Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KWA Jalala AFRIKA, NAJUA WEWE SI BIKIRA!

>> Thursday, September 06, 2007

Afrika imekuwa ni sehemu ambayo mataifa mengine yanailenga kuleta uchafu wao ambao wanaona si vizuri kuwa nao nchini mwao.
Mimi binafsi , natishika sana na tamaa za pesa ambazo zimesababisha viongozi wetu Afrika kuruhusu mataifa mengine kugeuza Afrika kuwa jalala.

Kidonda hiki kimefumuliwa na taarifa zilizojaa katika vyombo vya habari zionyeshazo jinsi gani mataifa mengi duniani yanarudisha mali zilizotengenezwa China huko huko Uchina kutokana na kuwa na sumu na pia kasoro chungu mbovu.

Nafikiri kama wewe ni mfuatiliaji wa habari, utastukia katika miezi hii michache, kuanzia vyakula mpaka madoli ya watoto yamerudishwa Uchina kutokana na kuwa na sumu. Kuanzia wanyama Marekani mpaka watoto wamedhurika kwa sumu au kwa vifaa kutotengenezwa kwa kuangalia usalama wa watoto

CHA KUJIULIZA:
Hivi ni nani anafuatilia vifaa , vyakula hivi hatari, vikirudishwa Uchina vinapelekwa wapi?

Kiniogopeshacho ni kwamba inawezekana vifaa hivi na vyakula hivi , haviharibiwi.
Vinauzwa kwetu sisi Waafrika kwa bei ya cheeee.
Sina ushahidi na hili, lakini naamini kabisa hili jambo linatokea na lishatokea.

Si unakumbuka:

  • Wamarekani wanamchezo wakutoa hata kwa msaada vile walivyostukia haviwafai kama vyakula au kwa nia nyingine zilizojificha zinufaizazo Marekani na sio Afrika . Unakumbuka hii?
  • Mambo mengine mengi yaliyogeuza Afrika kuwa jalala.

Sasaaaa...

  • Tuachie na Wachina wageuze Afrika jalala?
  • Kama hatutaki kuachia, nani anafuatilia hizi mali za kichina ambazo zimejaa Afrika?
  • AU ni mpaka tufe?

Afrika inabidi ijiadhari na mpenzi mpya huyu wa Kichina. Isije ikawa hata Uwanja mpya wa Tanzania ni moja ya jalala, maana nasikia ukijikwaa kwenye kiti kinaweza kung'oka.Ukifunga maji kwa nguvu unaweza ukaongoka na bomba zima la maji!

Tuwe macho na Afrika yetu hata kama katika swala hili haina bikira.

Duh!Naacha!
Baadaye basi!
Mpate Bilal akija na Soul Sista!

6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Rundugai 7:32 am  

hapa umelonga ni kweli habari hizi zimeandikwa sana na vyombo vya habari vya magharibi.Lakini hapa kwetu kimya tu.
Na wamejaa tele ukubisha nenda sinza,kinondoni karibu nao watagombea ubalozi wa nyumba kumi tumekwisha na bidhaa hapo kariakoo ndio usiseme si kwamba wana maduka makubwa ya kutisha ni kama yale ya watani zangu na wamejaa haswa

Honest Peter 3:57 pm  

Ni ukweli mtupu mzee kituturu,kwani swala la Africa kipekee TZ kuwa dampo ni makubaliano ya wakubwa kaka,wanavuta cha juu alafu sisi ndio tunaumia,tunabaki kunyoosheana vidole tu.lakini kaka ipo siku waTz watachoka na kufanya kitu kitakachoshangaza dunia.kaka kituturu kazi nzuri.

Simon Kitururu 12:24 pm  

@Chediel na Honest:Kazi Kwelikweli

luihamu 6:59 pm  

Katibu uemeeleza vizuri mkuu.

anani iwe nanyi.

luihamu 7:00 pm  

samahani,amani iwe nanyi

Simon Kitururu 3:45 am  

@Rasta Luihamu:Asante!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP