Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wadau EEH! ASANTENI! TUKO PAMOJA!

>> Wednesday, September 05, 2007

Kuna kitu rahisi sana kusahau!
Nacho nikuwashukuru washikaji wanaotupa kampani kila siku katika shida na raha.
Mimi kama Mdau ambaye kwa miaka zaidi ya Kumi na tatu nimekuwa naishi mbali na nyumbani,marafiki na wadau mbalimbali ninaokutana nao au kujuana nao ni muhimu sana kwangu, na wamekuwa msaada mkubwa kwangu kiakili na kimaisha.
Mnikosoavyo na mnifundishavyo ni muhimu sana kwangu.

Bila nyinyi nafikiri ingekuwa vigumu kuweza kuwa Simon mmjuaye.Na nafikiri ningekuwa mpweke sana katika maisha haya ambayo unapoishi, hata jirani humjui zaidi ya kupungiana, na hilo ni kwa bahati bahati hasa katika maisha haya tuishiyo yaendayo kwa spidi kali.

Nashukuru sana kwa yote!Ningependa kutaja majina lakini itashindikana kutokana na wingi wa washikaji zangu ambao wote ni muhimu.

ASANTENI SANA!
NA SAMAHANI KWA WOTE NILIOWAKWAZA NA KUWAKOSEA!
Unajua tena miye ni binadamu!

Ngojaniseme....

Usistuke hakuna sauti, nakuzingua tu mdau!

Lakini....
Ngoja niweke baadhi ya picha zangu na wadau niliokuwa nao ndani ya siku hizi chache zilizopita.

(WADAU WENGINE POPOTE DUNIANI NISAMEHENI! MNAWEZA KWENDA MOJA KWA MOJA KWENYE VIDEO YA X-plastaz , chini kabisa ya post hii.)

DUH!
Kabla ya picha wadau tuliokuwa pamoja mnakumbuka hii?:-)


Clemoo uliniua mbavu.

Mnakumbuka hii pia......?


Picha za baadhi ya washikaji wangu siku chache zilizopita na mimi...

Powered by www.myfabrik.com


Kwa mara nyingine:
ASANTENI WADAU WOTE!


Siku njema!
Na tulieni na X Plastaz

7 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Chemi Che-Mponda 7:22 pm  

A Day in the Life of Simon. Safi sana.

Simon Kitururu 7:56 pm  

@Da Chemi:Ingekuwa mali kweli kama kila siku zingekuwa zinaenda murwaa!Maana siku nyingine ukiamka tu unaanza na kujikwaa wakati unatoka kitandani.

Egidio Ndabagoye 8:03 am  

Washikaji ni muhimu sana ukiwa mitaa ya mbali na nyumbani.Nami nawashukuru washikaji wa mitaa hiyo kwa kutokukuangusha.

Simon Kitururu 8:02 pm  

@Egdio: Ukiwa pekee yako hukawii kurukwa na akili.

Aliko 6:10 pm  

yule mdada wakisonjo anavyopiga shot duuh kama msoviet kazi kweli ulaya maanke hii action ingekua kule mogadishu ni murder case

Simon Kitururu 3:38 pm  

@Aliko:Si Utani!

Unknown 2:18 pm  

Safi kwa kifupi nimeikubali. nami nicheki ktk http://artsfede.blogspot.com/

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP