Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

DUNIA, Binadamu na VIUMBE VYOTE ni KWA AJILI ya PANYA!

>> Sunday, January 04, 2009

Kama wewe ni MGAGAGIGIKOKO, Muislamu, Mkiristu kama sio Mkiristo, na kwa mbali unaimani zenye IMANI zenye imani hata AMBAZO unaweza kunukuuu WALIOANDIKA ukweli baada ya miaka mia fulani baada ya UMFUATAYE alivyosema walioamini na KUKARIRIRI kusema , UTAAMINI dunia na viumbe vyake ni kwa ajili ya BINADAMU.

Ukiamini hivyo, UNAWEZA kushangaa na KUTOELEWA waaminio umuhimu wa viumbe vingine ambavyo vingine vinakusaidia kulainisha chakula tumboni ili ukishiba MWILI nao USHIBE kwa virutubisho.

KWA yeyote AAMINIYE CHOCHOTE, kwa kuamini AMEJIJENGEA UKUTA wa kuelewa NI NINI ni KWELI.

Hakuna aaminiye CHOCHOTE mwenye UHAKIKA kila siku na AAMINICHO.

Kama UNAUHAKIKA na uaminicho,UAMINICHO siyo IMANI.

IMANI kiboko inakuacha USIJUE kila kitu ili UAMINI tu kuwa labda ni kweli hata MBINGUNI ni KUZURI ingawa dini yako inakujulisha aliyekuwa MKUU WA MALAIKA a.k.a SHETANI alikuwepo MBINGUNI halafu hakuridhikanako na akataka zaidi kama tu umtamanivyo ASIYE WAKO.

Na ukiamini SIMULIZI...
...unaweza kuamini kuwa: ''WACHA shetani afukuzwe kwa kutaka zaidi mbinguni'', ingawa SISI eti hapa duniani penyewe bado TUNA TAKA zaidi hata UKOKO!:-(


Lakini....
...hata MUNGU wa UPENDO huonekana anakuadhibu kama tu tabia za lijitu fulani!:-(
KATIKA jicho la AMUAMINIYE ikiwa pamoja na KUSALI kila akipepesa MJICHo kama TOCHI halafu bado ayaombayo hayatimii na MPENDWA ndugu ANAFARIKI wakati akiSHAfariki maana yakuishi kwa MUOMBAJI haipo, kuna wajiulizao mara mbili sababu za kuendelea kujipendekeza kwa Mungu.

Swali:


  • Ushawahi kustukia muamini MUNGU akijiuliza kama kuna MUNGU?

TEMBEA UONE!

Ukizunguka DUNIANI na kukutana na BINADAMU wengine wenye IMANI TOFAUTI, utastukia labda, HATA UKWELI uliokuwa nao umeathiriwa na imani yako iliyoathirika na IMANI YA JAMII yako kama ile tu ikuaminishayo MBINGU IKO JUU na sio CHINI.

Swali:


  • Kama DUNIA inaelea katika ULIMWENGU huu wenye SAYARI lukuki, CHINI ni WAPI?

Tukirudi AFRIKA,...
....kilema cha wasomi wengi wa KIAFRIKA, ni kujenga HOJA na kujaribu kuamini majawabu ya matatizo , katika kutumia jicho au kuzingatia MISINGI ya kuelewa itokanayo na imani za dini hasa za KIKRISTO au KIISLAMU.

Kumbuka kuwa....
...hoja au misingi ya matatuzi ikijengeka juu ya MISINGI isiyoeleweka kwa watatuzi kama misingi ya IMANI, hatima yake ni UWEZO MDOGO wa KUELEWA tatizo.

Kama imani yako inakuongoza jinsi ya kuelewa, huwezi KUELEWA wasiofuata misingi ILIYOKUFANYA uelewe UELEWAVYO.

NAACHA!

Tupumzike kwa kwenda JAPANI kupata tena wimbo wa HITARU UTADA umsifiao MDOLI...


Au tu tumsikilize STING azungumzie SURA ya moyo , katika SHAPE of my HEART....

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP