Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Chakula cha Mawazo!- Ukimwi!

>> Friday, November 24, 2006


Jacob Zuma alidai alioga kuzuia virusi baada ya kufanya mapenzi na mwanadada mwenye ukimwi.











Kwa nini binadamu anauwezo wakufanya mapenzi na mtu mwenye ukimwi kwa hiari yake mwenyewe hata kama anajua kuna kufa?Je unamkumbuka Jacob Zuma?

Niliwahi kuulizwa maisha ni nini? Swali hili nikashindwa kulijibu kwani lili nisababishia maswali mengine mengi sana. Naamini binadamu mara nyingi anaishi akitafuta maana ya au uthamani wa maisha! Kwa wengine maisha yanaanza kuwa na maana pale anapo kuwa na watoto. Hivyo watoto wake wana kamilisha au kutoa jibu la kwanini aamke asubuhi kwenda kazini au hata ajitunze. Wengine maisha kwake yanakamilika kupitia mitazamo ya kidini. Anaamini yuko hapa kwa mpango wa Mungu na hivyo basi moja ya mambo yaletayo maana kwake ni pamoja na kumtukuza Mwenyezi Mungu. Anautunza mwili wake kwa sababu mwili ni hekalu la Mwenyezi Mungu. Kuna mwingine maisha hayana jibu sahihi. Hivyo ni lazima awe katika hali ambayo inamsahaulisha machungu ya maisha ambayo yanaonekana ndio pekee yana tawala maisha.Wengine wanaishi maisha yakutokujali lakini wakijua kuwa hawajali. Wengine wanaishi maisha ya kutojali lakini kwa sababu hawajui wamejiingiza kwenye nini.

Hivi ushawahi kujiuliza kwanini unataka kuishi muda mrefu?Hivi ushawahi kutamani maisha waishio Wazee wa miaka mingi? Hivi ukikumba ukimwi na maisha yako yakafupika na labda ukafa kwa kuteseka sana inakutisha? Je, ukikumba mdudu utawatesa watu wa karibu yako?


Lakini hayo yote ni maswala ambayo wewe mtu mzima unaweza kuyatafakari. Kwa watoto ambao wanakumbwa katika janga hawana chaguo kubwa. Hawana uwezo wa kuelewa hata wamekumbwa na nini!Hawajui ngono wala nini! Je unawakumbuka hawa watoto wanao kumbwa katika janga kama hili?Mimi sijui mengi lakini nafikiri angalau viumbe wasio na hatia wasiingizwe katika kasheshe litokanalo na chaguo mtu mzima mwenye akili timamu achagualo kufanya.Tujaribu kuwafikiria watoto. Tujaribu kuwafikiria watu tunao wajali. Hivi wewe unamjali nani?Je, uko tayari kivyako au ukishakufa ndio imetoka hiyo ndugu na jamaa watafanya mambo?

Angalia nyumba hii ya Rehema hapo Kenya:

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP