Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUIVA ni MWANZO wa KUOZA kwa TUNDA!

>> Friday, September 21, 2007

Wengi wetu hufurahia tunda likiiva.

Tatizo la tunda likishaiva, ni muelekeo wake.

Lakini....

Tunda likiiva , hatua inayofuata ni kuiva sana, halafu kuoza.
Tunda lililooza wengi tunalikwepa ingawa ndio mimba ya mbegu zitubarikizo na mimea kedekede.

  • Kuiva ni kufikia katika kikomo cha kipengele.
Chakusikitisha ni kwamba ukifikia kikomo cha kipengele unaweza usistukie mwenyewe.
Halafu wanaostukia wanaweza wasiwe na uhakika na ulipofikia, kutokana na kukumbuka yale wayahusianisho na kipindi mambo yako yalipoiva.
  • Kuiva ni kufikia mwisho wa ngazi.
Ukifika mwisho wa ngazi kilichobakia ni kushuka.

Duh!

Ukifikia ngazi ya mwisho ,unaweza ukapaa, kama unamabawa au helkopta ya kukuchukua hapo ngazini na kukupaisha juu zaidi ya jengo ambalo kiurefu huzidi ngazi.

WIKI MWISHO NJEMA!
Burudika na Mr Nice

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

KKMie 8:14 pm  

Yaani unajaribu kutuambia kuwa wachanga(wabichi) kukakua (pevuka) alafu tukakomaa(iva) na sasa tumezeeka(kuoza) na tukisha zeeka ndio mwanzo wa wengine kuja (mmea wa tunda kuota).

Hakika makunyanzi yakianza usoni watu huongeza kasi yakufanya mambo iwe ni kujenga, kungonoka, kuzaa na kuwa karibu na ndugu, jamaa na marafiki.

To be honest sijui naongelea nini hapa hahahahahaha!

Si, kazi nzuri keep it tight!

Simon Kitururu 3:24 am  

@Dinah!Duh! Lol!Unatabia,baya ya kunielewa weee. Unikomeeee..!Hahaha!LMAO!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP