele ya sufuria fulani , unaweza ukaonja hiyo mboga na utandu, na wote tukaamini kuwa umeonja mboga na hukudokoa.

Nilipokuwa nafuatilia maswala ya kwanini watu kupenda kula uroda pekupeku hata kama wanajua kuna UKIMWI, nikastuka kupata data zionyeshazo kuwa watalii wengi kutoka nchi za ulaya kaskazini , wasafirio kwa ajili ya kutafuta uroda(sex tourism), mara nyingi hulipia ngono kwa bei ya kuvaa soksi lakini kisiri katika shughuli huibia na kuvua soksi.

Si unajua tena pekupeku bei yake ni ghali kuliko na soksi. Kisa cha wengi kuvua soksi kisiri wakiwa kiwanjani , ni kujaribu kukomesha au kuvunja sheria, kwasababu wameambiwa na mwanadada lazima wavae soksi kwani anaogopa magonjwa au atapandisha bei. Kitu kama hiki ambacho chaweza kutafsiriwa kama cha kijinga, kinatokea tu kutokana na silika ya baadhi ya watu ya kuvunja sheria.
Nakubali lakini wapo wavuao soksi au kutovaa kabisa soksi kwasababu wanasema wakivaa soksi chakula hakinogi.

Swali:
Ushawahi kukatiza katika uchochoro ambao umebandikwa kibao kisemacho;ni marufuku kupita hapa?

Duh!
Turudi kwenye dhambi......

Nakumbuka unakumbuka kuwa karibu dini zote zina jaribu sana kutukaza kufanya vitu fulani kwa sababu ni dhambi.
Dhambi inasemekani ni mbaya sana.
Tatizo la dhambi ni kautamu kake, hata katika dini zetu , dhambi hizi utamu kunoga, zimeelezewa kinamna ambayo inaonyesha ni vigumu sana kuzikwepa. Lakini nahisi watu wengi wanajizuia kufanya dhambi kutokana na hofu ya baada ya kufa watajibu nini kuhusu madhambi waliyokuwa wanashabikia pale chobisi.

Chakutisha ni kwamba dhambi zinazoeleka.
Ndio maana unakuta wahubiri wa dini karibu zote, ukiwafuatilia, utakuta kunatudhambi wanatufanya kwa bidii tu.

Tudhambi twa:

  • ngono nje ya ndoa,
  • kuiba sadaka,
  • kugombanisha waumini
  • kudanganya
  • kuua kwa jina la dini au Mungu
  • ku...
  • nk.
Na wengi huweza kufanya hizi dhambi, baada tu ya kutoka kuwatisha wawasikilizao jinsi gani watakavyo chomwa jehanamu kwa kuzitenda hizi nanihii.

Lakini tukumbuke...

  • Ukifanya dhambi mara ya kumi , kuna tofauti na ile ya kwanza.
  • Dhambi uirudiayo mara ya ishirini, haikutesi katika dhamira kama ile ya kwanza ya kumchungulia nanihino akioga.

Swali:
Ushastukia kale kadhambi utendako, ambako kako kwenye dhamira, kale usikotaka kukafikiria sana?

Usitishike !
Ni siri yako hiyo, sisi hatujui!
Na sisi wote tuna dhambi, ingawa nasikia binadamu wengine wameshinda lotto yakuitwa watakatifu.

DUH!

TUTUBU LAKINI!

Kumbuka :

  • Dini nyingine zinasema dhambi za kukusudia hautasamehewa. Kwahiyo kama umeshazifanya na kuzirudia mara kenda na uche...Jehanamu inaweza ikawa inasubiri.
  • Sina uhakika kama ukihama hiyo dini ikutiayo hatiani sasa na kwenda katika ile isemayo utasamehewa, kama utaponyeka.

Duh!
NAACHA BASI!
Tutulie na nyepesi nyepesi kutoka Japan ihusuyo doli liitwalo Kuma kama iletwavyo na Hikaru Utada , katika wimbo boku wa kuma


Read more...

KABLA HUJAMCHOKA KIPENZI!

Kipenzi,mpenzi.
Mtoto mzuri kweli!
Msichana analipa , si utani!

AU......

Kijana hendisamu , mwanadada hakawi kumuota zile ndoto nzuri nzuri zijazo hata akiwa macho!
Bonge la buzi.

Inawezekana hata jina hulijui , lakini umemtungia lako la kisiri!
DUH!
Penzi limenoga hata kama ni la alinacha!
Chochote afanyacho wakionea kwa upande mtamu.
Wale wakustuao kwamba nonihino anaupande mchungu usioujua , unawaona wachawi wanakuletea kiwingu.
Akijamba hunusi harufu mbaya!
Sana sana anakufanya ucheke kwani ni kichekesho tosha.
Anavyokoroma akilala, ni bomba la wimbo na kibembelezo masikioni mwako.

Siku zinaenda.............!

Hali halisi inaota makucha!
Kwa sababu hata uliponogewa ilikuwa ni hali halisi.
Kilicho cha maana na kisicho maana vinabadilishana viti.
Kifurahisho na kinachouzi vinagombania kiti kimoja.

  • Akikugusa kwa mapenzi , anakusumbua na kukumbusha uguswapo na nzi au buibui.
  • Akikoroma unahama chumba.

  • Ukimaliza kazi ofisini , unaanza kuwaza utafute kisingizio gani cha kuchelewa kurudi nyumbani.

Tatizo ...

Visingizio vipo.
Ukweli ni kwamba penzi limegeuka sura.
Ukweli ni kwamba humchukii mpenzi.
Kwasababu penzi likibadilika sura, bado ni penzi.

Ila...

Ni penzi jipya linalohitaji kuangaliwa kwa jicho jipya na kulipalilia kwa jembe tofauti.
Inawezekana inabidi mpaka ubadilishe hata mbolea, kwa penzi hili kustawi tena.
Kwani penzi hili ni rahisi kufichwa nyuma ya ....
  • Majukumu ya kulea watoto
  • Kazi nyingi ofisini
  • Matiti yamelala siku hizi
  • Umeota kitambi
  • Viagra hazipatikani kirahisi
  • au hata...... .
Lakini......
Kuishi na penzi jipya yawezekana.

Lakini......

Swali:

  • Unaruhusiwa kumchoka kipenzi na kutojisikia unafanyakosa?
  • Ushastukia kipenzi uliyemchoka waweza kumtamani ukimuona kadakwa na mtu mwingine?
DUH!
LAKINI......?

Siku njema!
Mpate Billy Ocean akikupa jinsi Ghafla alivyostukia kapenda!

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP